FX Swahili

You might also like

Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 45

Forex inasimama badala ya neno FOREIGN EXCHANGE, Ambapo unakuwa

unabadili sarafu moja toka sarafu nyingine. Mfano kama ukitoka Tanzania
unatumia TSH ukaenda Kenya ambapo wanatumia KSH itakubidi ubadilishe
sarafu yako ya kitanzania kwenda katika saafu ya kikenya. Kwa zoezi hilo
unakuwa umeshafanya FOREX.
Hapo kinachofanyika ni hiki, TSH/KSH kwamba unauza sarafu ya
kitanzania kwa kununua sarafu ya kikenya. Hili tutaliona katika platform
hii. utakutana na vitu kama USD/CHF GBP/JPY EUR/USD
Hapo kinachofanyika ni hiki, TSH/KSH kwamba unauza sarafu ya
kitanzania kwa kununua sarafu ya kikenya. Hili tutaliona katika platform
hii. utakutana na vitu kama USD/CHF GBP/JPY EUR/USD
Kubadilisha hela huku mtandaoni ni biashara ambayo inazungusha hela
nyingi kupita aina yoyote ya biashara ulimwenguni kwa siku. Kwa siku
biashara hii mzunguko wake wa hela ni zaidi ya $5 TRILLION. Wakati stock
exchange ya New York kwa siku ni $22.4billion, Tokyo ni $18.4 billion na
London ni $7.2 billion kwa siku. Na hizo ni stock exchange kubwa duniani,
hivo FOREX ONLINE ni kubwa kuliko hizi stock exchange.
Biashara hii mara ya kwanza ilikuwa ikifanywa na Institution kubwa za
kifedha kama benki kuu za nchi na mabank ya kibiashara. Lakini
kulingana na mapinduzi ya kiteknolojia hata wewe sasa unaweza kuingia
katika hii biashara kutokana kuwepo na mtu wa kati ambaye unaingia
kwenye soko kupitia yeye. Huyu anaitwa BROKER. Unafungua kaunti kwake
unaingiza kiwango cha mtaji unachotaka kuanza kufanya nacho biashara
(NB- kila broker ana kiwango chake cha chini cha wewe kuweza kuingiza
mtaji hivyo ni chaguo lako umtumie yupi)
Je, hii biashara ina muhimu wowote kwako? Jibu linategemea wewe
unahitaji nini
1. Kama unataka soko ambalo halilali.
2. Kama unataka fursa ya kufanya biashara mda wowote katika siku.
3. Kama unataka kutengeneza kiasi kikubwa cha pesa.
Basi nadhani FOREX ni mahala sahihi kwa hayo yote
NB: Kama utaweza tengeneza kiasi kikubwa cha pesa ndani ya mda mfupi,
pia unaweza kupoteza kiwango cha fedha ndani ya mda mfupi huohuo
Watu gani wanaokuwepo/wanaoshiriki katika hii biashara?
1. Benki kuu (Central banks)
2. Serikali (Government)
3. Umoja wa wawekezaji(investment coorperation)
4. Wafanyabiashara wa duniani kote(businessies worldwide)
5 Wafanyabiashara wadogo(Retail trader)
Maeneo vitovu katika hii biashara duniani ni:
1. NEW YORK (United States Dollar USD)
2. LONDON (Euro EUR and Pound GBP)
3. FRANKFURT (France franc CHF)
4. TOKYO (Japanese YEN JPY)
5. SYDNEY(Austarlian dollar AUD)
Soko la FOREX hufunguliwa jumapili saa 6 usiku na kufungwa Ijumaa saa
5:59 usiku hivo ndani ya huu mda una uwezo wa kufanya biashara

