You are on page 1of 12

www.annuurpapers.co.

tz

Sauti ya Waislamu

(17) WAPI KAMA ARAFA!


Mwenyezi Mungu Ameandaa MKUTANO MKUU Aloupa jina la HAJJ, unaowakusanya waislamu kutoka kila pembe ya dunia katika viwanja vya Arafa huko Makka. Wewe ndugu yetu umeshahudhuria huko angalau mara moja, na kujisikia ndani ya moyo wako kuwa u-miongoni mwa waislamu? Karibu na wahi kujiunga na Ahlu Sunna wal Jamaa. Gharama zote ni Dola 4,300. Tafadhaliwasiliana nasi ifuatavyo: Tanzania Bara: 0717224437; 0777462022;Unguja: 0777458075;Pemba: 0776357117.

ISSN 0856 - 3861 Na. 1074 RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7 - 13, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

Msiba mkubwa: Dini Mseto yaja


Waislam, Wakristo kufundishwa dini moja Ni Heri Zanzibar watakuwa na nchi yao Bukoba kuna nini? Bakwata walitoka huko
Maalim Seif Sharif Hamad. Ismail Jussa Ladhu

Zanzibar walilia Benki Kuu, Uraia


Hawa ni viongozi wa Dini mkoani Kagera waliohudhuria uzinduzi mihutasari ya somo la Dini na Maadili. Katikati kutoka kushoto ni Askofu Elisa Buberwa KKKT, Askofu Nestory Timanywa Jimbo Katoliki la Bukoba, Askofu Severine Niwemugizi Jimbo Katoliki la Rulenge, nyuma kabisa ni Masista na Mapadre kutoka Kigoma, na mstari wa kwanza ni viongozi wa BAKWATA mkoa wa Kagera.

Wasiotaka Dola kamili wajitokeze Mgombea Urais asitokee Dodoma Wakumbusha ya Kura za Karume

Vita kubwa ipo mbele


Ni vita ya kuondoa dhulma, ubaguzi Bila kungoa MFUMO hakuna salama
KUNA mikasa mingi imetokea humu Tanzania ambayo haielezeki imetokea wapi na wala kwa nini imetokea. Lawama kubwa wametwikwa Waislamu ingawa mpaka leo hii Jeshi la Polisi halaweza kuwakisha mahakamani watu waliochoma msikiti Tunduma. Waislamu tuwe macho,

Inaendelea Uk. 3

Wajumbe wa kikao cha uzinduzi wa mihutasari ya somo la dini na maadili wakisiliza kwa makini na utulivu. Habari Uk. 12

tutumie akili ya asili kuchanganua mambo. Vita kubwa iliyoko mbele yenu ni kuondoa dhulma iliyoshamiri nchini. Lengo liwe ni kutafuta j i n s i g a n i Wa i s l a m u wanaweza kuushinda huu "MFUMO" ili Wananchi wote wa nchi hii wawe na haki sawa na waishi kwa amani kama ilivyokawaida. Uk. 8

2
www.annuurpapers.co.tz

Tahariri/Tangazo
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013


11. Kwa upande mwingine, Pass mark ya Mathematics ilipanda kutoka 32 mwaka 2011 hadi 42, mwaka 2012. Hakuna sababu zozote za kitaalamu zinazoweza kufafanua jambo hili hasa ikizingatiwa kuwa somo hili kwa miaka yote ndio limekuwa likiongoza kwa kufeli watahiniwa. Labda M h e s h i m i wa S e l a s i n i atueleze mtaalamu wake wa PhD First Class ana maelezo gani. Kukosekana ufafanuzi wa kitaalamu, zipo tuhuma kuwa mambo kama haya yanafanyika kwa sababu wapo baadhi ya watahiniwa wanarahisishiwa kufaulu na ikitokea takribani wote wakapata A na B tu, hasa kwa somo kama hesabu, hufanyika maarifa i l i k u o n d o a wa s i wa s i u n a o we z a k u j e n g e k a . Na namna moja wapo ya k u o n d o a wa s i wa s i n i k u f a n ya m a a r i f a kuhakikisha kuwa zinakuwepo japo C na D chache. Lakini ukifanya hivi pia maana yake ni kuwa unawafelisha wanafunzi wengi waliotumia akili zao. Kutokana na tuhuma kama hizi, kumekuwa na kilio cha Watanzania kuwa pafanyike uchunguzi wa kina na ulio huru ili kulinusuru taifa na janga la kuzalisha A za kusaidiwa ambazo hatimaye zitatupa First Class za kuchakachua na huenda hili ndio tatizo kubwa linalofanya taifa hili lisipige hatua katika maendeleo. Tu m e a m b i wa k u wa NECTA inaongozwa na mtu aliye na Shahada ya Uzamivu ya Daraja la Kwanza. Sisi hatutaki kujua mengi sana ya utaalamu wake ila machache tu: Ni sababu zipi za kitaalamu za kupandisha A ya hesabu kutoka 75 mpaka 86? Ni sababu gani ameona umuhimu wa kuajiri mtaalamu wa Bible Knowledge lakini akaona hakuna haja kwa Islamic Knowledge? Ni kwa nini baada ya Mtihani kusahihishwa na wasahihishaji kurekodi alama, anajifungia na Kamati yake ya Kutunuku kwa SIRI kwa takribani miezi miwili toka usahihishaji ufanyike? Anafanyia nini alama hizo? Zipo tuhuma kuwa toka Waislamu walalamikie m a t o k e o ya m i t i h a n i ambapo Baraza lililazimika kuyabadili baada ya kuona kuwa palifanyika makosa, idadi ya walimu wenye majina yanayoashiria kuwa ni Waislamu imekatwa sana. Kwa nini?

AN-NUUR

AN-NUUR S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786


MAONI YETU

Kama hizi ndio First Class zetu nchi haiendi kokote


ZIPO tuhuma nzito dhidi ya Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani ( N E C TA ) D r. J o y c e Ndalichako ambazo mpaka sasa hazapatiwa majibu. Tuhuma hizo ni pamoja na ubaguzi na ubalakala (double standard) katika kutoa madaraja kwa watahiniwa. Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali rasmi za kiserikali, imegundulika kuwa NECTA imekuwa ikiwarahisishia wanafunzi wa Kikristo kufaulu na k u p a t a m a d a r a j a ya juu na wakati huo huo kuwajengea mazingira ya k u f e l i wa n a f u n z i wa Kiislamu. Moja ya njia hizo ni kupandisha viwango vya ufaulu kwa wanafunzi wa Kiislamu na kwa upande mwingine kushusha viwango hivyo. Hii ina maana kuwa wakati ilitarajiwa kama ili kupata A mtahiniwa wa somo la Bible Knowledge alitakiwa kupata , kwa mfano, alama 75 na kwa mtahiniwa wa Somo la Islamic Knowledge iwe hivyo hivyo, lakini kwa NECTA sio hivyo. Kwa A hiyo hiyo mtahiniwa Muislamu anaweza kutakiwa kuwa na 85 ili kupata A hiyo hiyo. Na sio pass mark tu, lakini hata pass range hutumika pia kufanya hujuma. D kwa mmoja inaweza kufanywa kuanzia 25 mpaka 40 huku C ikianzia 41 na wengine ikafanywa 35 mapaka 44 huku C ikianzia 45. Namba hizo ni mfano tu lakini yamebainishwa katika tafiti jinsi pass mark na pass range zinavyotumika kuhujumu baadhi ya watahiniwa na kuwarahisishia ufaulu wengine. Katiba ya nchi inasema k u wa N i m a r u f u k u

kwa mtu kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa kazi au shughuli yoyote ya Mamlaka ya Nchi. (Sehemu ya Tatu Kif: 12 (4)) Katika kufafanua nini maana ya ubaguzi kifungu 12 (5) kinasema kuwa Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa mashariti ya Ibara hii neno kubagua maana yake ni kutimiza haja, haki au mahitaji mengineyo kwa watu mbalimbali kwa kuzingatia utaifa wao, kabila, pahala walipotokea, maoni yao kisiasa, rangi, dini, jinsia au hali yao ya maisha kwa namna ambayo watu wa aina fulani wanafanywa au kuhesabiwa kuwa dhaifu au duni na kuwekewa vikwazo au mashariti ya vipingamizi ambapo watu wa aina nyingine wanatendewa tofauti au wanapewa fursa au faida iliyoko nje ya mashariti au sifa za lazioma Bible Knowledge na Islamic Knowledge yote n i m a s o m o ya d i n i , unaposema kuwa A kwa Mkristo ni 75 lakini kwa A hiyo hiyo Muislamu ni lazima apte 85, je huu sio ubaguzi? Je, ubaguzi huu ndio Mbatia anaohimiza Dr. Joyce Ndalichako aendelee kuufanya bila kuogopa? Ukiweka pass mark ya A kuwa ni 75 mpaka 100, maana yake ni kuwa kwanza unafanya kuwa wepesi kwa watahiniwa kupata A, lakini pia unatoa fursa kwa watahiniwa wengi kupata hiyo A. Na kwa upande mwingine unapopandisha k u wa 8 5 m p a k a 1 0 0 ni kuwa unaweka ugumu na kupunguza idadi ya watakaopata hiyo A. Nini lengo la ubalakala huu? Huku

ni kuwawekea vikwazo Waislamu au mashariti na vipingamizi vya kufaulu ambapo Wakristo wanarahisishiwa. Je, hii inafanywa makusudi ili kuziwezesha zile shule zinazotakiwa kutesa ziendelee kutesa kila mwaka? Je, hii ndiyo kazi Mheshimiwa Mbatia anayomwambia Dkt. Ndalichako aendelee kuifanya bila kuogopa? Baraza la Mitihani limeajiri Mchungaji anayeratibu somo la Bible Knowledge, lakini limegoma kabisa kuajiri Maratibu wa Somo la Maarifa ya Uislamu. Je, huu nao sio ubaguzi kwa m u j i b u wa K a t i b a ya nchi? Wakati NECTA ikiajiri Mchungaji na wataalamu wa lugha za Kiingereza, Kiswahili na Kifaransa, imegoma pia kuweka Mtaalamu wa Lugha ya Kiarabu na kufanya somo hilo kuratibiwa na mtu asiyejua hata Alifu. Je, huu ndio utaalamu unaotokana na PhD First Class? Moja ya tafiti zinaonyesha kuwa katika somo la Hesabu, mwaka 2011 ili kupata A mtahiniwa alitakiwa kupata alama 75. Lakini mwaka 2012 ili upate A ilikuwa lazima uwe na alama 86 ambayo inaongeza ugumu wa kupata alama kwa point

Al-farouq Seminary Secondary school is seeking for the suitable Headmaster for the school. Qualications: The person should: 1. Be a Tanzanian. 2. Be a holder of at least a degree in Education. 3. Have held the position for not less than three years or have served as a deputy for not less than ve years. 4. Have a proven good track record. 5. Knowledge of Arabic will be an added advantage. A good package would be offered. He should be ready to assume ofce immediately. Applications with C.V and testimonials, should reach the undersigned through emails below on or before 15th June 2013. The Director, P.O.Box.9211.Dar-es-salam. Email: tanzania@direct-aid.org. cc. abuibrahim05@yahoo.com

