Download as doc, pdf, or txt
Download as doc, pdf, or txt
You are on page 1of 8

1

Je, fungu la kumi limeamriwa ndani ya Agano Jipya?

1. Utangulizi

Ndani ya Agano Jipya, mistari ya Math.23:23,24 Bwana Yesu Kristo


anazungumzia kuhusu zaka. Wale wanaofundisha kwamba Wakristo ni
lazima walipe zaka hutumia huu mstari kwamba Bwana Yesu alithibitisha
kuendelea kwa Sheria ya Musa ya zaka kwa Kanisa Lake. Halafu waalimu
hao wa zaka hufafanua kwamba zaka hiyo ni moja ya kumi ya kila kitu.

Waalimu hawa wa zaka ni waongo. Kweli kuhusiana na zaka ni hizi


zifuatazo:

 Sheria ya Musa kuhusu zaka haikuwa kamwe moja ya kumi ya kila


kitu unachopata;
 Hekalu (sasa linachukuliwa kuwa ni jengo la kanisa) halikupokea
mafungu yote ya kumi yaliyotolewa na Waisraeli;
 Fungu la kumi kamwe halikuamriwa wala kufanywa na Kanisa la
kwanza;
 Fungu la kumi kama agano la mafanikio huhusika na wale tu
wanaotafuta kuhesabiwa haki kwa Sheria; na
 Wale wanaodai fungu la kumi kwa kila kitu unachopata
wanatambulishwa kuwa ni Waandishi na Mafarisayo ambao
walikuwa ni maadui wa kihistoria wa Kristo.

2. Sheria ya Musa kuhusu zaka haikuwa kamwe moja ya kumi ya


kila kitu unachopata, Kumb.14:22

 Mwisraeli wa kale alipiga hesabu na kulipa zaka zake mara moja tu


kwa mwaka baada ya mavuno. Katika mwaka alinunua na kuuza,
alibadilisahana nguvu kazi yake kwa bidhaa za watu wengine, na
bidhaa zake kwa nguvu kazi ya watu wengine; na katika haya mapato
yake, hakulipa zaka yo yote. Mwaka mzima, yeye na familia yake
walikula mazao ya nchi na ya wanyama. Haingii akilini kuwaza
kwamba Waisraeli walitakiwa kuweka rekodi sahihi kwa kila kitu
walichopata katika mwaka, ili kwamba wahakikishe kwamba
wamelipa moja ya kumi ya kila kitu walichopata kama zaka;
2

 Mwisraeli hakuamriwa kutoa zaka kwa kila kitu alichopata na


kutumia katika mwaka mzima, bali ilikuwa juu ya nyongeza katika
mwisho wa mwaka.

3. Hekalu (sasa linachukuliwa kuwa jengo la kanisa) halikupokea


mafungu yote ya kumi yaliyotolewa na Waisraeli, Hes.18:26,28

Kwa kweli, makuhani wa Hekaluni hawakupokea kamwe zaka zo zote


moja kwa moja kutoka kwa watu. Ni Walawi pekee walipashwa kupokea
zaka na walilipa moja ya kumi ya ile zaka (moja ya kumi) kwa makuhani.
Kwa hiyo, makuhani na Hekalu walipokea moja ya kumi ya zaka.
Sehemu kubwa ya kuwategemeza makuhani na Hekalu ilitokana na
dhabihu (matoleo) yaliyoamriwa chini ya Sheria, Kumb.14:23.

Nani anayekula zaka? Siyo Mlawi wala siyo kuhani! Katika Israeli, kila
jamaa ilitarajiwa kwenda Yerusalemu mara moja kwa mwaka kutembelea
Hekalu. Baadhi ya zaka zilitumika kulipia gharama za safari na pia
zingetumika kutoa matoleo ambayo yaliamriwa chini ya Sheria. Walikula
na kunywa zaka zao wenyewe, Kumb.14:24,25,26. Zaka zilitumika
kugharimia hija ya familia kwenda Yerusalemu mara moja kwa mwaka,
Kumb.14:27,28,29.

Zaka katika Israeli ya zamani ilikuwa kodi ya mapato. Kila walichokula


katika mwaka mzima hakikuingia katika mahesabu na mara moja kila
miaka mitatu zaka kamili ilitolewa kwa Walawi wa sehemu hiyo pamoja
na maskini katika mji wao, Kumb.26:12; Amo.4:4. Walawi walifanya
kazi kama mahakimu na waalimu wa shule vijijini ambamo walikaa.
Kwa hiyo zaka ya mwaka wa tatu ilitolewa kutegemeza waamuzi wa
hiyo sehemu na kugharimia afya, elimu na mambo ya jamii.

