Somo La Kutengeneza Tambi Za Dengu

You might also like

Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 1

SOMO LA KUTENGENEZA TAMBI ZA DENGU

MAHITAJI
 Unga wa dengu ½ kilo
 Binzari nyembamba ½ kijiko cha mezani
 Unga wa pilipili manga kijiko 1 cha chai
 Unga wa mchele ¼ kilo
 Chumvi kiasi
 Mafuta ya alizezi ½ lita
 Baking powder

JINSI YA KUTENGENEZA
 Changanya unga wa mchele pamoja na ule wa dengu kasha chukua nyunyuza baking powder na
baadae chumvi.
 Weka unga wa binzari nyembamba na pilipili manga
 Changanya vizuri na kasha weka maji kidogo kidogo huku ukikanda hadi liwe donge gumu kama
unavyofanya kwenye maandazi.
 Baada ya hapo weka donge lako pembeni na funika.Acha likae kwa muda wa nusu saa hadi saa
moja.
 Baada ya hapo chukua karai la mafuta weka jikoni hadi mafuta yapate moto kabisa.Kisha
chukuwa mashini ya kupikia tambi[spaghetti] na weka donge lako. Kandamiza taratibu huku
ukiruhusu minyororo ya tambi kuingia kwenye mafuta yako yaliyo jikoni.
 Weka kiasi kiasi huku ukikaanga.acha mpaka zitakapokuwa zimeiva na kukauka vizuri.Ipua na
weka pembeni.
 Weka kwenye sahani safi na kavu.tambi zako zitakuwa tayari kwa kuliwa.
 Tafuta fingushio vizuri funga kasha peleka sokoni.
ANZA NA ULICHONACHO,ANZA SASA.

You might also like