Professional Documents
Culture Documents
BIBLIA YA WATOTO, Toleo La Kwanza, 2017. JC-RECORDS STUDIO, Mwandishi-Magulya Meja.
BIBLIA YA WATOTO, Toleo La Kwanza, 2017. JC-RECORDS STUDIO, Mwandishi-Magulya Meja.
YA
WATOTO
JC-RECORDS STUDIO.
Barua pepe:books@jcrecordsstudio.com
I
SHUKURANI
Bila yeye kuwa kiongozi wangu na mshawishi mkuu kwangu basi nisingeweza
kuandika kitabu hiki cha BIBLIA YA WATOTO. Kupitia Roho Mtakatifu
amenitia moyo, amenipa faraja na ameniinua ili nipate kukamilisha vyema wito
wa kuandika kitabu hiki cha BIBLIA YA WATOTO.
Kutoka sakafu ya moyo wangu namshukuru mama yangu Dr. Neema Ellah
Kapalata , Marafiki zangu wawili wa karibu sana Amanda Audax Kapalata na
Jayden-Christ Magulya Meja kwakua nami wakati wote, wakinitia moyo na
kunipa nguvu ya kuitikia wito wangu Kiroho.
II
TABARUKU
Kitabu hiki nakitabaruku kwa rafiki yangu wa karibu sana na mtoto wangu
Jayden-christ Magulya Meja.
Baraka ya uwepo wako imeyapa sura mpya maisha yangu katika namna ya
kipekee sana, hakika Mungu amekutumia kunibadilisha.
Nimeona matendo makuu na upendo mkuu wa Mungu kupitia wewe.
Kitabu hiki ni maalumu kwa ajili ya watoto wote na wazazi wote kupitia baraka
niliyopewa na Mungu ya mwanangu mpendwa Jayden-christ Magulya Meja.
III
YALIYOMO
HAKI MILIKI - I
SHUKURANI - II
TABARUKU - III
YALIYOMO - IV
UTANGULIZI -V
IV
UTANGULIZI
Jukumu la malezi mema kwa watoto wetu ni msingi mkuu na wajibu wa kila
mzazi.
Hakuna njia sahihi zaidi kama kutumia nyenzo bora kabisa katika malezi, yani
mafundisho matakatifu ya neno la Mungu.
Kitabu hiki cha BIBLIA YA WATOTO kinatoa fursa nzuri kwa wazazi au
walezi kufafanua kiurahisi hadithi za mafundisho matakatifu kutoka katika
Biblia.
Kitabu hiki pia kimelenga kuwajengea watoto ufahamu wa matendo makuu ya
Mungu.
Ufahamu huu utawasaidia watoto kukua katika mazingira ya kumfahamu na
kumtumikia Mungu.
Sote tunatambua kuwa neno la Mungu ni chanzo kikuu cha maarifa, hivyo
maarifa haya ya neno la Mungu yatawajenga watoto wetu kuwa wanajamii bora.
Kitabu hiki kimesheheni picha za kuvutia zenye kuakisi simulizi kutoka katika
Biblia.
Nimatumaini yangu kuwa kitabu hiki cha BIBLIA YA WATOTO kitaboresha
malezi bora na mema kwa watoto wetu na kujenga misingi imara ya familia zetu
katika kumtumikia na kumuabudu Mungu.
Mungu awabariki wazazi wote na kuwatumia kama vyombo vyake katika
kusimamia malezi bora ya watoto. Amina.
V
MUNGU AUMBA ULIMWENGU-Sura ya kwanza
Mungu alipoanza kuumba Mbingu na Dunia, Dunia ilikua haina umbo, hivyo
alisema ufanyike mwanga, nao ukafanyika.
Kisha akagawanya giza na nuru, giza akaita usiku na nuru akaita mchana, kwa
pamoja vikafanya siku moja.
Mungu akasema maji yajigawanye, yalipojigawa basi juu ikafanyika anga na
chini ikafanyika bahari. Yote haya yalifanyika siku ya pili ya uumbaji.
