Professional Documents
Culture Documents
Ilala Mag
Ilala Mag
TAHARIRI
Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini Tanzania zipo kwa mujibu wa Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 145. Kwa
kutambua umuhimu wa vyombo hivi Serikali ya Tanzania imekuwa ikichukua
hatua mbalimbali za kuziboresha. Hata hivyo maboresho yaliyochukuliwa na
Serikali ya Awamu ya Tano nchini yameendelea kuzipa nguvu zaidi Mamlaka
hizi kujiendesha.
Sote kwa pamoja tumeshuhudia ufanisi wa utekelezaji wa maagizo mbalimbali
yaliyotolewa. Toleo hili linaanisha baadhi ya maeneo kati ya mengi ambayo
yamefanyika Katika Manispaa ya Ilala kwa kipindi cha takribani miaka miwili
na nusu 2015 hadi Juni 2018 katika Sekta za huduma za Jamii ikiwemo
ongezeko la uandikishaji wa Wanafunzi katika shule za msingi sambamba na
kuboresha miundombinu ya Elimu, Huduma za Mama na Mtoto, Afya,
Uanzishaji wa Viwanda vidogovidogo, Ujenzi wa Barabara katikati ya Mji,
Matumizi ya Mifumo ya Kielektroniki katika kukusanya maduhuli ya Serikali
Uboreshaji wa miundombinu ya Jiji la Dar es Salaam unaojumuisha
upendezeshaji wa mandhari pamoja na Usafi wa Mazingira.
Agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Hassan Suluhu kuhusiana na mazoezi ya viungo kwa Watumishi limetekelezwa
kikamilifu katika Manispaa ya Ilala. Badala ya kufanyika Jumammosi ya Pili ya
kila mwezi Watumishi wameamua kufanya mazoezi hayo mara tatu kwa kila
wiki hii inatokana na manufaa yatokanayo na mazoezi hayo. Si wao tu utaratibu
huo umeweza kuvuta Watumishi wengine kutoka Taasisi za Serikali zilizopo
karibu na Ofisi za Mnispaa ya Ilala. Hongera Makamu wa Rais kwa kuliona hili
la afya za Watumishi.
Pongezi pia zinaelekezwa kwa Viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala
(Madiwani) ambao wamekuwa wakishirikiana na Watendaji kuhakikisha
maelekezo na maagizo ya Serikali yanatekelezwa.
Bodi ya Uhariri
Bibi Tabu F. Shaibu Wajumbe Mhariri Mshauri
Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Neema Njau Said Mwishehe
Habari, Mawasiliano, Habari na Hashim Jumbe Msanifu Kurasa
George Mwakyembe NPC - KIUTA
Uhusiano
Mchapishaji
(Mwenyekiti) NPC - KIUTA
1
Sauti ya Ilala
Tumeboresha huduma.
Na Simon Nyalobi
2
Sauti ya Ilala
MEYA wa Manispaa ya Ilala, Mhe Charles Kuyeko, anaeleza katika kipindi cha
takribani miaka miwili na nusu, Manispaa hiyo imefanikiwa kusimamia katika
maeneo tofauti ikiwemo ukusanyaji wa mapato.
Anaeleza Manispaa hiyo iliamua kutumia mashine hizo, baada ya kujua faida
zake katika udhibiti wa mapato katika taasisi za umma na binafsi.
3
Sauti ya Ilala
“Tunahakikisha hakuna fedha yoyote inayotumika bila ya kupitishwa na kamati
ya Fedha na Utawala na hatimaye katika Baraza la Madiwani,”anasema.
Anafafanua kuwa, baada ya kuanza kutumiwa kwa mashine hizo kwa kipindi
cha mwaka wa fedha 2015/16 mapato yalipanda kufikia milioni 80 hadi 85,
ambapo kabla ya matumizi ya mashine yalikuwa milioni 15 hadi 20.
Kwa mujibu wa Kuyeko, Manispaa ya Ilala, imepata hati safi kutoka kwa Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kwa kipindi cha mwaka 2016/17, baada
ya kufanikiwa kupata hati hiyo kwa kipindi cha mwaka 2015/16.
Huduma za Kijamii
Akizungumzia utoaji wa huduma za jamii, alisema kuwa katika Manispaa hiyo
umeboreka na kurahisishwa zaidi.
4
Sauti ya Ilala
“Vituo hivi vitakuwa na ofisi zote, kutakuwa na ofisi ya Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA), benki mbalimbali na ofisi zetu za Manispaa, hii itampungizia
gharama za muda na fedha mfanyabiashara kufika Manispaa.
Miundombinu
Kuhusu ujenzi wa miundombinu, anasema manispaa imefanikiwa kujenga
barabara za lami zenye urefu wa Kilomita 4.6 kutoka Segerea hadi Bonyokwa
na Mombasa hadi Moshi Bar.
