Professional Documents
Culture Documents
Maoni Juu Ya Katiba Pendekezwa by Board of Engineer
Maoni Juu Ya Katiba Pendekezwa by Board of Engineer
(b)
(c)
(d)
Angalizo:
Kwa kuwa wajumbe wa Bunge la kutunga Katiba wana
uwezekano mkubwa wa kuweka vifungu vinavyopendelea watu
au makundi ya watu fulani, Sheria ya mabadiliko ya Katiba
ingerejewa ili kiwekwe kifungu kitakachozuia wajumbe hao
kugombea nafasi za kuchaguliwa mwanzoni mwa matumizi ya
Katiba mpya. Hatua hii itawafanya wajumbe hao kuachana na
ubinafsi.
Iwapo angalizo la hapo juu halitapendeza, basi sheria irejewe ili
kulifanya Bunge la kutunga sheria lisijumuishe wanasiasa wengi
kama ilivyo kwenye sheria ya sasa. Ikumbukwe kwamba suala la
kuwa na wabunge wote na wawakilishi wote na wajumbe
wachache wa kuchaguliwa na Rais litaelekea zaidi kwenye
maamuzi ya kisiasa badala ya kitaifa.
2.
SEHEMU YA PILI:
MAONI KWENYE RASIMU.
2.1
(c)
ii)
(d)
2.2
SURA YA PILI.
(a) Ibara ya 11: Malengo makuu.
Maoni:
i) Kifungu (2) kinaainisha nyanja zitakazotumika kuendeleza
na kuimarisha lengo kuu la katiba bila kutaja Sayansi na
Teknolojia.
4
SURA YA TATU.
(a) Ibara ya 17: Mgongano wa kimaslahi.
Maoni:
Katika kifungu (1), rafiki na ndugu wa karibu hawako bayana.
Mapendekezo:
Katiba itamke kwamba Bunge litatunga sheria ya kuondoa utata
huo.
(b) Ibara ya 19: Matumizi ya masharti ya maadili kwa watumishi wa
umma.
Maoni:
Ibara hii inasema kwamba masharti yaliyoainishwa katika ibara za
13 mpaka 18 yatatumika pia kwa watumishi wa umma baada ya
kufanyiwa marekebisho stahiki.
Je marekebisho haya yatafanywa na nani na lini?
Je marekebisho stahiki ni yapi?
Mapendekezo:
Katiba iweke jambo hili wazi.
5
2.4
SURA YA NNE.
(a) Ibara ya 34: Haki ya kufanya kazi.
Mapendekezo:
Kifungu (2), kiboreshwe kwa kuongeza mwishoni mwake maneno
yafuatayo; kulingana na utaratibu uliyowekwa na Bunge
kisheria
(b) Ibara ya 39: Haki ya watu waliyo chini ya ulinzi
Maoni:
Kifungu (3) kinazuia Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kupelekwa nje kwa mashtaka au mahojiano bila ridhaa yake.
Kifungu hiki kinaonekana kukinzana na kifungu 12(d) cha
Rasimu hii.
Mapendekezo:
Kifungu hiki kibadilishwe kwa kuweka maneno ridhaa ya
serikali badala ya maneno ridhaa yake.
(d)
2.5
SURA YA SITA.
(a)
(b)
ii)
iii)
Mapendekezo:
i) Katika ibara hii itamkwe wazi kwamba Katiba ya Jamhuri
ya Muungano ndiyo Katiba mama na kwamba Katiba za
washirika wa Muungano zitakuwa sehemu ya Katiba hiyo.
ii) Kuhusu utekelezaji wa mambo ambayo siyo ya Muungano
Katiba ielekeze Bunge kutunga sheria na taratibu za
kushughulikia masuala hayo kwa kuzingatia maudhui ya
Katiba mama. Utaratibu uliyo rahisi ni kuliweka suala hili
katika ofisi ya Makamu wa Rais.
