Professional Documents
Culture Documents
Annuur 1075
Annuur 1075
Annuur 1075
tz
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1075 SHAABAN 1434, IJUMAA JUNI 14-20, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
VIONGOZI wa Uamsho walikuwa wakiuliza, Je, mnautaka? Sasa Jaji Mstaafu wa Tanzania Jaji Mark Bomani anasema kuwa ingekuwa vyema kabla ya kujadili muundo wa muungano, watu waulizwe je, bado wanautaka? Uk. 7
FOLENI ya waliohama CCM. Wanachama hawa vijana, wanawake na wanaume huko Matemwe katika mkutano wa CUF, wameamua kujiunga na CUF kutokana na sera yake ya kudai mamlaka kamili ya Zanzibar.
2
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
Tahariri/Makala
AN-NUUR
MAONI YETU
WENGI tunafahamu kwamba imekuwa ndio nia ya serikali kutoa ruzuku kwa taasisi za afya za mashirika ya dini. Nia ilikuwa nzuri, kuziwezesha taasisi hizo kutoa huduma nafuu kwa wananchi hasa makabwela, hususan mahali ambapo hakuna hospitali, zahanati wala kituo cha afya cha serikali. Aidha tunafahamu lengo zuri la serikali la kutoa misamaha ya kodi kwa taasisi hizi za dini, ni kuziwezesha taasisi hizo kuingiza bidhaa na vifaa vya huduma kwa unafuu, ili kuziwezesha kutoa huduma hizo kwa unafuu zaidi kwa wananchi, hususan wale wa daraja la kawaida na lile la chini kimapato. Lakini ni ukweli usiopingika kwamba, fursa hizi zinazotolewa na serikali kwa taasisi hizo, pamoja na nia nzuri ya kuziwezesha kutoa huduma kwa gharama nafuu kwa umma, lakini nia hiyo imekuwa ikitumiwa vibaya. Badala ya wananchi kupata ile nafuu iliyokusudiwa, wamekuwa wakibebeshwa mzigo wa gharama licha ya serikali yao kudia sehemu kubwa ya gharama hizo. Hadi tunaandika maoni haya, ni uhakika kwamba hakuna hospitali ya kanisa i n a yo t o a h u d u m a k wa kuzingatia nafuu inayotolewa na serikali. Hii ina maana kwamba, pamoja na kuondolewa kodi, kupewa ruzuku na serikali, lakini hakuna nafuu inayopatikana katika hospitali, zahanati na vituo vya afya vya makanisa. Kwa kifupi ni kwamba, hatuoni tofauti ya bei za huduma za afya kati ya hospitali hizi za ruzuku na zile za binafsi au taasisi ambazo hazina bahati ya ruzuku au msamaha wa kodi. Wakati mwingine, hata huduma zilizokusudiwa k u t o l e wa k a t i k a v i t u o hivi vya huduma za afya vya mashirika haya yanayoonekana ni ya kiroho na kiadilifu, wakati mwingine huwa hazipo. Kila uchao wimbo ni dawa hakuna n.k. Na kwa kuwa pamoja na kwamba serikali inatoa ruzuku na dawa katika taasisi hizo za kiroho, lakini hakuna ufuatiliaji wa karibu unaofanywa na serikali juu
AN-NUUR
ya matumizi ya ruzuku na dawa zinazotolewa katika taasisi hizi. Mwanya huo hutumika barabara kufanya udhalimu wa afya kwa wananchi walio wengi huku wachache wakifaidi. Serikali imeshasema kwamba ina mpango wa kujenga zahanati kila ki. A i d h a i n a m p a n g o wa kuongeza idadi ya vituo vya afya baada ya kuzifanya Hospitali karibu zote za mikoa kuwa za rufaa. Ili kuharakisha mpango huo wa serikali ambao ndio muhimu zaidi kwa maslahi ya wananchi, kuna haja sasa ya serikali kufanya uamuzi mgumu. Nao si mwingine ni kuondoa utaratibu wake wa kutoa ruzuku kwa mashirika na taasisi za afya za kidini, na kuelekeza mapato yake katika kujenga zahanati na vituo vyake vya afya kwa maslahi ya umma wa Watanzania. Hapo hata ukitokea ubadhirifu, ufisadi au hujuma, wananchi wa t a k u wa n a h a k i n a mamlaka ya kuihoji serikali kodi zao zimetumikaje kiasi cha wao kukosa huduma iliyokusudiwa. Lakini hilo ni vigumu kufanyika kwenye mashirika ya dini ambayo ndio yanayomiliki vituo hivyo vya afya. Kuendelea kuyakumbatia mashirika ya afya ya dini na kuyapa majukumu ya kiserikali katika kuhudumia Watanzania, ni sawa na kuendelea kuwahujumu Watanzania katika afya zao. Utaratibu wa ruzuku za afya katika taasisi za afya za kidini ufutwe sasa. Zengwe na kuboreshwa hospitali za serikali. Zile za madhehebu ya dini zijiendehshe zenyewe kwa kupitia njia zake za mapato. Hatudhani kama zilianzishwa ili ziendeshwe na serikali. Katika utaratibu wa sasa kwa kweli ni serikali inazisaidia taasisi za kidini sio taasisi hizo kuisaidia serikali. Ufupi wa maneno serikali inatumia fedha za walipa kodi kuimarisha Wakristo na Ukristo huku ikiwaweka kando wananchi wa dini nyingine. Na huu ndio Waislamu wanasema kuwa ni ubaguzi, upendeleo na dhulma. Serikali ijenge hospitali zake za kutosha sio kuimarisha za taasisi za kidini.