Fundisho la zaka, kama linavyofundishwa na kupokelewa na Wakristo


wengi leo ni la uongo. Ni jambo lililotungwa na viongozi wa dini.
Wala halionekani, wala kutetewa na Sheria ya Musa. Wameidharau
na kuitafsiri vibaya Biblia na kukudanganya.

4. Zaka kamwe haikuamriwa wala kutolewa na Kanisa la kwanza,


2Wakor.9:7

Je, unaweza ukaonyesha wapi ndani ya Agano Jipya tunaweza kuona


waamini wakilipa zaka, au miongoni mwa Mitume wakidai zaka?
3

Nyaraka zimejaa majadiliano kuhusu utoaji kwa ajili ya kutegemeza


wahubiri, waalimu na maskini. Lakini hakuna mahali po pote miongoni
mwa Mitume wakidai zaka au kukumbushia kulipa zaka.

Je, inaweza kusemwa vipi ikiwa mtu hatoi kwa lazima ikiwa anaitii
Sheria ya zaka? Je, ni kwa vipi itasemekana ikiwa mtu hatoi kwa
lazima, ikiwa anashawishika kwamba atalaaniwa na umaskini ikiwa
atashindwa kulipa zaka? Katika waraka wa kwanza wa Wakorintho, kwa
nini Paulo hawakumbushi waamini kwamba inawalazimu kulipa zile
zaka na kwamba ana haki ya kuzipokea zile zaka?

Na katika Math.23:23 ikieleweka kwamba hii ni amri kwa Kanisa, ni kwa


vipi kamwe haijasisitizwa na Mtume yo yote? Hakika, hii ilikuwa ni
njia rahisi ya uhakika wa mapato ya viongozi wa kanisa. Yesu, katika
Math.23:34 anawaeleza Mafarisayo, na si wanafunzi Wake. Na Yeye
Bwana anaita swala kuhusu zaka kuwa ni mbu, Math.23:24. Na kwa
hiyo kwa wakusanyaji wa zaka wa Ukristo Mkengeufu, mbu ni ngamia.

4.1 Simulizi ya utoaji zaka wa Ibrahimu katika Waeb.7:1,2,4;


Yakobo (Mwa.28:22)

Katika Mwanzo 14, Ibrahimu anaenda kumuokoa nduguye Lutu na


wenzake waliokuwa wametekwa. Watekaji waliihusuru miji ya Sodoma
na Gomora ambako Lutu aliishi, na walikuwa wakirudi mijini kwao.
Ibrahimu alichukua watumishi 318 pamoja naye, na kuiokoa familia ya
Lutu. Pia alichukua nyara kutoka kwa watekaji walizokuwa
wamezichukua. Baada ya Ibrahimu kuwarudishia mali zao wakazi wa
Sodoma, yeye alitoa moja ya kumi ya nyara kwa Melkizedeki. Ni wakati
huu na huu tu, tunaambiwa Ibrahimu alilipa zaka kwa mtu. Haitajwi
kwamba alikwenda nyumbani na kukata moja ya kumi ya mali zake.
Wala hatuambiwi mahali po pote kwamba, Ibrahimu alilipa zaka kutoka
kwenye mapato yake.

Lengo la mlango wa 7 wa Waebrania siyo kuanzisha sheria ya zaka, bali


ni kuonyesha ni jinsi gani Yesu Kristo alikuwa kivuli katika alama, ni
mifano pote katika Agano la Kale.

Je, Yakobo katika Mwa.28:22 alimtoleaje Mungu moja ya kumi?


Hapakuwa na viongozi wa dini karibu kuzipokea zaka hizi wala
hapakuwa na Hekalu kuzileta humo. Labda Yakobo alizitoa kwa maskini,
4

labda ziliteketezwa kwenye moto. Lakini jambo moja la uhakika: zaka


hizi hazikwenda ghalani mwa mtu. Angalia hii haikuwa amri kwa
Yakobo kutoka kwa Mungu, bali ilikuwa nadhiri iliyofanywa na
Yakobo kwa Mungu. Kitendo hiki cha kale hakifanyiki kuwa sheria
kwa Kanisa, kwa kuwa kutahiriwa pia kulikuwepo kabla ya Sheria ya
Musa, Yoh.7:22; Wagal.5:2.

Lakini Wakristo waliojitoa kwa Mungu wao daima watatoa zaidi ya


moja ya kumi ya kati ya vingi walivyonavyo na kumletea Mungu. Na
Mungu hupima na kutambua utoaji wao.