FAIDA ZA FOREX
1. Una uwezo wa kufanaya biashara sehemu yeyote ulipo
2. Unaweza kutoa faida hela zako mda wowote ndani ya siku za wiki.
3. Sheria rahisi.
4. Inapatikana masaa 24
5. Uwiano mzuri kwa kiasi kidogo unaweza ingiza faida kubwa. (Leverage)
6. Upatikanaji wa FAIDA kubwa na kwa haraka.
HASARA ZA FOREX
1. Upatikanaji wa HASARA kubwa na kwa muda mfupi.
2. Hii sio biashara ambayo kila mtu anaweza kuifanya.
Kwa miaka kadhaa mpaka sasa, kumekuwa na list kubwa ya watu
wakiingia katia hii platform ya forex na ndoto kubwa ni kupata uhurru wa
kifedha na kukua kiuchumi kutokana na hadithi/myths za kutamanishwa
kupitia mitandao au jamaa zao wa karibu.
Ahadi za kutengeneza mamilioni ya fedha ndani ya mwezi na kuacha kazi
kwa week ni vitu vinavyoongelewa sana na waliofanikiwa katika biashara
hii. kwa hio naenda kukushirikisha baadhi ya myths/hadithi kadhaa
ambazo pengine umeshazisikia au utaendelea kuzisikia sana.
Kupata mamilioni ya shillingi ndani ya mwezi mmoja na kuacha maisha ya
ufanyaji wa kazi za kila siku ni mawazo yaliyovichwani mwa watu wengi
yawezekana na wewe mmojawapo.
Sasa hapa naenda kukusimulia baadhi ya hadithi hizo ambazo zipo sana
vichwani mwetu au tunaendelea kuzisikia kupitia platform hii ya forex;
HADITHI YA KWANZA
KUWEPO KWA NJIA(STRATEGY) BORA KUPITA NYINGINE.
Watu wengi wamekuwa wakijikita kutafuta njia ambayo itawetengenezea
hela kwa 100%. Ukimuuliza mtu yeyote mpya anaejifunza forex kama kuna
siri ambayo watu waliofanikiwa katika forex wanatumia, asilimia kubwa ya
majibu yao watakwambia NDIO.
Watu wengi wanafikiri traders waliofanikiwa wanatengeneza hela kila siku
kupitia njia/strategy fulani iliyo tukufu au nzuri kushinda zote. Kitu
ambacho sio kweli.
Hata traders waliofanikiwa huwa wanapoteza 30% ya trades zao kila
mwezi. tatizo ni kuwa trades wapya wanazichukia na kuzitupa trades zao
zilizowaingizia hasara.
Lakini traders waliofanikiwa hukubari kupoteza katika siku tatu na
wanabaki na msimamo katika mpango kazi/plan kwani mara nyingi huwa
ni long term trades na hata wanavokutana na hasara mwanzoni huamini
baada ya ule mda watakuja kupata faida yao.
Hebu jaribu kufikilia jambo hili. unavozungusha sarafu kuna uwezekano
wa kuanguka upande wa mwenge au upande wa kichwa kwa uwiano sawa.
Je, ukizungusha mara 100 utapata 50 kichwa na 50 mwenge? jibu ni
hapana. Lakini kama utazungusha mara 1000 au mara 10000 kuna
uwezekano wa kupata 50 kichwa na 50 mwenge.
Hiki ndicho nachotaka kukwambia kuhusu mpango wako wa kufanya
biashara ya forex. kama njia utayochagua kutumia ina ubora wa 60% basi
ifanye mara kwa mara kufikia au kukaribia hio 60% hata kama utapata
hasara mara kadhaa, lakini mwisho wa siku uwe upande wa faida
HADITHI YA PILI
FOREX NI MCHEZO WA 50-50
Watu wengi wanaamini kuwa forex ni mchezo wa 50-50, wanafikiri kuwa
soko litaenda juu au litaenda chini tu na kusahau kuna mda soko hucheza
katika eneo fulani. (consolidation)
Kwa nadharia hio tu ya kuwepo wa soko kucheza katika eneo moja tayari
sio mchezo wa 50-50, cha kufanya ni kufanya analysis zako kwa usahihi
zaidi.
HADITHI YA TATU
UNAWEZA KUTENGENEZA HELA KWA KUCLICK TU BUTTON
Hili ni jambo tunalolisikia sana kwa wenzetu na kufanya watu wengi
waingie katika forex wakidhani ni kitu rahisi sana kwa kubonyeza tu button
unapata fedha.
