Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 110

SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

WIZARA YA MIUNDOMBINU NA
MAWASILIANO
HOTUBA YA MAKADIRIO YA MAPATO NA
MATUMIZI YA WIZARA YA MIUNDOMBINU
NA MAWASILIANO KWA MWAKA WA FEDHA
2014/2015

JUNI 2014

YALIYOMO
I

UKURASA

UTANGULIZI ............................................................. 4

II.
UTEKELEZAJI WA KAZI ZA KAWAIDA NA MAENDELEO
KWA MWAKA 2013/2014 NA MALENGO YA MWAKA
2014/201. 6
IIa) OFISI KUU PEMBA ..................................................... 8
IIb) UTAWALA NA SERA ................................................... 9
(i) IDARA YA MIPANGO, SERA NA UTAFITI ....................... 10
(i-1) MIRADI YA MAENDELEO ............................................. 11
(i-1.1) MIRADI YA UJENZI WA BARABARA

11

(i-1.1.1) Mradi wa Barabara Tatu za Kaskazini Pemba ........... 12


(i-1.1.2) Mradi wa Barabara ya Wete-Chake ......................... 13
(i-1.1.3) Mradi wa Barabara ya Ole-Kengeja ......................... 14
(i-1.1.4) Mradi wa Barabara za Vijijini Kaskazini Pemba: ........ 14
(i-1.1.5) Mradi wa Barabara Zinazoingia Mjini Unguja ........... 15
(i-1.1.6) Mradi wa Barabara 3 za Vijijini Unguja .................... 16
(i-1.1.7) Mradi wa Barabara 6 za Vijijini Unguja .................... 16
(i-1.2) MIRADI YA SEKTA YA USAFIRI WA ANGA .................. 17
(ii) IDARA YA UTUMISHI NA UENDESHAJI ........................ 26
IIc. SEKTA YA USAFIRI WA NCHI KAVU. .......................... 28
2

(i) IDARA YA UJENZI NA UTUNZAJI WA BARABARA ........... 29


(ii) IDARA YA USAFIRI NA LESENI ................................... 34
IId) SEKTA YA MAWASILIANO ......................................... 37
(i) IDARA YA MAWASILIANO ........................................... 38
IIe) SEKTA YA USAFIRI WA ANGA ................................... 41
(i) MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE ZANZIBAR ............ 41
IIf) SEKTA YA USAFIRI WA BAHARINI ............................. 48
(i) MAMLAKA YA USAFIRI BAHARINI.............................. 48
(ii) SHIRIKA LA BANDARI ................................................ 52
(iii) SHIRIKA LA MELI NA UWAKALA............................... 57
III HITIMISHO. .............................................................. 60
IV. MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2014/2015 .............. 62
KIAMBATANISHO NAMBA 1: ............................................ 63
KIAMBATANISHO NAMBA 2: ............................................ 67
KIAMBATANISHO NAMBA 3: ........................................... 70
KIMBATANISHO NAMBA 4:............................................ 725
KIAMBATANISHO NAMBA 5: .......................................... 933
KIAMBATANISHO NAMBA 6: .......................................... 988
KIAMBATANISHO NAMBA 7: ........................................ 1033
KIAMBATANISHO NAMBA 8: .......................................10909
3

I:

UTANGULIZI

1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba


Baraza lako likae kama Kamati, ili liweze kupokea,
kujadili na hatimae kupitisha Mpango na Makadirio
ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya
Miundombinu na Mawasiliano, kwa kazi za kawaida
na maendeleo kwa mwaka wa fedha 2014/2015.
2. Mheshimiwa
Spika,
naomba
nianze
kwa
kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai na
kutuwezesha kukutana tena leo kujadili maendeleo ya
Sekta ya Usafiri na Mawasiliano na ya Taifa kwa
ujumla.
3. Mheshimiwa Spika, napenda vile vile nimpongeze
na kumshukuru kwa namna ya pekee Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Ali
Mohamed Shein kwa ushauri na miongozo anayoitoa
kwa Wizara katika kuendeleza Sekta ya Usafiri na
Mawasiliano na kuendelea kuiongoza vyema nchi yetu.
4. Mheshimiwa Spika, niruhusu pia nitumie fursa hii
kuwashukuru Makamo wa Kwanza wa Rais, Mhe.
Maalim Seif Sharif Hamad, pamoja na Makamo wa Pili
wa Rais, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, kwa uongozi wao
imara na wa mfano ambao umesaidia sana Wizara hii
katika utekelezaji wa majukumu yake.
5. Mheshimiwa Spika, naomba nimalizie kwa pongezi
zifuatazo: kwanza kwako wewe binafsi Mhe. Spika,
4

Naibu wako, na Wenyeviti wa Baraza kwa kuendelea


kuliongoza Baraza letu kwa staha, uvumilivu mkubwa
na
bila
kuyumba
katika
kusimamia
kanuni
tulizojiwekea. Pili, Mawaziri wenzangu na Wawakilishi
wote kwa kazi nzuri wanayofanya na kwa ushirikiano
mzuri wanaonipa katika kutekeleza majukumu yangu
kama Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano. Tatu,
na mwisho familia yangu na wapiga kura wa Jimbo la
Uchaguzi la Ziwani ambao wameendelea kunionyesha
upendo na ushirikiano mkubwa hata pale ninapokuwa
nimebanwa na majukumu ya kitaifa nje ya Jimbo langu
la uchaguzi.
6. Mheshimiwa Spika, hotuba hii imezingatia kikamilifu
maudhui yaliyomo kwenye Hotuba ya Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora, anayesimamia
Tume ya Mipango Mhe. Dkt. Mwinyihaji Makame
Mwadini; na Waziri wa Fedha Mhe. Omar Yussuf Mzee,
zilizowasilishwa katika Baraza lako Tukufu tarehe 14
Mei, 2014. Naomba kuwashukuru na kuwapongeza
kwa hotuba zao zilizotoa ufafanuzi wa kina kuhusu
utekelezaji wa mipango ya maendeleo kwa mwaka
2013/2014 na mwelekeo wa shughuli za Serikali na
dira ya Bajeti ya Serikali katika mwaka 2014/2015.
7. Mheshimiwa Spika, naomba kuishukuru Kamati ya
Kudumu ya Baraza la Wawakilishi ya Mawasiliano na
Ujenzi chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Mahmoud
Mohamed Mussa, Mwakilishi wa Jimbo la Kikwajuni
kwa kazi nzuri na kubwa ya uchambuzi wa kina wa
5

Taarifa ya Utekelezaji wa Majukumu ya Sekta katika


mwaka 2013/2014 na Mapendekezo ya Mpango na
Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2014/2015. Pamoja na
kuipongeza Kamati kwa kazi nzuri, Wizara pia
itazingatia maoni na ushauri wa Kamati katika
kuimarisha utendaji wa Sekta ya Usafiri na
Mawasiliano nchini.
II: UTEKELEZAJI WA KAZI ZA KAWAIDA
NA MAENDELEO KWA MWAKA 2013/2014
NA MALENGO YA MWAKA 2014/2015
8. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo ya
awali, niruhusu sasa nifanye mapitio ya utekelezaji wa
kazi za kawaida na maendeleo za Wizara ya
Miundombinu na Mawasiliano kwa mwaka 2013/2014
na kutoa maelezo kuhusu Malengo na Makadirio ya
bajeti ya Wizara kwa mwaka 2014/2015. Utekelezaji
wa kazi za kawaida na maendeleo kwa mwaka
2013/2014 ulizingatia: Dira ya Taifa ya Maendeleo ya
mwaka 2020, Malengo ya Mkakati wa Kukuza Uchumi
na Kupunguza Umaskini (MKUZA II), ahadi na maagizo
ya Serikali, pamoja na Sera na Mipango ya Kisekta,
Kitaifa na Kimataifa.
9. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha
2013/2014 Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano
ilikadiriwa kutumia jumla ya TZS bilioni 5.192 kwa kazi
za kawaida. Kati ya fedha hizo TZS bilioni 3.26 ikiwa ni
6

mshahara na TZS bilioni 1.93 ni kwa ajili ya matumizi


mengineyo. Kwa upande wa kazi za maendeleo Wizara
ilipanga kutumia jumla ya TZS bilioni 14.90. Aidha,
Wizara ilipangiwa kukusanya jumla ya TZS milioni
406.2.
Hadi kufikia mwezi Machi 2014, fedha halisi
zilizopatikana ni TZS bilioni 3.362 kwa matumizi ya kazi
za kawaida, sawa na asilimia 64.75. Kati ya hizo TZS
bilioni 2.709 ni mshahara sawa na asilimia 83 na TZS
milioni 652.368 ni matumizi mengineyo sawa na
asilimia 33. Aidha, jumla ya TZS bilioni 4.376
zilipatikana kwa kazi za maendeleo sawa na asilimia
35.70 ya makadirio ya mwaka 2013/2014. Wizara pia,
ilikusanya jumla ya TZS milioni 314.248, sawa na
asilimia 77. (Kiambatanisho Namba 1).
10. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Miundombinu na
Mawasiliano inatekeleza majukumu yake ya kisekta
kupitia Idara, Mamlaka na Mashirika yaliomo ndani ya
Wizara, taasisi binafsi na baadhi ya taasisi za
Muungano kama ifuatavyo:i) Ofisi Kuu Pemba
ii) Utawala na Sera
Idara ya Mipango, Sera, na Utafiti,
Idara ya Uendeshaji na Utumishi.
iii) Sekta ya Usafiri wa Barabara
7

Idara ya Ujenzi na Utunzaji wa


Barabara,
Idara ya Usafiri na Leseni.
iv) Sekta ya Mawasiliano
Idara ya Mawasiliano.
v) Sekta ya Usafiri wa Anga:
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (ZAA),
vi) Sekta ya Usafiri wa Baharini
a. Mamlaka ya Usafiri Baharini (ZMA).
b. Shirika la Meli na Uwakala (SHIPCO).
c. Shirika la Bandari (ZPC).

IIa) OFISI KUU PEMBA


11. Mheshimiwa Spika, Ofisi Kuu Pemba inaratibu na
kusimamia shughuli za Wizara ya Miundombinu na
Mawasiliano kwa upande wa Pemba.
Katika kipindi cha 2013/2014 Ofisi Kuu Pemba
imeendelea kutekeleza kazi mbali mbali za uratibu wa
shughuli za Wizara kwa upande wa Pemba.
12. Mheshimiwa Spika, katika kipindi hicho Ofisi Kuu
Pemba ilikadiriwa kutumia jumla ya TZS bilioni 1.277
kwa kazi za kawaida na kukusanya jumla ya TZS
milioni 50.2 kutoka kwenye vianzio vyake vya mapato.
8

Kati ya fedha hizo TZS milioni 877 ni mshahara na TZS


milioni 400 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo.
Hadi Machi 2014 fedha zilizoingizwa ni TZS milioni
858.724 sawa na asilimia 67. Kati ya hizo TZS 733.06
sawa na asilimia 83.5 ni mshahara na TZS milioni
125.664 sawa na asilimia 31 ni kwa ajili ya matumizi
mengineyo. Ofisi Kuu Pemba imekusanya jumla ya TZS
milioni 44.550 sawa na asilimia 89.
MALENGO YA MWAKA 2014/2015
13. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2014/2015 Ofisi
Kuu Pemba itaendelea kuratibu na kusimamia kazi za
Wizara za kawaida na maendeleo kwa upande wa
Pemba. Malengo yote yanasimamiwa na Idara husika
na Ofisi Kuu Pemba inaratibu malengo hayo kwa kila
Idara. Katika kipindi hicho, Ofisi Kuu Pemba
inakadiriwa kukusanya jumla ya TZS milioni 62 na
inaombewa jumla ya TZS bilioni 1.362 kwa matumizi
ya kazi za kawaida. Kati ya hizo TZS bilioni 1.081 ni
mshahara na TZS milioni 280.78 ni matumizi
mengineyo.

IIb) UTAWALA NA SERA


14. Mheshimiwa Spika, Kazi za uratibu wa Sera,
Mipango na Miradi ya Maendeleo ya Wizara ya
Miundombinu na Mawasiliano zinasimamiwa na Idara
9

ya Mipango, Sera na Utafiti. Aidha, masuala ya


uendeshaji, utumishi na utawala hutekelezwa kupitia
Idara ya Uendeshaji na Utumishi.

(i) IDARA YA MIPANGO, SERA NA UTAFITI


15. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2013/2014
Idara ya Mipango, Sera na Utafiti iliendelea na kazi za
uratibu na kusimamia utekelezaji wa Sera na Mipango
ya sekta ya Usafiri na Mawasiliano ikiwemo kubuni,
kutayarisha na kufuatilia utekelezaji wa miradi ya
maendeleo na kufanya maandalizi ya utafiti wa kisekta.
HATUA ZA UTEKELEZAJI (2013/2014)
16. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha 2013/2014,
Idara iliendelea kuratibu na kusimamia utekelezaji wa
Sera ya Usafiri Zanzibar, Sera ya Mawasiliano pamoja
na Mpango Mkuu wa Taifa wa Usafiri wa Zanzibar
(Zanzibar Transport Master Plan).
Idara kupitia programu ya mageuzi ya mfumo wa
taasisi inayoendelea inakamilisha Mpango wa
utekelezaji wa mageuzi ya taasisi za Wizara ikihusisha
maandalizi ya Mpango wa Uendeshaji Kibiashara
(Business Plans) kwa kila Taasisi itakayohusika na
mageuzi hayo pamoja na Sheria zinazohusiana na
taasisi hizo.
10

Idara pia, imeratibu na kufuatilia taratibu za


uanzishwaji wa vyuo vya ubaharia na urubani. Kwa
upande wa uanzishwaji wa chuo cha ubaharia, Wizara
imefanya mazungumzo na kampuni ya Rom Solution
ambayo imewasilisha mapendekezo ya mradi wa
uanzishwaji wa Chuo cha Ubaharia kwa kuanzia na
Upembuzi yakinifu ikiwemo uhakiki wa kisheria,
kuandaa malengo ya muda mfupi na muda mrefu,
kuandaa mpango wa mafunzo na mitaala pamoja na
kuandaa mahitaji ya majengo ya Chuo hicho.

