Professional Documents
Culture Documents
Imaan Newspaper Issue 5
Imaan Newspaper Issue 5
Mhadhiri maarufu
Afrika Mashariki Uk 7
21 Rajab 1436, Jumatatu, mei11 - 17, 2015
Maandamano
ya Waislamu
www.islamicftz.org
Sheikh Ponda
atoweka Moro
Uk 3
Maandalizi yaiva
Vituo vya
kuandikisha
wapiga kura
vyawekwa
makanisani
Head office, Lumumba Street, Opp: Viwanja vya Mnazi Mmoja, P. O Box 779 Dar es Salaam, Tanzania
Tell: 255 22 2182482/ 255 222184419, Fax: 255 22 2181424, E-mail: info@Binslum.com
Uk 5
habari
www.islamicftz.org
aasisi ya Dhi Nureyn Islamic Foundation yenye makao makuu mkoani Iringa kwa kushirikiana na taasisi ya Al
Muntada Islamic Trust ya nchini
Uingereza imefanikisha zoezi la kutibu watoto
wenye magonjwa ya moyo bila ya kuwafanyia
upasuaji kwa kuziba matundu yaliyopo kwenye
moyo kwa kutumia kifaa maalum kiitwacho
Cathlet.
Tiba hiyo inafanyika kwa mara ya kwanza
hapa nchini kupitia idara ya tiba ya upasuaji wa
moyo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kushirikiana na madaktari bingwa kutoka hospitali ya Prince Sultan Cardiac iliyopo katika jiji la
Riyadh nchini Saudi Arabia.
Zoezi hilo ambalo lilianza Jumamosi iliyopita litakuwa ni la siku tisa hadi Ijumaa ya wiki hii.
Muasisi na Mwenyekiti wa taasisi ya Dhi
Afyais natural
source of sweet
drinking water
from underground stream
which is blended
with essential
minerals to support and aid perfect metabolism.
Nureyn, Sheikh Said Abri, amewahimiza wananchi kutumia fursa hiyo, kwa kuwapeleka watoto wao kupata matibabu hayo yanayotolewa
bure.
Hakika ni furaha kutoa matumaini mapya
kwa watoto hawa wenye ugonjwa wa moyo, na
ni furaha zaidi kwa mzazi ambaye atamuona
mtoto wake, kipenzi chake, anazaliwa upya na
kuaga machungu ya maradhi yaliyokuwa
yakimsumbua, amesema Sheikh Said Abri.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa hospitali ya
Taifa ya Muhimbili, Dk. Hussen Kidanto alisema, huu ni mwaka mzuri kwa upande wa tiba
kwa Tanzania.
Hadi kufikia mwezi April mwaka huu jumla
ya wagonjwa 453 wamefanyiwa upasuaji wa
moyo na wagonjwa 110 wamefanyiwa uchunguzi wa mishipa ya damu na utaratibu wa kushirikiana na wataalam kutoka nje ya nchi tutauendeleza, ameeleza Dk. Kidanto.
nyakati za swala
WATERCOM LIMITED
P.o. Box 20409, Plot N.4005, Kisarawe11 area
Temeke,Daresalaam, Tanzania
www.watercomtz.com, E-mail:info@watercomtz.com
Na.
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
MJI
DAR ES SALAAM(6.75 S, 39.25 E)
ZANZIBAR(6.17 S, 39.25 E)
TANGA(5 S, 38.25 E)
MOROGORO(8 S, 37 E)
MTWARA(10.67 S, 39 E)
ARUSHA(3 S, 36 E)
DODOMA(6 S, 36 E)
MBEYA(8.5 S, 33 E)
KIGOMA(5 S, 30 E)
MWANZA(2.75 S, 32.75 E)
KAGERA(4.66 S, 30.67 E)
TABORA(5.5 S, 32.83 E)
SHINYANGA(3.75 S, 33 E)
SINGIDA(5.5 S, 34.5 E)
IRINGA(9 S, 35 E)
FAJR
5:13
5:12
5:15
5:23
5:18
5:21
5:25
5:40
5:48
5:34
5:44
5:37
5:34
5:30
5:32
DHUHUR
12:20
12:23
12:24
12:29
12:21
12:33
12:33
12:45
12:57
12:46
12:54
12:46
12:45
12:39
12:37
ASR
3:42
3:42
3:46
3:50
3:41
3:56
3:55
4:06
4:19
4:09
4:17
4:08
4:07
4:01
3:58
MAGHARIB
6:15
6:15
6:21
6:22
6:10
6:32
6:29
6:37
6:54
6:46
6:52
6:42
6:44
6:35
6:29
ISHAA
7:23
7:24
7:29
7:30
7:19
7:40
7:37
7:46
8:02
7:54
8:00
7:50
7:52
7:43
7:37
habari
www.islamicftz.org
Maandamano ya Waislamu
Waislamu
wakiwa katika
moja ya
mikusanyiko. (na
mpiga picha wetu)
NA WAANDISHI WETU
Na Mwandishi Wetu
3
reza, huku wakifanyiwa vitendo vya
kudhalilishwa?
Hamisi Kilongole wa msikiti wa
Chihota, Tandika alihoji: Au ni umati
wa watu waliojitokeza kumuunga
mkono Gwajima ndio ulioitisha Serikali? Nasi tutajitokeza Ijumaa, huenda
Serikali itaelewa uchungu wetu.
Kilongole pia aliasa Serikali itoe
kibali cha maandamano hayo, kwani
lengo si kufanya vurugu bali kuelezea
hisia zao.
Waislamu hao walisema, si haki
hata kidogo kuendelea kuwashikilia viongozi wa Kiislamu huku sheria inatoa
mwanya kwao kupatiwa dhamana
hizo.
Leo hii ni miaka miwili sasa Sheikh
Ponda yuko gerezani, tena akiwa ni
mgonjwa. Cha ajabu hapatiwi dhamana kisa Mkurugenzi Wa Mashtaka
nchini hataki, hiyo sio haki hata kidogo, amelieleza Imaan, mmoja wa viongozi waandamizi wa Baraza la Vijana
wa Kiislamu nchini, akiongea na
mwandishi katika msikiti wa
Kichangani, Magomeni.
Kiongozi huyo, akiongea kwa hisia,
alisema, huenda hayo yanatokea kutokana na vijana wa Kiislamu kutokuonesha hisia zao juu ya mambo yanayojitokeza nchini.
Waislamu wengi walioongea na
waandishi wa gazeti la Imaan walidai
kuwa Serikali kwa muda mrefu imekuwa haiyatili manani madai yao, jambo ambalo wamesema, linajenga taswira ya wao kubaguliwa.
Madai ya Waislamu hapa nchini
yanapopelekwa Serikalini ni nadra
sana kufanyiwa kazi, hapa dhana iliopo
ni kuwa Waislamu ni wakorofi tu, jambo ambalo si sahihi, Maneno Saidi wa
Buguruni amelalamika.
Kuhusiana na suala la Mahakama
ya kadhi, Waislamu hao wamesema,
Serikali imepuuza suala hilo kwa
muda.
Mmoja wa waumini, mkazi wa
Kibaha, mkoa wa Pwani alisema, Waislamu wamedai mahakama ya kadhi
kwa muda mrefu ila hawapewi bila
sababu za msingi, hali inayoonesha
kuwa bila kibali cha maaskofu Waislamu wa Tanzania hawawezi kupata haki
zao.
