Mem Bulletin 99 Online PDF

You might also like

Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 16

HABARI

HabariZA
za
NISHATI
nishati&MADINI
&madini

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Toleo
No.99
51
Toleo No.

Limesambazwa
kwa Taasisi na
Idara
zote
2015 25 - 30, 2015
Limesambazwa
kwa
Taasisi
naMEM
Idara zote MEM Tarehe
- 23-29 Januari ,Desemba

Nawatakia heri ya
e
g
n
u
b
a
W
Maulid,
Krismasi
Waimwagia sifa MEM, TANESCO, REA

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AZINDUA RASMI BODI YA TANESCO -Uk2

n Hakikisheni
Somahabari Uk.2
umeme haukatiki
n Wasikilizeni Wananchi
wakati wote

Waziri wa Nishati
na Madini, Profesa
Sospeter Muhongo

Naibu Waziri wa Nishati na


Madini, anayeshughulikia
Madini Stephen Masele

Naibu Waziri wa Nishati na


Madini anayeshughulikia
Nishati, Charles Kitwanga

Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO,


Mhandisi Felchesmi
Mramba

Mkurugenzi Mkuu wa
REA, Dk. Lutengano
Mwakahesya

Tanzanite iliyokamatwa KIA yafikia USD 1.2m

JWTZ wapongezwa kunusuru mtambo wa Msimbati-Uk4

Soma
habari
Uk. 4

Ofisi ya M awasiliano Serik alini inapokea habari za matukio mbalimbali


kwa ajili ya News Bullettin hii ya Wizar a ya Nishati na Madini
Ofisi ya Mawasiliano Serik alini inapokea habari za matukio mbalimbali
Wasiliana nasi Kitengo cha Mawasiliano kwa simu Namba +255 22 2110490 Fax 2110389 Mob: +255 732 999263
kwa
ajili ya
News
Bullettin
hiiGhorofa
na Jarida
la(MEM)
Wizar
a yapepe:
Nishati
na Madini
au Fika
Ofisi
ya Mawasiliano
ya Tano
Barua
badra77@yahoo.com
Wasiliana nasi Kitengo cha Mawasiliano kwa simu Namba +255 22 2110490 Fax 2110389 Mob: +255 732 999263
au Fika Ofisi ya Mawasiliano Ghorofa ya Tano (MEM) Barua pepe: badra77@yahoo.com

Habari za nishati/madini

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Nawatakia heri ya Maulid, Krismasi


Na Mwandishi Wetu

aziri wa Nishati na
Madini, Prof. Sospeter
Muhongo anawatakia
heri na fanaka ya
Sikukuu ya Maulid na
Krismasi watumishi wote wa Wizara na
Taasisi zote zilizo chini yake.
Waziri Muhongo ambaye kwa
sasa anaendelea na ziara yake katika
Mikoa ya Kanda ya Ziwa kukagua
miradi mbalimbali ya umeme pamoja
na kuzungumza wachimbaji wadogo
wa madini ametuma salamu hizo huku
akiwataka watumishi wote kutumia
Sikukuu hii kutafakari vema namna
ya kuleta mabadiliko ya utendaji kila
mtu kwa nafasi yake aliyonayo ili
kuhakikisha kila mtumishi anatatua kero

za watanzania.
Prof. Muhongo ameongeza kwamba
katika kipindi hiki cha Sikukuu watendaji
wenye dhamana na sekta ya umeme
kuhakikisha Watanzania wanapata
umeme wa uhakika bila kukatika.
Amewaagiza Mameneja wa Mikoa
wa TANESCO kuwa makini na
miundombinu ya umeme kwamba
kuhakikisha kuwa hazianguki na nyaya
hazikatiki hovyo katika kipindi hiki
ambacho mvua zimeanza kunyesha
katika mikoa mbalimbali nchini.
Aidha, Waziri amewataka watendaji
wote wa vituo vinavyozalisha umeme
pamoja na Menejimenti ya TANESCO
na Idara ya Nishati, Wizarani
kuhakikisha kwamba baadhi ya
mitambo iliyoharibika inatengenezwa
haraka na kuendelea kuzalisha umeme
kama kawaida.

Aidha,
Prof.
Muhongo
anawakumbusha Watendaji Idara
ya Nishati wa Wizara, Mameneja
waandamizi wa Kanda na Mameneja
wa vituo vya kuzalisha maji kwa njia
ya maji kutembelea vyanzo vya maji
na kuzungumza Wananchi pmoja na
wadau wengine wakiwamo Mamlaka
za Mabonde, Wizara zinazohusika na
maji pamoja na wakulima ili kupata
ufumbuzi wa matumizi bora ya maji
katika kuzalisha umeme.
Pia Waziri ameiagiza TANESCO
kuimarisha kitengo chake cha ukaguzi
wa umeme kwa wateja (Revenue
Protection Unit) kudhibiti wizi wa
umeme ili kuokoa upotevu wa fedha.
Idara ya Madini pamoja na Wakala
wa ukaguzi wa Madini nchini (TMAA)
nao wameagizwa kuimarisha ulinzi
na ukaguzi katika mipaka na viwanja

vya ndege ili kudhibiti utoroshwaji wa


madini hususan madini ya Tanzanite.
Kwa upande mwingine Prof.
Muhongo amewakaribisha Watanzania
kuwekeza katika miradi ya kuzalisha
umeme kwa kutumia gesi asilia, Makaa
ya mawe, maji, jua, upepo, Jotoardhi,
mawimbi, mabaki ya mimea na
bayogesi.
Pamoja na kuzoeleka kwamba kila
mwisho wa mwaka Watumishi wengi
katika taasisi mbalimbali hupendelea
kwenda likizo, kwa mwaka huu ni
tofauti katika Wizara ya Nishati na
Madini kwa watendaji waandamizi
ambapo Waziri mwenye dhamana na
Wizara hii aliwazuia kwenda likizo
badala yake wahakikishe wanatatua kero
zinazowakabili Watanzania ikiwamo
kero ya tatizo la kukatika umeme mara
kwa mara.

Kuchelewa kwa Miradi


ya umeme, DSM
n

Dkt. Kalemani aagiza


iendelee kutekelezwa Jan 20

Na Asteria Muhozya,
Dar es Salaam

ufuatia
kuchelewa
kukamilika kwa miradi
ya ujenzi wa Kuboresha
miundombinu
ya
Kusafirisha na Kusambaza
umeme katika jiji la Dar es Salaam
kupitia mradi wa Tanzania Energy
Development and Access Program
(TEDAP) chini ya ufadhili wa Benki ya
Dunia, Mkandarasi Kampuni ya SAE
Power Line ya Italia kwa ushirikiano
na Transrail Structures, wametakiwa
kukamilisha miradi hiyo ifikapo mwezi
Februari mwakani.
Hatua hiyo inafuatia ziara ya
Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Dkt. Kalemani kutembelea ujenzi
wa miundombinu hiyo jijini Dar es
Salaam, katika vituo vya Kurasini,
Mbagala, Kipawa na Gongolamboto,
inayosimamiwa na TANESCO,
ambayo
kukamilikwa
kwake
kutawezesha zaidi ya wakazi 10,000 wa
jijini Dar es Salaam, kuunganishwa na
nishati ya umeme.
Dkt.
Kalemani
ameiagiza
TANESCO, kuhakikisha kuwa, hadi
ifikapo tarehe 15 Januari mwakani, iwe
imekwishawalipa fidia wakazi 83 wa
Mbagala Charambe, Kiburugwa na
Kitunda ambao walikubali fidia ya kiasi
cha shilingi 717 milioni zilizotengwa
kupisha ujenzi wa mradi huo.
Bado kuna wananchi wapatao
23 ambao hawajaridhia malipo ya

fidia yao. TANESCO kamilisheni


mazungumzo hayo haraka walipwe ili
kupisha ujenzi uendelee, kwa sababu
hatuwezi kusababisha watu zaidi ya
elfu 10 kukosa umeme sababu ya watu
23. Nataka ifikapo tarehe 20 Januari
Mkandarasi aendelee na kazi,alisema
Kalemani.
Katika hatua nyingine, Dkt.
Kalemani
aliwataka
wananchi
kushirikiana na Serikali ili kuwezesha
miradi mbalimbali ya umeme
kutekelezwa kutokana na umuhimu
wa nishati hiyo kiuchumi. Kama kuna
wananchi wanazuia miradi ya umeme
tupeni nafasi tufanye kazi, umeme ni
uchumi na maendeleo,aliongeza Dkt.
Kalemani.
Pia,
ameitaka
TANESCO,
kuhakikisha inaacha urasimu wa
kukatwa kwa umeme hasa kipindi
cha kuelekea sikukuu za mwisho wa
mwaka za Krismasi na mwaka mpya ili
kuwafanya wananchi wapate huduma
hiyo muhimu.
Naye, Mhandisi Mkuu wa Miradi,
Frank Mashalo, kutoka TANESCO
alieleza kuwa, kuchelewa kukamilika
kwa wakati kwa miradi hiyo
kumetokana na wananchi wa baadhi
ya maeneo ya Mbagala kugomea
malipo ya fidia.
Kwa upande wake, Naibu Katibu
Mkuu Wizara ya Nishati na Madini,
Mhandisi Paul Masanja, akitoa
majumuisho alieleza kuwa, ziara hiyo
imesaidia kuona udhaifu wa utekelezaji
wa miradi hiyo na hivyo aliahidi
kuhakikisha kwamba mapungufu yote

