Professional Documents
Culture Documents
Jivunie Kiswahili
Jivunie Kiswahili
JIVUNIE KISWAHILI
UAMILIAJI LUGHA SARUFI MAJUMUI NA UAMILIAJI LUGHA YA PILI.
Makala haya yataangalia maana ya sarufi majumui, masuala ya msingi yanayohusu
maarifa ya lugha, sifa za sarufi majumui, sarufi majumui na uamiliaji lugha ya pili na
mwisho tathmini. Kwa mujibu wa Chomsky (1976:29) kama alivyonukuliwa na Ellis
(1996:430) sarufi majumui ni mfumo wa kanuni na sheria ambazo ni msingi wa lugha
za binadamu (tafsiri yangu). Muasisi wa nadharia hii ni Noam Chomsky. Msingi wa
nadharia hii ni kwamba binadamu anapozaliwa anakuwa na maarifa asilia ambayo
humsaidia katika ujifunzaji lugha; mambo ya ndani na nje ambao husaidia katika
uamiliaji wa lugha. Maarifa haya hupatikana pale tu binadamu anapozaliwa kwani
huwa na kifaa cha uamiliaji lugha ambacho kinakuwa na kanuni majumui na kanuni
badilifu ambazo hukutana na tajiriba (uwezo wa jamii katika lugha) na kusababisha
uamiliajli lugha kutokea. Waamiliaji wa lugha ya kwanza huwa na maarifa asilia
ambayo huwawezesha kuiamili lugha yao kwa kutumia maarifa hayo. Hivyo maarifa
hayo yanaamshwa na tajiriba ambayo mjifunzaji anaikuta katika jamii iliyomzunguka
na hatimaye kukutana na maarifa asilia katika kifaa cha uamiliaji lugha hatimaye
kuzalisha sarufi mahsusi ya lugha husika. Waamiliaji wa lugha ya pili wanakuwa na
lugha ya kwanza ambapo sifa za sarufi majumui bado humwezesha kuamili lugha ya
pili, kwani kanuni badilifu na kanuni majumui zilizojengwa kwa misingi ya lugha ya
kwanza hutumika katika kuamilia lugha ya pili. Hivyo kwa mujibu wa nadharia ya
sarufi majumui inamsaidia mjifunzaji katika kuamili lugha ya pili. Wataalam
mbalimbali wameweza kujadili juu ya uwezo wa sarufi majumui wa kuwa kifaa
weazeshi cha kujifunza lugha ya pili, kuna wataalam wanaokubali na wanaokataa
mchango huo. Kama Flyn (1984-1987) anavyoelezea kama alivyonukuliwa na Ellis
(1996:453) kifaa cha uamiliaji lugha ya kwanza kitahusika na mchakato wa ujifunzaji
lugha ya pili. Akaendelea kusema kanuni badilifu za lugha ya kwanza na lugha ya pili
zikiwa sawa ujifunzaji utakuwa rahisi kwa sababu mjifunzaji wa lugha ya pili ana
uwezo wa kuhusisha miundo wakati kanuni hizo zikitofautiana kati ya lugha ya
kwanza na lugha ya pili ni vigumu kujifunza. Flyin yeye anaunga mkono juu ya
sarufi majumui kuwa kifaa wezeshi katika ujifunzaji wa lugha ya pili. Kwani
anaamini bado maarifa ambayo mjifunzaji wa lugha ya kwanza anayoyatumia katika
ujifunzaji wa lugha hiyo, ndiyo yale yale anayoyatumia mjifunzaji wa lugha ya pili.
