Professional Documents
Culture Documents
Historia Ya CCM Tangu TANU Na ASP
Historia Ya CCM Tangu TANU Na ASP
Historia Ya CCM Tangu TANU Na ASP
UTANGULIZI:
1.1
Maelezo ya awali
Chama cha Mapinduzi (CCM) kilizaliwa tarehe 5 Februari, 1977 kutokana na kuvunjwa
kwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) na Afro-Shirazi Party (ASP).
Tendo hilo la kihistoria lilikuwa ni la kuendeleza utamaduni uliokuwa umeanza huko
nyuma wa kuunganisha nguvu kwa lengo la kujiimarisha katika mapambano. Kwa
mfano, ASP kwa upande wa Zanzibar ilitokana na kuungana kwa African Association
(AA) na Shirazi Association (SA), tendo ambalo liliunganisha nguvu za wanyonge katika
mapambano ya kuundoa usultani na utawala wa kikoloni wa Kiingereza. Kwa upande
wa Tanzania Bara, TANU ilitokana na kujibadilisha kwa Tanganyika African Association
(TAA) kutoka jumuiya ya kutetea maslahi ya kijamii na kuwa chama cha siasa.
Kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika tarehe 9 Desemba, 1961 na ule wa Zanzibar
kupitia Mapinduzi ya tarehe 12 Januari, 1964, kulifanya TANU na ASP viwe
vimekamilisha jukumu la ukombozi wa nchi hizi kutoka makucha ya ukoloni mkongwe
na usultani. Hata hivyo, vyama vya siasa hivi viliendelea kukabiliwa na majukumu ya
kuendeleza mapambano ya ukombozi katika Afrika
na kote duniani; kujenga
Tanganyika na Zanzibar huru kiuchumi na kijamii na kuimarisha umoja na mshikamano
wa kitaifa,
Katika mazingira ya ubeberu duniani wakati huo na hali ya unyonge wa mataifa haya
machanga, yakielewa kuwa umoja ni nguvu, Tanganyika na Zanzibar zilibaini umuhimu
wa muungano, hivyo ziliamua kuungana tarehe 26 Aprili, 1964. Muungano huo ndio
uliowezesha kuzaliwa kwa Tanzania. Chini ya Muungano huo, Tanzania iliendelea kuwa
na vyama vya siasa viwili, yaani TANU na ASP katika mazingira ya chama kimoja cha
siasa. Vyama hivi vilitambua fika kwamba vinahitaji chombo madhubuti cha uongozi
katika kutekeleza majukumu yake ya ukombozi kwa ukamilifu hivyo uamuzi ulifanywa
rasmi wa kuvunja TANU na ASP na kuundwa kwa Chama Cha Mapinduzi tarehe 5
Februari, 1977.
Katiba ya CCM, katika Azimio la Mkutano Mkuu wa Taifa wa Pamoja wa TANU na ASP
tarehe 21 January, 1977, inaeleza kuwa, (uk. 2-3), ...kwa kauli moja tunaamua na
kutamka rasmi kuvunjwa kwa Tanganyika African Union(TANU) na AfroShirazi Party (ASP) ifikapo tarehe 5 Februari, 1977 na wakati huohuo
kuundwa kwa Chama kipya cha pekee na chenye uwezo wa mwisho katika
mambo yote kwa mujibu wa Katiba.
