Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 11

KITABU CHA SALA

Mwandishi: Moh'd Humaid Abdulla Al Khatry

YALIYOMO KITABUNI
(1) Neno la mwandishi 1 (21) Imamu akikosea 42
(2) Usafi-Tohara 7 (22) Adhana 48
(3) Kuoga 9 (23) Sala ulizoziacha 49
(5) Kutia udhu 9 (24) Sala ya msafiri 51
(6) Uchafu-najsi 13 (25) Sala ya ndegeni 54
(7) Damu 14 (26) Sala ya mgonjwa 55
(8) Dua za udhu 16 (27) Sala za sunna 58
(9) Kutayammam 17 (28) Sala za usiku 61
(10) Sala 22 (29) Witri 64
(11) Sala za faridha 25 (30) Taraweh 67
(12) Nguzo za sala 26 (31) Sala ya tawafu 69
(13) Namna ya kusali 29 (32) Kuomba haja 70
(16) Sala ya jamaa 34 (33) Kupatwa mwezi 73
(20) Yanayoharibu sala 38 (34) Sala ya maiti 74

basi (Muhammad) vumilia wanayoyasema na mtakase Mola wako (kwa kusoma sifa
zake) na msifu na kumshukuru (kwa kutaja wema wake) (yaani MUABUDU) kabla
kuchomoza jua na kabla kutua. Na nyakati za usiku mtakase (pia) na ncha za mchana ili
uridhike ( na utakayopewa).

(wafasiri wa Qur-an wengi, ikiwa ni pamoja na Skeikh Abdulla Saleh, wanasema kuwa sala tano
zimetajwa katika aya hii. Tazama tafsiri ya sheikh . Abdulla. Surat 20-130).

UTANGULIZI
Kitabu Kipya cha Sala
Chapa ya mara hii ni kitabu chengine kabisa kwani takriba nimefuata sawa sawa maagizo
niliyoyapata kutoka kwa wasomaji wa chapa za kabla yake isipokuwa kidogo sana. Pia nimeyatoa
mengine na kuongeza yale ambayo umuhimu wake umefurutu ada. Muhimu ni kuwa hichi kitabu
ni kidogo hakiwezi kuchukua mambo mengi. Kwa hivyo tutayaacha baadhi hasa yale yenye
kukataliwa na mashekhe wengine. Ndio maana mara nyengine hutumia neno baadhi kama baadhi
ya sunna na mara nyengine hata hatusemi baadhi ujuwe kama yako mengine tumeyaacha.
Naomba samahani kwa makosa yote ya lugha na uchapishaji na mengineyo, makosa
mkituonesha itakuwa bora tutayasahihisha katika chapa za baadae.Kwa kukusudia tumekariri
(tumeripiti) baadhi ya mambo usijali.

Chukuwa Chako Kimoja


Vitabu hivi hutolewa bure kwa waislamu lakini pia vinauzwa kwa sababu wengine haviwafikii
vya bure kwa vile wanakuwa wako mbali na wagawaji au wagawaji hawawapi, mara zote huwa
wanawapa jamaa au jirani au marafiki. Inasikitisha wengine huvieka zaidi ya kimoja katika
nyumba moja. Kwanini hawawapi wenzao. Hawataki thawabu. Ukimjuilisha mtu jambo la kheri
ni kama umelifanya. Licha ya kuwa umemsaidia kulifanya. Jambo jengine la kusikitisha ni kuwa
mtu atakuuliza suala ukishamjibu ukamwambia tazama katika kile kitabu atakwambia nipe
chengine kile sijui nilikiweka wapi. Huu si uungwana hata kidogo! Na kuna wakati wengi huwa
hawavipati hata kwa kutaka kuvinunua. Na kila mtu husema hajui chake kilipo.

Hata Kusali hutaki.


Hivi karibuni nilisikia qasida ambayo inamueleza mvivu au mchache wa imani akiambiwa "Hata
kusali hutaki". Kwani aliyekuwa hasali hana sababu hata ndogo ni kuwa hataki tu. Wenye sababu
za kukubalika ni mwenye hedhi, ujusi, kichaa-wazimu, na watoto wadogo. Hata mgonjwa sana
haruhusiwi kuacha kusali. Mtu asiache sala kwa kuwa hajui kusali au hana nguo au nguo yake si
safi au kwa kuwa amekwenda choo na hana maji au hajapata maji ya kuoga hedhi au hana maji
naye amepata janaba au ametiwa pingu kifungoni Mola atunusuru- wala asiache sala kwa kuwa
kuna vita milio ya bunduki inasikika kwa karibu au msafiri na chombo kinakwenda mrama au
anatoja mkojo au damu mfululizo pia ujana, kusahau, na hata kulala. Mtu asiache sala kwa hali
yoyote, muhimu ajuwe tu katika hali kama hizi atasali vipi. Inshallah kitabu hichi kimekusudiwa
kitusaidie. Kwa ufupi yanatosha maneno ya aliyesema:-
Mwenye kuacha kusali
Ndiye kafiri wa kweli
Kwa hadithi ya Rasuli
Sikia tena sikia

Na aliyemuusia:-
Nakuusia na sala
Usiiache Allah allah
Tutosheke na maneno hayo.