(i-1) MIRADI YA MAENDELEO


17. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa uratibu na
usimamizi wa miradi ya maendeleo, jumla ya Miradi ya
Maendeleo 14 ya ujenzi wa miundombinu ya barabara,
viwanja vya ndege na bandari pamoja na mradi wa
Mageuzi ya mfumo wa taasisi (Kiambatanisho
Namba 2) imetekelezwa kama ifuatavyo:(i-1.1) MIRADI YA UJENZI WA BARABARA
18. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia programu ya
ujenzi wa barabara, iliendelea kutekeleza jumla ya
miradi saba (7) ya ujenzi wa barabara katika kipindi
cha 2013/2014. Taarifa za utekelezaji wa miradi hiyo
kwa kipindi kilichopita na fedha inazoombewa kwa
mwaka 2014/15 ni kama ifuatavyo:
11

(i-1.1.1) Mradi wa Barabara Tatu za Kaskazini


Pemba
19. Mheshimiwa Spika, Mradi huu unaogharamiwa
kwa mkopo kutoka Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo
ya Afrika (BADEA) na Mfuko wa Maendeleo wa Saudi
Arabia (Saudi Fund) pamoja na fedha za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar unazihusisha barabara za Wete
Konde (kilomita 15) na Wete Gando (kilomita 15)
kwa awamu ya kwanza umefikia hatua mbali mbali za
kifusi.
Mheshimiwa Spika, Mradi huu ulisita kwa muda
kutokana na Mkandarasi kusimamisha ujenzi kwa
sababu ya kuchelewa kulipwa na Wafadhili na Serikali.
Hata hivyo, baada ya Wizara kufuatilia kwa kina
Mkandarasi alilipwa jumla ya Dola za Kimarekani
milioni 2.74 ikiwa ni malipo kutoka kwa Wafadhili.
Kwa upande wa Serikali, Mkandarasi huyo amelipwa
deni lake lote la TZS bilioni 2.855 alilokuwa akidai kwa
barabara hizi kwa kipindi cha Julai hadi Septemba
2013. Kwa ujumla Mkandarasi amelipwa jumla ya TZS
bilioni 6.079 hadi kufikia mwezi Septemba 2013. Aidha,
Mkandarasi amelipwa USD milioni 3 alizokuwa akidai
Serikali kwa mradi wa ujenzi wa barabara ya Amani Dunga, Mfenesini - Bumbwini na Madaraja ya barabara
ya Mahonda - Donge - Mkokotoni.
12

Baada ya kufanyika malipo hayo, Mkandarasi alikubali


kuendelea na kazi za ujenzi na kuanza kazi rasmi
mwezi wa Aprili 2014. Kwa sasa kazi za ujenzi wa
barabara hizo zinaendelea vizuri na kutarajiwa
kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.
20. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2014/2015 mradi unaombewa jumla ya TZS bilioni
2.425 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu.

(i-1.1.2) Mradi wa Barabara ya Wete-Chake


21. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara hii yenye
urefu wa kilometa 22 umepangwa kufanyika katika
awamu ya pili ya Mradi wa Barabara Tatu za Kaskazini
Pemba ambapo jumla ya USD milioni 23 zinatarajiwa
kutumika. Tayari Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania imeshatiliana saini ya mkopo wa USD milioni
10 na benki ya BADEA kwa ajili ya ujenzi wa barabara
hii. Juhudi za kukamilisha taratibu za kusaini mkopo
wa USD milioni 10 na Mfadhili wa pili (SAUDI Fund)
zinaendelea.
22. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha
2014/2015 Wizara inakusudia kuanza taratibu za
kumpata Mshauri wa kufanya mapitio ya usanifu wa
barabara na usimamizi wa ujenzi baada ya kukamilika
kwa taratibu za mkopo kutoka Saudi Fund. Jumla ya
TZS milioni 100 zinaombwa kwa ajili ya malipo ya fidia.
13

(i-1.1.3) Mradi wa Barabara ya Ole-Kengeja


23. Mheshimiwa Spika, Mradi wa Barabara ya OleKengeja unagharamiwa kwa mkopo kutoka Jumuiya ya
Nchi zinazosafirisha Mafuta kwa Wingi Duniani (OPEC)
na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar una lengo la
kuijenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia
Ole hadi Kengeja yenye urefu wa kilomita 35. Hatua za
kumpata Msimamizi wa Mradi zimekamilika na kazi ya
upimaji wa barabara hiyo zimeanza ambapo jumla ya
kilomita saba (7km) zimeshapimwa na taratibu za
manunuzi ya zana za ujenzi zinaendelea kupitia fedha
za Mfadhili. Jumla ya TZS milioni 20 zimepatikana
kutoka Serikalini kwa mwaka wa fedha 2013/2014.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Serikali inakusudia
kuendelea na matayarisho ya ujenzi wa barabara hii na
jumla ya TZS milioni 500 zinaombwa kwa ajili ya
malipo ya fidia.

(i-1.1.4) Mradi wa Barabara za Vijijini Kaskazini


Pemba:
24. Mheshimiwa Spika, Mradi huu uliogharamiwa kwa
kutumia ruzuku kutoka Serikali ya Marekani kupitia
Mfuko wa Changamoto ya Milenia (MCC) na fedha za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ulikuwa na lengo la
kujenga kwa kiwango cha lami barabara 5 za Kaskazini
Pemba zenye jumla ya kilometa 35. Mradi huo ambao
ulihusisha barabara za: Mzambarauni-Pandani-Finya
14

(kilometa 7.9), Bahanasa-Daya-Mtwambwe (kilometa


13.6), Chwale-Kojani (kilometa 1.9), KipanganiKangagani (kilometa 8.9) na Mzambarauni-Mapofu
(kilometa 8.9) umekamilika na kuzinduliwa rasmi
mwezi Machi mwaka huu. Hadi kufikia mwezi Machi
2014, jumla ya TZS milioni 40 zimepatikana sawa na
asilimia 27 ya makadirio.

(i-1.1.5) Mradi wa Barabara Zinazoingia Mjini


Unguja
25. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ambao
bado haujapata mfadhili ni kuzitanua na kuzifanyia
matengenezo makubwa barabara 7 zenye urefu wa
kilometa 83 zinazoingia katika mji wa Zanzibar.
Barabara zenyewe ni Bububu-Mtoni-Kinazini-Malindi
Port (kilometa 19), Creek road-Mkunazini-Mnazi Mmoja
(kilometa 1.28), Tunguu-Fuoni-Magomeni-KariakooMkunazini (kilometa 13.3), Welezo-Amani-NgamboKariakoo (kilometa 3.5), Mtoni-Amani-Kiembesamaki
(kilometa 8.5), Uwanja wa Ndege-Kiembe SamakiKilimani-Mnazi Mmoja (kilometa 7) na BububuMahonda-Mkokotoni (kilometa 31). Juhudi za kutafuta
fedha za ujenzi wa barabara hizi zinaendelea na hadi
kufikia mwezi Machi 2014 hakuna fedha iliyopatikana
kutoka kwa Wafadhili kwa ajili ya mradi huo.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015, Wizara itaendelea
na juhudi za kutafuta fedha kwa njia ya msaada au
mkopo kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili
15

ya utekelezaji wa mradi na unaombewa jumla ya TZS


50 milioni.

(i-1.1.6) Mradi wa Barabara 3 za Vijijini Unguja


26. Mheshimiwa Spika, mradi huu unaoendelea
unagharamiwa kwa mkopo kutoka Benki ya Kiarabu ya
Maendeleo ya Afrika (BADEA) na fedha za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar unazijumuisha barabara za
Kizimbani-Kiboje (kilometa 7.2); Koani-Jumbi (kilometa
6.3); na Jendele-Cheju-Kaebona (kilometa 11.7). Hadi
kufikia mwezi wa Machi 2014, jumla ya TZS milioni 405
zimepatikana
ambapo
jumla
kilometa
11.7
zimeshawekwa kifusi cha tabaka la chini kwa barabara
ya Jendele-Cheju-Kaebona na kilometa 4.2 za barabara
ya Koani Jumbi zimesafishwa. Pamoja na
changamoto za ulipaji fidia mradi unatarajiwa
kukamilika mwishoni mwa mwaka huu kwa mujibu wa
mkataba.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015, Wizara inakusudia
kuendelea na utekelezaji wa mradi huu na unaombewa
jumla ya TZS 1.6 bilioni kwa ajili ya malipo ya fidia na
mchango wa Serikali.

(i-1.1.7) Mradi wa Barabara 6 za Vijijini Unguja


27. Mheshimiwa Spika, mradi huu una lengo la
kufanya upembuzi yakinifu, usanifu na utayarishaji wa
zabuni wa barabara 6 za vijijini Unguja zenye urefu wa
16

kilometa 62.6 unagharimiwa kwa mkopo kutoka Benki


ya Maendeleo ya Afrika (AfDB). Barabara hizo ni:
Matemwe-Muyuni (kilometa 7), Kichwele-Pangeni
(kilometa 4.8), Njianne-Umbuji-Uroa (kilometa 11),
Jozani-Charawe-Ukongoroni-Bwejuu (kilometa 22.2),
Fuoni-Kombeni (kilometa 8.5), na Mkwajuni-Kijini
(kilometa 9.1). Hatua za utekelezaji wa mradi huu ni
kukamilika kwa uchambuzi yakinifu wa awali wa mradi
huu.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015, Wizara itakamilisha
upembuzi yakinifu na matayarisho ya zabuni za mradi
huo kwa kutumia fedha za Mfadhili.
28. Mheshimiwa Spika, kwa jumla, kwa mwaka wa
fedha 2014/2015 Wizara itaendelea na utekelezaji wa
miradi niliyokwishakuieleza kwenye sekta ya usafiri wa
barabara ambapo jumla ya TZS bilioni 4.975
zinaombwa kutoka Serikalini. (Kiambatanisho
Namba 2)
(i-1.2) MIRADI YA SEKTA YA USAFIRI WA
ANGA
29. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa sekta ya
usafiri wa anga Wizara ilipanga kutekeleza jumla ya
miradi 4 ya ujenzi wa miundombinu ya viwanja vya
ndege vya Unguja na Pemba katika mwaka 2013/2014.
Utekelezaji wa miradi hiyo kwa kipindi kilichopita na
17

fedha zinazoombwa kwa mwaka ujao wa fedha ziko


kama ifuatavyo:-

(i-1.2.1) Uendelezaji Ujenzi wa Uzio.


30. Mheshimiwa Spika, Mradi huu unalengo la kujenga
uzio wenye urefu wa kilometa 11.9 katika kiwanja cha
ndege cha kimataifa cha Abeid Amani Karume. Hadi
kufikia mwezi Machi, 2014 jumla ya kilometa 8.59 za
uzio zimeshajengwa sawa na asilimia 73.5 ya lengo.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Wizara inakusudia
kuendelea na mradi huu kwa kutumia fedha za
maendeleo.

(i-1.2.2) Ujenzi wa Jengo Jipya la Abiria


Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid
Amani Karume
31. Mheshimiwa Spika, Baada ya mradi huu kusita
kwa muda, mnamo mwezi wa Juni 2013 Wizara ya
Miundombinu na Mawasiliano ilitoa ruhusa kwa
mkandarasi kuendelea na ujenzi kwa kuzingatia
marekebisho yalioyopendekezwa na Mshauri Mwelekezi
kampuni ya ADPi ya Ufaransa. Marekebisho hayo
yatabadilisha mfumo wa uegeshaji wa ndege kubwa
kutoka mbele ya jengo (airside) na badala yake
kuegesha upande wa kusini ya jengo, kuongeza
ukubwa wa jengo kutoka mita za mraba 17,800 hadi
23,000, kuongeza eneo la kuegeshea ndege kutoka
18

mita za mraba 23,000 hadi mita za mraba 37,300,


kuongeza urefu wa jengo kwa upande wa kusini kwa
mita 36 na upana mita 75 na kuongeza sehemu ya
mbele (lobby) ya jengo kwa mita 18.
32. Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu Baraza lako
tukufu kuwa kazi za ujenzi wa jengo jipya zinaendelea
kwa kukamilisha uwekaji wa vyuma (steel structure)
eneo liloongezeka upande wa kusini na sehemu ya
mbele (canopy/lobby). Kwa eneo liloongezeka kwa
upande wa kusini tayari limefikia asilimia 75. Ujenzi
wa sehemu ya mbele (canopy/lobby) tayari imefikia
asilimia 80. Pia ujenzi wa ngazi za jengo unaendelea
kwa kuchimba misingi kulingana na marekebisho ya
michoro.
33. Mheshimiwa Spika, Mkandarasi pia anaendelea
kukamilisha ujenzi wa makazi na ofisi mpya ambayo
iko katika hatua za mwisho ambapo baadhi ya maeneo
tayari yanatumika. Aidha vifaa vya ujenzi kama kokoto,
saruji na nondo kwa ajili ya kuweka zege ya ghorofa
ya kwanza ya jengo zimefika kwenye eneo la ujenzi.
Pia kazi ya kufunga nondo kwenye ghorofa ya pili
zimeanza kwa mataarisho ya kuweka zege.
34. Mheshimiwa Spika, kuhusu kazi za ukamilishaji na
uthibitishaji wa michoro (Usanifu na Uhandisi), Mshauri
Mwelekezi anaendelea kupitia michoro iliyowasilishwa
na inayosubiri kuthibitishwa na Wizara kwa mfano,
19

mfumo wa uingiaji na utokaji wa abiria, mizigo,


wafanyakazi pamoja na utoaji wa takataka ndani ya
jengo. Pia, ADPi wamekamilisha kupitia michoro mbali
mbali ikiwemo ya Usanifu (architectural drawings),
Uhandisi (Engineering Drawings) Plumbing drawings
and michoro ya mfumo wa vipoza joto (Heat,
ventilation and Air Condition). Mkandarasi pia
amewasilisha marekebisho ya mpangilio wa matumizi
ya vyumba vya jengo na ripoti ya usalama wa moto
(fire safety report). Taarifa zote hizi kwa sasa
zinapitiwa na Mshauri Mwelekezi kabla ya kuishauri
Wizara ili kuthibitishwa.
35. Mheshimiwa Spika, Naomba pia ifahamike
kwamba awamu hii ya uthibitishaji michoro, haimzui
Mkandarasi kuendelea na kazi za Ujenzi, kwa maana
hatua hii ya kuendelea na marekebisho ya michoro ni
suala la kawaida katika taratibu za Ujenzi. Ni matarajio
ya Serikali kwamba Mradi huo utakamilika kabla ya
mwisho wa mwaka 2015.
36. Mheshimiwa Spika, Hadi kufikia mwezi Machi 2014
jumla ya TZS milioni 807.798 zimepatikana sawa na
asilimia 59 ya makadirio.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Mradi unaombewa
jumla ya TZS bilioni 1.950 kwa ajili ya huduma ya
Ushauri na Usimamizi wa Mradi.