UHAI ni jambo la msingi na la umuhimu wa kipekee katika maisha ya mwanadamu. Uhai wa mwanadamu unategemea zaidi afya na siha nzuri. Ili kupata maisha salama, ni lazima mwanadamu awe ana uhakika wa kula na kunywa na kuhakikisha anapata matibabu pale anapopata hitilafu ya afya yake iwe ni kwa maradhi, kwa kuumia au anapopata matatizo ya kisaikolojia. Yatakuwa ni maisha ya hatari sana iwapo mwanadamnu atakosa uhakika wa kupata mahitaji muhimu yaliyotajwa. Bila shaka akishindwa kula, atadhoofu kimwili na kiakili na hatima yake ni kifo. Kadhalika akikosa matibabu pale afya yake inapokumbana na maradhi, hatima yake ni kifo pia. Hata hivyo, katika hali ya kawaida, kula na kunywa ni mambo ambayo yapo ndani ya uwezo wa binadamu mwenyewe. Kwamba atahakikishia anatumia nguvu zake na uwezo wake kupata mlo. Hata serikali haina bajeti ya kulisha kila mtu katika himaya yake, ikiamini kuwa huo ni wajibu wa kila raia wake kujihakikishia mlo, malazi na mavazi. Msaada wa serikali katika mahitaji hayo muhimu ni iwapo tu, jamii imepatwa na majanga au maafa. Lakini katika suala zima la afya za watu, haiwezekani kila mmoja akawa mfamasia, mkunga, muuguzi au daktari wa kujitibia au kutengeneza dawa pale anapougua au kupata madhara ya kiafya. Katika hili, serikali au taasisi zinawajibika kutoa huduma hiyo ili kulinda afya za watu wake. Na katika jukumu hili la serikali, utendaji unakuwa ni wa huduma zaidi kuliko biashara, kwa kuwa kulinda afya na uhai wa watu wake ni jambo la msingi kwa mwanadamu yeyote. Kadhalika mashirika ya dini kwa uhalisia wake, yamebuniwa kwa ajili ya kutoa huduma za kiroho na kimwili kwa watu. Lakini lengo kubwa zaidi ni kuhakikisha kuwa huduma zinazotolewa na mashirika haya ya dini, zinakuwa na nafuu na za kiutu zaidi, kwa kuwa zinafuata zaidi misingi ya imani za kidini katika kutoa huduma hizo za kiroho na kimwili. Kwa msingi huo, sehemu kubwa ya mashirika ya kidini, ambayo mengi ni ya hiari, kujitolea au ya kusaidia, yamekuwepo kwa ajili ya
nafuu kwa wananchi. A i d h a , M b u n g e h u yo aliihoji serikali kama iko tayari kupandisha hadhi zahanati ya Bumbile, ili iweze kuhudumia visiwa vya Bumbile, Kalebe na Makibwa vilivyo mbali na hospitali za misheni za Ndolage, Rwantege na Kagondo. Dk. Rashidi alilieleza Bunge kuwa ruzuku hiyo inayotolewa na serikali, ni mbali na ile iliyotolewa na halmashauri za mashirika ya dini kutoka katika mfuko wa maendeleo na mishahara ya watumishi walioshikizwa katika hospitali hizo. Sambamba na hilo, Waziri Rashid alisema serikali inaendelea kuboresha mazingira yatakayoziwezesha hospitali hizo ziweze kutoa huduma bora kwa wananchi kwa gharama nafuu. Ukiacha ruzuku hizo kutoka serikalini na katika Halmashauri zake, ni wazi kwamba, serikali kwa miaka m i n g i i m e k u wa h a i t o z i kodi (VAT) katika bidhaa zinazoagizwa au kuingizwa nchini na taasisi za dini. Bidhaa hizo ziwe zinaingizwa nchini kama misaada au zimeagizwa na taasisi husika, hazitozwi kodi. KCMC ikiwa ni taasisi ya dini, nayo ni mongoni mwa taasisi zinazofaidika na kuondolewa kodi hii. We n g i t u n a k u m b u k a namna serikali ilivyowasilisha taarifa yake bungeni ya kuondoa msamaha maalumu wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa mashirika ya dini, baada ya kubaini kupoteza mapato mengi kupitia mwanya huo. Hii ilikuwa ni katika mjadala wa bajeti ya serikali bungeni mwaka 2009/2010. Hoja ya serikali kufuta msamaha huo ilikuwa ni kufuatia kubaini kwamba imekuwa ikipoteza mapato mengi kupitia misamaha ya kodi kwa taasisi hizi, lakini msamaha yenyewe ilikuwa ikitumiwa vibaya na nafuu yake haiwafikii walengwa hivyo kupoteza lengo la serikali. Badala yake inawanufaisha wajanja wachache wanaoendesha taasisi hizo za dini. Kwamba serikali inatoa misamaha kwa mashirika na taasisi za dini, ili kuzipa nafuu taasisi hizo kuwahudumia wananchi kwa gharama nafuu zaidi. Lakini hali haikuwa hivyo, kwani huduma bado ziliendelea kuwa za gharama za juu na za kibiashara zaidi na kunufaisha watu wachache
Inaendelea Uk. 4
Habari
AN-NUUR
Asa Elimu wa Mkoa wa Kagera, Florian Kimolo ya mwavuli wa Dini na Maadili, wao hawakupinga msimamo wao ukawa sawa na ule wa EDMASHUTA. Msomi wa Chuo Kikuu aliyeshiriki warhsa ile (Mkristo) aliishangaa serikali kuvunja katiba kwa kuingilia mambo ya dini. Kama inavyoelezwa katika nyaraka mbalimbali, malengo makuu ya E D M A S H U TA n i ( i ) Kuhakikisha somo la DINI na MAADILI linafundishwa vema shuleni kuanzia shule za awali hadi vyuoni. Pili, kuboresha mihutasari na mitaala ya somo la dini katika shule za Msingi na sekondari na kuandaa mihutasari na mitaala kwa vyuo vya Ualimu TatU, kuweka mikakati ya kuandaa walimu na njia bora za kufundishia na kujifunzia somo la dini na maadili. Inaelezwa kuwa sababu kubwa ya kuja na Somo la Dini na Maadili ni kuwa iliyotolewa ni kuwa (eti) masomo ya Islamic Knowledge na Bible hayahusianishwi na maadili mfano vita dhidi ya ukimwi, rushwa, ukahaba, ubakaji, ugaidi, ujambazi n.k Na kwamba somo hilo ni muhimu katika kuimarisha nguvu katika mshikamano wetu na umoja miongoni mwa Watanzania ili kujenga maadili. H o j a ya m s i n g i ya Waislamu ni kuwa kuwa na somo moja ambalo linaweza kusomeshwa na John au Ali, maana yake ni kuwa kwanza utakuwa umechanganya Qur an n a B i b l i a n a k u f a n ya rejea moja ya dini wakati vitabu hivyo havipo sawa. Pili, utakachokuwa unafundisha hakitakuwa na imani ya Mungu wala uchamungu. Itakuwa ni academics kama ilivyo jiografia na masomo mengine. Lakini hoja nyingine ni kuwa maelezo yanayotolewa kuwa mihutasari ya somo la dini kuwa hayahusishi imani na maadili, hayana ukweli kwa kuwa kwanza yanatolewa kwa ujumla mno lakini pili tofauti na Ukristo Uislamu ni mfumo mzima wa maisha ya binafsi na kijamii na katika kufundisha Uislamu mambo yote yaliyotajwa kama mapungufu yamezingatiwa katika mihutasari ya somo la Islamic Knowledege n a E l i m u ya D i n i ya Kiislamu. Utati zaidi unaonyesha kuwa jambo hili limekuwa likifanywa kwa siri mno tangu mwaka 2004 ilipotangazwa kwa mara ya kwanza kuwa serikali ina mpango wa kufundisha somo la Dini moja. Waislamu walipopinga kwa kumuandikia barua Rais wakati huo mheshimiwa Benjamin William Mkapa, EDUSHUTA ikabadilishwa na kuwa EDIMASHUTA m wa k a 2 0 0 6 a m b a p o walikutana na Rais Kikwete na kuanza mchakato wa Dini na Maadili.