4.2 Wakristo wazingatie utoaji wa Agano Jipya

 Math.6:1-4: Je, utawezaje kuhakikisha kwamba mkono wa


kushoto usijue mkono wa kulia unavyotoa ikiwa kuna moja ya
kumi? Ni amri ya wazi ya Bwana wetu Yesu Kristo kutokufuatilia
jinsi gani tumekuwa watoaji wema kwa Kanisa. Pia hii inahusisha
kuweka rekodi za utoaji wako mwishoni mwa mwaka. Wewe
utajua na wao watajua pia ni jinsi gani umetoa. Kwamba Bwana
aliwaaambia Mafarisayo kutokuacha kutoa zaka inaonyesha
hukumu Yake juu yao: kwamba hawakuwa miongoni mwa kondoo
Wake. Ilikuwa ni tabia ya Bwana wetu kuwatia hamasa katika
kujihesabia haki kwao katika matendo yao, na hata kuongezea
kipimo, ili kwamba kuwaonyesha kwamba hawakuhesabiwa haki
kwa matendo haya;
 Mkristo anatoa kila kitu, Luk.14:33: Katika Luk.18:22 yule mtu
alipoambiwa na Bwana kutoa mali zake, hakuweza, na
alijisikitikia. Katika swala la fedha, kulipa zaka haikutosha kwa
mtu huyu ili ahesabiwe haki kwa fedha. Kwa hiyo uza kila kitu
ulichonacho. Angalia Matendo mlango wa 5;
 Bwana Yesu aliwaaamuru wanafunzi Wake kuuza vyote na
kuvitoa, Luk.12:33: Kutoa zaka ni njia rahisi ya kukwepa swala la
kuachilia kila kitu. Na Wakristo hudiriki kufikiri kwamba kwa
kutoa zaka wametimiza hitaji la kuwa mwanafunzi wa kweli. Pindi
mtu anapoachilia kila kitu kwa ajili ya Kristo, Bwana anaweza
kuamua kumfanya kuwa msimamizi juu ya fedha Zake. Mtu
ambaye anaendelea kuachilia vyote pia ataendelea kufanikiwa. Ni
jukumu lako mwenyewe kuweka mambo sawa na Bwana wetu
kuhusu maisha yako na fedha zako. Ukijidanganya kuhusu nini
5

inahitajika kuwa mwanafunzi wa Yesu, Yeye anajua. Pia na wewe


unajua.

5. Kutoa zaka kama agano la mafanikio huhusika tu na wale


wanaotafuta kuhesabiwa haki kwa sheria, Luk.17:10

Kuna sababu tatu kwa wale wanaokubaliana na fundisho kama


linavyofundishwa leo na Ukristo Mkengeufu:

 Watu hawa wako katika hali ya uchanga wa kiroho na


kutokufahamu: Kama watamwogopa Mungu na kutetemeka mbele
za Neno Lake, Isa.66:2, wataziangalia Biblia zao wenyewe na kuuona
ukweli;
 Wanafikiri kumlipa Mungu ‘fungu Lake’: Hii ni hivyo ili kwamba
wafanye cho chote kile na fedha iliyobaki. Pia wasifiwe na wenzao;
na
 Wanaamini kwamba kulipa zaka ni kama kuwekeza fedha katika
benki au soko la mitaji: Wanategemea kufanikishwa na Mungu kwa
kulipa zaka. Kwa namna ya kutosha, wanafanikiwa, ili kwamba
fundisho la mafanikio kupitia zaka lionekane sahihi.

Wale wanaofundisha fundisho la zaka kwa Wakristo, mara nyingi


watataja ahadi za mafanikio kutoka Agano la Kale, Mal.3:10.

Fungu hili linasema kwamba, ukitoa zaka kwa uaminifu utabarikiwa. Tatizo
ni kwamba huruhusiwi kuchukua na kuchagua sheria zipi za Agano la
Kale ambazo unataka uzipokee na zipi uziache. Ahadi zile zile
zinaambatana na sheria zingine pia, Kumb.12:28; 28:1-6; Wal.26:3-6. Pindi
unapojifunga na ahadi yo yote inayohusiana na utii wa sheria, umeingia
tayari katika agano la Sheria, Yak.2:10.