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani, (wa kwanza


kushoto), akiongozwa na Meneja Mwandamizi Miradi ya Umeme
wa TANESCO, Gregory Chegere kukagua maendeleo ya mradi wa
kuboresha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme katika
Jiji la Dar es Salaam katika kituo cha Mbagala. Kulia ni Mhandisi wa
miradi (TANESCO), Frank Mashalo. Wengine nyuma ni Naibu Katibu
Mkuu, Mhandisi Paul Masanja (nyuma kulia) na Kamishna Msaidizi wa
Nishati anayeshughulikia maendeleo ya Nishati, James Andilile.
yanayafanyiwa kazi na kukamilika kwa
mujibu wa maagizo na maelekezo ya
Dkt. Kalemani.
Kwa upande wake Kamishna
Masaidizi wa Nishati, anayeshughulia
Maendeleo ya Nishati, James Andilile,
alisema kuwa utekelezaji wa miradi
hiyo utafuatiliwa kwa karibu ikiwemo
kuhakikisha kwamba changamoto za
mradi huo zinatafutiwa suluhisho la
kutosha.
Gharama za ujenzi wa mradi huo
ulioanza mwaka 2010 na kusainiwa
mwaka 2012 ni Dola za Marekani

milioni 34.2 ambapo tayari serikali


imekwishalipa dola za Marekani
milioni 28.
Mbali na Dar es Salaam, mradi
wa kuboresha miundombinu ya
Kusafirisha na Kusambaza Umeme
wa (TEDAP) pia unatekelezwa katika
mikoa ya Arusha, na Kilimanjaro.
Katika hatua nyingine, Dkt.
Kalemani alifanya ziara ya kushtukiza
katika ofisi ya TANESCO, Kinondoni
Kusini ili kuona namna wananchi
wanavyohudumiwa katika ofisi hizo na
kuangalia utendaji kazi wa ofisi hiyo.

NewsBulletin

Habari za nishati/madini

http://www.mem.go.tz

TANESCO yatakiwa kuwa makini

MEM

Tahariri

Na Mohamed Saif- Mwanza

Na Badra Masoud

Tusherehekee Sikukuu
umeme ukiwaka!!

Wiki hii Watanzania wataungana na waumini wengine


duniani kusherehekea Sikukuu za Maulid ya kuzaliwa kwa
Mtume Muhammad (S.A.W) usiku wa Jumatano kuamkia
Alhamisi ya tarehe 24 na Sikukuu ya Krismasi, kuzaliwa Yesu
Kristo itakayosherehekewa Ijumaa tarehe 25.
Kwa hakika Sikukuu hizi ni kubwa hivyo, Watanzania na
waumini wengine duniani wana kila sababu ya kusherehekea
kwa amani na furaha sikukuu hizo. Hivyo, ili kutimia kwa
sherehe hizo, hakuna asiyelewa moja ya huduma muhimu
kukamilisha siku hizo ni upatikanaji wa huduma ya umeme.
Umeme huleta furaha, na inapotokea umeme kukatika
ghafla nyakati za usiku wakati ambapo familia au kundi la
watu wanaangalia TV, utasikia wakitoa sauti za masikitiko na
unapowaka wanashangilia huku wakipiga kelele.
Kwa dalili hizo ni wazi kwamba katika Sikukuu hizi za
Maulid na Krismasi kwa namna moja ama nyingine huduma
ya umeme ni kichocheo kikubwa katika kufanikisha Sikukuu
hizi.
Maulid ambayo husomwa nyakati za usiku katika maeneo
mbalimbali nchini ambapo maeneo hayo yote huhitaji mwanga
wa taa ili watu wote waliohudhuria waweze kuona namna
shughuli nzima ya usomaji wa Maulid unavyofanyika kuanzia
mwanzo hadi mwisho.
Kwa upande wa Krismasi, katika maeneo ya Makanisa,
waumini wanahitaji umeme ili ibada hiyo ifanyike katika
mwanga na si gizani ikizingatiwa ibada hufanyika usiku wa
tarehe 24 katika misa za mkesha.
Hayo ni maeneo machache tu niliyoyataja ambayo
yanaonyesha umuhimu wa umeme bila kusahau majumbani
ambapo huko ndiyo familia hukutana kwa ajili ya kusherehea.
Sababu hizo ndizo zinazopelekea kuonyesha kwamba
Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO wana dhamana
kubwa waliyoibeba katika kuhakikisha kwamba Watanzania
wanapata huduma hiyo ya umeme; Hii ni kusema kwamba
wahusika hawana budi kuhakikisha umeme unapatikana
katika kipindi chote cha Sikukuu.
Hivyo hivyo, tunatambua na kuheshimu agizo la Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuwazuia
Watendaji wa Wizara na TANESCO kwenda likizo katika
kipindi hiki cha Sikukuu.
Tunaamini kwamba Prof. Muhongo ana nia njema na
kuwajali sana Watanzania ndiyo maana ameamua kupigana
kufa na kupona kuhakikisha tatizo la umeme na tatizo la
kukatika kwa umeme mara kwa mara linakoma na hasa katika
kipindi hiki cha Krismasi na Maulid.
Bila kusahau kwamba Prof. Muhongo ameamua yeye
kutokusherehekea Krismasi kwa kuendelea na ziara za kukagua
vituo vya kuzalisha umeme na ofisi za kutoa huduma za
TANESCO ambapo kwa sasa yupo Kanda ya Ziwa ambapo
pia anakutana na Wachimbaji wadogo wa madini wa Kanda
hiyo.
Tunasema Prof. Muhongo songambele, Watanzania
wanaelewa vema dhamira yako ya kizalendo katika
kuhakikisha kuwa umeme wa kutosha, uhakika na wa bei
nafuu unapatikana ili nchi yetu iweze kuwa ya katika kipato
cha kati ifikapo mwaka 2025.

hirika la Umeme Tanzania (Tanesco),


limetakiwa kuwa makini wakati wa
kuingia mikataba na Wakandarasi
ili kuepuka kuuziwa mitambo hafifu
na kusababisha hasara na migogoro
isiyo ya lazima.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa
Sospeter Muhongo ametoa agizo hilo
alipofanya ziara kwenye mitambo ya kuzalisha
umeme ya Nyakato ya jijini Mwanza.
Mara baada ya kukagua mitambo hiyo
yenye uwezo wa kuzalisha Megawati 60,
Profesa Muhongo alijionea mitambo mitatu
ambayo ilikuwa imeharibika.
Profesa Muhongo alisema alichogundua
tangu ameanza ziara ya kukagua mitambo ya
kuzalisha umeme maeneo mbalimbali nchini
ni kuwa Shirika hilo linaonekana kutumia
watu wa kati katika kununua mitambo yake.
Alisema haoni sababu ya Shirika hilo
kununua mitambo yake kutoka kwenye
kampuni ambazo hazina viwanda vya
kutengeneza mitambo husika wakati zipo
kampuni mahiri duniani zenye kutengeneza
mitambo bora.
Hawa inaonekana wanatumia watu

ambao hawatengenezi mitambo na ndio


maana tunashuhudia tunauziwa mitambo
hafifu ambayo katika kipindi kifupi tangu
imeanza uzalishaji baadhi imeharibika,
alisema.
Alisema sheria ya manunuzi haiwazuii
Tanesco kuingia mikataba ya moja kwa moja
na kampuni ambazo zinatengeneza mitambo.
Akizungumzia kituo hicho, Meneja wa
Kituo Mhandisi Ernest Mzenya alisema
Kituo hicho kilianza kufanya kazi mnamo
mwaka 2013 na kinayo mitambo 10 ya
kuzalisha umeme ambapo kila mtambo una
uwezo wa kuzalisha megawati 6.
Hata hivyo, Mhandisi Mzenya alisema
hivi sasa ni mitambo Saba tu ambayo inafanya
kazi kwani mitambo mitatu imeharibika.
Alisema ilipofika mwaka 2014 ikiwa
ni mwaka mmoja tu tangu mitambo hiyo
kuanza kufanya kazi mtambo mmojawapo
uliharibika. Aliendelea kueleza kwamba
mwaka jana katika miezi tofauti mitambo
miwili iliharibika na hivyo kufanya ndani ya
kipindi cha miaka miwili jumla ya mitambo
mitatu kuharibika.
Meneja huyo alisema wanatarajia
kukutana na Mkandarasi aliyewauzia
mitambo hiyo mwishoni mwa mwezi Januari

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akikagua vipuli


vilivyoharibika vya mitambo ya kuzalisha umeme ya Nyakato ya jijini Mwanza.
KWA HABARI PIGA SIMU
kitengo cha mawasiliano

TEL-2110490
FAX-2110389
MOB-0732999263
Bodi ya uhariri
Mhariri Mkuu: Badra Masoud
Msanifu: Lucas Gordon
Waandishi: Veronica Simba, Asteria Muhozya, Greyson
Mwase Teresia Mhagama, Mohamed Saif, Rhoda James ,
Nuru Mwasampeta na Zuena Msuya

Five
Pillars of
Reforms
increase efficiency
Quality delivery
of goods/service
satisfAction of
the client
satisfaction of
business partners
satisfAction of
shareholders

Habari za nishati/madini

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Tanzanite iliyokamatwa KIA yafikia


