Professional Documents
Culture Documents
ANNUUR 1164a
ANNUUR 1164a
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1164 RABIUL THANI 1436, IJUMAA , FEBRUARI 13-19, 2015 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
Uk.14
Wanahitaji na kutaraji
vyama vyao vya siasa
wanavyoviamini na
k u v i k u b a l i k u wa
vitawafikisha pazuri.
Lakini huenda
watakubali wasipige
kura au wauze
MMOJA wa waliokuwa
Masultan wa Zanzibar.
Tahariri/Makala ya Mtangazaji
AN-NUUR
AN-NUUR
STOCKHOLM (WAFA)
President Mahmoud Abbas
Tuesday expressed hope that
the Swedish recognition of
the state of Palestine will
leverage the international
communitys support of the
Palestinians' just cause.
Abbas commended
Swedens recent recognition
of Palestine as in independent
state, which, according to
him, bolsters the Palestinian
peoples struggle toward
freedom and independence.
He called upon other
Habari
AN-NUUR
Na Bakari Mwakangwale
MFUNGWA aliyeingia
gerezani Segerea akiitwa
Collins Javan Omundi,
ametoka akibeba jina la
Muhammad.
Neno, Al-Shabaab,
ndio limekuwa sababu ya
mfungwa huyo kusilimu,
akiacha imani yake ya awali
ya Kikristo.
Akisimulia kisa cha
kusilimu kwake, Omundi
anasema kuwa, alivyokuwa
akifahamu ni kuwa AlShabaab, ina maana ya
gaidi hatari na katili.
Kwa tafsiri na ufahamu
huo, anasema, ilikuwa ni
jambo la kushtua kwake
alipoingia gerezani na
kukutana na mtu anaitwa
Al-Shabaab.
Mfungwa huyo raia wa
Kenya, ambaye baada ya
kusilimu alichagua jina la
Muhammad, akiongea na
mwandishi wa habari hizi
muda mchache baada ya
kutoka gerezani, alisema
nchini Kenya, neno AlShabab ni kitu hatari sana
kutokana na matukio
yanayohusishwa na kundi
hilo.
Bw. Mohammed alisema,
a k i wa g e r e z a n i h u m o
alisilimishwa na Masheikh
Mselem na Farid, baada ya
kukutana na kijana mmoja
wa Kiislamu, maarufu
gerezani humo kwa jina
la Al-Shabab, ambaye
waliingia naye katika
mjadala wa hoja kuhusu
Dini ya Uislamu na Ukristo.
Anasema, ule ukaribu
wake na Shabani akitaka
kujua ni kwa nini alijiita
jina baya kama hilo, ndio
kukazaa urafiki uliokuja
kuibua mjadala wa mambo
ya kidini na hatimaye
kusilimu.
Bw. Mohammed, ambaye
alijikuta anahukumiwa
kwenda jela kwa kosa
la kupatwa na hatia ya
kuwepo nchini kinyume
cha sheria, alisema baada
ya kuingia gerezani humo
kwa mara ya kwanza akiwa
mahabusu, alistuka kusikia
kijana huyo akiitwa AlShabab na wenzake na
huku akifurahia jina hilo.
Anasema, alisilimu
Januari 7, 2015, baada ya
kuwa mahabusu na kujikuta
anaanza kudadisi mambo
ya kiimani baada ya kusikia
kijana mmoja aliyemkuta
humo mahabusu, akiitwa
Al-Shabab.
Bw. Mohammed, alisema
huyo kijana jina lake halisi
ni Shaban, lakini humo
gerezani anajulikana zaidi
yanayohusu Uislamu.
Alisema, katika muda
aliokaa na Masheikh
wa n a o t u h u m i wa k wa
ugaidi, walimfundisha nini
Uislamu na kuzidi kubaini
kiundani kuwa Uislamu
ni dini nzuri kinyume na
inavyochafuliwa kupitia
propaganda.
Nimesilimu nikiwa
gerezani, sasa nimetoka
nataka niusome zaidi
Uisamu ili nipate kuwa
muelimishaji kuhusu
Uislamu. Nataka nije
nikutane tena na ndugu
zangu niliowaacha
gerezani na mimi nikiwa
Muislamu haswa. Alisema
Bw. Mohammed.
Alisema, baada ya
k usilimu alifurahi na
SHEIKH Ponda Issa Ponda akiongozwa na makachero wa polisi muda mfupi baada
ya kesi yake kusikilizwa.
4
MTU yoyote hii leo ikiwa ataingia
katika mitandao ya kijamii na
kusoma mjadala unaofanyika
kuhusu Mahakama ya Kadhi,
ni lazima atapata mshtuko
mkubwa kutokana na lugha
kali na wakati mwingine matusi
kati ya hao wanaojadiliana. Kila
upande ukitupa shutuma na
maneno makali dhidi ya upande
mwingine. Ukipitia majadiliano
yote kitu kimoja kinachojitokeza
wazi na dhahiri kabisa ni kuwa
kuna mpasuko mkubwa kati ya
Waislamu na Wakristo kuhusu
Mahakama ya Kadhi. Chuki na
uadui sasa upo wazi bila kificho.
Hili linawezekana vipi wakati
viongozi wetu wanatuambia
kuwa Baba wa Taifa alituachia
misingi imara ya umoja? Wahenga
wamesema dalili ya mvua ni
mawingu. Suali la kujiuliza ni hili,
wapi sisi kama taifa tumejikwaa?
Wengi katika hao wanaojadili
h i y o M a h a k a m a ya K a d h i
ukweli ni kuwa hawaijui vyema
historia ya Tanzania au ukipenda
Tanganyika. Wengi katika hawa
waliojizinga katika malumbano
haya, baadhi ni watu wazima
walio na umri zaidi ya miaka 50
na vijana ambao wamezaliwa
baada ya Tanganyika kupata
uhuru wake mwaka 1961. Mjadala
unafanyika katika mazingira ya
ujinga wa kutojua historia. Sasa
hapa linakuja swali, imekuwaje
kuwa watu hawa ambao kwa sasa
ndiyo wengi katika jamii yetu hii
leo hawaijua historia ya nchi yao?
Vipi tumekuwa na Chuo Kikuu
kwa karibu ya nusu karne na sasa
vimeongezeka vingine vingi,
lakini hadi sasa ikawa historia
yetu ni ya kubabaisha haijakaa
sawa hadi leo? Mimi sitatoa jibu
kwa sasa ingawa jibu ninalo.
Huko vyuoni ni historia gani
inasomeshwa ambayo inawafanya
watu wasijijue?
Baadhi ya wachangiaji katika
h i y o m i t a n d a o ya k i j a m i i
na inaelekea hao ni Wakristo,
wanasema iweje Mahakama ya
Kadhi igharimiwe na serikali ilhali
serikali hii haina dini? Waislamu
wanaleta jibu wakisema mbona
serikali inatoa mabilioni kila
mwaka kwa makanisa kuhudumia
taasisi zao kupitia Memorandum
of Understanding (MoU)? Kwa
wale ambao labda hawaujui huu
mkataba ni kuwa mwaka wa 1992
Serikali ya Tanzania ilitiliana
sahihi mkataba na makanisa,
mkataba uliokuja kujulikana kama
Memorandum of Understanding.
Makubaliano ambayo serikali
iliridhia na kuidhinisha elimu,
h u d u m a z a j a m i i n a a f ya
ziendeshwe na Christian Council
of Tanzania (CCT) na Tanzania
Episcopal Conference (TEC) kwa
kushirikiana na serikali. Mkataba
huu ulitayarishwa na Dr. Costa
Mahalu, wa Kitivo cha Sheria
Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam
na ukatiwa sahihi na Waziri
wa Nchi katika Ofisi ya Waziri
Mkuu, wakati huo Mheshimiwa
Edward Lowassa. Kikubwa
katika mkataba huu kwanza ni
Makala
Mahakama ya Kadhi:
AN-NUUR
U k we l i n i k u wa u k o l o n i
umeingia Tanganyika umekuta
Waislamu wakijihukumu kwa
kitabu chao. Mmishionari
Johan Krapf kaja Tanganyika na
alipokelewa na Chifu Kimweri
wa Usambaa mwaka 1848. Krapf
alipokelewa kwa ukarimu wa
hali ya juu na alimkuta Chifu
Kimweri Muislamu, anajua
kusoma na kuandika kwa herufi
za Kiarabu akihukumu katika
barza yake iliyokuwa Vuga.