Makosa Yetu Katika Sala


Kisha kuna makosa mengi tunayafanya kwa kutoipa sala umuhimu wake wa kutosha
unayostahiki. Hapa nitataja kadiri nitayokumbuka ila tu nakuomba kila siku itazame sala yako
utafute njia nzuri zaidi ya kuitengeneza, Kwa lugha ya siku hizi kuiboresha, sala yako ndio
raslimali yako leo na kesho.
(1) Kuifanya sala ni ada ya kuinama na kuinuka tu labda na kusoma tukasahau ikhlasi na
khushuu. Wanasema kuifanya sala ni ada si ibada. Ikhlasi katika sala ni kusali kwa kumuabudu
Mungu peke yake na khushuu ni kumnyenyekea.
(2) Kungojea mpaka mtu awe mzee ndio aanze kusali maana dini na dunia, wanasema mambo
mawili haya hayaendi pamoja.
(3) Kuchelewa kusali ndani ya wakati hasa sala ya alfajiri kwa kusingizia usingizi. Kumbuka
Mtume wetu S. A. W. aliposema kuwa hakuna sala nzito kwa wanafik kama sala ya isha na
ya alfajiri. Na lau kama wangejua yaliyomo ndani ya sala hizo wangelizikimbilia japo kwa
kusota. Yaani asiyeweza kwenda angalisota ili azipate jamaa msikitini. Hawa ni wanafik wewe
utafanya nini.?
(4) Mrembo huacha sala impite kwa sababu akitia udhu itaharibika rangi ya midomo yake au
macho.
(5) Mfanyakazi, muuza samaki au hata mjenzi husali nje ya wakati kwa kuwa nguo zake hazifai
kusalia. Kumbuka Mtume S. A. W. alipoulizwa ni ipi amali nzuri akajibu kuwa ni sala ndani ya
wakati wake.
(6) Msafiri wa jangwani, msituni na hata mvuvi baharini huacha sala impite kwa kuwa hajui
upande wa kibla. Sababu hii haikubaliki.
(7) Aliyemaliza nifasi hungojea mpaka amalize siku arubaini kwani huulizwa arubaini yako lini.
Inafurahisha tabia hii sasa inaanza kuondoka hakuna tena mjinga. Na pia wengine wanaona kero
kukaa siku arubaini watapitwa na ya ulimwengu na umri ni mfupi! Na wanataka kwenda na
wakati.
(8) Mwenye hedhi huacha sala ya wakati ule ilipomaliza hedhi pengine kwa sababu ya kumgoja
shoga yake waende kisimani pamoja wakati wa magharibi ndio aoge. Hata hii sala ya kipindi
kimoja mtu asiiwache ajitahidi aisali ndani ya wakate wake.
Angalia- kuna mashekhe wanaosema ikiwa hedhi au ujusi umemaliza wakati wa laasiri basu asali
na adhuhuri iliyompita. Ikiwa ni wakati wa isha basi asali na magharibi iliyompita kabla yake.
Kwa sababu sala haza zina wakati mmoja.
(9) Mgema, mlevi, mzinifu mcheza kamari na kama hawa, wao hawasali hungojea mpaka
watubie kwani wamesikia kuwa ukitubia hutakabaliwa, na Mola ni karimu. Tuwasaidie vipi watu
kama hawa?
(10) Seremala, muhunzi na kama hao husali nje ya wakati kwani wakiingia msikitini itabidi
wapoteze wakati mdogo kwa kumsubiri imamu. Au wataingia msikitini sala ya jamaa imekwisha.
Ni makosa makubwa.
(11) Wengi utawaona siku zote, na mpaka leo, wanaingia msikitini na kila mmoja anasali peke
yake. Hawasali pamoja. Sababu kubwa hawana wakuwasalisha. Uislamu gani huu?.
Hii ni mifano kidoko tu wala haijakusudiwa mtu yeyote. Ikitokezea kukugusa hujakusudiwa
wewe ni bahati na juu ya hivyo tunaomba msamaha. Na namuomba Mola akusaidie uweze
kujirakibisha. Haja tuliyoumbiwa ni kumuabudu Mola. Naye anasema {Sikuumba majini na
watu ila kwa kuwa waniabudu}. Sala ni fungu kubwa la ibada.
Ndugu yenu,
Moh'd Humaid Abdullah Al Khatry.
P. O. Box 945 P.C. 130 Adheiba,
Sultanate of Oman.
T: +96899214396
I5. 0.09