AN-NUUR
Katika rai ya viongozi h a o k wa Wa z i r i M k u u , ilikuwa ni kuisihi serikali kusitisha azma hiyo, kwa vile ingeweza kuleta sura mbaya kwa wahisani wa nje, ambao ndio wanasaidia mashirika hayo kuleta misaada nchini. Waziri Pinda alisema aliwaelewa viongozi hao, ingawa pia aliwaeleza nia nzuri iliyokuwa nayo serikali katika mpango huo, kwani fedha hizo zingekusanywa zingeweza kuleta mchango mkubwa kwa maendeleo ya wananchi wote. Viongozi hao wa mashirika ya dini waliahidi kuisaidia serikali katika kuwasaka na kuwadhibiti viongozi wa dini wanaotumia mianya ya misamaha hiyo. Akiwasilisha bajeti ya serikali kwa mwaka 2009/2010, aliyekuwa Waziri wa Fedha, Bw. Mustafa Mkulo, alisema hatua ya kufuta misamaha ya kodi itahusisha madhehebu yote ya dini na kwamba haitahusu vifaa vya kiroho na ibada. Alisema serikali imefikia hatua hiyo baada ya kubaini taasisi kadhaa za kidini zinatumia vibaya misamaha hiyo na badala yake kujinufaisha binafsi. Alisema serikali imetangaza kufuta matangazo 405 yanayotoa misamaha ya kodi kwa kampuni binafsi, asasi zisizo za kiserikali zikiwamo taasisi za dini na mashirika ya miradi ya kimataifa. Wengi tunafahamu kuwa
hata katika ule mkataba kati ya Serikali na Makanisa (MoU) wa mwaka 1992, pamoja nakwamba unaitaka Serikali kuyapa makanisa misaada ya kifedha, lakini pia ulikuwa unaibana serikali kuziombea taasisi za makanisa misaada. Bila shaka mkataba huo umekuwa kichocheo kikubwa cha taasisi kama KCMC kunufaika. Pamoja na kuwepo fursa zote hizo, inashangaza na kusikitisha kwamba hospitali hizi za mashirika ya dini ndizo zimekuwa vinara wa gharama za juu za matibabu nchini. Tu n a h o j i , s a s a k u n a haja gani ya serikali kutoa misamaha ya kodi na kutoa ruzuku kwa mashirika haya ya dini huku yakiwa vinara
wa kutoza gharama kubwa za matibabu? Kwa bahati mbaya kabisa, serikali pamoja na kuchota fedha hazina na kuzipa taasisi hizi za kidini, lakini haina mamlaka wala ujasiri wa kufanyia ukaguzi fedha zake iwapo zimetumika kihalali. Nieleweke tu kwamba, s i p i n g i m a s h i r i k a h a ya ya dini kuongeza bei ya huduma zao. Bali yangeweza kufanya hivyo, kwanza kwa kutochukua ruzuku serikalini, ruzuku ambayo ni zao la kodi za Watanzania wote. Pili, iwapo taasisi hizi za dini zingekuwa hazina misamaha ya kosi ya serikali na wala hazina mgawo wowote kutoka MSD wala Halmashauri zetu. Inaendelea Uk. 5
STASHAHADA (DIPLOMA)
AWE AMAMALIZA KIDATO CHA S ITA NA KUPATA KUANZIA PRINCIPLA (E) 1 NA S UBS IDIARY (S )-1
CHUO NI CHA BWENI KWA WASICHANA NA WAVULANA HUDUMA ZETU NI ZA KIWANGO CHA HALI YA JUU. ADA NI NAFUU SANA KULIKO POPOTE NA INALIPWA KWA AWAMU WAHI SASA NAFASI NI CHACHE WAHITIMU WOTE WANAAJIRIWA SERIKALINI
KUJIUNGA NA CHUO PIGA SIMU MOJA KWA MOJA CHUONI
MKUU WA CHUO
0713 673495
MAELEZO: 1 . WA N A F U N Z I W O T E WA L I O C H A G U L I WA WANATAKIWA KUCHUKUA MAELEZO YA KUJIUNGA NA SHULE (JOINING INSTRUCTION) SHULENI .PIA UNAWEZA KUPATA MAELEKEZO KWENYE TOVUTI:www. ipctz.org 2. SHULE ITAFUNGULIWA RASMI TAREHE 30/06/2013. 3. MAOMBI MAPYA YANAENDELEA KUPOKELEWA HADI TAREHE 23/06/2013.HIVYO NENDA KACHUKUE FOMU NA UIRUDISHE UBUNGO AU NYASAKA ISLAMIC KABLA YA TAREHE HIYO. KARIBU NYASAKA ISLAMIC HIGH SCHOOL NA TUNAWATAKIA MAANDALIZI MEMA. WABILLAH TUFIIQ MKUU WA SHULE.
5
ALIYEKUWA mfanyikazi wa shirika la Ujasusi la CIA nchini Marekani Edward Snowden, ambaye alitoa siri ya serikali yake kuchunguza mitandao na mawasiliano ya simu za watu duniani sasa hajulikani aliko. Snowden, aliyefichua siri hiyo akiwa Hong Kong ametoweka baada ya kuondoka ghaa kwenye hoteli alimokuwa anaishi. Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 29, alisema kuwa aliamua kutoa siri hiyo kwa lengo la kuwakomboa watu duniani kutoka serikali ya Marekani na kuionyesha
Habari za Kimataifa/Tangazo
AN-NUUR
Baada ya kukosa nafuu zote hizi wanazopata, hapo wangekuwa na hiari ya kupandisha gharama vile wanavyotaka. Hakuna angewauliza. Lakini pia wanastahili kuondoa hizi kauli mbiu za huduma nafuu ambazo tunazo na kama geresha za kidini kama msamaria mwema nk. wakati wao wanafanya biashara kamili. Niseme tu kwamba umeka wakati sasa serikali kuamia kwa dhati kwamba haipo tayari kunufaisha kundi la watu wabinafsi wachache na kuwaangamiza wananchi walio wengi. Hizi ruzuku na misamaha ya kodi, ikiratibiwa na kusimamiwa vizuri, inaweza kuwa ahueni kwa Watanzania wote. Kuna haja kwa serikali sasa kufuta mara moja hii misamaha inayonufaisha wajanja wachache, na fedha i n a yo p a t i k a n a i n a we z a kusaidia kujengwa vituo zaidi vya afya nchini. Pia kwa serikali kuondoa ruzuku na misamaha katika mashirika ya kidini yaliyokosa utu na uaminifu, kunaweza kuleta ongezeko kubwa la mapato ambayo yatasaidia kupatikana huduma bora, nafuu na za kuaminika kwa Watanzania wote katika hospitali za rufaa mikoani kama Mawenzi, Sekou Toure, Amana, Mwanayamala nk. Kama lengo la serikali ni kutoa huduma nafuu za afya kwa wananchi wake, basi wakati ni sasa wa kufanya maamuzi bila hofu. Taasisi za dini zilianzisha vituo vya afya kwa hiari yao kwa lengo la kuisaidia serikali kutoa huduma kwa wananchi. Hazikuanzishwa ili zisaidiwe na serikali kujiendesha katika kutekeleza kazi hiyo. Wao waisaidie seriali, sio serikali wazisadie taasisi hizo huku zenyewe zikifanya biashara. Kazi ya seriali ni kuzipa vibali na kuziwekea miundo mbinu kama barabara, maji, umeme nk. Sio kupewa
OUAGADOUGOU Serikali ya Mali na waasi wa Tuareg wamekubaliana kuhusu kufanyika kwa uchaguzi Mkuu mwezi ujao katika eneo la Kidal, ambalo kundi hilo linathibiti. Maafikiano hayo yalikiwa siku ya Jumatatu jini Ouagadougou, nchini Burkinafaso baada ya siku tatu ya mazungumzo kati ya pande mbili hizo, muda mfupi baada ya majeshi ya serikali kuanza oparesheni dhidi ya kundi jingine la waasi la MNLA. Kundi la MNLA limekataa wito wa serikali ya Mali kurudisha silaha na linapinga kuwasili majeshi ya serikali mjini Kidal. Serikali ya Ba ma k o imekuwa ikisema inataka kusimika uongozi wake katika eneo la Kidal kabla ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 mwezi ujao na kutishia kuchukua mji huo iwapo suluhu haitapatikana. Kundi la Tuareg kwa muda mrefu limekuwa likitaka kujitenga na kujiongoza kivyao na wanaliita Azawad kwa madai kuwa eneo hilo l i m e k u wa l i k i t e n g wa kimaendeleo na kisiasa na uongozi wa Bamako. Baada ya kufanyika mapinduzi ya serikali n c h i n i h u m o m wa k a uliopita, kundi la Turaeg
Pamoja na hayo tunahoji kilichoisukuma uongozi wa hospitali hiyo kupandisha gharama ghafla huku ukitambua kuwa hospitali hiyo imeteuliwa na serikali kutoa huduma kwa wananchi kwa mujibu wa makubaliano na serikali na kupokea ruzuku.