Mahakama hiyo iliingizwa katika
ilani ya chama cha Mapinduzi (CCM)
mwaka 2005, kuwa kikiingia madarakani kitawapatia Waislamu mahakama hiyo, lakini hadi leo kimeshindwa
kufanya hivyo.
Wakati hayo yakijiri, viongozi wa
Kiislamu walipotafutwa na gazeti hili
kuzungumzia mustakabali wa madai
yao na uwepo wa maandamano hayo,
Sheikh Rajabu Katimba alisema: Sina
cha kueleza kwa sasa, tulishamaliza,
kwani hukupata tamko letu? Wakati
muafaka ukifika tutazungumza.
nana na mumewe.
Khadija aliliambia gazeti la Imaan kuwa Jeshi la Magereza
lilimwambia mumewe amehamishiwa Dar es Salaam kwa usalama
wake kwa sababu katika gereza la
Morogoro kuna mgogoro wa
wakulima na wafugaji.
Mwanzo wa kadhia:
Taarifa zilizosambaa awali na
kusababisha taharuki kubwa zilianza siku ya Ijumaa baada ya wakili
www.islamicftz.org
tujikumbushe
adaraka yakachukuliwa na
mwanae, Nuuru d-Din
Zink ambaye naye alipambana na wapiganaji wa
crusade lakini hakufaulu kuwashinda.
Hapo ndipo, hatimaye, Allah akamuinua kiongozi mpya kuja kuzikomboa ardhi za Waislamu, naye ni Salahud-Din
Al-Ayyubiy au kifupi Saladin. Endelea
na kisa hiki cha kusisimua:
Katika kipindi hiki, Misri ilikuwa
chini ya dola ya mashia Fatmiyyin (The
Fatimid Dynasty). Watawala wa kishia
walikuwa wakishirikiana na wapiganaji
wa crusade waliozikalia ardhi za Waislamu.
Pamoja na kushirikiana nao, mwaka
1160 ma-crusaders wakaivamia Misri
kujaribu kuiteka. Nuuru d-Din Zink
akatuma jeshi kwenda kuwahami ndugu zake Waislamu. Kiongozi wa jeshi
hili alikuwa Jemadari Mkurdi, Shirkuh
huku Salahud-Din Al-Ayyubiy, mpwa
wa Shirkuh, akiwa miongoni mwa wapiganaji.
Shirkuh na jeshi lake wakafanikiwa
kuwashinda ma-crusaders na kuikomboa Misri, lakini akafariki kwa homa ya
matumbo muda mfupi baadae. Mpwa
wake Salahud-Din Al-Ayyubiy akashika
hatamu za uongozi wa jeshi hilo la Waislamu. Na huo ukawa mwisho wa utawala wa mashia Fatmiyyin Misri.
Hivi ndivyo Allah alivyomuinua
mkombozi wa ardhi takatifu Baitull
Muqaddas, Salahud-Din Al-Ayyubiy,
Mkurdi ambaye hata hakuwa mwarabu, kuonesha kwamba Uislamu si dini
ya Waarabu kama makafiri wanavyopenda ifahamike.
Lakini ni nani huyu Salahud-Din AlAyyubiy? Alikuwa kijana wa miaka 36
wakati akishika hatamu za kuiongoza
Misri, ikiwa sehemu ya dola ya Kiislamu
ikiongozwa na Wakurdi.
Wanahistoria Waislamu na makafiri
wanamuelezea kama mtu mnyenyekevu asiyependa makuu. Hakujali kuhusu
anasa za dunia kama wafanyavyo watu
wenye madaraka kama yake. Azma yake
kubwa ilikuwa ni kuzikomboa ardhi za
Waislamu kutoka mikononi mwa
makafiri.
msalaba.
Lakini, kwanza alilazimika kushughulikia masalia ya mashia Fatmiyyin
walioleta chokochoko kwa lengo la kutaka kuiteka tena Misri. Kulikuwa na
kundi likiitwa Hashaashiiyn (wazungu
wakaitamka kama Assassins) ambalo
mbinu yao kubwa ilikuwa ni kuendesha
mauaji ya siri (assassinations) ya viongozi Waislamu na hata wana msalaba.
Hili hatimaye lilishindwa.
Maandalizi ya Waislamu yalichukua
miaka kadhaa. Hadi kufikia mwaka
1180 Miladia, Salahud-Din Al-Ayyubiy
alikuwa amefanikiwa kuunganisha
nguvu za Waislamu tayari kuikomboa
ardhi takatifu ya Baitul Muqaddas (Jerusalem).
Wakati huo wana msalaba (crusaders) walikuwa wameparaganyika, hawana uongozi mmoja na wakitofautiana wao kwa wao. Hii ndiyo hali waliyokuwa nayo Waislamu wakati walipopoteza ardhi zao kwa wana msalaba hao
miaka 80 nyuma.
Mwaka 1182 Salahud-Din Al-Ayyubiy alivuka kutoka Misri kwenda ardhi
zilizokaliwa na wana msalaba na kuanza
mashambulizi dhidi ya wana msalaba
wa Franks ambao asili yao ni Ujerumani. Tukumbuke hawa ndio waliomuua
Imaad ad-Din Zengi.
Mpinzani mkubwa mwenye nguvu
na katili katika wana msalaba alikuwa
ni Reynald wa Chatillon, mmoja wa
kikosi cha wapiganaji waliojulikana
kama Knight Templers. Hawa ndio
waliokuja kuanzisha Umasonia duniani
chini ya misingi ya Hashaashiin.
Huyu Reynald wa Chatillon alikuwa
akiwavamia Waislamu katika ardhi zilizokaliwa na wana msalaba na kuwaua
na kushambulia misafara iliyokuwa ikienda Makka kwa ajili ya ibada ya hijja.
Reynald hata alitishia kuishambulia
miji ya Makka na Madina.
Salahud-Din Al-Ayyubiy hakuvu-
kutoka misikitini
Waislamu nchini wametakiwa kumuiga Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) kwa vitendo kwa kuwa
yeye ni mwalimu wa dini ya Uislamu.
Wito huo umetolewa na Sheikh Muhammad
Mujahid katika ibada ya swala ya Ijumaa iliyoswaliwa
katika msikiti wa Umar bin Khatwab uliopo mtaa
wa Jangwani jijini Dar e salaam na akaonya kuwa ili
amali ihesabiwe kuwa ibada haina budi kutekelezwa
kwa mujibu wa alivyofundisha Mtume. Sheikh Mujahid alisema jamii ya Waislamu inapaswa kujiepusha
na ibada zisizothibiti katika dini, kwani kufanya hivyo
kunapelekea mtu kuandikiwa madhambi mbele ya Allah . Aidha, aIiwakumbusha Waislamu kufanya ibada
kwa kutegemea malipo kwa Allah katika mwezi huu
wa Rajab sanjari na kujiepusha kufanya maasi, kwani
kufanya hivyo ni kujidhulumu nafsi na pia ni makosa
makubwa . (YUSUPH AMIN)
habari
www.islamicftz.org
Mwenyekiti wa Tume
ya Taifa ya Uchaguzi,
Jaji Mstaafu Damian
Lubuva.
NA SELEMANI MAGALI
inatoka UK 2
Wakili Nassoro
aliongeza: Tulikwenda Ukonga ili
kuongea nae atuambie kwa nini alihamishwa kutoka Morogoro kuletwa Dar es Salaam, na kwa nini apelekwe gereza la wafungwa (Ukonga)
na sio la mahabusu, lakini tuliambiwa hayupo Ukonga.