Ni wazi kuwa Chifu Kimweri
hakuwa anahukumu kutoka,
Order in Council, kutoka India
kwani Waingereza walikuwa bado
hawajafika.
Chifu Kimweri alikuwa
anahukumu kwa sheria kama
walivyohukumiana Waislamu
katika ukanda wa pwani ya Afrika
Mashariki kwa miaka mingi. Mimi
nimekuwa na kupata fahamu
katika Tanganyika ya 1950/60
na nina kumbukumbu za hizi
mahakama za kadhi na baadhi
ya hawa mahakimu nimewaona
kwa macho yangu ama wakiwa
katika mahakama wakihukumu
na wengine nimewaona mitaani
na wengine nimewaona
wakisuhubiana na wazee wangu.
Namkumbuka Sheikh Abdallah
Simba kutoka Songea. Nikifumba
macho ni kama vile namuona
Sheikh Abdallah Simba. Alikuwa
kija Dar es Salaam na Land Rover
yake mwenyewe na siku zote
akivaa kanzu, koti na tarbush.
Sheikh Abdallah Simba alikuwa
AN-NUUR
Makala
hawakuwahi kufikishwa
mahakamani au kufunguliwa
mashtaka.
Jaji
Schomburg
amekumbusha kuwa bila
kuwepo kwa mahakama
maalumu ya Umoja wa
Mataifa, watu wengi
waliosababisha maafa ya
Wa n ya r wa n d a wa p a t a o
800,000 wangeweza
kuukwepa mkono wa sheria.
Pamoja na hayo, Jaji huyo
wa zamani amekosoa pia
namna ambavyo Jumuiya ya
Kimataifa ilichelewa kuingilia
kati mgogoro wa Rwanda
hadi pale ambapo mamia
kwa maelfu ya raia, wengi
wao Watutsi, walipokuwa
tayari wameuliwa.
"Hata mahakama ya Umoja
wa Mataifa inayoshughulikia
mauaji ya kimbari ya Rwanda
ilianzishwa kwa kuchelewa.
Mahakama hiyo ilipaswa
iundwe mwishoni mwa
mwaka 1993 au mwanzoni
mwa 1994", alikosoa Jaji
Schomburg.
Jaji huyo, ambaye alifanya
kazi kwenye mahakama
hiyo kuanzia mwaka 2001
hadi 2008, hakuishia hapo.
Alielezea kushangazwa
kwake na ukweli kwamba
hakuna Mfaransa hata mmoja
aliyefunguliwa mashtaka,
licha ya kwamba baadhi ya
Wafaransa walituhumiwa
kuuza silaha nchini Rwanda
katika miaka ya 1990s na
kwamba, wakati mwingine
hata walizigawa silaha hizo
kwa Wahutu.
Alisema wakati fulani
serikali ya Rwanda ilijaribu
kuwafungulia mashtaka
wahusika, lakini bila
mafanikio. Jaji Schomburg
anasema Ufaransa haina
nia ya kweli kufanya
uchunguzi wa kipindi hicho
kilichogubikwa na giza.
Hata hivyo Jaji Schomburg
ameisifu mahakama ya Umoja
wa Mataifa ya kushughulikia
mauaji ya kimbari ya
Rwanda, kwa kupiga hatua
za haraka kuwawajibisha
wahusika na kuwapatia
haki wale walioonewa na
hii imekwenda haraka
hata kuliko vile ambavyo
Ujerumani ilivyoendesha
kesi za waliohusika katika
mauaji ya Wayahudi chini ya
utawala wa Wanazi. (DW).
PAPA Francis.
ya Mapinduzi ya Kiislamu
ya nchini Iran, Kamanda
Habibullah Sayyari, alisema
kuwa, hivi sasa taifa la Iran
linajivunia juhudi za wasomi
na vijana wake, ambao
wameweza kuzalisha aina
mbalimbali za silaha na zana
za kisasa kabisa kwa kiwango
cha kimataifa.
Aliyataja mafanikio
hayo kuwa ni mwiba
kwenye macho ya maadui
wasiolitakia mema taifa na
watu wa Iran ya Kiislamu.
Aidha ameelezea matatizo
yaliyokuwa yakilikabili
jeshi la Iran katika kipindi
c h a u t a wa l a wa S h a h ,
kutokana na kufuata
kibubusa siasa za Marekani
na kuongeza kuwa, wakati
ule maamuzi na mipango
yote yaliyokuwa yakihusu
zana, silaha, mazoezi ya
kijeshi na mambo mengine
yalikuwa yakichukuliwa
n a Wa s h i n g t o n b i l a ya
kuwahusisha wataalamu wa
Iran, suala ambalo liliifanya
Iran kubakia tegemezi wakati
wote.
MATAMSHI ya Rais wa
Marekani, Barack Obama,
ya k u wa t a k a Wa k r i s t o
kutambua kwamba Uislamu
si dini pekee inayohusishwa
na vurugu na mauaji, na
kwamba Vita vya Msalaba
n a v i t e n d o v ya u g a i d i
vinavyofanywa na vikundi
vyenye misimamo mikali.
Rais Obama alitoa kauli
hiyo wiki iliyopita, katika
siku ya taifa ya maombi,
alipofananisha Vita vya
Msalaba na vitendo vya
ugaidi vinavyofanywa na
vikundi vyenye misimamo
mikali.
Rais Obama aliongeza
kuwa, wakati wa vita
vitakatifu, watu walifanya
vitendo vya kutisha kwa jina
la Kristo. Alisisitiza kuwa
nchini Marekani, utumwa
na sheria za kibaguzi, zote
pia zilihalalishwa kwa jina
la Kristo.
Kauli hiyo imezua
mtafaruku duniani na baadhi
wameanza kuhoji kama
kiongozi huyo wa kwanza
mweusi wa Marekani ni
Mkristo.
Kwenye hotuba yake hiyo,
Rais Obama alilitaja kundi la
Daesh kuwa limeasi Uislamu
kwa kutenda jinai na vitendo
vya kikatili katika eneo la
Mashariki ya Kati.
Makundi kama ya Daesh
yamekuwa yakitekeleza jinai
na mauaji dhidi ya watu wasio
na hatia kwa kupata misaada
ya kifedha na kisilaha kutoka
nchi za Magharibi na baadhi
ya nchi za Kiarabu za Ghuba
ya Uajemi. (irib).
6
QURAN tukufu ni kitabu
cha Mwenyezi Mungu
kilichoteremshwa juu
ya moyo wa Mtume
Muhammad (S.A.W.) ili
aiongoze kwayo jinsi ya
wanadamu na ili utulizane
juu yake ulimwengu. Kwa
hiyo Quran juu yake
kutasimama kiyama cha
ulimwengu. Na kwa hiyo
Quran anapozwa mwenye
kupozwa na anafanikiwa
mwenye kufanikiwa.
Quran inatunyanyua juu
ya ulimwengu. Isipokuwa
ni kwamba haitaki
kwetu kujitoa katika huo
ulimwengu. Inapanda na
sisi juu ya ulimwengu,
wakati ambapo inataka
kwetu tuzinduke kwa
yaliyo madogo sana
katika mafungu yake, kwa
kawaida na mazoea, na
inazama na sisi kutupeleka
kwenye vina vilivyo zama
sana kwa binadamu ili
tusikilize pamoja kwenye
maungulio ya raho yake
ambayo yamejificha
sana na maumivu yaliyo
manyonge sana ya moyo
wake.
Quran inatuchukua
na kutupeleka kwenye
maeneo mapya ambayo
hayajagunduliwa katika
maeneo ya roho, na
inakwenda na sisi kwenye
vipeo vyenye kutisha na
vilele vya juu sana kisha
inatutahadharisha na
kugeuka nyuma. Na kama
si hivyo, tutapatwa na
SAHABA mmoja
aliwahi kumwomba
Mtume (s.a.w.) awape
taarifa kumhusu yeye
mwenyewe. Naye
akawaambia hivi:
"Mimi ndiye mtu ambaye
Ibrahim (a.s.) aliomba nije,
na ambaye Yesu (Nabii
Isa ibn Maryam) (a.s.)
alitangaza hahari njema
za ujio wangu.