Katika elimu, anasema wamefanikiwa kulitekeleza agizo la Rais Dk. Dk. John
Magufuli, la kutaka shule ziwe madawati ya kutosha na kuongeza ujenzi wa
vyumba vya madarasa.
“Sisi tulienda mbali zaidi ya agizo la Rais Magufuli, tuliona hatuwezi kutengeneza
madawati pekee yake bali kujenga na madarasa, tulijua kutakuwa na ongezeko
la wanafunzi kutokana na elimu kuwa bure,”anasema.
5
Sauti ya Ilala
Hivyo, wananchi wa manispaa hiyo, ni budi kuwaunga mkono viongozi wao
katika dhamira hiyo, ili kuipaisha manispaa hiyo kiuchumi.
Katika kipindi cha takribani miaka miwili na nusu cha Serikali ya Awamu ya
Tano, inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, mambo
mbalimbali ya kimaendeleo yameendelea kutekelezwa kama yalivyoainishwa
kwenye Mkakati wa Taifa wa kuinua Uchumi, huku Sekta ya Elimu ikiwa ni
moja ya Sekta zilizopewa kipaumbele katika ustawi wa Taifa la Tanzania.
Katika kutekeleza azma hiyo, Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Ufundi ilitoa
Waraka wa Elimu namba 5 wa Mwaka 2015 ambao unafuta ada kwa Elimu ya
Sekondari kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne kwa Shule za Umma na
michango yote katika Elimu msingi, hivyo basi, Waraka huu unafuta Waraka
namba 8 wa Mwaka 2011 kuhusu michango Shuleni.
6
Sauti ya Ilala
Kuanza kwa utekelezaji wa Elimu msingi bila malipo, Manispaa ya Ilala kupitia
Idara ya Elimu Msingi imefanya jitihada mbalimbali za kuboresha Sekta hiyo
ili kutoa wigo mpana wa upatikanaji wa Elimu iliyo bora kwa kuboresha
Mazingira ya kujifunzia kwa Wanafunzi kwa maana ya kuongeza nyenzo muhimu
katika Miundombinu na Samani, mfano: vyumba vya Madarasa, matundu ya
vyoo, Ofisi na Madawati.
7
Sauti ya Ilala
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Mbunge
wa Jimbo la Ilala Mh. M.A. Zungu Madawati yaliyotolewa na Ofisi ya Bunge kwa niaba ya
Wabunge waliopata mgao huo katika awamu ya kwanza.
8
Sauti ya Ilala
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo
na baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge wakati wa hafla ya utoaji Madawati
kwa Waheshimiwa Wabunge kwa ajili ya Shule zilizopo kwenye Majimbo yao.
Aidha, hadi kufikia mwaka 2018 Shule mpya mbili zilijengwa kutokana na
fedha za Ruzuku zilizotolewa na Mhe. Rais Magufuli, Shule hizo ni Shule ya
Msingi Maghorofani na Lubakaya, nazo zimesaidia sana kupunguza
msongamano wa Wanafunzi darasani na kupunguza Wanafunzi kutembea
muda mrefu kufuata Shule.
9
Sauti ya Ilala
Shule ya Msingi Maghorofani ni moja kati ya Shule mpya zilizojengwa kutokana na fedha
za Ruzuku zilizotolewa na Mhe. Rais John Magufuli.
10
Sauti ya Ilala
Nini maaana ya Elimu msingi bila malipo?
Utoaji wa Elimu msingi bila malipo una maana ya kwamba Mwanafunzi atasoma
bila Mzazi/ Mlezi kulipa ada wala michango ya fedha iliyokuwa ikitozwa Shuleni
kabla ya kotolewa kwa Waraka wa Elimu namba 5 wa mwaka 2015. Serikali
itagharamia ada ya Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya kutwa na bweni
iliyokuwa inatolewa na Mzazi au Mlezi kwa Shule za Serikali.
Katika kutekeleza Sera ya Elimu bila malipo, Serikali kupitia Waraka wa Elimu
namba 5 wa mwaka 2015 umeelezea nini wajibu wake na majukumu ya Mzazi/
Mlezi katika utekelezaji wake sambamba na majukumu ya Wakuu wa Shule
na Kamati/Bodi za Shule na Jamii kwa ujumla.
Katika kuhakikisha kuwa kila Mtoto anapata elimu bila kujali mapungufu yake,
Serikali imenunua vifaa vya kujifunzia kwa Wanafunzi wenye uhitaji maalum
sambamba na vifaa vya kufundishia kwa Walimu wanaofundisha Watoto wenye
mahitaji maalum ikiwa ni kielelezo cha kutimiza ahadi za Mhe. Rais Dkt. John
Pombe Magufuli.
11
Sauti ya Ilala
ajili ya Wanafunzi wenye mahitaji maalum ambapo itanufaisha Shule za Msingi
213 kati ya Shule 408 na Shule 22 za Sekondari kati ya Shule 43 zenye
Wanafunzi wenye mahitaji maalum”.
