Professional Documents
Culture Documents
Historia Ya TKU Na THBUB - First Draft - Sungu 2
Historia Ya TKU Na THBUB - First Draft - Sungu 2
(THBUB)
THBUB
Majukumu, Mafanikio na Changamoto
UTANGULIZI...........................................................................................................................3
2
UTANGULIZI
Historia ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) inaanzia mwaka 1966
ilipoundwa Tume ya Kudumu ya Uchunguzi (TKU) ambayo ilivunjwa mnamo mwaka 2001.
3
SEHEMU YA KWANZA
4
1.1 Utangulizi
Tume ya Kudumu ya Uchunguzi ni chombo kilichoundwa kikatiba chini ya kifungu
cha Sheria Na. 67-(1) ya mwaka 1965 ambacho kinasema kwamba ni lazima kuwepo
kwa Tume ya Kudumu ya Uchunguzi ambayo ina mamlaka ya kuchunguza tabia na
mwenendo wa kila mtu katika mamlaka yake au sehemu binafsi.
Chombo hiki kilianza kufanya kazi kisheria kwa sheria (Sheria Na. 25/1966) ambayo
inaipa Tume mamlaka ya kuchunguza malalamiko yote yanayohusiana na matumizi
mabaya ya ofisi kwa watumishi wa umma.
Kutoa elimu kwa umma juu ya mfumo mzima wa mgawanyo wa madaraka na njia
muhimu za kufuata kabla ya kuleta malalamiko Tume ya Kudumu ya Uchunguzi.
Kupokea malalamiko.
5
3. Nd. K.M. Kikwete 1967 - 1971
4. Sheikh Abdallah Iddi Chaurembo 1969 - 1973
5. Nd. Wilson Nkeno Bizuru 1972 - 1976
6. Nd. Alhaji Mharami Mfaume 1973 - 1977
7. Nd. John Rwemigira Kibogoyo 1976 - 1978
8. Bibi Thekla Grace Mchauru 1976 - 1978
9. Nd. John Baptist Mwenda 1976 - 1978
10. Nd. Samson Kishosha Gabba 1978 - 1983
11. Nd. Ali Ame Chum 1978 - 1983
12. Nd. Rabia Mohamed Hamdani 1978 - 1983
13. Nd. Ephraim Kulwa Mvanga 1978 - 1984
14. Nd. Vincent Magoma Dimiso 1983 - 1984
15. Nd. Asia Amour Hassan 1983 - 1989
16. Nd. Mohamed Khatibu Suleiman Reja 1984 - 1990
17. Nd. Crispin Tungaraza 1985 - 1991
18. Bibi Margreth Lilian Ngude 1985 - 1991
19. Nd. Mwinyiwesa Idarous 1989 - 1993
20. Nd. Haji M. Haji 1990 - 1996
21. Nd. I.S.A. Kasembo 1991 - 1995
22. Nd. A.S. Kabongo 1993 - 1999
23. Nd. Halima Hamisi 1994 - 2000
24. Nd. Ramadhani Shabani 1997 - 2002
Tume ya Kudumu ya Uchunguzi ilikuwa sehemu pekee kwa wakati huo ambako
raia waliweza kupeleka malalamiko yao kuhusiana na matumizi mabaya ya
madaraka na ofisi yaliyofanywa na baadhi ya viongozi wa umma dhidi ya
wananchi na kufanyiwa uchunguzi.
6
Kwa kipindi cha miaka 20 Tume ilikuwa ikipokea wastani wa malalamiko 3,000
kwa mwaka, haya ni yale yaliyoletwa kwa maandishi na kufunguliwa majalada.
Mengi ya malalamiko hayo yalielekezwa kwenye mamlaka husika na mengine
yalishughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi. Aidha, mengine yaliachwa kwa sababu
mbalimbali baada ya kufanyiwa uchunguzi na mengine yalionekana hayana
msingi.
1.6 Changamoto
Watu kukosa imani na utendaji wa Tume kwa kuwa ushahidi ulionyesha kuwa
kulikuwa na ongezeko la utumiaji mbaya wa madaraka miongoni mwa Watumishi
na viongozi wa umma.
Urasimu katika mfumo mzima wa utendaji kazi serikalini ulifanya utoaji huduma
kwa Wananchi kuwa wa taratibu na kufanya wale waliokuwa wanadai haki zao
kuendelea kusubiri kwa muda mrefu bila mafanikio. Hii ilisababisha kutokuwa na
mahusiano mazuri kati ya Tume ya Kudumu ya Uchunguzi, taasisi za serikali na
Wananchi.
Uhaba wa vitendea kazi, mfano magari na ukosefu wa fedha za kutosha kwa ajili
ya kufanikisha malengo ya Tume, hali hii ilisababisha kazi nyingi kutofanyika
kwa wakati na nyingine kutofanyika kabisa.
