Professional Documents
Culture Documents
Maulid Ya Mtume (Saw)
Maulid Ya Mtume (Saw)
PRESS RELEASE
Zanzibar 1.12.2017
Sherehe hizo za kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) ambazo hufanyika kila
mwaka Kitaifa hapa Zanzibar ni miongoni mwa kawaida na mila ya Waislamu wa
Zanzibar.
Alhaj Dk. Shein aliungana na Waislamu na wananchi hao wakiwemo viongozi mbali
mbali wa Dini na Serikali pamoja na wananchi ambapo pia, Mama Mwanamwema Shein
nae alihudhuria Maulid hayo akiwa pamoja na viongozi wengine wanawake wa Kitaifa.
Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji alitumia fursa hiyo kuwakaribishwa
wananchi wote pamoja na viongozi mbali mbali akiwemo Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein
katika sherehe hizo za Maulid.
Akisoma khutba Sheikh Muhammed Kassim Said kutoka Kamisheni ya Wakfu na Mali
ya Amana aliwataka Waislamu kuwa kitu kimoja huku akiwasisitiza umuhimu wa
kusaidiana na kuhurumiana kwa lengo la kupata rehema za Allah.
Sheikh Muhammed pia, alitumia fursa hiyo kukemea mambo maovu katika jamii hasa
suala la unyanyasaji wa wanawake na watoto ikiwa ni pamoja na suala zima la ubakaji
jambo ambalo limeanza kushamiri hivi sasa katika jamii na kueleza athari zake na
kutaka mashirikiano ya pamoja katika kulipiga vita.
2
Aidha, alieleza kuwa ni jukumu la Waislamu kusherehekea siku hii adhimu pamoja na
kufuata mafunzo ya Mtume Muhammad (S.A.W) aliyokuja nayo.
Maulid hayo yalimalizika kwa Mlango wa dua uliosomwa na Sheikh Wazir Hassan
Choum, kutoka Mkoa wa Mjini Magharibi na hatimae kufungwa kwa fatha iliyosomwa
na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Qabih chini ya mshereheshaji
Sheikh Hamza Zubeir Rijal.