12
Sauti ya Ilala
NA MWANDISHI WETU
ILALA
Anasema katika kutoa huduma hizo wanazingatia umri, jinsia, jinsi ambapo
kazi hiyo inafanywa bila kuzingatia umri, dini, kabila, utaifa wala itikadi yoyote.
13
Sauti ya Ilala
Anasema katika mpango huo pia walifanikiwa kutoa elimu ya kisaikolojia kwa
watoto 500 walioathirika na ukatili wa kijinsia, mfano ngoni, kimwili na
kutelekezwa.
Fransisca anasema pia wanaendelea kutoa elimu na mafunzo kwa kundi hilo
ili waweze kutambua fursa mbalimbali zinazotolewa hapa nchini na Serikali ya
awamu ya tano pamoja na asasi nyinginezo binafsi na za kiserikali.
Bajeti
14
Sauti ya Ilala
”Tumelenga kama Idara kulikomboa kundi hili kwa kuhakikisha wanaacha
uchuuzi na badala yake wanakuwa wazalishaji wa bidhaa kubwa wenye viwanda
vidogo vidogo,”anasema Fransisca,
Vijana
Fransisca anasema zaidi ya vijana 1,500 wa manispaa hiyo wamenufaika na
mafunzo ya ujasiriamali na kupata vifaa vya cherehani, fundi uashi na umeme
ambapo mafunzo hayo yametolewa kwa ushirikiano na Shirika la Plan
International.
Pia anasema idara yake imefanikiwa kuzifunga kambi 15 zilizokuwa za dawa
za kulevya na kuunda vikundi vidogo vidogo ambavyo vinajihusisha na shughuli
za manispaa.
Mafanikio
Anasema wamefanikiwa kutoa mikopo kwa vijana zaidi ya 400 kupitia asilimia
10 ya mapato ya ndani ya manispaa hiyo kwa ushirikiano wa benki ya DCB.
Pia wamefanikiwa kuwashirikisha Vijana na Wanawake katika maonyesho
mbalimbali ya Kitaifa.
15
Sauti ya Ilala
Mkurugenzi Ilala: Nidhamu ya Kazi imeongezeka
Na mwandishi wetu Ilala
16
Sauti ya Ilala
Anazungumziaje utoaji wa huduma kwa Wateja/Wananchi?
Mkurugenzi Palela anaeleza kuwa katika kipindi hiki cha takribani miaka miwili
ya Serikali ya awamu ya tano kumekuwa na mabadiliko ya kiutendaji ya namna
watumishi wanavyowahudumia wateja/Wananchi katika sekta zao. Malalamiko
ya wananchi wengi yamepungua wamekuwa wakiridhika na jinsi
wanavyopokelewa na kuhudumiwa. Kila mtumishi amekuwa akijituma katika
eneo lake na kupunguza misururu mirefu ya watu wanaosubiri kuhudumiwa.
Aidha kiwango cha mahudhurio kimeongezeka. Katika kuhakikisha hakuna
udanganyifu wa mahudhurio kwa Watumishi, Halmashauri ya Manispaa ya
Ilala kwa makusudi kabisa iliamua kufunga mashine za Kielektroniki (Bio-
Metric attendance Register) ambapo mtumishi atasaini wakati anaingia ofisini
na wakati wa kutoka. Hivyo imekuwa viguni mtumishi kudanganya muda ambao
alifika na kuondoka kazini. Aidha uvaaji wa vitambulisho vya Watumishi
unazingatiwa.
17
Sauti ya Ilala
Stahiki za Watumishi
Katika kipindi cha takribani miaka miwili ya uongozi wa Serikali ya awamu ya
Tano ya Mheshimiwa John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imeweza kuboresha stahiki
mbalimbali za Watumishi wake kama vile kulipa nauli za likizo kwa watumishi
wake kwa wakati, kulipa gharama za kuwasafirisha watumishi wake waliostaafu
katika utumishi wa umma kwa wakati. Kiasi cha Sh 917,329,200 zimelipwa
kwa watumishi 474 katika kipindi cha miaka miwili.
18
Sauti ya Ilala
19
Sauti ya Ilala
Wakazi wa Buguruni Kisiwani wakiwa wanasubiri kupatiwa fedha kutoka kwa maofisa
wa Kwa Manispaa ya Ilala ambapo fedha hutolewa kwa kaya masikini kila baada ya miezi
miwili ili wajikimu na kujikwamua kimaisha.
Mradi huo wa TASAF umeweza kuwainua wanufaika kutoka hatua moja hadi
nyingine hasa kimaendeleo.
Kaya ya Bi. Asha Salumu ina jumla ya watu nane (8) kati ya hao wajukuu ni
watatu (3) ambao wanasoma, mjukuu mmoja anasoma darasa la pili (2), wa
pili anasoma darasa la nne (4) na watatu anasoma darasa la kwanza (1).