Usemi huu unadokeza
aya zifuatazo za Qur an:
Ewe Mola mlezi
wetu! Waletee Mtume
a n a ye t o k a n a n a wa o ,
a wa s o m e e a ya z a k o ,
na awafundishe Kitabu
(chako) na hikima
(nyingine) na awatakase
(na kila mabaya). Hakika
wewe ndiwe mwenye
nguvu, mwenye hekima
(Surat Al-Baqarah, 2:129).
Na Isa bin Mariamu
aliposema: Enyi Wana
wa Israili! Hakika mimi
ni Mtume wa Mwenyezi
Mungu
kwenu,
ninayethibitisha yaliyo
kuwa kabla yangu katika
Ta u r a t i , n a m w e n y e
kubashiria habari njema za
kuja Mtume atakayekuja
baada yangu; ambaye jina
lake litakuwa ni Ahmad
Makala
AN-NUUR
Mwangaza wa Quran
(Muhammad)! Lakini
alipowaletea hoja zilizo
wazi, walisema: Huu ni
uchawi ulio dhaahiri!"
(Surat As-Saff, 61:6).
M t u m e ( s . a . w . ) wa
Allah (s.w.t.) alikuwa
akitazamiwa au akingojewa
kuwa atakuja. Manabii
w o t e wa l i o m t a n g u l i a
walimwongelea Mtume
(s.a.w.) na walitabiri ujio
wake.
Aya ya Qur'an 3:81
inataja waziwazi kuwa
Mola (s.w.t.) Alifanya
Kiaga (covenant)
maalum na Manabii
kwamba watamwamini
na watamsaidia Mjumbe
huyo atakayekuja baada
yao na atakayethibitisha
ujumbe waliouleta wao.
N a p a l e M we n ye z i
Mungu Alipochukua
ahadi (kiaga) kwa Manabii:
Nikisha kukupeni
Kitabu na hikima, kisha
akakujieni Mtume mwenye
kusadikisha mliyonayo, ni
akamwondokea kutoka
Seiri, aliangaza kutoka
kilima cha Paran, akaja
Meribath-kadeshi. Upande
wa mkono wake wa kuume
palikuwa na sheria moto
moto kwao.
[NB. Tafsiri hii ni ya
Biblia ya Kiswahili ya
"Bible Societies of Kenya and
Tanzania, Union Version,
1952".
Tafsiri hii inakanganya
makusudi hapo inapotaja
'Merebath Kadesh na
kutowataja masahaba au
watakatifu 10,000 kama
ziandikavyo tafsiri nyingi
za Kiingereza (na za lugha
zingine za kigeni) kama
Biblia hii "Authorized
King James Version, 1979",
ambayo imeandika hivi:
"Deuteronomy 33:2 And
he (Moses) said, The Lord
came from Sinai and rose
up from Se'ir unto them;
he shined forth from mount
Paran, and he came with ten
thousand saints: from his
kwetu na yasiyoonekana
katika ulimwengu. Nayo
inatufundisha kwamba,
yule ambaye hakuwa
mmoja katika dhati yake,
hakuungana katika fikra
ya k e h a k u k u s a n y i k a
katika hisia yake hatakuwa
na fungu lolote katika
maonekano ya nuru za
umoja na upweke kwa
sababu imani ya kweli ni
ile ambayo inachimbuka
kutoka katika uwepo wa
binadamu kwa ujumla
wake. Na Quran baada
ya hapo, ni chemchem ya
nguvu yenye kumiminika
kutokana na nguvu
zisizoonekana ili wapate
nguvu kwa hiyo Quran
wany ong e na wa pat e
uhai kwayo wafu, na hiyo
Quran ndiyo akili ambayo
imepelekwa kwa ajili ya
wazimu wa nyakati zote na
ni mionzi ya roho ya tangu
juu ya viza vya nyoyo
na nafsi kwani matamko
yake yamebebeshwa
mawingu ya uhai na aya
zake zinatona umande
wa uzuri na utukufu.
Na kwa kiasi ambacho
mwanadamu anakosa
kuijuwa Quran, kunakuwa
kutoijuwa kwake nafsi
yake na ulimwengu ulio
pambizoni mwake.
Kwa hakika hiyo
Quran, ndiyo uamsho wa
utashi wa upwekeshaji
na maumbile yake
kutoka katika maficho ya
Inaendelea Uk. 7
right hand sent a fiery law
for them.
Ambayo tafsiri yake
halisi ya Kiswahili ni kama
ifuatavyo:
"Kumbukumbu la
Torati 33:2 naye (Musa)
alikuja kutoka Sinai,
akawaondokea kutoka
Seiri kuja kwao; Aliangaza
kutoka kilima cha Parani,
na alikuja na watakatifu
elfu kumi. Kutoka katika
mkono wake wa kuume
ilikuja sheria motomoto
kwa ajili yao.
Aya hii ya Torati
inaongelea kwa pamoja
juu ya Nabii Musa, Nabii
Isa (Yesu, na Muhammad
(a.s.). Kwa mfano ikitaja
Sinai kule ndiko Nabii
Musa (a.s.) alikoongea
na Mwenyezi Mung u
(s.w.t.) akapewa Kitabu
cha Taurati (Torati).
Inapoitaja Seiri, pale
ni mahali huko Palestina,
a m b a k o Ye s u ( a . s . )
alipokea Wahyi (Ufunuo
wa Kiungu). Na ikitajwa
Paran, ndiko ambako
Mwenyezi Mungu
(s.w.t) Alikojidhihirisha
Yeye Mwenyewe kwa
walimwengu kwa mara ya
Inaendelea Uk. 7
7
Inatoka Uk. 6
mwanadamu. Na hiyo
Quran, ndiyo dhati ya
ulimwengu na moyo wake.
Ni akili ngapi imepanda
juu nazo? Hakika kanuni
za maumbile na taratibu za
ulimwengu, zinaungana
katika mbingu ya matamko
ya k e n a a ya z a k e n a
katikati yake inalala akili
yote na kutokana nayo
inanusa pumzi za maisha
na ndani yake zinaungana
nguvu za maumbile
na ubora na vyote
hivyo vinazama katika
mmiminiko la mapenzi ya
Mwenyezi Mungu nayo
inazitia nguvu, nguvu za
vitambuzi na inafungua
madirisha ya fikra na
inawasha mageuzi ya
hamu katika shina la nyoyo
na roho. Ama wabora wa
fikra, wao wanakuta humo
ubora wote na ushujaa
wote, na ukubwa wote. Ni
fikra ngapi imezifitini? Na
muonjaji sana imemathiri?
Na ufasaha umepiga na
umeinama kwa sababu ya
ufasaha wake?
Kwa hakika Quran
imechanachana sanda
za ukimya kuhusiana
na utume uliopita, na
imewasimamisha Mitume
waliyotangulia kutoka
katika malazi yao na
imewatamkisha ili waseme
tamko la ukweli kuhusu
Muhammad (s.a.w.) na ili
aliwazike kwa pumzi zao
na aufuate mwenendo wao
na kwa yale waliyoyapata
miongoni mwa ushupavu
wa watu wao na yale
Inatoka Uk. 6
mwisho kwa Wahyi Wake
Aliyompelekea Nabii
Muhammad (s.a. w).
Paran ni safu ya milima
kule Makka. Imetajwa
katika Taurat na Torati ya
Biblia katika aya nyingi
pamoja na aya hii ifuatayo:
Mwanzo 21:19,21, kuwa
mahali pale ni jangwani
ambako Hajiri (Hagar )
alikoachwa na mume
wake, lbrahimu (a.s.) ili
aishi na mwanawe, Ismail
( au Ishmael) aliyekuwa
mwana wa kwanza wa
Nabii Ibrahim na mkewe
Hajiri, na kwa kuwa wote
wawili, hususani mwanae
Ismail, walikuwa na kiu
sana, Mwenyezi Mungu
(s. w.t) akamtengenezea
k i s i m a ( c h a m a j i ya
Zamzam).
Kumbuka kuwa
Muhammad (s.a.w) ni
kizazi cha Nabii Ismail
(Ishmael), wakati Yesu ni
kizazi cha Is-haq (Isaka
au Isac) na wote wawili,
Muhammad na Yesu na
babu zao wakuu (wahenga
wao), yaani Ismail na Is-
Makala
AN-NUUR
Mwangaza wa Quran
waliyoyamiminiwa juu
yao miongoni mwa uovu
na adhabu.