Mungu akasema maji yote yajikusanye yafanyike bahari ili ipatikane nchi kavu,
na hivyo ndivyo ilivyofanyika.
Kisha Mungu aliumba mimea ya aina mbalimbali, haya yote yalifanyika siku ya
tatu ya uumbaji.
Mungu akaumba Jua ili litoe mwanga wakati wa mchana, kisha akaumba Mwezi
ili utoe nuru wakati wa usiku, pia akaumba Nyota za angani. Haya yote
yalitendeka siku ya nne ya uumbaji.
Mungu akasema vifanyike viumbe ndani ya Bahari, Mito na Maziwa.
Wakafanyika Samaki na viumbe hai wengine wengi wa aina mbalimbali wa
majini.
Mungu akasema anga ifanyike kuwa na Ndege wa kila aina, navyo ndivyo
ilivyofanyika.
Mungu akaubariki uumbaji wote, haya yote yalifanyika siku ya tano ya uumbaji.
Mungu akasema Dunia ijazwe wanyama wa kila aina watambaao, watembeao na
pia wadudu wa aina mbalimbali.
Kisha Mungu akamuumba Mwanadamu kwa taswira yake, akamuona ni kiumbe
bora kuliko viumbe vyake vyote, hivyo akapewa utawala juu ya viumbe vingine
vyote katika uso wa Dunia, kuanzia katika Bahari, Nchi kavu na Angani.
Mungu alimuumba kwanza mwanaume ambaye jina lake alimuita Adamu na
kisha akamuumba mwanamke kwa kutumia ubavu wa Adamu, naye jina lake
aliitwa Hawa.
Akawabariki wote na kisha akawambia wazae na kuujaza ulimwengu. Haya yote
yalifanyika katika siku ya sita ya uumbaji.
Siku ya saba Mungu alipumzika na hakufanya kazi yoyote . Mungu aliibariki
siku ya saba na kuifanya kuwa siku takatifu ya Mungu.
Uumbaji wa Mungu kama unavyoonekana katika picha. Ndege, wanyama,
mimea, mito na anga.
1
MUNGU AUMBA ULIMWENGU-Sura ya kwanza
Viumbe hai vyote viliishi kwa amani na furaha, hapakua na tabu, dhiki wala
magonjwa.
Somo la kujifunza:
Je, ni somo gani la kimaadili ambalo tunaweza kujifunza kupitia uumbaji
wa Mungu?
2
ADAMU NA HAWA-Sura ya pili
3
ADAMU NA HAWA-Sura ya pili
Somo la kujifunza:
Je, ni somo gani la kimaadili ambalo tunaweza kujifunza kupitia uumbwaji
wa Adamu na Hawa?
4
MAJARIBU NA DHAMBI Sura ya tatu
5
MAJARIBU NA DHAMBI Sura ya tatu
Basi Hawa akatamani kula tunda lile, hivyo akaamua kulichuma na kula,
akaenda pia kumpa mume wake Adamu, naye akaingia katika mtego wa Shetani
kwa kula tunda alilopewa na Hawa.
Baada ya kukiuka amri ya Mungu ya kutokula tunda la mti wa katikati ya
bustani, macho yao yakafunguka na kujiona kuwa wako watupu.
Wakaingiwa na aibu na kutafuta majani na magome ya miti ili wapate kujistiri.
Ilipofika jioni wakasikia sauti ya Mungu ikiita Uko wapi Adamu?
Adam akajibu, Nimesikia sauti yako lakini naogopa niko mtupu.
Mungu akamuuliza, Ni nani amekwambia kwamba uko mtupu?
Adam akajibu, Huyu mwanamke uliyenipa kama msaidizi wangu, kanipa tunda
la mti uliotukataza nami nikala.
Mungu akamuuliza Hawa, Kwa nini umefanya hivyo?
Somo la kujifunza:
Je, ni somo gani la kimaadili ambalo tunaweza kujifunza kupitia majaribu
ya dhambi ya Adamu na Hawa?
