Professional Documents
Culture Documents
Taarifa Kutoka Kwa Mbunge Wa Bunge La Afrika La Afrika Mashariki
Taarifa Kutoka Kwa Mbunge Wa Bunge La Afrika La Afrika Mashariki
AFRIKA
MASHARIKI
(EALA-TZ)
SHY-ROSE
BHANJI
09/11/2014
Kwa siku kadhaa sasa, mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari
- ndani na nje ya Tanzania vimekuwa vikiandika na kutangaza habari za
kile kinachodaiwa kuwa tuhuma dhidi yangu zilizotolewa na baadhi ya
Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA).
Tuhuma hizo ambazo kimsingi ni mkakati wenye ajenda ya siri nyuma
yake, umekuzwa na hata kufikia hatua ya baadhi ya Waheshimiwa
Wabunge kukwamisha baadhi ya shughuli za Bunge hilo mjini Kigali,
Rwanda.
Kuvunjika kwa kikao hicho kulitokana na madai ya baadhi ya wabunge
waliokuwa wakishinikiza Bunge linichukulie hatua kwa kuniondoa kwenye
Ujumbe wa Kamati ya Uongozi ya EALA.
Madai yao ni pamoja na lugha mbaya kwa baadhi ya wabunge, kuwatukana
baadhi ya marais wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, ulevi wa
kupindukia na kufanya fujo, kuvunja chupa ndani ya ndege na hatimaye
kufungwa pingu wakati wa ziara ya baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wa
EALA nchini Ubelgiji.
Madai yote haya hayana ukweli wowote na yanalenga kuniharibia jina na
sifa yangu ya utendaji kazi wangu katika Bunge la Afrika Mashariki. Lengo
kuu la shutuma hizi ni kunivunja nguvu na ari ya kutetea maslahi ya nchi
yangu na Afrika Mashariki kwa ujumla. Shutuma hizi zinadhihirisha
waziwazi chuki kubwa walioyonayo maadui zangu kwa vile daima
nilisimama kidete kuhakikisha Spika wa Eala Dr. Margaret Zziwa
haondolewi madarakani kwani hoja hiyo haikuwa na maslahi ya Tanzania
na ilikuwa ni kinyume na malengo ya EAC.
Kwa tuhuma nzito kama hizo nilitarajia kupata mawasiliano rasmi ya
kimaandishi kutoka kwa uongozi wa bunge kutaja shutuma zote dhidi
yangu na ni nani anayelalamika. Hilo halikufanyika
Kwa mfano madai ya ulevi wa kupindukia, kufanya fujo na kuvunja chupa
ndani ya ndege ni kosa kubwa la jinai (ugaidi). Madai haya yalipaswa kuwa
na ushahidi kwa sababu si rahisi abiria afanye fujo ndani ya ndege, halafu
aachwe hivi hivi bila kuchukuliwa hatua za kisheria. Safari yetu ya Ubelgiji
tulitumia usafiri wa Shirika la Ndege la KLM. Iwapo tuhuma hizi zingekuwa
na ukweli shirika hilo lisingesita kunichukulia hatua za kisheria.
Tuhuma kama hizi zinapashwa kupelekwa kwenye Kamati ya Uongozi ya
Bunge (EALA Commission) ambayo ina mamlaka ya kushughulikia jambo
hilo. Spika aliitisha kikao cha kamati hiyo lakini kilikosa akidi kwa
makusudi kabisa kutoka kwa baadhi ya wajumbe.
Lengo na makusudi ya kutohudhuria kikao hicho ilikuwa ni kupeleka hoja
hiyo moja kwa moja bungeni ili nichukuliwe hatua za kinidhamu bila ya
mimi kama mtuhumiwa kusikilizwa.
Baada ya kikao cha Kamati ya Uongozi kukosa akidi, hatua iliyofuata ni kwa
Mbunge kutoka Uganda, Dora Byamukama, (aliyeshindwa kwenye
uchaguzi wa uspika 2012 Juni mwaka 2012 dhidi ya Dr. Zziwa) kuwasilisha
hoja kwenye kikao cha Bunge, akipendekeza niadhibiwe kwa kuvuliwa
Ujumbe wa Kamati ya Uongozi.
Katika hilo, hekima ilitawala kuwa sikutendewa haki kwani sikupewa
malalamiko kimaandishi; badala yake hoja hiyo ililetwa jumla. Kwa hilo la
kukosa kunipa mashitaka kimaandishi, wabunge wengi wa Tanzania
waliamua kutoka nje ya Bunge kuonyesha msimamo wao dhidi ya
upungufu wa ukiukwaji wa mtuhumiwa kutopewa kimaaandishi mashtaka
dhidi yake na fursa ya kujitetea (Natural Justice).
Baada ya kukwama kwa hoja hiyo, baadhi ya wenyeviti wa Kamati na
baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Uongozi walitangaza kujiuzulu nafasi
zao. Walifanya hivyo ili kushinikiza Bunge linivue Ujumbe katika Kamati ya
Uongozi.
Hata hivyo, katika hatua ya kushangaza, Wenyeviti wawili kati ya
waliotangaza kujiuzulu wameonekana wakiendesha vikao vya kamati zao
katika miji ya Kigali, Rwanda na Nairobi, Kenya. Ni Mhe. Dora Byamukama
(kamati ya sheria) na Mhe. Martin Nduwimana (Kamati ya Maendeleo ya
Jamii) ambaye alishiriki kama mwenyekiti katika mkutano wa EAC
iliofanyika Nairobi kuanzia tarehe 5-7 Novemba. (Hii nimeshuhudia kwa
macho yangu maana nilihudhuria mkutano huo)