Kiswahili 3&4

You might also like

Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 4

KELLY’S ENGLISH MEDIUM SCHOOLS (KEMS)

MASWALI MBALI MBALI YA KISWAHILI: DARASA LA NNE

Chagua herufi ya jibu sahihi katika sentensi zifuatazo;

1. Samaki wa maji chumvi wana__________ nzuri (mabaka, ladha, chumvi, rangi)


2. Vitabu __________ juu ya meza (viko, vimo, zipo, vimekaa)
3. Pili alimuua mbwa wake kwa____________ (bomu, risasi,, bunduki)
4. Hawa watu ni chanda na pete______________ (marafiki, majirani, wanaishi karibu karibu)
5. Ni vizuri kufuata___________- ya shule (haki, ratiba, nidhamu, kazi)
6. Rehema ni hodari wa_____________ mashairi (kughairi, kughani, kukubali, kuchapa)
7. Hapo ___________ za kale binadamu alifanana na Sokwe (mwanzoni, zamani, mwishoni, katikati)
8. Mchwa huishi kwa kuzaliana kwenye____________ (mzinga, zizi, kichuguu, kichukuu)
9. Huyu ni___________ wa hapa kijijini kwetu (mkungu, mkunga, mkonge, mkenge)
10. Jose alipigwa_________ kuonekana eneo la shule kwa sababu ya wizi (tetemeko, marufuku, nadra)
11. Jua huchomoza asubuhi upande wa__________ (chini, juu, magharibi, mashariki)
12. Wagonjwa hulazwa_________ (chumbani, wodini, chumbani, nyumbani)
13. Baba___________ mama ni wazazi wangu (na, ni, wa, ya)
14. Ili tufaulu mitihani yetu____________ kusoma kwa bidii (ni budi, hatuna budi, si lazima, tuwahi)
15. Aghalabu maana yake ni____________ (maranyingi, mara moja, nadra, marachache)
16. Shangazi aliweka fedha na funguo_________ ndani ya pochi (yake, zake, wake, lake)
17. _______ ya ng’ombe ipo mgongoni (pembe, nundu, kwato, kinga)
18. ___________ mvua zikanyesha na watu wakapanda mbegu za kila aina (fukuto, hatimaye, maarufu)
19. Ali___________ pesa katika kiganja cha mkono na kukimbia hadi dukani (adhimisha, hamaki,
fumbata, tabasamu, shuhudia)
20. _________ ya shule yetu ni shati jeupe na siketi bluu (sare, vazi, rangi)
21. Kila siku nina amka____________ ili kufanya usafi ( alasiri, alfajiri, jioni, adhuhuri)
22. Sakafu ya nyumba imetengenezwa kwa____________ (saruji, sarufi, majivu, theluji)
23. Kabla ya kuanza biashara ni lazima uwe na______ (faida, fidia, kiasi, mtaji)
24. Usifanye________ kwenye biashara (zaidi, kero, mzaha, salio)
25. Wakatafakari maana yake ni___________________ (wakasahau, wakakariri, wakafikiri)
26.
Pigia msitari neon lililo tofauti na mengine kati ya haya yafuatayo
27. Nyumba, kibanda, ghorofa, mti
28. Maji, maziwa, soda, ugali
29. Meli, jahazi, mtumbwi, mlima

1 Jupis Sengo 0754982679 sengojupendosengo@yahoo.com 0782737884


30. Ng’ombe, mchngwa, mndimu, mpapai
31. Nyoka, nyuki, nyigu, dondola
32. Kisu, kijiko, sufuria, ugali
33. Gari, bajaji, farasi, Andrea
34. Jicho, kucha, ulimi, ngozi, pua
35. Shati, suruali, fulana, viatu
Tumia neon moja linalo jumuisha haya yafuatayo
36. Shati, gauni, fulana, sketi-
37. soda, juisi, sharubati, konyagi-
38. Mbuzi, kondoo, ng’ombe, mbwa-
39. Almasi, dhahabu, shaba, tanzanite-
40. Mahindi, mpunga, mtama, uwele-
41. Ugali, ndizi, viazi, wali-
42. Papai, nanasi, chungwa, embe-
43. Karoti, nyanya, kitunguu, pilipili-
Andika kinyume cha maneno yafuatayo
44. Mbele_____________
45. Baridi _____________
46. Nadra_____________
47. Huzuni ____________
48. Mvuli ________________
49. Kusanya ___________
50. Mwalimu ____________
51. Tajiri _____________
52. Afya _______________
53. Polepole _____________
54. Vunjika moyo ______________
Andika umoja au wingi wa maneno yafuatayo
Umoja wingi
55. ___________ mawe
56. Ukuta ________________
57. _________ masanduku
58. __________ kwato
59. Uji ______________
60. Gulio ________
61. ________ mashine
62. _______ mifereji
63. Kijiko ____________
64. Meza ____________
Andika visawe vya maneno yafuatayo
65. Tembo______________
66. Garimoshi ______________
67. KIfungua mimba_______________
68. Jokofu ______________
69. Keti_________________