Hata hivyo Clahsen na Muysken (1986-1991) kama walivyonukuliwa na Ellis
(1996:454) wanasema uamiliaji wa lugha ya pili ni tofauti na uamiliaji lugha ya
kwanza muamiliaji lugha ya kwanza huwa na kifaa wezeshi cha uamiliaji lugha
wakati wa lugha ya pili hutumia mbinu za lugha ya kwanza katika kujifunza lugha ya
pili wanaendelea kusema muamiliaji lugha ya pili huhitaji nadharia ya isimu wakati
wajifunzaji lugha ya pili huhitaji naharia tambuzi. Hata hivyo sarufi majumui
imeangaliwa katika mitazamo tofautitofauti, hivyo kuonesha ubora lakini pia
mapungufu yake katika ufundishaji wa lugha: Kwa kuwa na sarufi majumui tunaona
kuwa sifa za lugha huingiliana, hivyo mwingiliano wa lugha ya kwanza na ya pili
unaweza kumwezesha muamiliaji lugha ya pili pale miundo ya lugha ya kwanza na
lugha ya pili itafanana na hata ikitofautiana mjifunzaji anakuwa na uwezo wa
kujiundia miundo yake itakayomsaidia katika ujifunzaji wake kwa kutumia sifa
majumui za lugha. Flynn (1984;1987) kama alivyonukuliwa na Ellis(1996;453)
anaeleza kuwa kifaa cha uamiliaji lugha ya kwanza kinaweza kutumika katika
uamiliaji wa lugha ya pili. Kama kanuni badilifu za lugha ya kwanza na ya pili
zinauhusiano hurahisisha ujifunzaji. Hivyo yeye anakubali kabisa kuwa sarufi
majumui ni kifaa wezeshi katika ujifunzaji wa lugha ya pili, anaamini sifa za
mjifunzaji wa lugha ya kwanza ndizo ambazo anakuwa nazo mjifunzaji wa lugha ya
pili. Aidha Ellis (1994:461) anaeleza ubora wa sarufi majumui kuwa imetoa msingi
wa uibukaji wa nadharia zingine za ujifunzaji lugha baada ya kuegemea kwenye
maarifa asilia anayozaliwa nayo binadamu. Pia imeweza kueleza sifa majumui za
lugha mbalimbali za ulimwengu kwa ufupi, hivyo kusababisha sifa za lugha
kueleweka kwa urahisi kwa wajifunzaji wa lugha ya pili. Kwa mujibu wa Ellis
(1994:458) udhaifu huu unajidhihirisha katika maeneo kadhaa, kiini cha sarufi
majumui yenyewe, pia mbinu zilizotumika kukusanyia data. Hivyo inaonekana kuwa
10
11
Daniel
Jones
..........................Inaendelea
anaiona
fonimu
kuwa
ni
[umbo]
halisi.
12
13
MOFOFONEMIKI YA KISWAHILI
Katika mada hii tumeangalia fasili ya mofofonemiki kwa mujibu wa wataalam
mbalimbali, kisha tukaangalia kwa ufupi historia ya nadharia ya mofofonemiki na
katika kiini cha mada tumejadili sababu zilizopelekea kuibuka kwa nadharia ya
mofofonemiki. Kwa kuanza na fasili ya mofofonemiki kwa mujibu wa mtandao wa
Wikipedia wanafafanua mofofonemiki kuwa ni tawi la isimu linalojishughulisha na
mwingiliano wa michakato ya kimofolojia na kifonolojia au kifonetiki. Pia
hujishughulisha na mabadiliko ya sauti yanayotokea katika mofimu wakati
zinapoungana kuunda maneno. (Tafsiri yetu). fasili hii ina mapungufu fulani kwani,
mofofonemiki haijishughulishi na michakato yote ya kifonolojia na kimofolojia bali
ni baadhi tu ya michakato hiyo ambayo ilishindwa kufafanuliwa kwa kutumia data za
kifonolojia au kifonetiki peke yake. The New Oxford American Dictionary
inafafanua kwamba, mofofonolojia/mofofonemiki ni tawi la isimu linalojishughulisha
na uwakilishi wa kifonolojia wa mofimu. Hivyo basi tunaweza kusema kuwa,
mofofonemiki ni tawi la isimu linaloshughulikia matumizi ya kimofolojia katika
kueleza baadhi ya tofauti za kifonolojia ambazo isingewezekana kuzielezea kwa
kutumia data za kifonetiki au kifonolojia peke yake. Baada ya kuangalia fasili ya
neno mofofonemiki ifuatayo ni historia fupi ya nadharia ya mofofonemiki. Kwa
mujibu wa Massamba (2010:82) akimrejelea Martnet (1965) anafafanua kwamba,
istilahi hii mofofonemiki/mofofonolojia ilipendekezwa kwa mara ya kwanza na N.S.