USD milioni 1.2
n
n

Chambo asema operesheni ni endelevu


Makalla atoa saa 24 raia wa
kigeni wasio na vibali kuondoka

Teresia Mhagama na
Asteria Muhozya

atibu
Mkuu
Wizara
ya Nishati na Madini,
Mhandisi Omar Chambo
ameeleza kuwa madini aina
ya Tanzanite yaliyokamatwa
yakitoroshwa nje ya nchi bila kuwa na
vibali tarehe 15 Desemba, 2015 kupitia
uwanja wa ndege wa Kimataifa wa
Kilimanjaro (KIA) yamefikia thamani ya
Dola za Marekani milioni 1,207,990.
Katibu Mkuu alisema hayo jijini
Arusha wakati wa kikao chake na
Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa
ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara
ambazo zimeamua kufanya kazi kwa
pamoja ili kudhibiti utoroshaji wa madini
ya Tanzanite na kufuatilia kwa karibu
shughuli za uchimbaji na biashara ya
madini hayo ili yanufaishe taifa.
Katibu Mkuu alisema kuwa Tanzanite
hiyo ghafi yenye uzito wa gramu 2,015.59
ilikuwa ikitoroshwa na raia wa India, Jain
Anurag aliyekuwa akitaka kuelekea mji
wa Jaipur kwa kutumia shirika la ndege la
Qatar.
Nataka niwaeleze watanzania
wanaoshirikiana na raia wa kigeni
kutorosha Tanzanite kuwa wajiepushe
na biashara hii haramu kwani hatua
kali zitaendelea kuchukuliwa dhidi yao
na hatuna mzaha katika hili, alisema
Mhandisi Chambo.
Alieleza kuwa madini hayo
yaliyokamatwa yameshataifishwa kama
ambavyo sheria na kanuni za madini
zinavyoelekeza na kwamba zoezi hilo la
ukamataji watorosha madini hufanywa
na Wizara ya Nishati na Madini kupitia
Wakala wake wa Ukaguzi wa Madini
(TMAA) kwa kushirikina na Taasisi
nyingine kama Mamlaka ya Viwanja vya
Ndege, Jeshi la Polisi, Idara ya Usalama
wa Taifa, Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) na Idara ya Uhamiaji.
Aidha alieleza kuwa serikali itafuta
leseni za wafanyabiashara wa madini
watakaobainika kutorosha rasilimali
hiyo nje ya nchi ikiwemo kuwakamata
wachimbaji
na
wafanyabiashara
wanaokwepa kulipa kodi stahiki kwa
serikali.
Ili kudhibiti utoroshaji madini
unaofanywa na wafanyabiashara wenye
leseni na wasio na leseni, wazawa na
wasio wazawa, tumeshajipanga kwa
kushirikiana na Kamati za Ulinzi na
Usalama za mikoa mitatu ya Manyara,
Kilimanjaro na Arusha ili kudhibiti hali
hii na Tanzania ibaki kama kinara katika
uzalishaji na uuzaji wa madini haya na
sio nchi nyingine, alisema Mhandisi
Chambo.

Kuhusu wachimbaji wadogo nchini,


alisema kuwa serikali itaendelea kugawa
maeneo ya uchimbaji madini kwa
wachimbaji hao ikiwa ni pamoja na utoaji
ruzuku, uagizaji wa zana kama baruti na
utoaji wa mafunzo huku akitoa angalizo
kuwa wachimbaji hao wanapaswa kuwa
waaminifu na kuhakikisha kuwa wanalipa
kodi stahiki serikalini badala ya kusubiri
kuchukuliwa hatua za kisheria.
Wakati huohuo Mwenyekiti wa
Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa
ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara na

Mkuu wa mkoa wa
Kilimanjaro, Amos
Makalla alitoa masaa
24 kwa raia wa kigeni
wote wanaojihusisha
na biashara ya madini
ya Tanzanite na madini mengine kinyume
cha sheria kuondoka nchini mara moja na
watakaokaidi agizo hilo watachukuliwa
hatua kali za kisheria.
Agizo hilo alilitoa baada ya Kamati
hiyo kubaini kwamba uwepo wa wageni
mbalimbali kutoka nje ya nchi hususani
Kenya, Sri Lanka, Nepal na India ambao
hujihusisha na biashara ya Tanzanite bila
kuwa na leseni zinazowaruhusu kufanya
hivyo na hatimaye hutorosha madini hayo
kwenda nje ya nchi.

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Omar Chambo (wa


pili kulia) akitembelea baadhi ya vitalu vya uchimbaji madini ya Tanzanite
katika eneo la Mirelani mkoani Manyara mara baada ya kumaliza kikao
kikao chake na Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha,
Kilimanjaro na Manyara ambazo zimeamua kufanya kazi kwa pamoja ili
kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite.Kulia kwake ni Afisa Madini
Mkazi katika Ofisi ya Madini Mirelani, Mhandisi Henry Mditi.

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Omar Chambo


(wa kwanza kulia) akiangalia moja ya mashine zinazotumika katika
shughuli za uchimbaji madini katika eneo la Mirelani mkoani Manyara
wakati alipotembelea eneo hilo mara baada ya kumaliza kikao kikao
chake na Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro
na Manyara ambazo zimeamua kufanya kazi kwa pamoja ili kudhibiti
utoroshaji wa madini ya Tanzanite.

TANESCO yatakiwa
kuwa makini
>>INATOKA UK. 3
mwakani ili kujadili namna ya
kutengeneza mitambo hiyo.
Alisema endapo mazungumzo
hayo yatashindwa kuzaa matunda
kwa pande hizo mbili kushindwa
kukubaliana, watarejea kwenye
sheria.
Taarifa
hiyo
ilimkasirisha
Waziri Muhongo na hivyo kuagiza
wataalamu wote waliohusika kwenye
manunuzi ya mitambo hiyo kutoa
maelezo ya kina haraka.
Juzi
nilikuwa
Somanga
Fungu na nimekutana na tatizo la
namna hii; hili halikubaliki lazima
waliotufikisha hapa wafahamike na
tayari nimemuagiza Mkurugenzi wa
Tanesco, alisema Profesa Muhongo.
Alisema tayari Tanesco inazo
kesi zaidi ya mia moja na hata hivyo
ni nadra kushinda na badala yake ni
fedha nyingi zinatumika na huwa
zinachukua miaka mingi.
Aliwaagiza kukaa pamoja na
endapo muafaka haukupatikana
wafike kwake kwa ajili ya
mazungumzo zaidi.
Waziri Muhongo alibainisha
kuwa aliamua kufanya ziara ili
kujionea hali halisi ya uzalishaji
umeme, aliongeza kuwa katika ziara
zake alizokwishafanya aligundua
kuwa hakukuwa na umakini wakati
wa ununuzi wa mitambo husika.
Ilipaswa wataalamu wafanye
uchunguzi wa mitambo na
kujiridhisha kabla mitambo hiyo
haijaletwa nchini, alisema Prof.
Muhongo.
Mbali na suala la umakini kwenye
ununuzi, Profesa Muhongo alisema
wataalamu wanapaswa kufuata
taratibu za uendeshaji wa mitambo
na hivyo aliwaasa kuwa makini muda
wote wakati wa kuendesha mitambo
hiyo.
Aidha, mara baada ya kutembelea
kituo hicho, Profesa Muhongo
alifanya ziara ya kushtukiza kwenye
kituo cha huduma kwa wateja cha
shirika hilo cha mkoani humo na
kuzungumza na wateja waliokuwa
kituoni hapo wakisubiri huduma.
Rashid Abubakar ni miongoni
mwa
wateja
waliokuwepo
kituoni hapo ambaye alimueleza
Waziri Muhongo kuwa huduma
zinazotolewa na shirika hilo
haziridhishi.
Alimueleza Waziri Muhongo
kuwa tangu tarehe 12 nguzo moja
maeneo anayoishi iligongwa na gari
na kuanguka lakini hadi sasa hakuna
hatua iliyochukuliwa na Shirika hilo
mbali na kupatiwa taarifa za mara
kwa mara.
Kufuatia malalamiko hayo Profesa
Muhongo alimkumbusha Meneja
wa Kanda ya Ziwa wa Shirika hilo,
Mhandisi Amos Maganga kutekeleza
maagizo aliyoyatoa kwa uongozi
wa TANESCO ya kuboresha kwa
huduma hadi kufikia tarehe 15 mwezi
ujao.

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Habari za nishati/madini

PURA kuanza Julai, 2016


Na Rhoda James,
Dar es Salaam

erikali kupitia Wizara ya


Nishati na Madini, iko kwenye
mchakato
wa
kuanzisha
Mamlaka ya Udhibiti wa
Shughuli za Mkondo wa juu wa
Mafuta (Petroleum Upstream Regulatory
Authority PURA) ifikapo mwezi Julai,
2016.
Kwa mujibu wa sheria mpya ya
mafuta (PA 2015) PURA ndiyo chombo
kitakacho mshauri Waziri wa Nishati na
Madini masuala ya kiufundi (Technical
advice) kuhusu shughuli za utafutaji na

uzalishaji wa mafuta na gesi asilia nchini.