Tulipofika gerezani hapo tulionesha vitambulisho vyetu na
watu wa mapokezi waliingia ndani,
waliporudi walituambia Sheikh
Ponda hayuko pale, Wakili Nassoro
aliliambia gazeti la Imaan.
Kwa mujibu wa wakili Nassoro,
majibu ya Jeshi la Magereza ya siku
ya Ijumaa yaliongeza taharuki juu
ya hali ya Sheikh Ponda, hususan
ukizingatia kuwa huko nyuma Jeshi
la Magereza limekuwa likiwapa
ushirikiano mzuri tu kila walipotaka kuonana naye.
5
habari ofisini kwake, Mwenyekiti TACCEO, Martina Kabisama, amekiri kuwepo hali hiyo na kudai kuwa serikali imekiuka jukumu lake kwa kuruhusu vituo
hivyo kuwekwa kanisani.
Alisema, uwepo wa vituo hivyo katika
makanisa ni kasoro kubwa inayohitaji
kufanyiwa marekebisho, vinginevyo
kunaweza kukasababisha kundi kubwa
la waumini wa dini nyingine kuachwa
bila kuandikishwa, hivyo kuwanyima
haki yao ya msingi .
Kabisama ameongeza kuwa, kuweka
vituo hivyo makanisani kunaweza kuwazuia watu wengi wakiwemo hata Wakristo ambao kwa namna moja ama nyingine
hawapendi kufika katika makanisa hayo
kutokana na sababu wanazozifahamu.
Nadhani kuna haja ya kurekebisha
kasoro hizi, kuacha makanisa au nyumba
nyingine za ibada kutumika kama vituo
vya kuandikishwa wapiga kura si sahihi,
kwani waumini wa dini nyingine
watashindwa kushiriki kutokana na
woga au kuwa na imani tofauti, alieleza
Kabisama.
Ukiacha kasoro hiyo Kabisama
ametaja kasoro zingine ambazo zimebainika katika zoezi hilo kuwa ni pamoja
na mwitikio mdogo wa wananchi katika
vituo vya kuandikishwa kwa kile alichokitaja kuwepo elimu ndogo ya wapiga kura
inayotolewa juu ya umuhimu wa zoezi
hilo.
Amesema, ili kukabiliana na changamoto hizo tume ya taifa ya uchaguzi inapaswa kuongeza idadi ya asasi za kiraia ili
zitoe elimu hiyo na kuwavutia wananchi
walio wengi kujitokeza kujiandikisha.
Katika wilaya ya Ruangwa siku tatu
za mwanzo watu wachache walijitokeza
na hata kituo cha Kitandi Gulioni April
27, 2015 tulishuhudia watu 44 peke yake
wakiandikishwa, alisema Kabisama.
Pia ametaja kasoro nyingine katika
zoezi hilo kuwa ni pamoja na zoezi kupitiliza muda wake hadi kufikia saa sita,
watu kuandikishwa bila kuchukuliwa
alama za vidole, zoezi kushindwa kufanyika kwa wakati kutokana na kukosekana kwa mashine za kuandikishia (BVR)
na kundi kubwa la watu kutoandikishwa
kutokana muda kumalizika.
Kufuatia hali hiyo wameishauri tume
ya taifa ya uchaguzi kuboresha mchakato
wa zoezi hilo na pia serikali itimize wajibu wake wa kuipa fedha tume.
Zoezi la kuandikisha wapiga kura kwa
mfumo wa kielektroniki (Biometric voters registration-BVR) ulianza rasmi Febuari 23, 2015 katika Halmashauri ya
Mji wa Makambako mkoani Njombe kisha kuendelea katika mikoa ya Lindi,
Mtwara, Ruvuma na Iringa.
kesi yake na huku akitumikia kifungo hicho cha nje, Sheikh Ponda alikwenda mjini Morogoro mwaka
2013 kuhudhuria sherehe za Idul
Adhha ambako nusura apoteze
maisha baada ya kupigwa risasi.
Wakati akipatiwa matibabu ya
majeraha ya risasi Hospitali ya Taifa
Muhimbili, Sheikh Ponda alitiwa
pingu na kafunguliwa mashitaka
Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro akituhumiwa kuvunja
masharti ya kifungo chake cha nje,
kesi ambayo ilikuwa inaendelea
hadi sasa.
Wakati kesi ya Morogoro ikiunguruma, Sheikh Ponda alishinda
rufani yake Mahakama ya Kisutu,
na siyo tu kuachiwa huru, bali pia
kuruhusiwa kuwashitaki waliouza
mali ya waqfu ya Waislamu
Changombe Markaz.
hutolewa na kuchapishwa
The Islamic Foundation,P.O.Box 6011 Morogoro, Tanzania,E-mail: imaanmedia3@gmail.com
mhariri mtendaji: 0715 559 944, Mhariri: 0786 779 669, afisa masoko: 0785 500 502
TOVUTI: www.islamicftz.org
tahariri / uchambuzi
nasaha za wiki
akati za chini kwa chini na kufanikiwa kuunganisha wanajeshi wanaomuunga mkono na wale wana
mgambo wa Kihouth waliokuwa
maadui zake wakati wa utawala
wake.
Lengo la Ali Abdallah Saleh na
genge hili ni kuiondoa Serikali halali
ya Abdo Rabboh Mansour madarakani kwa mtutu wa bunduki.
Ikumbukwe, jeshi la serikali tawala lilidhoofishwa kwa ndani na
halikuwa na nguvu tena ya kuweza
kupambana na makundi ya waasi
Katika kipindi hiki cha vita, silaha zote walizonazo Wahouth wanapata kutoka Iran.
Wahouth ni waasi na kila mtu
analijua hilo. Sasa ni kwa nini tuibebeshe Saudi Arabia peke yake lawama hii? Kwani ni lipi lengo la Iran
na Houth katika sakata hili kama si
kutaka kueneza Ushia na kuchochea
vita vya kiitikadi? Nini lengo la Iran
kama si kutaka kuleta vita baina ya
Waarabu na Wafursi?
Au nini lengo la Iran kama si kutaka kuchochea ugaidi na kuleta vita
vya Wayemen kwa Wayemen ili hatimae Iran kidogo kidogo ipate nafasi ya kuidhibiti Saudi Arabia na
nchi za ghuba kwa kila upande, na
hatimae kufikia lengo la kujitanua
kidini, kisiasa na kiuchumi?
Nimalizie nasaha zangu kwa
kueleza sababu tano zilizoipelekea
Saudia Arabia na nchi za ghuba kuingia katika vita hii.
Mosi, hatari ya kujisogeza kwa
Iran kwenye mipaka ya nchi za ghuba. Pili, kuimarika kwa ushawishi
wa Iran kusini mwa ghuba ya Uarabuni.
Tatu, Wahouth kwenda kinyume
na makubalianao ya Novemba 2011
ya nchi za Kiarabu, kwa kuchukua
hatua ya kuipindua Serikali iliyo
madarakani kwa nguvu ya mtutu
wa bunduki.
Sababu ya nne ni kulinda maslahi ya nchi za ghuba yaliyo katika ardhi ya Yemen na tano, kuikwamua
Bab al- Mandab kutoka kwenye
udhibiti wa Wahouth, kwani kimkakati hili ni eneo nyeti kwa usalama
wa mataifa ya ghuba na ndio njia
kuu ya meli za mizigo na mafuta na
maslahi mengine ya kiuchumi.