Muungano wa TANU na ASP ndio uliowezesha CCM kuwa Chama chenye nguvu, imara
na madhubuti, hivyo kuwa Chama cha siasa pekee chenye uwezo wa hali ya juu wa
kuwaunganisha Watanzania. Aidha, CCM kimeweza kuwaongoza wananchi katika
2
Historia ya CCM tangu TANU na ASP ina umuhimu wa pekee katika Taifa letu katika
kuelewa tulikotoka, tulipo hivi sasa na tunakoelekea. Historia ya nchi yetu haiwezi
kukamilika bila ya historia ya vyama hivi vya ukombozi. Historia hutoa mafunzo na ni
mwelekezaji pia, kwa hiyo ni wajibu wa Watanzania, hasa wanachama wa CCM
kujifunza kutokana na historia yetu. Kazi kubwa na ya msingi inayofanyika katika
kujifunza historia hiyo, ni kurithisha dhamira ya kujituma na kudumisha uhuru wa nchi
yetu. Hivyo, ili kuendelea kukijenga Chama, na kuimarisha uwezo wa kuendelea
kukamata dola barabara kwa namna endelevu, hapana budi ihakikishwe kuwa historia
ya CCM inabeba pia jukumu la msingi la kusaidia:
1.3
Pamoja na kwamba Chama Cha Mapinduzi kuwa kilizaliwa rasmi tarehe 5 Februari,
1977, chimbuko lake linaanzia miaka mingi kabla, sambamba na historia ya uhai wa
taifa la Tanzania. Mizizi ya historia ya CCM imo ndani ya harakati za kukataa ukoloni na
usultani, zilizofanywa na wananchi wa Tanzania. Wahenga wetu kwa pamoja tangu
enzi, walionyesha wazi kukataa kwao kutawaliwa. Historia ya Tanzania inao utajiri wa
3
mifano mingi ya harakati hizo japokuwa zilijengwa katika misingi ya ukoo na ujirani,
katika wilaya na mikoa mbalimbali hata kabla ya kuundwa kwa vyama vya TANU na
ASP.
Wananchi hao waliotutangulia walikataa kunyonywa, kupuuzwa, kubaguliwa,
kutawaliwa, kunyanyaswa na kugawanywa katika misingi ya rangi, kabila, dini, jinsia,
nk. Utu na uhuru wao ulikuwa na thamani kubwa sana. Hivyo waliamua kupambana
dhidi ya udhalimu huo. Baadhi ya mifano ya jitihada za mapambano ya awali ni Vita ya
Majimaji huko Umatumbi na maeneo ya kusini, Mbiru huko Upare, Waluguru, Wameru,
Wahehe na mengineyo huko Unguja, Pemba, Kanda ya Ziwa na katika jamii za
wafugaji. Ari, utashi, uzalendo na dhamira ya kweli ya kutaka kujitawala
vilivyojidhihirisha katika harakati hizo, viliotesha mizizi iliyoshikilia uhai wa vyama vya
TANU na ASP.
2.0
2.1
TAA iliundwa 1948 kufuatia tukio la kutengana kwa African Association (AA) ya
Tanganyika na Zanzibar. AA ilizaliwa Dar es Salaam 1927 chini ya uongozi wa Cecil
Matola akiwa Rais na Kleist P. Sykes akiwa Katibu. Malengo ya AA yalikuwa ni
kupigania haki, maslahi na umoja wa Waafrika. AA ilikuwa na matawi yake makuu
Dodoma na Zanzibar. Aidha, AA ilifungua matawi katika miji iliyokuwa makao makuu ya
wilaya.
Katiba ya TAA ilitamka wazi kwamba Chama hicho hakikuwa na malengo ya kisiasa.
Mwaka 1953 yalifanyika mabadiliko ya uongozi katika TAA. Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere alichaguliwa kuwa Rais wa TAA. Chini ya uongozi mpya, Katiba ya TAA
ilionekana kwamba isingeweza kukidhi malengo ya kisiasa. Mwalimu alipewa jukumu
la kuandaa Katiba mpya ya TAA ambayo ingezingatia malengo ya kisiasa. Baada ya
uandaaji wa Katiba hiyo kukamilika, haja ya kubadili jina ilionekana dhahiri na majina
mengi yalipendekezwa likiwemo la TANU. Nafasi ya TAA ilichukuliwa na TANU
iliyozaliwa tarehe 7 Julai, 1954. TANU ilirithi matawi ya TAA, wanachama na viongozi
wa TAA katika maeneo mengi.
