Professional Documents
Culture Documents
Rasimu Ya Tamko Tahadhari Ya Ebola Agosti 2018
Rasimu Ya Tamko Tahadhari Ya Ebola Agosti 2018
Rasimu Ya Tamko Tahadhari Ya Ebola Agosti 2018
Utangulizi
Ndugu wanahabari,
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
inaendelea kutoa taarifa kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika
nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Nchi hiyo ya
DRC imetangaza tena kuwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola mnamo
tarehe 1 mwezi Agosti, 2018, ambapo jumla ya wagonjwa 26 na vifo 10
vilitolewa taarifa na wagonjwa 4 kati yao walithibitishwa kimaabara kuwa
na ugonjwa wa Ebola. Wagonjwa hawa wametokea katika vijiji/Maeneo
ya Mangina ikiwa ni kama km 30 tu magharibi mwa mji wa Beni kwenye
jimbo la Kivu Kaskazini linalopakana na nchi ya Uganda ikiwa ni kama
km 100 tu, na pia likiwa karibu sana na nchi ya Rwanda.
1
Huu ni mlipuko wa 10 wa ugonjwa wa Ebola kutokea nchini DRC, na
umetokea wiki moja baada ya nchi hiyo kutangaza kuisha kwa mlipuko
mwingine uliotokea mwezi Mei mwaka huu ambao ulikuwa katika jimbo
la Equator, Magharibi mwa DRC, umbali wa zaidi ya km 2,000 kutoka
eneo la huu mlipuko mpya uliotokea.
Ndugu wanahabari,
2
Ugonjwa wa Ebola
Dalili za Ugonjwa
3
Namna ya Kujikinga na ugonjwa wa Ebola:
4
Hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa na Wizara
kufuatia kupatikana kwa taarifa ya Ugonjwa huu huko DRC
Kufuatia kuwepo kwa taarifa hizi tangu mwezi Mei 2018, hatua zifuatazo
zinaendelea/zimechukuliwa na Wizara ili kujiandaa kukabiliana na
mlipuko huo:
1. Kufanya tathmini ya utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola
nchini (Operational readiness assessment) kwa nchi nzima kwa
kushirikiana na WHO na kuainisha mapungufu ambayo
yanapaswa kufanyiwa kazi. Mapungufu hayo yanaendelea
kuyafanyiwa kazi ili kujenga uwezo na utayari katika nchi yetu.
5
5. Wizara imepokea vifaa vya kukabiliana na Ebola kutoka WHO
vikiwemo; Thermo scanners, Vifaa Kinga, au PPE, kama vile
gloves, body bags, vifaa vya ufungashaji wa sampuli nk. Vifaa
hivyo vimeanza kusambazwa mikoani kupitia MSD
6
c. Zoezi la udhibiti wa matukio ya dharura (simulation exercise)
katika ngazi ya Taifa
Hitimisho