0773 215 898
hazina yetu
www.islamicftz.org
NA YUSUFU AHMADI
Sheikh Bachu
Yungali hai miongoni mwa Waislamu
Mawaidha yake bado yanufaisha wengi
kosuko kama mwalimu wake.
Alipokea vitisho kutoka Serikalini na kwa baadhi ya makadhi wa
Zanzibar waliotamani kumfungia
shughuli zake.
Kadhi wa wakati ule ambae sitamtaja jina alimuita Sheikh Bachu zaidi ya mara tatu ofisini kwake
akimtisha na kumpa changamoto
asome na atafsiri Quran mbele
yake kama yeye ni Sheikh kweli,
amesimulia Sheikh Yussuf.
Kwa mujibu wa maelezo ya
Sheikh Yussuf, mahubiri ya mare-
www.islamicftz.org
akati wasomi
wakubwa na mabingwa wa sayansi wanashangazwa na
namna Quran inavyorandana na
tafiti mbalimbali za kisayansi, hebu
tuangalie walau maandiko kidogo
ya vitabu vingine vya kidini ambavyo
baadhi ya wasomi walidai eti ndiko
Muhammad alikonakili Quran
vinavyosema juu ya mambo ya
kisayansi.
Katika Mambo ya Walawi, 11:123, Biblia inataja sifa za wanyama
mbalimbali wanaoliwa na wale ambao hawaruhusiwi kuliwa.
Mambo ya Walawi 11:20 inasema hivi: Tena vyote vitambaavyo
vyenye mabawa viendavyo kwa miguu minne, hivi ni machukizo
kwenu. Katika Biblia ya Kiingereza
vitambaavyo vyenye mabawa viendavyo kwa miguu minne, vimetajwa kama flying insects that walk
on all fours.
Hapa Biblia inakataza kula
wadudu au insects wenye miguu
minne. Haijapatapo kutokea tangu
dunia kuumbwa hadi leo kuonekana au kuwepo mdudu au insect
mwenye miguu minne!
Kwa mantiki hii, ni jambo mu-
mlinganiaji
Sheikh Muhammad Duwaysh
Mambo ya msingi kwa
khatwibu wa Ijumaa
Ilipoishia: Khatwibu aelewe
kwamba kuna kundi la Waislamu
hawajihusishi na matukio mbali
mbali yanayouhusu umma na
wala hawajali. Kundi hili linahitaji kuzinduliwa ili wajue nini kinaendelea katika kadhia za Waislamu. Mtu wa karibu nao zaidi
ambaye watu hawa wanaweza
kumtegemea ni khatwibu wa ijumaa
Sita, kuoanisha mada na waswaliji: Khatwibu atoe mada ambayo inaendana na wanaoswali
katika msikiti wake. Kwa mfano,
iwapo waumini wengi katika
msikiti husika ni wageni, kutoa
mada ambayo itakuwa inahusu
matatizo ya jamii ya mahala hapo
si sawa.
Na vile vile msikiti ambao
huswaliwa na wanafunzi wengi si
hekima kutoa khutba inayohusu
matatizo ya ndoa kwa sababu wanafunzi wengi watakuwa hawajaoa.
Kwa hiyo ni wajibu wa khatwibu kuelewa vilivyo hali za waswaliji katika msikiti wake na achague
mada ya khutba inayoendana na
hali zao na yale wanayoyahitajia.
Saba, kuwa na elimu ya kutosha kuhusu khutba: Khatwibu wa
ijumaa aepuke kufupisha mada
kwa sentensi fupi fupi pasina kufafanua watu waelewe. Vile vile
na na kauli za wanawazuoni na
ahakikishe kwamba msikilizaji wa
khutba anakinai kwa maelezo yake
na ananufaika.
Nane, kuelezea kwa kina:
Khatwibu awe na ujuzi wa kutosha na sahihi kuhusu mada aitoayo. Ujuzi wake utokane na
utafutaji (bahthi) wake katika
Quran na hadith za Mtume zilizo
sahihi na wala asitumie hadith
dhaifu (Dhuafaau) au za kutunga
(Mawdhuu).
Kwa hiyo ni wajibu wa khatwibu ajue jinsi ya kuthibitisha hadith
sahihi katika vitabu vya hadith za
Mtume (Rehma na amani ziwe
juu yake) au ajipambe na yale yaliyosemwa na wanawazuoni kuhusu
daraja ya kila hadith anayotaka
kuitumia katika khutba.
Tisa, kuepuka tetesi: haitakikani khatwibu kurukia tetesi
azisikiazo mtaani au katika vyombo vya habari na kuegemeza au
kusheheneza khutba yake na
khabari hizo pasina kuthibitisha
na kubaini ili kujua uhakika wake.
Kumi, masuala ya kitaalamu:
Khatwibu anaweza kuzungumzia
kuhusu masuala ya utabibu au
fani yoyote makhsusi. Mtu anapozungumzia jambo ambalo si fani
yake, aweza kukosea sana. Kwa
hiyo khatwibu afanye juhudi kujua habari hizo kwa kina kutoka
kwa watu wa fani husika kuepuka
kusema maneno ya kushangaza
kwa watu ikawa fedheha kwake.
www.islamicftz.org
ncha ya kalamu
Sheikh Muhammad Issa
Wahamiaji
haramu au
wakimbizi?
Hapa, tunaona kila upande unautupia lawama upande mwingine.
Lakini swali la msingi ni je, wimbi
hili la wakimbizi kutoka Afrika
kwenda Ulaya linasababishwa na
uduni wa maendeleo?
Mbona hatukuwahi kuona hali
kama hii miaka kadhaa nyuma na
uduni wa maendeleo ukiwa upo katika nchi hizi? Ni lazima kuna jambo
la ziada kando na uduni wa maendeleo au hali ya maisha.
Katika kitabu Migration and
Globalization: Challenges and Perspectives for the Research Infrastructure, Klaus F. Zimmermann anasema: Watu huhama kwa nia ya
kuboresha hali zao za kiuchumi, kujihakikishia mazingira salama zaidi
kuishi, kuungana na familia zao au
kukimbia mateso katika nchi zao za
asili.
Zimmermann anatupa fikra nyingine, kwamba inawezekana kabisa
hawa wanaoitwa wahamiaji haramu si wahamiaji bali ni wakimbizi.
ipo wanachokikimbia hali ngumu ya maisha,
kukosekana usalama na
mateso katika nchi zao.
Ni wazi hawaendi Ulaya kuungana
na ndugu zao.
Hili la kuboresha hali zao za maisha haliwezi kuwa kweli, kwa sababu
hali ngumu za maisha kwa Waafrika
zilikuwepo hata kabla ujio wa wakoloni. Kipindi hicho, hawakujazana
katika mitumbwi kukikabili kifo ili
kufika Ulaya.
Waafrika waliendelea kukabili
mazingira yao duni kama watu wengine kwa sababu chambilecho cha
waswahili mtu kwao.
Tofauti ni kwamba, walikuwa
wakiishi katika hali ya usalama na
amani, pasipo kuwepo mateso wala
khofu kutoka kwa watawala, wala
magenge ya wauaji na makundi ya
waasi yenye kupigania madaraka
katika nchi nyingi za Afrika kwa
mtutu wa bunduki baada ya
kushindwa katika uchaguzi wa kidemokrasia ya kimagharibi.
Nchi nyingi za Afrika baada ya
uhuru zilitawaliwa na wazawa waliosomeshwa katika mfumo wa elimu
wa kimagharibi.