Asilimia 80 ya watu wanaojiunga katika forex hupoteza mitaji yao yote
ndani ya miezi mi3 ya mwanzo kwa kukosa maarifa na kutofanya mazoezi
ya vitendo mara kwa mara katika hii biashara.
Forex ni kama fani nyingine. Inahitaji kusoma, kufanya majaribia, kuifatilia
kwa karibu na kw juhudi ndipo uje utengeneze hela. imenichukua zaidi ya
miezi 6 kujifunza kuanzia february mpaka september mpaka kuja kuanza
kutengeneza faida.
HADITHI YA NNE.
UNAHITAJI NJIA/STRATEGY YA KISASA ZAIDI ILI UTENGENEZE FEDHA
KIURAHISI.
Hii ni hadithi ambayo ipo kwa traders walio wengi, wakiamini unahitaji njia
fulani ambayo ni bora kuliko zote, indicators bora au muunganiko wa
indicators nyingi ili uwe accurate.
Hata pale unapokuja kuwapatia njia rahisi wanaona kama ni upuuzi mtupu
na kuidharau. wanaamini njia iliyocomplicated ni njia bora kuupita zote.
lakini kiuhalisia traders wengi waliofanikiwa wanatrade kwa njia rahisi
sana na wengine hawatumii kabisa hata indicators.
Lakini nataka kukambia ubora wa strategy upo mikononi mwa mtu husika
atakaemake commitment na hio strategy. unaweza kuwapa watu wawili
strategy moja kisha mmoja akachoma akaunti na mwingine akafanikiwa
kupitia hio strategy.
Hii ni kwa sababu kila mtu anatrade na kuona vitu tofauti. kwa hio sio njia
gani ni nzuri bali ni jinsi gani utaichukua hio njia na kuiwekea mkazo
ndipo utakapofanikiwa.
2. AINA YA WAFANYABIASHARA KATIKA FOREX.
Hii ni eneo muhimu sana kulijua na wewe kufanya maamuzi unataka uwe
mfanyabiashara wa aina gani. Hivyo kabla hujaanza ni bora kujitathmini
wewe ni mfanyabiashara wa aina gani na utumie njia zipi katika kufanya
biashara yako.
1. SCALPER
Huyu ni mfanyabiashara anaekuwa katika soko kwa mda mfupi sana. Mara
nyingi anaingia na kutoka katika trade na dakika kadhaa tu. Kivutia
kikubwa kwa trader wa aina hii huona faida au hasara ndani ya mda mfupi
tu. Msingi mkubwa wa scalper ni kuwa na uwezo wa kufikiri haraka na
kuweza kumantain pressure. Kulingana na mda mfupi wa fursa scalper
huamua aingie katika hio fursa au aache.
2. DAY TRADER
Huyu ni trader ni yule ambae huingia katika trade siku husika na kutoka
katika trade siku hio hio.Tofauti na scalper, yeye huingia katika trade na
kuisubiri ndani ya dakika 30 au saa. Uzuri wa kuwa day trader ni mda wa
kutosha wa kufanya zako analysis. mara nyingi huwa na mda maalum wa
kuingia katika trades zake. Na mda ukifika wanasubiri fursa ijitengeneze
na kuingiza trades zao, hutumia dakika 30, saa moja mpaka saa 4
timeframe kufanya analysis zao.
3. SWING TRADER
hawa ni traders wanaofanya biashara kila siku.... kwa kua kila siku
kunakuwa na nafasi za mtiririko/swings katika soko. ukitokea mtririko wa
kupanda wanapanda nao.. ukitokea wa kushuka wanashuka nao. Hawa
wanafocus sana katika kuangalia mtiririko wenye asili ya uimara zaidi. na
mara nyingi hutokea katika kufunguliwa kwa soko la london (London open)
na New York open.Hawa wanafanana sana na day trader huwa wanaingia
na kutoka katika soko ndani ya siku husika
4. POSITION TRADER
Hawa huingia katika trade kwa siku kadhaa au week. Hii ni aina nzuri kwa
wale ambao hawana mda wa kuangalia chart kila siku.
Hawa pia tunaambiwa ni traders ambao wanachukua profit sana
ukizingatia wanakua kwenye market kwa mda mrefu hivo kuchukua faida
ya week au mwezi. Hivyo aina hii ni kwa wale wenye mitaji mikubwa