Waasisi wa TANU ambao walihudhuria na kushiriki katika Mkutano wa kuzaliwa kwa
TANU walikuwa 17:
(1)
(2)
(3)
(4)
(5)
(6)
(7)
(8)
(9)
(10)
(11)
(12)
(13)
(14)
(15)
(16)
(17)
Katika miaka 1950, wakulima walikwishajiunga na kuanzisha vyama vya kuuza mazao
yao ya biashara ili waweze kupata bei nzuri kwa kupunguza gharama ya mtu wa kati
ambaye alikuwa ni mfanyabiashara wa Kiasia. Baadhi ya Vyama vya Ushirika
vilivyokuwepo kabla ya TANU ni:
Kwa kuwepo vyama vya ushirika, ujumbe wa TANU kuwafikia wananchi ulirahisishwa.
Wanachama wa vyama vya ushirika walijiunga na TANU. Wanachama na viongozi wa
vyama vya ushirika waliunga mkono TANU katika madai yake ya kudai uhuru. Baadhi
ya viongozi wa vyama vya ushirika walichaguliwa kuwa viongozi wa TANU katika ngazi
ya Taifa. Kwa mfano:
TANU nayo iliunga mkono vyama vya ushirika katika madai yake ya bei nzuri ya mazao
yao na kuondoa ushuru wa kahawa uliokuwa unatozwa na Serikali Kuu. Aidha, TANU
ilihimiza na kuwahamasisha wananchi kuanzisha na kuimarisha vyama vya ushirika.
Kazi hii ya kuhimiza na kuhamasisha wananchi kujiunga na ushirika iliendelea kufanywa
na TANU hata baada ya Tanganyika kupata uhuru wake.
Baada ya Uhuru, TANU iliuona ushirika kuwa ni chombo cha kuleta maendeleo hivyo
wananchi walihimizwa kuanzisha ushirika katika maeneo ambayo hayakuwa na vyama
vya ushirika. Hali hii inaendelea hadi hivi sasa ambapo katika mfumo wa uchumi wa
Soko, CCM inauona ushirika kuwa ni chombo cha kumwezesha mwananchi
kiuchumi katika kumiliki na kuendesha uchumi wa Taifa lake.
2.4 TANU ilizaliwa katika mazingira ya vyama vya wafanyakazi:
Lengo kuu la Vyama vya Wafanyakazi lilikuwa ni kutetea maslahi ya wafanyakazi.
Baadhi ya vyama vya wafanyakazi ni:
Chama
Chama
Chama
Chama
Chama
Chama
Chama
Chama
Chama
cha
cha
cha
cha
cha
cha
cha
cha
cha
nyongeza ya mshahara
mapumziko ya mchana siku ya kazi
umri wa kustaafu na
kuondoa ubaguzi katika ajira na huduma za jamii.
Vyama vya wafayakazi vilisaidia kuvunja ukabila na hivyo kuwa chanzo cha umoja.
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi lilisaidia kueneza TANU kwa njia zifuatazo:
Vyama vya Wafanyakazi vilifanya yote hayo kwa kuelewa kwamba uhuru ndio
ungekuwa suluhisho la kweli la matatizo yao.
Kama ilivyokuwa kwa vyama vya ushirika, baadhi ya viongozi wa vyama vya
wafanyakazi walichaguliwa kuwa viongozi wa TANU. Mwaka 1958, Katibu Mkuu wa
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi, Mzee Rashid Mfaume Kawawa, alichaguliwa kuwa
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya TANU. Toka wakati huo hadi hivi sasa, Mzee
Kawawa amekuwa na uongozi uliotukuka katika TANU/CCM.
Kwa upande wake, TANU iliunga mkono madai ya vyama vya wafanyakazi na migomo
ya wafanyakazi. Katika historia ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi, mgomo wa
wafanyakazi wa Shamba la Mazinde huko Tanga na mgomo wa wafanyakazi wa
Kiwanda cha Bia Dar es Salaam ni miongoni mwa migomo maarufu.
