Praying God's Word

You might also like

Download as doc, pdf, or txt
Download as doc, pdf, or txt
You are on page 1of 28

PRAYING GOD’S WORD

MANENO YA MAANDIKO MATAKATIFU AMBAYO


YAWEZA KUTUMIKA KUJIKABIDHI KATIKA ULINZI
WA KIMUNGU

Aya 208 za Maandiko matakatifu ambazo zaweza


kutumika katika kuomba ulinzi wa Kimungu
peterleonard864@gmail.com

0
UTANGULIZI
Ni muhimu tukumbuke kuwa neno la Mungu li hai na tena lina
nguvu. Tunasoma katika (Ebr. 4:12) kwamba; “Maana Neno la neno la
Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote
ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo
na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na
makusudi ya moyo.” Pia soma Isaya 55:11. Maandiko matakatifu yana
uvuvio wa Roho Mtakatifu. Yana pumzi ya kimungu ndani yake na kwa
hiyo ni maneno yaliyo hai. Maneno haya yanatuongoza kumfikia Yesu
mwenyewe ambaye yeye ndiye neno wa Mungu aliyekuwako kwa
Mungu, naye alikuwa mungu, vitu vyote vilifanyika kwake na wala
1
pasipo yeye hakuna lililoweza kufanyika. Ni neno aliyefanyika mwili
akakaa kwetu. (Yoh 1:1…) Katekisimu ya kanisa katoliki inafundisha
kuwa neno la Mungu ni sala ya kikristu.
Bwana wetu Yesu Kristu ni kielelezo chetu katika kutumia maandiko
matakatifu kama sala. Katika (Mt. 27:46 na Mk 15:34) Tunaona kuwa
Yesu alipokuwa msalabani alisali na kusema “Mungu wangu Mungu
wangu mbona umeniacha?” Maneno haya ya sala ya Yesu yanapatikana
katika (Zaburi 22:1) Pia katika (Lk. 23:46) Tunaona kuwa Yesu
alipokuwa msalabani amekaribia kukata roho alimwita baba akisali
maneno ya zaburi na kusema: “mikononi mwako naiweka roho yangu”.
Maneno kama haya yanapatikana katika (Zaburi 31:5). Katika mifano
hii tunapata kujifunza kuwa Yesu alikuwa amejawa na neno la Mungu
ndani yake na alilitumia kama sala yake. Hivyo ndivyo nasi
inavyotupasa. Mtume Paulo anafundisha katika waraka wake kwa
Wakolosai (Kol. 3:16) kwa kuandika kuwa, “Neno la Kristu na likae
kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana
kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu
kwa neema mioyoni mwenu.” Imetupasa kujawa neno la Mungu. Kila
siku tuchukue Muda kusoma neno la Mungu na kulitafakari na kuliweka
katika kumbukumbu za akili zetu. Kiwango cha nguvu ya kiroho tuliyo
nayo hutegemea sana kiwango cha neno la Mungu tulichonacho ndani
mwetu na kiwango cha kutumia hilo neno la Mungu katika sala na
Maisha yetu ya kila siku kwa ujumla.
2
Kuna uhitaji wa kuwa na utajiri wa ufahamu wa neno la Mungu;
kuna uhitaji wa kujua maandiko matakatifu kwa kiasi kikubwa. Kwa
hiyo Chukua muda wako kusoma na kukariri(memorize) neno la Mungu
na kulitumia katika kusali. Kumbuka pia Roho wa Mungu hutumia na
hutusaidia kutumia maandiko haya tunayoyafahamu katika kusali. Aya
hizi zipatazo 200 zimeandikwa ili kukurahisishia wewe uweze kuzisoma
na kuzikariri. Aya hizi pamoja na kuwa zenye manufaa mengi katika
Maisha yetu, ni nzuri hasa katika sala ya kuomba ulinzi wa kimungu
dhidi ya adui mwovu wa maisha mema ya kiroho na ya kimwili. Roho
wa Mungu akujalie paji la akili na elimu, uweze kusoma, kuelewa na
kutumia aya hizi.