3.MISAMIATI KATIKA BIASHARA YA FOREX


Kuna misamiati mbalimbali ambayo tutakuwa/utakutana nayo katika hii
biashara ya FX. Misamiati hii kama utaweza kuielewa vizuri basi nina
hakika kutakuwa hakuna shaka ya wewe kuwa katika soko.
1. BASE CURRENCY
Hiki ni kiini msingi katika kununua au kuuza katika forex. kama utabuy
USD/JPY Hii ni kumaanisha unanunua dola ya kimarekani na wakati
huohuo unauza yen ya kijapani.
2. QUOTE CURRENCY
Hii ni ile sarafu ya pili katika pair ya sarafu husika unapofanya trade.
Mfano USD/JPY, JPY ndio quote currency.
3. LONG/BULLISH
Hii ni termonology ambayo unasikia watu wakiiongelea. kama imepatikana
opportunity ya kulong/bullish hapa maana yake NUNUA. Bull ni aina za
mnyama ambae anakula majani hivo candlestick zake nyingi zinakuwa
zikiwakilishwa na rangi ya kijani. Huyu mnyama akitaka kukudhuru
huinamisha kichwa chini na anakunyanyua kwa kukuchota kukupeleka juu.
Hivyo katika Forex hapa inamaanisha soko linatoka chini linapanda juu.
4. SHORT/BEARISH
Kama imepatikana opportunity ya kushort/bearish hapa maana yake UZA..
Bear ni aina ya mnyama ambae anakula nyama, hivo candlestick yake
huwakilishwa na rangi nyekundu. Huyu mnyama anavyokudhuru huruka
juu kisha hukushusha chini. Hii katika forex inamaanisha soko linatoka
juu kushuka chini.
5. PIP (PERCENTAGE IN POINT)
Hiki i kiasi cha thamani kinachocheza kulingana na mzunguko wa sarafu
husika katika biashara. Huanza kuhesabiwa kutoka desimali ya nne katika
pair mfano thamani ya USD/CHF ni 1.1379, thamani hii ikimove toka
1.13*79* mpaka 1.13*80* hapo inakuwa ni 1 pip
Isipokuwa kwa pair inazohusisha sarafu ya YEN nafasi za decimal zitakuwa
tatu na sio nne kama pair nyingine. Mfano USD/JPY=1.137 hivo pip
unaanza kuhesabu kwenye 7
6. LOT SIZE
Hii ni thamani inayotumika kugundua faida au hasara.
standard lot size 1.00=$10 kwa pip moja
min lot size 0.10=$1 kwa pip moja
micro lot size 0.01=10 cent kwa pip moja

7. TAKE PROFIT (TP)


Hili ni eneo ambalo utaamua kutoka nje ya soko baada ya faida. Eneo
ambalo utaona faida uliyopata inakutosha au ni eneo ambali price inaweza
kugeuka na kukuingizia hasara.
Unapoingia kwenye soko analysis zako zinakuonesha sarafu
itapanda/kushuka mpaka eneo Fulani then baada ya hapo itageuka trends
Ila haujui itachukua mda gani mpaka kufika katika hio price. Sasa huwezi
kukaa kwenye screen yako mda wote kuisubiri hio point. Unachokifanya
unaset kwamba price ikifika katika hilo eneo trade yake ijifunge
automatically kisha ww ukirudi au ukimaliza mambo yako kama itakuwa
ilifika katika hio point uje ukutane na profit yako. Hapo ndo panaitwa TAKE
PROFIT.
8. STOP LOSS(SL)
Hili ni eneo ambalo utaamua kutoka nje kwa hasara either kwa kuona
analysis yako ilikuw na makosa au unaamini upande wa hasara uliopo
utaongezeka zaidi hivyo badala ya kupata hasara kubwa unaamua
kuchukua hasara kidogo. Wanasema kama hutakubali hasara basi jiandae
kupokea mama wa hasara kwa lazima.
Kwenye market ukishafanya analysis unaona kuna fursa ya kupanda kwa
sarafu hivo unaamua kuinunua ikiwa chini ili ikifika juu uiuze na ile tofauti
ya bei ulonunua na utakayokuja kuuza ndo inakuwa faida Na wewe uliingia
sokoni kwa hio currency labda, Sasa baada ya kufanya hio analysis
inatokea news mfano ya kushuka kwa ajira mfano marekani So kwa namna
yoyote currency baada ya kupanda itashuka... Maana itakuwa weak.Sasa
unakuta na wewe ulishaingia so unagundua itashuka sana hivo unaamua
kutoka katika soko katika hasara ndogo ili usipate hasara zaidi kwani
haujui hio currency itashuka mpaka wapi. Hio ndo inaitwa STOP LOSS
4.AINA ZA ODA KATIKA SOKO
Kuna aina mbalimbali katika soko ambazo unaweza kuzitumia katika
kuingiza trade yako. Hapa nimekuandalia aina tatu tu za msingi japo zipo
zaidi ya hizo
1. MARKET ORDER
Hii ni pale unapogundua tu katika soko kuna fursa ya kuuza/kununa kisha
unabonyeza kitufe cha kununa/kuuza wakati huo na kuingia katika soko.
2. BUY STOP
Ukifanya analysis katika soko utagundua kuna fursa fulani inatokea katika
soko. Au imeonesha dalili za kutokea. Lakini sio mda wote utakuwa katika
kioo chako cha kompyuta. Hivo unaweka pending order ya kununua kama
price itafika eneo fulani. Hivo utaweza kuendelea na shughuli zako kisha
price ikifika pale itajinunua na kukuingiza kwenye market.
3. SELL STOP.
Kama maelezo yalivyo katika buy stop hii pia ni hivyo hivyo.. isipokuwa
hapa unaweka oda kama price itashuka basi ijiuze na kukuingiza kwenye
market ikifika point fulaniii.
5.AINA ZA KUFANYA BIASHARA.
Katika forex kuna aina tatu za kufanya biashara, hapa nitazielezea mbili za
msingi ambazo wewe ungependa kuchagua ni ipi itakuwa nzuri kwako.
Japo mimi ningependekeza mtumie aina yangu ambayo kiupande wangu
nimeiona anaweza kumudu mtu yeyote. Siwaaminishi kwamba ni rahisi
lakini nina imani mtu yeyote anaweza kuimudu.
1. Fundamental Analysis
Huu ni ufanyaji wa biashara kwa kuliangalia soko kulingana na shughuli
za kiuchumi,kisiasa na kijamii ambazo hupelekea kuleta madhara katika
suala zima la demand and supply
2. Technical Analysis
Ni somo ya kucheza kwa thamani ya sarafu, kwa lugha nyingine hii ni sawa
na chati.
Katika fundamental kikubwa kinachoangaliwa ni news lakini katika
technical analysis kinachoangaliwa ni historia ya price ilifanya nini na
huwa ina tabia ya kufanya nini. hivyo NEWS pekee ndio kitu ambacho
hakiheshimu chart kwani pindi inavotokea haifuati kanuni za chart.
Hapa chini nimekuwekea NEWS zenye madhara makubwa pia.