Mfumo huu haukuwa na lengo la
kumuelimisha mwanafunzi kuja
kuitumikia Afrika, bali kuwa nyenzo
ya kuingiza watu katika Ukristo na
kuwaandaa kuwa watumishi wa tawala za kikoloni.
Mfumo huu wa elimu ulizalisha
wasomi butu, wasiojua jinsi ya kuvitumia vipawa vyao kukabiliana na
mabeberu wa nchi za magharibi.
Wengi wa wasomi hawa walihitimu
katika nchi hizo hizo za Ulaya na kurudi kuja kuzitawala nchi zao.
Jinsi wasomi hawa wanavyotawala utadhani walichosomea ni
kuiba mali ya umma, kuuza kwa bei
chee rasilimali za Afrika kwa
wawekezaji wa nchi za kimagharibi
na kuwakandamiza Waafrika wen-
zao.
Waafrika hatukuishia hapa,bali
tawala za kidikteta zilizowekwa madarakani na wamagharibi zikaikumba Afrika.
Naam, ubadhirifu wa mali ya
umma, ufisadi, usimamizi mbovu
wa rasilimali za mataifa ya Afrika
na rushwa ni miongoni mwa sababu zinazopelekea wimbi la wahamiaji haramu kwenda Ulaya.
Kugombea madaraka ni chanzo kingine, kwa kuwa kinasababisha ukabila, ukandamizaji wa
makundi dhaifu katika jamii na
machafuko ya kivita katika nchi
nyingi za Afrika.
Jambo moja la kufahamu hapa
ni kwamba, katika nchi za Afrika
zenye kukumbwa na machafuko
na ukosefu mkubwa wa usalama
na amani ni nchi za magaharibi na
kaskazini. Nchi za Chad, Niger,
Gambia, Senegal, Bukina Faso, Afrika ya Kati, Guinea, Mauritania
na Mali.
Matokeo ya machafuko katika
nchi hizo ni kukosekana amani na
usalama katika bara la Afrika, hivyo
watu wanakimbia kutafuta palipo
na usalama na amani.
Kwa kuwa katika nchi za Afrika
hakuna nchi isiyo na migogoro yake
ya ndani, chaguo jepesi linakuwa
Ulaya, ulimwengu wa kwanza, penye
maisha ya raha na amani, ingawa
wengi wakifika huko wamejikuta
wakiishi maisha ya dhiki kubwa.
Lakini, wakimbizi hawa pia wanatoka nchi za mashariki ya kati
zenye machafuko na vita, zikiwemo;
Uturuki, Syria, Iraq, Afghanistan,
Eritrea na Yemen.
Kwa hiyo sababu moja kuu ya
wimbi hili la wakimbizi kwenda
Ulaya ni ukosefu wa usalama,
mateso na vita kati nchi wanapotoka
wakimbizi.
Kwa kiasi fulani maneno ya
mwandishi Athur Kemp yana ukweli ndani yake, sisi wenyewe Waafrika na serikali zetu ndiyo wa kulaumiwa kwa tatizo hili la wakimbizi
kutoka Afrika kwenda Ulaya.
Lakini kwa kiasi kikubwa pia
Ulaya na Marekani zinahusika. Tukumbuke maneno ya Nigel Farage
kuhusu hatua ya Ulaya kuisambaratisha Libya.
Marekani na washirika wake wanatuhumiwa kutengeneza makundi
ya kigaidi kufanikisha lengo lao la
kubadili tawala wasizozitaka kuelekea mfumo mpya wa dunia New
world Order.
Wamasonia wanaamini kuwa
Order comes from Chaos yaani
mpangilio au nidhamu huja kutokana na mparaganyiko. Dunia ilianza
kwa Chaos waliyoiita Big Bhang!
Mlipuko mkuu. Baada ya mlipuko
(chaos) ndiyo tukapata nidhamu ya
sayari, ikiwemo dunia tunayoishi
penye mazingira ya nidhamu (Order).
Kwa hiyo katika kutengeneza
mfumo mpya wa ulimwengu,
Wamarekani na washirika wake
wameunda Al-Qaeda,ISIS, An-nusra, Boko Haram, Al-Shabaab n.k.
Na sisi Waafrika tumeunda Seleka, Anti-Balaka, Mungiki n.k. matokeo ya makundi haya ni vita,
mauaji, mateso na kupelekea vichocheo vikubwa vya wakimbizi.
Kwa upande mwingine, kuna
magenge ya wavushaji wakimbizi
hawa yanayojitengenezea mabilioni
ya fedha.
Watu hawa hufanikiwa kwa
sababu nchi zetu zimeoza kwa
rushwa, kwa hiyo wanachofanya ni
kuwalipa maafisa wa uhamiaji mipakani kuvusha mizigo yao. Hawa
wanaitwa human traffickers au
wasafirishaji wa binadamu.
Mwaka 2011 pekee, zaidi ya wasafirishaji 9,000 nchini Uturuki walijilimbikizia Dola za Kimarekani milioni 303 sawa na Shilingi za Kitanzania 575,700,000,000 (Trilioni
5.75).
kwa hiyo hili si tatizo la wakimbizi
tu, lakini pia ni tatizo la biashara ya
binadamu kinyume na sheria za kimataifa.
Kwa hili Waafrika si wa kulaumiwa peke yao, bali pia magenge ya wazungu yanayowezesha kuwavusha
wakimbizi kutoka Afrika kwenda
Ulaya. Bila magenge haya tatizo hili
la wahamiaji haramu kwenda
Ulaya lisingekuwepo.
Suluhisho si kulaumiana, bali
kutafuta jinsi ya kuzuia sababu za
Waafrika kukimbia na kwenda
Ulaya.
Inaonekana sababu hizi ziko
ndani yetu, ndani ya nchi zetu. Serikali za Afrika zitende haki kwa raia
wake, zisimamie rasilimali vizuri, zijenge mazingira ya uwazi na uwajibikaji kwa viongozi.
Waafrika wa makundi mbali
mbali tuondoe fikra za kibaguzi
kama zinavyotokea huko Afrika ya
Kusini, hali ambayo inasababisha
ukosefu wa usalama na amani. Chuki za kidini kama zilivyotokea Afrika
ya Kati na kupelekea mauaji ya raia,
na zinavyoanza kutokea hapa Tanzania, ni sababu tosha ya kuzalisha
wakimbizi wa kesho kwenda Ulaya.
Tukumbuke kuwa tusipochukua
hatua muwafaka kwa wakati muwafaka, kila mmoja wetu ni mkimbizi
mtarajiwa.
10
makala maalum
www.islamicftz.org
11
www.islamicftz.org
makala maalum
Mfalme Sulayman
wa Saudia
NA ABUU MAYSARA
sasa kati ya Saudia na Iran inaanzia miaka takriban 90 iliyopita, ambapo mnamo 1925 Iran ilikuwa ikiongozwa na
ufalme wa Shah na Saudia ikiongozwa
na ufalme wa ukoo wa Saud.
Kufuatia mapinduzi ya Iran ya mwaka
1979, utawala wa kishia ulinyakua madaraka nchini humo na kufunga mlango
wa uongozi wa kifalme, huku ukifungua
mlango wa uimamu wa kishia.
Kwa upande wa Saudia, ukiachilia
mabadiliko machache ya mwaka 2005
katika mambo ya kisiasa, nchi hiyo imebaki chini ya utawala wa kifalme unaoongozwa na ukoo wa Saud, lakini ukitoa nafasi ya maulamaa wa Kisunni
kuongoza masuala ya kidini.