1. Maana, Daudi mwenyewe asema katika chuo cha Zaburi, Bwana


alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, hata
niwaweke adui zako Kuwa kiti cha kuwekea miguu yako. -(Luka
20:42-43)
2. Mungu huondoka, adui zake wakatawanyika, Nao wamchukiao
huukimbia uso wake. –(Zaburi 68:1)
3. Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu
zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. (Luka
10:19)
4. (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika
Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha mawazo na kila kitu
3
kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara
kila fikira ipate kumtii Kristo; (2 Wakorintho 10:4-5)
5. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za
Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na
nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza
hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza
kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya
haki kifuani, na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya
amani; zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo
mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. Tena
ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la
Mungu; kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho,
mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea
watakatifu wote; -(Waefeso 6:11-18)
6. Na ahimidiwe Bwana, mwamba wangu, Anifundishaye mikono
yangu vita, Vidole vyangu kupigana. –(Zaburi 144:1)
7. Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni
nani aliye juu yetu? –(Warumi 8:31)
8. Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali
kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata
kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani
4
yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo. –
(Waebrania 4:12)
9. Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na
upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake;
na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake. -(Ufunuo wa
Yohana 1:16)
10.Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo; sasa mkuu wa ulimwengu
huu atatupwa nje. –(Yohana 12:31)
11. Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa;
usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu
pamoja nawe kila uendako. -(Yoshua 1:9)
12.Nanyi mtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu chini ya
nyayo za miguu yenu; katika siku ile niifanyayo, asema Bwana wa
majeshi. -(Malaki 4:3)
13.Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma; Hujikwaa na kuangamia
mbele zako. –(Zaburi 9:3)
14.Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma; Hujikwaa na kuangamia
mbele zako. –(Zaburi 9:3)
15.Tena ikiwa baada ya hayo hamtaki kunisikiza, ndipo nitawaadhibu
zaidi mara saba kwa ajili ya dhambi zenu. -(Mambo ya Walawi
26:18)
16.Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza. -(Yohana 1:5)
17.Na pepo wachafu, kila walipomwona, walianguka mbele yake,
5
wakalia wakisema, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu. -(Marko 3:11)
18.Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu
watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; -(Marko 16:17)
19.Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta
kwa miguu. –(Zaburi 91:13)
20.kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda
kuwapigania juu ya adui zenu, ili kuwaokoa ninyi. –(Kumbukumbu
la Torati 20:4)
21.Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu
Yesu Kristo. –(1 Wakorintho 15:57)
22.Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko
wale walio pamoja nao. -(2 Wafalme 6:16)
23.Ee Bwana, uyasikilize maneno yangu, Ukuangalie kutafakari
kwangu. –(Zaburi 5:1)
24.nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na
maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za
miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo. -
(Kumbukumbu la Torati 12:3)
25.Ee Bwana, utete nao wanaoteta nami, Upigane nao wanaopigana
nami. –(Zaburi 35:1)
26.Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni
nani aliye juu yetu? -(Warumi 8:31)
27.Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi
6
mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko
yeye aliye katika dunia. (1 Yohana 4:4)
28.Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali
ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya
majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. –(Waefeso
6:12)
29.Avunjaye amekwea juu mbele yao; Wamebomoa mahali, wakapita
mpaka langoni, Wakatoka nje huko; Mfalme wao naye amepita
akiwatangulia, Naye Bwana ametangulia mbele yao. –(Mika 2:13)
30.Bwana ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lake. –(Kutoka 15:3)
31.Kelele milimani kama kelele za watu wengi sana; kelele za falme