Edward Snowden.
italiachia jeshi la Umoja wa Mataifa jukumu la kulinda amani mwezi ujao, baada ya kuwepo nchini humo tangu mapema mwaka huu (r.fr).
6
Na Hashim Saiboko KWA muda mrefu sasa Wa i s l a m u w a m e j e n g a hoja kwamba kuna ubaguzi ambapo wananchi hawatendewi sawa na kwamba ubaguzi huu hufanywa na baadhi ya watendaji wa serikai na taasisi za umma. Waislamu wameweka wazi kwamba utaratibu huu ambao ni haramu kwa kuwa uko kinyume na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siyo mfumo rasmi. Aidha wamekuwa wakieleza kwa kutumia vigezo vinavyokubalika kisayansi kwamba mfumo huu unaendeshwa na watu binafsi ambao unaweza kusema kuwa wana mawazo ya kibaguzi, chuki na kwamba hawaitakii mema nchi yetu. Lakini kwa bahati mbaya watu hawa wapo wengi na mahali pengi katika sekta mbalimbali hapa nchini. Katika makongamano ya kitaifa yaliyofanyika mwaka 2011 Diamond Jubilee na pia nchi nzima Waislamu waliwasilisha rasmi serikalini kijitabu kilichojaa vielelezo jinsi serikali inavyotumia rasilimali za umma kulinufaisha kanisa. Katika kijitabu kile na kwenye makongamano yao Waislamu wameuelezea utaratibu huu wa kuwabagua na kuwalazimisha wao kuwa raia wa daraja la pili kwa jina la mfumokristo. Lakini sasa inaonekana nongwa kutamka msamiati huo. Nadhani muhimu hapa sio neno. Tuchukue tafsiri halisi ya wanaotoa msamiati huo na kuangalia madai yao kama ni ya kweli au la. Tuwahukumu kwa ukweli au uwongo wa madai yao sio kwa msamiati. Pamoja na harakati zote za kuzunguka nchi nzima kueleza mawazo yao juu ya ubaguzi wanaoona kufanyika nchini, serikali haikujali wala kusema lolote juu ya madai hayo ya Waislamu. Ilipiga kimya. Baada ya muda kupita na kama tulivyotegemea maaskofu walianza kuishinikiza serikali iwachukulie hatua watu inaodai wanachochea mauaji, uharibifu wa mali za makanisa na uvunjivu wa amani. Kama tulivyozoea huko nyuma na kama tulivyoona wakati wa mauaji ya Mwembechai mwaka 1998, serikali ghaa ikaibuka na kuanza kutoa vitisho kwa Waislamu. Waislamu waliokutana Diamond Jubilee na viongozi wao wakawa ndiyo walengwa. Maaskofu wanataka wakamatwe na
MAKALA
AN-NUUR
DKT. Joyce Ndalichako, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania kuchukuliwa hatua mara moja. Katika mlolongo huo kwa mara ya kwanza hotuba ya Rais ya mwisho wa mwezi wa Machi 2013 ikaongelea kwa kirefu dhana ya mfumokristo. Vyombo vya habari na waandishi wa habari, maaskofu wenyewe na watendaji wa serikali, wanalenga kuharibu maana ya dhana ya mfumokristo. Upotoshaji huu ni wa makusudi kwani tafsiri halisi ya neno hili imo kwenye kijitabu nilichokitaji ambayo imewasilishwa serikalini na bila shaka kama ambavyo maaskofu waliweza kupata DVD za makongamano ya Waislamu yaliyofanyika kote nchini, pia watakuwa wamepata kijitabu kile. Katika sehemu yake ya utangulizi dhana ya mfumokristo imeelezwa kama ifuatavyo, Hivi sasa imebainika kwa Waislamu na wananchi wenzao walio wengi nchini kwamba Mfumokristo, ni mfumo wa UDINI dhidi ya Uislamu na Waislamu . Japo kwa misingi ya kiserikali mfumo huu haupo rasmi, kiutendaji, mfumo huu umefanywa kuwa mila, desturi na utamaduni wa watendaji walio wengi serikalini na katika taasisi za nchi ambako unatumika kukandamiza na kudhulumu haki za Waislamu. Aidha utamaduni huu umeenezwa pia kwa watendaji walio wengi katika taasisi za umma, jumuiya zisizo za kiserikali na katika baadhi ya mashirika binafsi nchini. Kwa kutumia dhana hii hutashangaa kuona kwamba juhudi zinafanyika kupotosha ukweli kwani hakuna anayeweza kusimama kutetea ubaguzi. Ndiyo tunaona zinafanyika juhudi za kunyamazisha sauti za wale wanaopinga mfumo huo. Na kama ulivyokuwa msemo wa Kiingereza dead man tell no tales hivyo ukitaka kuvuruga ushahidi unaua shahidi. Labda tujikumbushe nini hasa ulikuwa ujumbe wa Waislamu kwa wenzao. Tazama utangulizi wa waraka wa Waislamu uliosomwa Diamond Jubilee 16.10.2011, kauli ya Waislamu katika makongamano yaliyofanyika sehemu zote nchini inawakumbusha na kuwanasihi viongozi wa nchi, serikali, vyama vya siasa, taasisi na mashirika yote kwamba Waislamu ni binadamu, na Watanzania, Waislamu ni wananchi. Wana haki ya kuheshimiwa na kuthaminiwa kwa misingi hiyo. Kuendelea kuwabagua na kuwakandamiza, siyo tu kunawagawa wananchi kitaifa; bali kunaandaa mazingira ya vurugu na machafuko yanayoweza kutokea hapo baadae. Maana kanuni ya ukandamizaji huzaa ukombozi. Na ukombozi hutokea pale wadhulumiwa wanapoona njia zilizopo za kuondoa dhulma hazitumiki kwa makusudi. Na hivyo
7
Na Mwandishi Wetu
Matangazo
SHAABAN 1434, IJUMAA JUNI 14-20, 2013 likipendekezwa na tume zote zilizowahi kuundwa kuhusu muundo wa Muungano. Bomani alizitaja tume hizo kuwa ni ya Jaji Francis Nyalali ya mwaka 1991 na Kamati ya Jaji Robert Kisanga ya mwaka 1998. Alisema, muundo wa Serikali mbili uliopo ulibuniwa haraka haraka na waasisi wa nchi hizi mbili Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Hayati Sheikh Abeid Karume na kwamba muundo huo umekuwa ndio chanzo cha migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara hasa kwa upande wa Zanzibar. Kwa upande mwingine, wakati Jaji Bomani akitoa maoni ya kuunga mkono Serikali Tatu, Kamati Kuu ya CCM iliyokutana Dodoma imetoa tamko linaloonesha kuwa bado chama hicho kinapigania kuwepo kwa Serikali mbili. Hata hivyo, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya
Inaendelea Uk. 11
AN-NUUR