Uhusiano kati ya Saudia na Iran unaweza kutazamwa katika ngwe (phase)
mbili, Kabla ya mapinduzi ya Iran (mwaka 1929-1979) na baada ya mapinduzi ya
Iran (1979 hadi sasa).
ikiwemo Iran.
Nyingine zilikuwa Jordan, Uturuki,
Iraq na Pakistan. Saudi Arabia ilihofia
mkataba huu wa kusaidiana kiulinzi uliowaleta Waingereza karibu na dola za Bani
Haashimu (waliokuwa watawala wa
Makka na Madina kabla ya utawala wa
Saud). Kwa hiyo Iran na Saudia zikaanza
kutofautiana.
Mgogoro kati ya Waisraeli na Waarabu
uliifanya Iran itofautiane na Saudia.
Wakati mataifa ya kiarabu yakipigana na
Israeli katika vita ya mwaka 1956, Iran
ilikuwa na uhusiano kamili wa kibalozi
na Israeli.
Mwaka 1975, Mfalme Faisal wa Saudia
aliuawa. Khalid akashika hatamu za uongozi. Kwa upande wa Iran, sera za Shah
Muhammad Reza Shah zilizojulikana
kama Shahs white revolution zilikuwa
zikikasirisha wa-Iran na kupelekea
ufalme wa Pahlavi kupinduliwa mwaka
1979.
Mashia wa Iran kama yalivyonukuliwa katika Nasir al-Said,Tarikh Al Saud, vol. 1 ([Beirut]: Ittihad shab al-jazira al-arabiyya, n.d.): 392-403.
Msomaji, pima mwenyewe maneno ya chuki
kama haya yalivyoweza kuharibu uhusiano baina
ya Saudia na Iran. Serikali ya Saudia Arabia ilijibu
mapigo kwa kwanza, kupiga marufuku maandamano ya mahujaji wakati wa hijja.
Pili, Saudia ilipunguza idadi ya mahujaji kutoka Iran kutoka 150,000 kwa mwaka (idadi kubwa
zaidi kuliko nchi yoyote ile) hadi 45,000 tu.
Saudia ilifanya hivyo ikitambua kuwa kwa kupunguzwa idadi ya mahujaji wao Iran itasusia kuleta mahujaji, hivyo kuepuka kurudiwa kwa tukio
kama lile la mwaka 1987.
Kwa muda wote wa mgogoro huu wa mahujaji,
Saudia ilikuwa haijavunja uhusiano na Iran,
pamoja na ubalozi wake kuvamiwa na kundi la
watu wenye hasira na kuuawa kwa afisa wake wa
ubalozi.
Aprili 1988, Saudi Arabia ikakata rasmi uhusiano wake na Iran, isiwezekane kabisa kwa wa
Iran kupata visa za hijja.
Kama ilivyotazamiwa, Iran ilisusia hija mwaka
1988, mwaka ambao pia Ayatollah Khomeini alifariki. Iran iliendelea kususa hadi mwaka 1989.
Pamoja na kutokuwapo mahujaji wa Iran, milipuko miwili ilitokea mjini Makkah mwaka huo
(1989) na kuua mahujaji wawili.
Polisi wa Saudia waliwatia nguvuni zaidi ya mahujaji 30 wa kishia kutoka Kuwait na mwezi Septemba mwaka huo watu 16 kati ya hao wakauawa
hadharani kwa kosa hilo.
Ingawa walikiri kutumwa na maafisa wa ubalozi wa Iran huko Kuwait, Serikali ya Saudia
haikusema lolote kuhusu Iran kwa kukosa ushahidi madhubuti.
Mwaka 1990, wabunge 140 wa bunge la Iran
wakaandika barua ya wazi kwa Saudia wakiweka
masharti ya mahujaji wa Iran kurejea tena.
Miongoni mwa masharti hayo ni Saudia kuomba radhi, ilipe fidia damu za mahujaji wa Iran waliokufa mwaka 1987 na pia ikubali idadi ya mahujaji 150,000 kama awali na waruhusiwe kufanya
maandamano ya kuwalaani washirikina.
Saudi Arabia ilikataa masharti yote hayo, na
hivyo kususia huku kukaendelea kwa mwaka wa
tatu. Wakati wa msimu wa hijja, Ayatollah Ali
Khamenei akasema:
Makka iko salama kwa washauri wa Marekani
na wamiliki wa makampuni ya mafuta, lakini
haiko salama kwa Waislamu wenyewe (Ujumbe
wa Khamenei kwa mahujaji, Radio Tehran, 28
Juni 1990, FBIS, 2 Julai 1990).
Kiongozi wa kidini
Iran - Ali Khamenei
12
www.islamicftz.org
Je hutenguka udhu wa
mtu anayemuosha mwanawe najisi?
S w a l i : Iliulizwa
Kamati ya Kudumu ya
Fat-waa, je kumgusa au
kumpa mkono mwanam-
Swali: Iliulizwa Kamati ya Kudumu ya Fat-waa: Je udhu unachanguka kwa sababu ya kuwatazama wanawake na wanaume walio
u c h i ? Na j e u d h u w a m t u
huchanguka kwa kuangalia utupu
wake?
Jawabu: Hauchanguki udhu
wa mtu aliyetawadha kwa sababu
ya kuwatazama wanawake na wanaume walio uchi, wala kwa kujiangalia yeye mwenyewe, kwani
hakuna ushahidi katika suala hili.
[Lajnatud Daimah 5/270].
Je huchanguka udhu wa
Swali: Iliulizwa Kamati ya Kudumu ya Fat-waa, je mkunga hutakiwa kuoga au udhu unamtosha?
Jawabu: Mkunga hawajibiki
kuoga au kutawadha kwa sababu
ya kusimamia taratibu za uzazi wa
mjamzito, isipokuwa mkunga anapotaka kuswali huwajibika kuiosha najisi iliyoingia kwenye nguo
au mwili wake.
Lakini mkunga hutenguka
udhu endapo atagusa utupu wa
mjamzito wakati wa kuzaa. [Fatawa laj-natud Daimah 5/316].
Je malai ya nywele na
rangi ya mdomo inatengua udhu?
Swali: Aliulizwa Sheikh Muhamad bin Swaleh Uthaimin Allah amrehemu: Je mwanamke kutumia cream ya nywele na rangi
ya mdomo (lipstic) kunachangua
udhu?
Jawabu: Mwanamke kujipaka cream au mafuta ya aina yoyote
hakutengui udhu, na hata funga
haiharibiki. Isipokuwa katika
funga, kama lipstic itakuwa na
ladha, na kama hiyo ladha ya lip
stick itakuwa inapenya tumboni
kwake, hapo isitumike.[Fataawa
na Rasailu za Sheikh ibn Uthaimin
4/201].
afya yako
Pazi Mwinyimvua
na wanadamu wote kwa ujumla kufanya uchaguzi wa vyakula kwa kuzingatia vigezo viwili. Vigezo hivyo ni
uhalali na ubora (uzuri) wa vyakula.
Vyakula vya haramu tunavyotakiwa kuwa mbali navyo ni kama vile
vyakula vya wizi, mali au vyakula
vilivyopatikana kwa njia za rushwa,
nyama iliyokufa bila ya kuchinjwa,
mnyama aliyechinjwa kwa kutimiza
masharti ya wachawi, na nyama ya
nguruwe.