Tume ilitumia rasilimali chache zilizokuepo kipindi hicho kuhakikisha kuwa kazi
za Tume zinaendelea kufanyika kwa ufanisi bila kuathiri kwa kiasi kikubwa
jitihada za kuwahudumia Wananchi.
7
SEHEMU YA PILI
8
2.1 Utangulizi
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ni chombo huru cha Serikali
kinachojitegemea ambacho kinahusika na kulinda, kuhifadhi na kutetea haki za
binadamu na misingi ya utawala bora hapa Tanzania.
9
2.4 Majukumu ya Tume
Ibara ya 130 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kifungu cha 6(1)
cha sheria Na.7/2001 zinafafanua majukumu ya Tume. Majukumu hayo ni haya
yafuatayo:
Kuhamasisha nchini hifadhi ya haki za binadamu na wajibu kwa jamii kwa mujibu
wa Katiba na sheria za nchi.
Kutoa ushauri kwa Serikali na vyombo vingine vya umma na vya sekta binafsi
kuhusu haki za binadamu na utawala bora.
Kufanya utafiti, kutoa na kueneza elimu kwa umma kuhusu haki za binadamu na
misingi ya utawala bora.
10
Tume ina Katibu Mtendaji ambaye huteuliwa na Rais baada ya mashauriano na
Tume. Huyu ndiye msimamizi mkuu wa kazi za siku hadi siku kuhusu masuala ya
kiutawala na utekelezaji wa maamuzi ya kisera ya Tume.
11
12
Aidha, kuna vitengo vifuatavyo katika Tume:
1. Kitengo cha Uhasibu na Fedha
2. Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani wa Hesabu
3. Kitengo cha Teknolojia, Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
4. Kitengo cha Ununuzi na Ugavi.
5. Kitengo cha Mipango, Ufuatiliaji na Tathimini
Pia kuna Ofisi ya Zanzibar na Ofisi za Matawi za Tume kama ifuatavyo:
1. Ofisi ya Zanzibar
2. Ofisi ya Tawi Mwanza
3. Ofisi ya Tawi Lindi
4. Ofisi ya Tawi Pemba
5. Ofisi ya Tawi Dar Es Salaam
2.6 Viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
13
19. Mhe. Nyanda Josiah Shuli 2019 - hadi sasa
14
Makamishna Wasaidizi 2002 – 2019
JINA MWAKA
1. Mhe. Costantine Biseko Luguli Mugusi 2007 - 2010
2. Mhe. Fahamu Hamidu Mtulya 2007 - 2010
15
Watumishi
Tangu mwaka 2003/2004 Tume imekuwa ikiajiri watumishi wapya ili kukidhi
mahitaji ya rasilimali watu. Hadi hivi sasa Tume inao jumla ya watumishi 154 katika
nafasi mbalimbali. Hivyo kuna upungufu wa watumishi 65. Idadi hiyo ni pungufu
kidogo kufikia idadi ya watumishi wanaohitajika yaani 219 kwa mwaka wa fedha
2020/2021.
Dar es Salaam (Kanda ya Mashariki), ipo mtaa wa Luthuli Kitalu na. 8 katika
jengo lijulikanalo kama “Haki House”. Tarehe 28 Januari, 2003 Tume
ilikabidhiwa jengo hilo jipya. Jengo hili lilijengwa kwa ufadhili wa serikali ya
Denmark. Jengo hilo lilifunguliwa rasmi Aprili 30, 2003 na makamu wa rais wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein kwa niaba ya
aliyekuwa Rais wa awamu ya tatu, Mhe. Benjamini William Mkapa.
Zanzíbar (ofisi ya tawi yenye hadhi ya kitaifa), ipo katika jengo la Kamisheni ya
Wakfu na Mali za Amana, eneo la Mbweni.
Mwanza (Kanda ya Ziwa), ipo mtaa wa Liberty, ndani ya jengo la Benki ya Taifa
ya Biashara, Ghorofa ya tatu (3).
Lindi (Kanda ya Kusini), ipo mtaa wa Wailesi, Barabara iendayo kwa Mkuu wa
Mkoa, ndani ya jengo la zamani la TTCL.
Pemba (Tawi), ipo Wete Pemba, mtaa wa Kitutia, mkabala na ofisi za posta wete.
Aidha, kwa Dodoma, Tume ina ofisi nyingine mbili katika majengo ya Chuo
Kikuu cha Dodoma (UDOM) yaliyopo katika Kitivo cha Sayansi ya Jamii.
2.8 Mafanikio
Tangu Tume ianze kufanyakazi mwaka 2001 hadi hii leo imepata mafanikio mengi.