Trubetzkoy (1929). Trubetzkoy alitumia istilahi hii kwa maana ya tawi la isimu
ilinaloshughulikia matumizi ya mafolojia katika kuelezea baadhi ya tofauti za
kifonolojia ambazo isingewezekana kuzielezea kwa kutumia data za kifonolojia au
kifonetiki peke yake. Baada ya kuangalia historia fupi ya mofofonemiki yafuatayo ni
mambo yaliyosababisha kuibuka kwa nadharia ya mofofonemiki. Kuchunguza
ubadilikaji wa sauti ambao usingeweza kuelezwa kwa kutumia data za kifonolojia
peke yake. Baadhi yao wakapendekeza kuwapo kwa kiwango cha kimofofonemiki
pamoja na kipashio umbo kiini kama kiwakilishi cha mofimu, kwa hiyo
14
walipendekeza hivyo baada ya kushindwa kujua ipi ni alofoni ya fonimu ipi kwa
kutumia kigezo cha kifonetiki pekee Kwa mfano;
walishindwa kujua /k/ ni alofoni ya /c/ au /c/ ni alofoni ya /k/ Kwa mfano hata katika
lugha ya kurusi ruka = mkono runoj = a mkono Mzizi ni ruk na ru
Wanamofofonemiki walichunguza wakagundua kuwa katika mazingira fulani /k/
hubadilika kuwa // baada ya kufuatiwa na noj. Hivyo wakapendekeza umbo kiini
la maneno haya ni ruKa au runoj umbo kiini lake lilitambulika kama {K} au {}
Katika lugha ya Kiswahili kuna mabadiliko ya sauti yanayotokea katika baadhi ya
maneno baada ya sauti fulani kufuatiwa na kiambishi cha unominishaji (i) kwa mfano
katika maneno yafuatayo;
Fuata fuasi
Penda Penzi
Cheka Cheshi
Pika Pishi Pia
Wanamofofonemiki walichunguza ubadilishanaji huu wa sauti kwani walishindwa
kujua ipi ni alofoni ya fonimu ipi. Ndipo wakagundua kuwa katika mazingira fulani
/t/ hubadilika kuwa /s/ baada ya kufuatwa na mofimu ya unominishaji i pia sauti /d/
hubadilika na kuwa /z/ baada ya kufuatwa na mofimu ya unominishaji i Baada ya
kupendekeza umbo kiini maneno haya yakaandikwa kama ifuatavyo: kwa mfano
neno {fuaTa} umbo {T} likawa umbo kiini ambalo linawakilisha sauti zote mbili
yaani /t/ na /s/, pia neno {piKa} umbo kiini lake ni {K} ambalo linawakilisha sauti /k/
na // Kuchunguza mabadiliko ya sauti yanayotokea mofimu zinapoungana. Kwa
mfano;
katika lugha ya Kiswahili, U + ima wima I + etu yetu Mu + alimu Mwalimu U
+ imbo wimbo Vi + ake vyake Wanamofofonemiki wakagundua kuwa sauti fulani
huweza kuungana na kuunda sauti moja na kubadili umbo la neno. Chunguza
muundo wa kifonolojia wa mofimu katika lugha.
15
Else
[els]
Place
[pleis]
Wanamofofonemiki
wakachunguza
16
17
njia hii ni ya taratibu mno kuliko njia zingine katika ukusanyaji wa data. Hojaji
zimegawanyika katika makundi makubwa mawili; kwanza hojaji funge na hojaji za
wazi (zisizo funge). Hojaji funge maswali yake yako wazi na yanaeleweka kwa
watafitiwa. Maswali yanayoulizwa yanakuwa sawa kwa watafitiwa wote, yanalenga
kutoa jibu moja tu. Mfano ndiyo au hapana, au ya kuchagua a,b,c,d. hayaruhusu
mtafitiwa kuweka hisia zake. Muundo wa maswali waweza kuwa funge.
Kwa mfano;
ANDIKA N KAMA JIBU NI NDIYO NA H KAMA JIBU NI HAPANA. AU
CHAGUA HERUFI YA JIBU SAHII TU. Hojaji isiyo funge ni hojaji ambayo
inamruhusu mtafitiwa kutoa maelezo/kujieleza/au kutoa maoni ya ziada (kutoa
ufanuzi zaidi kadri ya uelewa wake kulingana na jinsi alivyoulizwa) Hojaji kama njia
ya ukusanyaji data ina kanuni muhimu za kuzingatiwa wakati wa kuiandaaa. Mtafiti
hana budi kuzingatia mambo yafuatayo;
kwanza; ajue TATIZO LA UTAFITI. Mtafiti akishajua tatizo la utafiti itamsaidia
kuandaa hojaji yake katika muundo unaotakiwa. Kwa mfano; atajua ni eneo gani
ataenda kufanyia utafiti wake, umri wa watafitiwa, jinsia na kiwango chao cha elimu.