Waalimu wa zaka hufikiri kufundisha kwamba unaweza kuiacha sheria yote


kasoro kutii kifungu kimoja. Zaka ilikuwa ni kanuni ya kijamii iliyotawala
taifa la Israeli. Ni Walawi tu waliruhusiwa kukusanya zaka. Zaka siyo
sehemu ya Amri Kumi, na hakuna po pote pale ilipoamriwa kwa
Kanisa, na wala haikufundishwa wala kutendwa na Wakristo mpaka
sehemu ya mwisho ya karne ya 6. Zaka ni sehemu ya agano la Mungu
na Wayahudi tu, Yer.31:31,32; Waeb.8:7,8,13.
5.1 Sisi tulio Wakristo tuna AGANO JIPYA
6

Kwa Wakristo utaratibu wa zamani umepita. Yesu alisema, Sheria na


manabii vilikuwepo mpaka Yohana, Luk.16:16. Kwa maneno mengine
agano la Sheria, kama lilivyothibitishwa na manabii, lilisitishwa wakati wa
kuonekana Yohana Mbatizaji, Wagal.5:3.

Hoja ya Wagalatia katika mlango wa 5, ni kutahiriwa. Lakini kutahiriwa ni


sehemu tu ya Sheria Moja. Kwa hiyo, mlipaji wa zaka hujitahidi kujihesabia
haki mwenyewe katika swala hili moja, kwamba amempa Mungu ‘sehemu
Yake’, na kwa hiyo amehesabiwa haki kwa utii kwa sheria kwa jambo hili
moja. Hakuna tofauti na wale waliosisitiza kutahiriwa! Hawakusisitiza
katika kurudi jumla kwa Sheria yote ya Musa, bali kipengere kimoja tu.
Mtume Paulo anasema katika Wagal.5:3 kwamba pia na mlipaji zaka
anayejihesabia haki kwa vitendo vyake kwa msingi wa Agano la Kale,
ameanguka kutoka kwenye NEEMA. Angalia pia Wagal.3:19.

Huwezi ukazamia ndani ya Agano la Kale na kufikiria kuchomoa


kanuni moja ili upate faida kwamba ‘uko chini ya laana usipofanya!. Ni
vema kabisa ukatenda sheria yote pia kwa ukamilifu, au utaishia kuwa
na laana. Hakuna jambo dogo mbele za Mungu. Sikia Paulo anavyosema
katika Wafil.3:8,9.

Cho chote kile unachohesabu kwako kama haki yako ndipo kutokana
na hicho unapata ujasiri wako mbele za Mungu. Ukijisikia kwamba
umeliweka sawa swala la fedha na Mungu kwa kulipa zaka, basi
umekuwa chini ya laana: umekuwa na haki yako mwenyewe.

Mwanafunzi mtii na wa kweli wa Bwana Yesu Kristo ni muangalifu kwa


kutokuruhusu mkono wake wa kushoto usijue kile ambacho mkono wake wa
kulia unafanya katika swala la utoaji. Pia unajua kwamba, pindi mtu
atakapoachilia vyote alivyonavyo, hawezi kuwa mwanafunzi wa Yesu,
Luk.14:33. Hatakiwi kwa hali yo yote ile awe mbinafsi na kuwa na
matumizi ya binafsi ya fedha zake zilizobaki eti kwa sababu amemlipa
Mungu ‘sehemu Yake’.

Katika Luk.17:10, Bwana wetu anatuambia kwamba baada ya kufanya


mambo yote aliyotuamuru sisi, tuseme kwamba sisi ni watumwa tusio
na faida. Kwa usemi huu pekee, Bwana wetu ametupilia mbali ndoto zo
zote zile ambazo tunaweza kuwa nazo kuhusu kwamba Mungu anatudai sisi
kwa sababu tumetenda kile tulichofikiri kwamba kilikuwa wajibu wetu
katika jambo dogo na pekee. Wazo kwamba Mungu anatupa mafanikio
7

kwa kubadilishana na zaka limekataliwa kabisa na sentenso moja


kutoka kwa Mtume Paulo, War.11:35. Sentenso hii si tu inalaani zaka
kwa ajili ya mafanikio, lakini kila fundisho lingine lo lote la “nipe mimi na
Mungu atakupa wewe” ambalo manabii wa uongo wa Ukristo Mkengeufu
wanapenda kuishabikia. Wengine “hutabiri” kwamba kiasi fulani cha fedha
kitakuja kwa wale wanaotoa ahadi! Ni aibu na kufuru kabisa kwa jina la
Bwana wetu kwa sababu ya watu wachoyo hawa na mafundisho yao maovu
na ya uongo! Msikilize Paulo anavyosema pia katika 1Tim.6:7,8,9,10.

Kwa Mungu, yote yawezekana, Math.19:24-26, na kutakuwa wanaume na


wanawake mbinguni ambao walikuwa matajiri wakati “walipolala na Yesu”,
lakini watu hawa ni maalumu. Siyo rahisi kwa ngamia kupita kwenye tundu
la sindano.