2 Jupis Sengo 0754982679 sengojupendosengo@yahoo.com 0782737884


Jaza nafasi zilizoachwa kwa ajili yako
70. Keti maana yake ni_______________
71. Mtu ambaye hasikii huitwa ___________________
72. Mtu ambaye hawezi kutembea huitwa___________________
73. Mtu asiye na pua huitwa_____________________
74. Mtu asiyeona huitwa__________________
75. Mtu asiyeongea huitwa_______________________
76. Mtu asiye na meno huitwa_______________
77. Mtu anayeendesha treni huitwa_____________
78. Waislamu daima_____________ kwenye msikiti.
79. Nyumba ya nyuki huitwa__________________
80. Mtoto wa ndege huitwa__________________ wakati huo motto wa ng’ombe ni____________
81. Mtu anayefanya kazi ya kufua na kupiga pasi nguo huitwa _________________
82. Mtu anayefanya kazi ya kusafisha vyoo huitwa___________
83. Mtu anayejenga nyumba kwa kutumia tofali na mawe huitwa__________
84. Mtu anayetengeneza vitu vya thamani kama shanga na heleni huitwa____________

Kamilisha methali, jibu vitendawili au toa maana ya nahau

85. Haraka haraka _____________________


86. _____________________- mati nyuma
87. Usiache mbachao __________________________
88. Mvumilivu__________________________
89. Kila mtu humwabudu apitapo _____________________
90. Fikiri kabla ya__________________
91. Kila niendapo hunifuata _________________
92. Haba na haba____________________
93. Kula chumvi nyingi__________________________
94. Chapa mguu_____________________________
95. Nyumba yangu ina mlango juu ___________________
96. Pruu! Mpaka Maka ___________________
97. Hesabu yake haina faida_____________
98. Bwana afya wa porini _________________
99. Pita huko nipite huku tuonane katikati _________________
100. Mwamvuli upo msituni __________________
101. Mama hachoki kunibeba_________________
Jaza sehemu zilizoachwa wazi kwa kutumia maneno; kabla ya, baada ya, kwa ajili ya, bila
shaka, huna budi, mara kwa mara
102. Wingu jeusi limetanda angani kote____________ mvua itanyesha sasa hivi
103. Ukitaka kufaulu ____________ kusoma kwa bidii
104. _____________ kumsubiri muda mrefu, hatimaye mgeni aliwasili
105. ______________ kuanza kujibu swali lolote lile ni vizuri kulisoma tena na tena
106. Anafaulu kwa sababu hupitia masomo yake_______________
107. Wageni wote tayari wamewasili_____________ kikao
Chagua nahau zifuatazo kukamilisha maana katika sentensi zinazofuata

3 Jupis Sengo 0754982679 sengojupendosengo@yahoo.com 0782737884


Usingizi ulipaa, fedha lukuki, walikaa chonjo, waliangua kicheko, walipigwa butwaa, walitega
sikio, kufuja mali
108. Watu wote_______________ waliposikia Juma ameuawa na majambazi
109. Wanafunzi wote___________________ walipomwona mwalimu wao anacheza dansi.
110. Alikuwa na________ lakini hakuwa na mippango mizuri ya matumizi.
111. Baada ya kuota ndoto ya kutisha ____________ usiku wote.
112. Wanakijiji ____________ kumsikiliza mgombea wa ubunge wake alipofanya kampeni yake.
Andika katika wakati mbalimbali kama ulivyo elekezwa
113. Anacheza vizuri (uliopita)
114. Watakula wali wa Kyela (uliopo timilifu)
115. Ameangua vibaya sana (uliopita)
116. Watoto wamefaulu mitihani yao vizuri (ujao)
117. Kila mmoja aliandika barua ya kujieleza (uliopo)
118. Wanafunzi watacheza uwanjani (hali ya mazoea)
Weka alama sahihi za uandishi katika sentensi zifuatazo
119. Kwanini umechelewa kufika shule
120. mwalimu amemwambia serina kuwa aondoke
121. mama aliniagiza kuwa ninunue vitu vifuatavyo kisu kijiko sahani kikombe
122. Lo wameadhibiwa tena
123. Wanafunzi wote walifika jumatatu na alhamisi
124. Rais wa kenya anaitwa uhuru Kenyatta
125. Dada alisema nina hasira sana na wewe
Tumia herufi zifuatazo kuunda maneno ya Kiswahili
126. Luemi-
127. Mulimwa-
128. Sehul-
129. Lumii-
130. Mobak-
131. Suuki-
132. Ragi-
133. Sadara-
134. Dogoro-
135. Komno-

4 Jupis Sengo 0754982679 sengojupendosengo@yahoo.com 0782737884

You might also like