Shamba la Mazinde lilikuwa mali ya bepari mmoja wa Kiingereza, mwanachama
mashuhuri wa United Tanganyika Party (UTP) aliyewahi kushiriki katika kugombea na
kushindwa na mgombea wa TANU katika Uchaguzi Mkuu wa Baraza la Kutunga Sheria
mwaka 1958. Wafanyakazi katika Shamba la Mazinde walijiunga na Chama cha
Wafanyakazi Mashambani (Tanganyika Plantation Workers Union TPWU) ambacho
kilikuwa kimeshirikishwa katika Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi. Mmiliki wa
Shamba la Mazinde alikuwa na tabia ya kuwafukuza wafanyakazi walioonyesha kupinga
UTP na walioamua kujiunga na Chama cha Wafanyakazi Mashambani. Katika harakati
za kuwaunga mkono wenzao waliofukuzwa, wafanyakazi wote elfu tatu (3,000)
waliamua kugoma na matokeo yake wote walifukuzwa kazi.
Jitihada za TFL kusuluhisha mgogoro huo kati ya Mwajiri na wafanyakazi zilishindikana.
TFL na TANU kwa pamoja viliunga mkono mgomo wa wafanyakazi wa Shamba la
Mazinde. TANU kupitia Mwalimu Nyerere ilitoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Tanga
kuwahifadhi wafanyakazi waliofukuzwa kazi. Wananchi waliitikia wito wa TANU na
kuwapokea na kuishi nao. Aidha, TFL na TANU vilitoa wito kwa wananchi kususia
shamba la Mazinde. Wafanyakazi hao hawakurejea kazini hata baada ya mmiliki
kuwataka kufanya hivyo. Matokeo yake ni kwamba mmiliki huyu wa Shamba la
Mazinde hakuchukua muda akafilisika na akarejea kwao Uingereza.
Huu ulikuwa ni ushindi wa TANU na TFL. TANU ilitambuliwa na wafanyakazi
mashambani na iliendelea kuimarika. Kwa kuwa ngome ya UTP, na baadaye African
National Congress (ANC) ilikuwa huko Tanga pigo hili lilisababisha kifo cha UTP na
kuzorota kwa ANC.
Kuhusu mgomo wa Kiwanda cha Bia Dar es Salaam, mgomo ulianza Aprili hadi Juni,
1958. Mgomo uliwashirikisha wafanyakazi wapatao mia tatu (300). Wafanyakazi
7
Kama kawaida yao, wananchi waliitika wito na maombi ya TANU. Kwa kupitia migomo
TANU ilizidi kuimarika miongoni mwa wafanyakazi.
2.5
2.6
2.7
TANU ilianzisha rasmi mwaka 1955 sehemu ya Wanawake wa TANU. Chama kilitambua
kwamba mapambano ya kudai uhuru yasingeweza kufanikiwa bila ya kulitumia jeshi
kubwa la Wanawake. Chama kilimpata Bibi Titi Mohamed na kumpa jukumu la
kuwakusanya wanawake ili washiriki katika mapambano ya kudai uhuru. Sehemu ya
Wanawake ilipewa majukumu yafuatayo:
Katiba ya TANU ya mwaka 1954, sehemu ya sita, ilitoa nafasi kwa vijana kuunda umoja
wao ili waweze kushiriki kwa ukamilifu katika mapambano ya kudai uhuru. Umoja wa
Vijana ulikuwa na majukumu yafuatayo:
2.8
Licha ya hila na vikwazo vya mkoloni, TANU ilijikuta ina mtihani mgumu wa kuamua
kushiriki ama kutokushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa kwanza mwaka 1958. Akifungua
kikao cha kwanza cha Baraza la Kutunga Sheria mwaka 1956, Gavana Edward Twining
alitangaza kuwa Serikali ilikuwa na mpango wa kufanya Uchaguzi Mkuu wa kwanza
mnamo 1958. Sharti moja kubwa la uchaguzi huo lilikuwa kwamba kila mpiga kura
apige kura tatu: moja kwa Mzungu, moja kwa Mwasia na moja kwa Mwafrika.