Wokovu wa milele na uzima wa milele kamwe havitolewi ndani au chini


ya Sheria ya Musa kama zawadi au thawabu ya kutii sheria. Kila ahadi
inayotoa thawabu kwa kutii Sheria ya Musa inahusika na usalama wa
muda na baraka ya muda tu. Bwana Yesu alisema, “haki yenu isipozidi
haki hiyo ya waandishi na mafarisayo, hamtaingia kamwe katika
ufalme wa mbinguni, Math.5:20. Yesu ni mpatanishi wa Agano lililo
bora zaidi, ambalo liliweka ahadi bora zaidi, Waeb.8:6; bali Sheria ya
Musa inaahidi maisha marefu, afya njema, mafanikio, na nguvu juu ya
adui wote, kwa wote watakapotii, Kumb.28:1-13.

Ahadi za Agano Jipya zinajumuisha mengi ya haya, lakini yanatolewa


kama zawadi au thawabu kwa IMANI, na yanajumuisha UZIMA WA
MILELE. Haki inayomkirimia mtu uzima wa milele ni ya ubora tofauti
kuliko ile inayopatikana kupitia baadhi ya kazi za utendaji wa Sheria
ya Musa. Wale wanaopata usalama kutokana na baadhi ya kazi za
utendaji wa sheria ya Musa wameanguka kutoka kwenye neema, na
mwisho wao watahukumiwa kuhusiana na jinsi gani waliitii Sheria ya
Musa ya zaka na sheria zingine 612. Mungu huwatumia hawa watoa zaka
kutegemeza kazi Yake hapa duniani na anawazawadia kulingana na ahadi ya
Musa, bali mwishowe, Yeye anawahesabu kama wageni. Angalia
Math.17:24-27; Kut.30:31; 38:26; Luk.22:25-27.

Kwa maneno ‘wana ni mahuru’, Math.17:26, Bwana wetu anawafungua


wote wanafunzi Wake na wajibu wa kulipa kodi ya aina yo yote, zaka au
kiasi Fulani kwa msingi wa kawaida katika kuutegemeza Ufalme Wake.
8

Kodi hii, Bwana wetu anasema kwa kukubaliana na Petro kwamba


inachukuliwa kwa wageni. Neno wageni katika msemo wa Kiebrania kila
mara lina maana ya wale walio nje ya agano la Mungu. Na kwa hiyo
itatimilika, kwamba, mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki,
Mith.13:22.

Hakuna rekodi kwamba Bwana wetu alilipa zaka baada ya kuanza huduma
Yake. Wale wote wanaodai moja ya kumi ya kila kitu unachopata
wanatambulishwa na waandishi na mafarisayo, waliokuwa adui wa
kihistoria wa Kristo. Wakati wa Bwana wetu, kulikuwa na kanisa “rasmi”
moja tu la Israeli:Hekalu la Yerusalemu. Waalimu wa leo wa zaka
wanafanya nyumba (jingo) ya kanisa lao kuwa sawa na Hekalu la Mungu na
hujitia kukaa katika kiti cha Musa, Math.23:1-3. Lakini kumbuka Mungu
haishi tena ndani ya mahekalu yaliyofanywa kwa mikono ya wanadamu,
Mdo.7:48. Kama imejiwekea wajibu kwa mtu mwingine anayekaa kwenye
kiti cha Musa, basi kulipa zaka hizo ni lazima. Kuna gharama za kutunza
jingo, watumishi na mambo mengine yanayotolewa. Tofauti ya Mafarisayo
wa Israeli ya Kale na Mafarisayo wa Ukristo Mkengeufu iko katika mstari
wa Mdo.17:24,25. Angalia pia Mdo.7:48; Math.23:38. Mapambo ya
majengo hayo ni kwa ajili yako wewe siyo kwa ajili ya Mungu.

Mwisho, katika Biblia kuna mtu mmoja aliyedai kulipwa moja ya kumi ya
kila kitu ulichopata. Mtu huyo ni Mfalme Sauli, 1Sam.8:15,17. Hapa
kwenye mistari hii hakuna nyongeza. Sauli atachukua moja ya kumi ya kila
kitu ulichonacho au kupata. Lakini sikia yale anayosema Bwana kuhusu
Mfalme Sauli katika 1Sam.8:18. watu pamoja na hayo waliendelea
kuvumilia maovu ya Sauli, 1Sam.8:7, kwa sababu ni rahisi kumlipa yeye
moja ya kumi yake kwa sababu ni rahisi kufanya hivyo kuliko kuchukuliana
na maneno ya Bwana Yesu Kristo, Luk.18:22. Angalia pia kuhusu hawa
Mafarisayo katika Luk.18:11,12.

You might also like