Vacancy-Headmaster

Bismillahir Rahmanir Rahiim

Zanzibar walilia Benki Kuu, Uraia


Na Mwandishi Wetu
KATIKA hatua hii ya awali ya kuchambua Rasimu ya Katiba Mpya, imedhihirika kuwa Wazanzibari walio wengi, pamoja na kufurahia suala la kuwa na Serikali tatu, wanataka pia wawe na Uraia wao, Uhamiaji, Benki Kuu na Mambo ya Nje. Wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema kuwa kwa mujibu wa mapendekezo ya l i yo t o l e wa , t a k r i b a n mambo yote yanayohusu shughuli zenye gharama kubwa za kila siku za nchi yametolewa katika muungano na kila serikali ya nchi mshirika (Tanganyika na Zanzibar) itaendesha mambo hayo yenyewe. Na kwamba Zanzibar inahitaji mamlaka kamili ili iweze kupanga sera zake na uchumi wake na hivyo kuweza kumudu gharama za mambo lukuki ambayo sasa hayatakuwa chini ya mwamvuli wa muungano. Mambo yanayodaiwa kuwa yakiingizwa katika Katiba yataipa Zanzibar Mamlaka ya kujimudu ni pamoja na Uraia, Uhamiaji, Sarafu na Benki Kuu, Mambo ya Nje na Vyama vya siasa. Pengine kwa kudhani kuwa mambo hayo ni muhimu kwa Zanzibar, baadhi ya watu wameanza kusema kuwa iwapo hayataingizwa, kuna kila sababu ya kupiga kura ya HAPANA Kwa katiba itakayokuja. Kuhusu suala la Uraia na Uhamiaji inaelezwa kuwa mambo haya yakiwa ya muungano, Zanzibar itashindwa kuhimili wimbi la uhamaji na usalama wake kwa kukosa udhibiti wa moja kwa moja wa watu wanaoingia na kufanya makazi ya kudumu. Na kwamba hilo likifanyika, i n a we z a k u f i k i a m a h a l i Zanzibar ikafurika wageni raia na hiyo ikawa njia nyepesi ya kuja na hoja ya nchi moja Serikali moja. Utambulisho wa Mzanzibari na haki zinazofungamana na sera za uraia na Mambo ya Nje, ndio itakuwa basi tena. Tutakosa utambulisho wa nchi yetu nje ya Zanzibar na twabaan tutakosa fursa muhimu kwa sasa za ajira za kibalozi ambazo kwa wibi kubwa la vijana wasomi tulionao vyuoni hili tungeliangalia sana kama ni fursa ya kukuza uchumi na kipato cha mtu mmoja mmoja na jamii kwa jumla. Anasema mmoja wa wachambuzi kama uchambuzi wake ulivyochapishwa katika mitandao ya kamii. Kwa upande wa Benki Kuu na Sarafu inaelezwa kuwa kwa kufanya mambo hayo kuwa ya muungano, Zanzibar itashindwa kupanga na kudhibiti uchumi wake. Uchumi wetu tutategemea pande zote za jamhuri zitengamae kiuchumi eti ndio nasi tufanikiwe, haina maana wenzetu hawawezi kutengamaa najuwa wana rasilimali nyingi, ardhi na watu wengi lakini kwa Zanzibar fursa yake iko karibu kama tutatulia na kuwa huru kufanya maamuzi huru. Tatizo hapa inabidi upande mmoja uchelewe kumsubiri mwengine, hii sarafu ikishuka wote tumeshuka, haijalishi wewe uchumi wako ni imara kwa kiasi gani bado Zanzibar itakuwa hivi hivi kama leo. Hapa muungano huu si dawa kwa Zanzibar kama ilivyo leo. Inasikitisha sana. Amesema mchambuzi huyo. Kuhusu la vyama vya siasa inaelezwa kuwa, muda wote Zanzibar itakuwa inatawaliwa na vyama vilivyo na nguvu Tanganyika hata kama Zanzibar havikubaliki. A n g a l i a m i a k a 1 8 ya siasa za uhasama za kuendekeza uvyama n a Wa z a n z i b a r i k u k o s a mamlaka na kimaamuzi ya kisiasa kulivyoiathiri Zanzibar. Inawezekana kwa Wazanzibari watu wenye utamaduni mmoja, lugha silka na muingiliano barabara tungeona mfumo fulani wa siasa ambao ni wa jamuhuri unatuathiri tungeleta mfumo wa aina yetu kwa mazingira yetu. Leo tutalazimika kufuata tu. hapa patazidisha uhasama na utengano wa Wazanzibari unaoweza kuchochewa na watu wenye nia mbaya ambao wameunganishwa na siasa za vyama watatutilia sumu za kisiasa. Lakini zaidi tutakosa n g u v u ya m a a m u z i ya kuweka wazalendo wetu katika nafasi za Urais (kama sasa maamuzi ya viongozi yanavyofanyika Dodoma) na hili litakuwa na athari kiuchumi, ukishatwezwa nguvu kisiasa unapoteza uzalendo na nguvu zako za kiuchumi.

Habari

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013

AN-NUUR

MAPENDEKEZO YA KAMATI YA MARIDHIANO ZANZIBAR KUHUSU UPI UWE MWELEKEO WA WAZANZIBARI KATIKA KUIJADILI RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ITAKAYOTOLEWA NA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA
UTANGULIZI: Baada ya wananchi wa Zanzibar kutoa maoni yao juu ya vipi Muungano wa Zanzibar na Tanganyika unapaswa kuwa, hatimaye Tume ya Mabadiliko ya Katiba inatarajiwa kutoa rasimu ya awali ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya mwishoni mwa mwezi Mei na mwanzoni mwa mwezi Juni 2013. Wakati tunaisubiri kwa hamu rasimu hiyo itolewe na kujua kilichomo, sisi wa j u m b e wa K a m a t i ya Maridhiano Zanzibar tumekaa na kutafakari juu ya u p i u n a p a s wa k u wa mwelekeo wa Wazanzibari katika kuadili rasimu hiyo pale itakapotoka. Baada ya mashauriano ya kina kati ya wajumbe wa Kamati ya Maridhiano na pia kwa kuwahusisha watu wengine mashuhuri hapa Zanzibar, tumekuja na mapendekezo yafuatayo ambayo leo hii tunayawasilisha kwa wananchi wa Zanzibar kupitia Kongamano hili. Haya si maagizo bali ni mashauri yenu na pindi mkiyakubali basi tutakuombeni tuyafanyie kazi kwa pamoja kwa kuyatumia katika kuipokea na kujadili rasimu pale itakapotolewa. Mapendekezo yetu ni kama ifuatavyo: 1. Jina la Muungano: Muungano huu umetokana na Jamhuri mbili kuungana kwa hiyari. Jamhuri hizo ni Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika. Jina la awali lililotajwa katika Mkataba wa Muungano la muungano wa jamhuri hizi mbili lilikuwa ni Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Jina hili baadaye mwezi Oktoba 1964 lilibadilishwa na kuitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ukiangalia mifano ya nchi nyingine zilizoungana, jina la muungano huweka bayana kwamba zilizoungana ni zaidi ya nchi moja, zaidi ya falme moja au zaidi ya jamhuri moja. Kwa mfano, muungano wa nchi (states) za Marekani unaitwa kwa kiingereza United States of America (USA), ule uliokuwa muungano wa jamhuri za kisovieti ukiitwa Union of Soviet Socialist Republics (USSR) na ule muungano wa falme za kiarabu unaitwa United Arab Emirates (UAE). Ili kuondosha dhana iliyojengeka kwamba muungano wa jamhuri zetu mbili umeunda nchi moja na kuzifuta nchi zetu, Katiba Mpya inapaswa kuweka jina linalotambua msingi huo na historia hiyo. Hivyo basi, jina jipya liwe ni Muungano wa Jamhuri za Tanzania na kwa kiingereza United Republics of Tanzania. Jina hili litasaidia utambulisho wa nchi wanachama katika uwanja wa kimataifa pale litapoambatanishwa katika nyaraka zote rasmi pamoja na jina la nchi husika. Kwa maana hiyo katika uwanja wa k i m a t a i f a n a k a t i k a pasi za kusafiria utaweka wazi na kuwa na UNITED REPUBLICS OF TANZANIA REPUBLIC OF ZANZIBAR na UNITED REPUBLICS OF TANZANIA REPUBLIC OF TANGANYIKA. 2. Mipaka ya Zanzibar na Tanganyika: Wa k a t i z i n a u n g a n a , Zanzibar na Tanganyika zilikuwa tayari ni nchi zenye m a m l a k a k a m i l i z i k i wa ni wanachama wa Umoja wa Mataifa na hivyo kila moja ilikuwa na mipaka yake inayoeleweka. Katiba na sheria za nchi mbili hizi ziliweka bayana mipaka hiyo na mipaka hiyo ilitambuliwa chini ya sheria za kimataifa. Rasimu ya Katiba Mpya ni lazima itamke kwa uwazi kabisa na kutambua na kuheshimu mipaka ya nchi mbili hizi kama ilivyokuwa kabla ya siku ya Muungano tarehe 26 Aprili, 1964. Baada ya hapo, Katiba ya Zanzibar na Katiba ya Tanganyika (itakayotungwa baada ya kupata Katiba mpya ya Muungano) kila moja iweke wazi mipaka yake. 3. Uraia: Uraia ndiyo msingi wa ujananchi. Kwa vyovyote vile Katiba Mpya isumuishe suala la Uraia kuwa la pamoja kupitia Muungano. Kila nchi mwanachama katika muungano ibakie na uraia wake na iratibu masuala yote yanayohusu uraia wake na raia zake. Kwa kufuata mfano kama wa Muungano wa Ulaya (European Union), u n a we z a k u wa n a h a k i inayotambulika kikatiba ya uhuru wa raia wa nchi moja mwanachama kwenda katika nchi nyengine mwanachama kupitia utaratibu maalum utakaowekwa (free movement of people). Hata hivyo, kila nchi mwanachama iwe na haki ya kuweka utaratibu wa vipi raia hao watafaidi haki na fursa za nchi mwanachama nyingine. Hili ni la muhimu hasa kwa nchi ndogo kama Zanzibar ambayo ina rasilimali ndogo ya ardhi na hasa ikizingatiwa kuwa ardhi ilikuwa mojawapo ya sababu kuu za kufanyika Mapinduzi. Katika hali kama hiyo, Zanzibar ina sababu nzito za kuona inadhibiti na kusimamia wenyewe Uraia wake na utambulisho wa raia hao. Hivyo basi, suala la Uraia lisiwemo katika mambo ya Muungano na badala yake kila nchi isimamie yenyewe

Inaendelea Uk. 4

Umesema uchambuzi huo na kutoa wito kwa Wazanzibari kusoma Rasimu ya Katiba kwa undani ili kugundua dosari kama hizo. Kwa hofu hiyo unapigwa mfano wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2000 ambapo katika kura za maoni za mgombea Urais kwa upande wa Zanzibar, waliokuwa wametakiwa na CCM Zanzibar, sio walioteuliwa kugombea Urais. Waliteuliwa waliokuwa na kura chache za Wazanzibari lakini waliokuwa wakipendeza zaidi kwa wana CCM Bara. Baadhi ya ambo yaliyotajwa katika uchambuzi huu wa awali, yanawiana kwa karibu na mapendekezo yaliyotolewa na ile Kamati ya Mzee Moyo. Katika mapendekezo yake kamati hiyo imesema kuwa, Uraia ndiyo msingi wa ujananchi. Kwa vyovyote vile Katiba Mpya isumuishe suala la Uraia kuwa la pamoja kupitia Muungano. Kila nchi mwanachama katika muungano ibakie na uraia wake na iratibu masuala yote yanayohusu uraia wake na raia zake. Kwa kufuata mfano kama wa Muungano wa Ulaya (European Union), u n a we z a k u wa n a h a k i inayotambulika kikatiba ya uhuru wa raia wa nchi moja mwanachama kwenda katika nchi nyengine mwanachama kupitia utaratibu maalum utakaowekwa (free movement of people). Hata hivyo, kila nchi mwanachama iwe na haki ya kuweka utaratibu wa vipi raia hao watafaidi haki na fursa za nchi mwanachama nyingine. Kamati hiyo ikasema kuwa Uraia ni jambo muhimu h a s a k wa n c h i n d o g o kama Zanzibar ambayo ina rasilimali ndogo ya ardhi na hasa ikizingatiwa kuwa ardhi ilikuwa mojawapo ya sababu kuu za kufanyika Mapinduzi. Katika hali kama hiyo, Zanzibar ina sababu nzito za kuona inadhibiti na kusimamia wenyewe Uraia wake na utambulisho wa raia hao. Ikasisitiza Kamati hiyo kuwa, kwa vyovyote itakavyokuwa suala la Uraia lisiwemo katika mambo ya Muungano na badala yake kila nchi isimamie yenyewe masuala ya Uraia. Na kwa sababu hizo hizo ikapendekezwa kuwa hata Uhamiaji, kila nchi iwe na Idara yake ya Uhamiaji. Kamati inasema, kutokana na sababu tulizozitaja hapo juu kuhusiana na suala la Uraia inapelekea wazi kuwa kila nchi mwanachama idhibiti na kusimamia wenyewe mambo ya Uhamiaji. Hivyo b a s i , r a s i m u ya K a t i b a Mpya isijumuishe suala la

Inaendelea Uk. 4

Habari

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013

AN-NUUR

Zanzibar walilia Benki Kuu, Uraia


Inatoka Uk. 3
masuala ya Uraia. Hata hivyo, kunaweza k u k a we p o c h o m b o c h a pamoja kinachojumuisha nchi mbili hizi cha kuratibu masuala ya Uraia na haki na fursa ambazo raia wanaweza kuwa nazo kwa kila upande. 4. Uhamiaji: Kutokana na sababu tulizozitaja hapo juu kuhusiana na suala la Uraia inapelekea wazi kuwa kila nchi mwanachama idhibiti na kusimamia wenyewe mambo ya Uhamiaji. Hivyo basi, rasimu ya Katiba Mpya isumuishe suala la Uhamiaji kuwa ni suala la Muungano. Kila nchi mwanachama kati ya Zanzibar na Tanganyika iwe na paspoti yake yenyewe yenye kubeba jina la nchi yake na nembo yake ya Taifa na yenye kudhamini usalama wa raia wake nje ya nchi kupitia uhakikisho unaotolewa na Serikali ya nchi husika. I l i k u o n e s h a s u r a ya k u we p o m u u n g a n o wa kisiasa, paspoti za nchi mbili hizo zinaweza kuwa na jina la Muungano juu na kufuatiwa na jina la nchi mwanachama likiambatana na nembo ya Taifa ya nchi hiyo. Kwa mfano, UNITED REPUBLICS OF TANZANIA ZANZIBAR PASSPORT na UNITED REPUBLICS OF TANZANIA TANGANYIKA PASSPORT. Kwa upande mwengine kunaweza kukawa na mamlaka ya kuratibu masuala ya uhamiaji wa nchi hizi mbili (Union immigration regulatory authority) kwa lengo la kuweka na kuratibu mfumo mzuri wa mawasiliano kati ya mamlaka za uhamiaji za nchi mbili hizi. 5. Mambo ya Nje: Mamlaka juu ya mambo ya nje na uwezo wa nchi kuingia mikataba na nchi nyingine na mashirika ya kimataifa ndiyo roho ya nchi yoyote duniani kutambulika kimataifa na kuweza kusimamia mamlaka yake ya ndani yanapohitaji mashirikiano na nchi nyengine. Ili nchi iweze kutambulika kimataifa inapaswa kuwa na mambo manne yafuatayo: (a) Eneo la ardhi lenye mipaka inayotambulika; (b) Wa t u w a n a o i s h i kwenye eneo hilo wanaojitambulisha na eneo hilo; (c) Serikali inayotekeleza majukumu yake; na (d) Uwezo wa kuingia katika mahusiano ya kimataifa na nchi nyengine. Kwa msingi huo, Wazanzibari wanahitaji kuona kuwa Mambo ya Nje haumuishwi katika orodha ya mambo ya Muungano