Akitoa hotuba katika Mkutano Mkuu
wa Tatu wa Programu ya Ushirikiano wa
Kitaasisi kati ya Tanzania na Norway,
uliofanyika Makao Makuu ya Wizara,
jijini Dar es Salaam, Naibu Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,
Mhandisi Paul Masanja alisema kuwa,
tangu kuanzishwa kwa Programu
hiyo, imefanikisha pamoja na mambo
mengine uundaji wa Sera ya Gesi Asilia,
Sheria ya Mafuta na Petroli ya mwaka
2015, Sera na Sheria hiyo inaweka
mfumo imara wa Kisheria na kiutawala
katika usimamizi na udhibiti wa shughuli
zote za mafuta na gesi asilia nchini.
Masanja aliongeza kuwa, Sheria ya

Mafuta na Gesi Asilia ya mwaka 2015


imepelekea uundwaji wa Taasisi mbili
mpya ambazo ni Mamlaka ya Udhibiti
wa Shughuli za Mafuta na Gesi asilia
(PURA) na Ofisi ya Ushauri kuhusu
Petroli na Gesi asilia (Oil and Gas
Advisory Bureau- OGAB)
Aidha, nyezo hizo zimeweka wazi
majukumu mapya na wajibu wa Shirika
la Maendeleo ya Petroli Tanzania
(TPDC). Kwa sasa TPDC itajiendesha
kibiashara na kuachana na shughuli za
udhibiti.
Pia Naibu Katibu Mkuu alieleza
kwamba Norway imekuwa ni msaada
mkubwa kwa Tanzania, kwani imesaidia
sekta ya Nishati tangu mwaka 1975

kwenye Mradi wa Songo Songo,


alisisitiza Mhandisi Masanja.
Masajaalitumiafursahiyokuishukuru
Serikali ya Norway kwa niaba ya Serikali
ya Tanzania na kueleza kuwa, ni rai ya
Serikali kuona kuwa Norway inaendelea
kushiriki kikamilifu katika Mchakato
wa uundwaji wa mamlaka ya PURA
hususan katika kuwajengea uwezo
watumishi.
Kwa upande wake kiongozi wa
ujumbe huo, Trygue Bendiksby kutoka
Norway katika mkutano huo alishukuru
kwa ushirikiano uliopo baina ya nchi
hizo na kuahidi kuendelea kutoa
ushirikiano katika kutekeleza majukumu
mbalimbali.
Mkutano huo wa Programu ya
ushirikiano wa Kitaasisi ni wa Tatu tangu
Programu ilipoanza mwezi Februari,
2013, na hufanyika kila mwaka kati ya
nchi hizo mbili.

Naibu Katibu Mkuu (katikati), Mhandisi Paul Masanja akiwa katika picha
ya pamoja na Viongozi waandamizi kutoka Idara ya Nishati na Uongozi wa
Norway katika Mkutano huo wa Ushirikiano wa Kitaasisi kati ya Tanzania
na Norway.

Baadhi ya watendaji kutoka Wizara


ya Nishati na Madini na Serikali
ya Norway wakifuatilia masuala
yaliyokuwa yakizungumzwa katika
kikao hicho.

Naibu Katibu Mkuu,


Mhandisi Paul Masanja
(mbele) akiwa katika
Mkutano wa Ushirikiano
wa Kitaasisi kati ya Tanzania
na Norway. Wengine katika
picha na Uongozi kutoka
nchi ya Norway.

Habari za nishati/madini

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Harakisheni mazungumzo ya kuiuzia


Gesi Dangote - Profesa Muhongo

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kushoto) akielekeza jambo wakati wa ziara yake
katika Kiwanda cha Saruji cha Dangote. Anayemfuatia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Fatma Ally akifuatiwa na
Balozi wa Tanzania Nchini Msumbiji, Shamim Nyanduga.

Na Mohamed Saif

aziri wa Nishati na
Madini,
Profesa
Sospeter
Muhongo
ameagiza kuharakishwa
kwa mazungumzo ya
kuiuzia Gesi Asilia kampuni ya kuzalisha
saruji ya Dangote iliyojenga mitambo
yake mkoani Mtwara.
Agizo hilo limetolewa hivi karibuni
mkoani Mtwara wakati wa ziara yake ya
kukagua mitambo ya kuzalisha umeme ya
Mtwara, Kituo cha kuchakata Gesi Asilia
cha Madimba, Kiwanda cha kutengeneza
saruji cha Dangote na Kituo cha kuzalisha

umeme cha Somanga Fungu.


Waziri Muhongo alielezwa kuwa
kwa sasa kiwanda hicho kinazalisha
umeme kwa kutumia mitambo ya kukodi
ya kutumia mafuta ambayo inazalisha
kiasi cha megawati 42 hivyo kuongeza
gharama za uendeshaji.
Ilielezwa kuwa Kiwanda hicho
kinao mpango wa kuzalisha umeme
kwa kutumia gesi asilia ama makaa ya
mawe ambapo ilielezwa kuwa jumla ya
Megawati 75 zitazalishwa.
Mbali na hilo, Waziri Muhongo
alielezwa kuwa kiwanda hicho kina
matatizo ya kutopata malighafi ya jasi na
makaa ya mawe kwa wakati na kwa kiasi

Mitambo
ya kuzalisha
umeme
iliyokodishwa
kutoka China
na Kampuni
ya Dangote.

kinachohitajika kutoka kwa makampuni


ya Kitanzania yanayochimba madini
hayo.
Waziri
Muhongo
alisema
amesikitishwa kuona kiwanda hicho
hakijapatiwa umeme wa Tanesco na
badala yake kinatumia umeme wa
mitambo ya kukodi.
Waziri muhongo aliagiza wataalam
wa Wizara ya Nishati na Madini, Shirika
la Umeme Tanzania (TANESCO),
Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC),
na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO)
wakutane na kampuni ya Dangote
kuzungumzia suala la kumuuzia Gesi
Asilia na makaa ya mawe kwa ajili ya

kuzalisha umeme.
Profesa Muhongo alitumia
fursa hiyo kuzialika kampuni za
Watanzania kuwekeza kwenye
uzalishaji umeme kwa kutumia
vyanzo mbalimbali.
Mtaalamu
ametueleza
kwamba tunayo gesi ya kutosha
hivyo
watanzania
jitokezeni
muwekeze. Kuna matoleo ya gesi
Mtwara, Lindi, Mkuranga na Dar
es salaam; Watanzania wajitokeze
kuwekeza na hususan maeneo ya
Lindi na Mkuranga ambayo hadi
sasa hayana uwekezaji mkubwa,
alisema.
Hata hivyo Profesa Muhongo
aliupongeza uongozi wa Dangote
kwa hatua waliyofikia ya ujenzi wa
kiwanda hicho .
Aidha, Profesa Muhongo
aliambatana na Balozi wa Tanzania
nchini
Msumbiji,
Shamim
Nyanduga ambaye alikuwa mkoani
Mtwara kikazi.
Waziri Muhongo alimuomba
Balozi
huyo
kuhakikisha
anahamasisha Wafanyabiashara wa
Kitanzania waliopo nchini humo
kununua saruji ya Tanzania ili
kukuza Biashara ya nchini.
Profesa Muhongo alisema kuwa
Serikali imeamua kwa makusudi
kuwapa kipaumbele wazawa
wauze jasi na makaa ya mawe kwa
Dangote ili kuongeza kipato kwa
wananchi wake.
Aliwaagiza watoa huduma
husika wahakikishe wanazingatia
mkataba walioingia na Kampuni
hiyo na kuepuka kufanya kazi
kienyeji.
Profesa
Muhongo
aliiasa
kampuni hiyo kuhakikisha inauza
saruji yake kwa bei nafuu. Alisema
lengo la Serikali ni kuhakikisha vifaa
vya ujenzi nchini ikiwemo saruji
vinashuka bei ili kuwapa unafuu wa
ujenzi wananchi.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati)


alipotembelea eneo linalotumiwa na Kiwanda cha Dangote kwa
ajili ya kuchimba chokaa. Kushoto ni Balozi wa Tanzania Nchini
Msumbiji, Shamim Nyanduga na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya
Mtwara, Fatma Ally.

NewsBulletin

Habari za nishati/madini

http://www.mem.go.tz

GST yabaini chanzo mipasuko ya ardhi Olborot


Na Samwel Mtuwa

akazi
wa
wilaya
ya
Chemba
katika kijiji cha
Olborot tarafa
ya Goima kata ya Mrijo katika
kitongoji cha Bomba mkoani
Dodoma walipatwa na mshtuko
kutokana na mpasuko mkubwa
wa ardhi uliosababishwa na
mvua zinazoendelea kunyesha
nchini.
Akizungumza na MEM
Bulletin, Mwenyekiti wa serikali
ya kijiji cha Olborot Abdallah
Suti alisema kuwa tarehe
13 Desemba, 2015, mvua
kubwa ilinyesha kwa muda
wa masaa mawili mfululizo na
baada ya kumalizika ukatokea
mpasuko mkubwa katika ardhi
uliopelekea kuathiri zaidi ya
kaya 21.
Ilikuwa siku ya jumapili
mchana mvua ilinyesha kwa
muda wa saa mbili mapema
baada ya kuisha , tukaona ardhi
inapasuka na kuacha mashimo
makubwa sehemu mbalimbali
katika kijiji chetu alisema Suti.
Suti
aliongeza
kuwa
kutokana na hali hiyo
waliwasiliana na mamlaka
mbalimbali za serikali ikiwemo
Wakala wa Jiolojia Tanzania
(GST) ili kupata taarifa za
kiuchunguzi
kwa ajili ya
kuchukua tahadhari.
Mtalaam wa majanga
ya asili kutoka GST, Gabriel

Mbogoni baada ya kufanya


uchunguzi alisema kuwa eneo
hilo la Olborot lipo katika
ukanda wa bonde la ufa (East
African Rift Valley System)
ambalo kwa kawaida huwa na
mipasuko ya miamba ardhini.
Utafiti wa awali umeonesha
kwamba eneo hilo lipo katika
mbuga ya Sikwakwa yenye
udongo mweusi wa mfinyanzi
(black cotton soil) ambayo
imezungukwa na safu za
milima.
Alisema kuwa kutokana na
eneo hilo kutokupata mvua za
kutosha kwa kipindi kirefu kuna
uwezekano kwamba kina cha
maji ya ardhini (ground water)
kilipungua kwa kiasi kikubwa
na kusababisha kuwepo kwa
nafasi wazi ardhini. Tukio la
kunyesha kwa mvua kubwa
mnamo tarehe 13/12/2015
katika eneo hilo lilisababisha
eneo husika kufurika maji
ambayo yalipenya ardhini na
kufuata mipasuko ya miamba
hali ambayo ilisababisha
udongo pia kuchukuliwa na
maji na kuacha nyufa kubwa ..
Akitoa
ushauri
kwa
wakazi wa kijiji mara baada ya
kufanya uchunguzi , Mbogoni
alishauri kuwa eneo hilo sio
salama kutokana na jiografia
inayozunguka eneo hilo.
Akielezea kuhusu ujenzi
katika eneo hilo Mbogoni
alisema athari za mipasuko
katika nyumba za kijiji hicho
zinatokana na idadi kubwa ya

nyumba hizo kujengwa bila


kuzingatia viwango ambapo
misingi ya nyumba hizo
haikuwa imara kwani baadhi
ya nyumba zilijengwa kwa
kozi mbili au tatu tu kwa tofali
za kuchoma wakati kina cha
udongo huo wa mfinyanzi ni
zaidi ya mita tatu hali ambayo
inahitaji msingi wa nyumba
ambao ni imara.
Gabriel Mbogoni na
Godson Kamihanda
kutoka Wakala wa Jiolojia
Tanzania (GST) wakifanya
upimaji wa mpasuko ili
kujua chanzo chake.