Usafi Tohara na Udhu


Kisharia Muislamu ni msafi. Kwa hivyo mtu akisilimu hutakiwa aoge (akoge) naye awe msafi
kama waislamu wenzake. Muislamu anakuwa mchafu kwa kuchafuka. Hapo ndio hubidi aoge,
lakini ibada nyengine kama sala usafi wa kuoga tu hautoshi inabidi pia mtu awe na udhu. Mambo
ambayo humbidi mtu aoge ni:-
(1) Hedhi (2) Janaba
(3) Nifasi (4) Kufa (maiti aoshwe)
(5) Kusilimu (6) Kurejea katika uislamu kwa aliyetoka (7)
Kuwa na najsi mwilini bila ya kujua sehemu ilipo.

Ama kuoga kwa sunna ni:-


(1) Siku ya Ijumaa. (2) Siku ya sikukuu.
(3) Baada ya kuosha maiti. (4) Kuhirimia Hijja au Umra.
(5) Baada ya kupiga chuku (kuumika).

Kwa kweli ni uzuri kukoga kila siku na hasa:_


(1) Baada ya kazi. (2) Baada kurudi safari refu.
(3) Baada ya kuamka. (4) Baada ya kufungua Ihram.
(5) Kutoka kizuka- Sio lazima wala si sunna.
(6) Baada ya kuzuia damu ya Istihadha (hii ina maelezo marefu, utayapata palipohusika.)
Kuoga ni kuwa na nia moyoni ya lile ulilokusudia kuoga na kujieneza maji mwili wote. Ni
muhimu sana maji yafike sehemu zote za mwili. Yaingie ndani ya mipasuko na ndani ya mikunjo
kama ya kitovu na chini ya kucha. Yaingie puani na mdomoni na kila yanapoweza kufika, hata
ikiwa ni kwa tabu. Kunuia moyoni inatosha. Haikatazwi kutamka. Tutatia hapa matamshi ya nia
kwa anayetaka.

Nia ya kuoga chochote ni kusema:-

au

Na ikiwa unapenda kutaja hasa kile unachotaka kukioga basi ni hivi:-


(1)Kwa janaba ni kusema:-

(2)Kwa hedhi ni kusema:-

(3) Na kwa nifasi ni kusema:-

Kuanzia leo huna haja ya mwalimu wala somo wa kukuosha ujusi wala kukutoa kizuka! Au vipi?
Mola akuekee. Amyn.

Namna ya kuoga
Kuoga kama tulivyosema ni kutia nia na kueneza maji mwili wote, inatosha. Ukitaka ukamilifu
wake kwa ufupi ni hivi:-
(1) Tia nia kama tulivyoeleza.
(2) Osha viganja.
(3) Osha tupu mpaka ziwe safi.
(4) Osha midomo na pua.
(5)Tia udhu kamili ila inatosha kusema usiikamilishe.
(6) Osha kichwa upande wa kulia kisha wa kushoto.
(7) Osha uso, masikio, shingo, na mwili wote upande wa kulia kisha wa kushoto.
(8) Unapoosha iwe unapitisha mkono na kusuguwa kwa sabuni ikiyumkinika, sabuni sio sharti.
(9)Kuhusu kuosha maiti tumetoa kitabu kiitwacho Huduma za Maiti jipatie ukisome.
(10) Sio lazima kufuata mpango huu.

Kutia Udhu
Muislamu akitaka kusali, kuhirimia hijja au umra, na hata kukamata mas-hafu, kwa kauli ya
maulamaa wengi, ni lazima awe na udhu. Ni jambo la maana sana unapojifunza kutia udhu na
kusali ujifunze kwa kumtazama anayejua ili umuige usitosheke na maelezo haya machache.
Ukishajua kutia udhu na kusali mwambie anayejua akutazame kama unafanya ndivyo.