20

(i-1.2.3) Ujenzi wa Maegesho na Njia ya


Kupitia Ndege uwanja wa ndege wa
Kimataifa.
37. Mheshimiwa Spika, Mradi huu una lengo la
kujenga sehemu ya maegesho ya ndege (apron) na
kuimarisha njia za kupitia ndege (taxiways) katika
Kiwanja cha Ndege cha kimataifa cha Abeid Amani
Karume. Mradi huu unagharamiwa kwa mkopo
kutoka Benki ya Dunia na fedha za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar. Hadi kufikia mwezi Machi
2014, ujenzi wa njia tatu za kupitia ndege
umekamilika na ujenzi wa njia mbili mpya
unaendelea na uimarishaji wa njia moja. Aidha, kazi
za uwekaji wa kifusi na lami kwenye eneo jipya la
maegesho ya ndege zinaendelea na jumla ya TZS
milioni 75 zilipatikana kutoka Serikalini sawa na
asilimia 3 ya makadirio.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 jumla ya TZS
milioni 975 zinaombwa kwa ajili ya kugharamia ujenzi
wa uzio.

(i-1.2.4) Uimarishaji wa huduma


Uwanja wa Ndege Pemba

za

38. Mheshimiwa
Spika,
Mradi
huu
unagharamiwa na Serikali ya Mapinduzi pekee na
una lengo la kuweka taa katika barabara ya
kurukia na kutulia ndege na kufanya upembuzi
yakinifu na usanifu wa huduma mbali mbali katika
21

kiwanja hicho. Hadi kufikia mwezi Machi 2014,


hakuna kazi iliyofanyika kutokana na ukosefu wa
fedha. Katika kulipatia ufumbuzi wa kudumu suala
la uimarishaji wa Kiwanja hicho, Serikali imefanya
maamuzi rasmi ya kutekeleza Mradi huo kwa njia
ya mkopo kutoka Benki ya Exim ya Uturuki kupitia
Kampuni ya Renaisance ya
nchi hiyo.
Makubaliano ya awali ya kazi yalifanyika mwishoni
mwa mwaka 2013 baina ya Serikali kupitia Wizara
ya Fedha na Kampuni ya Renaisance ya Uturuki.
Baada ya makubaliano hayo kampuni hiyo ilipeleka
wataalamu wake Pemba kwa ajili ya kupata taarifa
zaidi ya uwanja huo. Rasimu ya Upembuzi Yakinifu
wa Kifedha na Kimazingira imekamilishwa na
kuwasilishwa Wizarani kwa ajili ya kupata maoni
ya kitaalamu. Aidha, gharama za awali kwa ajili ya
kazi za ujenzi zimewasilishwa na zinaendelea
kufanyiwa mapitio ya kina.
39. Mheshimiwa Spika, Uimarishaji wa uwanja
huo utajumuisha jengo jipya la abiria, kuongeza
urefu wa njia ya kutulia na kurukia ndege kutoka
mita 1,500 hadi mita 2,300, ujenzi wa uzio
kuzunguka uwanja mzima, uwekaji wa taa za
kuongozea ndege wakati wa kuruka na kutua,
kulikarabati jengo la abiria liliopo pamoja na
huduma nyengine za kiwanja hicho. Lengo la
ongezeko hilo ni kukiwezesha Kiwanja hicho
kuweza kutua ndege kubwa zaidi ya sasa ikiwemo
Boeing 737 200.
22

40. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha


2014/2015 Wizara inakusudia kuendelea na
utekelezaji wa mradi huu kwa mkopo kupitia Benki
ya Exim ya Uturuki.
41. Mheshimiwa Spika, kwa ujumla kwa mwaka
wa fedha 2014/2015 Wizara inakusudia kuendelea
na utekelezaji wa miradi ya usafiri wa Anga na
jumla ya TZS bilioni 2.925 zinaombwa kutoka
Serikalini (Kiambatanisho Namba 2)

MRADI WA
MPIGADURI

UJENZI

WA

BANDARI

YA

42. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa


uimarishaji miundombinu ya bandari, Wizara tayari
imekamilisha kazi ya Upembuzi Yakinifu ya Ujenzi
wa Bandari mpya ya Mpigaduri. Aidha Wizara
imetiliana saini makubaliano ya ujenzi wa Bandari
hiyo kati yake na Kampuni ya China Harbour
Engineering Company (CHEC) baada ya kukamilika
kwa kazi za Upembuzi Yakinifu. Aidha, Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania tayari imewasilisha
rasmi maombi ya mkopo wa ujenzi wa Bandari
hiyo kutoka Benki ya Exim ya China kupitia Serikali
ya nchi hiyo.

23

Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Jumla ya TZS


milioni 500 zinaombwa kwa ajili ya utekelezaji wa
mradi huo.
MRADI WA UJENZI WA MELI MPYA YA
ABIRIA NA MIZIGO YA SERIKALI.
43. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wa ahadi ya
Serikali ya kujenga meli mpya ya abiria na mizigo
kupitia bajeti yake wenyewe unaendelea. Katika
utekelezaji wa ahadi hiyo, mnamo tarehe 10
Julai, 2013 Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
ilitiliana saini na Kampuni ya DAEWOO
International ya Korea Kusini ya ujenzi wa meli
hiyo. Napenda kuchukua fursa hii kuliarifu Baraza
lako Tukufu kwamba ujenzi wa meli hiyo
unaendelea kwa kukamilisha kazi za usanifu na
uandaaji wa michoro ya meli hiyo. Aidha, zoezi la
ukataji wa vyuma vya meli hiyo (steel cutting)
zimezinduliwa rasmi mwezi Machi 2014 na kazi za
ulazaji wa mkuku (keel laying) zinatarajiwa
kufanyika ifikapo mwezi Julai 2014 baada ya
kukamilika kwa kazi za usanifu. Ni matumaini yetu
kuwa ujenzi wa meli hiyo utakamilika mapema
mwaka 2015 kwa mujibu wa ratiba ya ujenzi wa
meli hiyo.
44. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014
Idara ya Mipango, Sera na Utafiti ilipangiwa
kutumia jumla ya TZS milioni 288 kwa matumizi
24

ya kazi za kawaida. Hadi Machi 2014, fedha


zilizopatikana kwa kazi za kawaida ni TZS 83.137
sawa na asilimia 29 ya makadirio.
MALENGO YA MWAKA 2014/2015
45. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2014/2015,
Idara ya Mipango, Sera na Utafiti itaratibu na
kutekeleza mambo yafuatayo: Maandalizi ya Sheria, Kanuni na Mpango
Mkakati wa utekelezaji wa Sera ya TEHAMA;
Kufanya tafiti mbali mbali zinazohusiana
na sekta ya usafiri na mawasiliano kwa
lengo la kuongeza ufanisi na tija katika
kazi za ujenzi wa miundombinu;
Kuratibu na kusimamia mpango wa
Serikali wa kuanzisha Chuo cha Ubaharia
na Urubani;
Kukusanya na kuchambua takwimu za
maendeleo ya Sekta na kuweka mpango
bora wa utunzaji wa kumbukumbu;
Kuratibu mashirikiano ya kisekta baina ya
taasisi za ndani, kikanda na nje ya nchi.
46. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka 2014/2015
Idara ya Mipango, Sera na Utafiti inaombewa
jumla ya TZS milioni 200 kwa matumizi ya kazi za
kawaida.
25

(ii)
IDARA
UENDESHAJI

YA

UTUMISHI

NA

47. Mheshimiwa Spika, Idara ya Uendeshaji na


Utumishi inajukumu la kutekeleza kazi zifuatazo: Kusimamia na kuratibu majukumu ya
kiutumishi ikiwemo ajira, na upandishaji wa
vyeo kwa watumishi wa Wizara.
Kuwaendeleza wafanyakazi wa Wizara kwa
kuwajengea uwezo kielimu na kusimamia
maslahi yao.
Kusimamia na kuhakikisha kuwa sheria ya
utumishi wa Umma na sheria ya manunuzi
na uondoshaji wa mali chakavu za Serikali
zinasimamiwa vizuri na zinafuatwa.
Kusimamia shughuli za uendeshaji wa kazi
za ofisi za kila siku kwa kuimarisha mazingira
mazuri ya utendaji wa kazi kwa kuhakikisha
vitendea kazi vinapatikana kwa wakati.
Kusimamia na kuimarisha mawasiliano ya
habari na ofisi nyingine.
48. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha
2013/2014 Idara imetekeleza na kusimamia
masuala ya kiutumishi na uendeshaji ya Wizara
kwa ujumla. Idara imewapatia mafunzo mbali
mbali jumla ya wafanyakazi 94. Kati ya hao,
wafanyakazi 48 walipatiwa mafunzo ya muda
26

mrefu na wafanyakazi 46 walipatiwa mafunzo


ndani ya muda mfupi. (Kiambatanisho Namba
3). Aidha, Wizara iliajiri wafanyakazi wapya 42
pamoja na kustaafisha wafanyakazi 34 na
kuwapatia mafao yao.
Idara pia, kwa kushirikiana na Wizara ya Kazi na
Utumishi wa Umma imewapandisha vyeo
wafanyakazi
wote
wanaostahili
ikihusisha
wafanyakazi wenye uzoefu wa muda mrefu na
kuhakikisha kuwa wanalipwa mishahara yao kwa
mujibu wa mabadiliko ya mishahara ya watumishi
kama yalivyotolewa na Serikali mwezi Februari
2014.
Vile vile, Wizara kupitia Idara
kusimamia ujenzi wa Jengo
ukarabati wa majengo mengine
eneo la Kisauni ambayo hivi
kama Makao Makuu ya Wizara.

hii imeratibu na
Jipya moja na
manne (4) katika
sasa yanatumika

49. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha


2013/2014 Idara ya Uendeshaji na Utumishi
ilipangiwa kutumia jumla ya TZS milioni 501.4 kwa
matumizi ya kazi za kawaida na jumla ya TZS
bilioni 2.082 kwa mishahara ya watumishi wote wa
Wizara. Fedha halisi zilizotolewa katika kipindi cha
Julai 2013 hadi Machi 2014 ni TZS milioni 217.946
sawa na asilimia 43.47 kwa matumizi ya kawaida
27

na TZS bilioni 1.798 sawa na asilimia 86 kwa


matumizi ya mishahara.
MALENGO KWA MWAKA 2014/2015
50. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2014/2015
Idara itaendelea kutekeleza majukumu yake ya
uendeshaji
wa ofisi na utumishi kama
ilivyopangiwa. Aidha, Wizara kupitia Idara hii
itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Rais Kazi na
Utumishi wa Umma kuratibu maelekezo na
miongozo yote kuhusiana na masuala ya
kiutumishi kama yatakavyotolewa.
51. Mheshimiwa Spika, ili kuongeza ujuzi,
ufanisi na tija kwa wafanyakazi wa Wizara, katika
mwaka 2014/2015 Idara imepanga kuwapatia
mafunzo jumla ya wafanyakazi 12 kwa Unguja na
wafanyakazi 9 kwa Pemba kwa mujibu wa
mpango wa mafunzo wa Wizara.
Katika mwaka 2014/2015, Idara ya Uendeshaji na
Utumishi inaombewa jumla ya TZS milioni 376.936
kwa matumizi ya kazi za kawaida na TZS milioni
2.892 kwa mishahara ya wafanyakazi wa Wizara.

IIc. SEKTA YA USAFIRI WA NCHI KAVU.


52. Mheshimiwa Spika, Sekta ya Usafiri wa Nchi
Kavu ni muhimu katika kuchangia ukuaji wa
28

uchumi wa nchi yetu na ustawi wa jamii kwa


kusafirisha wananchi mijini na vijijini na bidhaa za
wakulima.
Katika kipindi cha mwaka 2013/2014, Wizara ya
Miundombinu na Mawasiliano kupitia Idara ya
Ujenzi na Utunzaji Barabara na Idara ya Usafiri na
Leseni imeendelea kuimarisha miundombinu ya
barabara na huduma za usafiri wa barabara kwa
kuendeleza kazi za ujenzi na utunzaji wa barabara,
madaraja na kusimamia masuala ya usalama
barabarani.

(i) IDARA YA UJENZI NA UTUNZAJI WA


BARABARA

53. Mheshimiwa Spika, kazi za ujenzi na utunzaji


wa barabara zinafanywa kupitia Idara ya Ujenzi na
Utunzaji Barabara. Hadi kufikia mwezi Machi 2014
Wizara kupitia Idara hii imezifanyia matengenezo
barabara mbali mbali mijini na vijijini (Unguja na
Pemba) na kufanya usafi wa barabara za lami
kadhaa
zenye
urefu
wa
kilometa
249
(Kiambatanisho Namba 4) kwa kutumia fedha
zinazotolewa na Mfuko wa Barabara chini ya
Makubaliano Maalum ya Utekelezaji (Performance
Agreement) kati ya Wizara na Mfuko huo.
54. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha
2013/2014, Idara ya Ujenzi na Utunzaji wa
29

Barabara ilipangiwa kukusanya jumla ya TZS


milioni 10 kutokana na mapato mengineyo na
ilitengewa jumla ya TZS milioni 250 kwa ajili ya
matumizi ya kazi za kawaida. Hadi Machi 2014
jumla ya TZS milioni 3.48 zimekusanywa ambazo
ni sawa na asilimia 35 na fedha zilizotolewa kwa
kazi za kawaida ni TZS milioni 81.28 sawa na
asilimia 33 ya makadirio.

MATENGENEZO YA BARABARA
55. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha
2013/2014,
Wizara
kupitia
programu
ya
matengenezo ya barabara, iliendelea kutekeleza
jumla ya miradi 5 ya ujenzi wa barabara kwa
kutumia bajeti ya Serikali pekee. Kwa mwaka
2014/2015 Wizara inakusudia kuendeleza miradi
hiyo kama ifuatavyo:-

(i) Barabara ya Mgagadu - Kiwani


56. Mheshimiwa
Spika,
Mradi
huu
unagharamiwa na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar na una lengo la kuijenga barabara ya
Mgagadu-Kiwani yenye jumla ya kilometa 7.6.
Hadi kufikia mwezi Machi 2014 jumla ya kilometa
7.6 zimekamilika kwa hatua ya kifusi tabaka mbali
mbali. Kutokana na kutopatikana kwa fedha za
30

Mradi kutoka Serikalini, Wizara ilifanya juhudi ya


kupata fedha kupitia Mfuko wa Barabara kwa ajili
ya ujenzi wa daraja katika kijiji cha Mbaoni.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015, Mradi
unaombewa jumla ya TZS milioni 300 kwa ajili ya
kuendelea na kazi za ujenzi wa barabara hii.