Sehemu ya
nyumba mojawapo
iliyoathiriwa na
mpasuko.

Bei ya Umeme lazima ishuke: Muhongo


Rhoda James

aziri
wa
Nishati
na
M a d i n i
Profesa
Sospeter
Muhongo ameliagiza Shirika
la Umeme Nchini (Tanesco)
kushusha bei ya Umeme ili
upatikaji wa nishati hiyo ilingane
na kipato cha Watanzania walio
wengi ambacho bado ni kidogo..
Agizo hilo alilitoa hivi
karibuni wakati alipotembelea
kituo cha kuzalisha umeme cha
IPTL kilichopo Tegeta jijini Dar
es Salaam.
Kituo hiki kinazalisha
Umeme usiopungua kilowatt
45 kwa siku na wananchi
mnawauzia kwa shilingi 180
hadi 187 kwa uniti, ina maana
mnatengeneza faida mara mbili
kwa kuwa mnazalisha uniti moja
kwa gharama inayoanzia shilingi
90 hadi 100 hivyo ni lazima bei
ya umeme ishuke ili kuendana
na maisha ya mwananchi wa
kawaida,Alisema
Profesa

Muhongo.
Mafuta yalikuwa yakiuzwa
kwa pipa Dola za Marekani
milioni 200, lakini yakashuka
hadi Dola milioni 100 na hivi
sasa tunapoongea yameshuka
zaidi kwani kwa pipa yanauzwa
kwa Dola za Marekani milioni
38, kwa hiyo umeme lazima
ushuke bei,alisisitiza Profesa
Muhongo.
Vilevile Profesa Muhongo
alisisitiza kuwa lazima Tanesco
watoe huduma kwa wakati
pale wananchi wanapohitaji
huduma mbalimbali kutoka
katika Shirika hilo. wananchi
wakipiga
simu
hawapati
huduma wanayohitaji (Service
maintenance) hii ni mbaya
lazima mjirekebishe, alisema
Profesa Muhongo.
Kwa upande wake, Meneja
wa kituo hicho cha IPTL,
Mhandisi Mohamed Kisiwa
alisema kituo hicho kimeanza
kufanya kazi mwaka 2009 na
kinazalisha umeme kutoka
kwenye mitambo mitano
iliyopo katika kituo hicho kiasi
cha megawati 43.6 kwa siku.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akioneshwa mitambo ya uzalishaji


umeme ya IPTL iliyopo Tegeta jijini Dar es Salaam.

Habari za nishati/madini

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Vijiji 5000 vyapata umeme


Rhoda James

Wizara ya Nishati na Madini kupitia


Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
imesema hadi mwaka huu (2015)
vijiji vipatavyo 5,000 vimeunganishwa
na nishati ya umeme kupitia miradi
inayosimamiwa na Wakala huo.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi

Mkuu wa Wakala huo, Dkt. Lutengano


Mwakahesya wakati wa kikao na
Naibu Waziri wa Nishati na Madini,
Dkt. Medard Kalemani kilichofanyika
katika ukumbi wa Wizara ya Nishati na
Madini jijini Dar es Salaam.
Dkt. Mwakahesya alisema kuwa
hadi sasa vijiji visivyopugua 5,000

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Medard Kalemani (mbele)


akiwa katika kikao cha Viongozi Waandamizi kutoka Shirika la
Umeme Tanzania (TANESCO), Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA).

vimepata umeme. Upatikanaji wa


umeme huu umesaidia masuala mengi
ikiwemo kuimarisha uchumi wa nchi
kwa kiwango kikubwa, upatikanaji wa
ajira kwa wananchi, na upatikanaji wa
umeme wa uhakika,.
Aliongeza kuwa ujenzi wa miradi ya
umeme vijijini ni kigezo cha msingi na

muhimu katika maendeleo ya Taifa na


kueleza kuwa vijiji ambavyo havijapata
umeme vitegemee kupata umeme hivi
karibuni.
Kwa upande wake, Dkt. Kalemani
alisema kuwa Wizara bado ina kazi
kubwa ya kufanya katika kuhakikisha
wananchi wanapata nishati ya umeme
ya uhakika na kwa gharama nafuu na
kueleza kuwa Wizara itashirikiana na
Taasisi zake katika kuhakikisha hilo
linafanikiwa.

Viongozi Waandamizi kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TENESCO),


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na Wakala
wa Nishati Vijijini (REA) wakiwa kwenye kikao na Naibu Waziri wa
Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani katika Ukumbi wa Wizara ya
Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.

Viongozi Waandamizi
kutoka Wakala wa
Nishati Vijijini (REA) na
Mamlaka ya Udhibiti
wa Nishati na Maji
(EWURA) wakati wa
kikao kilichofanyika
Wizarana na Naibu
Waziri wa Nishati
na Madini, Merdard
Kalemani.

Pro. Muhongo Aahidi maeneo zaidi kwa Wachimbaji Wadogo

Na Mohamed Saif,
Kanda ya Ziwa

aziri
wa
Nishati
na
Madini,
Profesa
Sospeter
Muhongo amefanya kikao
na Shirikisho la Wachimbaji
Wadogo (FEMATA), Viongozi
wa Shirikisho la Wachimbaji
Madini Wadogo wa mkoa wa
Geita (GEREMA), mkoa wa

Mwanza (MWAREMA) na
wachimbaji wadogo wa mikoa
hiyo miwili na kuwaahidi
kuendelea kuwatafutia maeneo
ya uchimbaji madini.
Aliyasema hayo katika kikao
kilichofanyikia katika Ukumbi
wa Mikutano wa Ofisi ya
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza
na kueleza kuwa Serikali pia
itawanyanganya maeneo watu
wote wanaohodhi maeneo
ya uchimbaji madini bila
kuyaendeleza.
Profesa Muhongo pia

amealigiza Shirika la Madini


la
Taifa
(STAMICO)
kufanya kazi kwa karibu na
Wakala wa Jiolojia Tanzania
(GST) kuhakikisha maeneo
wanayopewa
wachimbaji
wadogo
wa
madini
yamefanyiwa utafiti ili kuzuia
tabia ya baadhi ya wachimbaji
wadogo
kuchimba
kwa
kuhamahama.
Vilevile
ameiagiza
STAMICO
kusaidia
wachimbaji wadogo katika
masuala mbalimbali kama

kuwatengenezea
maandiko
yatakayowasaidia
katika
masuala mbalimbali ikiwemo
utafutaji wa mikopo katika
Taaisisi za Kifedha na kutoa
ushauri wa uchimbaji bora wa
madini.
Profesa Muhongo pia
aliagiza kuwa kabla ya kuisha
kwa mwaka wa Fedha wa
2015/16, Wizara ya Nishati na
Madini iitishe kikao na Wakala
wa Jiolojia Tanzania (GST),
Shirika la Madini la Taifa
(STAMICO), viongozi wa

FEMATA na MWAREMA
kujadili namna ya kuleta ufanisi
katika uchimbaji wa madini
mdogo nchini.
Aidha aliwataka wachimbaji
madini
nchini
kutunza
mazingira wakati wote wa
shughuli zao na kutovamia
maeneo halali ya utafiti na
uchimbaji mkubwa wa madini
na wazingatie utunzaji wa
amani na kuepuka uchochezi
wa aina yoyote.

NewsBulletin

Habari za nishati/madini

http://www.mem.go.tz

TPDC ikiwajibika kwa jamii


Mkuu wa
Wilaya ya
Mkuranga,
Abdallah
Kihato akitoa
neno la
shukrani baada
ya kukabidhiwa
kiasi cha shilingi
milioni kumi
(10,000,000)
kwa ajili ya
ujenzi wa
kisima cha maji
katika kijiji cha
Njia Nne.
Wanakijiji
wa kijiji cha
Njia Nne
waliohudhuria
shughuli ya
makabidhiano
ya kiasi
cha shilingi
milioni kumi
(10,000,000)
kwa ajili ya
ujenzi wa kisima
cha maji katika
kijiji hicho.

Meneja Mawasiliano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania


(TPDC), Marie Msellemu (wa pili kulia) akikabidhi mfano wa hundi ya
shilingi milioni kumi (10,000,000) kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga,
Abdallah Kihato (wa tatu kulia) kwa ajili ya ujenzi wa kisima cha maji
katika kijiji cha Njia Nne.

Maonesho ya 5 ya Kimataifa ya Vito ya Arusha


yenye aina mbalimbali za vito zikiwemo
Tanzanite, Ruby, Sapphire, Tsavorite,
Rhodolite, Spessartite, Tourmaline,
Chrysoberyl na Almasi yanatarajiwa kuvutia
Zaidi ya kampuni 100 za wafanyabiashara na
wachimbaji madini ya Vito kutoka Tanzania na
nchi zingine za Afrika Mashariki, Kati na Kusini;
na zaidi ya wanunuzi 500 kutoka zaidi ya nchi 25
ulimwenguni

Jisajili na Ushiriki Sasa!!!