Uhamiaji kuwa ni suala la Muungano. Wa k a t i h u o huo, wasiotaka Mamlaka kamili ya Serikali na Dola ya Zanzibar, wametakiwa kujitokeza hadharani kama ilivyo kwa wanaopigania mambo hayo. H a yo ya m e s e m wa n a Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akiunga mkono kauli iliyotolewa awali na Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar Eddi Riyami ya kuwataka Wa z a n z i b a r i wa s i o t a k a mamlaka kamili ya Zanzibar wajitokeze hadharani kama wanavyofanya wale wanaodai mamlaka kamili ya Zanzibar. Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF ametoa wito huo katika viwanja vya Kibanda maiti mjini Zanzibar katika mkutano wa hadhara uliolenga kusherehekea Umoja wa Wazanzibari ulioasisiwa kufuatia maridhiano ya kisiasa. Maalim Seif amesema, hatua ya Wazanzibari kudai mamlaka ni haki yao, na kwamba hakuna dhambi ya kudai jambo hilo. A m e f a h a m i s h a k u wa Wazanzibari walio wengi wameungana kudai mamlaka ya nchi yao kwa njia ya amani na demokrasia, na kutoa wito kwa wale wasiotaka mamlaka ya Zanzibar wajitokeze hadharani. Amewahakikishia wananchi kuwa hatorudi nyuma katika kuitetea Zanzibar kuwa na mamlaka yake, ili iweze kutambulika kimataifa na kuweza kuratibu na kushughulikia mambo yake ya nje. Kwa upande wake Katibu wa kamati ya maridhiano Ismail Jussa Ladhu, amewaomba viongozi wa vyama vyote kushirikiana na wananchi katika kudai mamlaka ya nchi, ili Wazanzibari waweze kujikomboa kutokana na kile alichokiita ukoloni wa Tanganyika. Katika risala ya wananchi wa mikoa mitano ya Zanzibar iliyosomwa na Ameir bin A m e i r k u t o k a B we j u u , amesema pamoja na mambo m e n g i n e , k a t i b a m p ya izingatie uwepo wa Jamhuri ya Zanzibar na uraia wake. Mambo mengine waliyotaka yatolewe katika orodha ya mambo ya Muungano ni pamoja na sarafu, Benki Kuu, Mambo ya Nje, vyama vya siasa, Baraza la Mitihani pamoja na mafuta na gesi.

Inatoka Uk. 3

M A P E N D E K E Z O Y A K A M AT I Y A MARIDHIANO ZANZIBAR KUHUSU UPI U W E M W E L E K E O WA WA Z A N Z I B A R I KATIKA KUADILI RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ITAKAYOTOLEWA NA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA
na badala yake kila nchi isimamie yenyewe mamlaka yake juu ya mambo ya nje. Hata hivyo, uratibu wa sera ya mambo ya nje (foreign policy coordination) inaweza kuwa ni suala la muungano lakini utekelezaji wake kila nchi ikausimamia kupitia Wizara yake ya Mambo ya Nje. Uratibu wa sera ya mambo ya nje unaweza kufanywa kupitia chombo cha pamoja kitakachoundwa na Wizara za Mambo ya Nje za nchi mbili hizi kwa mfano kuwa na Council on Foreign Policy. Kutokana na hoja hizo hapo juu inabaki kuwa kila nchi iwe na uanachama na kiti chake katika Umoja wa Mataifa na jumuiya nyengine za kimataifa. Hayo si ajabu katika miungano. Umoja wa Jamhuri za Kisoshalisti za Kisovieti (USSR) ulikuwa na uanachama na kiti chake Umoja wa Mataifa lakini miongoni mwa nchi wanachama, Jamhuri tatu za Ukraine, Belarus na Georgia ziliamua kuwa na uanachama na viti vyao katika Umoja wa Mataifa na hilo liliwezekana. Kwa msingi huo huo, Zanzibar iwe na uanchama wa k e k a t i k a U m o j a wa Mataifa, Umoja wa Afrika, Jumuiya ya Madola, Jumuiya ya Afrika Mashariki, Jumuiya ya SADC na jumuiya nyengine za kikanda na za kimataifa. 6. Sarafu, Benki Kuu, Mikopo na Biashara ya Nchi za Nje, Ushuru wa Forodha, Kodi ya Mapato na Kodi ya Mashirika: Uchumi si suala la Muungano hata katika Katiba inayotumika sasa. Hata hivyo, nyenzo za kuendeshea na kusimamia uchumi wa nchi kwa maana ya sera za fedha na uchumi (scal and monetary policies) zimeendelea kudhibitiwa kupitia Serikali ya Muungano. Vyombo vikuu vinavyosimamia sera hizo ambavyo ni Benki Kuu (BOT), Mamlaka ya Kodi Tanzania (TRA) na Wizara ya Fedha ya Serikali ya Muungano vimekuwa vikifanya maamuzi na kuyatekeleza bila ya kuzingatia kuwa kwa maumbile uchumi wa Zanzibar ambao ni uchumi unaotegemea utoaji wa huduma (service oriented economy) hauwezi kuwa sawa na uchumi wa Tanganyika ambao unategemea rasilimali (resource based economy). Sera za fedha na uchumi zikiwemo zile zinazohusu udhibiti wa sarafu na viwango vya kodi, ushuru na riba katika mabenki zimekuwa zikitungwa bila ya kuzingatia msingi huo wa chumi mbili zilizo tofauti na badala yake mara zote zimeegemezwa kwenye kulinda maslahi ya uchumi wa Tanganyika. Sarafu ya pamoja imekuwa ikishuka thamani kwa kasi kila uchao kutokana na sababu nyingi lakini miongoni mwake zaidi zinatokana na uendeshaji mbaya wa uchumi wa Tanganyika. Serikali inapochapisha sarafu zaidi ili kudhibiti mfumko wa bei athari zake zinaikumba pia Zanzibar. Zanzibar inahitaji kujikomboa kiuchumi ili iweze kutekeleza malengo ya Mapinduzi kwa wananchi wake na hivyo inahitaji kuwa na mamlaka yake kamili katika kusimamia masuala ya sera za fedha na uchumi yakiwemo masuala yote yanayohusu sarafu, viwango vya kodi na ushuru pamoja na riba katika mabenki, mikopo na biashara ya nchi za nje. Kutokana na hali hiyo, masuala ya sarafu, benki kuu, mikopo na biashara ya nchi za nje, ushuru wa forodha, kodi ya mapato na kodi ya mashirika kila nchi inapaswa iyasimamie yenyewe. 7. Polisi: Pamoja na kuwemo katika mambo ya awali ya Muungano lakini uendeshaji wa Polisi u m e k u wa n a m a t a t i z o yake katika muungano. Miaka yote Polisi Zanzibar imekuwa ikilalamika kuwa inachukuliwa kama vile ni Mkoa tu na hata bajeti na mahitaji yake mengine yanachukuliwa hivyo hivyo na makao makuu ya Polisi yaliyopo Dar es Salaam. Katika nchi nyingi duniani Polisi ambayo inashughulika na usalama wa raia na mali zao imekuwa ikiendeshwa chini ya Serikali za Manispaa na hata Majimbo seuze kwa nchi kama ilivyo Zanzibar. Ukiondoa mishahara na bajeti ndogo ya uendeshaji inayotolewa na makao makuu ya Polisi, gharama nyengine za uendeshaji wa polisi kwa Zanzibar zimekuwa zikichangiwa na mamlaka za Zanzibar ikiwemo Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB). Hivyo basi, wakati umeka kuona mamlaka kuhusu Polisi yanaondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano na kila nchi ishughulikie yenyewe Polisi yake. 8. Mafuta na Gesi Asilia (pamoja na maliasili nyengine zote):

Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kwa niaba ya Wazanzibari lilishafanya m a a m u z i m we z i A p r i l i 2009 kuyaondoa masuala ya mafuta na gesi asilia kutoka kwenye orodha ya mambo ya Muungano. Mbali na maazimio ya Baraza la Wawakilishi, masuala ya mafuta na gesi asilia yanahusu uchumi ambalo si suala la Muungano. Katiba Mpya haipaswi kuyajumuisha masuala hayo mawili (pamoja na maliasili nyengine kwa ujumla) kuwa mambo ya Muungano. Hivyo basi, rasimu yoyote itakayoyajumuisha masuala hayo ya Mafuta na Gesi Asilia (pamoja na maliasili nyengine zote kwa ujumla) kuwa masuala ya Muungano haitakubalika kwa Wazanzibari. 9. Vyama vya Siasa: M u u n g a n o u l i u n d wa n a J a m h u r i y a Wa t u wa Zanzibar na Jamhuri ya Ta n g a n y i k a k u p i t i a serikali zao. Mazungumzo yaliyopelekea muungano huo na hata utekelezaji wa hatua za kuunganisha nchi mbili hizi katika muungano hayakuhusisha vyama vya siasa vya wakati huo, ASP kwa upande wa Zanzibar na TANU kwa upande wa Tanganyika. Ndiyo maana kwa miaka 13 ya Muungano (kuanzia 1964 hadi 1977) kila nchi kati ya nchi mbili hizi iliendelea kuongozwa na chama chake cha siasa. Moja kati ya dhoruba kubwa dhidi ya makubaliano ya asili ya muungano huu ambayo ni Mkataba wa Muungano ilikuwa ni kuunganisha vyama vya siasa vya ASP na TANU na kuunda CCM ambacho kilitangazia kushika hatamu na kuwa juu ya vyombo vyengine vyote vya nchi zikiwemo Serikali. Utaratibu huo uliingizwa ndani ya Katiba za nchi na hivyo kuuhalalisha kisheria. Tokea wakati huo, Zanzibar imekosa mamlaka ya kisiasa ya kufanya maamuzi yake kwa mambo yanayoihusu. Na pale ilipofanya hivyo ilifanya kwa kutegemea na kujiamini kwa uongozi uliopo Zanzibar ingawa majaribio ya kutumia nguvu ya vyama kuzuia maamuzi kama hayo yamekuwa yakifanyika na baadhi ya wakati kufuzu. Maongozi ya nchi yoyote yanategemea historia, mila na utamaduni wa watu wa nchi husika. Kwa msingi huo basi, na ili Zanzibar iweze kurejesha mamlaka yake ya kisiasa katika kufanya na kusimamia maamuzi kwa mambo yake, rasimu ya Katiba haipaswi kujumuisha suala la vyama vya siasa kuwa ni jambo la Muungano. Zanzibar na Tanganyika kila moja iweze kuandikisha vyama vyake vya siasa. 10. U t a r a t i b u w a uendeshaji wa Mambo ya Inaendelea Uk. 5

Habari za Kimataifa

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013

AN-NUUR

WA N A H A R A K AT I w a Hizbullah nchini Lebanon wamewaangamiza waasi 20 wanaopigana dhidi ya serikali ya Syria nchini Lebanon. Habari zinasema, wanamgambo hao wameuawa katika mapigano yaliyotokea Jumapili iliyopita mjini Balabak, kusini mwa Lebanon. Awa l i wa a s i h a o wanaopambana dhidi ya serikali ya Syria waliushambulia mji huo kwa maroketi kutoka katika maeneo ya mpakani ya Syria na kusababisha uharibifu wa mali.

Hizbullah waangamiza waasi 20 Lebanon Tanzania yaiomba Japan kusaidia masomo ya sayansi na hisabati
Aidha siku ya Ijumaa waasi hao waliyashambulia kwa maroketi 14 maeneo ya Nabi Shith na Nasiriya, yaliyo karibu na mji wa Balabak upande wa mashariki mwa Lebanon. Kuendelea mashambulizi ya waasi dhidi ya maeneo ya mpakani ya Lebanon, yamewatia hasira kubwa raia wa nchi hiyo. Hali hiyo imewalazimu v i o n g o z i wa H i z b u l l a h kutoa onyo kwa waasi hao n a k u b a i n i s h a k wa m b a hawarudi nyuma kutokana na vitisho vyao. Hivi karibuni Naibu wa Baraza la Utendaji la Wanarakati hao, Sheikh Nabil Kaouk, alinukuliwa akisema kuwa mashambulizi ya waasi wa Syria dhidi ya maeneo ya mpakani ya Lebanon hayawezi kuwafanya wanaharakati hao kubadili mwelekeo wake kuhusiana na masuala ya Syria.