Tatu izingatie usuli wa watafitiwa kama vile jina, umri jinsia, kabila na kiwango cha
elimu. Hii inasaidia mtatifi katika uchambuzi wa data kujua amehoji watu wa umri
gani na amehoji watu wa kiwango gani cha elimu. Pili ni mtiririko mzuri wa maswali;
ili kutengeneza/kuandaa hojaji nzuri na kupata majiu sahihi mtafiti lazima azingatie
mtiririko
mzuri
wa
uaandaaji
wa
maswali.
Mtiririko
mzuri
unaondoa
uvulivuli/ukakasi kwa mtafitiwa, hivyo basi maswali lazima yawe katika mtiririko
ufuatao; Kuanzia maswali mepesi kwenda maswali magumu, hii itampa moyo
mtafitiwa au kumvutia na kuonesha ushirikiano lakini pia yatamvutia na kumpa moyo
hivyo ataonesha ushirikiano au kupata hamasa ya kutaka kutoa majibu zaidi. Maswali
hayo yawe na uhusiano/ muwala. Maswali yafuatayo hayana budi kuekwa; maswali
yanayomtaka mtafitiwa kufikiri sana maswali yanayomhusu mtafitiwa, mfano una
watoto wangapi, mkewe yuko wapi, kwa nini huna mtoto? Maswali yanayohusiana
18
na mali za mtafitiwa, mfano je una magari mangapi? Au unalipwa kiasi gani kwa
siku? Maswali yanayofuata baada ya maswali ambayo hayana budi kuepukwa ni
maswali yanayohusiana na mada ya utafiti. Ambayo yanamtaka mtafitiwa kufikiri
kiundani ili kuweza kutoa majibu sahihi. Mfano, nafasi ya uchaguzi wa lugha ya
Kiswahili kama lugha ya kufundishia elimu ya juu. Maswali yalenge nini kinapelekea
Kiswahili kuteuliwa kuwa lugha ya kufundishia elimu ya juu. Au tatizo la utafiti ni
watoto wa mtaani. Kwa hiyo maswali yalenge sababu za kuwepo watoto wa mitaani.
Maswali magumu yaulizwe mwishoni. Hii ina faida kwa sababu, hata kama mtafitiwa
atashindwa kujibu kutokana na sababu mbalimbali maswali yale ya awali yatakuwa
yanatosha kutoa taarifa muhimu zinazohusu tatizo la utafiti. Pia mtiririko wa maswali
lazima uanze na maswali ya jumla kwenda maswali mahususi. Mtafitiwa hana budi
kuelewa kuwa majibu yaliyotolewa ni kwa ajili ya utafiti huo. jinsi/namna ya utungaji
wa maswali hayo; kutunga maswali katika mtiririko mzuri kwa kuanza na maswali
rahisi kwenda magumu lakini pia kwa kuzingatia maswali ya jumla kwenda maswali
mahususi. Maswali magumu yanaulizwa mwishoni. Maswali yanayotungwa yawe
wazi, yasiwe na upendeleo wa kijinsia au kisiasa au kidini. Maswali yazingatie
vigezo vifuatavyo; Maswali, yawe mafupi, yenye wazo moja, pia yawepo maswali ya
majibu mafupi ya ndiyo au hapana, ya kuchagua na yawepo maswali ya kutoa
maelezo. maswali yaeleweke/yawe sanifu maswali yaendane na uwezo wa kufikiri
wa mtafitiwa, mfano unasuka kwa mwaka mara ngapi? Swali hilo ni gumu kwa
maana hiyo lingeweza kuulizwa kuwa, kwa wiki unasuka mara ngapi? Hii itasaidia
kufikiria kwa haraka. Kanuni ya pili hojaji isiwe ndefu sana, na kila hojaji iwe na
lengo moja tu. Matokeo ya hojaji kuwa ndefu itamchosha mtafitiwa. Muhimu
maswali yasidokeze majiu. Kwa mfano Hivi wewe ndo Honest? Hapa hospitali
nasikia hakuna huduma nzuri ni kweli? Tatu izingatie usuli wa watafitiwa kama vile
jina, umri jinsia, kabila na kiwango cha elimu. Hii inasaidia mtatifi katika uchambuzi
wa data kujua amehoji watu wa umri gani na amehoji watu wa kiwango gani cha
elimu.