Kwa hakika ametikisa
Muhammad (s.a.w.) kwa
ulingano wake moyo wa
mbingu zikakungutika
mpaka zikawa ni ziaka
la mishale ya moto
inayochomoka iliyozipata
nyoyo za mashetani
na wafuasi wao katika
mushirikina popote
watakapokutwa na
vyovyote watakavyokuwa.
Kati ya moyo wa
Muhammad (s.a.w.) na
moyo wa Al-Kaaba, pana
hamu yenye kubadilishwa
ya ndani na yenye kina
sana. Imezama katika
uzamani, hiyo Al-Kaaba
ni pacha wake katika
kupatikana. Nayo ni nusu
ya dhati yake na ni baadhi
ya mafungu ya johari
ya hakika yake katika
vioo vya ulimwengu wa
mfano. Na siku ambayo
Makkah iliweka amana
yake iliyo ghali mbele ya
ulimwengu, yaliifinika
Al-Kaaba maungu ya
huzuni kwa sababu ya
yale yatakayoletwa na
m a s i k u ya j a y o h u k o
mbele miongoni mwa
kufariqiana na kutengana
kulikopangwa, ambako
hapana makimbilio yoyote
na kutuka kwake kabla ya
makadirio kutoa nafasi na
k a t i k a m a wa z o ya k e
fikra na maana mapya
yaliyoongezwa ambayo
aya zinayachukua
kutokana na muundo wake
wa kilugha na wakifasihi
na hazivuki mpaka kabisa
katika kuwa mbali na
misingi ya tafsiri na nguzo
zake zenye kujulikana.
Hapana shaka kwamba
mawazo haya yalitolewa
na mazingira ya wakati wa
wakati huu na yaliyafunua
hayo maarifa ya wakati
huu na elimu zake na
maelekezo yake ya kifikra
na ya kiroho na Mwenyezi
Mungu amrehemu AnNours ambaye alisema:
Hakika zama ni mfasiri
mkubwa sana wa Quran.
Na mimi nina matumaini
makubwa sana kwamba
mawazo haya kuhusiana
na baadhi ya aya za Quran
tukufu yatapata mwangwi
mpana sana katika fikra
ya msomaji wa Kiarabu
n a h i s i a ya k e , k wa n i
kuyafasiri haya matendo
ya wito na ya kifikra ya
Al-Ustadh Fathullah
kwenda kwenye lugha
ya Kiarabu ni kitendo cha
kuzichangamsha fikra na
kazi hizi ni kubadilisha
katika uwanja wa maarifa
ambako ni kuzuri sana
kali ya akili za wenye
kushughulika na mambo
ya imani na masuala ya
Uislamu hapa Uturuki na
huko katika ulimwengu
wa Kiarabu.
N i n a m u o m b a
Mwenyezi Mungu amlipe
kutokana nasi Al-Ustadh
aliye mbora Fethullah
Gullen malipo na rehma
ya M we n ye z i M u n g u
mwenye uwezo mkubwa
sana, ayaweke malipo
hayo katika madaftari ya
matendo yake katika siku
ambayo hayatafaa mali
wala watoto isipokuwa
kwa atakayemwendea
Mwenyezi Mung u na
moyo uliyosalimika.
Ya e l e w e h a y o , n a
sifa njema anazistahiki
Mwenyezi Mungu
m wa n z o n a m w i s h o .
Arehemu Mwenyezi
Mungu na aokoe na
abarikiwe juu ya mwisho
wa Manabii na Bwana
wa Mitume Muhammad
(s.a.w.) aliye mwaminifu
na juu ya jamaa zake na
maswahaba zake wote.
(Huu ni utangulizi
kama ulivyoandikwa na
Adib Ibrahim A-Dabbaqh
wa Kitabu Miyangaza
ya Quran katika mbingu
ya hisia kilichotungwa
na Muhammad Fethullah
Gullen. Kimefasiriwa
kutoka Lugha ya Kiarabu
kuja katika Kiswahili na
Sheikh Suleiman Amran
Kilemile.)
(Mwa 21:15)
Na k a m a t uj ua v y o ,
kisima cha Zamzam pia
kiko katika eneo lile Parani
(yaani kule Makka), kama
ilivyosema Qur'an:
M o l a we t u M l e z i !
Hakika mimi nimewaweka
baadhi ya dhuriya zangu
(Hajara na Ismaili) katika
bonde (hili la Makka) lisilo
kuwa na mimea, kwenye
Nyumba yako takatifu
(ya Al- Kaaba), ewe Mola
wetu Mlezi, ili washike
swala, Basi zijaalie nyoyo
za watu zielekee kwao,
na waruzuku matunda,
ili wapate kushukuru.
(Surar Ibrahim, 14:37).
Ni kwa sababu ya tabiri
za dhahiri kama hizi
ndani hata ya Taurati (ya
watu wa Kitabu, yaani
Mayahudi na Wakristo),
ndiyo Mayahudi walimjua
na kumtazamia kuja Nabii
wa Mwisho, na wakajua
kwamba atatokezea kule
Parani, yaani Makka.
Hiyo
aya
ya
Kumbukumbu la Torati
( D e u t e r o n o m y ) , k wa
mujibu wa Makala ya
Kiarabu iliyopigwa chapa
j i j i ni L o nd o n m na m o
mwak wa 1944, imeandika
kama hivi:
Deuteronomy 33:2 He
came with myriads of holy
ones, in his right hand was
an axe of fire with two edges.
Ambayo maanaye
kwa Kiswahili ni kama
i f u a t a v y o : A l i k u j a
n a wa t a k a t i f u we n g i
(maswahaba) na katika
mkono wake wa kuume
akiwa na shoka (jambia)
lenye ncha mbili.
(Kumbukumbu la Torati
33:2)
Aya hii inaongelea juu
ya Nabii aliyetabiriwa
ambaye atakuja na
maswahaba wengi ambao
ni watakatifu sana, na
ataruhusiwa na ataamriwa
kupigana na maadui zake
wakimchokoza.
(Uchambuzi wa Maisha
ya Nabii Muhammad,
kama ilivyoandikwa na
M. Fetullah Gulen.)
Makala
AN-NUUR
lakini hawakupewa
ushindi yaani waliibiwa
na kuporwa ushindi wao.
Tangu hapo hadi leo, huo
ndio umekuwa wimbo wao
wa kuwadanganya wananchi
ambao hadi sasa hawajaamka
kuwa CUF ni chama cha
watu tu wenye kuwachezea
mchezo fulani wa kisanii ili
kupata maslahi yao binafsi na
hata sio ya kichama angalau.
CCM, ilikuwa na iko kama
hivyo tangu zamani. Na kwa
bahati mbaya, CUF imefuata
nyayo hizo hizo. CCM ya leo
imejaa viongozi wabinafsi.
Ubinafsi huzaa ufisadi.
CCM imejaa watu wasio
na uchungu na nchi yao na
hata hawawaonelei huruma
wananchi wanaowaongoza.
Nayo CUF imefuata nyayo
hizo hizo tena. Kwa mfano,
mchakato wa kuwapata
wabunge na wawakilishi
wa CUF umejaa ukiritimba.
Na hata hao viongozi
wenyewe wa majimbo
wakishapatikana, huoni
wanachokifanya majimboni
zaidi ya ujasiriamali wao
binafsi.
Ndani ya CUF kuna watu
a m b a o n d i o n g u z o ya
kipembe ya CUF. Lakini
kisichojulikana ni kuwa
nguzo hiyo haimaniki wala
haitegemeki kwa sababu ni
mbovu na ndio chanzo cha
chama cha CUF kubwagwa
hata kikishinda uchaguzi
kwa asilimia mia ngapi!
Tusiwasahau na wale
waliojivisha mbawa ili wakale
karamu ya ndege angani.
Shiba ilipowazidia mbawa
zikapapatuka wakaanguka
chini. Ukweli ukafichuka.
Tukawajuwa kuwa walikuwa
wanafiki ndani ya chama. Na
mifamo haiishii hapa tu. Kuna
makobe wengi ndani ya CUF
waliojivalisha mbawa ili kuila
karamu ya ndege angani.
