Timam Tea Inawafaa Watu Wote

You might also like

Download as doc, pdf, or txt
Download as doc, pdf, or txt
You are on page 1of 6

TIMAMU TEA INAWAFAA WATU WOTE!

-1

Juma Killaghai

Tangu kuingia sokoni kwa chai ya Timamu, baadhi ya watu wamekuwa wakiuliza iwapo
wanaweza kuitumia hata kama hawana tatizo lolote la kiafya. Ili kupunguza wingi wa
wanaouliza swali hili ni vema tukafikisha kwa wasomaji makala kadhaa fupi zinayolenga
kujibu swali hili. Kila makala itajikita katika kuzungumzia manufaa na faida za kiafya za
kila moja, kati ya makundi mbalimbali ya viini lishe yaliyomo kwenye hii chai ya Haiiba
Timamu. Makala ya leo itazungumzia kundi la vitamini. Hata hivyo, kama utangulizi,
kwa minajili ya kueleweka zaidi, ni vema wasomaji wetu wakatambua kuwa magonjwa
yamegawanyika katika makundi mawili makuu.

MARADHI YA KUAMBUKIZA

Kundi la kwanza ni lile la maradhi ya kuambukiza. Haya ni yale maradhi yanayozaliwa


mwilini kutokana na mwili kuvamiwa na vimelea hai vyenye uwezo wa kusababisha
maradhi pale ambapozitakuta kinga za mwili za mhusika zinafanya kazi chini ya
kiwango. Vimelea hivi ni bacteria, virusi, fangasi, protozoa, minyoo na aina ya
chembechembe za protini zinazoitwa prions. Mfano wa magonjwa yanayosababishwa na
vimelea hivi ni kama malaria, kipindupindu, kifua kikuu, nakadhalika. Aghalabu tiba ya
maradhi haya huwa ni kutumia dawa kwa njia ya kunywa, sindano au dripu, na wakati
mwingine kwa kupaka; ikiwa katika dozi maalum. Yaani, mgonjwa mwenye uzito fulani
anatakiwa atumie dawa fulani fulani, kwa mpangilio fulani kwa kutwa, na kwa idadi ya
siku fulani.

MARADHI YA KIMFUMO

Kundi la pili ni lile la maradhi ya kimfumo (metabolic diseases). Haya ni yale magonjwa
yanayozaliwa mwilini kutokana na mifumo ya mwili kushindwa kufanya kazi kwa
utaratibu uliokusudiwa. Kwa mfano kiasi cha sukari kwenye damu ya mtu wa kawaida
(siyo mgonjwa wa kisukari), kinatakiwa kiwe chini ya 7.7 mmol/l (140 mg/dl), kiasi cha
masaa mawili hivi baada ya kula.

Kiasi hiki kikiwa juu ya hapa maana yake ni kwamba mfumo wa mhusika wa kuhamisha
sukari kutoka kwenye damu na kuipeleka huko kwenye seli inakotakiwa iwepo haufanyi
kazi inavyotakiwa. Mfano mwingine. Mtu ambaye siyo mgonjwa anatakiwa kuwa na
kiwango cha juu cha shinikizo la la damu cha kati ya mmHg 110 – 120; na kiwango cha
chini cha mmHg 80.

Nje ya viwango hivi maana yake ni kwamba kuna shida katika eneo fulani la mfumo wa
mzunguko wake wa damu. Shida inaweza kuwa mishipa ya damu imekakamaa na
hainyumbuliki kupanuka pale inapohitajika, na kwa maana hiyo shinikizo la damu
linakuwa kubwa kwenye kuta za mishipa hiyo pale damu inaposukumwa kusambazwa
mwilini. Shida pia inaweza kuwa kasi ndogo ya utaratibu wa uvunjifu na uundaji wa
kemikali mwilini (slow metabolism), hali inayopelekea kasi ndogo ya usukumaji wa
damu wakati wa kuisambaza mwilini na hivyo kuweka shinikizo dogo katika kuwa za
mishipa ya damu.