19
20
HASARA
Ni vigumu kukabiliana nayo, kwa maana kwamba inaibua ugumu wa kubaini majibu
sahihi ya swali lililoulizwa hii ni kwa sababu maelezo yanakuwa mengi. Pia
mtafitiwa anaweza akawa na mtizamo hasi kwa hiyo akajibu ndivyo sivyo. Kwa
hakika hojaji nzuri haina budi kutumia njia zote mbili yaani njia ya maswali funge na
njia ya maswali ya wazi. Kwani kwa kufanya hivyo unaweza kupata majibu ya ndiyo
au hapana kadri ya maswali yaliyoulizwa, lakini pia utapata maoni mbalimbali na
picha halisi kulingana na mtizamo wa mtafitiwa. Mtafiti lazima awe makini katika
maneno anayotumia katika kuaandaa maswali, maneno yawe na maana. Pia mtafiti
lazima atumie sentensi rahisi. Maneno ambayo ni magumu ambayo hayaeleweke,
istilahi za kitaalumaau na yenye maana zaidi ya moja lazima yaepukwe. Pia maneno
ambayo hayaendani na utamaduni wa jamii husika lazima yaepukwe Kimsingi utunzi
wa maswali na utumiaji wa maneno ni sanaa ambayo inahitaji mtu kujifunza.
MJENGO WA FASIHI SIMULIZI NA FASIHI ANDISHI MJENGO WA
FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI. MJENGO WA FASIHI ANDISHI YA
KISWAHILI
21
22
23
24
kuunda maneno. Kutokana na fasili hii, kipashio cha msingi katika uchambuzi wa
kimofolojia ni neno ambalo ndilo hutumika kuunda darajia ya sintaksia. Vilevile
maumbo ya kimofolojia huathiri vipengele vingine vya kisintaksia, kwa mfano,
sentensi zifuatazo hufafanua zaidi:
1. Mtoto anacheza.
2. Watoto wanacheza. Katika mifano hii tunaona kwamba mofimu m- na wa- katika
upande wa kiima zimeathiri utokeaji wa mofimu a- na wa- katika upande wa kiarifu.
Pia kanuni za mfuatano na mpangilio wa mofimu au viambishi zikifuatwa huunda
maneno katika miundoya kisintaksia.
Mifano:
1. Alicheza = a-li-chez-a
2. Anaimba = a-na-imb-a
Kwa ujumla kipengele cha umoja na wingi katika maumbo ya kimofolojia ndicho
kinachoathiri umbo linalofuata jina na kuathiri muundo wa sentensi nzima.
Mifano:
1. Mwalimu alikuwa anafundisha.
2. Walimu walikuwa wanafundisha.
Tunaona katika mifano hii maumbo ya umoja na wingi ya maneno Mwalimu na
Walimu yameathiri mpangilio mzima wa sentensi. Uhusiano baina ya semantiki na
sintaksia. Habwe na Karanja wakimnukuu Richard na Wenzake (1985) wanasema
Semantiki ni stadi ya maana. Semantiki ni utanzu unaochunguza maana katika lugha
ya mwandamu. Wanaendelea kusema semantiki hutafiti maana za fonimu, mofimu,
maneno na tungo. Kwa hiyo kutokana na fasili hii maana hushughulikiwa katika
vitengo au viwango vyote vya lugha ambavyo ni fonolojia, mofolojia na sintaksia.
25
Mifano:
a) Paka mweusi amepotea.
b) Mweusi paka amepotea.
c)Amepotea mweusi paka.