6.AINA 11 MUHIMU ZA CANDLESTICK PATTERN


Kuna candlestick 11 za muhimu ambazo tunaziita CANDLESTICK PATTERN,
Candles hizi ni kiashiria kikubwa sana cha kufanya entry kama zitatokea
maeneo ya SUPPORT na RESISTANCE.
1. DOJI.
Hii hutokea pale ambapo bei ya kuuza na kufungua imekuwa ni moja.
Tazama picha hapo chini na maelezo yake.

2. ENGULFING.
Hii hutokea pale ambapo candle ya pili imeizidi umbo na pin candlestick ya
nyuma katika eneo la RESISTANCE au SUPPORT. Tazama picha hapo chini
na maelezo yake.
3. HARAMI.
Hii hutokea ambapo candle ya kwanza imezidi umbo na candle inayofuata
mbele yake. Tazama picha hapo chini na maelezo yake

4. DARK CLOUD COVER.


Hii ni pattern ambayo huashiria kugeuka kwa soko kwenda kuuza mara
inapokuwa imetokea kwenye RESISTANCE. Tazama picha hapo chini na
maelezo yake
5. PIERCING.
Hii ni pattern ambayo huashiria kugeuka kwa soko kwenda kununua mara
inapokuwa imetokea katika SUPPORT. Tazama picha hapo chini na maelezo
yake

6. SHOOTING STAR.
Hii ni candle inayokuwa peke yake inayoashiria kugeuka soko kwenda
kuuza, hutokea eneo la RESISTANCE. Tazama picha hapo chini na maelezo
yake
7. INVERTED HAMMER.
Hii pia ni candle inayokuwa peke yake inayoashiria kugeuka kwa soko
kwenda kununua inapokuwa imetokea/imejitengeneza eneo la SUPPORT.
Tazama picha hapo chini na maelezo yake

8. HAMMER.
Hii ni candle inayokuwa peke yake ikiashiria kugeuka kwa soko kwenda
kuuza inapokuwa imetokea katika eneo la RESISTANCE. Tazama picha hapo
chini na maelezo yake
9. HANGING MAN.
Hii ni candle inayokuwa peke yake ikiashiria kugeuka kwa soko kwenda
kuuza inapokuwa imetokea katika eneo la RESISTANCE. Tazama picha hapo
chini na maelezo yake