Suala hili la kura ya Mseto lilijadiliwa kwa undani katika Mkutano Mkuu wa TANU
uliofanyika Tabora mwaka 1958 na kuhudhuriwa na Wajumbe 300 kutoka sehemu zote
za Tanzania Bara. Ili kupata nafasi nzuri ya kujadili agenda hii, Mwalimu Nyerere
aliomba asiwe Mwenyekiti wa kikao hicho, nafasi yake ilichukuliwa na Mwalimu Kihere
kutoka Tanga.
Mwalimu Nyerere aliweza kuushawishi Mkutano kukubali kushiriki katika Uchaguzi Mkuu
wa kwanza mwaka 1958.
Hoja za Mwalimu zilikuwa ni kwamba kama TANU
isingeshiriki, ingekuwa imeshindwa kwani isingekuwa na wawakilishi katika Baraza la
Kutunga Sheria. Kujitoa katika uchaguzi huo kungekuwa na maana ya kujitoa katika
uwanja wa mapambano ambao sasa ungemilikiwa na UTP. Uamuzi wa TANU kushiriki
katika uchaguzi huo ulikuwa ni wa busara kwani wagombea wote waliosimamishwa kwa
tiketi ya TANU walishinda na hivyo TANU kunyakua viti vyote vya wajumbe wa
kuchaguliwa wa Baraza la Kutunga Sheria.
Matokeo ya kukubali kura ya mseto, aliyekuwa Katibu Mwenezi wa TANU, Ndugu Zuberi
Mtemvu aliamua kuachana na TANU na kuanzisha African National Congress (ANC)
mwaka 1958. Hata hivyo toka kuanzishwa kwake hadi kifo chake, ANC haikupata hata
kiti kimoja katika Baraza la Kutunga Sheria. Aidha, Ndugu Mtemvu alibwagwa kwa
11
Uhuru wa Tanganyika ulipatikana katika kipindi cha miaka saba tu ya kudai uhuru.
Kipindi hiki ni kifupi. Siri ya TANU ya ushindi ilitokana pamoja na mambo yafuatayo:
Aidha TANU iliweza kushinda changamoto katika sura ya hila na vikwazo kadhaa na
kupata mafanikio kama vile:3.0
ASP
NA HARAKATI ZA MAPAMBANO DHIDI YA
KIINGEREZA NA USULTANI WA KIARABU
3.1
UKOLONI WA
(iii)
(iv)
(v)
ASP ilizaliwa baada ya Vita Kuu ya Pili. Uingereza ilitoka vitani ikiwa
maskini ajabu ikilinganishwa na kipindi kabla ya vita na haikuwezekana
tena kuendelea kushikilia makoloni yake. Marekani ilizuka katika vita ikiwa
Taifa lenye nguvu zaidi kuliko mataifa yote ya Ulaya Magharibi.
ASP ilizaliwa baada ya vyama vya siasa vingine kuwa vimeibuka katika
nchi nyingine za Afrika hasa TANU ambayo ilikuwa na mahusiano ya
karibu na ASP. Hata kabla ya ASP, kulikuwa na uhusiano wa kihistoria
uliojengeka tangu kuanzishwa kwa AA Tanzania Bara na Zanzibar na vile
vile kuendeleza ushirikiano huo kupitia TAA na AA ya Zanzibar. Hata
wakati wa kuunganisha AA na SA na kuunda ASP, Rais wa TANU Mwalimu
Nyerere alihudhuria Mkutano huo.
3.2
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
(AA):
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Sheikh
Thabiti Kombo
Muhidini Ali Omar
Ali Ameir
Ameir Tajo
Ali Khamis
Mdungi Ussi
Haji Khatibu
Othman Sharif
14
Katika uchaguzi huo, ASP ilipata viti 5 kati ya 6. Kiti hicho kimoja cha Stone Town
kilichukuliwa na mgombea wa Muslim Association ambacho kilikuwa Chama cha
Wahindi wasiokuwa Hindu. Ingawa HIZBU ilisimamisha wagombea katika majimbo yote
6 ya uchaguzi, hawakupata kiti hata kimoja.