Katika mifano hii tunaona kwamba sentensi a) ina maana kutokana na kwamba
imefuata mpangilio sahihi wa maneno katika tungo na sentesi zilizobaki hazina
maana kutokana na sababu kwamba hazijafuata mpangilio ulio sahihi. Kwa mantiki
hii, kwa kuwa semantiki hushughulikia viwango vyote vya lugha, basi hushughulikia
pia kiwango cha sintaksia ambapo huangalia maana za tungo. Tungo yoyote ni lazima
ilete maana inayokubalika na wazungumzaji au watumiaji wa lugha husika, kama
itakuwa kinyume basi haitakuwa tungo bali ni orodha ya maneno tu. Mfano: Mtoto
anacheza mpira uwanjani. Mtoto uwanjani mpira anacheza. Tukiangalia mifano hii
tutagundua kwamba katika sentensi ya kwanza mpangilio wake wa vipashio unaleta
maana lakini sentensi ya pili haina maana kutokana na kuwa na mpangilio mbaya wa
maneno. Kwa hiyo tunaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa sintaksia haiwezi
kutenganishwa na vitengo vingine vya lugha kwa kuwa kuna uhusiano wa moja kwa
moja baina ya vipengele hivi vya lugha na kwa hiyo hutegemeana kati ya kipengele
kimoja na kingine. Kwa mfano, huwezi kupata mofolojia (neno) bila kupitia ngazi ya
fonolojia na pia huwezi kuwa na ngazi ya sintaksia (sentensi/tungo) bila kupitia ngazi
ya fonolojia na mofolojia lakini vitengo vyote hivi hutawaliwa na kitengo cha
semantika ili kuleta mawasiliano miongoni mwa wazungumzaji.
MAREJEO Habwe, J na P. Karanja (2007). Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi:
Phoenix Publishers Ltd. Massamba, D.P.B na wenzake (1999). Sarufi Miundo ya
Kiswahili Sanifu: Sekondari na Vyuo. Dar essalaam: TUKI. Rubanza, Y.I (1996).
Mofolojia ya Kiswahili. Dar es salaam: Chuo Kikuu Huria cha Tanzania. TUKI
26
(2004).Kamusi
ya
Kiswahili
Sanifu.
Dar
es
salaam:
TUKI.
27
KIAMBISHI TAMATI NI
Makala haya yatashughulikia ufupisho wa makala ya Swahili forum iliyohaririwa na
rose marie beck, Thomas gelder na wemer graefner katika uchambuzi wa kiambishi
tamati cha mahali ni, tathmini na mwisho hitimisho. Makala haya yanahusu asili na
usambaaji wa kiambishi tamati cha mahali ni. Karibu lugha zote za kibantu kuna
ngeli tatu za mahali zenye viambishi pa, ku, mu, kwa mfano katika lugha ya kisangu
viambishi hivi vya mahali hujitokeza pia katika maneno ya mu-khati, pa-khati, na kukhati. Kwa upande wa lugha ya kiswahili mofimu hizi yaani pa, ku, mu hutumika
kama viwakilishi vionyeshi kwa mfano hapa, huku na humu na vilevile hufanya kazi
kama viwakilishi vimilikishi. Kwa mfano kwetu, kwao na mwao. Dai hili limetolewa
na Beck na wenzake (1994). Swali la msingi, kama viambishi vya mahali
vinavyojitokeza katika ngeli hizo, kiambishi ni- hakipo, kiambishi hiki kimetoka
wapi?
NADHARIA YA UDENGUZI
NADHARIA YA UDENGUZI
KATIKA
28
29
(i) Maumbile kama vile jinsia, umri, tambo, rangi nk. Pia hutofautiana dini, kiuchumi
nk.