(ii) Barabara ya Mkanyageni-Kangani


57. Mheshimiwa Spika, Mradi huu una lengo
la kuijenga barabara inayoanzia Mkanyageni
hadi Kangani yenye urefu wa kilomita 6.5 kwa
kiwango cha lami. Mradi huu mwanzoni
ulipangwa kutekelezwa baada ya kukamilika
kwa
barabara
ya
Mgagadu-Kiwani
na
unagharamiwa na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar. Hata hivyo, kwa mwaka huu wa
fedha Wizara imepanga kujenga daraja moja la
tasini ambapo jumla ya TZS milioni 180
zimetengwa kupitia Mfuko wa Barabara. Aidha
ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha kifusi
utafanywa
kupitia
mradi
wa
MIVARF
unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika
(ADB) kupitia Wizara ya Kilimo unaotarajiwa
kuanza robo ya kwanza ya mwaka 2014/2015.

31

(iii) Barabara ya Amani-Mtoni (Benjamin


Mkapa)
Mheshimiwa Spika, huu ni mradi
unaoendelea
ambapo
Wizara
ilipanga
kukamilisha ujenzi wa sehemu ya pili ya
barabara hiyo yenye jumla ya urefu wa
kilometa 2.4 kwa kiwango cha lami, ujenzi wa
mtaro wa maji ya mvua mita 200, kalvati ndogo
ndogo 6 na kulipia fidia za nyumba kwa ajili ya
kuruhusu ujenzi wa barabara hiyo.

58.

Hadi kufikia mwezi Machi 2014 ujenzi wa kilometa


1.6 kwa kiwango cha lami umekamilika. Aidha,
kazi za ujenzi wa mtaro kwa mawe na saruji
wenye urefu wa mita 120, ujenzi wa kalvati ndogo
mbili (2) pamoja na ujenzi wa kingo za zege
(curbstones) zenye urefu wa kilometa 1.4
zimefanyika.
Kutokana na uhaba wa fedha za kulipia fidia,
ujenzi wa barabara hii ulisita kwa sababu ya
kutolipwa fidia ya nyumba eneo lenye urefu wa
kilometa 0.8 ili kukamilisha ujenzi wa barabara
yote. Hata hivyo, Wizara inaendelea na taratibu za
malipo ya fidia ya eneo hilo baada ya kupata
fedha kupitia Mfuko wa Barabara ili kuruhusu kazi
za ujenzi kuendelea. Kazi za ujenzi wa barabara hii
32

unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Oktoba


2014.
59. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha
2014/2015 Wizara inakusudia kukamilisha ujenzi
wa sehemu ya barabara iliyobakia kwa kutumia
fedha za Mfuko wa Barabara.

(iv) Barabara ya Ole-Konde.


60. Mheshimiwa Spika, Mradi huu mpya una
lengo la kuifanyia matengenezo ya muda maalum
(Periodic maintenance) barabara inayoanzia
Melitano hadi Madenjani kwa urefu wa kilometa
12.3.
Hadi kufikia mwezi Machi 2014 taratibu za
kumpata Mkandarasi atakaefanya kazi hiyo
zinaendelea kufanyika.
61. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2014/2015 Wizara inakusudia kutekeleza mradi
huu kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara.

(v) Barabara ya Njianne-Umbuji


62. Mheshimiwa Spika, Mradi huu una lengo la
kuifanyia matengenezo ya muda maalum (Periodic
maintenance) kwa kiwango cha lami barabara
inayoanzia Njianne hadi Umbuji yenye urefu wa
33

kilometa 5. Hadi kufikia mwezi wa Machi 2014


jumla ya kilometa 3 za barabara hiyo zimejengwa
kwa kifusi.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Wizara
itaendelea kutekeleza mradi huu kwa kutumia
fedha za Mfuko wa Barabara.
MALENGO YA IDARA (2014/2015)
63. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha
2014/2015
Idara
itaendelea
kuzifanyia
matengenezo barabara mbali mbali zenye jumla
ya urefu wa kilometa 697 Unguja na Pemba ili
ziendelee kutumika kwa wakati wote kwa kutumia
fedha za Mfuko wa Barabara. (Kiambatanisho
Namba 4).
Idara inatarajia kukusanya jumla ya TZS
10,000,000 na inaombewa jumla ya TZS milioni
165.488 kwa matumizi ya kazi za kawaida.

(ii) IDARA YA USAFIRI NA LESENI


64. Mheshimiwa Spika, Idara hii inasimamia
usalama wa watumiaji wote wa barabara,
kuendesha shughuli za ukaguzi wa vyombo vya
moto, kusimamia mafunzo ya udereva, upasishaji
madereva wanafunzi na walimu wa skuli za
34

udereva, utoaji huduma za usafirishaji abiria na


mizigo kwa njia ya barabara pamoja na kutoa
vitambulisho vya utingo na madereva. Aidha,
Idara inasimamia na kuendesha Karakana Kuu ya
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliyoko Chumbuni
na sehemu ya mitambo iliyoko Pemba.
HATUA ZA UTEKELEZAJI (2013/2014)
65. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Idara hii
imeendelea kusimamia utekelezaji wa Kanuni
mbali mbali za Sheria ya Usafiri Barabarani ya
mwaka 2003 ili kusaidia kuimarisha usalama wa
usafiri barabarani kwa kufanya ukaguzi wa
vyombo vya moto na kutoa leseni za usafirishaji.
66. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwezi wa
Machi
2014
jumla
ya
vyombo
27,731
vimekaguliwa ukilinganisha na vyombo 28,067
vilivyokaguliwa katika kipindi cha mwaka
2012/2013. Aidha, ruhusa za usafirishaji kwa njia
ya barabara ziliendelea kutolewa ambapo katika
kipindi hicho Idara imetoa ruhusa za njia na
usafirishaji 1,896 kwa magari ya biashara mbali
mbali Unguja na Pemba ukilinganisha na ruhusa
2,015 zilizotolewa katika kipindi cha Julai 2012
hadi Machi 2013 ikiwa ni pungufu ya aslimia 5.9.

35

67. Mheshimiwa Spika, katika kipindi hicho Idara


imewafanyia jumla ya madereva wanafunzi 5,721
mitihani ya nadharia na vitendo na kutoa leseni za
madereva wanafunzi 7,218. (Kiambatanisho
Namba 5) Idara pia, imeendesha vipindi mbali
mbali kuhusiana na usalama barabarani (elimu
kwa umma) kwa kutumia vyombo vya habari.
68. Mheshimiwa Spika, Idadi ya magari
yaliofanyiwa matengenezo katika Karakana Kuu na
Sehemu ya Mitambo Pemba iliongezeka kwa
asilimia 40. Jumla ya magari 628 yalifanyiwa
matengenezo katika kipindi cha Julai 2013 hadi
Machi 2014 ukilinganisha na magari 447
yaliofanyiwa
matengenezo
katika
kipindi
kilichopita.
69. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha
2013/2014 Idara ilipangiwa kukusanya jumla ya
TZS milioni 346 na kutumia jumla ya TZS milioni
300 kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia Machi 2014,
Idara ilikusanya jumla ya TZS milioni 266.218
sawa na asilimia 77 na iliingiziwa jumla ya TZS
milioni 64.298 kwa kazi za kawaida sawa na
asilimia 21 ya makadirio.
MALENGO YA IDARA (2014/2015)

36

70. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha mwaka


wa fedha 2014/2015, Idara itaendelea kusimamia
matumizi bora ya barabara kwa ajili ya kuimarisha
usalama wa watumiaji wa barabara kwa
kuendelea kutoa elimu ya usalama barabarani na
kuimarisha ukaguzi wa vyombo vya moto.
Juhudi zitaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha
kuwa Karakana Kuu ya Unguja na Sehemu ya
Mitambo Pemba zinaimarishwa kwa kupatiwa vifaa
vya kisasa na wafanyakazi wenye ujuzi ili ziweze
kufanya kazi zake ipasavyo.
71. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2014/2015
Idara ya Usafiri na Leseni inatarajia kukusanya
jumla ya TZS milioni 364 na inaombewa jumla ya
TZS milioni 200.585 kwa matumizi ya kazi za
kawaida.

IId) SEKTA YA MAWASILIANO


72. Mheshimiwa Spika, Sekta ya Mawasiliano
imeendelea kutoa mchango mkubwa katika ukuaji
uchumi na huduma za kijamii katika nchi yetu na
inajumuisha utoaji wa huduma za mawasiliano
kwa njia ya posta, simu na huduma za teknolojia
ya habari na mawasiliano. Lengo na Sekta hii ni
kuharakisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano katika sekta ya umma na binafsi, ili
37

wananchi wa Zanzibar wanufaike na teknolojia


mpya za TEHAMA zinazovumbuliwa ulimwenguni.

(i) IDARA YA MAWASILIANO


73. Mheshimiwa Spika, Idara hii ina jukumu la
kusimamia huduma za mawasiliano na masuala ya
Taasisi za Mawasiliano za Serikali ya Jamhuri ya
Muungano zilizopo Zanzibar. Idara pia, ina jukumu
la
kuratibu
na
kusimamia
uwekaji
wa
miundombinu ya mawasiliano na kuhakikisha
kuwepo kwa nyenzo za mawasiliano zilizo bora
zitakazorahisisha ukuwaji wa uchumi na biashara
kitaifa na kimataifa.
HATUA ZA UTEKELEZAJI (2013/2014)
74. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka 2013/2014
Idara ilikamilisha Sera ya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano Zanzibar na kutoa mchango wa
kiufundi katika masuala ya teknolojia ya habari na
mawasiliano, ushauri na muongozo katika uwekaji
wa miundombinu ya mawasiliano kama vile
mkonga wa taifa na ujenzi wa minara ya simu.
Aidha, Idara ilifanya ukaguzi na usimamizi wa
utumiaji wa minara ikiwemo ya simu na mtandao.
Jumla ya minara 229 kutoka makampuni
mbalimbali. Idara pia, iliratibu na kusimamia
38

mabadiliko ya teknolojia na uwekaji wa Anuani za


Makaazi (post code).
MATUMIZI YA MKONGA WA MAWASILIANO
75. Mheshimiwa Spika, Mkonga wa mawasiliano
ni miundombinu ya mawasiliano iliyotandikwa
chini ya ardhi, yenye uwezo mkubwa wa
kusafirisha habari data, habari picha, habari video
kwa kasi kubwa zaidi. Miundombinu ya mkonga
wa mawasiliano imegawanyika katika sehemu kuu
tatu:1- Backabone Network
2- Distribution Network
3- Last mile Network
Hivyo basi, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
imeweka miundombinu hiyo kwa hatua ya
"Backbone Network" tu ambayo ina uwezo
mkubwa sana wa kusafirisha mawasiliano. Pia,
Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya Zantel
inaendelea kuweka miundombinu ya "last mile"
katika taasisi mbali mbali za Serikali. Jumla ya
taasisi 84 tayari zimeshafikiwa na "fiber optic"
na ili kuziwezesha ofisi hizo kupata huduma za
mtandao wa nje duniani kote (internet) na
mtandao wa ndani ya nchi (intranet).
39

MALENGO YA IDARA (2014/2015)


76. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2014/2015 Idara itaendelea kuratibu na kufuatilia
utekelezaji wa Sera ya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano hapa Zanzibar, kwa kuandaa Sheria
na Kanuni za TEHAMA na Mpango Mkakati wa
TEHAMA kwa mashirikiano na Idara ya Mipango,
Sera na Utafiti.
Idara itaandaa kanuni za miundombinu ya
mawasiliano ili tuweze kusimamia, kudhibiti na
kukusanya mapato kupitia minara na mikonga ya
mawasiliano kwa wanaomiliki.
Idara pia, itasimamia mkonga wa taifa wa
mawasiliano kwa kushirikiana na Kampuni ya
Zantel kwa upande wa matumizi ya Serikali na
Taasisi binafsi.
77. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka 2013/2014,
Idara ya Mawasiliano ilipangiwa kutumia jumla ya
TZS milioni 255.6 na hadi kufikia Machi, 2014
fedha iliyopatikana ni TZS milioni 80.039 sawa na
asilimia 31.31 ya makadirio.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Idara
inaombewa jumla ya TZS milioni 179.527 kwa ajili
ya kazi za kawaida.
40

MASHIRIKIANO YA IDARA NA TCRA


78. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Miundombinu
na Mawasiliano kwa kushirikiana na Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaendelea na
mchakato wa mradi wa uwekaji wa simbo za posta
na anuwani za makaazi (postcode). Hivi sasa,
tayari mzabuni ameshapatikana ambapo kampuni
ya Mwananchi Supply Ltd ya Zanzibar ndio
iliyoshinda kwa hatua ya majaribio kwenye shehia
nne zifuatazo: Mombasa na Chukwani Unguja, na
Limbani na Selemu kwa upande wa Pemba.

IIe) SEKTA YA USAFIRI WA ANGA


79. Mheshimiwa Spika, sekta ya usafiri wa anga
inajumuisha huduma za viwanja vya ndege na
udhibiti wa usalama wa usafiri wa anga. Huduma
hizi zinatolewa kupitia Mamlaka ya Viwanja vya
Ndege Zanzibar kwa mashirikiano na taasisi mbali
mbali za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na sekta binafsi.