(c)
(d)
ii)
iii)
Mapendekezo:
Majukumu yanayofanywa na mawaziri hawa ni majukumu ya
ofisi ya Makamu wa Rais. Kuwepo kwao ni kuonesha udhaifu au
kutokuwepo kwa dhamira ya muungano.
(e)
(f)
Mapendekezo
Katiba itamke kwamba kutakuwa na Rais wa Jamhuri wa
Muungano na Makamu wake. Viongozi wa Serikali za washirika
waitwe Mawaziri Mkuu.
2.6
(b)
12
(c)
13
2.7
2.8
2.9
181.
Majukumu ya usimamizi
(1) Serikali itahakikisha kwamba inajenga na kusimamia miundombinu
stahiki na ya kutosha kwa mahitaji ya wananchi na ukuaji wa uchumi
wa Taifa.
(2) Bunge litatunga sheria inayoweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba
vitendea kazi vya utoaji wa huduma au uzalishaji mali vina ubora
unaotakiwa kwa kazi husika pamoja na teknolojia stahiki inayozingatia
usalama wa watu na utunzaji wa mazingira.
(3) Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa sheria kuhakikisha kwamba
majengo na majenzi yanawekewa viwango na usimamizi ili kuboresha
mipango miji na kulinda matumizi ya ardhi na usalama wa watu na mali
zao.
(4) Wakati wote serikali itahakikisha kwamba raia wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania wanajengewa uwezo wa kushiriki kwenye
shughuli za uchumi na maendeleo ya Taifa kivitendo kwa kuweka
mazingira na mipango ya makusudi ya kufikia lengo hilo.
SEHEMU YA PILI
UWEKEZAJI
182. Misingi ya uwekezaji
1) Serikali itahakikisha kwamba kila uwekezaji unaofanyika nchini;
(a) Unazingatia mpango mahsusi uliowekwa na Taifa kwa
madhumuni stahili.
(b) Unaongeza fursa za kuwaendeleza raia wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
(c) Unaliongezea Taifa fursa za kuuza mali zilizokamilika nje ya
nchi.
183. Masharti ya uwekezaji
1) Kila anayewekeza nchini atalazimika kuingia ubia na raia wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa kiwango kitakachowekwa kila inapobidi na
mamlaka ya nchi au Bunge.
17
SEHEMU YA TATU
UTAYARISHAJI NA USIMAMIZI WA VIWANGO
184. Maeneo ya viwango
1) Maeneo yanayotakiwa kuwekewa viwango ni haya yafuatayo;
(a) Vyakula, dawa, vipodozi na vitu vinginevyo vinavyotumiwa na
watu na wanyama.
(b) Matumizi ya viwandani na makazi ya watu
(c) Vitendea kazi mbalimbali
(d) Melighafi kwa matumizi mbalimbali
(e) Mengineyo kama yatakavyoainishwa na sheria ya Bunge.
185. Majukumu ya utayarishaji na usimamizi
1) Bunge litatunga sheria inayoweka utaratibu wa kutayarisha na kusimamia
viwango katika maeneo yaliyotajwa kwenye ibara 184.
2) Utayarishaji wa viwango vya taifa utazigatia viwango vya kimataifa na
mazingira ya ndani ya nchi.
SEHEMU YA NNE
UTUNZAJI WA MAZINGIRA
186. Maana ya mzingira
Mazingira kwa maana ya Katiba hii yanajumuisha mambo yafuatayo;
(a) Hewa na tabia ya nchi
(b) Maji katika hali mbalimbali
(c) Ardhi
18
SEHEMU YA TANO
UENDELEZAJI WA SAYANSI NA TEKNOLOJIA
188. Tume ya Sayansi na Teknolojia
Kutakuwa na Tume ya kuendeleza Sayansi na Teknolojia kwa manufaa na
maendeleo ya ustawi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na watu wake.
Tume hiyo itateuliwa kwa sheria na utaratibu utakaotungwa na Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
(d)
(e)
MWISHO
20