za mataifa waliokutana pamoja; Bwana wa majeshi anapanga jeshi
kwa vita; -(Isaya 13:4)
32.Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda,
kwa yeye aliyetupenda. –(Warumi 8:37)
33.Ni nani Mfalme wa utukufu? Bwana mwenye nguvu, hodari,
Bwana hodari wa vita. –(Zaburi 24:8)
34.Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye
ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika? –
(Mathayo 26:53)
35.Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba mashaka makubwa yatokayo
kwa Bwana yatakuwa kati yao; na kila mmoja wao atakamata
mkono wa jirani yake, na mkono wake utainuliwa ili kushindana
7
na mkono wa jirani yake. -(Zekaria 14:13)
36.Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani;
naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si
kinga kilichotolewa motoni? –(Zekaria 3:2)
37.Hupiga mbio kama mashujaa; huupanda ukuta kama watu wa vita;
nao huendelea mbele kila mmoja katika njia zake, wala
hawapotoshi safu zao. Wala hapana mmoja amsukumaye
mwenzake; huendelea mbele kila mmoja katika njia yake;
hujifanyizia njia kwa nguvu kati ya silaha, wala hawaachi kuifuata
njia yao. –(Yoeli 2:7-8)
38.Huurukia mji; hupiga mbio juu ya ukuta; hupanda na kuingia
ndani ya nyumba; huingia madirishani kama aingiavyo mwivi. –
(Yoeli 2:9)
39.nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya
uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe
utamponda kisigino. –(Mwanzo 3:15)
40.Akasema, Lifungue dirisha linaloelekea mashariki; akalifungua.
Basi Elisha akasema, Piga; akapiga. Akasema, Mshale wa Bwana
wa kushinda, naam, mshale wa kushinda Shamu, kwa maana
utawapiga Washami katika Afeki hata utakapowaangamiza. –(2
Wafalme 13:17)
41.Hawa watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana Kondoo
atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme
8
wa Wafalme, na hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na
wateule, na waaminifu. –(Ufunuo wa Yohana 17:14)
42.Waaibishwe, wafedheheshwe, Wanaoitafuta nafsi yangu.
Warudishwe nyuma, wafadhaishwe, Wanaonizulia mabaya. -
(Zaburi 35:4)
43.Wawe kama makapi mbele ya upepo, Malaika wa Bwana
akiwaangusha chini. –(Zaburi 35:5)
44.Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa
nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye
ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu. -(Ufunuo
wa Yohana 12:12)
45.Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe,
na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa
haki ahukumu na kufanya vita. –(Ufunuo wa Yohana 19:11)
46.Naam, Mungu anipatiaye kisasi, Na kuwatweza watu chini yangu,
-(2 Samweli 22:48)
47.Na kunileta nje nitoke kwa adui zangu; Naam, waniinua juu yao
walioniinukia; Waniponya na mtu wa jeuri. –(2 Samweli 22:49)
48.watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru
kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata
afya. –(Marko 16:18)
49.Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia Bwana wimbo huu
wakanena, na kusema, Nitamwimbia Bwana, kwa maana
9
ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini. –
(Kutoka 15:1)
50.Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri,
mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha
mataifa! –(Isaya 14:12)
51.Bwana, mkono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo, Bwana,
mkono wako wa kuume wawaseta-seta adui. –(Kutoka 15:6)
52.Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; Umenifanyizia nafasi
wakati wa shida; Unifadhili na kuisikia sala yangu. –(Zaburi 4:1)
53.Tazama, moto ulishuka kutoka mbinguni, ukawateketeza wale
akida wa hamsini wawili wa kwanza pamoja na hamsini wao; laiti
sasa roho yangu na iwe na thamani machoni pako. –(2 Wafalme
1:14)
54.Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni
kama umeme. (Luka 10:18)
55.Farasi huwekwa tayari kwa siku ya vita; Lakini Bwana ndiye
aletaye wokovu. –(Mithali 21:31)
56.maana Mungu wetu ni moto ulao. –(Waebrania 12:29)
57.Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema,
Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu
sawasawa na neno la Elisha. –(2 Wafalme 6:18)
58.Utupe umeme, uwatawanye, Uipige mishale yako, uwafadhaishe.
–(Zaburi 144:6)
10
59.Piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele
ulioitiwa, ukaungama maungamo mazuri mbele ya mashahidi
wengi. -(1 Timotheo 6:12)
60.Huwafanya malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa
moto wa miali. -(Zaburi 104:4)
61.Maana hao adui zako, Ee Bwana, Hao adui zako watapotea, Na
watendao maovu watatawanyika wote pia. –(Zaburi 92:9)
62.Ulimi wangu nao utasimulia Haki yako mchana kutwa. Kwa
maana wameaibishwa, Wametahayarika, wanaonitakia mabaya. –
(Zaburi 71:24)
63.Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini! Kwa ajili