(i) MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE


ZANZIBAR
80. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha
2013/2014 Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
imesimamia, kuendesha na kuendeleza viwanja
vya ndege vya Unguja na Pemba kwa kuzingatia
41

miongozo na kanuni za Kitaifa na Kimataifa. Aidha,


Mamlaka imetekeleza miradi mbali mbali ya
uimarishaji huduma za ndege, abiria na mizigo
katika viwanja vya ndege vya Zanzibar ili kukidhi
haja na matakwa ya watumiaji kwa kiwango
kinachokubalika.
HATUA ZA UTEKELEZAJI KWA MWAKA
2013/2014.
81. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha mwaka
wa fedha 2013/14 Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
imehudumia jumla ya safari za ndege 45,801
ikilinganishwa na safari 43,339 zilizohudumiwa
katika kipindi kama hicho cha mwaka 2012/2013,
sawa na ongezeko la asilimia 5.7. Kati ya safari
hizo safari za ndege 38,453 zilihudumiwa katika
kiwanja cha Kimataifa cha Abedi Amani Karume na
safari za ndege 7,348
zilihudumiwa katika
kiwanja cha Pemba.
82. Mheshimiwa
Spika,
Idadi
ya
abiria
waliohudumiwa iliongezeka kutoka abiria 649,724
mwaka 2012/2013 na kufikia abiria 727,151 Julai
2013 hadi Machi 2014 sawa na asilimia 11. Kati ya
abiria hao, abiria 668,804 walihudumiwa katika
kiwanja cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume
na abiria 58,347 walihudumiwa katika kiwanja cha
Pemba. Aidha, abiria waliopita (Transit) wamefikia
42

76,680. Ongezeko hili la abiria limetokana na


kuongezeka kwa shughuli za utalii, biashara na
kijamii. Idadi ya abiria wa nje ni 302,479 na abiria
wa ndani ni 424,672. (Kiambatanisho Namba
6).
Kwa upande wa mizigo (freight) jumla ya tani
1,396 zilihudumiwa katika viwanja vya Unguja na
Pemba ikilinganishwa na tani 850 zilizohudumiwa
katika kipindi kilichopita ikiwa ni ongezeko la
asilimia 64. Ongezeko hili limetokana na
kuongezeka kwa idadi ya ndege maalum za
mizigo.
MAPATO NA MATUMIZI KWA MAMLAKA.
83. Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Viwanja vya
Ndege Zanzibar kwa mwaka wa fedha wa 2013/14
ilipanga kukusanya jumla ya TZS bilioni 4.7 kutoka
vyanzo vyake vya mapato ya ndani.
Hadi kufikia mwezi Machi 2014
Mamlaka
imekusanya mapato halisi ya TZS bilioni 3.1
kutoka ada ya utuaji wa ndege, kodi za ofisi, faida
ya biashara (concession fees), huduma za kumbi
za watu mashuhuri, ada za kuegesha magari na
mapato mengineyo, sawa na asilimia 65.2 ya
makadirio. Aidha, jumla ya TZS bilioni 3.4 sawa na
asilimia 67 ya makadirio ya matumizi zilitumika
katika kipindi hicho.
43

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO


2013/2014.
84. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha
2013/2014, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
Zanzibar iliendelea kuimarisha usalama katika
viwanja vya ndege kwa kuongeza mitambo na
mfumo wa kufuatilia mienendo ya shughuli za
usalama na uendeshaji wa kiwanja (CCTV) na
mashine za upekuzi kwa kiwanja cha Kimataifa
cha Abeid Amani Karume kupitia miradi ifuatayo:
Ujenzi wa ukumbi (business arrival lounge)
85. Mheshimiwa Spika, Mradi huu ulikusudia
kujenga ukumbi mpya wa kufikia abiria (business
arrival lounge) tayari umemalizika kwa asilimia
100 na uko tayari kwa matumizi. Jumla ya TZS
milioni.225.69 zimetumika.
Ujenzi wa kituo cha biashara (business
centre)
86. Mheshimiwa Spika, Mradi wa ujenzi wa kituo
cha biashara uliokuwa na lengo la kujenga ofisi za
wadau, sambamba na kutoa fursa za ajira kwa
vijana
pamoja na
kuongeza mapato kwa
Mamlaka, ujenzi wa mkahawa pamoja na ujenzi
wa ofisi kwa awamu ya mwanzo umekamilika na
jumla ya ofisi saba (7) zimeshajengwa. Hatua
inayoendelea sasa ni ukamilishaji wa awamu ya
44

pili ya ujenzi wa ofisi saba (7) zilizobakia. Mradi


huu umegharimu TZS milioni 249.44.
Ununuzi wa mashine za ukaguzi (x-rays
machines)
87. Mheshimiwa Spika, Mradi huu ulikusudia
kununua mashine nne (4) za ukaguzi kwa ajili ya
kuimarisha hali ya usalama katika kiwanja cha
ndege cha kimataifa cha Abeid Amani Karume
(AAKIA). Mzabuni wa kampuni ya (HISCO
SECURITY
DETECTION
PRODUCTS)
tayari
ameshapatikana na hatua iliyobakia ni kutiliana
saini mkataba wa utekelezaji mradi huo. Mradi
huu umegharimu TZS milioni 960.
Uwekaji
system)

kipaza

sauti

(public

address

88. Mheshimiwa Spika, Mradi huu ambao


uliokuwa na lengo la kufunga kipaza sauti kwa ajili
ya
kuwaondolea
usumbufu
abiria
tayari
umekamilika tayari kipaza sauti hicho kinatumika.
Mradi huu umegharimu jumla ya TZS milioni 24.4.
89. Mheshimiwa Spika, kwa ujumla miradi yote
imegharimu TZS bilioni 1.49.

45

MALENGO YA MAMLAKA
2014/2015.

KWA

MWAKA

90. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015


Mamlaka ya Viwanja vya ndege kupitia viwanja
vya ndege vya Unguja na Pemba inatarajia
kuhudumia jumla ya ndege 48,091 na abiria
763,508.
Mamlaka pia, itaendelea kuvifanyia matengenezo
viwanja vyake vya ndege na kuimarisha utoaji wa
huduma mbali mbali za abiria, ndege na mizigo ili
kukuza mahitaji ya Usafiri wa Anga kupitia miradi
ifuatayo ambayo kwa ujumla wake inatarajiwa
kugharimu TZS milioni 400:i.

Ufungaji wa mkanda wa mizigo (conveyor


belt) kwa ajili ya kuhudumia mizigo katika
kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Abeid
Amani Karume katika eneo la kuwasili abiria.

ii.

Ujenzi wa kipaa (canopy) eneo la kuwasili


abiria hadi eneo la maegesho ya magari kwa
ajili ya kujenga mazingira mazuri kwa
wananchi wanaosubiri wageni wao katika
eneo la maegesho.

iii.

Kufanya matengenezo ya sehemu ya


kuondokea abiria wa ndani katika jengo la
huduma (service building).
46

iv.

Kufanya Upembuzi yakinifu wa uwekaji wa


kifaa cha kuongozea ndege (ILS) kwa ajili ya
kumuwezesha rubani kuweza kuona vizuri
uwanja katika kipindi cha mvua na hali ya
mawingu na hivyo kuhakikisha usalama wa
ndege na abiria.

91.
Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2014/2015 Mamlaka inakadiria kukusanya jumla
ya TZS bilioni 4.9 na kutumia jumla ya TZS bilioni
4.9 kwa kazi za kawaida na maendeleo. Kati ya
hizo TZS 4.5 ni makusanyo yatokanayo na vianzio
vya mapato vya Mamlaka na TZS milioni 400
zitatokana na "safety fee".
MASHIRIKIANO NA TAASISI ZA MUUNGANO
92. Mheshimiwa
Spika,
katika
mwaka
2013/2014, Wizara iliendelea kushirikiana na
taasisi za Muungano zilizopo hapa Zanzibar
(Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) na
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) katika
utoaji wa huduma na usimamizi wa Sekta ya
Usafiri wa Anga. Mashirikiano na taasisi hizi
yamechangia kwa kiasi kikubwa katika upatikanaji
wa huduma na usimamizi mzuri wa sekta hii.

47

IIf) SEKTA YA USAFIRI WA BAHARINI


93. Mheshimiwa Spika, Sekta ya Usafiri Baharini
inajumuisha huduma za bandari, huduma za
usafiri wa baharini na udhibiti wa usalama wa
usafiri baharini. Huduma za bandari na usafiri wa
baharini zinatolewa kupitia Shirika la Bandari,
Shirika la Meli na Uwakala pamoja na sekta
binafsi. Aidha, udhibiti wa usalama wa usafiri
baharini unasimamiwa na Mamlaka ya Usafiri
Baharini.

(i) MAMLAKA YA USAFIRI BAHARINI


94. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Mamlaka
ya Usafiri Baharini iliendelea kusimamia udhibiti
wa usalama wa usafiri wa baharini kwa kuzingatia
Sheria ya Usafiri Baharini ya mwaka 2006 na
Kanuni zake pamoja na itifaki na mikataba mbali
mbali ya kimataifa iliyoridhiwa na nchi yetu.
HATUA ZA UTEKELEZAJI (2013/2014)

Usimamiaji wa usalama wa usafiri baharini


95. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014
Mamlaka ya Usafiri wa Baharini iliendelea
kusimamia usalama wa vyombo vya baharini vya
48

abiria na mizigo. Katika kipindi hichi Mamlaka


iliandaa Kanuni moja ya Training and Certification
na kufanya mapitio ya kanuni za Sheria ya
Usafiri Baharini na kuzifanyia marekebisho. Aidha,
Mamlaka kwa kutumia kanuni za kusimamia
makampuni na taasisi zinazotoa huduma katika
bandari na meli, iliendelea na hatua za kuwapatia
leseni waendeshaji wa huduma hizo na kudhibiti
shughuli zao.
96. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha
2013/2014 Mamlaka ilisajili jumla ya meli 15 zenye
uzito wa ujazo (GRT) 9,127 kwa usajili wa ndani
(Tanzania Zanzibar Registry ) na meli 62 zenye
uzito wa ujazo (GRT) 343,653 kwa usajili wa nje
(Tanzania Zanzibar
International
Registry).
(Kiambatanisho Namba 7). Aidha, vyombo
vidogo vidogo 112 vilisajiliwa pamoja na kutolewa
vitabu vya mabaharia (Discharge Books) 676 na
vitambulisho vya kimataifa vya mabaharia 19.
Mamlaka pia imetoa leseni za manahodha (Boat
Master Licences ) 92 na Boat Engineer 12.
Vile vile, Mamlaka ilikagua jumla ya meli 52 zenye
uzito wa ujazo (GRT) 41,626 na kuthibitisha
mikataba 262 ya mabaharia wanaosafiri na meli za
nje kupitia kampuni ya DANAOS.

49

97. Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Usafiri


Baharini imefanya vikao mbali mbali vya wadau
wa sekta ya usafiri baharini ikiwemo vikao vya
ushirikiano na SUMATRA, Kamati za Ulinzi na
Usalama za Mikoa na Wilaya zote na Wakuu wa
Madiko Unguja na Pemba kuhusiana na
masuala ya usalama wa vyombo vidogo vidogo
kuzitumia bandari zisizo rasmi. Jumla ya vikao
14 na wadau hao wa sekta ya usafiri baharini
vimefanyika. Aidha, Mamlaka imefanya zoezi
maalum la kuhakiki utaratibu wa udhibiti wa
uuzaji wa tiketi za magendo na utumiaji wa
vitambulisho wakati wa ununuzi wa tiketi na
uingiaji bandarini.
Vile vile, Mamlaka ya Usafiri Baharini
na
SUMATRA zimeendelea kushirikiana katika
masuala yanayohusu ukaguzi na uhakiki wa
ubora wa vyombo vya usafiri wa baharini,
taratibu za utafutaji na uokozi na kubadilishana
taarifa muhimu.
98. Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Usafiri
Baharini kwa mwaka
2013/2014 ilikadiria
kukusanya jumla ya TZS bilioni 1.738 na kutumia
jumla ya TZS bilioni 1.625 kwa matumizi ya
kawaida.
Hadi kufikia mwezi Machi 2014, jumla ya TZS
milioni 872.66 zimekusanywa sawa na asilimia
50

51 ya makadirio na kutumia jumla ya TZS milioni


792.27 sawa na asilimia 49 ya makadirio.
MALENGO YA
(2014/2015).

MAMLAKA

KWA

MWAKA

99. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha


2014/2015, Mamlaka itaendelea kusimamia
masuala ya usafiri baharini kwa kufanya ukaguzi
na kutoa leseni za vyombo vya baharini, utoaji wa
leseni za manahodha na kukuza vyanzo vyake vya
mapato pamoja na kukamilisha kanuni tano za
Sheria ya Usafiri Baharini ili ziendelee kutumika.
Aidha, Mamlaka itaendelea kudhibiti shughuli za
makampuni na taasisi zinazotoa huduma katika
bandari na meli na kuwapatia leseni. Vile vile,
usajili wa meli za kimataifa utafanywa na Mamlaka
ya Usafiri Baharini yenyewe na kuondokana na
uwakala.
100. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2014/2015 Mamlaka imepanga kukusanya jumla
ya TZS bilioni 1.380 na kutumia jumla ya TZS
bilioni 1.359 kwa matumizi ya kazi za kawaida
ikiwemo ruzuku ya TZS milioni 300 ya mishahara
ya Mamlaka.

51

Huduma za Bandari
(ii) SHIRIKA LA BANDARI
101. Mheshimwa Spika, Shirika la Bandari lina
jukumu la kutoa huduma za uingizaji na utoaji
meli katika bandari za Unguja na Pemba, ufungaji
na ufunguaji wa meli kwenye gati, uangalizi wa
alama za kuongozea usafiri wa meli (minara na
maboya), uteremshaji na upakiaji wa bidhaa
kwenye meli pamoja na vyombo vyengine vya
usafiri wa baharini. Vile vile, Shirika lina wajibu wa
kuhifadhi mizigo na utunzaji wake katika Bandari
pamoja na kuvifanyia matengenezo madogo
madogo vyombo mbali mbali vya usafiri wa
Baharini kwa kutumia Karakana yake ya Malindi.
HATUA ZA UTEKELEZAJI (2013/2014)
102.
Mheshimiwa Spika, Katika mwaka
2013/2014 Shirika lililenga kuhudumia meli za
kigeni 180 zenye uzito wa ujazo (GRT) 2.6
milioni. Hadi kufikia mwezi Machi 2014 jumla ya
meli za Kigeni 152 zenye uzito wa ujazo (GRT)
2.27 milioni zimehudumiwa sawa na asilimia 84
ya lengo. Aidha, meli za ndani zipatazo 2,913
zimehudumiwa pamoja na vyombo vya kienyeji
4,617 kati ya vyombo 4,100 vilivyokadiriwa.
Shirika pia, limehudumia jumla ya tani 49,363
ukilinganisha na tani 53,245 za mizigo
52

mchanganyiko zilizohudumiwa katika kipindi


kilichopita. Vile vile, Shirika limehudumia jumla
ya makontena 44,276 ikilinganishwa na
makontena 38,341 yaliohudumiwa katika kipindi
kama hicho kilichopita.
Kwa upande wa abiria jumla ya
abiria
1,776,101 wa ndani na abiria wa nje 2,654
wamehudumiwa kupitia bandari za Unguja na
Pemba.
Kazi za Kiufundi:
103.
Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha
Julai 2013 hadi Machi 2014 Karakana kuu ya
Shirika ilifanya kazi ya ubadilishaji wa Maboya
matatu (3) yanayotumia taa za nguvu ya jua
(Solar Power) katika Bandari ya Mkoani na Boya
moja (1) katika Bandari ya Wete.
104.
Mheshimiwa Spika, Shirika kupitia
karakana
yake
hiyo
pia,
imeyafanyia
matangenezo maboya manne (4) ya Solar
pamoja na kuunda maboya saba (7) bubu
ambapo maboya mawili (2) ni kwa ajili ya Meli za
mafuta katika Bandari ya Wesha na matano (5)
kwa ajili ya kuongozea vyombo vya baharini
katika Bandari hiyo.