VIONGOZI wa Uamsho walikuwa wakiuliza, Je, mnautaka? Sasa Jaji Mstaafu wa Tanzania Jaji Mark Bomani anasema kuwa ingekuwa vyema kabla ya kujadili muundo wa muungano, watu waulizwe je, bado wanautaka? Bomani alisema kabla ya rasimu hiyo haijapendekeza muundo wa Muungano wananchi walitakiwa waeleze kama bado wanautaka au la. Hivyo ndivyo alivyonukuliwa Jaji Bomani na baadhi ya magazeti wiki hii yakiarifu alivyotoa maoni yake alipozungumza na waandishi wa habari juu ya maoni yake kuhusu rasimu ya katiba mpya. Katika maoni yake, Jaji Bomani amepinga kutumiwa jina la TANZANIA BARA. Amenukuliwa akisema: Hili jambo la kuziita katika Rasimu ya Katiba
Mpya Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Zanzibar silipendi hata kidogo, tunaogopa nini kuiita Serikali ya Tanganyika. Jaji Mark Bomani ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa zamani, amesema kuwa kabla ya muungano kulikuwa na Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar ndio zikafanya Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania. Sasa kama tunarudi kuwa na serikali tatu, basi turudi kwa Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar. Akizungumza na waandishi wa habari mapema wiki hii, Jaji Bomani alisema: Pendekezo la kuwa na Serikali tatu limekuwa
INAWATANGAZIA NAFASI ZA MASOMO KIDATO CHA TANO (V) KWA MWAKA WA MASOMO 2013/2014
SHULE IPO CHALINZE WILAYA VA BAGAMOYO KILOMETA 7 KUTOKA NJIA PANDA YA CHALINZE-TANGA KUELEKEA MOROGORO. M I C H E P U O T U N AY O S O M E S H A N I - P C M , P C B , CBG,PGM,EGM,HE,HGL,HGK, HKL, HKA, KLA,HGA, KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA UONGOZI KWA NAMBA ZIFUATAZO: 0762-270378 0657-935148 0784-323203 FOMU ZlNAKOPATIKA MIKOANI KATIKA VITUO VIFUATAVYO: CHALINZE: Shuleni 0762270378, 0657935148, 0784-323203 Zanzibar: Rashid Masoud-Simu: 0777-478246 Dar es Salaam: Hassanali (Koosa stationery) - Simu: 0719-350044 au Yahya Tatee (Kariakoo)-Simu: 0715-361444 MOROGORO: Rama (Wastara) - Simu: 0718-778300 au Mohamed Shayo - MUM Simu: 0717-172804 Iringa: Sheikh Abdulkarim Mshana-Simu: 0715878883, au Sheikh Shamsi Elmi 0784 448484. Mbeya: Sheikh Suleman (Osi za Happy Nation) - Simu: 0783-840060. Tanga: Shemtoi (Raha Stationery) - Simu: 0714-335030. Mombo: Sheikh Biko (Lango la Msikiti Mkuu) simu: 0754 983733. Handeni: Sheikh Maga-Simu: 0657-093983/0782105735 Moshi: Mzee Issa Simu- 0766-796807 (Muuza Magazeti Msikiti wa Riadha) au KUTAYBA SACCOS Moshi Simu- 0716-109000 /0713-719441 Hai: Smart Stationery Services - Simu: 0717-806566 Arusha: Imamu Hambal Simu-0754-290329 Msikiti Mkuu wa Ijumaa au Abdulkarim Kandahar Simu- 0754 316948 (Masjid Qubah Shopping Centre). Babati:-Sheikh Juma Ibuva Simu-0714-262706 Singida: Sheikh Ramadhani ni Mtipe- Simu: 0786-797695 Dodoma: Sheikh Said Chobo-Simu: 0712-217072 Tabora/Nzega: Garden Cafe: Simu: 0784-640112 Kondoa: Mwalim Jabir Issa Isere-Simu: 0784 780869/0716 588420 Ibra Line Booking Ofces: Arusha, Moshi na DSM MLETE MWANAO CHALINZA ISLAMIC SEMINARY KWA DUNIA YAKE NA AKHERA YAKE Wabillahit Tawq
MAFUNZO MAALUM YA UJASIRI AMALI JINSI YA KUANZISHA BIASHARA BORA NA UANDAAJI WA MCHANGANUO WA BIASHARA
Jumuiya ya Wataalamu wa Kiislam Tanzania (TAMPRO) kupitia Kituo chake cha mafunzo na Ajira inawatangazia SEMINA YA UFUGAJI UJASIRI AMALI JINSI YA KUANZISHA BIASHARA BORA NA UANDAAJI WA MCHANGANUO WA BIASHARA kwa kutumia wataalamu wenye uzoefu wanaoshughulikia masuala hayo kwa muda mrefu. Semina itakuwa kama ifuatavyo:Walengwa: Wafanyabiashara wadogo wadogo, wahitimu wa vyuo vikuu na vya kati, wanaotaka kuanza biashara na watakaopenda . Siku: Jumamosi na Jumapili terehe 29 - 30 June 2013 Muda: Saa 3:00 asubuhi - 10:00 jioni Mahala: Osi Kuu ya TAMPRO Magomeni Usalama, Dar es Salaam Mada: ujasiri amali na mjasiriamali, uamuzi sahihi wa biashara unayotaka, uamuzi wa mshirika sahihi katika biashara, muundo bora wa biashara yako, uteuzi wa uongozi bora. kuanguka kwa biashara, leseni ya biashara (umuhimu wake na jinsi ya kupatikana), muundo wa mchanganuo wa biashara, kutengeneza mchanganuo bora wa biashara. Kujisajili: Shilingi 50,000/= kwa mtu mmoja. (Kwa ajili ya cheti cha ushiriki, Kitabu cha muongozo, na chakula). Kikundi/jumuiya ikisajili watu 10 watalipia 40,000 tu kila mmoja. Muhimu: Washiriki watapatiwa vyeti na kitabu cha muongozo kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili ili kukidhi haja. Pia watapata fursa ya kutengeneza michanganuo kivitendo chini ya usimamizi wa wataalamu bobezi katika fani ya uandishi wa miradi. Kujisajili: Ili kujisajili lipia ada yako kwenye namba 0714 151532, 0767151532 au ka TAMPRO Makao Makuu, Magomeni Usalama, jirani na Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni. Wahi kuijiandikisha kwani nafasi ni chache. Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia 0714 151532, 0767151532, 0716234391 MRATIBU MAFUNZO TAMPRO MAKAO MAKUU
Makala/Tangazo
AN-NUUR
Na Khalid S Mtwangi
INAFAHAMIKA kwamba viongozi wa Makanisa yote ya kila madh-hebi za Kikristo huwafundisha waumini wao uwongo mwingi kuhusu Uislamu na Waislamu. Nimebahatika kuvipata baadhi ya vitabu ambavyo hawa viongozi huwa wanavitumia kuwafundisha waumini wao Uislamu ni nini. Hapa chini naorodhesha baadhi ya mafundisho hayo. Waislamu, hasa masheikh na alim wote kwa jumla wayatafakari haya khalafu bila kukosa tafadhali wawaambie Waislamu ukweli uko wapi kati ya haya wanayozua Makasisi wa Kikristo na yale wao masheikh na alim wanayo wawaidhi waumini wao. Kwa Mfano imeandikwa: As a young man Muhammad was employed by Khadija, a wealthy widow, to manage her caravan trade. Although she was fifteen years her senior, Muhammad married Khadija when he was twenty-veAFTER HER D E AT H M U H A M M A D MARRIED A FURTHER T W E LV E W I V E S , THEREBY SANCTIONING P O LY G A M Y. ( Ta f s i r i : Akiwa kijana Muhammad aliajiriwa na Khadija, mwanamke tajiri, kuangalia misafara ya biashara. Ingawa Khadija alikuwa mkubwa kwake kwa miaka kumi na tano, Muhammad alimuowa Khadija wakati akiwa na umri wa miaka ishirini na tano. Baada ya kifo cha Khadija, Muhammad alioa wake kumi na mbili zaidi na hapo akahalalisha ndoa za wake wengi). Ni kweli hayo? Mengine yanahusu historia ya Uislamu Afrika ya Mashariki; kwa hili wapo waalimu wa zile shule za Kiislamu ambao bila shaka wao wanawafundisha wanafunzi wao historia kama hiyo. Ipi sahihi hiyo wao wanayoifundisha ama hii wanayoimwaga Makanisa kwa waumini wao? Ikumbukwe kwamba takriban