Wakishashiba tu, warudi
chini makwao waje waongeze
Makala
AN-NUUR
Kisiwandui.
Kama wakuu wa Baraza
la Mji wangefanya utafiti,
ingebidi kubakia na kituo
kile na huku wanatafuta
njia nyengine ya kudumu.
Lazima mwenye kuhusika
na watu ajuwe hao watu
wapo idadi ngapi na
wangapi wenye vipando
vyao hawategemei
vipando vya Umma na
wangapi wanatumia
magari ya serikali n.k.
Aidha, mtafiti
anaangalia kukua na
kuongezeka kwa watu nini
kinahitajika kufanyika,
kwa mfano kisiwa cha
Zanzibar katika mwaka
wa 1964 idadi ya watu
wake ilikuwa ni watu laki
tatu (300,000) laki mbili
ikiwa imestakimu Unguja
na laki moja ipo Pemba
na kutokana na Sensa
iliopita ya mwaka wa 2012
inatueleza kuwa idadi ya
watu wa Zanzibar kwa
sasa ni Milioni moja na laki
tatu (1,300,000) ongezeko
hili la watu linaingia
katika masafa yale yale
ya kisiwa ambacho watu
wameongezeka lakini
masafa ya kisiwa ndio yale
yale au unaweza kusema
hata yanapungua kwani
tunaelezwa kuwa kuna
maeneo yasiopungua 125
yamevamiwa na maji ya
chumvi baadhi ya maeneo
h a y o ya l i k u wa n i ya
kilimo, mengine ni makazi
ya watu.
Katika miaka ya sitini
kituo hicho cha Darajani
kilikuwa kinapokea
magari kwa siku nzima
magari yasiozidi 15
yakiwa ya Makunduchi
mawili, Fuoni moja,
Jumbi mawili, Nungwi
moja, Mkokotoni moja,
Kizimkazi moja, Chwaka
moja, Ndijani moja,
Bumbwini, Mangapwani
moja, Bwejuu moja,
Matemwe moja n.k Hio ni
miaka ya sitini kwa mfano
gari kutoka Makunduchi
likiingia mjini linabakia
hapo hadi mchana ndio
linarudi huwa na safari
moja tu kwa siku. Leo gari
hizo zinafanya hata safari
tatu kwa siku kutokana
n a m a h i t a j i ya wa t u .
Magari yameongezeka
kutokana na idadi ya
watu kuongezeka ambao
wanahitajia usafiri
nathubutu kusema kwa
siku ingia toka ya magari
hapo Darajani yanafikia
i d a d i ya k u i n g i a n a
kutoka kwa magari mia
Inaendelea Uk. 13
10
Na Omar Msangi
HIVI karibuni mwandishi
Mohammed Ghasani
aliandika makala
n d a n i ya k e a k a h o j i ,
k o s a l a Wa z a n z i b a r i
nini hata Tanganyika
iwanganganie hivyo
na kutowapa fursa ya
kupumua na kuamua aina
ya muungano wanaotaka.
Jibu la swali hilo
analieleza vizuri Waziri
M h e s h i m i wa Wi l l i a m
Lukuvi wakati akiongea
na waumini wenzake
Wa k r i s t o k a n i s a n i .
Anaeleza Mheshimiwa
L u k u v i a k i a n z a k wa
k u w a h o j i Wa k r i s t o
wenzake:
Eti tuwaache
W a z a n z i b a r i
wa j i t a wa l e w e n y e w e
n a Wa t a n g a n y i k a
Wazanzibari kule waliko,
asilimia 95 ni Waislamu.
Tunataka wajitangazie
serikali ya Kiislamu kule!
Hapana. Sauti
inasikika baadhi ya
waumini wakijibu. Kisha
anaendelea kuuliza
Lukuvi:
Mnajua madhara
yake? Inasikika sauti
ya waumini wakijibu:
Makubwa sana.
Wa z i r i L u k u v i
anaeeleza: Wale Waarabu
watarudi. Watazalisha
siasa kali kule watakuja
kutusumbua.
Mimi najua, kabisa.
Kwa hiyo ndugu zanguni,
mnaposikia mjadala kule,
kuna watu unaweza kuona
kama wana nia njema
wanataka kuwasemea
wale wanaoitwa
Tanganyika, lakini wana
siri yao moyoni. Kwamba
labda ikipatikana hii
serikali na sisi tutashinda
tutatawala.
Zanzibar ni nchi ndogo
sana. Ina watu milioni
moja na laki tatu. Sisi tuna
milioni arobaini. Unaweza
ukauliza, kwa nini sisi
tunaingangania sana ile?
Lakini sisi tunaangalia
mbele. Madhara ni
makubwa kuicha Zanzibar
kama ilivyo.bora tuwe
nao.
Bwana Ghasani, hilo
ndio jibu. Zanzibar
i k i a c h w a , Wa a r a b u
watarudi, watazalisha
Waislamu siasa kali,
wataisumbua Tanganyika.
Labda sasa swali ni je,
kwa nini Zanzibar nao
wasiwe na wasiwasi kuwa
wakiwa chini ya makucha
y a Wa t a n g a n y i k a ,
Wakristo watawapa tabu
Waislamu wa Zanzibar?
Mheshimiwa William
Lukuvi na wale aliokuwa
akiwahubiria kanisani,
Makala
AN-NUUR
11
Inatoka Uk. 10
Assad, Al-Shabaab, ISIS,
IS, Boko Haram n.k, nchi
zaidi ya saba zimevamiwa,
k u p i g wa m a b o m u n a
kushambuliwa kwa
makombora ya drones.
Hawa akina Karl Peters
wanaofanya haya, ndio
wa kuhofiwa kuwa wana
mpango wa kurudi
kutukalia au kutuletea
machafuko tuuwane
wenyewe kwa wenyewe
kisha wajifanye wasamaria
we m a wa k u t u s a i d i a
kijeshi na kikachero.
Na wakifanikiwa hilo,
machafuko hayaishi. Ndio
hali ya Nigeria, Yemen na
kwingineko.
Mamilioni ya Waislamu
wameuliwa kwa sababu ya
uwongo na propaganda
zao, mamilioni wakatiwa
vilema na mamilioni hivi
tunavyoandika, wamebaki
kuwa wakimbizi.
Kwa wenye chuki na
Waislamu, mara nyingi
huwa hawaangalii athari
ya machafuko, vita na
kuangamizwa kwa
nchi wala ile agenda ya
ujumla ya mabeberu.
Wanachotizama ni kuwa
Waislamu wameuliwa,
wanabamizwa. Wanameza
propaganda ya ugaidi
na kuhalalisha kuuliwa
Waislamu.
Ukirudi nyuma
kulikuwa kuna kitu
kinaitwa Operation Gladio
(Italian: Operazione
Gladio) au "stay-behind".
Walikufa sana Wazungu
wa Ulaya. Na hawa
walikuwa ni Wakristo.
Mabeberu katika Staybehind operations
zao ndani ya nchi za
NATO, hawakujali kuwa
wanaokufa ni Wazungu
w e n z a o n a Wa k r i s t o
wenzao pia.
Hivi sasa Ukraine
kuna zogo kubwa. Watu
wanauliwa. Kisa! Wenye
uchu wa mafuta wanataka
kuitia katika makucha
yao nchi hiyo bila kujali
watakufa watu wangapi
au nchi kuharibikiwa kiasi
gani kama ilivyoharibikiwa
Iraq na Syria.
Hatukuwahi kuwa na
ugomvi na wananchi wa
Somalia wala kuwa na
adui anaitwa magaidi wa
Kiislamu kutoka Somalia
(Al-Shabaab). Lakini
mabeberu kwa masilahi
yao wameivuruga nchi ile
wamezalisha Al-Shabaab,
wamewatangaza kuwa ni
magaidi wa Kanda hii ya
Afrika na sisi kama vipaza
sauti vinavyotumia betri
badala ya akili, tumekuwa
tukiimba wimbo huo huo.
Akizungumzia vita
dhidi ya ugaidi, aliyewahi
Makala
AN-NUUR
12
MAKALA/SHAIRI
UVIVU WA KUFIKIRI !
AN-NUUR
Rashid Makoko.