53

UTEKELEZAJI
MAENDELEO

WA

MIRADI

YA

105.
Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha
Julai 2013 hadi Machi, 2014 Shirika limetekeleza
miradi ifuatayo:i.

Matengenezo ya sakafu ya eneo la


kuhifadhia makontena bandarini Malindi.
Kazi za kuchimbua, kujaza kifusi na
kushindilia eneo hilo zimefanyika. Jumla
ya TZS milioni 164.01 zimetumika
kugharamia mradi huu.

ii.

Ujenzi wa jengo la Afisi bandarini. Mradi


huu umeshakamilika na kukabidhiwa
Shirika katika mwezi wa Aprili 2014
ambapo jumla ya TZS milioni 958.74
zimetumika.

iii.

Ununuzi na Ufungaji wa Taa za Solar


katika
minara
yote
mikubwa
ya
kuongozea Meli iliopo Unguja na Pemba.
Taa hizo tayari zimenunuliwa na
zimeshafungwa katika minara yote
mikubwa minane (8) ya Unguja na Pemba
na zinafanya kazi kama ilivyokusudiwa.
Jumla ya USD 221,700 zimetumika.

iv.

Ununuzi wa tagi kubwa kwa ajili ya


ufungaji na ufunguaji wa meli katika
54

bandari ya Malindi. Taratibu za manunuzi


zimekamilika na Shirika limetiliana saini
Mkataba wa matengenezo ya Tagi hiyo
katika mwezi wa Machi, 2014 na
Mkandarasi aliyeshinda Zabuni. Ujenzi wa
chombo hicho utaanza mara tu Shirika
litakapofanya malipo ya awali (Down
Payment) na unatarajiwa kuchukua miezi
sita (6). Mradi huu utagharimu jumla ya
Euro milioni 4.4 ambapo kwa sasa jumla
ya Euro milioni 1.32 zimeshalipwa sawa
na TZS bilioni 3.05.
v.

Uchimbaji wa Mchanga (Dredging) katika


Gati ya Malindi. Mradi
huu haujaanza
kutokana na hali ya kifedha kwa hivi
sasa. Hata hivyo Shirika limekusudia
kuutekeleza mradi huo mara tu hali
itakaporuhusu.

MAPATO NA MATUMIZI YA SHIRIKA


106. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha
Julai 2013 hadi Machi, 2014 Shirika lilikadiria
kukusanya jumla ya TZS bilioni 12.81. Hadi
kufikia mwezi wa Machi, 2014 jumla ya TZS
bilioni 14.60 zilikusanywa ikiwa ni sawa na
asilimia 114 makadirio ya kipindi hicho cha
miezi tisa. Aidha, Shirika lilipanga kutumia
jumla ya TZS bilioni 10.63 na hadi kufikia
55

Machi 2014 jumla ya TZS bilioni 10.47 pia


zimetumika kwa kazi za kawaida sawa na
asilimia 98.51.
MALENGO YA
2014/2015

SHIRIKA

KWA

MWAKA

107. Mheshimiwa
Spika,
kwa
mwaka
2014/2015 Shirika la Bandari linatarajia
kuhudumia jumla ya meli 185 za kigeni zenye
uzito (GRT) wa Tani 2.7 milioni, Meli za ndani
zipatazo 3,500 na Majahazi 5,000 pamoja na
kuhudumia tani 86,140 za mzigo mchanganyiko
na makontena 59,116.
108. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa
miradi ya maendeleo Shirika linatarajia
kuendelea na uimarishaji wa huduma na
rasilimali zake kwa kuikamilisha miradi
iliyoanzishwa mwaka wa Fedha unaomalizika
kama ilivyoelezwa hapo juu pamoja na
kuendelea na awamu ya tatu ya mradi wa
ununuzi wa vifaa vya kunyanyulia mizigo
bandarini.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Shirika la
Bandari limekadiria kukusanya jumla ya TZS
bilioni 19.81. Aidha katika kutekeleza malengo
yake Shirika limepanga kutumia jumla ya TZS
bilioni 16.22 kwa kazi za kawaida.
56

(iii) SHIRIKA LA MELI NA UWAKALA.


109. Mheshimiwa Spika, Shirika la Meli na
Uwakala limeendelea kutoa huduma za usafiri
wa baharini baina ya visiwa vya Unguja na
Pemba kwa kutumia meli ya MV Maendeleo.
Aidha, Shirika limekodisha meli ya MT
Ukombozi
kwa
kampuni
ya
GAPCO.
Changamoto kubwa inayoikabili Shirika ni
uchakavu wa meli zake. Ili kukabiliana na
changamoto hii Shirika liliendelea na utaratibu
maalum wa preventive maintenance kwa ajili
ya kupunguza matumizi makubwa yatokanayo
na matengenezo ya meli. Utaratibu huu
ulianzishwa mwaka jana kupitia ajira za
mkataba
za
Wahandisi
bingwa
wa
matengenezo
ya
meli
kutoka
Kenya.
Wataalamu hao kwa kushirikiana na Wahandisi
wetu wameweza kuzifanya meli za Shirika
ziendelee kufanyakazi vizuri.
HATUA ZA UTEKELEZAJI KWA MWAKA
2013/2014)
110. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai
2013 hadi Machi 2014 meli ya MV. Maendeleo
imefanya safari 100 kwa kusafirisha abiria na
mizigo katika visiwa vyetu. Kwa upande wa
abiria na mizigo, jumla ya abiria 82,980
57

walisafirishwa kwa kutumia meli hiyo na


shehena ya mizigo tani 17,218.986. Aidha,
Shirika limehudumia meli za kigeni zipatazo 128
zilizoingia nchini kwa kutumia bandari zetu.
MAPATO NA MATUMIZI YA SHIRIKA.
111. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha
Julai 2013 hadi Machi 2014 Shirika lilikusanya
jumla ya TZS bilioni 4.315 sawa na asilimia 79
ya makisio ya mwaka 2013/2014. Kati ya hizo
TZS bilioni 1.26 zilitokana na meli ya MV
Maendeleo na TZS bilioni 1.24 kutoka meli ya
MT. Ukombozi na TZS bilioni 1.28 kwa Uwakala
wa meli za kigeni.
Kwa upande wa matumizi, jumla ya TZS 4.314
bilioni sawa na asilimia 85 ya makisio ya
mwaka 2013/2014 zilitumika.
MALENGO YA
2014/2015

SHIRIKA

KWA

MWAKA

112. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa


fedha
2014/2015
Shirika
linategemea
kukusanya jumla ya TZS bilioni 6.63 kutokana
na vianzio vyake vya mapato na kutumia jumla
ya TZS bilioni 5.761 kwa matumizi ya kazi za
kawaida.
58

113. Mheshimiwa
Spika,
kwa
mwaka
2014/2015 Shirika litaendelea kutekeleza
majukumu yake ya uendeshaji wa meli za
Serikali kwa kusafirisha abiria na mizigo kwa
kutumia meli ya MV Maendeleo. Aidha, Shirika
litaendelea na utaratibu maalum wa preventive
maintenance ulioanzishwa mwaka jana kwa
ajili ya kupunguza matumizi makubwa
yatokanayo na matengenezo ya mara kwa
mara ya meli na kuzifanya meli zetu ziendelee
kufanya kazi vizuri hadi pale taratibu za
upatikanaji wa meli mpya zitakapokamilika.
Vile vile, Shirika litaendelea na taratibu za
kuajiri kwa mkataba wahandisi kwa kazi za
melini (Sign-on/Sign- off) na kuendelea kutoa
huduma za uwakala wa meli za kigeni
zinazoingia nchini kwa kutumia bandari zetu.

59

III: HITIMISHO.
114. Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Wizara
ya Miundombinu na Mawasiliano, napenda
kuwashukuru
kwa
dhati
wale
wote
walioshirikiana nasi katika kipindi cha mwaka
wa fedha 2013/2014 katika utekelezaji wa
majukumu yetu. Shukurani za pekee ziwaendee
Washirika
wa
Maendeleo
walioendelea
kushirikiana nasi katika kutekeleza programu na
mipango yetu ya uimarishaji miundombinu ya
usafiri na mawasiliano. Washirika hao ni
pamoja na Jamhuri ya Watu wa China, Norway,
Japan,
Saudi Arabia,
India,
Marekani,
Ujerumani, Oman na UAE. Mashirika ya
Kimataifa ni pamoja na Benki ya Dunia (World
Bank), China Exim Bank, Jumuiya ya Nchi za
Ulaya (EU), Benki ya Maendeleo ya Afrika
(ADB), Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya
Afrika (BADEA), Mfuko wa Umoja wa
Maendeleo ya Kimataifa wa Nchi Zinazosafirisha
Mafuta kwa Wingi ulimwenguni (OPEC Fund),
SAUDI Fund, NORAD, Mashirika ya Umoja wa
Mataifa ya UNDP, IMO na ICAO.
115. Mheshimiwa Spika, nitakuwa mchoyo wa
fadhila nisipowashukuru viongozi wenzangu na
nikianza na Mhe. Issa Haji Ussi Gavu, Naibu
Waziri, Dkt. Juma Malik Akil, Katibu Mkuu, Nd.
Tahir M.K. Abdullah na Wakurugenzi wote.
60

Aidha, nawashukuru Wenyeviti wa Bodi na


Watendaji Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya
Wizara, Wakuu wa Vitengo pamoja na
wafanyakazi wote wa Wizara ya Miundombinu
na taasisi zake kwa kuendelea kujituma kwa
juhudi na maarifa katika kutekeleza malengo na
majukumu ya Wizara yetu.
116. Mheshimiwa
Spika,
tunawashukuru
wadau wote wa sekta ya usafiri na mawasiliano
na hasa sekta binafsi ambao wametupatia
ushirikiano wa kutosha katika kuendeleza sekta
hii. Shukurani zangu za pekee nazitoa kwa
Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali na wafanyakazi
wote wa Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali
kwa kuchapa vizuri hotuba hii.

61

IV: MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA


2014/2015
117. Mheshimiwa Spika, kwa madhumuni ya
kuiwezesha Wizara ya Miundombinu na
Mawasiliano kutekeleza majukumu yake na
malengo yaliyoelezwa katika hotuba hii,
naomba kutoa hoja kwamba, Baraza lako
Tukufu liidhinishe jumla ya TZS bilioni 14.077
kwa ajili ya matumizi ya Wizara kwa mwaka wa
fedha 2014/2015. Kati ya fedha hizo, TZS
bilioni 5.677 ni kwa ajili ya kazi za kawaida na
TZS bilioni 8.40 ni kwa ajili ya kazi za
maendeleo.
Aidha, naliomba Baraza lako Tukufu kuruhusu
Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano
kukusanya mapato ya jumla ya TZS
436,000,000 kutokana na vianzio mbalimbali
vilivyomo ndani ya Wizara hii.
118. Mheshimiwa Spika
Naomba kutoa hoja.

62

KIAMBATANISHO NAMBA 1:
SEHEMU A: MUHTASARI WA MAKADIRIO YA FEDHA KWA KAZI ZA KAWAIDA, MAENDELEO NA MAPATO KWA KIPINDI CHA
JULAI 2013 HADI MACHI 2014 NA MAKISIO YA MWAKA 2014/2015

KASMA

MATUMIZI
HALISI
2012/2013

0301 PEMBA
0401 MIPANGO
0501 MAMLAKA YA USAFIRI BAHARINI.
0701 UUB
0801 LESENI

MAKADIRIO

FEDHA HALISI Julai 2013-Machi 2014

2013/2014

Mishahara/

Matumizi

Maposho

Mengineyo

Asilimia

Jumla

Makisikio

2014/2015

1,074,213,708

1,277,000,000

733,060,300

125,664,000

858,724,300

67%

1,362,501,000

108,007,210

288,000,000

83,137,770

83,137,770

29%

200,585,000

238,000,000

178,560,000

178,560,000

75%

300,000,000

1,271,433,402

250,000,000

81,282,842

81,282,842

33%

165,488,000

447,121,180

300,000,000

64,298,000

64,298,000

21%

200,585,000

63

KASMA

MATUMIZI
HALISI
2012/2013

0901 UENDESHAJI

0110 MAWASILIANO

JUMLA

MAKADIRIO

FEDHA HALISI Julai 2013-Machi 2014

2013/2014

Mishahara/

Matumizi

Maposho

Mengineyo

Asilimia

Jumla

Makisikio

2014/2015

1,135,464,070

2,583,400,000

1,798,064,362

217,946,860

2,016,011,222

86%

3,269,114,000

104,294,460

255,600,000

80,039,000

80,039,000

31%

179,527,000

4,140,534,030 5,192,000,000 2,709,684,662 652,368,472 3,362,053,134

64

5,677,800,000

Kiambatanisho 1: Inaendelea.

SEHEMU B: MAPATO

MAPATO
KASMA

HALISI
2012/2013

MAKADIRIO
2013/2014

FEDHA
ZILIKUSANYWA

ASILIMIA %

JULY-MACHI

MAKISIO
2014/2015

2013/2014
0301 PEMBA

47,882,500

50,200,000

44,550,559

89%

62,000,000

0701 UUB

6,650,000

10,000,000

3,480,000

35%

10,000,000

339,833,650

346,000,000

266,218,300

77%

364,000,000

394,366,150

406,200,000

314,248,859

77%

436,000,000

0801 LESENI
JUMLA

65

Kiambatisho 1: Inaendelea.