Namna ya kutia udhu ni hivi:-


(1) Hakikisha huna janaba wala hedhi wala nifasi wala najsi.
(2) Kwa kawaida mwanamme awe ametahiriwa.
(3) Ikiwa umekwenda choo kimojawapo jisafishe kwanza.
(4) Tia nia moyoni ya kujitoharisha tohara ya sala.
Kutamka nia si lazima.
(5) Soma yote kamili.
(6) Sukutuwa. Na ikiwa hukufunga fikisha maji kooni ufanye ghaaa.
(7) Tia maji puani.
(8) Osha uso wote. Kutoka sikio mpaka sikio. Na kutoka zinapoishia kuota nywele za utosini
mpaka chini kidevuni, kooni.
(9) Osha mikono yote miwili, anza na wakulia kutoka ncha ya vidole mpaka kupita vifundo
vya dhiraa.
(10) Pangusa kwa maji kichwa chote kuanzia usoni mpaka nyuma kichogoni. Wengine
wanasema unaweza kufupisha kwa kupaka maji kishungi, utosini tu.
(11) Osha au pangusa kwa maji masikio yote mawili nje na ndani. Masikio ni sehemu ya
kichwa.
(12) Osha miguu yote miwili mpaka vifundo juu ya nyayo, anza na mguu wakulia.
(13) Kumbuka kufikisha maji mwenye mipasuko kama ya nyayo na sehemu zilizojificha
kama chini ya kucha na kitovu.
(14) Ni sunna yenye thawabu nyingi kusuwaki kabla kuanza kutia udhu.

Lazima au Sunna
Wengine wanasema ni sunna kubwa na wengine wanatilia mkazo kuwa ni lazima:-
(1) Kufikisha maji mpaka chini ya mashina ya ndevu, wengine wanasema ni lazima ndio udhu
ukamilike.
(2) Kutokatiza. Usitawadhe kidogo kisha ukakamalisha baadaye. Na hivi pia wengine wanasema
ni lazima.
(3) Kutia udhu kwa kufuata nidhamu, mpango. Na ni kuosha kwa mpango tuliotaja kwa mfano
usitangulize miguu kabla ya mikono. Na pia wengine wanasema kutawadha kwa mpango ni
lazima.

Sunna za Udhu
(1) Kusuaki kabla ya kutia udhu.
(2) Kuosha viganja kabla kutia udhu.
(3) Kuosha viungo mara tatu tatu.
(4) Kuosha masikio ndani kisha nje kwa maji mengine
(5) Kuvisugua viungo au kupitisha mkono ukitawadha.
(6) Kuvibagua vidole yaani kupitisha kidole chenye maji baina ya vidole.
(7) Kuanza na kiungo cha upande wa kulia.
(8) Kutilia udhu mkono wa kulia.
(9) Kuzungusha pete hasa ikiwa imebana. Ikiwa imebana sana ni lazima.
(10) Kuelekea kibla ikiyumkinika.
(11) Kukaa kitako ikiyumkinika.
(12) Kuomba dua baada ya kutia udhu.
(13) kusali sala ya rakaa mbili baada ya kutia udhu, baada ya dua ya udhu.

Masikio ni sehemu ya kichwa kwa hivyo kukosha masikio wengine wanasema ni lazima sio hiari
kama nilivyosema kabla kidogo.

Yanayoharibu Udhu
Udhu unaweza kuharibika ikabidi utie tena. Yanayoharibu udhu ni mengi. Baadhi ya hayo ni:-
(1) Kutoka damu popote mwilini au usaha mwingi au kidogo ukiwa na damu.
(2) Kutoka chochote kwenye tupu mbili hata pumzi au sauti.
(3) Kutapika au kucheua.
(4) Kutamka, inasemekana na hata kusikiliza, kila baya kama kusema uongo, kusengenya,
kufitinisha, kutukana, kulaani, kuapiza na kama hayo.
(5) Kutazama mwili wa mwanamke ajnabi kwa kuupekuwa kwa macho. Mwanamke kinyume cha
mwanamme.
(6) Kulala usingizi au kusinzia ikatoka fahamu.
(7) Kugusana na uchi wowote.
(8) Kutazama uchi na zaidi kutazama kwa hamu.
(9) Kugusa najsi maji maji.
(10) Kupoteza fahamu hata kughumiwa, kuchanganyikiwa.
(11) Kucheka au kutabasamu ndani ya sala kunaharibu udhu kwa kauli ya maulamaa wengine..
Wengine wanasema inaharibika sala tu.
(12) Kumshirikisha Mola, kushiriki. Tunamuomba Mola atuepushe na kila aina za shirki.Amyn.
(13) Kwa mujibu wa kauli ya mashekhe wengi ni kuwa kumgusa mwanamke ajnabi kwa mikono
na hata mwili kwa mwili kunatengua udhu. Kwa mwanamke ni kinyume chake.
(14) Kugusana na maiti hata wa kibinaadamu.
(15) kugusana na mbwa au nguruwe.
(16) Kutia udhu uchi na kukaa uchi mbele za watu hupelekea kutoka udhu.