6
MAJARIBU NA DHAMBI Sura ya tatu
7
NUHU AJENGA SAFINA-Sura ya nne
8
NUHU AJENGA SAFINA-Sura ya nne
Mungu pia alimuagiza Nuhu kubeba hifadhi ya chakula kwa ajili ya kukidhi
mahitaji ya chakula katika kipindi chote cha gharika kubwa.
Baada ya siku saba Mungu mwenyewe alifunga mlango wa Safina.
Mvua ikaanza kunyesha usiku na mchana kwa siku arobaini bila kukoma.
Mungu akafungulia chemuchemu zote za ardhini. Mafuriko makubwa
yakatokea.
Maji yalikua mita saba juu ya kilele cha mlima mrefu kuliko yote Duniani.
Mungu akamuelekeza Nuhu aingize ndani ya safina Wanyama wawili wawili wa
kila aina ili wasidhurike.
9
NUHU AJENGA SAFINA-Sura ya nne
Somo la kujifunza:
Je, ni somo gani la kimaadili ambalo tunaweza kujifunza kupitia masimulizi
ya maandiko matakatifu kuhusu Nuhu na Safina?
10
MNARA WA BABELI-Sura ya tano
Baada ya kipindi cha gharika kupita, idadi ya watu ikaanza kuongezeka tena.
Wengi wakaweka makazi katika mji ulio mashariki mwa ardhi ya Babiloni.
Mungu aliamrisha watu kujiwekea viongozi miongoni mwa jamii zao.
Katika kipindi hicho alikuwepo muwindaji mmoja hodari aliyeitwa Nimrodi,
alikua ni mtu mwenye haiba ya kiungozi na mwenye ushawishi mkubwa.
Lakini Nimrodi hakua mwaminifu kwa Mungu, alitumia kipawa chake kikubwa
alichopewa na Mungu kuwashawishi watu wajenge jamii ambayo haikumuabudu
na kumtumikia Mungu.
11
MNARA WA BABELI-Sura ya tano
Mji wa Babeli ulikua alama ya umoja wa watu katika jamii ambayo ililenga
kutotii maamrisho ya Mungu.
Pia mnara wa Babeli ulikua ni alama ya umoja wa kidini ambao ulikua na
dhumuni la kupingana na mamlaka kuu ya Mungu.
Watu wale wakaanza kuujenga mnara wa Babeli huku wakishirikiana kwa
kugawana kazi mbalimbali kufanikisha adhima yao.
Kwakuwa wote walikua wakiongea lugha moja Mungu aliona ni rahisi kwao
kukubaliana kufanya kila jambo walitakalo.
Hivyo Mungu akawachanganya lugha yao, wakashindwa kuelewana tena.
Watu wote wakatawanyika sehemu mbalimbali Duniani kote, wengine wakaenda
Mashariki, wengine Magharibi, Kusini na Kaskazini.
Mahali hapo paliitwa Babeli ikimaanisha mchanganyiko au kuchanganyika.
Somo la kujifunza:
Je, ni somo gani la kimaadili ambalo tunaweza kujifunza kupitia watu wa
mnara wa Babeli?
12
MNARA WA BABELI-Sura ya tano
13
KUZALIWA KWA ISAKA-Sura ya sita
Siku moja Ibrahimu alikua pembezoni mwa nyumba yake, akaona watu watatu,
akawasalimu kwa kuwasujudia, kisha akawambia wasipite bila yeye
kuwakarimu kwa chakula.
14
KUZALIWA KWA ISAKA-Sura ya sita
15
KUZALIWA KWA ISAKA-Sura ya sita
Somo la kujifunza:
Je, ni somo gani la kimaadili ambalo tunaweza kujifunza kupitia
mafundisho matakatifu juu ya kuzaliwa kwa Isaka?
Kupitia kuzaliwa kwa Isaka tunajifunza kuwa Mungu hutimiza ahadi zake kwa
wakati alioupanga Yeye. Tunapaswa kumuamini na kumtegemea Mungu.
Kupitia Ibrahimu tunajifunza kuishika imani katika mazuri tunayobarikiwa na
Mungu na hata kipindi ambacho tunapitia magumu katika maisha yetu.