20
Sauti ya Ilala
Asha anapokea Sh.36000 kila baada yamiezi miwili ikiwa ni ruzuku ya msingi,
Sh.10,000) ni ruzuku ya kuwa na wajukuu na Sh.12000 niruzuku ya watoto
wanaosoma Shule ya msingi.
Aliishi kwenye nyumba mbovu ambayo ukuta wake napaa hazikufaa hali
iliyosababisha Serikali kumuamuru ahame kwani alikuwa kwenye eneo hatarishi
kwa maisha yake.
21
Sauti ya Ilala
“Maisha ya wajukuu wake kwenda Shule ni mtihani kwa upande wa mahitaji
kama vile viatu, daftari na sare za shule. Nyumba yangu kipindi hicho ilikuwa
mbovu, ukuta mbovu, paa mbovu hata iliamuriwa nihame.
“Mlo wangu ulikua washida, mavazi ya shida” kiasi kwamba nilikuwa najisikia
vibaya hapa mtaani, nilijiona ni mwenye bahati mbaya kwani hakuna
ambacho kwake kilikwenda vema kwenye maisha yake ya kila siku,”
anasimulia Mama huyo.
Bi. Asha akiwa amesimama pembeni mwa nyumba yake ambayo ameikarabati kwa fedha
za ruzuku kutoka TASAF.
22
Sauti ya Ilala
Muhimu kwa Mama huyo ni kwamba alikuwa na mipango thabiti ya kujikomboa
kutokana na ruzuku anayopokea na haonishida kusema ya moyoni mwake.
Kwa maisha aliyoishi hapo awali mambo yalikuwa hayaendi maana alikuwa
anakula mlo mmoja kwasiku. Hiyo ilinipelekea kukata tama siku zote. Sasa
TASAF imemsaidia kuboresha maisha yake baada ya kufika kwenye mtaa
wake.
23
Sauti ya Ilala
Aidha, Shule zilizoshiriki kwenye Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi kwa
mwaka 2017 kwa Wilaya ya Ilala Mjini, Jumla yake ni 112 zilizokuwa na idadi
ya Watahiniwa 12,841 waliosajiliwa kufanya Mtihani huo, kati yao Wavulana
wakiwa 6,181 na Wasichana ni 6,660, huku waliofanya Mtihani huo Jumla
yake ni 12,778 kati yao Wavulana wakiwa ni 6,145 na Wasichana ni 6,633
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Eng Stella Manyanya akiongea
na Wanafunzi wa shule ya Msingi Olympio katika kuwahamasisha kufanya kusoma kwa
bidii
24
Sauti ya Ilala
Kwa upande wa Wilaya ya Ilala Vijijini, Shule zilizoshiriki kwenye Mtihani wa
kumaliza Elimu ya Msingi kwa mwaka 2017 Jumla yake ni 72, zilizokuwa na
idadi ya Watahiniwa 8,863 waliosajiliwa kufanya Mtihani, kati yao Wavulana
wakiwa 4,097 na Wasichana ni 4,766, huku waliofanya Mtihani huo wakiwa ni
8,791 kati yao Wavulana ni 4,059 na Wasichana ni 4,732.
25
Sauti ya Ilala
Nafasi Shule Nafasi Shule
1 Tusiime 6 Kipawa Liberman
2 St. Joseph Millenium 7 Mtendeni
3 Genius King 8 Zanaki
4 Heritage 9 St. Therese
5 Havard 10 St. Mary’s
Aidha, zipo Shule ambazo zilikuwa na Watahiniwa chini ya Arobaini (-40) kwa
Wilaya ya Ilala Mjini, Shule hizo Jumla yake ni Ishirini na mbili (22), hivyo
Shule Kumi (10) bora zilizofanya vizuri ni hizi zifuatazo;
Nafasi Shule Nafasi Shule
1 Fontain Gate 6 Bariadi
2 Lusasaro 7 ACCT
3 ABC-Capital 8 Montesori Msimbazi
4 Agnes Michael 9 Patmo
5 Sabisa 10 Andrews
Kwa upande wa Wilaya ya Ilala Vijijini Shule zilizokuwa na Watahiniwa zaidi
ya Arobaini (40+) zilikuwa Hamsini na Moja (51) Katika kundi hilo, Shule
Kumi (10) bora zilizofanya vizuri kwenye kundi hilo ni hizi zifuatazo;
Nafasi Shule Nafasi Shule
1 Macedonia 6 Zabikha
2 Bati valley 7 Michael Mausa
3 Green hill 8 Daddy
4 Masaka 9 Nyamata
5 Benedict 10 Blessed Hill
Shule zilizokuwa na Watahiniwa chini ya Arobaini (-40) kwa Ilala Vijijini zilikuwa
Ishirini na Moja (21) Kwenye shule hizo, Shule Kumi (10) bora zilizofanya
vizuri kwenye kundi hilo ni hizi zifuatazo;
Nafasi Shule Nafasi Shule
1 Nyiw a 6 G i se la
2 Full Gospel 7 Erimelinda
3 Upendo Montessori 8 Heroes
4 Rosalia 9 Kwila
5 Holy Family 10 Trinity
Ukiondoa Matokeo ya Jumla kwa Shule za Manispaa ya Ilala, ndani yake zipo