MAPENDEKEZO YA K A M AT I YA MARIDHIANO ZANZIBAR


Inatoka Uk. 4 Muungano: Kwa yale mambo yatakayokubaliwa kubaki katika Muungano kama vile: Katiba ya Muungano wa Jamhuri za Tanzania; Serikali ya Muungano wa Jamhuri za Tanzania; Uratibu wa Sera ya Mambo ya Nje; Ulinzi; Usalama; M a m l a k a j u u ya mambo yanayohusika na hali ya hatari; Utumishi katika Serikali ya Muungano wa Jamhuri za Tanzania; na Mahkama ya Rufani ya Muungano wa Jamhuri za Tanzania. Utaratibu wa uendeshaji wake uwekwe wazi katika Katiba kwamba maamuzi yote yatafanywa kwa mashauriano na makubaliano kati ya nchi mbili zinazounda Muungano huu na yatakuwa halali tu iwapo yatafuata msingi huu. HITIMISHO: Haya kimsingi ndiyo mapendekezo yetu Kamati ya Maridhiano. Tunayaleta kwenu muyapokee, muyajadili na kuwaomba muyaridhie ili yawe ndiyo msingi wa mwelekeo wa wananchi wa Zanzibar ambao wengi wao waliojitokeza mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba walitaka nchi yao iwe na mamlaka kamili. Kwa mapendekezo haya, tunadhani Zanzibar na Tanganyika zitaendelea kuwa na mashirikiano ya kidugu kupitia mfumo mpya wa Muungano na wakati huo huo kila nchi mwanachama wa muungano ikibaki na mamlaka yake kamili katika yake maeneo ya msingi ambayo kila nchi hupenda kuwa nayo. Imetolewa: Zanzibar 25 Mei, 2013

vyama mbalimbali vya upinzani nchini Misri wamepinga ujenzi wa bwawa kwenye mto Nile nchini Ethiopia. Wa j u m b e h a o walifikia uamuzi wa k u i z u i a s e r i k a l i ya Ethiopia isenge bwawa kwenye maji ya mto Nile kufuatia kikao kilichoitishwa na Rais wa Misri, Mohamed Morsi mapema wiki hii, kujadili hatua ya hiyo jirani kutaka kujenga bwawa hilo. Ta a r i f a z i n a e l e z a kuwa kiongozi mmoja wa upinzani nchini Misri amesema kuwa, kadhia ya ujenzi wa bwawa hilo ni ya kitaifa hivyo kuyataka makundi yote nchini humo yashikamane kwa lengo la kutafuta njia za kuutatua mgogoro huo. Kikao hicho pia kimesisitiza juu ya kufuatwa sheria na taasisi za kimataifa kwa lengo la kuizuia Ethiopia isenge bwawa hilo, ambalo huenda likaziathiri Misri na Sudan katika sekta ya kilimo. Aw a l i R a i s Mohammad Morsi wa

CAIRO Taarifa kutoka Cairo zinasema kuwa, viongozi wa serikali na wakuu wa

Misri wapinga ujenzi wa bwawa Ethiopia


Misri, alivitaka vyama vyote vya kisiasa vikiwemo vya upinzani, kujadili mkakati wa Ethiopia wa kujenga bwawa kwa kutumia maji ya Mto Nile. Rais Morsi aliwaalika wanasiasa na viongozi wa taasisi mbalimbali nchini humo kuketi pamoja mapema Jumatatu kujadili kwa kina mpango huo wa Ethiopia, ambao huenda ukaathiri sekta ya kilimo katika nchi za Misri na Sudan. Hata hivyo baadhi ya viongozi wa vyama nchini humo wameripotiwa kukataa

TOKYO S e r i k a l i y a Ta n z a n i a imeiomba Japan kusaidia walimu wa hisabati na sayansi namna ya kufundisha walimu wa masomo hayo, kama njia ya kukabiliana haraka na uhaba mkubwa wa walimu wa masomo hayo nchini. Rais Kikwete alisema kuwa moja ya changamoto kubwa zinazoikabili sekta ya elimu nchini, ni ukosefu

wa walimu wa hisabati na sayansi, masomo ambayo ni msingi muhimu wa maendeleo ya nchi. Ombi hilo kwa Japan l i m e t o l e wa J u m a t a t u wiki hii, wakati Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Shirika la Ushirikiano na Misaada ya Kimataifa la Japan ( JICA), Dakta Akihiko Tanaka, mjini Yokohama. Aidha Rais Kikwete

ameiomba Japan kusaidia uchapishaji wa vitabu vya sayansi na hisabati, ili kuhakikisha kuwa kila mwanafunzi wa Tanzania anakuwa na nakala ya vitabu vya masomo hayo kama njia ya kuongeza ubora wa elimu nchini. Rais Kikwete alikuwa Japan kwa ziara ya siku saba kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Tano wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD), ambao umemalizika Jumanne wiki hii.

wito wa kushiriki katika kikao hicho. Uamuzi wa ghaa wa Ethiopia wa kubadilisha mwelekeo wa maji ya mto Nile kwa lengo la kujenga bwawa la al Nahdha, umezusha hofu kubwa kwa viongozi na wananchi wa Misri na Sudan.

Ahlul Daawa Hajj And Travel Agency


Inawatangazia Waislamu wote Kuwa Imeandaa Safari ya Hijja Mwaka 2013 Sawa na Mwaka 1434 Hijria kwa Dola US$ 3550 tu. Umra kwa Mwezi wa Ramadhani itakuwa ni Dola US$ 1995 Fomu zinapatikana katika osi zifuatazo:1. Osi ya Ahlul Daawa Dar es salaam Mtaa wa Dosi na Mkadini Nyumba Namba 26 Mkabala na Showroom ya Magari Tel 0713 730 444, au 0773 804101 au 0785 930444 na 0773 930444. 2. Osi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo Tel 0777 484982 au 0777 413 987. 3. Abubakar Maulana wa Markaz Kiwalani Dar es salaam 0784 453838 4. Abdallah Salehe Mazrui ( HOKO) Dar es salaam 0715 724 444 5. Salim Is-haq Dar es salaam 0754 286010 au 0774 786101 6. Dukani kwa Abdala Hadh Mazrui wete pemba 0777 482 665 7. Dukani kwa Mohamed Hadh Mazrui Mkoani Pemba 0777 456911 8. Sheikh Daudi khamis sheha 0777 679692 9. Maalim Seif Humoud Hamed Kijichi Zanzibar 0777 417736 Wahi kulipia. Osi ya Ahlul Daawa Dar es salaam 0713 730 444 au 0773 804101 au 0785 930444. Osi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo 0777 484982 au 0777 413 987. Maalim Seif Humoud Hamed Kijichi Zanzibar 0777 417736 Sheikh Salim Mohamed Salim 0774 412974 au Kupitia A CCOUNT NAMBA 048101000030 NBC Tanbih: Atakae maliza Taratibu zote kuanzia sasa Mpaka 15 July 2013 atapata Punguzo la asilimia 16% atalipia $ Dola 2982 tu. Atakae maliza Taratibu zote kuanzia Tarehe 16-july Hadi Tarehe 15 Augost 2013 atapata Punguzo la Asilimia sita 6% atalipia Dola $3337 tu. Kutakuwa na umra ya utangulizi kabla ya Umra ya Hijja kwa atakae maliza kufanya hivyo. Atakae maliza taratibu zote mwanzo ndie atakae shughulikiwa mwanzo. Ukilipia kwa njia ya Account kwanza piga simu 0774 412975. Kumbuka Kikundi cha Ahlul Daawa Kwa Bei nafuu kuliko wote na Huduma bora Kuliko wengi. Nyote mnakaribishwa

6
Na Shaaban Rajab
MATUKIO ya jeshi la polisi kuhusishwa na vitendo vya uhalifu nchini yamezidi kushika kasi nchini. Ni jambo linalofahamika kwamba kazi kubwa ya jeshi la polisi, ni kulinda usalama wa watu na mali zao na kuzua vitendo vyote vya kihalifu nchini. Hayo ndio majukumu ya msingi ya kuhalalishwa kuwepo jeshi hilo. Kutokana na majukumu hayo ya kiusalama ya jeshi letu la polisi, wananchi waliwaamini, kuwaheshimu na kuwategemea sana kiulinzi na kiusalama. Hata hivyo kadiri siku zilivyokuwa zikisonga mbele, jeshi hili limezidi kuporomoka kimaadili na kiutendaji, hali inayowafanya wananchi kukosa imani na jeshi hilo. Tamaa ya fedha kwa baadhi ya askari na watendaji wa ngazi za juu wa jeshi hilo imekuwa sababu kubwa ya chombo hiki kuyumba kiufanisi na kutiliwa mashaka. Rushwa inayotokana na tamaa ya kupata fedha au maslahi kwa njia za mkato, imewafanya askari wengi katika jeshi hilo kuweka pembeni wajibu wao wa msingi kwa wananchi na kujiingiza katika vitendo vya kihalifu. Badala ya kuwa vinara wa kupambana na uhalifu, sasa wamekuwa vinara wa kutumia sare za jeshi kuchuma chumo h a r a m u . Wa n a d h u l u m u , wanapora, wanabambikia watu kesi, wanaonea na kutesa watuhumiwa. Ile kazi ya msingi ya kuzuia uhalifu imekuwa ni chaguo la pili katika utendaji wa kazi zao. Ni hivi karibuni tu, gari la mkuu wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoa wa Arusha, lilikamatwa huko Himo Mkoani Kilimanjaro likisarisha bangi magunia 18 kwenda Tarakea Rombo. Habari zilizothibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz, zilipasha kuwa gari hilo lilikamatwa siku ya Jumamosi majira ya saa 4:00 usiku. Tukio hili linaonyesha ni jinsi gani baadhi ya askari wa jeshi letu la Polisi, tena wengine wakiwa ni vigogo katika jeshi hilo badala ya kuzuia uhalifu, wao ndio vinara wa uhalifu wenyewe. Jambo la kushangaza ni kwamba, hata yule askari dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo, naye ameripotiwa kutoroka akiwa mikononi mwa polisi wenyewe baada ya kukamatwa. Bila shaka utoro wa askari huu, hauwezi kuacha kuleta dhana za kuhusika kigogo ndani ya jeshi hilo katika tukio hilo. Siku za nyuma kidogo, Jeshi hilo mkoani Morogoro liliingia kwenye kashfa nzito baada ya askari wake watatu kukamatwa wakiwa na kichwa cha binadamu. Tukio hilo lilitokea Mei 7 mwaka huu katika eneo la Mgudeni huko Dumila wilayani Kilosa. Taarifa zinaelezwa kuwa polisi hao kwa kushirikiana na raia, walikwenda nyumbani kwa

MAKALA

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013


kujiingiza katika uhalifu na wasijulikane wamechukuliwa hatua gani, umeka wakati sasa tuseme basi. Aibu zinazoendelea kulikumba jeshi letu zikome. Kuna haja ya serikali kuchukua hatua za makusudi na za haraka kulisasha jeshi letu la polisi na mapema. Kwanza kwa kuundwa chombo maalum cha kushughulia jinai zinazofanywa na baadhi ya maosa na watendaji wa jeshi hili. Haja hii ni muhimu kwa kuwa uzoefu unaonyesha kuwa kutokana na mfumo ulipo, ni vigumu sana wahalifu ambao ni watendaji wa jeshi la polisi kukamatwa na kuhukumiwa kwa uhalifu wao. Hali hii inatokana na ukweli kwamba polisi ni chombo kilichopewa mamlaka kisheria kuchunguza, kukamata, kushtaki na kuendesha mashtaka kwa wahalifu. Katika mazingira haya ni vigumu wao wenyewe kujichunguza, kujikamata, kujishtaki, kujiendeshea mashtaka pale wanapohusishwa na matukio ya kihalifu. Katika mazingira haya ni vigumu sana kupatikana ushahidi wa kutosha wa kuwatia hatiani, kwa kuwa ni rahisi kwao kuchelewesha, kuvuruga, kuharibu, kupotosha na hata kupoteza ushahidi dhidi ya watu wao wenyewe, hivyo kusababish ugumu wa wahusika kupatikana na hatia na kuihumumiwa. Katika mfumo huu, ni vigumu kuwatia hatiani vigogo wanaofanya biashara ya bangi, wanaopora fedha kwa wafanyabiashara, wanaoklula rushwa, wanaodhulumu kwa nguvu na hata wale wanaoua. Kuna haja serikali kuunda FBI yake maalum inayojitegemea, chombo ambacho kitakuwa hakina mahusiano na chombo kingine chochote cha nguvu za dola, ambacho kazi yake kubwa itakuwa ni kuchunguza, kukamata na kuwashtaki watendaji wa vyombo vingine vya nguvu za dola nchini kama polisi. Biashara ya makamanda au maosa wa ngazi za juu polisi kufanya makosa katika vituo vyao, halafu adhabu yao iwe ni kuhamishwa makao makuu bila kazi ya kueleweka, hiyo siyo dawa sahihi ya kurekebisha hali. Aidha kuwafukuza tu wale askari wanaokutwa na makosa ya kihalifu au utovu wa nidhamu sio suluhu ya kuzuia uhalifu ndani ya jeshi letu. Lazima kiundwe chombo maalum cha dola kitakachojitegemea kwa ajili ya kuwawajibisha watendaji hawa wajeshi la polisi. Kwa kufanya hivyo nidhamu uadilifu ya jeshi hili utarejea na vitendo vya watu wao kujihusisha na vitendo vya kihalifu vitapungua kama sio kukoma kabisa. Na hapa ndipo wananchi waterejesha imani yao iliyopotea kwa jeshi hili.