16
KUZALIWA KWA ISAKA-Sura ya sita
17
NDOTO YA YUSUFU-Sura ya saba
18
NDOTO YA YUSUFU-Sura ya saba
Baba yake aliamua kumzawadia Yusufu koti zuri lenye rangi mchanganyiko,
lilikuwa ni koti la heshima na kimamlaka.
Kaka zake kwakuwa walimchukia Yusufu, siku moja walipanga njama ya
kumuua lakini mmoja kati ya kaka zake aliyeitwa Reubeni akawashauri
wasimuue lakini wamtupe katika shimo kubwa la kisima kilichokauka.
Walipomtupa katika shimo hilo ghafla wakaona wafanyabiashara Waishmaeli
kadhaa wakitoka Gileadi wakielekea Misri.
Mmoja wa kaka yake Yusufu aliyeitwa Yuda akawashauri wenzake wamtoe
shimoni na kuumuza kama mtumwa kwa wafanyabiashara wale Waishmaeli.
Hivyo walimuuza Yusufu kwa mfanyabiashara Muishmaeli kama mtumwa kwa
thamani ya vipande ishirini vya fedha.
19
NDOTO YA YUSUFU-Sura ya saba
Somo la kujifunza:
Ni somo gani la kimaadili tunalojifunza kupitia simulizi za mandiko
matakatifu juu ya ndoto ya Yusufu?
20
YUSUFU AKIWA MISRI-Sura ya nane
21
YUSUFU AKIWA MISRI-Sura ya nane
Kutokana imani yake iliyo imara, Yusufu alikataa kufanya dhambi hiyo.
Baada ya kushindwa kumrubuni Yusufu mke wa Farao akamsingizia Yusufu
kuwa alijaribu kumbaka. Farao akaamuru Yusufu akamatwe na kufungwa
gerezani.
Lakini kamwe Mungu hakumuacha Yusufu, akaendelea kusimama naye hata
alipokua gerezani, huko nako akafanywa kuwa kiongozi wa wafungwa wote.
Yusufu alibarikiwa kipawa cha kutafsiri ndoto.
Siku moja Farao aliota ndoto ambayo watu wote wenye elimu ya kutafsiri ndoto
pamoja na waganga wa jadi katika nchi ya Misri walishindwa kutafsiri ndoto ile.
Ndoto ya Farao ilikua hivi, ndotoni aliona ngombe saba walionona wakiwa
kando ya mto, wakatokea ngombe saba wengine walio dhaifu na wamekonda
sana. Ngombe hao saba waliodhoofika wakawala wale ngombe wazuri
walionona.
Kisha akaota ndoto nyingine, katika ndoto hii aliona masuke membamba saba
yametokeza katika bua moja. Masuke hayo saba yakakaushwa na upepo mkali
wa Mashariki, kisha yakajitokeza masuke mengine saba makubwa yaliyojaa.
Masuke yale membamba yaliyo kauka yakameza yale masuke mema yaliyojaa.
Baada ya Farao kusikia juu ya kipawa cha Yusufu kutafsiri ndoto akaamuru
Yusufu atolewe gerezani.
Yusufu akapelekwa mbele ya Farao, naye akaitafsiri ndoto ya Farao kwa
utimilifu mkubwa. Akamwambia Farao kutakua na kipindi cha neema kwa
miaka saba hivyo ni bora kuwa na hifadhi kubwa ya chakula kwakuwa baada ya
kipindi hicho kutatokea kipindi cha ukame mkubwa kwa miaka saba hivyo
hifadhi ya chakula itakayokuwepo itasaidia taifa la Misri na hata watu wengine
katika kipindi hicho cha njaa kali.
22
YUSUFU AKIWA MISRI-Sura ya nane
23
YUSUFU AKIWA MISRI-Sura ya nane
Somo la kujifunza:
Je, ni somo gani la kimaadili ambalo tunaweza kujifunza kupitia maisha ya
Yusufu akiwa Misri?
24
MUSA AFANYWA MWANA MFALME-Sura ya tisa
Wanaisraeli waliishi Misri kwa miaka mingi, wakaongezeka na kuwa wengi sana
kwa idadi.