mara zote, na hasa katika Kanisa Katoliki, analosema kiongozi wa Kanisa huwa halipingwi; ni ukweli kama vile Injili. Mengine yanaweza kabisa kuwa ni kashfa dhidi ya Uislamu, hivyo inakuwa ni jukumu la ulema kutuongoza hivyo watupe ukweli. Ikiwa kweli ni kahfa ni kwa vipengele gani. 1 Jina la kitabu: LAW GROSSARY OF ISLAMIC TERMS IN SWAHILI by Dr. Jan Knappert; P u b l i s h e d b y B E N E D I C T I N E P U B L I C AT I O N S , NDANDA-PERAMIHO, 2001 Mwandishi wa kitabu hiki, Jan Knappert, anasema hivi katika utangulizi:During the rst years of independence I was secretary of the Law Translations Committee, a body created by Sheikh Amri Abedi, who was, until death in early 196, Minister of Justice in the Republic of Tanzania. (Nadhani hakuna haja ya kutafsiri hili la kujigamba kwake) Kuhusu Iran ameandika hivi:If one asks about Iran, the reaction is either They practice the same Islam or They are wandering in error; because they worship Husayn, they are polytheists a n d s i n n e r s ( Ta f s i r i Wanafuata Uislamu huu huu. Ama Wanahangaika wakipotea kwa sababu wanamuabudu Husayn, wao wanaabudu miungu wengi (washirikina?) na ni watenda dhambi) pg. 9. 2. Anaendelea sasa akiingia katika historia:From the Portuguese records of the sixteenth and seventeenth century (sic) one may conclude that Islam was almost totally eradicated in towns like Mombasa and Malindi, the chief ports of the Swahili coast. Malindi was abandoned in midseventeenth century and so was Quelimani (now the ruins of Gedi) as a result of the Galla raidsWitu was destroyed by the British and Bagamoyo and Pangani by the Germans at the beginning of the colonial period Tafsiri: Kutokana na kumbukumbu za Wareno za karne ya kumi na sita na kumi na saba mtu anaweza kuamua kuwa Uislamu uliteketezwa kabisa kutoka miji kama vile Mombasa na Malindi, zilizokuwa bandari muhimu pwani ya sehemu za Waswahili. Waliikimbia
25% but not much higher. Islamic publications usually exaggerate their statistics. (Tafsiri: Huko Tanganyika Fr Schildknecht (Bavarian?) mtaalam bora kabisa, anakisia idadi ya Waislamu ni 22% mwaka 1963. Kuongeza Zanzibar na Pemba asili mia ya Waislamu sasa inaweza kuwa 25%, sio zaidi sana ya hapo. Majarida ya Waislamu kwa kawaida hutia sana chumvi takwimu zao). P 11 Pamoja na haya bila shaka Waislamu watakumbuka huko nyuma magazeti yanayochapishwa na baadhi ya makanisa ya nchi hii hakika yalikuwa yakichapisha kwa mapana kabisa hayo waliyokuwa wakisema kuwa ni tafsiri za Kuran na Hadith. Walika hata kuandika kuwa Rasuul-Llah Muhammad SAW alikufa kwa sababu aliugua UKIMWI. Astaghfirullah. Wa i s l a m u w a l i p o k u w a wakiwaandikia kutoa maelezo yaliyo sahihi wachapishaji wa magazeti hayo hawakuyatoa yale maoni na mafundisho waliyoyaandika Waislamu. Hawa hawakushutumiwa kwamba walikuwa wakikashifu dini zingine. Wasomaji tunawarifu kuwa makala hii itaendeklea wiki ijayo, inshaallah.
Waislamu wote nchini mnaalikwa kuhudhuria Tamasha la Ujenzi wa Kituo cha Kiislamu Shenge Juu Pemba litakalofanyika kuanzia tarehe 28, Juni 05 Julai, 2013. Shime Waislamu tujitahidi kuhudhuria kwa wingi. Wasio na wasaa wa kuhudhuria wachangie fedha na vifaa vya ujenzi. Tukumbuke, tukifanya hivyo tutakuwa tumefanya biashara na Allah (s.w) kwa mafanikio ya hapa duniani na malipo ya Pepo Quran (61:10-13) Muhimu: Kwa kupitia Tanga nauli ya kwenda na kurudi ni Tshs. 50,000/-. Wanatamasha wote wataripoti Tanga tarehe 24/06/2013 (0715 894111/0787 894111). Kwa kupitia Dar es Salaam nauni ni Tshs. 80,000/- kwenda na kurudi. Kuripoti Dar es Salam ni tarehe 25/06/2013 (0783 812576/0716 058538). Kila msari awe na kitambulisho. Mwisho wa kukusanya Nauli ni tarehe 20/06/2013. Wabillah Tawiq AMIR
Tangazo
AN-NUUR
P.O. Box 55105, Dar es Salaam Tel: +255 - 2450069, 0712974428 & 0659 204013 Fax: 022-2450822 WASICHANA
PCB ECA CBG KLA PCB HKL CBG HKL ECA HGK EGM CBG PCB ECA HGL HKL EGM HKL HGL EGM ECA CBM ECA HKL HGK CBG PCB HGK
1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 14 15 16 17 19 20 21 22 23 24 25
26
ABDALLAH O. ABDI ABDULWAHID R. RAMADHAN ABUBAKAR S. MSEKWA ALLY H. RAMADHAN ALLY N. TIMAMY ALLY S. BYARUGABA FUAD H. AHMMED HAJI M. JUMA HAMAD I. HAMAD HAMIS A.MDEE HUSSEIN ABDALLAH ISACK Y. HASSAN MALIK U. HAMIDU MBARAKA M. KIGZA MOHAMMED AMIR MOHAMMED S. HAMAD RAMJI H. TELLACK RASHID I. MUSSA SALUM A. MOHAMMED SEIF N. SAID SUDI YASIN TWALIB H. JAFFAR YAQUB O. KILIMA
SAID ATHUMAN
EGM HKL EGM HGE PCB PCM PCM PCB ECA ECA HGK PCM PCM PCB ECA EGM HKL ECA CBG PCB PCM HGK HGE
HGK
MAELEZO: 1. WANAFUNZI WOTE WALIOCHAGULIWA WANATAKIWA KUCHUKUA MAELEZO YA KUJIUNGA NA SHULE (JOINING INSTRUCTION) SHULENI UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOOL. PIA UNAWEZA KUPATA MAELEKEZO KWENYE TOVUTI:www.ipctz.org 2. SHULE ITAFUNGULIWA RASMI TAREHE 30/06/2013. 3. MAOMBI MAPYA YANAENDELEA KUPOKELEWA HADI TAREHE 23/06/2013. HIVYO FOMU NA UIRUDISHE UBUNGO AU KIRINNJIKO ISLAMIC KABLA YA TAREHE HIYO.