10. RAILWAY TRACK


Hii pattern hujumuisha candle mbili ambazo zinakuwa na maumbo
sawa/yaliyolingana katika maeneo ya RESISTANCE na SUPPORT. Tazama
picha hapo chini na maelezo yake
11. SPINING TOP.
Hii ni candle moja ambayo inakuwa ina umbo dogo la pin ndefu juu na
chini. Ikitokea katikati ya eneo la RESISTANCE na SUPPORT huashiria
kuendelea kwa trends, na kama ikitokea eneo la RESISTANCE au SUPPORT
huashiria kugeuka kwa soko. Tazama picha hapo chini na maelezo yake
7. SUPPORT AND RESISTANCE
SUPPORT: Hii ni point ya chini ambapo bei hufika na kugeuza.
RESISTANCE: Hii ni pointi ya juu ambayo bei hufikia na kugeuza.
Mfano: sakafu katika nyumba yako ni support na dari katika nyumba yako
tuichukulie kama resistance.
Haya maeneo ya support na resistance tunayaita kwa jina moja la ZONE.
YAFUATAYO NI MAMBO MUHIMU KUHUSU ZONE
1. Zones ni eneo na sio pointi ya bei.
2. Zones ni madoa katika chati ambapo bei inageuka mara nyingi
3. Zones yaweza kuwa juu au chini kulikokithiri katika chart
4. Zones ni sehemu ambazo wafanyabiashara wa chati tupu(naked traders)
hutafuta fursa za kuingia sokoni
5. Zones za support na resistance zinahitajika kurekebishwa mara kwa
mara.
6. Chati ya mistari husaidia naked traders kuweka Zones.
7. Support iliyotobolewa hugeuka kuwa Resistance na Resistance
iliyotobolewa hugeuka kuwa Support
JE, NI KWA NAMNA GANI UNAWEZA KUTAFUTA ZONES ZA SUPPORT AND
RESISTANCE?
1. Tumia chart kubwa kutafuta Zones zenye nguvu(Major zone), Kama
unatrade kwa chati ya saa moja basi tumia chati ya siku au week.
2. Tumia chati ya mistari kutafuta zones.
3. Usitilie maanani zones hafifu(minor zones)
CHANEL
Hii ni njia ambayo bei huifua ta na hujenga kingo ambapo bei haivuki
hapo.
Kuna aina 3 za chaneli hizi.
1. UPTREND CHANELI/CHANELI YA KUPANDA
2. DOWNTREND CHANELI/CHANELI YA KUSHUKA
3. SIDEWAY CHANEL/CHANELI MSAMBAMBA
TREND.
Hii ni pale ambapo bei ya sarafu Fulani inapanda juu, inashuka chini au
inacheza katika eneo Fulani(sonsolidation).
Hivyo bei inavyopanda juu inaitwa UPTREND.
Muda ambapo kunakuwa na UPTREND bei huenda JUU JUU (HIGHER HIGH)
NA JUU CHINI (HIGH LOW)
Bei inavyoshuka chini inaitwa DOWNTREND.
Huu ni muda ambapo bei inapungua kwa mtindo wa CHINI CHINI (LOWER
LOW) na CHINI JUU (LOWER HIGH)
Na pale bei inavocheza ndani ya eneo Fulani inaitwa SIDEWAY
TREND/CONSOLIDATION/LAMB/RANGING.
REVERSAL
Hii ni sehemu ambayo hutumika kuelezea sehemu ambapo TREND ya aina
moja hugeuka kuelekea aina nyingine ya TREND. Mfano bei ikiwa inapanda,
ikifika sehemu ikagoma kupanda na kugeuka basi kitendo hiko ndicho
tunaita REVERSAL.

Je REVERSAL hutokea wapi?