ya wingi wa nguvu zako, Adui zako watakuja kunyenyekea mbele
zako. –(Zaburi 66:3)
64.Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza;
nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukata-kata
mapingo ya chuma; -(Isaya 45:2)
65.Kwa fadhili zako utawakatilia mbali adui zangu; Na
kuwaangamiza wote wanitesao nafsi, Kwa maana mimi ni
mtumishi wako. -(Zaburi 143:12)
66.awajalieni, kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake, kufanywa
imara kwa nguvu, kwa kazi ya Roho wake katika utu wa ndani. –
(Waefeso 3:16)
67.Ulipofanya mambo ya kutisha tusiyoyatazamia, ulishuka, milima
11
ikatetema mbele zako. –(Isaya 64:3)
68.Bali nitawaponda watesi wake mbele yake, Nitawapiga
wanaomchukia. –(Zaburi 89:23)
69.Nami nitapeleka mavu mbele yako, watakaomfukuza Mhivi, na
Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako. –(Kutoka 23:28)
70.Wenye dhambi waangamizwe katika nchi, Watendao ubaya
wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. –(Zaburi
104:35)
71.Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye
vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu
yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi, -(Waebrania
2:14)
72.Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani
mwako, na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa
sababu ya kutiwa mafuta. -(Isaya 10:27)
73.Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu. Wavikwe laumu
na aibu wanaonitakia mabaya. –(Zaburi 71:13)
74.bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda
juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka;
watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia. –(Isaya 40:31)
75.Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza; Wakazama kama
risasi ndani ya maji makuu. –(Kutoka 15:10)
76.ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote wa hiyo nchi mbele yenu,
12
nanyi mtayaharibu mawe yao yote yenye kuchorwa sanamu, na
kuziharibu sanamu zao zote za kusubu, kuvunja-vunja mahali pao
pote palipoinuka; -(Hesabu-Numbers 33:52)
77.Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na
kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na
kuangamia. –(Isaya 41:11)
78.Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria,
chenye meno; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya
vilima kuwa kama makapi. –(Isaya 41:15)
79.Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama,
Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu! –
(Yohana 1:29)
80.Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao
mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima,
na chini ya kila mti wenye majani mabichi; -(Kumbukumbu la
Torati 12:2)
81.Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni
nini nitakalo zaidi? –(Luka 12:49)
82.Nchi yote na imwogope Bwana, Wote wakaao duniani na
wamche. –(Zaburi 33:8)
83.Mungu ni mwenye kutisha Kutoka patakatifu pako. Ndiye Mungu
wa Israeli; Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo. Na
ahimidiwe Mungu. –(Zaburi 68:35)
13
84.Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, Maana Yeye
atawakanyaga watesi wetu. –(Zaburi 108:13)
85.Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Naam, Mungu aghadhibikaye
kila siku. Mtu asiporejea ataunoa upanga wake; Ameupinda uta
wake na kuuweka tayari; Naye amemtengenezea silaha za kufisha,
Akifanya mishale yake kuwa ya moto. –(Zaburi 7:11-13)
86.Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, Maana Yeye
atawakanyaga watesi wetu. –(Zaburi 108:13)
87.Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Naam, Mungu aghadhibikaye
kila siku. –(Zaburi 7:11)
88.Mtu asiporejea ataunoa upanga wake; Ameupinda uta wake na
kuuweka tayari; -(Zaburi 7:12)
89.Naye amemtengenezea silaha za kufisha, Akifanya mishale yake
kuwa ya moto. –(Zaburi 7:13)
90.Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama,
Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda
apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba. –(Ufunuo
wa Yohana 5:5)
91.Kisulisuli kikiisha pita asiye haki hayuko tena; Bali mwenye haki
ni msingi wa milele. –(Mithali 10:25)
92.Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota
ulizoziratibisha; -(Zaburi 8:3)
93.Na wa Wagadi wakajitenga kumfuata Daudi ngomeni huko
14
nyikani, waume mashujaa, watu waliozoea vita, walioweza
kutumia ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kama nyuso za
simba, nao walikuwa wepesi kama kulungu juu ya milima; -
(Mambo ya Nyakati 12:8)
94.Basi, kwa kuwa nitamkatilia mbali nawe mtu mwenye haki na mtu
mbaya, upanga wangu utatoka alani mwake, uwe juu ya watu wote
wenye mwili toka kusini hata kaskazini, -(Ezekieli 21:4)
95.Mataifa wamezama katika shimo walilolifanya; Kwa wavu
waliouficha imenaswa miguu yao. –(Zaburi 9:15)