Mfalme mpya aliyekuwa mtawala wa Misri hakujua vyema juu ya msaada
mkubwa alioutoa Yusufu katika ustawi wa Misri na kuiepusha na janga kubwa la
ukame lililoikumba Misri kwa miaka saba.
Hakupendezwa kabisa na ongezeko kubwa la idadi ya Waisraeli nchini Misri.
Alihofia kuwa idadi yao itawapa nguvu na hata kuamua kuupinga utawala wa
Misri.
Hivyo mfalme akawapa wakati mgumu sana Wanaisraeli wote, aliwapa kazi
ngumu kupita kiasi, zenye mateso na unyanyasaji mkubwa.
Lakini Waisraeli walizidi kuzaliana na kuongezeka.
Baada ya Mfalme kuona Waisraeli wanaendelea kuongezeka, Mfalme akatoa
amri ya kuuwawa kwa kila mtoto wa kiume atakayezaliwa na Mama yeyote wa
Kiisraeli.
25
MUSA AFANYWA MWANA MFALME-Sura ya tisa
Mama mmoja wa kabila la Lawi alizaa mtoto mzuri wa kiume, alimficha kwa
miezi mitatu lakini hakuweza kuendelea kumficha tena.
Hivyo akaamua kumficha katika kikapu kilichotengenezwa kwa majani makavu
na kisha kupakwa lami.
Akamuweka mtoto wake katika kikapu hicho na kukificha katika majani marefu
pembezoni mwa mto Nile.
Katika muda wote huo Dada yake alikua akitazama kikapu hicho na kumlinda
mtoto. Baada ya muda akatokea binti Mfalme wa Misri, aliyeenda kuoga
pembezoni mwa mto Nile.
Akaona kikapu kile huku akisikia sauti ya Mtoto mchanga, aliingiwa na huruma
sana, naye akamwambia Dada yule ampeleke kwa Mama yoyote ili
amunyonyeshe na atakapokua basi atamchukua Mtoto huyo na kuishi naye
katika jumba la Mfalme.
Basi Dada yule akamchukua Musa na kumpeleka kwa Mama yake mzazi ili
aendelee kumtunza na kumnyonyesha bila yule binti Mfalme kujua kuwa mama
anayemtunza Musa ndiyo Mama mzazi wa Musa.
Baada ya mtoto kukua, binti Mfalme alimchukua Mtoto na kumuita jina lake
Musa likiwa na maana ya Aliyetwaliwa kutoka katika maji.
Somo la kujifunza:
Je, ni somo gani la kimaadili tunaloweza kujifunza kupitia simulizi za
maandiko matakatifu kuhusu kuzaliwa kwa Musa na kufanywa mwana
Mfalme?
Kuzaliwa kwa Musa kunatufundisha ni namna gani Mungu ana kusudi lake
katika kila jambo liwe baya au zuri.
Kusudio la Mungu hudhihirisha mema yote ambayo ametuandalia hata pale
tunapoona ni mabaya tu yanayotuzunguka.
Musa alizaliwa kipindi ambacho Mfalme alitoa agizo la kuuwawa kila Mtoto wa
kiume wa Kiisraeli lakini tunaona jinsi mipango ya Mungu ilivyojaa neema
kwani Musa hakuuwawa na aliweza hata kulelewa katika jumba la Mfalme kama
Mwanamfalme.
26
MUSA AONGEA NA MUNGU-Sura ya kumi
Musa aliishi Misri mpaka alipokua mtu mzima. Alikuwa ni mcha Mungu na
mwenye huruma sana juu ya mateso wanayopata Wanaisraeli.
Siku moja alimuona Mmisri mmoja akimpiga Muisraeli, alipotazama na kuona
hakuna watu katika eneo lile Musa alienda kuingilia ugomvi huo na kumpiga
Mmisri huyo kwa jiwe, bahati mbaya Mmisri huyo akafariki.
Taarifa zilipomfikia Mfalme akagadhibika na kuamuru Musa akamatwe mara
moja kwa mauaji hayo.
Musa akatoroka kuelekea nchi ya mbali na Misri, alikimbilia mahali palipoitwa
Midiani.
Musa alikaa huko kwa miaka arobaini, akaoa binti aliyeitwa Sipora.
Akiwa huko Midiani alifanya kazi ya kuchunga mifugo.
27
MUSA AONGEA NA MUNGU-Sura ya kumi
Siku moja akiwa anachunga mifugo, Musa akaona kichaka kikiwaka moto katika
mlima Horebu.
Musa alistaajabu kuona moto ule ukiwaka bila kukiteketeza kichaka kile, hivyo
akaamua kukisogelea.
Mara Mungu akamuita kwasauti na kumwambia, Vua viatu vyako kwasababu
mahali unapokanyaga ni patakatifu. Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, Isaka na
Yakobo. Nimeona watu wangu wanavyoteseka. Nitakutuma kwa Farao ili
kuwakomboa watu wangu kutoka misri.
Musa akiwa ni mwenye mashaka akamjibu, Mimi si kitu mbele ya Farao
nitamwambia nini mpaka akanisikiliza?
Mungu akamwambia, Mwambie Mimi niliye Mungu mkuu nimekuagiza.
Lakini Musa bado alionyesha mashaka juu ya uwezo wake katika kumkabili
Farao.
Basi Mungu akampa Musa nguvu za kutenda miujiza ili akamthibitishie Farao
uweza na ukuu wake.
Mungu akamuamuru Musa atupe fimbo chini, naye Musa akafanya hivyo,
hapohapo fimbo ikageuka kuwa nyoka, Musa akashituka na kutaka kukimbia.
Mungu akamwamuru amshike Nyoka yule mkiani, naye Musa akafanya hivyo,
muda huohuo tena Nyoka yule akageuka kuwa fimbo kama ilivyokua awali.
Ingawa Mungu alimuonyesha miujiza yote hiyo lakini bado Musa alikuwa na
wasiwasi wa kwenda kumkabili Farao, hivyo Musa akatoa kisingizio tena kuwa
yeye si muongeaji mzuri, hataweza kumueleza vyema Farao ujumbe uliotoka
kwa Mungu.
Mungu akamwambia atambariki ndugu yake aliyeitwa Haruni ili awe msemaji
wake mbele ya Farao.
Basi Musa akarejea Misri na kuwambia Waisraeli yale yote ambayo Mungu
amemuagiza.
28
MUSA AONGEA NA MUNGU-Sura ya kumi
Somo la kujifunza:
Je, ni somo gani la kimaadili ambalo tunaweza kujifunza kupitia uhusiano
wa karibu wa Musa na Mungu?
29
Kitabu hiki cha BIBLIA YA WATOTO ni barua ya upendo kutoka kwa
Mungu mwenye upendo mkuu kwa Watoto wote.
BIBLIA YA WATOTO ni kitabu kinachowapa Watoto baraka ya kuujua
ukweli kuhusu Mungu.
Ukweli wa matendo makuu yote ambayo Mungu alitufanyia wanadamu na
mambo ambayo tunapaswa kuyafanya ili kumpendeza Yeye aliye mkuu.
Barua hii ya upendo kutoka kwa Mungu inatufundisha namna gani
unavyotakiwa kuishi, inatuonya, inatuasa lakini pia inatueleza habari njema
ya wokovu wa mwanadamu kupitia Yesu Kristo.
Mungu mwenye enzi anataka tuisome barua hii ya upendo kutoka kwake kila
siku ili tumjue vyema, tumuabudu na kumtumikia.
Kitabu cha BIBLIA YA WATOTO kimeichambua barua ya upendo toka kwa
Mungu katika simulizi nyepesi ili zikapate kuwafunza watoto wote matendo
makuu ya Mungu aliye hai.
Kitabu hiki ni baraka ya kipekee kwa wazazi na watoto kwakua ni nyenzo
bora kabisa ya malezi mema yanayompendeza Mungu.
Sifa na utukufu urudi kwa Mungu.
PAGE 36