Kulikuwa na Sheikh
Seif Nassor Alhinawy
ambae alikuwa Akida
pale Tanga na akihukumu
kwa sheria. (Akida Seif
ndiye baba ya wachezaji
mpira mashuhuri katika
miaka ya 1960 hadi 1970,
Hemed Seif, Marshed Seif
na Rashid Seif, ambao
ukimtoa Marshed wote
ndugu zake walivaa jezi
ya taifa). Kwa kuthamini
taasisi hizi za Kiislamu,
kuna mtaa Waingereza
waliupa jina Akida Road
(sasa Mkwakwani Road)
kwa heshima ya Akida
Seif Nassor.
Katika Tanganyika, mji
wa Tanga ndiyo moja ya
miji iliyokuwa na historia
nzuri sana ya Mahakama
ya Kadhi. Mwanzo wa
miaka ya 1900 kulikuwa
na Kadhi Omar Stambuli
kisha akaja Kadhi Ali bin
Hemed Al-Buhry, Liwali
Abdulrahman bin Ali
Diwani, Liwali Rished
Abdallah, Omar Stambuli,
Juma Mwindadi , Said
bin Ali Al-Buhry (OBE),
Mohamed bin Ali AlBuhry.
Masheikh hawa baadhi
yao walifanya kazi ya
ukadhi Tanga na wengine
walikuwa Moshi, Arusha,
Mwanza na kwengineko
Tanganyika.
Tabora Sheikh Bilali
Mshorwa alikuwa
akihukumu kwa sheria
mahakamani. Huyu
Sheikh Bilali Mshorwa
akifahamiana vizuri
sana na babu yangu,
Salum Abdallah pale
Tabora kwani wao ndiyo
walikuwa wanamji na
wazee wa mjini wakati
wao. Moshi kwa Wachagga
alikuwapo Liwali Mussa
Mwinjanga akihukumu
Bomani. Liwali Mussa
alikuwa akifahamiana
na baba yangu na mtaa
aliokuwa akiishi Liwali
Mussa Mwinjanga toka
enzi hizo za ukoloni
ulikuwa ukijulikana kama
Liwali Street na jina hili
limebaki hivyo hadi hii
leo.
13
Makala
AN-NUUR
Inatoka Uk. 11
Pennsylvania, kiliandaa
kitu kilichojulikana kama
Unified Quest 2008
(war games test). Katika
gemu hiyo ya siku tano,
iliyohudhuriwa pia na
makamanda wa kijeshi
kutoka nchi za NATO na
Israel, walisema kuwa
walikuwa wakijiandaa ni
kwa jinsi gani watalinda
masilahi ya Marekani
ndani ya nchi ya Nigeria
ifikapo mwaka 2015.
Wa l i s e m a k u wa
inatarajiwa mwaka huo
nchi hiyo itasambaratika
kutokana na machafuko
(vitendo vya kigaidi) na
kwamba hata uchaguzi
wa mwaka huo itabidi
uahirishwe. Na kwamba
kuna uwezekano mkubwa
N i g e r i a k u g a wa n y wa
kutoka katika hali yake ya
sasa ya kuwa nchi kubwa
Afrika yenye idadi kubwa
ya watu na utajiri mkubwa
wa mafuta. Pengine iwe
Kaskazini na Kusini kwa
Wakristo.
Akizungumzia suala hilo
Februari 4, 2012, Balozi wa
Marekani nchini Nigeria
Bwana Terence McCulley,
a lite t e a s e rik a li ya k e
akisema kuwa, waliofanya
utabiri huo kuwa Nigeria
itasambaratika ifikapo
mwaka 2015 haikuwa
serikali ya Marekani bali
taasisi binafsi ikijulikana
kwa jina la Rand
Corporation and BoozAllen.
Hata hivyo, taasisi hizo
ndio wakala wa serikali na
S U L T A N I
w a
Oman,Qaboos bin Said
Al Said.
28. Sababu zilizotolewa
ni za kiusalama, kwamba
vyombo vya usalama
vinahitaji muda zaidi wa
kujiandaa kukabiliana na
kitisho cha Boko Haram.
Haijulikani iwapo ahadi
hiyo itatekelezwa au ndio
hatari ya kitisho itakuwa
kubwa zaidi.
Zipo taarifa nyingi juu
ya Boko Haram kwamba
na wenyewe ni katika zile
Intelligence Assets za
mabeberu.
Kwa hakika kama yapo
m a m b o ya k u s t a h i k i
kuwashughulisha
wanasiasa wetu, ni haya ya
hawa wanaotuwangia na
war games test pamoja na
Intelligence Assets zao
wakitutabiria machafuko
huku wakiweka mikakati
watakavyotukalia
kikachero na kijeshi. Sio
hizi porojo za kurudi
Muarabu wa Oman.
14
Makala
AN-NUUR
Baraza la Wazee wa TANU. Sheikh Suleiman Takadir wa pili chini kulia, wa pili
waliosimama Dossa Aziz, wa sita Julius Nyerere, wa saba John Rupia, wa tisa Said
Chamwenyewe, anayefuatia Jumbe Tambaza, Mshume Kiyate.
Askofu Makarios wa siasa
za ukombozi za Cyprus
na Ugiriki aliyekuwa
anapambana na ukoloni wa
Waingereza wakati yeye
alipokuwa anapambana
na Waingereza katika
ardhi ya Tanganyika.
Sasa kwa kuwa Suleiman
Takadir alikuwa Sheikh
na mpambanaji ndipo
wa l i m p a j i n a h i l o l a
Makarios na kwa
hakika jina hili lilimkaa,
likamwenea vyema na
yeye akalipenda.
Mikutano ya mwanzo ya
TANU ilikuwa ikifanyika
15
Na Ben Rijal
TUNAAMBIWA kuwa
Uisalamu ni mfumo
wa maisha. Kwahakika
maisha yote ya Muislamu
yam er at i bi wa katika
program maalumu, iwe
ya siku, wiki, mwezi
au mwaka. Maisha
ya M u i s l a m u t a n g u
anapozaliwa hadi
anapokufa, kuna taratibu
mbalimbali katika
Uislamu, taratibu ambazo
hutakiwa muumini
kuzifwata. Hakuna dini
ambayo ina programu
kamili ya matendo kama
dini ya Kiislamu. Angalia
mifano hii michache, mtu
anapokuwa Muislamu
Baligh mwenye akili
k i l a s i k u a t a t a k i wa
asali vipindi vitano
kuanzia asubuhi hadi
Isha na anaposhikamana
na salaa basi anakuwa
yupo kwenye program
maalumu kwani sala
haisaliwi anapotaka
mtu kusali, lakini sala
inasaliwa kwa wakati
maalumu uliowekwa.
Hayo ni kwa kila siku na
katika wiki unatakiwa
kujipanga kusali kwa
sala ya Ijumaa. Kisha
k a t i k a m wa k a k u n a
funga ya Ramadhani,
kuna kwenda kutimiza
n g u z o ya H i j j a k wa
mwenye uwezo. Hio yote
ni program Muislamu
ameekewa katika maisha
yake.
Maudhui ya makala
hii nikuangalia namna
tulivyofundishwa
kumpokea mtoto
anapozaliwa nini
anachohitajia kufanyiwa.
Ukweli kinachotakikana
sio tu kumpokea, lakini
huanza tangu mume na
mke wanapofanya kitendo
c h a n d o a . L e o wa n a
Saikolojia hutueleza kuwa
pale tunapotaka kwenda
kufanya unyumba, basi
twende kwa utartibu wala
tusikurupuke tu pale
tunapomaliza tendo au
ngono. Kwa kweli Bwana
Mtume Muhammad
S.A.W ameyaeleza hayo na
Makala
AN-NUUR
kututaka tunapowaendea
wake zetu, tuwaendee
kwa maneno mazuri na
kutofanya vishindo na
tusikupurukike kama
punda pale tunapomaliza
unyumba. Aidha tume
Suniwa pale tutapokuwa
tunakaribiya kutoa maji
ya uzazi tusiseme maneno
ya ajabu ajabu nakupiga
makelele, lakini tuseme
maneno yafwatayo:
Kwa jina la Mwenye
enzi Mungu, Ewe Mola
tulinde na Shetani na
utuhifadhi na chochote
utachoturuzuku na huyo
shetani. Taratibu hii
haipatikani kwenye dini
yoyote ile wala kwenye
falsafa yoyote ile ila katika
Uislamu.