96.Ila Bwana, Mungu wako, atawatoa mbele yako, atawatia mashaka,


mashaka makuu, hata waishe kuangamizwa. –(Kumbukumbu la
Torati 7:23)
97.kwake upo mkono wa mwili; ila kwetu yupo Bwana, Mungu wetu,
kutusaidia, na kutupigania mapigano yetu. Na watu
wakayategemea maneno ya Hezekia, mfalme wa Yuda. –(2 Mambo
ya Nyakati 32:8)
98.Akajivika haki kama deraya kifuani, na chapeo cha wokovu
kichwani pake, akajivika mavazi ya kisasi yawe mavazi yake, naye
alivikwa wivu kama joho. –(Isaya 59:17)
99.Hapo ndipo walipoingiwa na hofu nyingi, Maana Mungu yupo
pamoja na kizazi cha haki. –(Zaburi 14:5)
100. Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri, juu ya Bwana. –
15
(Mithali 21:30)
101. Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake,
ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake. –
(Ufunuo wa Yohana 12:16)
102. Sitayaogopa makumi elfu ya watu, Waliojipanga juu yangu
pande zote. –(Zaburi 3:6)
103. Bwana, uinuke, Mungu wangu, uniokoe, Maana umewapiga
taya adui zangu wote; Umewavunja meno wasio haki. –(Zaburi
3:7)
104. Wokovu una Bwana; Baraka yako na iwe juu ya watu wako. –
(Zaburi 3:80
105. Wakabwaga chini kila mtu fimbo yake, nazo zikawa nyoka;
lakini fimbo ya Haruni ikazimeza fimbo zao. –(Kutoka 7:12)
106. Bwana ndiye mwenye haki, Amezikata kamba zao wasio haki.
–(Zaburi 129:4)
107. Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, Watarudi nyuma,
kwa ghafula wataaibika. -(Zaburi 6:10)
108. Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni
wajasiri kama simba. –(Mithali 28:1)
109. Toeni dhabihu za haki, Na kumtumaini Bwana. –(Zaburi 4:5)
110. Hapo ndipo walipoingiwa na hofu nyingi, Maana Mungu yupo
pamoja na kizazi cha haki. –(Zaburi 14:5)
111. Maana umeniponya nafsi yangu na mauti, Macho yangu na
16
machozi, Na miguu yangu na kuanguka. –(Zaburi 116:8)
112. Bwana uondoke kwa hasira yako; Ujiinue juu ya jeuri ya watesi
wangu; Uamke kwa ajili yangu; Umeamuru hukumu. –(Zaburi7:6)
113. Mwenye haki atafurahi akionapo kisasi; Ataiosha miguu yake
katika damu ya wasio haki. –(Zaburi 58:10)
114. Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi
na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina
la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.
–(1 Samweli 17:45)
115. Washitaki wangu watavikwa fedheha, Watajivika aibu yao
kama joho. –(Zaburi 109:29)
116. Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi
utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa.
Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka
kwangu mimi, asema Bwana. –(Isaya 54:17)
117. Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani?
Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani? –(Zaburi 27:1)
118. Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia
zako zote. –(Zaburi 91:11)
119. Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo
ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako
ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. -
(Yohana 17:11)
17
120. Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa
mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele
yako kwa njia saba. –(Kumbukumbu la Torati 28:7)
121. Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi
kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye
atawatia ninyi mikononi mwetu. –(1 Samweli 17:47)
122. Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia,
akawa salama. –(Mithali 18:10)
123. Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye; -(Zaburi
121:3)
124. Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni,
Nitamwokoa na kumtukuza; -(Zaburi 91:15)
125. Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, Neno lako nimelingojea. –
(Zaburi 119:114)
126. Kutoka kwake lautoka mwisho wa mbingu, Na kuzunguka
kwake hata miisho yake, Wala kwa hari yake Hakuna kitu
kilichositirika. –(Zaburi 19:6)
127. Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto
mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye
ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba
wa milele, Mfalme wa amani. –(Isaya 9:6)
128. Adui wamekoma na kuachwa ukiwa milele. Nayo miji yao
uliing'oa; Hata kumbukumbu lao limepotea. –(Zaburi 9:6)
18
129. kwa kuwa Bwana. Mungu wako, yuatembea katika kituo
akuokoe, na kukutolea adui zako mbele yako; kwa hiyo na kiwe
kitakatifu kituo chako; asije akaona kitu kwako kisichokuwa safi,
akageuka na kukuacha. –(Kumbukumbu la Torati 23:14)
130. wala msimpe Ibilisi nafasi. –(Waefeso 4:27)
131. Bwana huwahifadhi wote wampendao, Na wote wasio haki
atawaangamiza. –(Zaburi 145:20)
132. Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa;
Mwanadamu atanitenda nini? –(Waebrania 13:6)
133. Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. –
(Yakobo 4:7)
134. Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka
palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu. –(Zaburi 91:14)
135. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana,
yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao. –(Mathayo
1:21)
136. Uwe kwangu mwamba wa makazi yangu, Nitakakokwenda
sikuzote. Umeamuru niokolewe, Ndiwe genge langu na ngome
yangu. –(Zaburi 71:3)
137. Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na
kuwalinda na yule mwovu. –(2 Wathesalonike 3:3)
138. Ee Bwana, uniponye na adui zangu; Nimekukimbilia Wewe,
unifiche. –(Zaburi 143:9)
19
139. Ee Bwana, uniponye na adui zangu; Nimekukimbilia Wewe,
unifiche. –(Zaburi 143:9)
140. Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso, Utanizungusha
nyimbo za wokovu. –(Zaburi 32:7)
141. Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachia matawi ya asili, wala
hatakuachia wewe. –(Warumi 11:21)
