Professional Documents
Culture Documents
Ufunguzi Wa Kituo Cha Taaluma Ya Uhasibu Bunju
Ufunguzi Wa Kituo Cha Taaluma Ya Uhasibu Bunju
Kwaupande
wake
MkurugenziMtendajiwaBodiyaTaifayaWahasibunaWakaguziwaHesabu, Bw. Pius
Manenoamesemakuwa,Kituo hicho kilichozinduliwa cha APC hadi kumalizika,
kitagharimu Sh. Bilioni 35 ambapo mpaka sasa fedha zilizotumika ni takribani Sh.
Bilioni 31.5.
Gharama halisi za ujenzi wa kituo hicho zilikuwa Bilioni 14 lakini kutokana na
mzabuni wa ujenzi kuchelewesha ujenzi ndio maana kumekuwa na Ongezeko la
kiasi hicho cha fedha aliongeza Bw. Maneno.
Ujenzi wa kituo hicho ambao uko katika eneo lenye ukubwa wa takribani ekari 14
umehusisha ujenzi wa Kumbi za mikutano zinazochukua zaidi ya watu 1600,
viwanja vya michezo na vyumba vya kisasa 108 vya kulala wageni.
Bw. Maneno amesema kuwa kujengwa kwa kituo hicho kutaifanya Bodi hiyo
kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kilichokuwa kikitumika kukodi kumbi za kufanyia
na kusahisha mitihani ya Bodi (NBAA).
Amezitaja faida zingine kuwa ni kuboreshwa kwa mazingira ya kitaaluma na
wanataaluma wa uhasibu pamoja nakuimarika kwa utawala bora na kuwa chachu
ya uchumi wa viwanda, kwa kuwa Kituo hicho, kinatoa elimu bora
itakayowawezesha wahitimu kuingia kwenye ushindani ndani ya nchi za Afrika
Mashariki na Duniani kwa ujumla.
Ujenzi wa Kituo hicho umedhaminiwa na serikali kupitia mkopo kutoka Mfuko wa
Hifadhi ya Jamii-NSSF, Bodi ya Uhasibu-NBAA na Mbia mwenza wa kituo hicho,
Mfuko wa Pensheni ya Watumishi wa Serikali-GEPF.
Mwisho