Shule za Serikali zilizofanya vizuri ambazo zipo katika kundi lililohusisha
Watahiniwa zaidi ya (+40) kwa Shule Kumi (10) za Wilaya ya Ilala Mjini
zilizofanya vizuri ni hizi zifuatazo;
26
Sauti ya Ilala
Nafasi Shule Nafasi Shule
1 Mtendeni 6 Msimbazi
2 Zanaki 7 Mkoani
3 Kiwalani 8 Maktaba
4 Msimbazi Mseto 9 Hekima
5 Lumumba 10 Ukonga Jica
Shule nyengine za Serikali zilizofanya vizuri ambazo zipo katika kundi
lililohusisha Watahiniwa chini ya (-40) kwa Shule za Ilala Vijijini ni hizi zifuatazo;
Nafasi Shule Nafasi Shule
1 Kiyombo 6 Kinyerezi Jica
2 Kig e z i 7 K in yerezi
3 Kibog a 8 K iv u le
4 Mafanikio 9 Kilimani
5 G ogo 10 B u yu ni
27
Sauti ya Ilala
28
Sauti ya Ilala
Rais wa shirika la KOICA Mi-Kyung Lee (katikati) ,akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam Mhe Paul Makonda, na Viongozi wengine wakiwa katika hafla ya kukata utepe
kuashiria kuzinduliwa kwa Hospitali ya mama na mtoto Chanika iliyopo katika Halmashauri
ya Manispaa ya Ilala.
29
Sauti ya Ilala
Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Selemani Said Jaffo akiwa katika Ziara ya ukaguzi wa athari
zilizosababishwa na mvua zilizonyesha Jijini Dar es Salaam katika picha ni moja ya eneo
lililoathiriwa eneo la Pugu Mnadani katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala
30
Sauti ya Ilala
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Mhe. Charles Kuyeko akizindua rasmi jengo la Ofisi
ya Mtaa wa Mtakuja katika Kata ya Vingunguti.
31
Sauti ya Ilala
Jengo la kutolea huduma ya Mama na Mtoto katika Zahanati ya Msongola baada ya ukarabati
Barabara ya Segerea Bonyokwa iliyojengwa kwa fedha za ndani (Own Source) kwa
kiwango cha Lami yenye urefu wa Km 2.0
32
Sauti ya Ilala
Madarasa matatu yaliyojengwa katika Shule ya Msingi Karakata kwa ufadhili wa “ Education
Program for Result” (P4R) progamu iliyopo katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
33
Sauti ya Ilala
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Sophia Mjema akuzindua huduma ya matibabu bure kwa
Wazee wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani, sambamba na mmoja kati ya
wazee waliopatiwa kadi ya huduma ya afya bure akionesha kadi yake
34
Sauti ya Ilala
Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko inavyoonekana kwa sasa baada ya kufanyiwa ukarabati
kwa fedha kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufaundi.
Mradi wa tanki la maji lenye uwezo wa kuhifadhi maji yenye ujazo wa lita 150,000 ambalo
litaunganishwa na Miundombinu ya DAWASCO kwa ajili ya kutoa huduma ya maji kwa
Wananchi wa Kata ya Kisukuru.
35
Sauti ya Ilala
Diwani wa Kata ya Ilala, Mhe. Saady Khimji akizindua Mradi wa Maji katika Mtaa wa
Sharifu Shamba, mradi uliojengwa kwa fedha za miradi ya maendeleo LGCDG.
36
Sauti ya Ilala
Wenyeviti Kamati za Mitaa wakiwa katika kiapo cha Utii na Uadilifu mara baada ya kuchaguliwa.
37
Sauti ya Ilala
Vijana wakiwa katika jitihada za kujikwamua kiuchumi , wakifanya biashara katika maeneo
yaliyorasimishwa katika mitaa ya Kariakoo.
38
Sauti ya Ilala
WATUMISHI WA MANISPAA YA ILALA WAHAMASIKA NA UTALII WA
NDANI, WATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA MIKUMI NA SAADANI
Na: Mwandishi wetu Ilala
Tanzania ni moja kati ya Nchi chache Duniani zilizobarikiwa kwa kuwa na wingi wa
vivutio vinavyowavuta Wageni kuona, kuburudika na kujifunza mambo mbalimbali
yanayoifaharisha Nchi yetu, kama vile uoto wa asili, Milima, Mito, Mabonde pamoja
na hifadhi za Mbuga za Wanyama zinazochagiza ukuaji wa Sekta ya Utalii Nchini.