Yale yenye khitilafu kuwa hayatengui udhu nimeyatia kwa kuchukuwa hadhari zaidi na kuepuka
khitilafu ili mtu asiharibikiwe ni bora au vipi? Na anayetaka kuyatoa aulize kwanza apate fikra za
mashekhe. Na ni kama nilivyosema haya ni baadhi tu.

Makruhu
Yasiyofaa kufanya au kupelekea kuharibu udhu pia si kidogo. Haya huitwa makruhu baadhi ya
hayo ni:-
(1) Kutumia maji mengi-israfu.
(2) Kutumia maji yamoto sana au baridi sana.
(3)Kuzidisha mara tatu tatu.
(4)Kuzungumza.Inasikitisha watu wengi huzungumza ndani ya kutia udhu.
(5) Kuvipiga viungo kwa maji.
(6) Kutia udhu usimama.
(7) Kusimama juu ya pahala pachafu.
(8) Kutia udhu chooni. Sio vyoo vya aina zote.
(9) Kutilia udhu vyombo vya dhahabu au fedha.
(10) Kutofikisha mara tatu tatu.
(11) Kutia udhu uchi pahala siri. Tumetaja kuwa ikiwa si pahala siri udhu haushiki, haukai. Na
Mola Anajua zaidi.

Najsi (Uchafu)
(1) Kila chenye kutoka kwenye tupu mbili ni najsi kama mavi, mkojo, manii, madii, madhii,
damu maji, maji yatokayo baada ya hedhi, mdudu, minyoo vijiwe na kama hayo.
(2) Matapishi na macheuo.
(3) Damu hata ile inayotoka puani na ya viumbe wengine ni najsi isipokuwa samaki kwa
madhehebu yetu. Hata hivyo si muruwa kusali na damu ndani ya mwili au nguo hata hiyo ya
samaki ila iwe hapana budi.Lisilo budi hutendwa.
(4) Mizoga (maiti).
(5) Mbwa na nguruwe.
(6) Vya kulewesha, maji maji.
(7) Usaha ukiwa na damu. Bora kuchukuliwa kuwa usaha wowote ni najsi.

Damu
Maelezo ya damu ni marefu yanahitaji kitabu peke yake, karibu kitatoka. Kwa hivyo hapa tutatia
kwa ufupi yale ambayo ni vibaya kuyapuuza.
Damu ni najsi na ni namna nne.
(1) Ya kawaida, hii hutoka kwa kujikata au kujichoma pia huweza kutoka bila mpango kama vile
mdomoni au puani.
(2) Ya Nifasi, hii ni kwa kuzaa hata kama hakutoka mototo.
(3) Ya istihadha, hii hutoka ukeni bila ya kuwa ya kawaida wala nifasi wala hedhi.Utaifahamu
katika maelezo yafuatayo. Damu hii nyekundu wekundu wa kawaida. Haina harufu. Ni nyepesi.
(4) Ya hedhi,hii hupata wanawake wanapofikia utu uzima takriban kila mwezi katika hali ya
uzima. Wekundu wake umekwendea weusi, umekoza. Ina harufu mbaya. Nzito nzito.
Kuhusu uzito na wepesi imekusudiwa ukichukua damu ya istihadha nusu kikombe kwa mfano na
ya istihadha nusu kikombe vilevile basi ya hedhi itakuwa ndiyo nzito. Si mwambii mtu afanye
hivyo lakini anaweza kukisia. Na ikibidi nimeshasema kabla lisilo budi hutendwa.