Kama watu wangezingatia kula
vya halali, dunia hii ingekuwa kisiwa
cha amani. Ndio kusema, tusingeshuhudia watu wakiwaua albino na
kuuza viungo vyao.
Wala tusingewaona watu wenye
dhamana ya kufanya kazi za umma au
katika sekta isiyokuwa ya umma wak-
za kufanya uchaguzi.
Na katika ardhi muna vipande
vinavyoungana (na kuzaa kwake
namna mbalimbali) na muna mabustani ya mizabibu, na mimea mingine,
na mitende ichipuayo katika shina
moja na isiyochipua katika shina
moja. Vyote vinanoshelezwa
(vinamiminiwa) na maji yale yale; na
tunavifanya bora baadhi yake (kuliko)
vyengine katika kula. Hakika katika
haya zimo ishara kwa watu wanaotia
mambo akilini (Raad, 13.3).
Katika aya hapo juu, Mwenyezi
Mungu anatufundisha namna ya
uhodari wake wa kuumba. Ingawa
maji ni yale yale na udongo ni ulele ule,
lakini anaumba aina tofauti za mimea
zenye ubora tofauti. Wanyama nao
ubora wao unatofautiana, ingawa wa-
13
www.islamicftz.org
uchumi na biashara
JAMAL ISSA
Aina za riba
A
metukuka
Mu u m b a
mbingu na ardhi mwenye
kuhimidiwa na kushukuriwa. Swala na salam
zimfike mbora wa viumbe aliye mjumbe wa
mwisho wa Rahman kwa
walimwengu wote, kisha
salam kwa wenye kufuata
muongozo.
Ndugu mpenzi msomaji karibu tena kwa
mara nyingine katika
mfululizo wa makala
zetu juu ya uchumi na biashara katika Uislamu.
Katika makala yetu ya leo
In Sha Allah tutadurusu
juu ya aina za riba.
Riba kwa ujumla ni
ziada au nyongeza inayopatikana bila kufanya
kazi. Riba katika lugha
ya kiarabu maana yake ni
ziada. Ama katika lugha
ya elimu ya fiq-hi maana
ya neno Riba, ni ile ziada
anayolipwa mdai juu ya
rasilimali yake.
Mwenyezi Mungu
anasema: Enyi mlio
amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na acheni riba
zilizobakia, ikiwa nyinyi
ni Waumini. Basi msipofanya jitangazieni vita na
Mwenyezi Mungu na
Mtume wake. Na mkitubu, basi haki yenu ni rasilimali zenu. Msidhulumu wala msidhulumiwe
(2:278-279).
Yaani msimdhulumu
mdaiwa kwa kumtaka
zaidi ya rasilimali; wala
msidhulumiwe kwa kupunguziwa rasilimali.
Mtume (Rehma na
amani ziwe juu yake)
amesema: Jiepusheni
na mambo saba yanayoangamiza. Masahaba
(Radhi za Allah ziwe juu
yao) wakamuuliza: Ni
yepi hayo ewe Mtume wa
Mwenyezi Mungu?
Akasema: Kumshirikisha Mwenyezi
Mungu, na uchawi, na
kuiuwa nafsi iliyoharamishwa na Mwenyezi
Mungu isipokuwa ikiwa
kwa ajili ya haki (kwa aliyefanya makosa yanayostahiki kuhukumiwa
auawe), na kula riba, na
kula mali ya yatima, na
kurudi nyuma katika vita
(ukawaacha wenzako
peke yao), na kuwasingizia uongo wanawake
wema wasio na makosa
walioamini (kuwa eti
wamezini) (Bukhari na
Muslim).
Na Mtume (Rehma
na amani ziwe juu yake)
amewalaani wote wanaoshiriki katika Riba.
Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) amesema: Mwenyezi Mungu
amemlaani anayekula
Riba na anayelisha na
kuongeza deni.
Allah anasema: Na akiwa (mdaiwa)
ana shida, basi (mdai) angoje mpaka
afarijike. Na mkiifanya deni kuwa ni
sadaka, basi ni bora kwenu, ikiwa mnajua (2:280).
Aidha, ili kufunga mlango wa nyuma
wa kula riba, katika hadith ya Anas ibn
Malik (Radhi za Allah ziwe juu yake)
Mtume (Rehma na amani ziwe juu
yake) amekataza mkopeshaji kupokea
zawadi kutoka kwa mkopaji.
Pia, katika hadith nyingine ya Anas
ibn Malik katika Sunan al-Bayhaqi,
Mtume (Rehma na amani ziwe juu
yake) amekataza mkopeshaji kuchukua
chakula au kupanda kipando cha mkopaji kama haikuwa ada yao kabla ya kukopeshana. Ukweli ni kwamba aina hii
ya riba imeshika hatamu katika wakati
wetu huu na kuwa moja ya sehemu ya
msingi ya uchumi na biashara.
Mfumo wote wa kifedha umejengwa
juu ya riba, kutoka kwenye vyama vya
kuweka akiba na kukopa mpaka benki
zinazoitwa benki za kibiashara (commercial banks). Taasisi zote hizi hujiendesha kwa riba kama chanzo mama
cha mapato.
Kutoka kwa Abu Hurayrah: Mtume
(Rehma na amani ziwe juu yake) amesema: Kwa hakika itakuja zama kwa
mwanadamu ambapo kila mtu atakula
riba na kama hatofanya hivyo vumbi
lake litamfikia (Abu Dawud, Ibn Majah).
Aina ya pili ya riba ni Riba Al Fadhil.
Riba ya kufadhilisha ni ile ya kubadilishana pesa kwa pesa au chakula kwa
chakula na kuchukuwa zaidi.
Kwa mfano, mtu anapokwenda kubadilisha dhahabu yenye uzito wa gram
kumi kwa ajili ya kupata dhahabu nyingine iliyomvutia zaidi, akalipwa bada-
Je nisikujulisheni juu ya watu bora kuliko wote baada ya Mtume wa Allah? Ni Abuu Bakr, kisha baada
ya Abuu Bakr ni Umar. Na laiti ningependa ningekujulisheni kuhusu watatu wao
(Tuhfatu Swiddiyq Fiy Fadhwaaili Abii Bakr Swiddiyq, Mjalada 1, uk. 7)
THOMAS
CARLYLE
(1795-1881):
makala
14
www.islamicftz.org
Jengokeya5@gmail.com 0783
174 730
15
www.islamicftz.org
Mahusiano ya kibinadamu
USTAADH HABIB HAMIM
Ulemavu wa akili:
Jamii inatakiwa kutambuwa uwepo wa watu wenye ulemavu, kuwathamini kwa ubinadamu wao na
kuwafanyia ihsani na wema kama Allah Taala anavyotuamrisha ndani ya
Quran tukufu akisema:
Na saidianeni katika wema na
uchamungu. Wala msisaidiane katika
dhambi na uadui. Na mcheni
Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi
Mungu ni mkali wa kuadhibu (5:2).
Katika hadith, Mtume anasema:
Kwa hakika Allah ameandika thawabu za kutenda ihsani katika kila kitu.
TOVUTI ZA KIISLAMU
mapitio ya vitabu
Kitabu: Al Fusuul Fii Mustwalahi Hadiithi rRasuuli
Mwandishi: Haafidh Thanaau-ll-waahi
Zaahidy
Mfasiri: Sheikh Muhammad Issa
MlangowaTatu Hadith zenye kukubaliwa
1. Swahihu:Nazo zimegawika
mafungu mawili;-
Na Khalid Omary
16
www.islamicftz.org
makala ya dini
mila na desturi
HAFSWA MADIWA
mmomonyoko wa maadili.