Wasiliana na: Kamati ya Maandalizi AGF
Simu: +255 784352299 or +255 767106773
Barua pepe: info@arushagemshow.com
:ama Ofisi za Madini za Kanda

Yameandaliwa na Wizara ya Nishati na Madini


kwa kushirikiana na
Chama cha Wafanyabiashara wa Madini (TAMIDA)

10

Habari za nishati/madini

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

kikao kujadili tanzanite

Mwenyekiti wa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro


na Manyara na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Amos Makalla (aliyesimama)
akizungumza na wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha,
Kilimanjaro na Manyara (hawapo pichani) ambazo zimeamua kufanya kazi kwa
pamoja ili kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite nje ya nchi. Wa kwanza
kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Omar Chambo, wa
kwanza kulia ni Katibu Tawala mkoa wa Manyara, Eliakim Maswi na wa pili kutoka
kulia ni Mkuu wa mkoa wa Arusha, Daud Ntibenda.

Afisa Madini Mkazi katika Ofisi ya Madini Mirelani, Mhandisi Henry Mditi
akitoa taarifa ya kazi zinazofanywa na Ofisi hiyo iliyopo katika wilaya ya
Simanjiro mkoani Manyara.Wanaosikiliza ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati
na Madini, Mhandisi Omar Chambo (wa pili kushoto), Wa kwanza kushoto
ni Kaimu Kamishna wa Madini, Mhandisi Ally Samaje. Wengine katika picha ni
Kamishna Msaidizi wa Madini sehemu ya Uthaminishaji Madini, Latifa Mtoro
(wa kwanza kulia) na wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Uunganishaji na
Ushirikishi Wadau katika Tasnia ya Uziduaji (EISF), Catherine Lyombe.

Katibu Tawala mkoa wa Manyara, Eliakim Maswi (wa kwanza kulia) akizungumza
na baadhi ya wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha,
Kilimanjaro na Manyara mara baada ya kumaliza kikao ambacho kilijadili masuala
mbalimbali ikiwemo udhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite nje ya nchi.

Makamishna Wasaidizi wa Madini,Wizara ya Nishati na Madini, kutoka kulia ni Julius


Sarota (Wachimbaji Wadogo), Latifa Mtoro (Uthaminishaji madini), Salim Salim (Uchumi
na Biashara) pamoja na Mkurugenzi wa Sheria, Justus Mulokozi (wa kwanza kushoto)
wakiwa katika kikao kilichojumuisha Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha,
Kilimanjaro na Manyara (hawapo pichani) ambazo zimeamua kufanya kazi kwa pamoja
ili kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite nje ya nchi.

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Omar Chambo (wa kwanza
kulia) akizungumza na baadhi ya wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa
ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara ambazo zimeamua kufanya kazi kwa pamoja ili
kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite nje ya nchi.

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Omar Chambo (wa kwanza
kushoto) akiwa katika moja ya vitalu vya uchimbaji madini ya Tanzanite katika eneo
la Mirelani mkoani Manyara wakati alipofanya ziara katika eneo hilo mara baada ya
kumaliza kikao kikao chake na Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha,
Kilimanjaro na Manyara ambazo zimeamua kufanya kazi kwa pamoja ili kudhibiti
utoroshaji wa madini ya Tanzanite.Kulia ni Afisa Madini Mkazi katika Ofisi ya Madini
Mirelani, Mhandisi Henry Mditi.

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Habari za nishati/madini

11

ZIARA YA NAIBU WAZIRI DAR ES SALAAM

Meneja Mwandamizi Miradi ya Umeme wa TANESCO, Gregory Chegere (kushoto)


akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (mwenye
tai nyekundu) kuhusu maendeleo ya kituo cha usafirishaji na usambazaji umeme cha
Mbagala jijini Dar es Salaam. Kituo hicho kimejengwa kupitia mradi wa Tanzania Energy
Development and Acess Program (TEDAP) chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia. Wengine
wanafuatilia ni Naibu Katibu Mkuu, Mhandisi Paul Masanja (nyuma ya Naibu Waziri) na
Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia maendeleo ya Nishati, James Andilile,
wengine ni Maafisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akizungumza na


baadhi ya wateja waliokuwa wakisubiri kuhudumiwa sehemu ya huduma za wateja
katika Ofisi ya TANESCO Kionondoni Kusini. Wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja. Wengine ni Maofisa
kutoka Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO.

Meneja wa TANESCO, Kinondoni Kusini, Gasper Msigwa, kulia akimweleza jambo


Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa kwanza kushoto) wakati
Dkt. Kalemani alipofanya ziara ya kushtukiza ofisini hapo kuona namna TANESCO
inavyowahudumia wananchi. Nyuma ya Dkt. Kalemani na Naibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja. Kulia nyuma ni Kamishna Msaidizi wa Nishati
anayeshughulikia Maendeleo ya Nishati, James Andilile na wengine ni Maofisa wa Wizara
na Wanahabari.

Naibu Katibu Mkuu, Mhandisi Paul Masanja (wa pili kulia) akijadiliana jambo na Kamishna
Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Maendeleo ya Nishati, James Andilile (wa kwanza
kulia) huku Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa kwanza
kushoto) akibadilishana jambo Meneja Mwandamizi Miradi ya Umeme wa TANESCO,
Gregory Chegere (wa pili kulia) wakati Dkt. Kalemani alipotembelea maendeleo ya
ujenzi huo unajengwa na Kampuni ya SAE Power Line ya Italia kwa ushirikiano na
Transrail Structures.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akizungumza na


Meneja Mawasiliano Ofisi ya TANESCO, Kinondoni Kusini. Naibu Waziri alifika ofisini
hapo katika ziara ya kushtukiza ili kujua kero mbalimbali zinazokutana nazo wananchi
ikiwa pia kuangalia namna ofisi hizo zinavyowahudumia wananchi. Wa kwanza kulia ni
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja na Kamishna
Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Maendeleo ya Nishati, James Andilile. Kushoto ni
Meneja wa TANESCO, Kinondoni Kusini, Gasper Msigwa.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa kwanza kulia) akiongea
jambo na watumishi wa ofisi ya Huduma kwa Wateja (TANESCO) wakati alipofanya
ziara ya kushtukiza katika ofisi ya TANESCO Kinondoni Kusini. Wengine ni Naibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja na Kamishna Msaidizi wa
Nishati anayeshughulikia Maendeleo ya Nishati, James Andilile.

12

Habari za nishati/madini

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

ZIARA YA PROFESA SOSPETER


MUHONGO KANDA YA KUSINI

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akikagua


mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia Gesi Asilia ya Kituo cha
Mtwara ambacho kinahudumia Mikoa ya Mtwara na Lindi.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akikagua


kituo cha kuchakata gesi asilia cha madimba mkoani Mtwara chenye
uwezo wa kusafisha gesi futi za ujazo milioni 210 kwa siku. Katikati ni
Meneja Mitambo ya Kuchakata Gesi Asilia, Mhandisi Sultan Pwaga.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa


Sospeter Muhongo, akimpa zawadi
ya picha, Balozi wa China nchini, Lu
Youqing, mara baada ya ufunguzi wa
mkutano wa Tatu wa Wanasayansi
Vijana Duniani.

Baadhi ya mitambo ya kuchakata Gesi Asilia ya Kituo cha Madimba


ambacho hivi karibuni kilitembelewa na Waziri wa Nishati na Madini,
Profesa Sospeter Muhongo

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia)


akizungumza wakati wa ziara ya kukagua kituo cha kuchakata gesi
asilia cha Madimba. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara,
Fatma Ally
Waziri wa
Nishati na
Madini, Profesa
Sospeter
Muhongo
(kushoto)
akimsikiliza
Meneja wa Kituo
cha Kuzalisha
Umeme cha
Somanga Fungu,
Mhandisi Job
Mwantinda
(kulia) wakati wa
ziara ya kukagua
mitambo ya
Kituo hicho.
Katikati ni
Meneja wa
Tanesco Kanda
ya Kusini, Joyce
Ngahyoma.

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Habari za nishati/madini

13

GST YAFANYA USAFI KATIKA


KITUO CHA MABASI DODOMA
Watumishi wa GST katika
picha ya pamoja wakiwa
na vifaa vya usafi baada ya
kumaliza kazi ya usafi katika
kituo cha mabasi mkoani
Dodoma.

Watumishi wa GST kwa pamoja wakifanya usafi katika kituo cha mabasi
Dodoma katika kushiriki zoezi la kuweka mji safi.

Mkurugenzi wa huduma za Maabara GST Augustna Rutaihwa akizungumza


na waandishi wa habari juu ya ushiriki wa GST katika kuweka mji safi.

Watumishi wa GST kwa pamoja wakiwa kituo cha mabasi Dodoma


wakishiriki zoezi la kuweka mji safi.