SEHEMU C: KAZI ZA MAENDELEO

KASMA

MATUMIZI
HALISI
2012/2013

0301 PEMBA
0401 MIPANGO
0701 UUB
JUMLA

FEDHA
MAKADIRIO

ZILIZOPATIKANA

2013/2014

JULY-MACHI

ASILIMIA %

MAKISIO
2014/2015

2013/2014

2,501,829,904

4,723,356,000

3,120,000,000

66

3,325,000,000

897,270,096

7,976,644,000

822,798,204

10

3,325,000,000

1,609,544,000

2,200,000,000

433,532,436

20

1,750,000,000

5,008,644,000

14,900,000,000

4,376,330,640

96

8,400,000,000

66

KIAMBATANISHO NAMBA 2:

MIRADI YA MAENDELEO ILIYOPANGWA/KUTEKELEZWA 2014/2015


NA.

1.

UJENZI

UREFU (km)

MFADHILI

BAJETI YA SMZ

RUZUKU/

(Tsh)

MKOPO (Tsh)

Ujenzi wa barabara 3 za Pemba


Wete Gando (13.6)
Wete Konde (15.1)

52.7

SMZ/BADEA
/SAUD FUND

2,425,000,000

11,999,998,000

100,000,000

Wete Chake (24)


2

Ujenzi wa barabara 3 za Pemba


Wete Chake (mradi mpya)

3.

Ujenzi wa barabara ya Mgagadu- Kiwani

4.

Ujenzi wa barabara ya Mkanyageni - Kangani

5.

Ujenzi wa barabara ya Ole Kengeja

24

7.6

SMZ/BADEA
/SAUD FUND
SMZ

300,000,000

6.5

SMZ

35

SMZ /OPEC

500,000,000

4,392,000,000

67

NA.

UJENZI

UREFU (km)

MFADHILI

BAJETI YA SMZ

RUZUKU/

(Tsh)

MKOPO (Tsh)

Upembuzi yakinifu wa barabara za vijijini-Unguja


6

(Matemwe Muyuni, Kichwele-Pangeni, Njia nneUmbuji-Uroa, Jozani-Charawe-Ukongoroni-Bwejuu

65.2

AfDB

1,754,456,000

ROAD FUND

50,000,000

1,600,000,000

7,500,000,000

4,975,000,000

25,646,454,000

SMZ/WB

975,000,000

14,600,000,000

SMZ /EXIM

1,950,000,000

110,840,000,000

naMkwajuni-Kijini) (mradi mpya)


7.
8

Ujenzi wa Barabara ya Amani Mtoni (Benjamin


Mkapa)
Barabara zinazoingia mjini

77.9

Ujenzi wa barabara 3 Vijijini -Unguja


9

Barabara ya Koani Jumbi (6.3)


Barabara ya Kizimbani Kiboje (7.2)
Barabara ya Jendele Cheju Kaebona (11.7)

25.2

SMZ/BADEA

JUMLA NDOGO

Ujenzi na utanuzi wa maegesho na njia za kupitia


10

ndege.

11

Ujenzi wa jengo jipya la abiria A.AKIA

68

NA.

UJENZI

UREFU (km)

MFADHILI

BAJETI YA SMZ

RUZUKU/

(Tsh)

MKOPO (Tsh)

CHINA
12

Uimarishaji huduma uwanja wa ndege wa Pemba

SMZ

13

Ujenzi wa bandari mpya Hubport - Maruhubi

SMZ

500,000,000

14

Mfumo wa mageuzi ya taasisi (Institutional reform)

ADB

654,456,000

3,425,000,000

126,094,456,000

8,400,000,000

151,740,910,000

JUMLA NDOGO
JUMLA KUU

69

KIAMBATANISHO NAMBA 3:

WAFANYAKAZI WALIOPATA MAFUNZO KWA KIPINDI CHA MWAKA 2013/2014.

IDARA

MASTERS
MKE

MME

PG/DIPLOMA
MKE

MME

MKE

MME

ADV.
DIPLOMA
MKE

MME

UENDESHAJI NA UTUMISHI
MIPANGO,SERA NA UTAFITI

DEGREE

DIPLOMA

CHETI

MKE

MME

MKE

MME

11

1
1

IDARA YA UTUNZAJI BARABARA


AFISI KUU PEMBA
JUMLA

15
5

IDARA YA MAWASILIANO
IDARA YA USAFIRI NA LESENI

JUMLA

1
6

13

19

48

70

MASOMO YA MUDA MFUPI

IDARA

W/WAKE

W/ME

JUMLA

UENDESHAJI NA UTUMISHI

MIPANGO,SERA NA UTAFITI

IDARA YA MAWASILIANO

IDARA YA USAFIRI NA LESENI


IDARA YA UTUNZAJI BARABARA

AFISI KUU PEMBA

JUMLA

37

46

71

KIMBATANISHO NAMBA 4:
BARABARA ZILIZOFANYIWA MATENGENEZO KUPITIA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA
WA FEDHA 2013/2014
Matengenezo ya kawaida ya barabara za lami (Routine maintenance for paved roads)
Kazi zilizofanywa na wafanyakazi wa idara ya barabara (Force account contract)
(Ukataji wa majani, kusafisha misingi na kuziba mashimo)
JINA LA BARABARA
SNO
UREFU (KM)
UNGUJA
1

Tunguu- Makunduchi

34.00

Kaebona-Kaepwani

6.00

Kibuteni-Kizimkazi Mkunguni

6.00

Mkwajuni-Matemwe

7.00

Mshelishelini-Pwanimchangani

7.50

Mwanakwerekwe-Tunguu

30.00

Mchinamwazo-Nyumbambili

1.20

Soko la mboga Buyu

1.20

72

JINA LA BARABARA

SNO

UREFU (KM)

Paje-Michamvi

17.82

10

Mtegani-Mtende

5.50

11

Dunga-Chwaka

14.40

12

Paje-Makunduchi

18.40

Jumla ndogo

149.02
PEMBA

Chake-Wete

30.00

Kilindini-micheweni

6.00

Konde-Kiuyu kwa Manda

3.50

Mkoani-Makombeni

5.00

Bogoa-Michenzani

3.00

Chanjaani-M/manne

4.00

Mbuguani-Mkoani Port

2.00

Mkoani-Shindi

2.20

73

JINA LA BARABARA

SNO
9

Mkoani-Ng'ombeni school

UREFU (KM)
0.50

Jumla ndogo

56.20

74

KIAMBATANISHO 4: INAENDELEA..
Matengenezo ya sehemu korofi - uwekaji wa lami
SNO
1
2
3
4

JINA LA BARABARA
UNGUJA
Upenja-Kiwengwa
Mkwajuni-Matemwe (sehemu ya Kilimani)
Uwekaji wa taa za nguvu za jua (Sola) za
kuongozea magari na CCTV sehemu ya
makutano ya barabara Malindi, Mkunazini na
Kwamchina mwanzo
Mwanakwerekwe-Tunguu ( Sehemu
yaTunguumwisho )
JUMLA

75

UREFU KM

MAELEZO

1.30
0.17
Kazi zimeanza

6.00
7.47

Matengenezo ya muda maalum (Periodic maintenance)


SNO
JINA LA BARABARA
UREFU KM
UNGUJA
Kikwajuni-Kisiwandui via Wireless (kiwango cha
1
0.50
lami)
2
Buyu-Chukwani (Kiwango cha lami)
0.70
3
Fuoni-Kibondemzungu (Kiwango cha kifusi)
2.00
Amani-Mtoni (uwekaji wa kingo za zege awamu
4
ya kwanza katikati ya barabara)- 1.6km
5
Njia nne-Umbuji (Kiwango cha lami)
5.00
6
Kivunge-Mkokotoni (Uwekaji wa lami)
3.30
7
Mkwajuni-Mshelishelini (Uwekaji wa lami)
2.00
8
Kwaabasi Hussein-Kilimahewa (Kiwango cha lami)
0.30
JUMLA NDOGO
13.80

1
2

PEMBA
Barabara ya Mtaa wa Kilo road (Kiwango cha
kifusi)
Barabara ya Mtaa wa Selemu (Kiwango cha
76

0.40
0.80

MAELEZO

Mkandarasi anafanya
matayarisho
Kazi zimekamilika
Kazi
Kazi
Kazi
Kazi

zinaendelea
zimekamilika
zimekamilika
zimekamilika

Kazi zinaendelea

SNO
3

JINA LA BARABARA

UREFU KM

kifusi)
Barabara ya Msitu wa Ngezi (kwa kiwango cha
Saruji na udongo)

1.20

Melitano-Madenjani (Kiwango cha lami)

12.30

5
6

Chake-Wesha (Kiwango cha lami)


Melitano-Machomanne(Kiwango cha lami)
JUMLA NDOGO

1.00
2.20
17.90

JUMLA KUU UNGUJA NA PEMBA

31.70

77

MAELEZO
Kazi zimekamilika
Taratibu za manunuzi
zinaendelea
Kazi zimekamilika
Kazi zinaendelea

KIAMBATANISHO 4: INAENDELEA..
Matengenezo ya dharura
SNO
1
2
1

AINA YA KAZI/JINA LA BARABARA


UNGUJA
Uchimbaji wa mtaro wa maji-Kwamchina mwanzo
(barabara ya Jang'ombe) kwa awamu ya kwanza
Matengenezo ya sehemu korofi sehemu ya Sogea
PEMBA
Ujenzi wa mtaro sehemu ya Kwachangawe
barabara ya Mkoani-Chake

78

UREFU KM

MAELEZO

0.23

Kazi zimekamilika

0.60

Kazi zinaendelea

0.12

Kazi zimekamilika

Matengenezo/ Ujenzi wa kalvati na mitaro


SNO JINA LA BARABARA

IDADI/KM

MAELEZO

PEMBA
Ujenzi wa kalvati (No)
1

Mgagadu-Kiwani

Konde Kiuyu

JUMLA

Ujenzi wa mitaro (Km)


Ole-Konde

0.20

Chake-Mkoani

0.40

JUMLA

0.60

79

Kazi zinaendelea

KIAMBATANISHO 4: INAENDELEA..
MALENGO KWA MWAKA WA FEDHA 2014/2015 KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA
BARABARA - ZANZIBAR.
Matengenezo ya kawaida barabara za lami (Routine maintenance for paved roads) zilizopangwa
kufanywa na Idara ya barabara (Force account contract)
(Ukataji wa majani, kusafisha misingi na kuziba mashimo)
UNGUJA
Ref
T3
R107

JINA LA BARABARA
Tunguu-Makunduchi

UREFU (KM)
34.00

Kaebona-Unguja Ukuu

6.00
18.00

R109

Paje - Makunduchi
Mtegani-Mtende

T002

Dunga - Chwaka

14.42

R108

Kibuteni-Kizimkazi

5.50

R115

M/shelini - P/Mchangani

7.50

R113

Mkwajuni - Matemwe

7.43

T8

5.50

80

Ref

JINA LA BARABARA

UREFU (KM)

T7

Pongwe - Matemwe

20.40

Mfenesini- Bumbwini-Mangapwani

13.82

T8

Paje - Michamvi

17.00

M/kwereke - Tunguu
Kwamchina mwanzo -Mbuyu mnene/nyumbambili

30.00
2.80

T3
F448

U220 Mazizini-Chukwani/U/ndege
9.00
Jumla
191.37
Matengenezo ya kawaida barabara za lami (Routine maintenance for paved roads) zilizopangwa
kufanywa na Idara ya barabara (Force account contract)
(Ukataji wa majani, kusafisha misingi na kuziba mashimo)

81

PEMBA
Ref
T31

JINA LA BARABARA

UREFU (KM)

Chake Chake - Wete

30

R199

Konde - Kiuyu cha Manda

3.5

T31

Chanjaani - M/Manne

T31

Mbuguani - Mkoani Port

T32

Kilindini - Micheweni

U301

Mkoani Port- Ngo'mbeni school

0.5

R161

Mkoani - Makombeni

F503

Bogoa - Michenzani

F502

Mkanyageni - Shidi
Jumla

2.2
56.20

82

KIAMBATANISHO 4: INAENDELEA..
Matengenezo ya kawaida barabara za lami (Routine maintenance for paved roads) zilizopangwa
kufanywa na wakandarasi/vikundi vya jamii (Contract account contract) (Ukataji wa majani, kusafisha
misingi na kuziba mashimo)
UNGUJA
Ref
1

JINA LA BARABARA

UREFU (KM)

Lot. 1

R119

Bububu - Mndo

3.94

F401

Kwanyanya-Mkanyageni

3.08

R102

Regezamwendo-Mfenesini

14.27

2
F402

Lot.2
Kitundu-Ndagaa

5.50

Amani -Dunga

12.74

F403

Koani - Machui - Kitumba

5.50

R103

Kidimni- Kitope

19.00

T2

Lot.3

83

Ref

JINA LA BARABARA

UREFU (KM)

T6

Kinyasini - Tunguu

26.76

T1

Mkwajuni - Nungwi

19.00

Lot.4

R114

Upenja - Kiwengwa

8.31

Kipilipilini - Pongwe
Mahonda - D/Mkokotoni

14.00
13.52

Njianne - Bambi

6.50

5
T1
T1

Lot.5
Kwanyanya - Mahonda
Mahonda-K/Mkokotoni

19.00
15.00

Lot. 6

T4

Mazizini - Fumba-Kwabakharesa

19.82

Kitogani - Paje

11.60

T7
T1
R104

R110

Lot.7
T1

Malindi jctn-Kwanyanya

10.00

T5

Mnazimmoja - U/ndege

3.00

84

Ref
U201

JINA LA BARABARA
Mtoni- Amani - K/samaki

UREFU (KM)
9.00

Jumla

239.54

85

KIAMBATANISHO 4: INAENDELEA..
Matengenezo ya kawaida barabara za lami (Routine maintenance for paved roads) zilizopangwa
kufanywa na wakandarasi/vikundi vya jamii (Contract account contract) (Ukataji wa majani, kusafisha
misingi na kuziba mashimo)
PEMBA
Ref
1

JINA LA BARABARA

UREFU (KM)

Lot.1

T32

Ole - Konde

25.50

T32

Madenjani - M/Takao

5.50

Lot.2

T31

Chajaani - Mbuguani(Mkoani)

27.50

R163

Mtuhaliwa - Chokocho

8.80

Lot.3

R178

Machomane - Vitongoji

7.00

R177

Chanjaani - U/Ndege

5.50

R179

Chake Chake - Wesha

8.00
86

Ref
4

JINA LA BARABARA

UREFU (KM)

Lot.4

R164

Mtambile - Kangani

6.4

R174

Chanjamjawiri - Tundauwa

11.0

R175

Chanjaani - Pujini

5.0

R169

3.2

R165

Kenya - Chambani
Mtambile - Mwambe

R202

Mizingani - Wambaa

9.4

9.4

Lot.5

R187

Bahanasa-Uondwe (Mtambwe)