AN-NUUR

mfanyabiashara aliyetajwa kwa jina la Samson Mura na kutaka kumbambikizia kesi ya mauaji. Polisi hao walidaiwa kuwa waliomba shilingi milioni 25 kutoka kwa mfanyabiashara huyo, ili wasimpeleke kituoni, kwa kosa hilo la kubambika. Harakati zote hizo bila shaka zinatokana na tamaa ya kupata fedha kwa njia haramu ya kutumia vibaya nafasi zao. Mei mwaka huu, jeshi la polisi pia liliingia katika kashfa hizo hizo za kihalifu, pale askari wake walipotuhumiwa kushirikiana na wafanyabiashara wanaokwepa kodi na maafisa wa Mamlaka ya Kodi-TRA, kuingiza bidhaa kupitia njia za panja za pwani ya bahari ya Hindi, yaani pwani ya Dar es Salaam na Bagamoyo. Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ilitangaza kuwakamata askari wake 16 kwa tuhuma za kushiriki na kupokea rushwa kutoka kwa wafanyabiashara wa magendo wanaovusha bidhaa zao kupitia bandari bubu kandokando ya Bahari ya Hindi na maeneo mengine. Hatua hiyo ilitokana na kubainika kuwa baadhi ya askari wametengeneza mtandao ulioanzishwa zaidi ya miezi sita kwa kushirikiana na baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ambao hukusanya fedha kinyume cha sheria kutoka kwa wafanyabiashara wasiotaka kulipa ushuru halali Serikalini. Si hayo tu katika tukio jingine, baadhi ya polisi walidaiwa kuhusika katika upotevu wa fedha zinazokadiriwa kufikia milioni 150 katika tukio la ujambazi lililotokea Kariakoo jijini Dar es Salaam. Katika tukio hilo lililotokea Desemba mwaka jana, Jeshi la

Polisi kichaka cha uhalifu?


Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam liliwashikilia askari Polisi watano kwa tuhuma za kuhusika na upotevu wa fedha hizo zilizokuwa zimeporwa na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi eneo la Kariakoo, ambapo ilidaiwa majambazi hao walipozidiwa nguvu walizitupa fedha hizo na kukimbia na polisi kuziokota. Watu watatu walipoteza maisha kwa kupigwa risasi na majambazi katika eneo la tukio hilo. Aidha kuna wakati iliripotiwa kuwa dawa za kulevya (unga) uliokuwa umekamatwa na jeshi hilo, ulipungua kilo kadhaa kuliko kiasi kilichokamatwa, na umebainika kupungukia mikononi mwa jeshi la polisi ambako huhifadhiwa kama kidhibiti. Ukiacha matukio hayo haramu, Polisi pia wanatuhumiwa kukithiri katika vitendo vya rushwa katika kutoa huduma yao kwa wananchi hususan katika vituo (posts). Siku hizi vituo vingi vya polisi vimegeuzwa ofisi za kuchuma chumo haramu kwa mshitaki na mshitakiwa. Mchezo unaofanyika ni kwa mlalamikaji kutoa pesa ili kupata haki na mlalamikiwa naye kutoa fedha ili kupindishwa haki. Polisi wa usalama barabarani nao wanatuhumiwa vikali kwa rushwa kupitia vyombo mbalimbali vya usafiri na usarishaji. Kuna tuhuma kwamba hata kile kiasi cha fedha za rushwa zinazopatikana barabarani huwafikia pia hata wakubwa maosini. Kwamba kuna hesabu fulani ambayo kila askari wa usalama barabarani, analazimika kupeleka kwa wakuu kila siku. Katika hali hii, usalama barabarani umekuwa dhulma

ASKARI Polisi wakiwa katika moja ya operesheni ya kutuliza ghaa

barabarani. Kwa staili hii, ni wazi kwamba hata yale makusanyo ya faini halali kwa wakosaji barabarani, yatakuwa ni kiduchu ikilinganishwa na kiasi kinachoishia mifukoni mwa askari hao na serikali kuambulia pato haba. Lakini ni polisi hao hao ambao hufanya kazi yao kwa weledi na uhodari kabisa, pale wanapopewa jukumu la kuthibiti mikutano ya hadhara ya kisiasa, mihadhara ya kidini au maandamano. Hapa wanaonyesha ufundi wao wa kudhibiti raia wasiokuwa na silaha kiasi cha kupiliza hata kuua. Haya ni baadhi tu ya matukio ya kihalifu, ambayo Jeshi letu la polisi limekuwa likihusishwa nayo. Matukio ya namna hii ndio yanayochochea zaidi wananchi kujichukulia sheria mikononi. Yote haya ni kwasababu kwa ushahidi wa matukio kama haya, wananchi wanafikia mahali wanakosa imani na utendaji wa jeshi lao. Lakini pia inaonekana kuwa jeshi la polisi limekuwa likitumika zaidi kisiasa. Hasa kwa kuzingatia kwamba jeshi letu limekuwa likitumia nguvu na vifaa vingi kudhibiti watu wanaoshiriki katika matukio ya kisiasa kama maandamano na mihadhara, kuliko yale ya kihalifu. Pamoja na askari wa jeshi la polisi mara kwa mara kuhusishwa na vitendo vya kihalifu, lakini mara nyingi askari wanaotuhumiwa kuhusika na uhalifu, kesi zao hazijulikani zinaishia wapi na wala hakuna taarifa zinazotolewa kwa umma kuhusu hatua walizochukuliwa dhidi ya watuhumiwa hao na hatma yao imekia wapi. Ili kukomesha mazea haya ya vyombo vya nguvu za dola

7
Na Shaaban Rajab. RAIS Barack Obama wa Marekani, anatarajiwa kuzuru nchini Julai Mosi mwaka huu. Hivi sasa serikali ipo katika harakati kubwa za maandalizi ya ujio wa mgeni huyo, ambaye tumeelezwa kuwa atatua nchini na ujumbe usiopungua watu 700. Huyu ni Rais wa tatu wa Marekani kuzuru nchini achilia mbali Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Taifa hilo kubwa. Kabla ya kuja Rais Obama, Juni 11 hadi 13, 2011, aliyekuwa Waziri wake wa Mambo ya Nje Bi. Hillary Clinton, ambaye pia ni mke wa Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton, naye alizuru nchini kwa ziara ya siku tatu. Kwa mara ya kwanza Rais wa Marekani kuzuru Tanzania tangu utawala wa marais 45 waliowahi kuliongoza Taifa hilo kubwa, ni Rais mstaafu Bill Clinton. Clinton alizuru nchini Agosti 27, 2000 kwa lengo la kushuhudia utiaji saini mkataba wa amani wa kumaliza mzozo nchini Burundi, haa iliyofanyika jijini Arusha ambapo msuluhishi mkuu wa mzozo huo alikuwa ni Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela. Hata hivyo katika ziara hiyo, mwenyeji wake alikuwa ni Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin William Mkapa. Pamoja na kwamba Tanzania ni nchi inayosika kwa amani na utulivu na ukarimu wa watu wake duniani kote, hilo halikuifanya Marekani kuiamini. Kabla ya kuja Clinton m a z i n g i r a y a Ta i f a yalibadilika. Makachero wa Marekani walitamalaki karibu maeneo yote nyeti ya Taifa letu. Tunakumbuka hata pale alipotua uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, kabla ya kuondoka uwanjani hapo na mwenyeji wake Rais Mkapa, mbwa wa Kimarekani walikagua barabara gari la kifahari alilotumia Rais wetu, chini ya ulinzi mkali wa makachero wa Marekani. Ulinzi wa serikali yetu uliwekwa kando. Mbwa aliokuja nao Clinton walinusa kila kona ya gari la Rais wetu, huku Maofisa wetu wa Usalama wa Taifa na viongozi wetu wakiwa kimya kando kushuhudia. Katika ziara hiyo, pamoja na kwamba Bw. Clinton alikuja kwa uzito wa jukumu la Burundi, lakini katika hali ya kushtusha kidogo, tulisikia kwamba Rais wetu Mkapa na Rais Clinton tayari wameshatiliana saini mkataba wa anga huru. Fursa ambayo Marekani imekuwa ikipata wakati mgumu sana kuridhiwa na mataifa mengine yanayofahamu vyema sera na tabia za ndani za Taifa hilo.

Makala/Matangazo

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013


Taifa hilo kubwa kuzuru nchini. Shida ni bughudha wanazopata baadhi ya watu wasio na hatia kwa sababu ya ugeni huo. Ikizingatiwa kwamba tayari kuna wimbo wa ugaidi unaovuma Zanzibar na Arusha, na ikizingatiwa kuwa makachero wa Marekani walishaombwa na serikali kusaidia kuchunguza kubaini watuhumiwa wa ugaidi huo, kuna dalili ya kurejea zile kadhia za kukamatwa Masheikh, simu kudhibitiwa hasa katika maeneo atakapokuwa au kupita mgeni huyo kama ilivyokuwa alipotua Bush. Lakini linalotia hofu zaidi ni falsafa ya Taifa hili kubwa, kwamba hawana raki wa kudumu wala adui wa kudumu, ila maslahi ya kudumu. Taifa hili lenye nguvu kubwa ya kiuchumi duniani, limejijengea sifa ya kutokuwa na uraki wa kuaminika kama hakuna maslahi hasa ya kiuchumi. Yanapokosekana maslahi haya, na uswahiba ni muhali kudumu kama ilivyodhihiri utawala wa enzi za Saddam Hussein wakati akiiongoza Iraq, uswahiba dhidi ya Pakistan. Kutokana na falsafa hiyo kongwe kwa Taifa hilo, ziara za White House nchini, zinaweza kuwa na sura ya uraki tu. Lakini pia inawezekana kabisa nyuma ya pazia yakalengwa maslahi makubwa, ambayo ni zaidi ya maslahi watakayopata Watanzania na serikali yao. Ifahamike tu kwamba kugunduliwa hazina kubwa ya gesi na uranium ukanda wa Kusini ni moja ya vivutio vikubwa kwa mataifa ya kibeberu.

AN-NUUR

Lakini serikali yetu haikuona sababu ya kutafakari kwa kina juu ya hatua hiyo kabla ya kukia maamuzi. Ziara ya Clinton ilifungulia fursa zaidi za viongozi wa Marekani kuzuru nchini. Bila shaka Clinton aligundua jambo hapa kwetu na kulifikisha jikoni White House kwa ajili ya kufanyiwa kazi hata baada ya yeye kuondoka. Tukio la kulipuliwa ubalozi wa Marekani jijini Dar es salaam na kule Nairobi Kenya Agosti 7, 1998, kunaweza kuwa kichocheo muhimu cha White House kuitambua vyema Tanzania na kuona kuna haja ya kuwepo mikakati kabambe ya kiusalama na ya kuvumbua fursa za kiuchumi pia. Tangu kipindi hicho, ziara za vigogo wa ngazi za juu wa White House zilikolea nchini kwa nyakati tofauti, ikilinganishwa na nchi nyingine za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Yawezekana ziara za vigogo hawa zikawa nyingi zaidi nchini ikilinganishwa na nchi zile wanazofanya katika nchi nyingine za bara la Afrika. Julai 13, 2005 mke wa Rais George Walker Bush, ambaye alichukua nafasi ya Clinton, Bi. Laura Bush alitua jijini Dar es Salaam kwa ziara ya siku mbili. Februari 2008 Rais George Walker Bush, akawa Rais wa pili wa Marekani kuja nchini, akiwa ameambatana na mkewe Bi. Laura, ambaye yeye alishakuwa mwenyeji kidogo kufuatia ziara yake ya awali. Hata hivyo safari hii ugeni huo wa Rais wa Marekani ulisababisha adha kubwa kwa Watanzania. Makachero walitanda Ikulu ya Dar es

Ya akina Bush, Clinton yasijirudie kwa Obama


Salaam na kuvinjari kila kona za Ikulu ambayo Mwalimu Julius Nyerere enzi za uhai wake iliita ni mahali patakatifu. Walininginia kwenye paa kama vile ndio wenyeji wa eneo hilo kuliko makachero wetu. Itakumbukwa kwamba hata mawasiliano ya simu yalikuwa ya taabu, magari yalipekuliwa, maeneo aliyopita mgeni huyo yalidhibitiwa kiasi cha raia kutopita maeneo hayo akiwa huru. Kwa kifupi ni kwamba ile amani, uhuru na ustaarabu wa Watanzania hutoweka kwa muda kila wanapokuja watu wa White House. Lakini tukio lililoshitua zaidi, ni kukamatwa na kuwekwa ndani baadhi ya Masheikh kule Arusha siku moja kabla ya Rais Bush kuwasili mkoani humo kuzuru kiwanda cha vyandarua. Kisa ni kile kilichoitwa wasiwasi wa ugaidi. Mashekh hao walikaa ndani bila hatia yeyote hadi alipoondoka Bush na msafara wake. Ombaomba na walemavu nao waliondolewa barabarani wanakoomba na kuswekwa ndani hadi waheshimiwa hawa waondoke. Itakumbukwa kwamba katika utawala Bw. Bush, ndiye aliyeshinikiza nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania, kuchukua sheria ya Patriotic Act, ambayo iliyozaa sheria ya chapchap ya ugaidi nchini. Sheria hiyo mara moja ilianza kutumika na kuleta athari kwa Masheikh wakituhumiwa ugaidi ambapo wapo waliokamatwa kuswekwa ndani na wengine kufukuzwa nchini huku baadhi ya taasisi za Kiislamu zikifungwa n.k.