Maelezo Kuhusu Damu


(1) Damu ya hedhi humtoka mwanamke mzima si kwa ugonjwa wala kuzaa wala kuumia.
Imekoza sana, wekundu wake ni kwendea weusi, nzito ukilinganisha na damu ya kawaida
na inanuka vibaya. " Ni maarufu kwa wanawake".
* Humtoka mwanamke baada ya kupata ukubwa. Kwa hivyo haimtoki kabla ya "kuvunja
ungo"yaani kubaleghe.
* Humtoka takriba kila mwezi.
* Kwa kawaida haizidi siku kumi wala haipungui siku tatu. Kwa hivyo ikizidi siku kumi huwa
pengine imechanganyika na ya istihadha mwanzo au mwisho.
* Kwa kawaida humtoka siku zile zile kila mwezi. Inaweza kuchelewa siku moja au kukawia. Pia
huweza ikatoka kabla siku zake kwa siku moja au mbili hivi. Na pia siku huweza kubadilika
ikabidi kufanya uchunguzi kujua siku mpya. Na huweza mtu asipate kabisa.
(2) Damu ya istihadha haina siku maalum na huenda mtu asipate maisha yake. Ni damu ya
kawaida itokayo kwenye utupu - uke.(3) Mtu akiwa na hedhi hafungi wala hasali wala hatufu
Kaaba huko Makka wala hashiki mas-haf. Mwenye istihadha hazuiliwi kufanya yote hayo.
(4) Ni muhimu mwanamke ajuwe tafauti ya hedhi na istihadha ili asifanye kosa la kuacha ibada
kwa kuchukulia ana hedhi wala sio, au kinyume chake.
(5) Mwanamke huweza kupata istihadha wakati wowote. Pia huweza kuunga mwanzo au
mwisho wa hedhi. Kwa hivyo mtu akipata hedhi kabla ya siku zake au ikiendelea basi lazima
afanye uchunguzi.
(6) Msichana akipata hedhi kwa mara ya mwanzo ndio ameshapata ukubwa ikiisha tu aanze
kufanya ibada. Asingojee kupitwa na sala hata moja wala siku ya kufunga.
(7) Kwa kawaida mwenye mimba hapati hedhi na pia mzee sana kama wa miaka sitini hivi.
(8) Mwenye nifasi hafanyi yale aliyokatazwa mwenye hedhi. Damu ya nifasi ikimaliza tu mtu
aoge aanze kufanya ibada asingoje siku arubaini.

Dua wakati wa Kutia Udhu


Si lazima wala si sunna kusoma dua kwa kila kiungo wakati wa kutia udhu. Haifai kuacha sala
kwa kusingizia kuwa mtu hajui dua hizi. Wasiojua wanaziita nia. Tusitie uzito katika dini. Kuna
wengine wanakataza kuzisoma kuepuka mashakil kama hayo. Wazamani waliona si makosa
kuzisoma. Kwa hivyo nitaziweka hapa ili anayezitaka azipate.

(1) Wakati wa kuanza kutia udhu mashekh wengi wanasema kuwa hii bismillahi
ni lazima:-

(2) Kusukutuwa:-

(3) Kutia maji puani:-

(4) Kuosha uso:-

(5) Kuosha mkono wa kulia:-

(6) Kuosha mkono wakushoto:-

(7) Kupangusa kichwa:-


(8) Kuosha masikio:-

(9) Kupangusa shingo( sio muhimu kupangusa shingo):-

(10) Kuosha mguu wakulia:-

(11) Kuosha mguu wa kushoto:-

Kutayammam
Kutayammam ni kutumia mchanga badala ya maji kwa kuoga au kutia udhu. Wengi wetu
zinatupita sala kwa kukosa maji au kushindwa kuyatumia au kukataa kutayammam. Kuna sababu
kama tatu hivi za kujiingiza katika makosa hayo:-
(1) Dharau. Mtu huona atasali akipata maji au atapoweza kuyatumia, wala hajishughulishi kwa
hoja kuwa atasali vipi naye hana maji. Hiyo si sababu ya kuitoa sala ndani ya wakati wake wala
hakuna nyengine, labda kuwa umelala au umesahau. Na si kawaida. Mtume (S. A. W.) aliulizwa
ni ipi amali bora kabisa akajibu kuwa ni sala ndani ya wakati wake, kama tulivyosema kabla.
Tutafute njia ya kujitoa katika vizuizi ili tusali ndani ya nyakati zake.
(2) Kuona kuwa kutayammam ni kitendo kigeni hivi wala hajapatapo kukifanya na pengine
hajamuona mtu hata mmoja kutayammam.
(3) Kuna na waliokuwa hawajui kutayammam. Au hata hawajasikiapo kusikia, mambo haya ni
mageni kwao hawajapatapo kuyaona. Na pengine akikifanya, watu wote watamkodolea macho na
pengine waulizane anafanya nini yule!?

Sasa tutazame njia ya kutusaidia kuyaondoa matatizo haya.