Tunatakiwa tufanye
nini mara tu mtoto
anapozaliwa?. Tendo la
kwanza ni kuadhiniwa
kwa mtoto. Mara tu mtoto
atapozaliwa, ni vyema
achukuliwe na baba yake
amuelekeze kibla kisha
amuadhinie kwenye shikio
la kulia la mtoto. Mtume
Muhammad S.A.W
alimuadhinia mjuukuu
wake Sayidna Hussein
r.a kama anavyoeleza
Aboo Raafi, Nilimuona
Bwana Mtume S.A.W
akimuadhinia Hussein bin
Ali baada ya kujifungua
kwa Bibi Fatmah .
Kuna wengine husema
kuwa baada ya adhana
ifuwatie Ikama (Iqama)
kwa shikio la kushoto,
kauli hii haina nguvu.
Nini Falsafa na hikma
ya kuadhiniwa mtoto?
Tumboni, mtoto huwa
hasikii chochote kile, na
mara tu anapozaliwa
huanza kusikia sauti, ni
vyema asikie maneno
mazuri, ikiwa moja la hilo
ni adhana.
Falsafa ya kuadhiniwa
mtoto ni kusikia maneno
ya adhana maneno
ambayo yanamtaja Mola
na Mtume wake, lakini leo
anazaliwa mtoto na huku
anasikia majimbo ya ajabu
ajabu. Nimezungumza
baba amchukue mtoto
amuadhinie kwa hospitali
za kwetu ni ngumu
mwanamume kuingia
wodi ya wanawake,
kwa Ulaya hilo ni jambo
la kawaida mume
anaruhusika na anabakia
kwenye chumba cha
kuzalishia kumuangalia
mke wake anavojifungua,
k wa h i o k a m a m z a z i
atakuwa na nguvu
za kufanya hivyo, basi
amuadhinie mwenyewe au
azungumze na wakunga.
Te n d o l a p i l i /
Tahneek : Tahneek ni
kumrambisha Tende mara
tu mtoto anapozaliwa.
Kurambishwa tende
watoto Bwana Mtume
amelifanya mara nyingi
tu. Ni vyema tahneek
akaifanya baba au mama
au mtu wa familia ya mtoto.
Nini Falsafa na hikma ya
Tahneek ? Anapozaliwa
mtoto huwa hana nguvu,
na sukari mwilini mwake
blood sugar huwa ipo
chini hypoglacymia
kuna hatari ya kuweza
kufa mtoto sukari ikawa
chini. Tahneek husaidia
misuli za mdomo. Tende
ni chakula chenye faida
kubwa sana mwilini. Suna
tuliotakiwa kuitekeleza
ni tende na siku hizi hiyo
tende hupatikana kila
mahali, verejee glucose
na chokleti ? Tusiiwache
Sunna hii kwa watoto wetu
wanapokuja duniani.
Tendo la tatu ni kutoa jina
: Tunavielewa vitu vinavyo
tuzunguka kutokana na
kuvipa majina. Majina
yanatusaidia kuelewa vitu.
Miti, wanyama na wadudu
mbalimbali wanaadamu
wa me ya i t a ma j i n a i l i
kuweza kuwatambua.
Kuna somo zima la elimu
ya viumbe taxonomy
ambalo kazi yake ni kutoa
majina ya viumbe kwa
njia za kisayansi. Kuwa
na majina kuna hikma
kubwa.
Wakati gani wa kutoa
majina? Kuna kauli mbili
na zote zinakubalika,
nazo ima tuwape majina
watoto wanapozaliwa kwa
siku ya kwanza au siku
ya saba. Bwana Samurah
anaeleza, Bwana Mtume
Muhammmad S.A.W
ametutaka tuchinje,
tunyoe na kutoa majina
siku ya saba. Ahmad (/7,
17), Abou Dawood E.T.
2/797/No 2831).
N a y e A n a s ( R A)
anaeleza: Kuna mtoto
alizaliwa na siku hiyo
hiyo hiyo akapelekwa
kwa Bwana Mtume
Muhammad S.A.W, na
Bwan Mtume akampa jina
tumetakiwa amchinjie
Kondoo au mbuzi wawili
kwa mtoto wa kiume na
Kondoo au mbuzi mmoja
kwa mtoto wa kike.
A q e e q a h h u f a n y wa
siku ya saba sambamba na
kutoa jina na kunyolewa
kwa mtoto. Nyama ipikwe
kisha igawiwe. Itakuwa
v ye m a i k i wa m a f u p a
hayatavunjwa.
Tendo la tano kumnyoa
mtoto nywele : Ni Suna
kunyoa watoto siku
ya saba. Kunyoa ni
k wa m wa n a m u m e n a
mwanamke. Nywele
z i p i m we k i s h a u z a n i
wake utiwe thamani ya
fedha na thamani ya pesa
wapewe maskini. Syd Ali
(RA) alifanya hivyo kwa
watoto wake, na ni vizuri
baada ya kumnyoa mtoto
apakwe mafuta. Siku
hizi hasa sisi wazee wa
Kiafrika husita kuwanyoa
mtoto eti nyewele za
mtoto anapozaliwa huwa
laini basi ukimnyoa huja
z a k a wa i d a k a s u m b a
hizi tuzitie mvunguni
tushikamane na Suna za
Bwana Mtume SAW.
Tendo la sita ni kutahiri
: Atahiriwe mtoto siku ya
7, 14 au 21. bada ya hapo
atahiriwe siku yoyote ile
bali asifike hata kubalighi.
Kwa wanawake sio lazima
wala Uislamu hausisitizi
mwanamke kutahiriwa.
Mila za wenzetu kumtahiri
mwanamke ni kumtoa
matamanio.
Baadhi ya makosa
wayafanyao watu
kutomuadhinia mtoto,
kuwacha tahneek yaani
kutomrambisha mtoto
tende na inapokosekana
tende badala yake iwe
kitu kitamu, kutotoa
jina hata baada ya wiki,
kuwa na khofu ukimwita
majina ya wazee wake
waliohai basi itacahangia
wao kufa haraka-hii ni
shirki, kutochinja, badala
yake kutoa thamani ya
mnyama, kutomchinjia
mtoto wa kike, kumchinjia
kondoo au mbuzi mmoja
tu kwa mtoto wa kiume,
kutochinja kupindukia
siku 21 ilhali mtu ana
uwezo, kuchinja mnyama
mmoja kwa mtoto zaidi
ya mmoja, kupinga kule
kuelezwa tusivunje
mifupa.
Kumnyoa mtoto upande
mmoja na kuuwachia
upande mwengine hii
inaitwa al-qaz, kumnyoa
mtoto wa kiume wala sio
wa kike kwa kuhofia kuwa
mtoto wa kike atalingana
na mtoto wa kiume, kuwa
na imani kuwa baadhi
ya watoto wakizaliwa
hawahitajiwi kutahiriwa.
16
Makala
AN-NUUR
17
Makala
Na Juma Killaghai
MAKALA ya leo ni ya nne na
ya mwisho, kati ya mfulululizo
wa makala tulizodhamiria kutoa
kwa malengo ya kujenga hoja
juu ya chai ya Haiiba Timamu
kuhitajiwa na kila mtu. Hoja ya
msingi iliyotawala makala zote tatu
zilizopita, na ambayo tunaiendeleza
katika makala hii, ni kuwa tiba ya
chai hii inatokana na kumrejeshea
muhusika viini lishe mbali mbali
muhimu vilivyopungua mwilini
mwake. Katika makala zilizotangulia
tulizungumzia makundi matatu
ya viini lishe vilivyomo kwenye
chai ya Haiiba Timamu. Tuliyataja
makundi haya kuwa ni yale ya
vitamini, madini lishe na tindikali
za amino, au vijenzi vya protini.
Makala yetu ya leo itataja kundi
la nne na la mwisho; hili si lingine
bali ni kundi la vizuia vioksidishaji
(anti-oxidants).
VIZUIA VIOKSIDISHAJI NI NINI? Vizuia
vioksidishaji ni molekuli (molecule)
zinazozuia mchakato wa kuoksidisha
molekuli nyingine. Kuokisidisha ni
muingiliano wa kikemia (chemical
reaction) unaopelekea molekuli
iliyookisidishwa kupoteza chembe
yenye/zenye umeme hasi (electron),
au kupoteza kiasili cha hydrogen
katika umbile lake, au umbile lake
kuongezewa kiasili cha oxygen.