KARIBU UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOOL NA TUNAWATAKIA MAANDALIZI MEMA.
NENDA KACHUKUE
10
Tangazo
AN-NUUR
11 12 13 14 15 16
17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 S/N 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47
IBRAHIM R. IBRAHIM IDD IBRAHIM MSOKE IDD KASSIM IDD ISMAIL HAMIDU MGAYA ISSA ATHUMANI IBRAHIM JIWA OMARY MSUNGU
JUMA HAJI JUMA JUMA HASSAN MUSSA JUMA KIBUA JUMA KHALID MUSTAFA KISATU KIBARY MWINYI MOHAMMED LUQMAN F. MTIKA MAKUNGU S. MAKUNGU MNG`WALA MOHAMED NASSORO MOHAMMED I. MATEMANGA MOHAMMED M. KABALA MOHAMMED O. MOHAMMED MOHAMMED T. FADHILI MUHAMMED R. MKONGO MULLAH M. MOHAMMED MWINSHEKHE H. IGUDU OMARI MOHAMED AWESO OMARY JUMANNE MSANGI RAMADHAN M. SHABAN SALEHE HAMISI KOMBO SHABAN A. NYANGE JINA KAMILI SHABAN IBRAHIM LUSAMA SIMAI SHAIBU NANDOPE SHARIF S. MWINDI SHOMAR R. IBRAHIM SHOMARI RAMADHANI JUMANNE SOUD SULEIMAN SOUD SULEIMAN ATHUMANI MALOZO SWALEHE HASSAN TARIQ ALAWI BARAKATI TARIQ SULEYMAN. SOUD YUSUF ABDALLAH MSANGI USAMA MOHAMED NASSOR
. 28
EGM
MCHEPUO
S/N
1 2 3 3 4 5 6 7 8 9 10
ABDALLAH I, ABDALLAH ADINAN HUSSEIN MZIMBIRI AHMADA A. JUMA ALLY M. ABDALLAH ALLY SALUM KHALFAN BABUU MOHAMED PAWA HAMID S. KAIS HAMZA HAMISI MAWAZO
HASHIM SHABANI MWASHEMBE
PCB HKL CBG HGK HGL HGE ECA PCB PCB PCB PCB
MAELEZO: 1. WANAFUNZI WOTE WALIOCHAGULIWA WANATAKIWA KUCHUKUA MAELEZO YA KUJIUNGA NA SHULE (JOINING INSTRUCTION) KATIKA SHULE YA UBUNGO ISLAMIC AU KIRINJIKO.PIA UNAWEZA KUPATA MAELEKEZO KWENYE TOVUTI:www.ipctz.org 2. SHULE ITAFUNGULIWA RASMI TAREHE 30/06/2013.KWA WANAFUNZI WANAOTOKEA DAR ES SALAAM KUTAKUWA NA USAFIRI WA PAMOJA SIKU HIYO.NENDA KALIPIE NAULI UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOOL KUANZIA TAREHE 25-28/06/2013. 3. MAOMBI MAPYA YANAENDELEA KUPOKELEWA HADI TAREHE 23/06/2013.HIVYO NENDA KACHUKUE FOMU NA UIRUDISHE UBUNGO AU KIRINNJIKO ISLAMIC KABLA YA TAREHE HIYO. KARIBU KIRINJIKO ISLAMIC HIGH SCHOOL NA TUNAWATAKIA MAANDALIZI MEMA. WABILLAH TUFIIQ MKUU WA SHULE.
48
PCB
11
Inatoka Uk. 7
Katiba, Jaji Joseph Warioba, ametahadharisha kuwa kungangania kuendesha nchi kwa kufuata mfumo wa sasa wa utawala wa Serikali mbili kunaweza kusababisha kuvunjika kwa Muungano badala ya kuuimarisha. Amesema, huu ni wakati wa kukubaliana na ukweli, kuzingatia na kuheshimu mawazo ya Wazanzibari vinginevyo tutaukosa kabisa Muungano uliodumu kwa takribani miaka 49 sasa. Jaji Warioba akiongea katika kipindi kimoja kinachorushwa na ITV alisema kuwa Zanzibar walikuwa na mambo mengi ya kutoridhishwa juu ya Muungano kuliko Tanzania Bara na kwamba Tume yake ilizingatia maoni ya walio wengi kabla ya kupendekeza mfumo wa serikali tatu. Kwa upande mwingine, msimamo wa Serikali mbili unaonekana kuelekea kukigharimu Chama Cha Mapinduzi hasa kwa upande wa Zanzibar ambapo
Inatoka Uk. 6 wanailalamikia kuwa ipo dhidi yao. Hawajali kama kufanya hivyo ni kinyume cha katiba ya nchi au ya chama cha siasa wanachokiwakilisha bungeni. Katika kulinda misingi hiyo huko bungeni basi wahusika hushirikiana bila kujali vyama na itikadi zao. Wabunge wa CCM huunganisha nguvu na akina Joseph Selasini (CHADEMA) - Rombo na Felix Mkosamali ( NCCRMAGEUZI) Muhambwe. Kauli ya Mheshimiwa Selasini kutuhumu uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma kuwa unaongoza chuo hicho kwa kuwabagua wanafunzi Wakristo haikukemewa na hao wabunge wa CCM waliochangia hoja za umoja na mshikamano katika mkutano wa kumsema Mheshimiwa Saidi Mtanda. Kwao udini ni kusema jambo litakalowanufaisha au kuwapa haki Waislamu. Kwa sababu hiyo hawakuonekana kushtushwa na matamshi hayo ya Selasini, lakini Mbunge wa Kondoa Kusini Mheshimiwa Juma Nkamia alipomkemea Selasini kama alivyonukuliwa akisema kwamba, Nadhani tatizo la pale UDOM ni Profesa Kikula na Profesa Mlacha (Shaban ) wanahukumiwa kwa dini zao, leo hii kungekuwa na Lyimo
Makala
SHAABAN 1434, IJUMAA JUNI 14-20, 2013 maoni yake unapaswa kuitwa Muungano wa Jamhuri za Tanzania, tofauti na ilivyo sasa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Maalim Seif amesema kuwa Zanzibar inahitaji kuwa na Mambo ya Nje, Sarafu, Benki Kuu, Uraia na Uhamiaji pamoja na Vyama vya Siasa. Tunataka Zanzibar iwe na uwezo wa kufanya mambo yake bila ya kuingiliwa, kwa mfano iwe na uwezo wa kujiunga na Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU), pamoja na FIFA, alieleza Maalim Seif. Ni katika mkutano huo ambapo Maalim Seif alikabidhi kadi za CUF 609 kwa wanachama wapya waliojiunga na chama hicho, ambapo ilielezwa kuwa 148 kati yao walirejesha kadi za CCM. Wakijieleza baadhi ya wanachama hao wapya wamesema kuwa wanataka kukipa nguvu chama ambacho kinapigania masilahi ya Zanzibar kama nchi na Serikali yake yenye mamlaka kamili.
