Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 7

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA
UMMA

Kumb. Na EA.7/96/01/H/81

15 Oktoba, 2015

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI


Sekretariati ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni chombo ambacho kimeundwa kwa
mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa
na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007 kifungu 29(1). Kwa mujibu wa Sheria hiyo, chombo
hiki, pamoja na kazi zingine kimepewa jukumu la kutangaza nafasi wazi za kazi
zinazotokea katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Waajiri (Taasisi za Umma).
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma anakaribisha maombi ya
Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 29 za kazi kwa ajili ya Katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

NB: MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.


i.
ii.
iii.

iv.

v.

Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45


Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.
Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia
katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za
kazi kwa waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.
Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye
anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees)
watatu wa kuaminika.
Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya
kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya
kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.
- Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
1

vi.

vii.

viii.
ix.

x.
xi.
xii.
xiii.

- Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI


- Computer Certificate
- Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
- Picha moja Passport size ya hivi karibuni.
Testmonials, Provisional Results, Statement of results, hati matokeo za
kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS)
HAVITAKUBALIWA.
Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na
kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU na NECTA).
Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba
isipokuwa kama wanakibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko
katika utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo
yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.
Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za
kisheria.
Mwisho wa kupokea maombi ya kazi ni tarehe 30 Oktoba, 2015
Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono katika ofisi za Sekretarieti ya ajira
HAURUHUSIWI.
Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili au Kiingereza

xiv. Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa


Ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo;

http://portal.ajira.go.tz/
(Anuani hii pia inapatikana kwenye tovuti ya Sektretarieti ya
ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa Recruitment Portal)
xv.

MUHIMU: KUMBUKA KUWEKA (ATTACH) BARUA YAKO YA


MAOMBI WAKATI WA KUFANYA MAOMBI YA KAZI. ANUANI YA
BARUA HIYO IELEKEZWE KWA KATIBU, OFISI YA RAIS
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA S.L.P
63100 DAR ES SALAAM.

1.0
1.1

1.2

1.3

AFISA MAMBO YA NJE DARAJA LA II (FOREIGN SERVICE OFFICER II)


NAFASI 8
MAJUKUMU YA KAZI
Kuandaa Muhtasari, nakala na taarifa zinazohusu masuala ya kimahusiano ya
kimataifa.
Kuhudhuria mikutano mbalimbali.
Kuandaa mahojiano.
Kufuatilia masuala mbalimbali ya kimataifa.
Kufanya utafiti juu ya masuala mbalimbali yanayohusu uchumi, siasa na jamii.
Kutunza kumbukumbu za matukio mbalimbali.
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Shahada ya Sanaa (B.A) ambao wamejiimarisha (major) katika
fani ya uhusiano wa Kimataifa (international Relations), Sheria au Uchumi kutoka
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.
Aidha wawe wamefanya na kufaulu mtihani unaotolewa Chuo cha Diplomasia,
Dar es Salaam.
MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D

2.0 AFISA WA SHERIA DARAJA LA II (LEGAL OFFICER GRADE II) NAFASI 3


2.1 MAJUKUMU YA KAZI
Hili ni daraja la mafunzo katika kazi, hivyo Maafisa wa Sheria katika daraja hili
watafanya kazi za kisheria kwa maelekezo ya Maafisa wa Sheria Waandamizi ikiwa ni
pamoja na:
Kutoa ushauri na kufanya utafiti wa kisheria pale anapohitajika kulingana na
Wizara, Idara ya Serikali ama sehemu aliko.
Kufanya mawasiliano na ofisi nyingine kuhusu masuala ya kisheria kwa
maelekezo ya Maafisa wa Sheria walio katika ngazi za juu.
2.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye shahada ya kwanza ya Sheria kutoka vyuo vinavyotambuliwa
na Serikali na waliomaliza mafunzo ya uwakili yanayotambuliwa na Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
2.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi
3.0 AFISA KUMBUKUMBU DARAJA LA II (RECORDS OFFICER GRADE II)
NAFASI 2
3