Lakini pamoja na uwepo wa vivutio vyote hivyo, bado kumekuwa na muitikio hafifu
wa Watanzania wanaotembelea maeneo hayo, ingawaje Serikali imekuwa ikitenga
bajeti kubwa kutangaza maeneo yenye vivutio na kuyaboresha kwa kuweka
Miundombinu bora na ya kisasa ili kuweza kufikika kwa kipindi chote cha mwaka.
Kwa kutambua umuhimu wa maeneo yenye vivutio Nchini mwetu na kuunga mkono
jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano ya kukuza Sekta ya Utalii, ndipo Watumishi
wa Manispaa ya Ilala waliposukumwa na nia ya kutembelea maeneo hayo yenye
vivutio kwa lengo la kujifunza na kujionea ufahari wa Nchi yao ya Tanzania.
39
Sauti ya Ilala
Kihistoria Mbuga ya Mikumi ilianzishwa mwaka 1964 iliitwa jina hilo kutokea
katika jina la asili la eneo ilipo Mbuga hiyo, ambalo ni ‘Mikumi’ huku Mbuga
hiyo ikiwa na vivutio mbalimbali vya Wanyamapori kama vile; Tembo, Twiga,
Simba, Swala, Nyati na Wanyama wengineo mbalimbali, huku Mbuga hiyo
ikikadiriwa kuwa na ukubwa wa Kilomita za Mraba 3,230.
40
Sauti ya Ilala
Hifadhi hiyo ya Saaadani imepandishwa hadhi na kuwa hifadhi kamili mwaka
2005 kutoka kuwa pori la akiba, ni ya upekee kwa sababu inapakana na
bahari ya Hindi na unapotembelea unaweza kufanya utalii wa nchi kavu, majini
na kwenye maeneo ya historia ya mambo ya kale.
Pia katika hifadhi ya Saadani unaweza kufanya utalii wa kutumia boti kwenye
Mto Wami kwenda umbali mrefu na kuna Ndege wengi na Wanyama aina ya
Viboko na Mamba ndani na nje ya maji na kwenda hadi sehemu ya Bahari na
Mto vinapokutana huku kukiwa na miti aina ya mikoko kwa uwanda wa pwani.
Afisa Utumishi Bwana Robert Muna wa kwanza kushoto akifurahia mchezo wa kuvuta
kamba sambamba na Watumishi wengine wa Manispaa ya Ilala kwenye fukwe za bahari
Hindi walipofanya ziara kwenye hifadhi ya Saadani.
41
Sauti ya Ilala
Hii ndio hifadhi ya Taifa ya Saadani, ukifika utajionea vitu vingi vinavyotia
raha kwa kiasi kikubwa mno, pia utajifunza na mila za Watu wa Pwani kwani
sehemu ya hifadhi hii kuna makazi ya Watu wanaoishi kwenye kijiji chenye
asili ya jina la Saadani.
42
Sauti ya Ilala
43
Sauti ya Ilala
44
Sauti ya Ilala
Muonekano wa shule ya Sekondari Pugu baada ya kubadilishwa kwa vigae vya asbestos
na kuezekwa upya kwa kutumia mabati.
46
Sauti ya Ilala
Ukarabati uliofanyika katika shule ya Sekondari Jangwani umegharimu jumla
ya Tsh Millioni 900 zimetumika kukarabati miundombinu ya shule hii, kwa
upande wa madarasa ukarabati uliofanyika ni pamoja na ofisi ya mkuu wa
shule, ofisi kuu ya walimu, ofisi ndogo ya walimu, ofisi ya taaluma, ofisi ya
mhasibu, madarasa 24,vyoo 15 vya walimu, maabara, vyoo vya wanafunzi 13
, ujenzi wa vyoo vipya 17 na mabafu 4 pamoja na ujenzi wa vyoo vitatau vya
matundu ambavyo vitatumika kwa matumizi ya dharura wakati maji
yanapokuwa yamekatika.
47
Sauti ya Ilala
48
Sauti ya Ilala
Ukarabati wa shule ya Sekondari Azania.
Shule ya Sekondari Azania ilianzishwa mwaka 1934 wakati huo ikiwa katika
mtaa wa Mtendeni ikijulikana kwa jina la Shule ya Msingi “Mtendeni Indian
Primary School”. Mwaka 1939 shule hii ilitaifishwa na kuwa shule ya Sekondari
ya Serikali ya mchanganyiko wa wavulana na wasichana. Mwaka 1965
wanafunzi wa kike walihamishiwa katika shule ya Serikali “Indian Secondary
School “ ambayo kwa sasa inajulikana kwa jina la Shule ya Sekondari Jangwani
na wavulana walihamishiwa kwenye majengo mapya yaliyokuwa katika
barabara ya Umoja wa Mataifa ambayo kwa sasa yanajulikana kwa jina na
Shule ya Sekondari Azania ambapo mwanafunzi wa kwanza mwenye asili ya
Kiafrika aliweza kusajiliwa.