Aghalabu maradhi ya kimfumo yanasababishwa na mambo manne makuu ambayo ni:

1. Upungufu wa viini lishe na virutubisho fulani fulani ndani ya mwili. Kwa mfano
maji; madini lishe, vitamini, tindikali mafuta zisizozalishwa mwilini (essential
fatty acids), vizuia vioksidishaji (anti-oxidants), na vijenzi vya protini
visivyozalishwa mwilini (essential amino acids);

2. Ulaji wa vyakula visivyokubaliwa na mwili, kwa mfano sukari ya viwandani na


baadhi ya vyakula vingine, haswa vile vilivyochakatuliwa (processed);

3. Sumu mbalimbali zinazolundikana mwilini kupitia taka zinazobaki mwilini baada


ya mchakato wa kutoa nishati na viini lishe kutoka katika chakula tunachokula, na
sumu mbalimbali zilizoingia mwilini kwa njia ya chakula, vinywaji, dawa,
vipodozi na hewa chafu. Mifano ya sumu hizi ni:

a. Jivu la tindikali linalobaki baada ya vyakula vya protini na wanga kuchakatuliwa


ndani ya mwili;

b. Kemikali mbalimbali zinazoingizwa mwilini kutokana na vinogesho (sweeteners)


mbalimbali bandia vinavyotumika kwenye vinywaji mbalimbali hasa vile
vinavyotangazwa kuwa havitiwi sukari;

c. Kemikali mbalimbali zinazozanazoingizwa mwilini kutokana na kemikali


mbalimbali zinazotumiwa kwenye vyakula na vinywaji kama vihifadhi (chemical
preservatives) na viongeza ladha (flavor enhancers);

d. Kemikali mbalimbali zinazoingizwa mwilini kutokana na kutumia maji


‘yaliyotakaswa’ na kemikali kama chlorine na Aluminum sulfate;

e. Mvuke wa zebaki (mercury) unaoingia mwilini kutokana na mchanganyiko wa


kuzibia matundu ya meno unaohusisha madini ya fedha na zebaki (mercury
amalgam);

f. Nakadhalika.

4. Msongo endelevu (chronic stress).

Msongo endelevu ni tishio kubwa sana kiafya. Sababu kubwa ni kwamba mwili huzalisha
tindikali nyingi sana pale mtu anapokabiliwa na msongo. Msongo endelevu hutumia
nishati nyingi sana ya mwili, na matumizi yoyote ya nishati huzaa tindikali kama zao la
ziada (by product). Aidha homoni mbalimbali zinazozalishwa na mwili ili kukusaidia
kukabiliana na msongo zina kawaida ya kuharibu vinasaba vya seli (DNA) iwapo
zitaachwa mwilini kwa muda mrefu bila kuondolewa. Uharibifu wa vinasaba huzaa
maradhi mengi sana ndani ya mwili, na haswa saratani.

Mfano wa maradhi ya kundi hili la maradhi ya kimfumo ni kama kisukari, ugonjwa wa


ini bonge (fatty liver disease), shinikizo la damu (hypertension), ugonjwa wa moyo,
ugonjwa wa jongo, saratani, magonjwa ya mifupa, magonjwa ya misuli, nakadhalika. Ili
kujihakikishia uhuru wa kuishi bila kukumbwa na maradhi haya ni muhimu kuishi
maisha ambayo kwa kiasi kikubwa yatakuwa yamejiweka mbali na visababishi hivi.

Baada ya utangulizi huu, sasa ni wakati muafaka wa kuingia katika mada yetu ya leo,
ambayo kama tulivyotangulia kuitambulisha hapo awali, inahusu kundi la viini lishe
vilivyomo katika Haiiba Timamu Tea, vinavyojulikana kama vitamini. Huu utakuwa ni
mwanzo wa majibu ya swali tuliloulizwa kuhusiana na ni nani anapaswa kutumia
Timamu Tea.

VITAMINI NI NINI?

Vitamini ni kemikali ya kiorganiki (moja ya viasili vyake ni carbon) ambayo mwili


unaihitaji kwa ajili ya kuendeleza uhai, lakini mwili hauna uwezo wa kuizalisha kwa
kiwango cha kutosha, au hauna uwezo wa kuizalisha kabisa. Upungufu wa vitamini
hupelekea kuathirika kwa ile michakato ya kibailojia inayosukumwa na vitamini hiyo na
hivyo kuzaa ugonjwa au magonjwa yanayohusiana na upungufu huo.