Mmomonyoko wa maadili unaanzia katika ngazi ya familia. Watoto hawapelekwi madrasa kujifunza elimu
ya dini na badala yake mtoto anapelekwa shule za kikristo. Matokeo yake
anakua katika maadili ya kutokumjua
Allah Taala. Mtoto anayekulia mazingira ya kutokumjua Allah hatoona
umuhimu wa kuoa au kuolewa, badala yake ataendekeza uzinifu. Aidha
Ashura aliongeza kwamba, vijana
wengi hawana hofu ya Mwnyezi
Mungu na hii inapelekea wao kuwa
mbali na mafundisho ya Mtume wetu
Muhammad (Rehma na amani ziwe
juu yake). Katika Qur-an tunafahamishwa kuwa: Hakika waumini ni
wale ambao anapotajwa Mwenyezi
Mungu nyoyo zao hujaa khofu, na wanapo somewa aya zake huwazidisha
imani, na wakamtegemea Mola wao
Mlezi. (8:2)
Kama vijana tungekuwa na imani
makala ya kimataifa
www.islamicftz.org
17
Mataifa ya
Magharibi
yanavyosaidia
dhulma
Palestina
Na Yusufu Ahmadi
oja ya migogoro
mikubwa inayotikisa na kuugawa
ulimwengu kwa
kipindi kirefu ni ule wa Israel na
Palestina. Ajenda ya mgogoro
huu imejitokeza mara nyingi
katika vikao vya Umoja wa
Mataifa (UN) tangu ulipoundwa mwaka 1945.
Licha ya vikao vilivyolenga
kuushughulikia mgogoro huo,
hali imebaki kama ilivyo, huku
wakazi wa Palestina wakiendelea kuteseka chini ya utawala wa
kimabavu wa Kizayuni.
Pamoja na mgogoro huo
kuangazwa zaidi mara baada ya
kuundwa kwa taifa la Israel
hapo mwaka 1948, sintofahamu ya eneo hili ilianza tangu
mwaka 1917 mara baada ya azimio la Balfour lililotangaza
msimamo wa Uingereza wa kuunga mkono uanzishawaji wa
taifa la Israel katika ardhi ya Palestina.
Azimio hilo lilitolewa kupitia
barua ya Waziri Mkuu wa
wakati huo, kwenda kwa kiongozi wa jamii ya Wayahaudi,
Baron Rothschild.
Katika miaka ya 1920s
wenyeji walishaanzisha upinzani dhidi ya ujio wa Wayahudi
nchini Palestina, huku Israeli
nayo ikiunda vikundi vya siri vya
kigaidi, vikiwemo Haganah na
Irgan ili kukabiliana na wenyeji.
Moja ya
sababu
zilizoifanya
Uingereza
kubadili
uamuzi na
kuruhusu
Wayahudi
kujenga
makazi yao
Palestina
badala ya
Uganda ni
woga wa
baadhi ya
wanasiasa
wa kukosa
uungwaji
mkono
toka kwa
Waingereza
wenye asili
ya Kiyahudi.
18
www.islamicftz.org
watoto / tangazo
www.islamicftz.org
19
kona ya watoto
nahida esmail
MBWA
Ni kisa ambacho ndani yake Allah (Subhaanahu Wataallah) anataja waumini wazuri
ambao walijificha pangoni wakiwa na mbwa
wao.
Hapo zamani za kale, katika mji mdogo, kulikuwa na kundi la vijana, ambao walimuamini
Mwenyenzi Mungu. Hata hivyo, waliishi na watu
ambao walipotoka na waliosahau maana halisi
ya kumuabudu Mungu mmoja.
Watu hao waliopotoka, walitengeneza sanamu ya mbao na mawe na kuanza kuyaabudu.
Mfalme aliwalazimisha wale vijana wachaMungu kuabudu masanamu. Walipokataa, Mfalme
aliwaagiza walinzi wake wawaadhibu vijana
wale.
Hata hivyo Allah, kwa rehema zake aliwasaidia wale vijana waumini wakakimbia na kujificha
pangoni. Allah akawafanya walale kwa miaka
300! Mbwa pia alilala mlangoni mwa pango
pamoja nao.
Walipoamka, hawakujua walikuwa wamelala
kwa muda gani. Walidhani walilala kwa labda
siku moja au masaa kadhaa.
Walikuwa na njaa, kwa hivyo mmoja wao alienda mjini na sarafu ya fedha kununua chakula.
Hata hivyo, huyo aliyeenda mjini alikuta kila kitu
kilikuwa kimebadilika kabisa.
Akakutana na mtu ambaye alikuwa akiuza
Tunachojifunza:
Mwanza
Arusha
Kigoma
Tabora
Moro
Dsm
Masafa ya Imaan FM
1
2
3
4
5
6
Daresalaam
Morogoro
Arusha
Mwanza
Kigoma
Tabora
104.5 Mhz
96.3 Mhz
90.8 Mhz
105.6 Mhz
92.5 Mhz
101.6 Mhz
7
8
9
10
11
12
Mbeya
Dodoma
Ruvuma
Mtwara
Zanzibar
Pemba
90.3 Mhz
102 Mhz
94.2 Mhz
90.9 Mhz
104.5 Mhz
104.5 Mhz
Mbeya
Ruvuma
Mtwara
20
www.islamicftz.org
MGOGORO
SAUDIA NA
IRAN: SIASA
AU DINI?
Uk 10
21 Rajab 1436, jumatatu Mei 11 - 17, 2015
Katika
kuhakikisha
inafikia
lengo la
kuupeleka
mbele
Uislamu na
Waislamu,
mwaka 1993
jumuiya ya
MSAUD chini
ya kamati
ya wazee
wa Kiislamu
ilianzisha
mpango wa
masomo ya
ziada katika
Shule ya
Kiislamu ya
Ridhwaa,
Kinondoni,
Dar es
salaam.
NA YUSUPH AMIN
Naye, Jumbe Ali ambaye naye aliwahi kuongoza Jumuiya hiyo alisema, enzi zao walitoa fursa kwa vijana
kufahamu elimu ya dini kwa uwazi
na urahisi kupitia misikiti, hususan
kwa wale waliokosa fursa ya kujifunza elimu hiyo utotoni.
Kiongozi mwingine aliyepita ambaye hakutaka kutajwa jina lake,
amesema, akilinganisha na sasa,
kipindi cha uongozi wake Waislamu
hawakuwa wenye kujiamini katika
kutetea haki zao kutokana na sababu
za kisiasa na ukosefu wa vyombo vya
kuwasilishia matatizo yao.
Aidha amefafanua kuwa MSAUD
ya wakati huo haikuwa jumuiya ya
wanafunzi tu, bali Waislamu wa nchi
nzima kutokana na kukosekana kwa
watetezi wa dini, kinyume na sasa
ambapo kuna taasisi nyingi kama
vile TAMPRO, TAMSYA na Baraza
Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu. Rai hii pia iliungwa mkono na
mwalimu Sadick Gogo, mmoja wa
viongozi waliopita wa MSAUD.
Jumuiya ya wanafunzi wa kiislamu wa chuo kikuu cha Dar-es-salaam (MSAUD) ilianzishwa miaka
ya 1960s na umaarufu wake ulidhihiri mwaka 1970.
hutolewa na kuchapishwa na The Islamic Foundation, P.O.Box 6011 Morogoro, Tanzania E-mail: imaanmedia3@gmail.com