Professional Documents
Culture Documents
Tangazo Njombe
Tangazo Njombe
Waliojiandikisha awali kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura la zamani ili kuhuisha taarifa
zao na kupata kadi mpya za kupigia kura.
Wale wote ambao wanazo sifa za kujiandikisha lakini hawajawahi kujiandikisha kwenye Daftari
Zoezi litaanza kufanyika Mkoani Njombe katika Halmashauri ya Mji wa Makambako na Mji wa Njombe.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inasisitiza wananchi wote wa Mji Mdogo wa Makambako kujitokeza kwa
wingi kuanzia tarehe 23/2/2015 mpaka tarehe 25/03/2015 kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la
Wapiga Kura ili kuwawezesha kupiga Kura ya Maoni na kuchagua Viongozi wao katika Uchaguzi Mkuu
wa mwaka huu 2015.
Vituo vya kujiandikisha vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 Asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni
Kumbuka:Hutaweza kupiga Kura ya Maoni au Kupiga Kura wakati wa Uchaguzi Mkuu kama utakuwa
hujajiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Nenda kajiandikishe sasa.
Ruth Masham
Kny: Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi