Professional Documents
Culture Documents
Maadhimisho Ya Nne Ya Umoja Wa Mataifa Kwa Wiki Ya Usalama Barabarani (Un Road Safety Week)
Maadhimisho Ya Nne Ya Umoja Wa Mataifa Kwa Wiki Ya Usalama Barabarani (Un Road Safety Week)
Wakati nchi za uchumi au kipato cha chini na cha kati hasa zilizopo kusini
mwa jangwa la Sahara zimeendelea kuchangia nusu ya idadi ya vifo
milioni 1.24 kwa mwaka ilhali nchi hizi zina namba ndogo zaidi ya vyombo
vya moto vya usafiri vilivyosajiwa.
Mpango huu ulitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua juu ya
usiamamizi wa ajenda ya usalama barabarani, usalama wa barabara na
uchukuzi ,usalama wa vyombo vya moto, usalama wa watumiaji wa
barabara na huduma stahiki kwa majeruhi wa ajali za barabarani.
Katika kipindi cha mwaka 2016 Jeshi la Polisi limeripoti vifo 3256 na majeruhi
8958.Katika ajali zilizopelekea vifo na majeruhi vyombo vya usafiri binafsi na
pikipiki vimechukua asilimia 48% ya ajali zote ukilinganisha na vyombo
vingine ambavyo ni magari ya abiria,baiskeli na magari ya mizigo.
Kama kauli mbiu ya maadhimisho haya mwaka huu kama nchi eneo la
kudhibiti mwendokasi ndani ya sheria, katika usimamizi wa sheria na
miundombinu bado tuna kazi ya kufanya.Takwimu za Jeshi la Polisi za mwaka
2016 zinaonesha vyombo vya usafiri binafsi na pikipiki vimechangia asilimia
48% ya ajali za barabarani. Ni vizuri kufahamu kuwa magari binafsi
yameendelela kusimamiwa na Sheria ya Usalama Barabarani yaani The Road
Traffic Act, Cap 168 [R.E.2002] Sheria hii imeendelea kwa kiasi fulani
kuruhusu mwendo usio na kikiomo katika maeneo yasiyo na makazi wala
vibao vya kulelekeza mwendo na katika mazingira haya magari binafsi
yameendlea kujikuta kuingia katika ajali. Kadhalika hata maeneo ambayo
vibao vianelekeza kiwango cha mwendo kasi bado katika saa ambazo askari
wa usalama barabarani hawapo barabarani madereva wameendelea kuvunja
sheria ilhali mhanga wa kwanaza wa madhara ya ajali hizi ni wale waliomo
katika chombo husika.
Ni wakati sahihi sasa kwa Serikali yetu kujumuisha juhudi za kupunguza ajali
au kuziondoa kwa kurekebisha mianya iliyopo katika sheria mama ya
Usalama barabarani ili ishabihiane na sheria nyingine zianazosimamia
usafirishaji kwa njia ya barabara nchini.Aidha ni wakati sahihi sasa wa Taifa
kuwa na mpango utakaoshughulikia usimamizi endelevu wa ajenda ya
usalama barabarani, kuangalia ubora wa vyombo vya usafirishaji
vinavyoingizwa nchini, kujumuisha elimu ya utumiaji salama wa barabara
katika mitaala yetu ya elimu na kuhakikisha usanifu na ujenzi wa
miundombinu yetu inazingatia ujenzi wa miundo mbinu salama kwa rika zote
kulingana na maeneo husika.