(1) Naamini kuwa mtu akifika hadi ya kusoma vitabu kama hivi atakuwa na haja na hamu ya
mambo ya dini yake. Basi lipi lakudharau kutayammam mtu ikampita sala ndani ya wakati
wake.
(2) Usiogope watu kukucheka wala usitake wakusifu. Fanya kwa ajili ya dini yako, na ikibidi
ufanye siri ni bora kuliko kuacha.
(3) Ni wepesi kupata mchanga. Jichukulie akiba ukisafiri hasa safari refu au ukipata kulazwa
hospitali juu sana kwa mfano ghorofa ya 6 na kama hivi, jali juu ya dini yako.

Sababu za kutayammam.
(1) Kuyakosa maji baada ya kuyatafuta kwa juhudi zote.
(2) Kudhuriwa na maji au kuchelewesha kupoa maradhi.
(3) Kuyahitajia maji kwa haja kubwa kama kunywa. Na hapana mengine.
(4) Kuwa maji ni baridi bila kiasi, hayagusiki, wala hapana uwezekano wa kuyazimua.
(5) Ukingojea maji utaikosa sala au utakuwa wakati umeshatoka. Na hii hasa ni sala ya idi au ya
maiti. Hatokezea makaburini, mavani hakuna maji ya kutosha au mifereji ni kidogo, waliongojea
zamu za mifereji wakakosa kumsalia maiti.. Usisali nje ya wakati kwa kuwa huna maji au
mchanga.

Sharti za Kutayammam
(1) Kuepo japo moja ya sababu za kutayammam ambazo tumeshazieleza hapo mwanzo.
(2) Kuwa na mchanga safi. Maulamaa wengine (sio wote) wanasema pia uwe haujatumika.
(3) Maulamaa wengine (sio wote) wanasema kutayammam baada ya kuwa umeshaingia wakati
wa ile haja.

Namna ya Kutayammam
(1)Tia azma yaani tia nia ya kujitoharisha lile ulilokusudia.
(2) Soma kamili kama ukitia udhu kwa maji.
(3) Weka au pangusa viganja vyako viwili vilivyokunjuliwa juu ya mchanga.
(4) Pangusa uso wote kwa marefu kwa viganja venye athari ya huo mchanga mara moja tu. Kabla
ungeweza kuupuliza kupunguza vumbi la mchanga.
(5) Weka au pangusa tena mara ya pili viganja vyako viwili vilivyokunjuliwa juu ya mchanga ule
ule. Maulamaa wengine wanasema inatosha kuweka mchanga mara moja tu.

(6) Pangusa mkono wa kulia kwa athari ya mchanga wa kiganja cha mkono wa kushoto na
pangusa mkono wa kushoto kwa athari ya mchanga wa kiganja cha mkono wakulia. Mikono
hupanguswa mpaka vifundoni tu vilipoanza viganja, panapovaliwa saa si dhiraa kamili. Na
hupanguswa kwa kuanzia nyuma ya viganja ncha ya vidole mpaka chini kifundoni na ndani
kiganja chote.
(7) Usisahau nidhamu, uso kabla viganja.
(8) Ukinyanyua mikono kupangusa uso ni uzuri ulete takbir.
(9) Pasiwe na muda baina ya kupangusa uso na viganja.
Jee umejaribu, umeona ugumu wowote!.Basi usiitowe sala ndani ya wakati wake kwa kukosa
maji.Wakati hauna mbadala ama maji yanao na ni mchanga.

Yanayoharibu Tayammam
(1) Ni yale yote yanayoharibu udhu.
(2) Kuondoka ile sababu ya kutayammam.
(3) Kutayammam nje ya wakati na hii kwa wale wanaosema kutayammam iwe wakati
umeshaingia.

Mambo mengine yahusuyo udhu na tayammam.