RAIS Jakaya Kikwete

GEORGE W. Bush

RAIS Barack Obama

Serikali ilionekana kushughulishwa barabara katika kutimiza matumizi ya sheria hiyo, licha ya wengi waliopata misukosuko kutodhihirika kuhusiana na ugaidi wenyewe. Kupokelewa haraka na kwa bashasha sheria hii ilionekana kukidhi haja ya aliyeileta kiasi cha kuimarisha urafiki wa pande mbili. Miradi ya vyandarua na MCC imeonekana kuwa kivutio kikubwa cha kuimarisha uswahiba wa pande mbili. Hatupingi viongozi wa

Msikiti wa Mtambani, unawatangazia Waislamu wote Muhadhara. Utakaofanyika:- Msikiti hapo (Mtambani) Siku:- Ijumaa, Juni 7/2013 (Leo). Baada ya Swala ya Al-Ijumaa. Muhadhiri:- Ustadhi SULEIMAN FILAMBI, toka Morogoro. Imam, Masjidi Mtambani Wabillah Tawq

MUHADHARA MASJID MTAMBANI

Inawatangazia Waislamu ibada ya ITIKAF. Mahali:- Masjidi Idrisa, Kariakoo. Siku:- Jumamosi, Juni 8/2013 Muda:- Baada ya Swalat Ishai Masheikh Mbalimbali watakuwepo, Inshaallah. Wabillah Tawiq

SHURA YA MAIMAM (T)

Makala/Tangazo

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013

AN-NUUR

Na Khalid S Mtwangi

HIVI sasa imekubalika na watu wengi kuwa kweli uhusiano kati ya Waislam na ndugu zao Wakristo sio mzuri kama inavyostahili. Wa n a o h u s i k a n a utawala wanatafuta njia ya kuinusuru nchi hii na majanga yanayoweza kutokea kutokana na hali hii isiyoridhisha. Tayari Rais Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, amekutana na viongozi wa dini kulizungumzia jambo hilo. Imependekezwa vile vile kuwa viongozi wa dini mbalimbali, hasa wale wa Kiislam na Kikristo wawe na mijadala na maongezi kuhusu jambo hili ili kutafuta njia ya kupoza yale yaliyochemka. Ni maoni ya msomi Dkt. Evarist Magoti wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kwamba mazungumzo kama hayo (dialogue) hayatakuwa na tija na tatizo litabaki pale pale. Soma maoni yake katika THE CITIZEN ON SUNDAY of May 26, 2013. Kuna sababu za msingi kabisa ambazo zinaweza kutolewa kuhakiki maoni hayo. Dkt. Evarist Magoti, katoa sababu za kitaalam za kisayansi ya siasa na za kisaikologia; lakini ziko pia za msingi kabisa. K w a n z a Wa i s l a m wanakumbuka, pengine zaidi ya ndugu zao Wakristo, kuwa katika mazungumzo hayo ya pamoja kumekuwa na msisitizo usiokuwa wa kawaida kuhusu mihadhara inayoitwa ya kashfa, ama pale wahadhiri wanashutumiwa kuwa wanakashifu dini za wengine. Jambo hili kwa kiasi kikubwa sana limemalizwa na mahakama kutokana na kesi ya Ustadh Rajab Dibagula, ambayo hukumu yake ilitolewa na Mahaklama ya Rufaa (ingawa hukumu ile ilikuwa ya kisiasa zaidi kuliko kutoa haki tupu). Hebu Wa i s l a m wakumbuke; hivi kweli malalamiko yao ya dhulma yanaweza kuondolewa pale ile inayoitwa mihadhara ya kashfa itapusitishwa ama itakapokoma? Bila shaka jibu

la swali hili la msingi litakuwa LA! Sasa inawezekana kabisa kuwa kumekuwa na msisitizo usiokuwa na kifani, juu ya kile kinachoitwa KASHFA kuliko lile la msingi la DHULMA wanayoipigia kelele Waislam. Ikiwa kweli kutakapokuwa hakuna ile kelele kuwa dini moja inakashifu dini nyingine, hapo ndipo tuamini patakuwa mwisho wa MFUMOKROSTO? Waislam wajiulize na watoe jibu wenyewe. Lakini muhimu zaidi ni kuwa macho, wasiwe wanadanganywa walale usingizi, ati hali sasa ni shwari wakati MFUMIOKRISTO ndio unapata nguvu zaidi. Masheikh wanaweza kuwa wanazungumza kila siku na Maaskofu kutafuta ridhaa (gani?) lakini hawa Maaskofu sio watendaji wanaotekeleza MFUMOKRISTO katika kazi na majukumu yao ya kila siku Serikalini. Kadhia ya mitihani ya somo la ISLAMIC KNOWLEDGE ni mfano mzuri sana. Uamuzi umetolewa na kuanza kutekelezwa wakati kila mtu, na hata Rais, anatia mkazo juu ya dialogue kati ya viongozi wa Kiislam na wa Kikiristo. Ni wazi kabisa kuwa kitendo hicho kilichotekelezwa na maafisa humo Wizara ya Elimu ni dhulma dhidi ya Waislam. Wamefanya hivyo wakati kuna kutoelewana kwa hali ya juu kabisa kati ya Waislam na Wakristo. Hawa watekelezaji ambao wengi wao, kama sio wote ni Wakristo, walionyesha dharau kubwa dhidi ya Waislam wa nchi hii. Baya zaidi ni kuwa hawa jamaa viongozi wa Kikristo walikuwemo katika njama za hujuma hiyo bila hata kuwatahadharisha wenzao Wa i s l a m . I n g a w a h i l o lisingetegemewa kutokea, Wakristo wasingeweza ama wasingetaka kuwajulisha Waislam hata kidogo. Basi kuna haja gani kuwa na hiyo inayoitwa dialogue? Ikubalike kuwa hivi sasa kuna vita vya maneno kati ya Waislam na Wakristo nchini humu. Inawezekana kabisa, kama baadhi ya watu wanavyodai, kuwa vita hivi vinachochewa na watu kutoka nje na wale wasioitakia mema Tanzania. Ati Waislam na wananchi wenzao Wakristo

Wakristo na Waislam: Panapotokea vita majeruhi wa kwanza ni ukweli


wamekuwa wakiishi kwa amani kwa muda mrefu sana, sasa iweje leo kuwe na mfarakano? Hili la kuchinja hasa liwaamshe Waislam kuwa kuna watu hawawapendi hata kidogo. Ukweli ni kuwa huko nyuma, Waislam walikuwa wastahamilivu sana, labda kwa vile walikuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru. Kwao ilikuwa muhimu kuukuza ule umoja wa kitaifa. Hayati Mwalimu Nyerere alilifahamu hilo na kalitumia vizuri sana. Sasa labda Waislam wameamka na kuutambua vizuri ule MFUMOKRISTO. Ndugu zao Wakristo hawakupenda iwe hivyo. Hivyo vimezuka hivyo vita vya maneneo. Wataalam wanasema kuwa panapozuka vita vya maneno tu kama humu Tanzania hivi sasa, majeruhi wa kwanza huwa UKWELI. Lakini sio hivyo tu, bali pia hata binadamu hutolewa kafara katika kutafuta ushindi wa vita hivyo. Kuna mifano mingi ambayo gazeti hili limeitoa katika zile harakati za Marekani, ati kupigana na ugaidi. Mpaka leo hii kuna mabishano ya nguvu kabisa kama kweli ni vijana wa Kiislam ndio waliendesha ndege kubomoa World Trade Centre pale New York na Pentagon huko Washington. Wako wanaosema na kuamini kuwa zilikuwa mbinu za Bw. George Bush, kupata sababu za kuishambulia Iraq na Afghanistan kwa maslahi ya Marekani. Historia nayo inatuambia kuwa hayo hayawezi kuwa ya kwanza. Wakati wa vinavyoitwa Vita Vikuu vya Kwanza, Waingereza waliitega meli yao kubwa ya abiria LUSITANIA, ipigwe kombora na kuzamishwa na Wajerumani. Meli hiyo ilikuwa na baharia takriban 1959; wakiwemo Wamarekani 128. Wakati huo Marekani walikuwa bado wanasita kujiunga na madola ya Ulaya kushiriki katika vita hivyo. Lakini kitendo cha kuzamishwa meli hiyo ya LUSITANIA na kupoteza maisha ya waMarekani 128, iliwafanya Marekani nao waingie katika vita vile (World War II 1939 mpaka 1945). Mbinu za Waingereza kuwatoa kafara Wananchi wake waliokuwa ndani ya meli ile zilifaulu. Huo ni mfano mmoja tu. Wasomaji wa historia wanakumbuka mkasa wa Pearl Harbour kule Hawaii. Hapo palikuwa na kituo kikubwa sana cha manowari na meli nyingine za kivita za Marekani. Hasa zile meli kubwa kubwa. Inastaajabisha sasa kwamba msururu (armada) wa meli za Japan takriban sita za kubeba ndege, na nyingine za kila aina zikikia kumi na tano ziliweza kusari kutoka huko Japan mpaka karibu kabisa, kiasi cha kilometa mia nne tu kutoka kituo hicho bila Marekani kutambua kuwa msururu wote huo umesari maelfu ya kilometa bila kutambulika. Haiwezekani hasa ikikumbukwa kuwa askari mmoja wa zamu aliziona meli hizo na madege katika radar zikikurubia. Alipowaeleza viongozi wake juu ya hatari hiyo walimwabia tu usijali. Basi kituo kilishambuliwa kwa nguvu sana na WaJapani na maisha ya askari wengi Marekani kupotea. Kama ilivyokuwa katika Vita Vikuu Vya Kwanza, safari hii pia wananchi wengi wa Marekani walikuwa hawakupendelea kushiriki katika vita hivi, iwe Ulaya dhidi ya Hitler ama Pacic dhidi ya Tojo Hideki, Waziri Mkuu wa Japani wakati ule. Hivyo mpaka leo historia inafundisha kuwa Rais

Franklin Delano Roosevelt, aliwatoa kafara askari wake na Wananchi wengine ili kupata kile alichokitaka. Nalo ni kutaka kujitosa vitani. Wa s o m a j i w a j a r i b u kukumbuka wataona kuwa kuna mikasa mingi imetokea humu Tanzania, ambayo haielezeki imetokea wapi na wala kwa nini imetokea. Lawama kubwa wametwikwa Waislam ingawa mpaka leo hii, Jeshi la Polisi Tanzania halijaweza kuwafikisha mahakamani watu hao waliochoma makanisa, kwa mfano. Hali kadhalika misikiti ilichomwa huko Tunduma mpaka leo imekuwa kimya bila taarifa yeyote kutoka kwa vyombo vya usalama. Waislam tuwe macho, tutumie akili ya asili kuchanganua mambo. Vita kubwa iliyoko mbele yenu ni kuondoa dhulma iliyoshamiri nchini kutokana na ule ambao sasa unajulikana wazi kama MFUMOKRISTO. Mihadhara sio jambo zito hata kidogo kwa vile Uislam umakuwa ukikashwa katika vijitabu vinavyozagazwa na Makanisa kwa muda mrefu sana. Hapajatokea rabsha kuhusu hilo. Lengo liwe ni kutafuta jinsi gani Waislam wanaweza kuushinda huu MFUMOKRISTO, ili Wananchi wote wa nchi hii wawe na haki sawa na waishi kwa amani kama ilivyokawaida.

Almadrasat Munawara Shaziliya ya Jibondo Maa, inakabiliwa na tatizo kubwa la vitabu hususan Misahafu, Juzuu na kitabu cha kufundishia cha Fath-lbaarii Sharhe Ibukharii. Tunaomba msaada wenu. Kwa mawasiliano tumia: 0715 059250, 0784 059250 Wabilah Tawq