Kwa kawaida huwa tunatakiwa tupate vitamini zote tunazohitaji kupitia katika lishe. Hata
hivyo kutokana na mapungufu mbalimbali yaliyoko katika lishe zetu inatokea tukawa na
upungufu wa baadhi ya vitamini na hivyo kukumbwa na magonjwa yanayohusiana na
huo upungufu.

VITAMINI MUHIMU ZILIZOMO KATIKA HAIIBA TIMAMU TEA

Baadhi ya vitamini muhimu zilizomo kwa wingi katika chai hii ni B1, B2, B3 na C.

Vitamini B1

Faida za Vitamini B1 ni nyingi. Faida tano muhimu ni pamoja na:

i. Uzalishaji wa nishati mwilini. Vitamini hii ina jukumu la kusaidia kubadilisha


sukari kuwa nishati. Katika kutimiza jukumu hili inafanya kazi kama kimeng’eny
a kinachooksidisha sukari (kuiongezea gesi ya oksigeni) ili kuibadili kuwa nishati
kwa ajili ya kuendesha vyema shughuli mbali mbali za viungo nyeti vya mwili
kama ubongo, moyo, mapafu na figo;

ii. Utendaji kazi wa mfumo wa mzunguko wa damu (cardio vascular system). Vita
mini hii inajukumu la kuzalisha kemikali tarishi (neurotransmitter) inayoitwa
acetylcholine. Kazi ya kemikali tarishi hii ni kupeleka taarifa mbalimbali baina ya
misuli na mishipa ya fahamu. Upungufu wa kemikali hii hupelekea mapigo ya
moyo kutokuwa katika mpangilio unaoeleweka (irregular heart-beat). Upungufu
mkubwa unaweza kupelekea kwenye moyo kushindwa kufanya kazi;

iii. Vitamini B1 kwa pamoja na tindikali za muhimu za mafuta za omega 3 na omega


6 huzuia ugonjwa wa macho unaouhusiana na lenzi ya macho kutanda ukungu;

iv. Kusaidia ubongo kufanya kazi vizuri. Vitamini hii husaidia kuboresha utunzaji wa
kumbukumbu na umakini, huimarisha mishipa ya fahamu na kukinga dhidi ya
magonjwa mbalimbali yanayohusisha kudhoofika kwa ubongo; na

v. Kusaidia kuimarika na kuboreka kwa utando unaozunguka mishipa ya fahamu na


hivyo kukinga dhidi ya uchakavu wa mishipa hiyo.

Vitamini B2

Faida za Vitamini B2 ni nyingi. Faida tano muhimu ni pamoja na:

i. Huzuia maumivu makali ya kichwa yanayoambatana na dalili nyingine kama


kichefuchefu, kutapika, kushindwa kuhimili mwanga mkalai na kelele, na wakati
mwingine kuona vimulimuli na kuhisi kama kuna kuna kuchomwa chomwa na
sindano kwenye mikono na miguu;

ii. Kufanya kazi kama kizuia kioksidishaji kinachosaidia kukinga dhidi ya magonjwa
ya moyo na saratani;

iii. Kusaidia katika kutibu maradhi ya upungufu wa damu na seli mundu (sickle cell);

iv. Inapambana na vitu vinavyochochea saratani mwilini (carcinogens); na

v. Inasaidia katika uchakatuaji wa protini, mafuta na wanga na hivyo katika


uzalishaji wa nishati mwilini.

Vitamini B3

Faida za Vitamini B3 ni nyingi. Faida tano muhimu ni pamoja na:

i. Husaidia sana katika kuulinda mwili wako dhidi ya ugonjwa wa moyo;

ii. Husaidia kupunguza kiwango cha lehemu mbaya (bad cholesterol) mwilini;

iii. Husaidia kuongeza kiwango cha lehemu nzuri (good cholesterol) mwilini;

iv. Tafiti pia zinaonyesha kuwa vitamini hii husaidia sana kupambana na ugonjwa wa
kupoteza kumbukumbu; na ugonjwa wa lenzi za macho kufunikwa na ukungu
(cataracts; ugonjwa wa mifupa dhaifu; ugonjwa wa kisukari cha udogoni (Type I
diabetes); na
v. Aidha vitamini hii imehusishwa na kusaidia kuboresha uzalishaji wa nishati
katika ngazi ya seli; kuboresha na kuimarisha mishipa ya fahamu; na kuimarisha
na kuboresha mfumo wa usagaji wa chakula.