Watumishi wa GST wakiongozana kwa pamoja kuelekea katika eneo


la kufanya usafi

14

Habari za nishati/madini

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Prof. Muhongo akaribisha wawekezaji


wa ndani uzalishaji Umeme

CTI, TPSF, TCCIA


zapongeza uteuzi wake

Teresia Mhagama

aziri wa Nishati na
Madini,
Profesa
Sospeter Muhongo
ametoa wito kwa
watu na
Taasisi
binafsi nchini kujitokeza na kuwekeza
katika kuzalisha nishati ya umeme ili
kuweza kuunga juhudi za serikali za
kuhakikisha nchi inakuwa na nishati
ya uhakika na ya gharama nafuu.
Profesa Muhongo aliyasema
hayo wakati wajumbe wanaounda
Shirikisho la Viwanda Tanzania
(CTI), Taasisi ya Sekta Binafsi
Tanzania (TPSF) na Chama cha
Wafanyabiashara, Wenye Viwanda
na Wakulima (TCCIA) walipofika
katika Wizara ya Nishati na Madini
ili kutoa pongezi kwa uteuzi wake na
kuwasilisha changamoto mbalimbali
za umeme wanazozipata katika
utekelezaji wa majukumu yao.
Kama nchi tuna rasilimali
zote za kuzalisha umeme, nyinyi
pia mnakaribishwa kuwekeza ama
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati)
kutafuta wawekezaji wenye nia ya
akiwa katika kikao na Wajumbe wanaounda Shirikisho la Viwanda
dhati kuwekeza nchini, hata hivyo
Tanzania (CTI), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) na Chama cha kama serikali tunajitahidi kuongeza
Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Wakulima (TCCIA) waliofika
umeme kwenye gridi ya Taifa na
katika Wizara ya Nishati na Madini ili kutoa pongezi kwa uteuzi wake ifikapo katikati ya mwezi Januari
na kuzungumza kuhusu masuala mbalimbali ya sekta ya umeme nchini. Kinyerezi I itaongeza megawati 80
katika gridi na ujenzi wa mitambo ya
Wengine katika picha ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini,
Mhandisi Omar Chambo (kushoto kwa Waziri), Mkurugenzi Mtendaji umeme ya Kinyerezi II itakayozalisha
umeme wa kiasi cha megawati 240
wa Shirika la Umeme (TANESCO), Mhandisi Felchesmi Mramba
itaanza muda wowote kwani masuala
(kushoto kwa Katibu Mkuu) na kulia kwa Waziri ni Mwenyekiti wa
ya kifedha yameshakamilika alisema
Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Dkt. Samuel Nyantahe.
Muhongo.
Alisema kuwa serikali pia inataka
kuzalisha umeme kwa kutumia
makaa ya mawe ambapo kuna tani
zaidi ya bilioni 9 nchini, na kualika
Taasisi hizo binafsi kushirikiana na
serikali kuzalisha umeme huo ambapo
makampuni binafsi yataruhusiwa
kumuuzia mteja moja kwa moja
ili kuweza kuleta ushindani wa
usambazaji wa nishati hiyo muhimu
kwa wananchi.
Profesa Muhongo aliongeza kuwa
serikali inakaribisha wawekezaji ili
wazalishe umeme kwenye miradi
midogo ya maji isiyozidi megawati 10
ambayo itasadia wananchi walio nje ya
gridi ya Taifa kupata umeme na kutaja
vyanzo vingine vya uzalishaji umeme
vinavyohitaji wawekezaji kuwa ni
upepo, jua, jotoardhi, mawimbi,
tungamotaka, na bayogesi.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Omar Chambo
Awali Mwenyekiti wa Shirikisho la
akijitambulisha kwa wajumbe wa wanaounda Shirikisho la Viwanda
Tanzania (CTI), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) na Chama cha Viwanda Tanzania (CTI) Dkt. Samuel
Nyantahe alisifu uteuzi wa Profesa
Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Wakulima (TCCIA) waliofika
katika Wizara ya Nishati na Madini ili kutoa pongezi Waziri wa Nishati Sospter Muhongo kuwa Waziri wa
Nishati na Madini na kueleza kuwa
na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) kwa uteuzi wake na
amekuwa na mchango mkubwa kwa
kuzungumza kuhusu masuala mbalimbali ya sekta ya umeme nchini.
Taifa katika kuhakikisha kuwa nchi
kulia kwa Waziri ni Mwenyekiti wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) inakuwa na nishati ya umeme ya
Dkt. Samuel Nyantahe.Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa TCCIA, kutosha kupitia vyanzo mbalimbali
Adam Zuku, wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Godfrey vya uzalishaji nishati hiyo.
Simbeye.

Alisema kuwa hali ya umeme sasa


si mbaya sana, lakini pia bado kuna
changamoto mbalimbali ambazo
Taasisi hizo wanakumbana nazo na
wameona ni vyema wakaziwasilisha
kwa Profesa Muhongo.
Alisema kuwa baadhi ya
changamoto hizo ni kukatika
umeme mara kwa mara, kupanda na
kushuka kwa kiwango cha umeme
ambacho hupelekea athari katika
mitambo inayotumika viwandani na
kutokuwepo kwa taarifa pale umeme
unapotaka kukatwa.

Changamoto
nyingine
tunayokumbana nayo ni kutokulipwa
kwa fidia kwa mitambo inayoungua
wakati umeme unapokatwa ghafla,
kuchelewa kwa watumishi wa Tanesco
katika eneo la tukio pale ambapo tatizo
la umeme linaripotiwa na pia kuwa
na bei kubwa za umeme ambazo
zinapeleka bidhaa tunazozalisha
pia kuuzwa kwa gharama kubwa,
alisisitiza Dkt. Nyantahe.
Alisema kuwa bidhaa zinazotoka
Tanzania hushindana na za nchi
nyingine za Mashariki na Kusini
mwa Afrika hivyo ni vizuri gharama
za umeme zikashuka ili bei ya bidhaa
hizo zishuke na hivyo kupata soko
kubwa nchi za nje.
Waziri wa Nishati na Madini,
Profesa Sospeter Muhongo akijibu
hoja hizo alisema kuwa Wizara
inatambua uwepo wa changamoto
za upatikanaji wa umeme wa uhakika
na wa gharama nafuu na kwamba
Wizara inafanyia kazi suala hilo.
Tunatambua kwamba umeme
hautoshi na ndio maana tumeamua
kuwa na energy mix, ya kwanza ni
kuzalisha umeme kwa njia ya gesi
ambayo tunayo ya kutosha kwani
mpaka sasa kiasi kilichopatikana ni
futi za ujazo trilioni 55.08, hivyo tuna
uwezo sasa wa kuzalisha umeme kwa
kusaidiana na makampuni binafsi,
alisema Muhongo.
Kuhusu suala la upunguzaji
wa bei za umeme, alisema kuwa
ameshawaagiza watendaji wa Shirika
la Umeme nchini (TANESCO) na
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma
za Nishati na Maji (EWURA)
kufanyia kazi suala hilo na kuwasilisha
mapendekezo kwake mnamo tarehe 2
Januari 2016 na kusema kuwa kwa
vyovyote vile bei hiyo lazima ipungue.
Profesa Muhongo pia alisisitiza
kufanya mabadiliko ya watendaji wa
Idara ya Nishati katika Wizara ya
Nishati na Madini na TANESCO
kutokana na sababu mbalimbali
ikiwemo urasimu, ukosefu wa ubunifu
katika uanzishaji na uendelezaji wa
miradi ya umeme, majadiliano ya
mikataba kuchukua muda mrefu na
kueleza kuwa yote hayo yanalenga
katika kuleta ufanisi katika sekta ya
umeme nchini.

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Habari za nishati/madini

15

Ijue Almasi adimu


ipatikanayo Tanzania
Na Roda James

anzania ni miongoni mwa


nchi zilizojaliwa kuwa na
aina mbalimbali za madini
na inatajwa kuwa kitovu cha
madini ya vito barani Afrika.
Miongoni mwa madini hayo ya vito
ni Almasi. Asili ya neno Almasi kwa
lugha ya Kiswahili haifahamiki vizuri
lakini warusi hutumia neno Almaz
kumaanisha Diamond kwa lugha ya
Kiingereza. Almasi ni mojawapo ya
madini adimu yenye mvuto mkubwa
kwa wavaaji wa vito tokea zama za
kale. Almasi inachukuliwa na wapenzi
wake kama kielelezo cha utukufu
(wafalme, watawala, makuhani na
watu wenye mamlaka); lakini pia
ni kielelezo cha utajiri na nguvu ya
kifedha kwa watumiaji wengine.
Kwa asili yake, madini ya almasi
hayana rangi (transparent with no hue);
hata hivyo kasoro katika uumbaji wake
yaani mchanganyiko wa kikemikali
na mpangilio usio sahihi wa atomu
(chemical impurities and structural
diffects) husababisha uwepo wa rangi
mbalimbali katika madini ya almasi.
Uwepo wa rangi unaweza kuongeza
au kupunguza thamani ya jiwe la almsi
kulingana na mahitaji ya soko. Rangi
zinazoongeza thamani ya almasi ni
nyekundu (ndiyo hadimu kuliko rangi
zote), Bluu na Pinki. Rangi zingine ni
njano, nyeusi, kijani na kahawia.
Hapa Tanzania, mgodi pekee
wenye historia kubwa ya uzalishaji
almasi ni mgodi wa Williamson
Diamonds Limited (WDL) ulioko
Kishapu Shinyanga. Mgodi huu
ambao pia unaitwa Mwadui kwa
heshima ya jina la chifu wa eneo hilo,
uligunduliwa na Mjiolojia Dk. John
Williamson mwaka 1940. WDL
ilisajiliwa rasmi kama kampuni
mwaka 1942 na Serikali ya kikoloni
kwa mtaji wa hisa 400 kila moja ikiwa
na bei ya 500 sawa na jumla ya mtaji
wa 200,000.
Mgodi huu unasifika duniani kwa
mambo mengi lakini pia ni miongoni
mwa wazalishaji wachache wa almasi
za rangi ya pinki (rangi adimu na
inayopendwa sana duaniani). Kwa
kawaida mgodi wenye umaarufu wa
kuzalisha almasi za rangi ya pinki
ni mgodi wa Agyle ulioko Australia
Magharibi ambao hutoa 90% ya
almasi zote ya pinki duniani.
Pamoja na uwepo wa mgodi wa
WDL, Tanzania pia inachimba almasi
kupitia mgodi wa kampuni ya El