Msaada wa vitabu

Hatari ya kuharakisha kulaani matukio ya ugaidi


Na Said Rajab KUFUATIA mauaji ya Padri Evarist Mushi kule Zanzibar na shambulio la bomu kwenye Kanisa Katoliki la Joseph Mfanyakazi lililosababisha vifo vya watu watatu mjini Arusha, neno kulaani lilisikika mara nyingi sana kupitia vyombo vya habari. Maaskofu, taasisi za Kiislamu, Wanasiasa, Masheikh na makundi mengine ya kijamii, wote walilaani mara moja vitendo vile viovu, kabla hata ya ukweli wote kufahamika kuhusu matukio yale. Wengine walikwenda mbali zaidi na kuanza kutoa kauli za kuwalaumu Waislamu, ingawa hawakujitokeza wazi. Baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristo walitangaza hadharani kwamba mashambulizi yale hayahusiani na dini, ingawa sina hakika kama dhamira zao zinafanana na kauli zao. Kwa sababu hawa wenzetu mara nyingi yale wanayodhihirisha kupitia vinywa vyao, ni tofauti kabisa na yale wanayohifadhi kwenye vifua vyao. Mimi ugomvi wangu siyo kulaani pale matukio maovu yanayofanyika, bali pale Waislamu wanapolaani matukio hayo bila ya kuwa waangalifu. Mazingira yaliyojengwa hapa nchini, i n a o n e k a n a Wa i s l a m u wakilaani kuuawa kwa Padri, au kanisa kupigwa bomu, inakuwa kama vile wanajikosha mbele ya umma! Ya a n i w a n a j a r i b u kuthibitisha kwamba wao hawahusiki. Mtazamo uliojengwa mbele ya umma ni kwamba Waislamu ndiyo wanaofanya mashambulizi hayo. Ni jambo la wazi kabisa na sijui kama baadhi yetu wanafahamu hivyo, kwamba vyombo vya habari vilikuwa vikijaribu sana kuifanya jamii nzima, wakiwemo Waislamu kulaani vikali matukio ya kuchomwa moto makanisa, kuuawa Padri Zanzibar na kanisa kupigwa bomu, ingawa havikufanya hivyo katika mauaji ya Mwembechai, Misikiti kuharibiwa Tunduma na mtoto kukojolea Quran Mbagala! S a s a Wa i s l a m u wanapolaani matukio hayo bila ya kuwa waangalifu, wanaweza kujikuta wakisukuma mbele ajenda za maadui dhidi yao bila wenyewe kujitambua. Miye huwa naogopa sana kuvamia mambo kwa kufuata mkumbo tu. Lazima tufahamu kwamba vyombo vya habari vina uwezo wa kujenga mtazamo na kuwafanya watu wajadili mambo na wachukue hatua kwa mrengo wa vyombo hivyo vinachokitaka. Angalia mfano wa hivi karibuni tu, Waislamu kupitia Jumuiya na Taasisi zao walikutana Jumapili iliyopita katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam, na kujadili masuala mazito yanayowahusu. Vyombo vya Habari karibu vyote vilialikwa kwenye mkutano huo. Lakini angalia vile ambavyo vimeripoti mkutano ule! Kimyaa kabisa kama vile haukufanyika! Lakini mkutano kama ule ungeitishwa na Wakristo kwa malengo yale yale, magazeti yote yangeandika, Televisheni na Redio zote zingetangaza. Waislamu wakiuawa kinyama Mwembechai, Maaskofu wanapongeza, lakini mauaji kama hayo yakifanywa Kanisani, baadhi ya Masheikh wanaungana na Maaskofu kulaani vikali - ujinga huu mpaka lini? Je? Waislamu wanafahamu tafsiri sahihi ya hali hiyo? Wakati kuna uhuru wa habari kwa makundi yote ya kijamii hapa nchini, inaonekana uhuru huo si kwa ajili ya Waislamu! Subiri Serikali itishie kuwaponda Waislamu au kuwatuhumu kwa vurugu, basi vyombo vyote vya habari nchini vitaandika kuwakanyaga Waislamu! Nimeshaweka bayana, lengo siyo kuwalaumu wale wanaolaani uovu unapofanyika, bali Waislamu wawe makini zaidi, kabla hawajakimbilia kulaani matukio hayo. Watu wabaya wanaweza kutumia fursa ya kuungwa mkono na Waislamu, japo kwa kra, kuwahujumu Waislamu wenyewe. Wanaweza kuwasingizia ndugu zetu kuwa wamehusika na uhalifu huo. Utafanyaje wakati tayari umeshalaani bila kikomo? Itabidi ukubaliane nao - unaanza kumkana ndugu yako! Kule Marekani, baada ya mabomu ya Boston, Waislamu walilaani mno mashambulizi yale, bila hata ya kuacha akiba ya maneno. Baadhi ya Maimamu mashuhuri, hawakutosheka na kuonyesha majonzi yao kwa waathirika, bali walitamka bayana kwamba Uislamu unakataza vitendo hivyo. Wa l i k w e n d a m b a l i zaidi hata kukataa kabisa kumzika mmoja wa watuhumiwa wa mabomu ya Boston kwenye makaburi ya Waislamu. Unajuaje kama kweli amehusika au unaingizwa tu kwenye ajenda usiyoifahamu? Kuna uwezekano wa hatari

Makala/Tangazo

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013

AN-NUUR

KITUO CHA MAFUNZO NA AJIRA CHA TAMPRO

SEMINA YA UFUGAJI BORA WA KUKU WA KIENYEJI


Jumuiya ya Wataalamu wa Kiislam Tanzania (TAMPRO) kupitia Kituo chake cha mafunzo na Ajira inawatangazia Semina ya Mafunzo ya Ufugaji Kuku wa Kienyeji na Ujasirimali kwa kutumia wataalamu wenye uzoefu wanaoshughulikia masuala hayo kwa muda mrefu. Semina itakuwa kama ifuatavyo:Walengwa: Wafugaji, wanaotaka kuanza kufuga, wajasiriamali wadogo wadogo na watakaopenda . Siku: Kuanzia Jumamosi, Jumapili na Ijumatatu terehe 8 -10 June 2013 Muda: Saa 3:00 asubuhi - 10:00 jioni Mahala: Osi Kuu ya TAMPRO Magomeni Usalama, Dar es Salaam Mada: Njia za ufugaji wa kuku, Uchaguzi wa kuku kwa ajili ya kufuga, Kuandaa chakula bora, magojwa ya kuku na tiba yake, Utunzaji wa vifaranga na mayai nk. Vile vile mafunzo ya kutafuta soko la bidhaa zinazotokana na kuku, kutunza mahesabu na kumbukumbu za fedha pamoja jinsi ya kukuza mtaji yatatolewa. Kujisajili: Shilingi 50,000/= kwa mtu mmoja. (Kwa ajili ya cheti cha ushiriki, Kitabu cha muongozo, na chakula kwa siku zote tatu) Muhimu: Washiriki watapatiwa vyeti na kitabu cha muongozo wa ufugaji kuku kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili ili kukidhi haja. Pia watapata fursa ya kutembelea na kusoma kwa vitendo (eld) Kujisajili: Ili kujisajili tuma SMS kwenye namba 0714 151532, 0767151532, 0716574266 au ka TAMPRO Makao Makuu, Magomeni Usalama, jirani na Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni. Wahi kuijiandikisha kwani nafasi ni chache. Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia 0714 151532, 0767151532, 0716574266 au info@tampro.org MRATIBU MAFUNZO TAMPRO MAKAO MAKUU

gani kwa Waislamu kulaani matukio hayo bila kikomo? Matatizo kadhaa yanakuja kichwani. Kwanza, kwa viongozi wa Waislamu kulaani matukio hayo jumla jumla bila ya uangalifu, inahamisha mzigo wa lawama kutoka kwa mshambuliaji halisi na sababu zilizomsukuma afanye hivyo. Yaani inapoteza maboya! Pili, kulaani sana kifo cha mtu mmoja kwa kiasi kikubwa, inapunguza thamani ya maisha ya maelfu ya watu waliouawa katika matukio mengine mabaya kama hayo, ambao mauaji yao hayapewi umuhimu mkubwa na wala hakuna anayelaani. Ta t u , i w a p o t a t i z o linaonekana lipo kwa jamii ya Waislamu, sera za kupambana na tatizo hilo zitalenga jamii nzima ya Waislamu. Kwanini Muislamu asiyehusika na uhalifu aadhibiwe kw a kosa ambalo hakufanya? Tunahitaji kuwa makini sana na baadhi ya vyombo vya habari vinapoendesha mijadala kuhusu matukio haya. Ukichunguza kwa makini, utaona ni mbinu tu ya kuwatuhumu Waislamu, japo hawasemi moja kwa moja. Jamii ya Waislamu ndiyo imekuwa begi la mazoezi ya masumbwi kwa wanasiasa na watendaji wa Serikali wanaolinda Mfumo Kristo. Vyombo hivi vimekuwa kimya kabisa kuzungumzia hatari za Mfumo Kristo kwa mustakabali wa taifa, lakini viko tayari kuwakaanga Wa i s l a m u y a n a p o t o k e a mauaji ya padri, makanisa kuchomwa moto au shambulio la bomu kanisani, kabla hata uchunguzi kufanyika! Badala ya kuwafichua wale walioasisi Mfumo Kristo hapa nchini, ambao unatishia kulisambaratisha taifa, wenyewe wanaendesha kampeni za kuwadhalilisha Wa i s l a m u w a n a o k e m e a mfumo huo. Baadhi yetu wamepoteza kujiamini na wamekubali kutumikia mfumo huo kama majaaliwa yao. Kuna funzo kubwa sana kwetu Waislamu jinsi ya kulaani matukio haya yanayoitwa ya kigaidi wakati yanapotokea. Tuache jazba na kufuata mkumbo wa kulaani. Kuna matokeo mabaya yasiyoonekana katika kulaani kwetu, iwapo hatutakuwa waangalifu.

10

Tangazo

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013

AN-NUUR

ISLAMIC PROPAGATION CENTRE


NAFASI ZA KIDATO CHA TANO 2013/2014
1. 2. 3. 4. 5. 6.

Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi bora ya Kiislamu kwa gharama nafuu. Shule hizi ni za mchanganyiko wa wavulana na wasichana na zinapokea wanafunzi wa bweni tu. Masomo yanayofundishwa ni Islamic knowledge, Combinations za SAYANSI, ARTS, BIASHARA pamoja na COMPYUTA. Muombaji awe na Crediti 3 au zaidi na angalau D ya Elimu ya Dini ya Kiislamu katika matokeo ya kidato cha nne. Ikiwa ana F au hakufanya Elimu ya Dini ya Kiislamu, basi awe tayari kusoma programu maalum ya Maarifa ya Uislamu atakapokuwa kidato cha tano. Kwa wale ambao walisharudisha fomu wanatakiwa wawasilishe result slips za matokeo mapya mapema kwenye osi waliporejesha fomu hizo ili yaunganishwe na fomu zao. Waombaji wapya wenye sifa wanashauriwa kuendelea kuchukua fomu. Waliokwisha omba wataleta result slip ya matokeo ya pili wakati wa kuripoti shuleni. Tarehe ya mwisho ya kurejesha fomu ni tarehe 23/06/2013. Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000/= katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini.
Arusha Kilimanjaro Osi ya Islamic Education Panel Jambo Plastic Ghorofa ya 2 mkabala na msikiti Mkuu Bondeni - 0763 282 371/ 0784 406 610 Moshi: Msikiti wa Riadha 0654 723 418 Same: Kirinjiko Islamic Secondry School: 0784 296424/0655 697 075 Uongofu Bookshop: - 0784 982525/ Mandia Shop - Lushoto: 0782257533 Nyasaka Islamic Secondary School 0717 417685/0786 417685 Osi ya Islamic Education Panel - Mwanza - Mtaa wa Ruji mkabala na Msikiti Al-Amin 0785 086 770 Duka la Kansolele -Stendi ya zamani sokoni - 0714587193 Bukoba: Alhuda Caf Kwa mzee Kinobe karibu na osi za TRA. - 0688 479 667 Msiikiti wa Majengo-0718866869 Kahama osi ya AN NUUR Karibu na msikiti wa Ibadhi: 0753 993930 Ubungo Islamic High School 0754 260 241/0712033556 Osi ya Islamic Ed. Panel Temeke -Msikiti wa Nurul Yakin 0655144474 Wasiliana na Ramadhani Chale :0715704380 Hijra Islamic Primary School : 0716 544757/0712 325086 Osis ya Islamic Ed. Panel karibu Nuru snack Hotel 0714285465 Babati: Shule ya Msingi Hangoni: 0784 667575 Msikiti wa mwanga Kigoma: 0753 355224 Kibondo Islamic Nursery School: 0784 442860 Kasulu: Murubona Isl.SS. 0714710802 Wapemba Store: 0784 974041/0786 959663 Amana Islamic S.S 0786 729 973 Kwa Kawanga Karibu na Msikiti wa NURU 0715 681701/0716791113 Mkuzo Islamic High School. 0716 791113 Duka la vifaa vya Kiislamu nje ya Msikiti wa Uyole 0713 200209 Rexona Video mkabala na Mbeya RETICO: 0713 200209 Sumbawanga: Masjid TAQWA 0717082 073 Kituo cha Kiislamu Isevya: 0784 944566 Madrastun Najah: 0714 522 122 Wete: Wete Islamic Education Center: 0777 432331 Madrasatul Fallah: 0777125074Osi ya ust. Yusufu Ally jirani na msikiti mkuu 0653705627

Tanga Mwanza Musoma Kagera Shinyanga Dar es SalaamMorogoro Dodoma Singida Manyara Kigoma Lindi Mtwara Songea Mbeya Rukwa Tabora Iringa Pemba Unguja Maa -

6. Pia Fomu zinapatikana kwenye Tovuti: www.ipctz.org. Ikumbukwe kuwa watakaopata fomu kupitia tovuti (download) watatakiwa kuzilipia wakati wa kuzirejesha.

USIKOSE NAFASI HII ADHIMU WAHI KUCHUKUA FOMU SASA!

Wabillah Tawiq MKURUGENZI

11
Na Mwandishi Wetu ILE Mahakama ya Kadhi iliyokuwa ikililiwa na Waislamu nchini, wakitaka irejeshwe na kutambuliwa rasmi na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, haipo katika rasimu ya mapendekezo ya katiba mpya. Hayo yamebainika katika haa ya uzinduzi wa Mapendekezo ya Rasimu ya Katiba Mpya uliyofanyika jijini Dar es Salaam Jumatatu wiki hii. Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, alisema Tume imependekeza kutoingizwa mahakama hiyo ndani ya katiba baada kuchambua na kutizama kwa kina utendaji wa Mahakama ya Kadhi ya Zanzibar, ambayo alidai imekuwa ikifanya kazi zake bila kuingizwa katika katiba ya Zanzibar. Aliongeza kuwa Waislamu watakuwa huru na haki ya kuanzisha na kuendesha Mahakama yao ya Kadhi hata bila ya mahakama hiyo kutambuliwa na Katiba ya nchi. Kwa muda mrefu Waislamu nchini wamekuwa wakiitaka serikali kurejesha mahakama ya Kadhi nchini, ili kutenda haki katika masuala ya kiibada, ambayo yamekuwa yakipindishwa katika mahakama za kawaida pale yanapotokea matatizo. Aidha walitaka mahakama hiyo ambayo itashughulika na mambo ya madai katika Uislamu, itambuliwe na katiba ili hata pale hukumu itakapotolewa na mahakama hiyo kwa misingi ya Shariah, basi yasiweze kupuuzwa na kutupwa na mahakama ya kawaida kwa kutotambuliwa kwake na katiba. Pia igharimiwe na serikali kwa kuwa Waislamu ni sehemu ya jamii ya watanzania na walipa kodi kama wananchi wengine. Masuala yaliyokuwa yashughulikiwe na Mahakama hiyo kuwa ni pamoja na Ndoa na Talaka, Mirathi, Wasia, Hiba, zawadi, tunu, wakfu, malezi ya watoto na usuluhishi wa migogoro ya Kiislamu. Serikali ya Tanzania mwaka jana ilikubaliana na Waislamu juu ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi, na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliunda Kamati maalum kati ya Taasisi za Kiislamu na

Makala/Tangazo

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013


kuendesha Mahakama za Kadhi katika nchi hizo ambazo zina Mahakama za Kadhi kwa muda mrefu. Alisema lengo ni kupata uzoefu na kujua njia bora ya kutuwezesha kuanzisha Mahakama hiyo nchini na kwamba, ziara hiyo ilitarajiwa kufanyika karibuni na kugharimiwa na Serikali. Hata hivyo kimya kilizidi kutawala, hadi pale ghafla aliposikika Mufti wa Bakwata Sheikh Issa Shaaban Simba, akimtangaza Kadhi Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abdullah Yusuf bin Ali bin Yusuf ash-Shirazi Mnyas mjini Dodoma. Hatua hiyo iliwashangaza Waislamu wengi nchini ambapo Masheikh na Waislamu kwa ujumla waliona hatua hiyo ya Bakwata ni usaliti kwa Waislam. Walisema inasikitisha kuona kuwa mwanzo liliundwa jopo la Masheikh kutoka taasisi mbalimbali za Kiislamu nchini kwa ajili ya kushughulikia mchakato wa kuanzishwa Mahakam hiyo lakini BAKWATA wamesaliti kuamua kukaa wenyewe na kuiunda mahakama hiyo, ambayo haina meno wala wataalam wala mpango kazi. Hivyo walihitimisha kwa kusema Kadhi huyo ni wa Bakwata na serikali na si wa Waislam. H i v y o Wa i s l a m u walitegemea kutumia fursa ya kutoa maoni yao ya kuwa na mahakama ya Kadhi katika mchakato wa Katiba mpya, ambapo hapo anaweza kupatikana Kadhi mwenye sifa walizozitaka.