10.36

R188

M/takao-Pandani-M/karim

13.44

R190

Kipangani-Kangagani

2.7

R195

Chwale-Likoni

1.9

R198

Mapofu-Finya Bahraini

5.5

R200

Daya-Makongeni

3.65
169.75

Jumla

87

Matengenezo ya kawaida barabara za kifusi (Routine maintenance for unpaved roads)


zilizopangwa kufanywa na Idara ya barabara (Force account contract)
UNGUJA
Ref

JINA LA BARABARA

UREFU (KM)

F413

Kwakisasi via Mwanyanyanya-Bububu school

F440

Donge- Mwanda

F412

Kama-KMKM

2.5

F421

Kijitoupele-Nyarugusu

2.5

F416

Fuoni-Kwarara

0.6

3.8
2

Jumla

11.4

88

KIAMBATANISHO 4: INAENDELEA..
Matengenezo ya sehemu Korofi (Spot improvement)
PEMBA
Ref

JINA LA BARABARA

Mkoani- Chake sehemu ya Kwachangawe


Matengenezo ya muda maalum (Periodic Maintenance)
Ref
JINA LA BARABARA

UREFU
(KM)
1.20
UREFU (KM)

UNGUJA
R101
T2

T1

Bumbwini-Kiongwe School (kwa kiwango cha kifusi)

4.3

M/kwerekwe Makaburini-Fuoni (kwa kiwango cha lami)

1.7

Tomondo Magereza - Mchina mwisho (kiwango cha lami)

1.5

Michenzani- Mtendeni (Kiwango cha lami)

0.7

Kikobweni-Mshelishelini (Kiwango cha lami)

5.28

Jumla
PEMBA

13.48

89

R199

Melitano-Madenjani (kiwango cha lami)

12.3

Pandani - Mlindo (Kiwango cha kifusi)

2.5

Jumla

14.8

Jumla yote (Unguja na Pemba)

28.28

Matengenezo ya Madaraja/Kalvati Kasha na Mitaro


Ref
JINA LA BARABARA

IDADI

Ujenzi wa kalvati kasha Unguja na Pemba


T1
R164

Bububu-Mahonda- Ujenzi wa daraja kasha la Kitope

1No

Kangani-Mkanyageni - Ujenzi wa kalvati kasha

1No

Jumla

2No

T32

Ujenzi wa Mitaro barabara za Pemba


ChakeChake-Mkoani road

0.4km

T32

Chake chake -Wete road

0.4km

Jumla

0.8km

90

KIAMBATANISHO 4: INAENDELEA..
Uwekaji wa alama za barabarani na mipaka ya miliki ya barabara
Ref

JINA LA BARABARA

IDADI

UNGUJA
Uwekaji wa alama za miliki ya barabara (Road reserve posts)
U204

Amani-Dunga road (10km)

100No

T1

Bububu - Mahonda (21km)

210No
310No

Jumla

91

Uwekaji wa alama za usalama barabarani (Road signs)


U204

Amani-Dunga road (10km)

60No

T1

Bububu - Mahonda (21km)

10No

Jumla

70No

Uchoraji wa mistari kwenye barabara (Road marking)


U201

Barabara ya Amani-Mtoni road (4km-4lines)

12,000m2
12,000m2

Jumla

92

KIAMBATANISHO NAMBA 5:
UKAGUZI WA VYOMBO VYA MOTO JULAI 2013 HADI MACHI 2014:
IDADI YA VYYOMBO VYA MOTO VILIVYOKAGULIWA
AINA
YA UKAGUZI
WA UKAGUZI
WA UKAGUZI
WA
VYOMBO
KAWAIDA
SHAKA
AJALI

GARI
MOTORCYCLE
JUMLA

UNGUJA

PEMBA

12,573
11,274
23,847

1,050
1,912
2,962

JUMLA

UNGUJA PEMBA UNGUJA PEMBA


75
22
97

13
3
16

93

548
221
769

33
7
40

14,292
13,439
27,731

Kiambatanisho 5: Inaendelea.
RUHUSA ZA NJIA NA USAFIRISHAJI
MAHALI
AINA YA HUDUMA ILIOTOLEWA
ZILIPOTOEWA

Daladala Shamba P/Hire Taxi Mizigo School

Staff H/Drive Jumla

UNGUJA

369

301

342

205

280

22

27

00

1,546

PEMBA

29

201

12

18

90

00

00

00

350

JUMLA

398

502

354

223

370

22

27

1,896

94

Kiambatanisho 5: Inaendelea.
TAKWIMU ZA MADEREVA WALIOJARIBIWA KUENDESHA VYOMBO VYA MOTO:
AINA
YA
WALIOJARIBIWA
WALIOFAULU
WALIOFELI
MADEREVA
KUENDESHA
KUENDESHA
KUENDESHA
Gari
M/c
Jumla
Gari
M/c
Jumla
Gari
M/c
Jumla
UNGUJA
2,443
1,473
3,916
1,775
1,301
3076
633
207
840
PEMBA
918
887
1,805
868
381
1,249
346
210
556
JUMLA
2,360
5,721
2,643
1,682
4,325
979
417
1,396
3,361

95

Kiambatanisho 5: Inaendelea.
UTOAJI WA LESENI KWA MADEREVA WANAFUNZI
DARAJA

B1

C1

D1

UNGUJA

34

2,511

2,646

453

290

968

308

7,218

PEMBA

478

251

75

43

13

51

74

985

JUMLA

34

2,989

2,897

81

496

303

1,019

382

8,203

96

JUMLA

Kiambatanisho 5: Inaendelea.
UKUSANYAJI WA MAPATO
S/No

Aina ya mapato

Unguja

Pemba

jumla

Majaribio ya madereva

41,288,500

7,478,500

48,767,000

Ukaguzi wa vyombo

156,270,000

16,569,500

172,839,500

Fomu za maombi

32,971,400

8,370,000

41,341,400

Kadi za njia

26,298,900

1,840,000

28,138,900

Mapato mengineyo

9,390,000

10,292,559

19,682,559

266,218,800

44,550,559

310,769,359

Jumla

97

KIAMBATANISHO NAMBA 6:
IDADI YA NDEGE ZILIZOHUDUMIWA KATIKA KIPINDI CHA JULAI 2013 HADI MACHI 2014
AINA YA

IDADI YA NDEGE

NDEGE

2012/2013
UNGUJA

PEMBA

SCHEDULE

22,369

6,096

CHARTER

13,568

CARGO

JUMLA

IDADI YA NDEGE

JUMLA

2013/2014
UNGUJA

PEMBA

28,465

21,977

7,014

28,991

236

13,804

15,257

268

15,525

124

124

PRIVATE

663

663

421

421

MILITARY

54

54

38

38

OTHERS

281

68

349

636

66

702

JUMLA

36,939

6,400

43,339

38,453

7,348

45,801

98

Kiambatanisho 6: Inaendelea.
IDADI YA ABIRIA WALIOHUDUMIWA KATIKA KIPINDI CHA JULAI 2013 HADI MACHI 2014
KIWANJA

IDADI YA ABIRIA

JUMLA

2012/2013
International

Domestic

256,637

343,468

PEMBA

37

49,582

JUMLA

256,674

393,050

UNGUJA

IDADI YA ABIRIA

JUMLA

2013/2014
International

Domestic

600,105

302,460

366,344

668,804

49,619

19

58,328

58,347

302,479

424,672

649,724

99

727,151

Kiambatanisho 6: Inaendelea.
KAMPUNI ZA NDEGE ZILIZOTUMIA KIWANJA CHA NDEGE CHA ABEID AMANI KARUME KWA
MWAKA 2013/2014
S/N
1

JINA LA KAMPUNI
Precision

VITUO
Dar,

Kilimanjaro,

NCHI INAYOTOKA
Mombasa, Tanzania

Nairobi
2

Coastal Travel

Zanzibar, Dar, Arusha,Tanga

Tanzania

Zan Air

Zanzibar, Pemba, Dar, Arusha

Tanzania

Auric Air

Dar, Zanzibar, Pemba

Tanzania

Flight Link

Dar, Zanzibar, Pemba

Tanzania

Air Advanture

Zanzibar, Dar, Arusha

Tanzania

As Salam Air

Dar, Zanzibar, Pemba,Tanga

Tanzania

100

S/N

JINA LA KAMPUNI

VITUO

NCHI INAYOTOKA

Pelican Air

Dar, Zanzibar

Tanzania

Regional Air

Dar, Zanzibar

Tanzania

10

Safari Air Link

Dar, Zanzibar

Tanzania

11

Shine Aviation

Dar, Zanzibar

Tanzania

12

Tanzan Air

Dar, Zanzibar

Tanzania

13

Tropical Air

Dar, Zanzibar, Pemba ,Arusha

Tanzania

14

Zenith Aviation

Dar, Zanzibar, Pemba

Tanzania

15

Twin Wing

Dar, Zanzibar

Tanzania

16

Air Excel

Zanzibar, Dar, Arusha

Tanzania

17

Fast Jet

Kilimanjaro, Zanzibar

Tanzania

18

Ethiopian Airline

Addis- Ababa

Ethiopia

19

540 Aviation

Mombasa, Nairobi

Kenya

20

Kenya Airways

Mombasa, Nairobi

101

Kenya

S/N

JINA LA KAMPUNI

VITUO

NCHI INAYOTOKA

21

Meridian Fly

Milan, Malpensa

Italy

22

Condor

Frankfut, Mombasa

Germany

23

Tui Airline

Brussels

Belgium

24

Travel Service

Budapest

Hungary

25

Neos Air

Milan

Italy

26

Oman Air

Muscat

Oman

27

Livingstone

Milan, Mombasa

Italy

28

Arkefly

Amsterdam, Huhgada, Mombasa

Netherlands

29

Alitalia

Milan, Mombasa

Italy

30

Mango

Johannesburg

South Africa

31

Xl Airways France

France

France

102

KIAMBATANISHO NAMBA 7:
ORODHA YA MELI ZILIZOSAJILIWA CHINI YA USAJILI WA NDANI ( LOCAL REGISTRY )
KIPINDI CHA
JULY 2013 MACHI 2014
S/N
1.
2.
3.
4.
5.
6.
7.
8.
9.
10.
11.
12.

JINA LA MELI
FATMAH-ZEHRA
COMARCO 185
CORMACO 186
CORMACO 184
NGATI HAKA
BERKAT MENJALA N0. 23
SEMUDERA PACIFIC NO. 3
ALRABEE1
FATIMA (EX TORGELOW)
MUNEERA ( EX SEMLOW)
TANYA
MEISA

UZITO (GRT)
341.38
629
629
629
258
587
498
1515
299.48
299
1295
949

103

S/N
13.
14.
15

JINA LA MELI
SVS GUARDSMAN
SVS AVERY
MARTIAL
JUMLA

UZITO (GRT)
168
168
863
9,127.86

104

Kiambatanisho 7: Inaendelea.
MELI ZILIZOSAJILIWA CHINI YA USAJILI KUPITIA TANZANIA ZANZIBAR
INTERNATIONAL REGISTER OF SHIPPING KIPINDI CHA JULY 2013 MACHI 2014
S/N
1
2.
3.
4.
5.
6.
7.
8.
9.
10.
11
12.
13.

Name of Vessel

UZITO (GRT)

RANYRAN
CANTE
ARABIAN SUN 2
SEA BIRD 1
SEA BIRD 3
AURIGA
TABUN
SAN JOSE
MED STAR
MEGAH CEMENT
PENTA
SYMPHONY
BARAWATI

479
13,322
412
215
248
55,962
26639
168
3,909
6,774
387.24
44190
55042

105

S/N
14.
15.
16.
17.
18.
19.
20.
21.
22.
23.
24.
25.
26.
27.
28.
29.
30.
31.

Name of Vessel
PERGIWO
RODE
SEA BREEZE
AL KHALEEJ 1
Vare
Danhaibianmao 171
Danhaibianmao 187
Danhaibianmao 189
Shuang Yang
SSE Angelina
Hai Jie
Harmony Liverstock
SSE Rhonica
Pendora
Roula
Kathy
Hamza 5
Sulaiman

UZITO (GRT)
23496
20818
5306
359
17183
125
125
125
199
158
198
2062
30
49.6
11506
203
224
161
106

S/N
32.
33.
34.
35.
36.
37.
38.
39.
40.
41.
42.
43.
44.
45.
46.
47.
48.
49.

Name of Vessel
Capricorn
Quality
Falcon 1
Onassis
Friendship I
Al Khaleej 4
Santa Cruz
Revana
Crystal Sun
Zheng Ying
Grann. St. Anne
Lampunchai
Mandalay
Hao Xiang 66
Malak
New Falcon
Rahma
Ang Quan

UZITO (GRT)
2187
712
861
671
683
205
179
1288
4722
168
1048
1381
420
1967
1040
4066
1473
11042
107

S/N
50.
51.
52.
53.
54.
55.
56.
57.
58.
59.
60.
61.
62.

Name of Vessel
Heng Yang 77
Delta 1
Revana I
Al Wakra
Hong Yuan
Gulf Trader
Chang Da
Chun Hing N0. 1
Sea Sul I
SL-D10
Hamal
Munsu
Victoria Star
JUMLA

UZITO (GRT)
375
2867
1332
3423
643
1197
124
177
2472
958
422
675
1485
343,653.84

108

KIAMBATANISHO NAMBA 8:
HUDUMA ZA MELI

S/NO

AINA YA MELI

1.

Meli za Nje

2.

Uzito wa Meli (GRT)

3.
4.

KIPINDI

ONGEZEKO/

JULAI, 2012

JULAI 2013

MACHI, 2013

MACHI, 2014

PUNGUZO (%)

133

152

14.29

1,929,141

2,227,955

15.49

Meli za Ndani

4,050

2,913

(28.07)

Mjahazi

4,456

4,617

3.61

109

Kiambatanisho 8: Inaendelea.
HUDUMA ZA MIZIGO

KIPINDI
S/NO

1.
2.
3.
4.
5.
6.

AINA YA MIZIGO

Mzigo Mchanganyiko
Makontena
Mafuta
Mzigo wa Majahazi
Abiria wa Ndani
Abiria wa Kigeni

JULAI, 2012
MACHI, 2013
53,245
38,341
26,711
83,785
1,641,849
2,053

110

JULAI, 2013
MACHI, 2014
49,363
44,276
40,133
116,802
1,776,101
2,654

ONGEZEKO/ PUNGUZO
(%)

(7.29)
15.48
50.25
39.41
8.18
29.27

You might also like