Professional Documents
Culture Documents
Tamasha Maisara
Tamasha Maisara
Tamasha Maisara
11 Januari , 2018
“Natambua kwamba kazi ya kulipandisha hadhi zaidi tamasha letu hili si ndogo ,
hata hivyo ninayo imani kubwa kwamba si tu uwezo wa kufikia malengo hayo
mnayo bali pia mnaweza.”
Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumatano, Januari 10, 2018) wakati
akifungua Tamasha la Nne la Biashara la Zanzibar lililofanyika kwenye viwanja
vya Maisara katika mkoa wa Mjini Magharib, wilaya ya Mjini.
”Hali hii humuwezesha mzalishaji kupata mrejesho kuhusu namna bidhaa yake
inavyokubalika kwenye soko, mapungufu yaliyopo kwenye bidha husika pamoja
na kuelewa maboresho anayotakiwa kuyafanya katika bidhaa au huduma.”
1
Waziri Mkuu alisema kuwa tamasha hilo linaweza kutumika kama nyenzo
muhimu katika kuanzisha mahusiano mazuri ya kibiashara kati ya mteja na
mfanyabiashara, hivyo kuwawezesha wajasiriamali kuwa na masoko ya uhakika.
Pia Waziri Mkuu alisema kufanyika kwa tamasha hilo ni sehemu ya utekelezaji
wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015 katika ibara ya 84 (f).
Balozi Amina aliseka kauli mbiu ya tamasha hilo kwa mwaka 2018 ni ‘wekeza
kwenye viwanda kwa uchumi na ajira’ inalengo la kuhamasisha wadau kuongeza
uelewa kwa wananchi juu ya falsafa na dhima ya ujenzi wa viwanda.
(MWISHO)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
ALHAMISI, JANUARI 11, 2018.