Baada ya uchaguzi huo, Zanzibar ilitawaliwa na vituko. Serikali ya kikoloni ilimteua Ali
Muhsin Barwani kuwa Waziri. Huyu alikuwa Rais wa ZNP (HIZBU) aliyeangushwa na
Abeid Amani Karume kwa kura 3,328 dhidi ya kura 918 katika Jimbo la Ngambo. ASP
iliwasilisha malalamiko yake kwa Balozi Mkazi wa Kiingereza dhidi ya uteuzi huo lakini
malalamiko hayo yalipuuzwa. Hii ikiwa ni kielelezo cha upendeleo aliokuwa nao Balozi
Mkazi wa Kiingereza kwa Waarabu chini ya ZNP.
Mwaka 1959 Sultan Khalifa bin Haroub alipata nafasi ya kutembelea Uingereza,
mwanae Seyyid Abdulla ndiye akawa Sultani wa muda na wakati huo akajiunga na ZNP.
Mwanae Sultan kujiunga katika Chama cha siasa ilikuwa ni mbinu ya kuwakandamiza
Waafrika.
Sultani na Balozi Mkazi wa Kiingereza walijitahidi kwa nguvu zao zote kuiangusha ASP.
Balozi Mkazi wa Kiingereza aliwaita Washirazi na kuwashawishi kuanzisha Chama chao
wakati Sultani naye aliwashawishi Washirazi wajitoe katika ASP.
Baadhi yao
walishawishika. Kwa mfano, Ameir Tajo alikwenda kinyume na matakwa na maadili ya
15
ASP kwa kumweleza Balozi Mkazi wa Kiingereza kwamba Zanzibar ipatiwe uhuru wake
baada ya miaka 10. Kamati Kuu ya ASP ilihitaji uhuru wa Zanzibar upatikane mwaka
1960. ASP ilimfukuza Ameir Tajo uanachama na uongozi. Aidha, Sheikh Mohammed
Shamte na Sheikh Ali Sharif Mussa walijiondoa kutoka ASP baada ya Sheikh Ameir Tajo
kufukuzwa.
Zanzibar and Pemba Peoples Party (ZPPP) ilizaliwa mwishoni mwa mwaka 1959. ZPPP
ilianzishwa na wanachama wa ASP waliofukuzwa na kujiondoa kutoka ASP. Rais wa
ZPPP alikuwa Sheikh Mohammed Shamte. Miongoni mwa viongozi mashuhuri wa ASP
waliounda ZPPP ni pamoja na Sheikh Ameir Tajo aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya
ASP na Mjumbe wa Baraza la Kutunga Sheria akiwa Mwakilishi wa Unguja Kusini na
Sheikh Ali Shariff Mussa ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Baraza la Kutunga Sheria
akiwakilisha Pemba Kaskazini. Ikumbukwe pia kwamba Sheikh Mohammed Shamte
alikuwa akiwakilisha Pemba Kusini katika Baraza la Kutunga Sheria. Kwa hiyo kuondoka
kwa hao Wajumbe 3 kulikuwa na maana ya ASP kubakia na Wajumbe 2 katika
Baraza la Kutunga Sheria. Wajumbe hao wawili ni Sheikh Abeid Amani Karume
akiwakilisha Jimbo la Ngambo na mwakilishi wa Unguja Kaskazini, Sheikh Daud
Mahmoud.
Kitendo cha kuzaliwa ZPPP kilifurahisha sana HIZBU na Balozi Mkazi wa Kiingereza.
Katika furaha hiyo, Balozi alitoa nafasi kwa Rais wa ZPPP, Sheikh Mohammed Shamte
kwenda kutembelea Uingereza na Marekani.
3.4
16
(3)
(4)
(5)
3.5
ASP, ZNP na ZPPP walishiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Pili uliofanyika Januari, 1961.
Tangazo la tarehe 16 Januari, 1961 lililotolewa na Balozi Mkazi wa Kiingereza lilieleza
wazi kwamba chama cho chote kitakachopata viti zaidi katika uchaguzi mkuu wa pili
ndicho kitakachounda Serikali. Katika uchaguzi huo, majimbo ya uchaguzi yalikuwa 22
yaani majimbo 13 Zanzibar na majimbo 9 Pemba.