Jina la Shule ya Sekondari Azania lilianza kutumika rasmi mwaka 1967 ikiwa
imesajiliwa kwa usajili namba 08.
Shule hii ina jumla ya wanafunzi 1787 ambapo kidato cha kwanza hadi cha
nne ina jumla ya wanafunzi 1403 pamoja na 384 ni wanafunzi wa kidato cha
tano na cha sita.
u
49
50
51
HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA
ii. Majengo makubwa kuwe na ramani (Outline scheme designs) Hati ya kumiliki kiwanja au barua ya toleo au leseni ya Makazi
iii Kuwasilisha michoro ya jengo na kumbukumbu husika za Kumbukumbu nyingine zinazohusu kiwanja hicho kama hati za
kiwanja mauzo,makabidhiano n.k.
iv. Kupata kibali kwa maandishi kinachitwa “Kibali cha Ujenzi”. Nakala za risiti ya kodi ya kiwanja na kodi ya majengo
Hivyo muendelezaji anatakiwa aandae mchoro wa awali (Outline plan) kwa Zifuatazo ni hatua zinazofuatwa wakati wa kuchunguza michoro hiyo:
utaratibu unaotakiwa ukionyesha aina ya ujenzi atakaokusudia kufanya ili
Kuwasilisha michoro na kulipa gharama za uchunguzi
aweze kupata ridhaa ya kuendelea na hatua za kuandaa michoro ya mwisho. (scrutiny fee).
Kuokoa muda na gharama, iwapo michoro ya mwisho itaonekana Kukaguliwa usanifu wa michoro
kuwa na dosari za kitaalam ambazo zitahitaji kufanyiwa
marekebisho. Kukaguliwa kiwanja kinachokusudiwa kuendelezwa
Kuwa na uhakika kuhusu mahitaji muhimu ya kuzingatiwa wakati Uchunguzi wa upimaji kiwanja
michoro inaandaliwa.
Uchunguzi wa matumizi ya jengo na uwiano
3. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA KIBALI CHA
UJENZI Uchunguzi wa Maafisa Afya
kufunguliwa na kusomeka. Michoro hiyo iwasilishwe kama ifuatavyo: Uchunguzi wa athari za mazingira (EIA)
Seti tatu za michoro ya jengo (Architectural drawings) Uchunguzi wa uimara wa jengo (Structural Drawings)
Seti mbili za michoro ya vyuma) structural drawings) kwa Kuandaliwa kwa maombi yaliokamilisha taratibu hizi na
majengo ya ghorofa.
kupele kwa kwenye Kamati ya Ujenzi ambayo wajumbe
4. MICHORO ILIYOANDALIWA IONYESHE NINI wake ni Madiwani
Hatimaye kuandika na kutoa kibali
Michoro itakayoandaliwa inatakiwa ionyeshe mambo yafuatayo:
7. FAIDA ZA KUJENGA NYUMBA IKIWA NA KIBALI CHA UJENZI
Jengo litakavyokuwa (Plan) Sections, elevations, Foundation and
roof Plan). Kuishi kwenye nyumbayo imethibitishwa kitaalamu kuwa ni salama
Namba ya eneo la kiwanja kilipo,Jina la Kampuni na anwani ya Kuwa na mazingira bora kwa kuwa na mji ulipangwa
Kampuni iliosanifu jengo husika. Kuepuka hasara na usumbufu unaoweza kutokea iwapo ujenzi
Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba umefanyika bila kibali kiwa ni pamoja na kushitakiwa mahakakani
kuvunjiwa na kulipa gharama za uvunjaji.
Ujazo wa kiwanja (Plot coverage)
Uwiano(Plot ratio)
Sauti ya Ilala
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda aliyepo upande wa kulia akiweka
tofali pamoja na Makamu wa Rais wa Shirika la KOICA kutoka Nchini Korea Kusini, Taemyon
Kwon, uwekaji wa tofali hilo uliashiria kuanza rasmi kwa ujenzi wa Hospitali ya Mama na
Mtoto Chanika
Aidha, ujenzi wa Hospitali hii ya Chanika umejumuisha wodi mbili zenye vitanda
120, (60 kwa kila moja) ambazo ni kwa ajili ya akina Mama ambao
hawajajifungua na waliojifungua, ICU mbili zenye vitanda 10 kila moja,Wodi
ya kujifungulia, Wodi ya Watoto njiti yenye vitanda 10, Vyumba vitatu vya
upasuaji, viwili vya upasuaji mkubwa na kimoja upasuaji mdogo, Maabara,
Idara ya uchunguzi wa mionzi, Idara ya ufuaji na utakasaji vyote hivi vina
vifaa vya kisasa.