Miongoni mwa mafanikio hayo ni pamoja na yafuatayo:
Hadi Desemba 31, 2019 Tume ilikuwa imeshughulikia na kuhitimisha mashauri
19,622 kati ya 27,346 yaliyopokelewa ambayo ni sawa na asilimia 72 ya mashauri
yote. Baadhi ya malalamiko hayo yameelekezwa kwenye mamlaka husika kwa
hatua zaidi. Aidha, zaidi ya asilimia 90 ya malalamiko yaliyopokelewa na
kushughulikiwa yanahusu ukiukwaji wa misingi ya utawala bora na chini ya
asilimia 10 yanahusu uvunjwaji wa haki za binadamu.
16
- Utafiti juu ya Unyanyasaji wa Watoto Tanzania Bara mwaka 2005
- Utafiti juu ya Mateso na Unyanyasaji unaofanywa na Vyombo vya Kutekeleza
Sheria Tanzania mwaka 2007
- Utafiti na Uchunguzi juu ya Utekelezaji wa Haki za Watoto Zanzibar mwaka
2008 na
- Utafiti juu ya Mauaji ya Watu wenye Ulemavu wa Ngozi (albino) na
Vikongwe wenye Macho Mekundu Tanzania Bara mwaka 2009.
Tume ilipata nafasi ya kupitia na kutoa maoni juu ya Sheria ya Kuzuia Ugaidi na
Sheria ya Kuzuia na Kudhibiti Kuenea kwa VVU na UKIMWI. Pia Tume ilishiriki
kwa sehemu kubwa katika mchakato wa maandalizi na utungaji wa Sheria ya
Mtoto.
Tume imeweza kutembelea magereza, vituo vya mafunzo na polisi mara kwa
mara kwa lengo la kufanya ukaguzi na kutoa elimu ya haki za binadamu na
misingi ya utawala bora kwa wafungwa, mahabusu, maafisa wa jeshi la magereza
na polisi. Ifuatayo ni adadi ya taasisi zilizotembelewa kila mwaka:
2003/04 21 36
2004/05 16 42
2005/06 37 75
2006/07 - -
2008/09 75 -
2009/10 62 -
2010/11 29 51
1
Takwimu hizi ni kwa kipindi cha July 1, 2007 hadi Machi 31, 2008
2
Ikiwa ni magereza matatu (3) Tanzania Bara na Vyuo 10 vya mafunzo visiwani Zanzibar
3
Ikiwa ni vituo vya polisi sita (6) Tanzania Bara na vituo vya polisi 25 Zanzibar.
17
2011/12 - -
2012/13 46 48
2013/14 - -
2014/15 - -
2015/16 37 32
2016/17 32 32
2017/18 9 6
2018/19 22 13
Imefanya ziara na kutoa elimu ya haki za binadamu na utawala bora katika Wilaya
zaidi ya 130 zilizoko katika Mikoa 26 ya Tanzania bara. Vilevile imetembelea
Mikoa yote mitano na Wilaya zake 10 visiwani Zanzibar.
18
ufumbuzi na mengine kuyaelekeza kwenye mamlaka husika kwa hatua zaidi.
Matokeo ya ziara hizo ni kuongezeka kwa idadi ya malalamiko yanayowasilishwa
Tume kila mwaka.
Imeweza kuandaa semina kwa wadau mbalimbali wakiwemo waandishi wa
habari, Asasi Zisizo za Kiserikali, watu wenye ulemavu, wabunge wa Bunge la
Muungano na wajumbe wa baraza la Wawakilishi la Zanzibar.
Tena katika maonesho hayo hayo yaliyofanyika katika viwanja vya CCM
Kirumba jijini Juni 2010, Tume ilishinda nafasi ya tatu katika tuzo ya utoaji
huduma bora. Kadhalika, katika ngazi ya kimataifa, Tume imepewa daraja ‘A’
miongoni mwa Taasisi za kitaifa za haki za binadamu. Tume imepangwa daraja
hilo la ‘A’ na Kamati ya Kimataifa ya Kuratibu Ukuzaji na Utetezi wa Haki za
Binadamu (The International Coordinating Committee on the Promotion and
Protection of Human Rights).
19
2.9 Changamoto
Tume inakabiliwa na changamoto zifuatazo katika kutekeleza majukumu yake:
Watanzania wengi kutokuwa na uelewa wa kutosha wa haki za binadamu na
misingi ya utawala bora.
Kutofikika kirahisi kwa Tume kutokana na huduma zake kuwa mbali na wananchi
walio wengi. Nchi inayokadiriwa kuwa na watu milioni 50 inatarajiwa
20
kuhudumiwa na Tume yenye ofisi sita tu zilizopo Dodoma, Dar es Salaam,
Zanzibar, Mwanza, Lindi na Pemba.
Pia tume inatarajia kufungua ofisi zaidi katika ngazi ya kanda na baadaye mikoa
kwa lengo la kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi.
21
22