Matokeo ya uchaguzi huo yalikuwa ifuatavyo:ASP viti 10 (viti 2 Pemba na 8 Unguja)
ZNP viti 9 ( viti 4 Pemba na 5 Unguja)
ZPPP viti 3 (viti 3 Pemba na 0 Unguja).
Kwa mujibu wa matokeo hayo, mshindi alikuwa ni ASP. Hata hivyo, matokeo
hayo yalibadilika baada ya Wajumbe 2 wa ZPPP Sheikh Mohammed Shamte na
Sheikh Bakari Mohammed Bakari kuamua kujiunga na ZNP na Mjumbe mmoja
Sheikh Ali Shariff Mussa kujiunga na ASP.
Kwa kuzingatia kwamba ASP na ZNP walikuwa na viti sawa katika Baraza la
Kutunga sheria, uamuzi ulifikiwa wa kuunda Serikali ya Mseto ambayo ilitakiwa
kudumu kwa muda wa miezi sita.
3.6
Katika uchaguzi huo, majimbo ya uchaguzi yaliongezwa toka 22 hadi 23. Jimbo jipya la
uchaguzi lilikuwa Mtambile, Pemba Kusini ambapo ZPPP ilikuwa na nguvu. ASP, ZNP,
ZPPP vilishiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Tatu.
Hata hivyo,
ZNP na ZPPP walikuwa na makubaliano kwamba anaposimamishwa mgombea wa ZNP
asisimamishwe mgombea wa ZPPP na kinyume chake. ASP ilisimamisha wagombea
wake katika majimbo yote 23 ya uchaguzi.
Matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Tatu uliofanyika tarehe 1 Juni, 1961:
Kuhusu kura, waliojiandikisha kupiga kura ni 94,218 na waliopiga kura ni 90,595 sawa
na asilimia 96.15. ASP ilipata asilimia 49.9 ya kura zote zilizopigwa, ZNP asilimia 35.0,
ZPPP asilimia 13.7 na kura zilizoharibika zilikuwa asilimia 1.4
Matokeo haya yanaonyesha kwamba ZNP na ZPPP kwa pamoja walipata viti 13 na ASP
viti 10.Balozi Mkazi wa Kiingereza alimwomba Sheikh Ali Muhsin Barwani, Rais wa ZNP
kuunda Serikali ya madaraka ambaye pia alitoa nafasi hiyo kwa Sheikh Mohammed
Shamte, Rais wa ZPPP kuwa Waziri Mkuu.
Uchaguzi Mkuu wa Tatu ulitawaliwa na vurugu:
Mkutano wa kwanza wa Katiba ulifanyika London Machi, 1962. ASP iliongozwa na Mzee
Karume na Othman Shariff wakati ZNP na ZPPP iliongozwa na Ali Muhsin Barwani
(ZNP) na Mohammed Shamte (ZPPP). Baada ya Mkutano huo, Umma Party chini ya
Abdurahaman Mohammed Babu ilizaliwa. Umma party ilikuwa na fikra za kimapinduzi,
hususan fikra za kikomunisti. Babu alijitoa ZNP na hili lilikuwa ni pigo kwa chama
hicho.
3.7
Kuhusu kura, ASP ilipata kura 87,085 sawa na asilimia 54.21; ZNP na ZPPP kwa pamoja
zilipata kura 73,559 sawa na asilimia 45.79 ya kura zote halali zilizopigwa.
Kwa matokeo hayo, Sheikh Mohammed Shamte alitakiwa na Balozi Mkazi wa Kiingereza
Kuunda Serikali ya Ndani tarehe 17 Julai, 1963. Mkutano wa Pili wa Katiba ulifanyika
18
London kuanzia tarehe 20 hadi 24 Septemba, 1963 na Zanzibar ilipewa uhuru wake wa
bandia tarehe 10 Desemba, 1963 kwa mujibu wa makubaliano ya Lancaster House
London.