Hilal Minerals Limited iliyopo jirani


na mgodi wa WDL huko Kishapu
Shinyanga. Almasi pia zinachimbwa
kwa uchimbaji mdogo katika eneo
la Maganzo, Kishapu Shinyanga,
Mabuki Mkoani Mwanza na maeneo
mengine ya nchi yetu.
Almasi za pinki hupatikana katika
migodi michache sana duniani na
uadimu wake hufanya madini haya
yatafutwe zaidi (high demand).
Tanzania inasifika kwa utoaji wa
Almasi za rangi ya Pinki katika Afrika.
Almasi za rangi ya pinki hupatika
kwa nadra sana ukiwa na madini
hayo umetukuka na wewe unakuwa
miongoni mwa watu maarufu au tajiri
sana.
Madini ya Almasi huuzwa na
kununuliwa kulingana na soko kwa
vigezo vya uzito (carat), usafi wa
jiwe (clarity) mkato (cut) na rangi
yake (colour) maarufu kama 4Cs!
Kwa upande wa rangi kipimo cha
ubora wake hujulikana kwa kutumia
mpangilio huu: kuanzia kundi D N, Rangi ya juu kabisa kwa Almasi
inaanzia D hadi N. Mpangilio huu
unaokubalika zaidi duniani ulitolewa
na Taasisi ya Jemolojia ya Marekani
(Gemmological Institute of America
GIA). Taasisi hii ndiyo bobefu zaidi
katika utambuzi na uthaminishaji wa
madini ya almasi na vito duniani.
Mwezi Septemba mwaka huu
2015, mgodi wa WDL ulibahatika
tena kupata jiwe kubwa la almasi
ya pinki lenye uzito wa carat 23.16.
Almasi hii imeweka rekodi nyingine
kwa mgodi wa Mwadui, kwani iliuzwa
kwa Dola za Marekani milioni 10.05
huko Antwerp nchini Ubelgiji. Hii ni
rekodi mpya kwa thamani kuwahi
kupatikana na kuuzwa kwa mgodi
huo au mgodi mwingine wowote wa
almasi hapa nchini.
Mbali na jiwe hili la carat 23.16
pinki nyingine kubwa kuwahi
kupatikana katika mgodi wa Mwadui
ilikuwa na uzito wa carat 54.5 ambayo
Dk. Williamson alimzawadia Malkia
wa Uingereza (Queen Elizabeth II)
mwaka 1947 kama zawadi ya harusi.
Jiwe hilo halikuwahi kuuzwa au
kuingizwa sokoni lakini linadhaniwa
kuwa ni almasi bora ya pinki kuwahi
kupatikana. Pinki hiyo iliyotolewa
kama zawadi kwa Malkia wa
Uingereza baadaye ilikatwa na kutoa
jiwe la carat 23.6 ambalo liliwekwa
katika mfano wa ua (Williamson pink
brooch). Pambo hili ni miongoni mwa
mapambo adimu yanayopendwa

Malkia Elizabeth wa Uingereza


kuvaliwa na Mtawala huyo wa
Uingereza.
Wananchi wanafaidika na uwepo
wa madini ya almasi kwa kiasi
kikubwa kwa kujipatia ajira za moja
kwa moja migodini au kupitia huduma
mbalimbali ikiwemo biashara na
migodi husika, ajira kwenye kampuni
zinazotoa huduma migodini na
biashara kati yao na waajiriwa kwenye
migodi inayowazunguka. Aidha,
Serikali hujipatia fedha za kigeni,
mapato kwa njia ya mrabaha, kodi
na tozo mbalimbali kwa mujibu wa
sheria. Mapato hayo yote yanapelekea
uchumi wa Tanzania kuimarika.
Faida za moja kwa moja za madini
hayo ni ajira. Mgodi wa Mwadui
unatoa ajira za kudumu takribani 600
pamoja na ajira zisizo za moja kwa
moja zaidi ya 500 kupitia kampuni
zinazotoa huduma mbalimbali
kwenye mgodi huo.
Pia upo Mgodi wa El Hillal
Minerals limited uliopo Wilayani
Kishapu ambao unazalisha madini
ya almasi. Nao unatoa ajira kwa
wafanyakazi takribani 200. Kwa

maana hiyo wafanyakazi zaidi ya 1500


wanaendesha maisha yao kutokana
na migodi hiyo miwili ya Williamson
na El Hillal bila kuhusisha wachimbaji
wadogo.
Takwimu za mwaka 2013 za
Mgodi wa Mwadui zinaonesha
kuwa mgodi huo ndiyo unashikilia
rekodi ya dunia ya kuwa mgodi pekee
uliochimbwa mfululizo kwa miaka 70;
ndiyo mgodi mkubwa zaidi duniani
unaochimbwa kwa stahili ya shimo la
wazi (open cast); unayo akiba ya almasi
inayokadiriwa kuwa carat milioni 40;
ukikadiriwa kuwa na uhai wa miaka
18 (Planned mine life). Aidha, mgodi
wa Mwadui unatarajiwa kuendelea
kuzalisha almasi kwa miaka mingine
50 ijayo.
Kumbe Tanzania tuna madini ya
kila aina na yenye thamani kubwa
sana, na ubora wa juu. Wachimbaji
wote wakubwa kwa wadogo wanao
jishughulisha na uchimbaji wa madini
Tanzania watoe ushirikiano kwa
Serikali katika ulipaji wa kodi mbali
mbali ili wananchi wa Tanzania
wafaidike na madini yao.

16

Habari za nishati/madini

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

SHIRIKA LA MAENDELEO YA
PETROLI TANZANIA (TPDC)

TAARIFA KWA UMMA


UPATIKANAJI WA HATI MILIKI YA ARDHI YA
MRADI WA KUCHAKATA NA KUSINDIKA GESI
ASILIA (LIQUEFIED NATURAL GAS -LNG) ENEO
LA LINDI
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linatoa
taarifa kwa umma juu ya upatikanaji wa hati miliki ya ardhi
kwa ajili ya mradi wa kuchakata na kusindika gesi asilia
(LNG). Upatikanaji wa hati miliki hii ni muendelezo wa
taarifa iliyotolewa kwa umma na Kamishna wa Ardhi juu
ya ubatilishaji wa miliki za ardhi ya tarehe 30 Oktoba 2015
na kuchapishwa katika gazeti la Daily News la tarehe 17
Novemba 2015.
Eneo la ardhi hii lipo katika kiwanja Na.1-Kitalu A,
Likongo katika Manispaa ya Lindi na lilipendekezwa na
kuchaguliwa kwa pamoja kati ya TPDC na wawekezaji
kutoka kampuni za kimataifa za utafutaji mafuta na gesi asilia
(IOCs) zinazofanya kazi zake hapa nchini. Kupatikana kwa
hati miliki ya ardhi hii ni hatua muhimu katika utekelezaji
wa mradi huu ambao unalenga kuendeleza gesi asilia
iliyogunduliwa katika kina kirefu cha bahari ya Hindi upande
wa Tanzania. Mradi huu utakapokamilika utawezesha
uzalishaji wa gesi asilia kwa mahitaji ya ndani ya nchi, kiasi
kingine kitasafirishwa nje ya nchi na kuliingizia taifa fedha za
kigeni.
Ardhi ambayo itatumika kujenga mradi huu ni hekta
2,071.705 na inamilikiwa na TPDC. Sambamba na mradi wa
LNG lipo eneo lipatalo zaidi ya hekta 17,000 linalozunguka
mradi. Eneo hili litatumika kwa ajili ya ujenzi wa viwanda
vikubwa vya kuzalisha bidhaa mbalimbali zitokanazo na
gesi asilia. Serikali kupitia TPDC inatoa wito kwa wananchi
kujiepusha na ununuzi wa maeneo haya kwani tayari
yamekwisha tengwa kwa miradi yenye manufaa kwa Taifa na
hivyo kujigawia au kuvamia itakuwa ni kinyume cha sheria za
nchi.

Imetolewa na;
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji,
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania,
P.O.Box 2774,
Dar-es-Salaam.
Tanzania.

WIZARA YA NISHATI NA MADINI


INAKARIBISHA WAWEKEZAJI
WA KITANZANIA KUWEKEZA KATIKA
MIUNDOMBINU YA UZALISHAJI UMEME
KATIKA VYANZO VIFUATAVYO:-

1.
2.
3.
4.

Gesi asilia (Natural Gas)


Makaa ya mawe (Coal)
Miradi mikubwa na midogo ya maji (Hydro)
Nishati jadidifu (Renewables):-

a)
Umeme wa Jua (Solar)
b) Umeme wa Upepo (Wind)
c)
Umeme wa Jotoardhi (Geothermal)
d) Umeme wa Mawimbi (Tides and Waves)
e)
Umeme wa Mabaki ya taka Tungamotaka
(Biomass)
f)
Bayogesi (Biogas).
Kwa mawasilano, wasiliana na wafuatao:WIZARA YA NISHATI NA MADINI:Samwel Mgweno
Simu ya mkononi Na. 0754651364
E.mail samuel.mgweno@mem.go.tz
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA
(TANESCO):Anitha Ishengoma
Simu ya mkononi 0687350076
E-mail anitha.ishengoma@tanesco.co.tz
Tangazo hili limtetolewa na: Wizara ya Nishati na
Madini

Kwa wadau wa sekta za Nishati na Madini, tembelea kurasa mpya za Wizara kwenye Mitandao
ya Kijamii ya Twitter na Facebook kwa anuani ya Nishati na Madini Karibu tuhabarishane na
tujadili kuhusu sekta za Nishati na Madini kwa maendeleo ya Watanzania wote.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

You might also like