(ii) Wahusika wasiobadilika (bapa) wanaobadilika (duara)
(iii) Wahusika ishara
(iv) Wahusika wafaili: Hujenga wahusika wakuu. Mulokozi (1996) Ametaja aina za
wahusika wa tamthilia; kuna wahusika wakuu:
(i) Mbabe /nguli
(ii) Mkinzani
(iii) Muwi (muovi)
Wahusika wadogo:
(i) Mfoili
(ii) Msimamizi
(iii) Chizi Wahusika hawa walioorodheshwa ni kutokana na uanishaji wa tamthilia za
kimagharibi. Tamthilia kwa upande wa fasihi ya Kiswahili zilifuata baadae, hivyo
ujitokezaji wa wahusika ukawa tofauti hasa baada ya kuingiza Uafrika (upya) katika
sanaa hizi. Hata kama aina ya mhusika ni ile ya Kimagharibi (Mfano msimulizi wa
chizi) lakini ujitokezaji wake ukaanza kuwa wa Kiafrika zaidi hapa ndipo tukaona
udenguzi unatokea, udenguzi huu hautokei kama ajali bali umelenga kuboresha na
kuhifanya tamthilia iendane na mazingira halisi ya fasihi ya Kiswahili, Katika
tamthilia ya Mkutano wa Pili wa Ndege ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi ni katika
matumizi ya wahusika wa kifasihi simulizi. Mwandishi ametumia wahusika wa
kifasihi simulizi ambao ni ndege na wanyama, katika tamthilia. Mfano katika (uk.14
15) mwandishi anasema: Tausi: enyi wa mashariki Poleeni Ogeleeni Chiriku: ko ko
likoo! ooooh! Magharibi sisahau Wahusika hawa (ndege na wanyama) hutumiwa
sana katika fasihi simulizi, hivyo mwandishi amedengua ujitokezaji wa wahusika si
binadamu pekee katika tamthilia za Kiswahili kuna wahusika wasio binadamu. Pia
katika tamthilia ya Jogoo Kijijini na Ngano ya Jadi ujitokezaji wa wahusika
kiudenguzi ni katika matumizi ya wahusika wa kifasihi simulizi. Mwandishi
amemtumia mhusika Joka akaliita sesota, kiishara kuwakilisha ukoloni na jinsi
30
ukoloni huu ulivyokomaa, akalipa joka hilo vichwa sabini, kuonyesha kiasi gani
unavyoziathiri nchi za Kiafrika. Mfano: Katika (uk.21) mwandishi anasema Kwani
Likuwa tabia makini Killa mwaka ukibaini Joka hushuka kijijini Kuchukua mali na
binti mwema mmoja. Matumizi ya joka ni udenguzi. Pia katika tamthilia ya Nguzo
Mama, ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi ni kupitia mhusika Chizi. Chizi kama
inavyoaminika katika jamii ni mtu asiyeweza kuongea neno la maana, lakini katika
tamthilia hii mwandishi amemtumia mhusika huyu na kumwonyesha akieleza kitu
cha msingi na muhimu. Mwandishi anasema: Chizi: Nani anapendeza? Waoneni watu
hawa Hawapendi demokrasia Nikisema yote mie Wananiita mie chizi Chizi mie au
nyie (uk. 29 31) Pia katika tamthilia hiyo hiyo ya Nguzo Mama ujitokezaji wa
wahusika kiudenguzi ni katika majina ya wahusika. Mwandishi amewapa wahusika
wake majina kwa kuanzia na Bi Moja Bi Nane. nk. Majina hayo yote huashiria
uhusika na kifasihi simulizi, kwa kuwa katika hadithi nyingi za Kifasihi simulizi,
huanza hivi. Hapa zamani za kale, palikuwa na baba mmoja na mama mmoja.
Hivyo mwandishi huyu ametumia majina ya kiidadi au kinamba ambayo ni majina
pia ya wahusika wa kifasihi simulizi katika tamthiliya ya Heshima Yangu ujitokezaji
wa wahusika kiudenguzi umejitokeza kupitia mhusika Mzee Issa. Mhusika huyo
anadai heshima ambayo yeye mwenyewe hajailinda heshima hiyo kwa kuzaa nje ya
ndoa na kuificha siri hiyo ya kuwa na mtoto nje ya ndoa yake. Mzee Issa alimkataa
Salum toka akiwa tumboni mwa mama yake, na kisa kutomjua baba yake hadi
ukubwani alipotaka kumuoa Rukia, ndipo anapoambiwa kuwa ni dada yake.
Mwandishi anaonyesha kuwa kuheshimiwa si kwa vile una umri mkubwa tu bali pia
matendo yako yanaweza kukuvunjia heshima hata kama una umri mkubwa.
Mwandishi anasema: Rukia (anasogea mbali na nyumba, anawaza kwa huzuni).
Heshima yangu, heshima yangu (Kimya kwa muda) Ni heshima gani ipatikanayo
katika kumkatalia Salum kijana mzuri, mwenye tabia nzuri na moyo wa imani, eti
kwa sababu ni mwana haramu? Ni kosa.....(uk. 10) Pia katika tamthiliya ya
Mashetani ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi unajitokeza kupitia wahusika wake
Juma na Kitaru. Mwandishi katika tamthilia hii amedengua ujitokezaji wao kutoka
31
kufikia hali ya kuwa na majina yao ya Juma na Kitaru hadi kwenye uhusika wa
kishetani na kibinadamu. Mwandishi ameonesha udenguzi wa wahusika kwani si hali
ya kawaida kwa wahusika kuchorwa hivyo, Mfano:- Muhusika katika tamthilia
akichorwa kama baba, basi atakuwa baba hadi mwisho wa tamthilia hiyo. Pia katika
tamthiliya ya Kivuli Kinaishi ujitokezaji wa uhusika kiudenguzi unajitokeza kupitia
mhusika Bi Kirembwe, ambaye ni mhusika mwanamke lakini amechorwa kitofauti na
wahusika wengine wanawake wanavyochorwa katika baadhi ya kazi za Fasihi.