142. Na itakuwa ya kwamba mtu awaye yote atakayeliita jina la
Bwana ataponywa; kwa kuwa katika mlima Sayuni na katika
Yerusalemu watakuwako watu watakaookoka, kama Bwana
alivyosema; na katika mabaki, hao awaitao Bwana. –(Yoeli 2:32)
143. Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika
mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala
mwali wa moto hautakuunguza. –(Isaya 43:2)
144. Mfano wake ni mtu ajengaye nyumba, na kuchimba chini sana,
na kuweka msingi juu ya mwamba; na kulipokuja gharika, mto
uliishukia nyumba ile kwa nguvu, usiweze kuitikisa; kwa kuwa
imejengwa vizuri. –(Luka 6:48)
145. Uamke, uwe macho ili kunipatia hukumu Kwa ajili ya madai
yangu, Mungu wangu na Bwana wangu. –(Zaburi 35:23)
146. Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka
utawaseta kwa miguu. –(Zaburi 91:13)
147. Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba
yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake
20
umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi. –(Ayubu
1:10)
148. Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya
upendo na ya moyo wa kiasi. –(2 Timotheo 1:7)
149. Nitasema, Bwana ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu nitakayemtumaini. –(Zaburi 91:2)
150. Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni
iharibuyo. –(Zaburi 91:3)
151. Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata
kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao. –(Zaburi 91:4)
152. Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo
navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia
kabisa, wala sitakuacha kabisa. –(Waebrania 13:5)
153. Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue
matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru. –(Warumi 13:12)
154. Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu, Na wale
walionichukia, Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi. –(Zaburi
18:17)
155. Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe;
wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu. –
(Yohana 10:28)
156. Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote; wala hakuna
mtu awezaye kuwapokonya katika mkono wa Baba yangu. –
21
(Yohana 10:29)
157. Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza. –
(Zaburi 50:15)
158. Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake
huwapatanisha naye. –(Mithali 16:7)
159. Ee Mungu wangu, uniopoe mkononi mwa mkorofi, Katika
mkono wake mwovu, mdhalimu, -(Zaburi 71:4)
160. Hata ulipofika mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari,
siku yake ya kumi na tatu, amri ya mfalme na mbiu yake
ilipowadia kutekelezwa; ambayo siku ile adui za Wayahudi
walitumaini kuwatawala, bali kumebadilika kinyume, hata
Wayahudi waliwatawala wale waliowachukia; -(Esta 9:1)
161. Bwana ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu,
Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, Ngao yangu, na
pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu. –(Zaburi 18:2)
162. akasema, Bwana ndiye jabali langu, na ngome yangu, na
mwokozi wangu, naam, wangu; -(2 Samweli 22:2)
163. Ni nani huyu atokaye Edomu, Mwenye mavazi ya kutiwa damu
kutoka Bosra? Huyu aliye na nguo za fahari, Anayekwenda katika
ukuu wa uweza wake? –(Isaya 63:1)
164. Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa
na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee
mfalme. –(Danieli 3:17)
22
165. Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi,
lakini mwili ni dhaifu. –(Mathayo 26:41)
166. Naam, tangu siku ya leo, mimi ndiye; wala hapana awezaye
kuokoa katika mkono wangu; mimi nitatenda kazi, naye ni nani
awezaye kuizuia? –(Isaya 43:13)
167. Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana humponya
nayo yote. -(Zaburi 34:19)
168. Bwana, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe, Uniokoe na
wote wanaonifuatia, uniponye. –(Zaburi 7:1)
169. Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze
kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; -(Isaya 59:1)
170. Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu, Na wale
walionichukia, Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi. –(Zaburi
18:17)
171. Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, ili kwa
kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, hata wasikie
Mataifa yote; nami nikaokolewa katika kinywa cha simba. –(2
Timotheo 4:17)
172. Tazama, jicho la Bwana li kwao wamchao, Wazingojeao fadhili
zake. –(Zaburi 33:18)
173. Yeye huwaponya nafsi zao na mauti, Na kuwahuisha wakati wa
njaa. -(Zaburi 33:19)
174. basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na
23
kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu; -
(2 Petro 2:9)
175. Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli. –
(Yohana 8:36)
176. Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya; Bali mwenye
haki atatoka katika taabu. –(Mithali 12:13)
177. Maana umeniponya nafsi yangu na mauti; Je! Hukuizuia miguu
yangu isianguke? Ili nienende mbele za Mungu Katika nuru ya
walio hai. –(Zaburi 56:13)
178. Ee Bwana, rehema zako ni nyingi, Unihuishe sawasawa na
hukumu zako. –(Zaburi 119:156)
179. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, niliyewaleta mtoke katika
nchi ya Misri, ili msiwe watumwa wao; nami nimeivunja miti ya
kongwa lenu, nikawaendesha mwende sawasawa. –(Mambo ya
Walawi 26:13)
180. Kwa haki yako uniponye, uniopoe, Unitegee sikio lako,
uniokoe. –(Zaburi 71:2)
181. tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru. –
(Yohana 8:32)
182. Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza,
Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele. –(Zaburi 55:22)

183. Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.


–(Zaburi 107:6)
24
184. Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,
Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo
ya adili. –(Waebrania 1:8)
185. Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili
awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu
zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. –(1
Petro 5:6-7)
186. Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale
wawatesao ninyi; -(2 Wathesalonike 1:6)
187. na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa
kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na
malaika wa uweza wake –(2 Wathesalonike 1:7)
188. … na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata
ukamilifu wa dahari. –(Mathayo 28:20)
189. usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa
maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia,
naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. –(Isaya
41:10)
190. Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana, Mbele za uso wa
Mungu wa Yakobo. –(Zaburi 114:7)
191. Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana. -
(Zaburi 118:17)
192. Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na
25
kuwaokoa. –(Zaburi 34:7)
193. Heri amkumbukaye mnyonge; Bwana atamwokoa siku ya
taabu. –(Zaburi 41:1)
194. Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe,
Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama. –(Zaburi 4:8)
195. Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi,
na kufanywa watumwa wa Mungu, mnayo faida yenu, ndiyo
kutakaswa, na mwisho wake ni uzima wa milele. –(Warumi 6:22)
196. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Kwa maana ametenda
mambo ya ajabu. Mkono wa kuume wake mwenyewe, Mkono
wake mtakatifu umemtendea wokovu. –(Zaburi 98:1)
197. Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule
anayemtumaini. –(Zaburi 34:8)
198. Ee Bwana, usimame, umkabili, umwinamishe, Kwa upanga
wako uniokoe nafsi na mtu mbaya. –(Zaburi 17:13)
199. Ee Bwana, kwa mkono wako uniokoe na watu, Watu wa dunia
hii ambao fungu lao li katika maisha haya. Matumbo yao wayajaza
kwa hazina yako, Hushiba wana, huwaachia watoto wao akiba zao,
-(Zaburi 17:14)
200. Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa
Israeli. –(Zaburi 121:4)
201. Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa
utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha
26
hatua zangu. –(Zaburi 40:2)
202. Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa
wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na
wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. –(Matendo ya
Mitume 16:25)
203. Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu hamwi
chini ya sheria, bali chini ya neema. –(Warumi 6:14)
204. Na Wewe, Bwana, U ngao yangu pande zote, Utukufu wangu
na mwinua kichwa changu. –(Zaburi 3:3)
205. Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana
ndilo litakalosimama. -(Mithali 19:21)
206. Ngao yangu ina Mungu, Awaokoaye wanyofu wa moyo.
-(Zaburi 7:10)
207. Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu
mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda
yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa
majeshi. –(Malaki 3:11)
208. Nijapokwenda kati ya shida utanihuisha, Utanyosha mkono juu
ya hasira ya adui zangu, Na mkono wako wa kuume utaniokoa. –
(Zaburi 138:7)

27

You might also like