Mapinduzi:
Mara baada ya uhuru, ASP ilianza maandalizi ya kufanya Mapinduzi. Kamati ya
Mapinduzi ya watu 14 iliteuliwa na Mzee Karume na kupewa jukumu la kuandaa na
kuendesha mapinduzi. Wajumbe wa Kamati hiyo walikuwa:
(1)
(2)
(3)
(4)
(5)
(6)
(7)
(8)
(9)
(10)
(11)
(12)
(13)
(14)
Seif Bakari
Said Washoto
Abdalla Natepe
Khamis Hemed
Said Idi Bavuai
Yussuf Himid
Pili Khamis
Mohammed Abdalla
Hafidh Suleiman
Hamid Ameir
Ramadhani Haji
Khamis Darwesh
Mohammed Mfaranyaki
John Okello
19
4.0
Kutoka TANU:
1.
2.
3.
4.
5.
6.
7.
8.
9.
10.
Ndugu
Ndugu
Ndugu
Ndugu
Ndugu
Ndugu
Ndugu
Ndugu
Ndugu
Ndugu
Peter A. Kisumo
Pius Msekwa
Daudi N. Mwakawago
Kingunge Ngombale-Mwiru
Jackson Kaaya
Peter S.Siyovelwa
Nicodemus M. Banduka
Lawi N. Sijaona
Beatrice P. Mhango
Basheikh A. Mikidadi
Mkutano Mkuu wa Pamoja wa vyama vya ASP na TANU uliofanyika tarehe 21 Januari,
1977 uliazimia ifuatavyo:Sisi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa pamoja wa TANU na ASP
tuliokutana leo tarehe 21 Januati, 1977 mjini Dar es Salaam, chini ya uongozi wa
pamoja wa Mwalimu Julius K. Nyerere, Rais wa TANU na Ndugu Aboud Jumbe,
20
4.2
CCM kama ilivyokuwa kwa TANU na ASP, kimeendelea kuongoza nchi yetu hata
chini ya mfumo wa vyama vingi vya siasa uliorejeshwa rasmi tarehe 1 Julai,
1992. Changamoto inayoikabili CCM ni kuendelea kuwa chombo cha uongozi
katika mazingira haya ya mfumo wa vyama vingi vya siasa na mazingira ya
utandawazi bila ya kuwepo Baba wa Taifa.
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alifariki dunia tarehe 14 Oktoba, 1999 Jijini
London katika Hospitali ya Mtakatifu Thomas. Kifo cha Baba wa Taifa kilikuwa ni
pigo kubwa kwa CCM na Taifa letu. Kwa Watanzania, Mwalimu ni maarufu kwa
sababu yeye ndiye mwanzilishi wa Taifa letu, ni mwanzilishi wa TANU hadi kuleta
uhuru; Mwalimu na Mzee Abeid Amani Karume ndio walioasisi Muungano;
Mwalimu na Mzee Aboud Jumbe ndio walioasisi CCM; Mwalimu ndiye aliyelijenga
21
HITIMISHO:
5.1
kuimarisha umoja;
kujenga utaifa na uzalendo;
kupanua demokrasia ndani ya chama;
kubadilika mara kwa mara kifikra na kimuundo kulingana na wakati;
pamoja na kutambua na kushughulikia matatizo ya wananchi.
CCM kinayo nafasi nzuri ya kujifunza mambo mengi mazuri kutokana na historia ya
TANU na ASP. Katika kipindi kinachotukabili inabidi CCM kikabiliane na changamoto
mbalimbali kwa kutumia mafunzo si tu yatokanayo na historia ya TANU na ASP, bali pia
kwa kuzingatia uzoefu wake hadi sasa. Changamoto ya utandawazi na majukumu ya
kisiasa, kiuchumi kiutamaduni na kijamii hayana majibu katika historia peke yake.
Mada zinazofuata zinatoa fursa ya kutafakari mustakabali, mbinu na mikakati ya
kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo mbele ya CCM ili kiendelee kushinda na
kuendelea kuwa Chama Tawala kinachokidhi matakwa ya Watanzania.
22