Mhusika huyu amechorwa kama mtawala na mwenye amri na sauti yakuwatisha hadi
wanaume. Hii ni tofauti kwa uchoraji wa wahusika wa kike katika tamthilia nyingi,
ambazo huwachora katika daraja la chini, duni na kukandamizwa. Mfano Martha
katika tamthiliya ya Kwenye Ukingo wa Thim, amechorwa ni mwanamke
anayekwenda na wakati lakini anakandamizwa na mfumo mzima wa jamii yake kwa
kuonyeshwa akipokonywa mali zote baada ya mume wake kufariki. Pia katika
tamthiliya ya Aliyeonja Pepo ujitokezaji wa uhusika kiudenguzi ni katika matumizi
ya wahusika wakifikirika au wa kiimani, ijapokuwa suala hili limejitokeza pia katika
riwaya za Kusadikika na Kufikirika lakini katika tamthilia hizi mwandishi
amekwenda mbali zaidi kwa kutumia usawiri wa pepo na uhusika wa kiimani zaidi
kuwakilisha mambo yaliyopo au yanayotendeka duniani na si nchi ya kidhahania
kama alivyofanya Shaaban Robert katika riwaya zake za Kufikirika na Kusadikika.
Mwandishi wa aliyeonja pepo ametumia wahusika kama malaika Ziraili, Sirafili,
Jaburili na wengine ambao huamini ni malaika au pepo kuwakilisha mambo
mbalimbali yanayotendeka duniani. Mfano: Mwandishi anasema: Ziraili: Wapi?
Jiburili: Huko ambako wewe bado hajajishughulisha nako Huko...........(uk.3). Katika
tamthiliya ya Lina Ubani ujitokezaji wa wahusika kiudenguzi ni kupitia mhusika Bibi
ambaye anajitokeza mwanzo kabisa mwa tamthilia kwa kuimba. Jambo ambalo ni
udenguzi wa kimuundo wa ujenzi wa tamthilia kwa kufuata misingi ya Kiaristotle,
ambao kimuundo anasisitiza wimbo katika tamthilia uwe mwishoni na si mwanzoni
mwa tamthilia kama alivyofanya mwandishi Penina Mhando katika tamthilia hii
katika ukurasa wa kwanza, mwandishi anatuonesha mhusika Bibi amekaa analia kwa
32
kiudenguzi
unajitokeza
kupitia
mhusika
Mwanahego.
Mwandishi
amemchora mhusika huyo kama mlevi lakini anaongea na kubishana na sauti mambo
yenye maana, tofauti na walevi walivyozoeleka katika jamii, kwamba ni watu
wasioweza kuchangia au kuongea mambo ya msingi katika jamii. Mwandishi
anasema; Mwanahego: Umoja na mke wamo mnajifunika wote shuka moja
Mwanahego na wewe tutakutana wapi ndipo tuwe na umoja....... wewe juu ya kilima,
mimi bondeni.....(Uk.46). Pia katika tamthiliya ya Morani ujitokezaji wa wahusika
kiudenguzi umejitokeza kupitia mhusika Jalia ambao ni mhusika wa kike ambaye
mwandishi amedengua kwa kuonyesha asishiriki bega kwa bega na katika kampeni
za kuwakamata wahujumu uchumi Jalia anashirikiana na mwenzake katika kampeni
hiyo na kuonyesha msimamo wa hali ya juu, na ushupavu wa wanawake katika
ukurasa wa 17 mwandishi anasema: Jalia: Na njia ya kuuzima moto ni kuwasha
moto; moto mkali zaidi. Hivyo ndiyo hatua kamili. Kwa kuhitimisha nadharia ya
Udenguzi na mawazo ya Brecht katika kuwachora wahusika yanalenga katika kuleta
upya
wa
fikra
kwa
watazamaji
na
wasomaji
wa
tamthilia.