Mchakato wa uoksidishaji ndani
ya mwili hutokea muda wote. Huu
ni sehemu ya mchakato wa ujenzi
na uvunjifu wa kemikali ndani ya
mwili, yaani metabolism. Mchakato
wa kuoksidisha unaweza kuzaa
c h e m b e c h e m b e z e n ye u m e m e
chanya zinazoitwa free radicals.
Kwa upande wake hizi free radicals
ni chembe zenye uwezo mkubwa
wa kuoksidisha, na hivyo kuwepo
kwake kunaweza kuzaa gharika
(chain reaction) ya uoksidishaji ndani
ya seli za mwili. Hali hii inaweza
kusababisha uharibifu mkubwa wa
seli au hata kifo cha seli husika.
Vizuia vioksidishaji huzuia hizi
gharika kutokea ndani ya seli. Badala
yake hivi vioksidishaji huoksidisha
hivi vizuia vioksidishaji na kwa hivyo
kuacha seli za mwili zikiwa katika
hali ya salama. Kwa kawaida mwili
unamiliki na kuendeleza mifumo
kadhaa ya vizuia vioksidishaji
mbalimbali. Vizuia vioksidishaji hivi
ni pamoja na glutathione, Vitamini
C, Vitamini A, na Vitamini E; pamoja
na vimengenya mbalimbali kama
catalase, superoxide dismutase
na peroxidases mbalimbali.
Kuwepo kwa kiwango kidogo cha
vizuia vioksidishaji au kuwepo
k w a v i m e n g e n y a n d a n i y a
AN-NUUR
18
Na Bakari Mwakangwale
UNAPOZUNGUMZIA
wanaharakati wa miaka ya
hivi karibuni ambao wana
mchango mkubwa katika
k u wa a m s h a Wa i s l a m u
nchini, huwezi kulikosa
jina la Amani Saad Fundi.
Ustadhi Fundi, kwa sasa
amekuwa haonekani kwa
muda mrefu katika harakati,
japo hali hii ipo miongini
mwa wengine wengi wa
mfano wake na wa wakati
wake.
Hii huenda ni kutokana
na sababu mbalimbali,
ambazo zimekuwa
zikiwakabili wanaharakati
hao wa enzi zake, yakiwemo
maradhi au kuwepo katika
harakati hizo kwa sura
nyingine kutokana na wigo
wa harakati za kuhuisha
Uislamu kupanuka hivi
sasa kulinganisha na wakati
uliopo.
An nuur, imekutana
na Ust. Fundi, lakini
ukimwangalia tu, utabaini
k u wa h u y u s i A m a n i
Saad Fundi, yule ambaye
alikuwa kamanda wa vijana
aliyepewa majukumu ya
kudhibiti ofisi za Bakwata,
Jijini Dar es Salaam, katika
miaka ya 1992.
Ustadh Fundi, hivi
sasa ukikutana naye
anakuangalia kwa shida
huku akigeuza uso wake ili
aipate taswira yako vizuri
aweze kukutambua, hapo
hapo akitegea kukupa
mkono kama ilivyo ada
y a Wa i s l a m u k a t i k a
kusalimiana ili wewe
uufate mkono wake ulipo,
na pengie ujitambulishe
kwake wewe ni nani.
Fundi, enzi za harakati
za miaka hiyo, alikuwa
anaweza kuongoza
mapambano akiwa mstari
wa mbele huku umma wa
Kiislamu ukiwa nyumba
yake ukiwa na matumaini
kuwa mbele kuna
kamanda,Shabaab.
Hivi sasa Ust. Fundi,
anatembea kwa msaada
wa mtu pembeni ili aweze
kufika mahali anapopahitaji.
Ukimuona Mwanaharakati
huyu, hakika utapata Ibra
ya kuutumikia uzima wako,
nguvu zako na elimu yako,
katika kuupigania Uislamu
kabla maradhi hayaja kufika.
Ni nini kimemsibu Ustadh
Fundi? Mwanaharakati
huyu, amepatwa na mtihani
wa maradhi ya shinikizo la
damu katika macho -presha
ya macho, maradhi ambayo
yamepoteza nuru yake ya
kuona.
Hadi sasa Ustadh Fundi
amebakia na jicho moja
tu ambalo linamwezesha
kuona kwa tabu, tena mpaka
ageuze shingo kwa maana
eneo analotumia kuona ni
sehemu ya mwisho ya jicho
huku jicho la pili likiwa
limepoteza nuru ya kuona
kabisa.
Ustadh Fundi, anasema
kutokana na maradhi ya
macho aliyonayo sasa
Makala
AN-NUUR
19
Tangazo
AN-NUUR
Waislamu kote nchini mnatangaziwa nafasi za kidato cha Tano kwa shule zifuatazo:
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL
SAME KILIMANJARO
NYASAKA ISLAMIC SECONDARY SCHOOL
MWANZA
UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOO L
DAR ES SALAAM
1. Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi bora ya Kiislamu.
2. Shule hizi ni za bweni za mchanganyiko wa wavulana na wasichana .
3. Zipo tahasusi za masomo (Subject Combinations) ya SAYANSI, ARTS na BIASHARA.
4.
Wanafunzi wote wanafundishwa Islamic Knowledge,Introduction to Arabic na matumizi ya compyuta pamoja na kutumia mtandao (internet)
katika kujifunza.
5. Muombaji anatakiwa awe na sifa za kujiunga na kidato cha tano kwa mujibu wa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
6. Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000/= katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini.
Arusha - Ofisi ya Islamic Education Panel, Jambo Plastic, Ghorofa ya 2 mkabala na msikiti Mkuu Bondeni
: 0783552414/0762817640.
Kilimanjaro
- Moshi: Msikiti wa Riadha :712 216490
- Same Juhudi Studio mkabala na Benki ya NMB Same: 0757 013344.
- Same: Kirinjiko Islamic Secondry School: 0784 296424/0655 697 075
- Usangi- Falhum Kibakaya : 0787 142054.
- Ugweno Kifula Shopping Centre- Yusuph Shanga : 078458776.
Tanga
- Twalut Islamc Centre Mabovu Darajani : 0715 894111
- Uongofu Bookshop: 0784 982525
- Korogwe: SHEMEA SHOP : 0754 690007/071569008.
- Mandia Shop - Lushoto: 0782257533.
-Handeni Mafiga -0782 105735/0657093983
Mwanza
- Nyasaka Islamic Secondary School : 0717 417685/0786 417685.
- Ofisi ya Islamic Education Panel Mtaa wa Rufiji mkabala na Msikiti Al-Amin 0785 086 770/0714097362.
Musoma
Shinyanga
Morogoro
Dodoma
Singida
Manyara
Kigoma
- Msikiti wa Mwandiga: 0714717727
- Kibondo Islamic Nursery School: 0766406669.
- Kasulu: Murubona Isl.SS: 0714710802.
Lindi
Mtwara
- Ofisi ya Islamic Education. Panel karibu na Nuru snack Hotel : 0786 425838/0784 928039.
- Ofisi ya Islamic Ed. Panel Masjid Rahma: 0784491196
Songea
- Kwa Kawanga Karibu na Msikiti wa NURU : 0713249264/0683670772.
- Mkuzo Islamic High School :0717 348375.
Mbeya
Rukwa
Tabora
Iringa
Pemba
Unguja
AN-NUUR
20
MAKALA
20
AN-NUUR
iliyosahauliwa katika
zoezi la kuweka majina
ya mitaa lililofanywa na
Wizara hiyo, hasa katika
mitaa ya Mji Mkwongwe
na baadhi ya mitaa ya
Ngambo.
Nae Waziri wa Wizara
hiyo Mhe. Juma Duni Haji
alisema kuwa Wizara hiyo
imeendelea kusimamia
utekelezaji wa kazi zake
za kawaidia na maendeleo
kwa kuzingatia Dira ya
Taifa ya Maendeleo (Vision
2020), Mkakati wa Kukuza
Uchumi na Kupunguza
Umasikini (MKUZAII),
Sera ya Usafiri Zanzibar
(2008), Mpango Mkuu
wa Usafiri pamoja na Sera
nyenginezo zinazohusika
(Habari kwa hisani ya
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar)
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.