52
Sauti ya Ilala
Moja kati ya nyumba za kuishi Watumishi waliopo Hospitali ya Mama na Mtoto Chanika,
nyumba hizi zimesaidia kuwapata Watumishi muhimu muda wote wanapohitajika hivyo
kurahisha huduma hasa za dharura
UTOAJI HUDUMA:
Ujenzi wa majengo haya umewezesha kuanza kutoa huduma za ndani (IPD
Services) ambazo zilianza tarehe 9 Oktoba 2017 kwa huduma za sehemu ya
wodi ya akina Mama wanaosubiria kujifungua (antenatal ward), wodi ya
Kujifungulia (Labour ward) na Wodi baada ya kujifungua (postnatal ward).
53
Sauti ya Ilala
Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam Bibi Theresia Mmbando akikagua vifaa
vilivyopo kwenye Hospitali ya Mama na Mtoto Chanika
Mganga Mfawidhi Hospitali ya Mama na Mtoto Chanika Dr. Richard M. Andrea (wa kwanza kulia)
akitoa maelezo kwa viongozi waliofika katika Hafla ya kukata utepe kuashiria uzinduzi wa Hospitali
katika moja ya wodi ya wamama ambao tayari wamekwisha jifungua.
54
Sauti ya Ilala
HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA YAUNGA MKONO NA
KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA KWA KUTUMIA VIUADUDU
Na Neema Njau.
55
Sauti ya Ilala
Elimu kwa Jamii
56
Sauti ya Ilala
Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema akigawa vyandarua katika kata
ya Gerezani
Maleria inaweza kuzuilika na kutibika kwa vitendea kazi rahisi kama vyandarua,
matumizi sahihi ya dawa sahihi ya malaria, upuliziaji wa dawa za mbu pamoja
kuuwa viluilui wa mbu kwa kutumia viua dudu.
57
Sauti ya Ilala
MANISPAA YA ILALA YAIMARISHA USAFI WA MAZINGIRA
Na Neema Njau
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imeongeza uwezo wake wa uondoshaji wa
taka ngumu kutoka 36%-50% ya mwaka 2015/2016 na kufikia 50%-55% ya
tani 110 zinazozalishwa kwa siku. Hali ya usafi kwa ujumla inaridhisha. Kupitia
gari maalum la matangazo ambalo limekuwa likitoa maelekezo mbalimbali
kuhusiana na usafi wa mazingira pamoja na vipindi katika vyombo vya habari
jamii imehamasika kwa kufanya kampeni shirikishi za usafi kwa kila Jumamosi
na Jumamosi ya kila mwisho wa mwezi kwa kata zote 36.
Katika utekelezaji wa dhana ya ushirikishaji wa sekta binafsi katika utoaji wa
huduma Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imeingia mkataba na makampuni
binafsi 7 yanayotoa huduma katika kata za katikati ya mji na vikundi vya
kijamii 26 vinavyotoa huduma ya kukusanya na kusafirisha taka kuzipeleka
dampo katika kata za pembezoni. Uthibitisho wa moja kwa moja unaweza
kupatikana katika eneo la kariakoo ambapo awali kulikuwa na changamoto ya
malundo ya takataka. Lakini kutokana na kuwepo kwa kampuni yenye uwezo
hali hiyo imeweza kudhibitiwa.
58
Sauti ya Ilala
59
Sauti ya Ilala
60
Sauti ya Ilala
Halmashauri inaendelea kukagua na kuhakikisha kuwa miradi yote
inayotekelezwa ndani ya Halmashauri, inayohofiwa kuleta athari kwa mazingira
inatekeleza matakwa hayo ya kisheria kabla ya kutekelezwa. Kwa kipindi cha
Julai 2016-Juni 2018, jumla ya miradi 108 imekaguliwa kwa kushirikiana na
Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Bwana Msongela Palela wa pili kuanzia kushoto akishiriki
katika mazoezi sambamba na Watumishi wengine wa Manispaa ya Ilala.
61
Sauti ya Ilala
Katibu Tawala Wilaya ya Ilala, Bwana Edward Mpogolo aliyepo upande wa kulia, akifanya
mazoezi ya kukimbia pamoja na Mwanasheria wa Manispaa ya Ilala, Wakili Bonaventure
Mwambaja.
Watumishi wa Manispaa ya Ilala wakiwa kwenye mazoezi ya pamoja viwanja vya Mnazi
Mmoja kama ilivyo kawaida ya siku ya Jumatatu, Jumatano na Ijumaa ambapo mazoezi
huanza baada ya masaa ya kazi.
62
Sauti ya Ilala
Jumamosi ya pili ya kila mwezi, Watumishi wa Manispaa ya Ilala hutekeleza agizo la Makamu
wa Rais kwa kufanya mazoezi asubuhi kwenye viwanja vya Jakaya Kikwete-Kidongo
Chekundu
63