3.1 MAJUKUMU YA KAZI


Hili ni daraja la mafunzo katika kazi hivyo atafanya kazi kwa maelekezo ya Maafisa
Kumbukumbu walio juu yake kwa cheo. Kazi atakazojifunza na kufanya ni zile
zifanywazo na Afisa Kumbukumbu Daraja la I: Kudhibiti mifumo ya kumbukumbu, kutunza, na kusimamia matumizi ya
kumbukumbu.
Kutambua na kutafuta kumbukumbu katika masjala.
Kudhibiti mfumo wa kumbukumbu zinazozalishwa na kompyuta, kutunza na
kusimamia matumizi yake.
3.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa mwenye Shahada ya Kwanza katika fani ya Utunzaji na Uhifadhi wa
Kumbukumbu (Records management & Archieves), Upimaji na Ramani na
nyingine zinazolingana nayo kutoka katika Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na
Serikali. Aidha wawe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
3.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali TGS D kwa mwezi.
4 MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU (NYARAKA) DARAJA LA II (RECORDS
MANAGEMENT ASSISTANT GRADE II) NAFASI 1
4.1 MAJUKUMU YA KAZI
Daraja hili ni la mafunzo katika kazi, hivyo atafanya kazi kwa maelekezo ya
Wasaidizi wa Kumbukumbu walio juu yake. Kazi atakazojifunza na kufanya ni
zile zifanywazo na Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja I: Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa na wasomaji.
Kudhibiti upokeaji, uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka.
Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/nyaraka katika makundi
kulingana na somo husika (classification and boxing) kwa ajili ya matumizi ya
ofisi.
Kuweka/kupanga kumbukumbu/nyaraka katika reki (file racks/cabinets) katika
masjala/vyumba vya kuhifadhia kumbukumbu.
Kuweka kumbukumbu (barua, nyaraka nk.) katika mafaili.
Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka kutoka Taasisi za Serikali
4.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne (IV) au sita (VI) wenye cheti cha utunzaji
kumbukumbu katika fani ya Masjala.
4.3 MSHAHARA
4

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGS B kwa mwezi

KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III (PERSONAL SECRETARY GRADE III)


NAFASI 10
5.1 MAJUKUMU YA KAZI
Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida.
Kusaidia kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu
wanapoweza kushughulikiwa.
Kusaidia kutunza taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za
vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa wakati
unaohitajika.
Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majadala, nyaraka au kitu chochote
kinachohitajika katika shughuli za kazi hapo ofisini.
Kusaidia kufikisha maelekezo ya Mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake na pia
kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao.
Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa Maofisa walio katika sehemu alipo,
na kuyakusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusika.
Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa amepangiwa na Msimamizi wake wa kazi.
5.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV waliohudhuria Mafunzo ya Uhazili na kufaulu
mtihani wa Hatua ya Tatu. Wawe wamefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na
Kiingereza maneno 80 kwa dakika moja na wawe wamepata mafunzo ya
Kompyuta kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali na kupata cheti
katika programu za Window, Microstoft Office, Internet, E-mail na Publisher.
5.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B kwa mwezi.

6 MHASIBU DARAJA LA II (ACCOUNTANT GRADE II) NAFASI 3


6.1 MAJUKUMU YA KAZI
Kuidhinisha hati za malipo.
Kuandika taarifa ya mapato na matumizi ya mwezi.
Kusimamia Wahasibu Wasaidizi katika kazi zao za kila siku.
Kusimamia shughuli za uhasibu kwenye Kitengo cha Idara.
Kuandika taarifa ya maduhuli.
6.1.1

SIFA ZA MWOMBAJI

Kuajiri wahitimu wa kidato cha sita (VI) wenye cheti cha kati cha uhasibu
(intermediate stage) kinachotolewa na NBAA au sifa zinazolingana na hizo.
AU
Wenye shahada/Stashahada ya juu ya uhasibu kutoka vyuo vinavyotambuliwa
na serikali.

6.1.2
MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
7 AFISA HABARI II (INFORMATION OFFICER GRADE II) NAFASI 1
7.1 MAJUKUMU YA KAZI
Kukusanya na kuandika habari.
Kupiga picha.
Kuandaa picha za maonyesho.
Kuandaa majarida na mabango (Posters).
Kukusanya takwimu mbalimbali.
Kuandaa majarida na vipeperushi.
Kuhifadhi picha na kuhudumia maktaba na marejeo.
7.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Awe na Shahada ya Kwanza au Stashahada ya Juu ya Uandishi wa Habari au
sifa inayolingana nayo kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
7.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
8 MCHUMI DARAJA LA II (ECONOMIST GRADE II) NAFASI 1
8.1 MAJUKUMU YA KAZI
Kuhudumia kamati mbalimbali za Bunge (Kamati za mahesabu ya Serikali,
Kamati ya mahesabu ya mashirika ya Umma)
Kukusanya takwimu na taarifa mbalimbali za kiuchumi kwa ajili ya uchambuzi na
uandaaji wa sera na mipango ya kiuchumi na kijamii
Kufanya utafiti na uchambuzi wa sera na vigezo vya kiuchumi jumla
Kufanya utafiti na kubainisha fursa zilizopo katika sekta husika
Kukusanya taarifa na takwimu zinazohitajika katika kubainisha vipaumbele vya
ustawi namaendeleo ya jamii.
Kutayarisha na kusambaza takwimu na taarifa za kiuchumi kwa wadau
8.2 SIFA ZA MWOMBAJI

Kuajiriwa wenye shahada ya Uzamili ambao wamejiimarisha (major) katika


mojawapo ya fani ya Uchumi (Economics) au Fedha (Finance) kutoka Chuo
chochote kinachotambuliwa na Serikali na wenye ujuzi wa kutumia kompyuta

8.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.

X.M. DAUDI
Katibu
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

You might also like