AN-NUUR

Hakuna Mahakama ya Kadhi-Tume


serikali ili kupata ufumbuzi wa utaratibu wa kuiendesha mahakama hiyo. Hata hivyo mpango huo ulipingwa vikali na viongozi wa Kikristo na kuitaka serikali kuachana na mpango huo kwa kwa madai kuwa ni wa kibaguzi na una nia ya kuisilimisha nchi. Hata hivyo baadae serikali ilisema imekubaliana na kuanzishwa mahakama hiyo lakini itakakuwa nje ya Mfumo wa Serikali na itagharimiwa na kuendeshwa na Waislamu wenyewe. Jambo hilo lilipingwa na Waislamu hivyo mjadala kati ya serikali na Waislamu kuendelea bila kujulikana ukomo wake. Kimya kilichukua nafasi huku serikali ikishindwa kutoa majibu muafaka juu ya hatma ya kuanzishwa mahakama hiyo. Hata hivyo suala hilo liliibuliwa tena na wabunge wakati wa vikao vya bunge 2012/20013. Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wakati akijibu hoja za wabunge zilizojadili kwenye hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara na Taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2012/2013, alisema kwamba mahakama hiyo itaanzishwa wakati wowote baada ya maandalizi kukamilika na kwamba, utekelezaji wake uko katika hatua nzuri baada ya kamati ndogo iliyoteuliwa na Waziri wa Katiba na Sheria yenye wawakilishi wa Waislamu na Serikali kutoa taarifa yake ya mwanzo ya namna ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi. Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda alitaja masuala yatakayoshughulikiwa katika Mahakama hiyo kuwa ni pamoja na Ndoa na Talaka, Mirathi, Wasia, Hiba/Zawadi/ Tunu, Wakfu; Malezi ya Watoto na Usuluhishi wa Migogoro ya Kiislamu na kwamba haitahusika na mashauri ya Jinai. Waziri Pinda alikuwa akijibu hoja za wabunge waliotaka kufahamu maendeleo ya Mahakama hiyo, huku wakitaka Serikali itimize ahadi yake hiyo ambayo ipo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005. Katika kikao cha mwisho cha pamoja kati ya Serikali na ujumbe wa Wawakilishi wa Waumini wa Kiislamu kilichofanyika Machi mwaka huu, tumekubaliana katika kuwezesha suala hilo liende kwa haraka, kwa kuanzia, ni vyema zikaanzishwa Mahakama za Kadhi katika baadhi ya maeneo machache nchini. Lengo ni kuwezesha umma kulielewa vizuri suala hili kinyume na hisia potofu zilizopo sasa zikihusisha

BI Aisha Sururu (katikati) akiongea katika kongamano la Waislamu lililofanyika Diamond Jubilee, Jijini Dar es Salaam Jumapili iliyopita.

Mahakama ya Kadhi na Sharia chini ya Dini ya Kiislamu. Alinukuliwa akisema Mh. Pinda. Aliongeza kuwa katika kikao cha mwisho cha Kamati Kuu inayosimamia suala hilo, iliamuliwa na pande zote kuwa baadhi ya wajumbe kutoka upande Waislamu na Serikali wakafanye ziara ya mafunzo katika nchi za India, Uingereza, Kenya na baadaye Zanzibar ili wakajifunze namna ya kuratibu na

Masjid Aswabirina

Kitunda kibeberu Dar es salaam. Uongozi wa Masjid Aswabirina Tunapenda kutoa shukran zetu za Dhati kwa Waislamu wote waliofanikisha Msikiti huu kukia hapa ulipo. Hivyo basi tunatarajia kufanya ufunguzi wa msikiti huo tarehe 28 Shaaban ili uanze kutumika Rasmi katika mwezi mtukufu wa Ramadhani. Ili kufanya ufunguzi huo tunaomba msaada wenu wa kujengewa choo, Kisima cha maji pamoja na ununuzi wa Uwanja uliopo mbele ya Msikiti gharama ya uwanja huo ni Milioni Tisa ( 9) kwa ajili ya upanuzi wa ujenzi wa shule ya awali na chuo. Pia Tunaendelea kuwaomba wahisani waendele kutusaidia ili kufanikisha kukamilika kwa ujenzi huu. Tuma Mchango wako Account Na: K.C.B 3300386233 jina la A/c Aswabirina au kwa Tigo Pesa 0714 565619 au Mpesa 0753 673820 Amir Khatibu Yunus

12

AN-NUUR
MAKALA

12

RAJAB 1434, IJUMAA JUNI 7-13, 2013

Usikose kusoma AN-NUUR kila Ijumaa

Msiba mkubwa: Dini Mseto yaja


Na Mwandishi Wetu SOMO la Dini Mseto sasa litafundishwa rasmi shuleni na vyuoni Tanzania nzima kuanzia Januari 2013, imefahamika. Kufuatia somo h i l o , wa t o t o s h u l e n i hawatafundishwa tena Imani na Uchamungu kwa mujibu wa Uislamu (au Ukristo), bali watafundishwa kupendana, maadili na kutii utawala (bora) bila kujali dini zao. Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kupitia Shirika la Utangazaji, TBC, ambalo ni Shirika la Serikali, mihutasari ya somo hilo ishaandaliwa na kupitishwa. Habari zilizopatikana katika mtandao wa TBC zinasema kuwa Mihutasari hiyo imezinduliwa rasmi na UMAKA, yaani Umoja wa Madhehebu Kagera wakishirikiana na Serikali b a a d a ya m i h u t a s a r i hiyo kupitishwa rasmi na Kamishina wa Elimu ili isambazwe katika shule zote tayari kwa kutumika kufundishia wanafunzi katika ngazi mbalimbali. Hata hivyo haikuweza kufahamika ni kwa nini jambo hilo limefanywa siri kati ya UMAKA na Serikali na hata uzinduzi wake kufanyikia Bukoba badala ya Dar es Salaam ambapo ndio Makao Makuu ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Somo la Dini na Maadili limerasmishwa rasmi kufundishwa shuleni na vyuoni baada ya UMAKA kuona umuhimu wa kuwa na mihutasari ambayo ni rasmi na inayotambuliwa na Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ili itumike kufundishia watoto pia na kutahiniwa kama masomo mengine. Habari zaidi zinasema kuwa Umoja wa Madhehebu Kagera (UMAKA) ulianzisha mchakato wa kuandaa m i h u t a s a r i ya s o m o la Dini na Maadili wakishirikiana na Serikali ili somo hilo liwe na mihutasari inayofanana katika kufundishia wanafunzi kuliko hapo awali ambapo somo hilo halikuwa na mihutasari ya kufundishia. Ikafafanuliwa kuwa Kupitia somo la Dini na Maadili, wanafunzi wa t a f u n z wa m a a d i l i mema ya kupendana na kuwapenda Watanzania wenzao, kujenga jamii ye n ye k u wa j i b i k a n a kumcha Mwenyezi Mungu bila kujali tofauti za ki-imani kwao, pia kulelewa na kukua katika malezi ya kufuata sheria na utawala bora. Katika kuboresha utumiaji wa Mihutasri hiyo mipya ya somo la Dini na Maadili, inaelezwa kuwa Serikali imeagiza somo hilo likaguliwe na wakaguzi wa serikali pamoja na walimu wakuu wa shule kama masomo mengine na kutahiniwa katika ngazi zote hadi ile ya taifa. Na kwamba kwa kuona umuhimu wa somo la Dini na Maadili kufundishwa shuleni, serikali imeamua m i h u t a s a r i ya s o m o hilo itumike Tanzania nzima badala ya Mikoa ya Kagera na Kigoma walioshirikiana na Serikali kuandaa mihutasari hiyo ili wanafunzi wote wa Tanzania wafunzwe dini na maadili ya Kitanzania. UMAKA ilianzishwa miaka ya 1980 ikiwa na lengo la kushirikiana na Serikali na kushauri masuala mbalimbali yahusuyo maadili, amani, usalama na maendeleo ya jamii ya Watanzania. UMAKA inajumuisha

BABA Askofu Nestory Timanywa Jimbo Katoliki La Bukoba, ambaye amestaafu hivi karibuni mmoja wa washiriki uzinduzi somo Dini na Maadili. Balaza la Maaskofu Tanzania (TEC), Balaza la Waislamu Tanzania (BAKWATA), na Baraza la Wakristo Tanzania (CCT). Imesema taarifa ya mtandao wa TBC. Kuzinduliwa kwa somo hili maana yake ni kuwa mwanafunzi Muislamu badala ya kufundishwa somo la Dini na Mwalimu Muislamu aliye na Elimu ya Dini ya Kiislamu, sasa anaweza kufundishwa na Mkatoliki, Sabato au hata Yahudi. K a m a inavyokumbukwa harakati za kuvunja taasisi ya Waislamu ya EAMWS n a b a a d a e k u u n d wa kwa Bakwata, ilianzia Bukoba na walitumika vijana na Masheikh wa Bukoba ambao baadhi yao walikuja kuwa viongozi wa Bakwata Makao Makuu kwa muda mrefu. Suala hili na Dini Mseto kuibukia tena Bukoba chini ya UMAKA, limewafanya Waislamu wengi kuhoji, Bukoba kunani? Baadhi ya Masheikh kutoka Zanzibar waliohojiwa wanasema kuwa Dua yao ni balaa hili lisiwakute kwa maana kuwa kama ingewezekana Zanzibar huru yenye mamlaka yake ije kabla ya somo la Dini Mseto k u a n z a k u s o m e s h wa skulini. Wanasema, pamoja na yote, lakini wanaamini kuwa hakuna kiongozi wa Zanzibar atakayekubali kuona mtoto wa Kizanzibari akisomeshwa Dini mseto. Habari zaidi zinasema kuwa kwa Dini Mseto kufanywa somo la lazima na lenye kutahiniwa, huenda kwa muda yale ya Maarifa ya Kiislamu yakafanywa kuwa somo la hiyari na yasiyotahiniwa na Serikali kabla ya kupigwa marufuku kabisa.

MATANGINI ISLAMIC SEMINARY


P.O.BOX 53732, TEL 2420088, MOBILE 0719-089737 E- mail: matanginiislamic@yahoo.com REG NO: 1337

MKUU WA SHULE YA MATANGINI ISLAMIC HIGH SCHOOL ILIYOPO DAR-ES SALAAM ANAWATANGAZIA NAFASI ZA MASOMO YA KIDATO CHA TANO KATIKA MICHEPUO YA HKL, HGK, HGA, HKA NA KLA. NAFASI KWA WANAOHAMIA NURSERY, PRIMARY NA SECONDARY ZIPO. FOMU ZINAPATIKANA: TANGA: MUONE MKUU WA SHULE YA MAAWA SECONDARY SCHOOL. KIGOMA: MUONE MKUU WA SHULE YA JIHADI SECONDARY SCHOOL. MOROGORO: MUSLIM UNIVERSITY MOUNE USTADH FILAMBI. DAR-ES SAALAM: KWA MKUU WA SHULE YA MATANGINI ISLAMIC HIGH SCHOOL NA MSIKITI WA KIBO MUONE USTADH YAHYA. SHULE NI YA BWENI NA KUTWA, KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA SIM 0719089737, 0712305928 AU 0715381405. MLETE MWANAO APATE ELIMU BORA NA MAADILI YA DINI(TUPO KIMARA MWISHO-DAR-ES SALLAM) MASOMO YATAANZA TAREHE 01/07/2013 (Wahi nafasi ni chache) NB:WANAFUNZI WOTE WALIOMALIZA KIDATO CHA SITA WAMEFAULU KUINGIA CHUO KIKUU.(2013) KARIBU SANA

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.

You might also like