vigumu kuelewa lengo la watu hawa kujidanganya kwamba amani maana yake ni Waislamu kunyamaza wakati wananyimwa haki zao. Na kama ilivyosemwa hapo juu bunge hili linaloendelea limetudhihirishia kwamba watu wenye mawazo ya kibaguzi hawaamini katika vyama vyao (CCM, NCCR-MAGEUZI, CUF na CHADEMA) zaidi kuliko wanavyojitoa kuulinda masilahi ya kundi fulani katika jamii. Mawakala hawa hawajali hata kama kwa hoja zisizokuwa na mashiko wataonekana majuha kwa wananchi. Hoja inatolewa kwamba NECTA inafelisha wanafunzi na kuwapasisha wengine kwa dini zao, lakini wakala wa kutetea ubaguzi anasimama na kusema, Dr Ndalichako ana PhD daraja la kwanza!!!!!! Hatua hii ya wabunge mawakala wa ubaguzi ndani ya CCM kuitisha kikao kuwajadili wale wanaojitoa kuinusuru nchi yao na madhara ya ubaguzi, kwetu sisi ambao wakati wote tumesimama kupinga ubaguzi haikutukatisha tamaa. Kitendo hiki kwetu ni kiashiria cha kuonesha jinsi wenye mawazo ya ubaguzi wanavyotapatapa. Na hili ni kwa sababu tunajua wazi kwamba ubaguzi haudumu.
AN-NUUR
pale haya yasingezungumzwa humu bungeni, wabunge hao hao walipiga kimya. Kuonesha ubalakala wa wabunge wa CCM, walipuuza pia taarifa za Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Mheshimiwa Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi alipoliambia bunge kwamba wako watendaji wa serikali wanaowahujumu mawaziri. Kauli hii ya Mheshimiwa Mwigulu imenukuliwa na gazeti la HabariLeo la Juni6, 2013 kama ifuatavyo, Kuna baadhi ya watendaji na wataalamu serikalini ambao si waaminifu wamekuwa wakiwaangusha mawaziri wetu kwa kusudi kwa sababu ya kutumiwa na watu. Naibu Katibu Mkuu huyo wa CCM aliyasema hayo w akati akichangia hotuba ya bajeti ya WEMU. Kwa akili ya kawaida tungedhani kwamba wabunge wa CCM wangeitisha kikao kujadili watumishi wa umma ambao wanatumia osi zao
mamia ya wanachama wake wameripotiwa kuhama na kujiunga na CUF. Inaelezwa kuwa wanachama hao wamekimbilia CUF kwa sababu wanaona kuwa chama hicho ndio chenye msimamo wa kuitetea Zanzibar kuwa na Dola yake huru yenye mamlaka kamaili. Katika mkutano wake wa hadhara hivi karibuni huko Matemwe, Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad alisema kuwa amefurahishwa na pendekezo la kuwa na Serikali tatu hata hivyo akasema kuwa kuna mambo kadhaa yanayohitajika kurekebishwa katika rasimu ya Katiba ili kukia lengo la kuwa na Zanzibar yenye mamlaka kamili. Ameyataja mambo hayo kuwa ni pamoja na jina la Muungano ambao kwa
kwani makusudio na maoni yaliyoambana na kuchapwa kwa barua zile yalionesha kulitetea Baraza la Mitihani na Dr Joyce Ndalichako na kujenga hoja dhidi ya Mheshimiwa Shukuru. Maneno haya ya Mheshimiwa Nchemba yanawiana na matukio haya ya kutaka kumsafisha Dr Joyce na kutia uzito hoja ya kumtaka Mheshimiwa Dr Shukuru Kawambwa ajiuzulu. Kwa kuwa kimantiki ilitarajiwa kwamba wabunge wote hasa wa CCM ambacho ndicho chama chenye mawaziri wanaohujumiwa na watendaji wasiokuwa waaminifu wakasirishwe na taarifa za Mheshimiwa Nchemba na kuitaka serikali kuwachukulia hatua watumishi hao, ukweli kwamba hao wanaojidai watetezi wa umoja na mshikamano wa kitaifa hawakuonesha kujali, basi inatulazimu kuhoji dhana ya amani kwa waheshimiwa hawa! Lakini pia inakuwa
12
AN-NUUR
MAKALA
12
2 Bw Nc uli dig
Bwana Yusuph Kileo (kushoto) akipokea tuzo aliyekabidhiwa na Kamishna Msaidizi wa jeshi la polisi Nchini Tanzania DCP Hamdani Makame Baada ya kazi nzuri aliyo ionyesha katika kuongezeza Ulinzi tovuti ya polisi Nchini Tanzania. Mwandishi Wetu KAMPUNI mbalimbali nchini yametakiwa kuwa makini na wizi wa mtandao kwa kujenga tabia ya kutoa mafunzo ya mara kwa mara kuhusiana na masuala ya ulinzi wa mitandao kwa wataalam wao. Aidha wametakiwa kujenga tabia ya kupitia mifumo (system) zao mara kwa mara ili kuhakikisha kuwa hakuna viashiria vyovyote vinavyoweza kuleta athari katika mitandao. Kampuni hizo zimetakiwa kuhakikisha k u wa z i n a wa t a a l a m ambao wapo tayari kujua na kuendelea kujifunza v ya n z o n a v i a s h i r i a mbalimbli vya uhalifu huu wa kimtandao na kuzuia mapema kabla hayajatokea ili kujiepusha na alichokiita fire fighting (kuhangaika kufanyia kazi tatizo baada ya kutokea). Hayo yameelezwa na Bw. Yusuph Kileo, ambaye ni mtaalam wa ulinzi wa mitandao na upelelezi wa makosa ya digitali, yaani Cyber security and Digital forensics investigation, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Hotel ya Holidai Inn jijini Dar es Salaam hivi karibuni, B w . K i l e o alisema makosa yanayosababishwa na utumiaji mbaya wa mitandao, yamekuwa yakiongezeka kila siku nchini Tanzania, Afrika na duniani kwa ujumla na kusababisha athari kubwa katika jamii. Alisema makosa hayo si tu yanaathiri Tanzania na Afrika pekee, bali yamekuwa tishio duniani
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.