(1) Ikiwa kutayammam ni kwa sala basi huharibika tayammam kwa kuondoka sababu ya
kutayammam kabla ya kumaliza kusali.
(2) Kwa kauli ya Maulamaa wengine kutayammam ni kwa kila wakati si kama udhu unaoweza
kusalia wakati mwengine kwa udhu ule ule.
(3) Ikiwa kutayammam ni kwa kukosa maji basi afadhali kutayammam mwiso wa wakati, ukisha
kukata tamaa ila ikwa toka mwanzo una hakika hutoyapata..
(4) Ukikosa maji na mchanga pia sala usiiwache ikatoka ndani ya wakati wake. Katika hali kama
hiyo tayammam kwa chochote chenye asli ya ardhi kama vumbi, jiwe au jabali. Pangusa viganja
juu ya jabali. Usiache sala hata ukikosa yote.
(5) Mtu anaweza kusali zaidi ya sala moja kwa tayammam moja. Wengine wanasema ikiwa ni
wakati ule ule tu ndio unaweza kufanya hivyo.
(6) Ni uzuri mtu kuwa na udhu kila wakati. Na ni uzuri kutia udhu juu ya udhu.
(7) Maulamaa wanasema asiyezuia damu au mkojo anaweza kusali laasiri wakati wa adhuhuri na
kusali isha wakati wa magharibi.
(8) Watu ambao watie udhu kila wakati wa sala na iwe wakati wa sala hiyo umeshaingia ni:-
* Mwenye kutayammam kwa kauli ya wengine.
*Mwenye kutoka damu mfululizo kama kwa kujikata.
*Mwenye kujambajamba ovyo.
*Mwenye maradhi ya kutojatoja mkojo. Asiyeweza kujizuia.
*Mwenye kutoka damu (ya pua) mara kwa mara.
*Mwenye kutoka damu ya istihadha.
*Mwenye kuchuuka. (asiyezuia uchafu utupu wa nyuma).
Mola Anajua zaidi.

Dua baada ya kutia udhu.


Maulamaa wanasema ni jambo la maana sana kusoma dua baada ya kutia udhu. Na wengine
wamesifu usomaji wa dua hizo hata kupita kiasi. Kwa hivyo ukimaliza kutia udhu:-
(1) Soma Sura yote.
(2)) Shahadia kama hivi:-

(3) Katika jumla ya dua hizo ni hii:-

(5) Dua nyengine katika kitabu Fiqh Sunna:-

(6) Mwisho ukitaka soma hii mara tatu:-

(7) Kuna sala husaliwa hapa, nayo pia imetiliwa mkazo. Inaitwa sala ya baada ya udhu. Ni rakaa
mbili, bora uisali. Hakikisha kuwa wakati unatosha na pia utaiwahi jamaa. Usiache jamaa
ikakupita.

SALA
Kuna mambo mengi yahusuyo sala ambayo ni lazima mtu ayajuwe. Mabingwa hawajayaeleza
yote katika kitabu kimoja. Ukitaka kuyajua yote au mengi itabidi usome na vitabu vyengine.
Soma hapa haya machache:-
(1) Mtu azisali sala zote za faridha jamaa msikitini. Mwanamme jirani na msikiti asiposali faridha
msikitini sala zake huwa hazitimii au ni kama hakusali ila kwa sababu za kukubalika. Sala ya
jamaa ni mara 27 ya mtu peke yake na Mola Humuongeza Amtakaye.
(2) Sala za sunna bora kuzisali nyumbani ila zile kama tahiyyatul masjid, ya baada ya kutufu,
tarawehe na ziko nyengine sunna za kawaida tu kwa mfano mwenye kufanya itikafu atasali zala
zote msikitini. Tutaeleza itikafu pahala pengine..
(3) Ama mwanamke atasali nyumbani kwake sala zote isipokuwa kama zile tulizosema na kusali
chumbani kwake ni bora zaidi.
(4) Siku ya Ijumaa sala ya Ijumaa ni lazima sio pendekezo.
(5) Msafiri akikamilisha masharti ya kusali safari basi lazima asali sala ya msafiri asilinganishe
na kufunga ambako ni bora kuliko kuakhirisha.
(6)Hakuna sababu ya kuacha sala ila hedhi, nifasi, utoto na kichaa. Kama huna hata moja ya hizo
basi usiache sala ndani ya wakati wake kwa hali yoyote ile.
(7) Sala ulizoziacha lazima uzilipe hata kama hujuwi ni ngapi au ni ujanani au popote pale. Pia
ulipe na suna za asubuhi na sala za witri.
(8) Maulamaa wengine wameeleza juu ya kafara ya mwenye kuacha sala. Na wengine
hawakulipa umuhimu jambo hili. Tutaeleza pahala pengine inshaallah. Kafara ni adhabu au
kutiwa adabu ya kufanya kosa. Mfano wa kafara ni kama kuambiwa ufunge siku kumi au uchinje
mnyama au ufunge miezi miwili mfululizo au uwalishe masikini na kama hayo.
(9) Ni uzuri kuvalia kwa kupendeza wakati wa sala na kujitia uturi yaani manukato hata kama
mtu yuko peke yake. Yawe kidogo sana ama mwanamke akiwa atasali nje au msikitini haifai
kufanya hivyo.
(10) Mtu awe anajisikia kisomo chote akisali peke yake.
This document was created with Win2PDF available at http://www.daneprairie.com.
The unregistered version of Win2PDF is for evaluation or non-commercial use only.

You might also like