Vitamini C

Hii ni vitamini yenye faida nyingi sana muhimu kiafya. Baadhi ya faida hizi ni pamoja
na:

i. Husaidia kupunguza ukali wa ugonjwa wa mafua na muda wa kuugua ugonjwa


huo;

ii. Huzuia mizio (allergies) kwa kusaidia kudhibiti uwepo wa homoni ya Histamine
mwilini;

iii. Ni tiba ya asili ya magonjwa ya ngozi ikiwa ni pamoja na kuopunguza kasi ya


kuzeeka kwa ngozi na kutengeneza makunyanzi;

iv. Inasaidia sana katika kutibu majeraha;

v. Inazuia athari za msongo katika mwili;

vi. Inawezesha ujenzi wa protini muhimu ya collagen ambayo ni muhimili


unaoshikilia tishu moja na nyingine ndani ya mwili. Kiwango kidogo cha
uundwaji wa collagen kunaweza kusababisha ugonjwa hatari wa scurvy;

vii. Inasaidia kupunguza kiwango cha lehemu (cholesterol) katika mzunguko wa


damu;

viii. Inasaidia kudumisha unyumbufu wa mishipa ya damu (elasticity) na hivyo


kupunguza uwezekano wa kupata shinikizo la damu na maradhi ya moyo;

ix. Ni kizuia kiokisidishaji chenye nguvu. Husaidia sana kuzimua chembechembe


zenye umeme chanya mwilini (free radicals) na hivyo kuzuia chembe hizo
kufanya uharibifu katika mfumo wa mzunguko wa damu mwilini na kusababisha
magonjwa ya moyo na kiharusi;

x. Inasaidia katika uratibu wa sukari kwenye damu na kupunguza madhara


yanayosababishwa na kiwango kingi cha sukari kwenye damu;

xi. Inasaidia katika matibabu ya saratani. Tafiti zinaonyesha kwamba dozi kubwa za
vitamini C ni mujarabu sana katika maangamizi ya seli za saratani;

xii. Ongezeko la vitamini C mwilini husaidia sana kudhibiti mwendelezo wa ugonjwa


wa kupoteza kumbukumbu pamoja na magonjwa mengine yanayoathiri mishipa
ya fahamu;
xiii. Husaidia sana kuzuia kupungua kwa upana wa njia ya hewa na hivyo huzuia
kupumua kwa tabu.

xiv. Huboresha utendaji kazi wa mapafu na hivyo ni msaada mkubwa kwa wagonjwa
wa pumu;

xv. Husaidia sana kupunguza uwezekano wa kupata ugonjwa wa cataracts (ukungu


kwenye lenzi za macho) na hivyo huzuia macho kupoteza uwezo wa kuona;

xvi. Inaweza kusaidia katika matibabu ya kifua kikuu. Baadhi ya tafiti zimeonyesha
kuwa vitamini C ina uwezo wa kuua bacteria wanaosababisha maradhi ya kifua
kikuu.

Siku zote kinga ni bora kuliko tiba. Kutokana na mazingira tunayoishi kuwa ni yenye
kufanana sana, kila mmoja wetu ni mgonjwa mtarajiwa. Hata hivyo tukumbuke kuwa
kinga ni bora kuliko tiba, hivyo pale ambapo kuna uwezerkano wa kujikinga ni bora
tukafanya hivyo. Kutokana na faida nyingi zinazoletwa na vitamini zilizoko katika Haiiba
Timamu Tea kama tulivyozielezea hapo juu ni wazi kabisa kuwa kila mtumiaji wa Haiiba
Timamu Tea, bila kujali hali yake ya kiafya anaweza kunufaika sana.

KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA WATENGENEZAJI WA CHAI HII, YAAINI


HERBAL IMPACT, KWA SIMU NAMBA: 0754281131; 0655281131; 0686281131; NA
0779281131 AU WATEMBELEE OFISINI KWAO:

MOSQUE STREET, NO.1574/144, KITUMBINI, DAR ES SALAAM (MKABALA


NA LANGO KUU LA KUINGILIA MSIKITI WA SUNNI)

You might also like