1. Eneo la Support.
2. Eneo la Resistance.
CONTINUATION.
Huu ni msamiati unaotumika kuelezea kuwa bei inaendelea na Trend yake
lakini kwa viashiria maalum kama kusita katika eneo Fulani au kurudi
nyuma kidogo kabla haijandelea.
Mfano
1. Kwenye downtrend ikaconsolidate then ikaendelea na kushuka.
2. Kwenye downtrend ikapanda juu kasha ikaendelea tena kushuka.
MARKET SWINGS.
Hii ni pale ambapo market ya inapanda na kushuka bila kujali hio trends
ni ya kushuka au ya kupanda. Pale unapoona price imepanda ile inaitwa
UP SWINGS, Na pale price imeshuka tunaita DOWN SWING. SWING hutokea
katika trends zote, Kwani soko limekaa kwa mtindo wa wave. Linapanda na
kushuka bila kujali trends ni ya wapi kinachotofautiana ni kuwa haishuki
na kupanda kwa kiwango sawa.
TRENDLINES
Hii ni mistari ambayo huchorwa kukutanisha vilele ambavyo
vimetengenezwa na UPSWINGS, au mashimo yaliotengenezwa na
DOWNSWINGS, Kukusaidia kujua hio trends inaenda wapi.
Unahitaji kimo cha chini cha vilele viwili ili kugundua DOWNTREND. Na
unahitaji kima cha chini cha mashimo mawili ili kugundua UPTREND.

Je nini kinamaanisha kama TRENDLINES mbili zikakutana.


Hii humaanisha kuwa trends moja imeisha hivo inafuata trends nyinigine.
THE LAST KISS.
Wafanyabiashara wanapoona bei haipandi juu wala kushuka chini zaidi,
hutambua kuwa bei iinaconsolidate na hakuna anaejua itaenda wapi. Hivyo
huchora box katika lile eneo ili endapo bei ikitoboa upande wowote
wanajua ndipo price inaelekea. Lakini bei inaweza ikatoka ndani ya hilo
eneo la consolidation lakini kumbe ikawa ni BREAKOUT. Matokeo yake
unafanya entry kasha price inageuka na kurudi tofauti na CALL yako.
LAST KISS inakuwa ni break out ambayo inatuhakikishia sasa TREND
inaenda upande sahihi. Baada ya price kutoka katika lile eneo ambalo
umelitenga halafu unaona inarudi tena usawa wa lile eneo kwa kuonesha
inaingia lakini CANDLESICK inafunga kwa kuona ni WICK imeingia katika
eneo lile kasha Price imefunga nje ya eneo la consolidation basi hiko ni
kiashiria cha kuwa huo upande ambao imeenda ndipo price itaelekea. Kwa
lugha rahisi ni pale price ikitoka katika eneo la consolidation kisha ikarudi
kugusa lile eneo bila kuingia (RETEST) hio ndio LAST KISS. Sio kila
BREAKOUTS katika eneo la consolidation ni LAST KISS lakini kila LAST KISS
ni BREAKOUTS.
BIG SHADOW
Nadharia ya kivuli kikubwa inazungumziwa kama pindi uonapo kivuli
kikubwa basi kuna mwanga unaosababisha kivuli hicho. Kama umekuwa
mfuatiliaji wa chart utakuwa ushawahi kuona kuna CANDLESTICK ni ndefu
sana na hakuna NEWS au Factor yeyote kubwa. Hii pia lazima itokee katika
eneo la RESISTANCE na SUPPORT. Na inarefer kama REVERSAL. Baadhi ya
watu wanaweza kuifananisha hii na ENGULFING, Lakini nataka kukwambia
hii ni zaidi ya ENGULFING.
Ikitokea katika RESISTANCE tunaiita BEARISH BIG SHADOW.
Ikitokea katika eneo la SUPPORT inaitwa BULLISH BIG SHADOW.
Pale ambapo zikajitengeneza candle mbili zilizofuata hio inaitwa BIG
SHADOW PATTERN.
SHERIA ZA BIG SHADOW.
1. Huu ni muundo wa CANDLESTICK mbili.
2. Candlestick ya pili katika kuundwa huku ndio tunayoiita BIG SHADOW
CANDLESTICK.
3. BIG SHADOW CANDLESTICK lazima iwe kubwa kwa urefu wa juu na chini
kuliko candlestick iliopita
4. BIG SHADOW lazima itokee kwenye ukanda wa SUPPORT na RESISTANCE.
5. BIG SHADOW hutokea kwa kwenda juu na chini kulikokithiri.
6. BEARISH BIG SHADOW CANDLESTICK hujifunga chini ya candle ya nyuma
yake.
7. BULISH BIG SHADOW CANDLESTICK hujifunga juu ya candle ya nyuma.
8. Kwa BULISH BIG SHADOW, Stop loss huwekwa pips chache chini ya ile
BULLISH BIG-SHADOW CANDLESTICK
9. Kwa BEARISH BIG-SHADOW, Stop loss huwekwa pips chache juu ya ile
BEARISH BIG-SHADOW CANDLLESTIICK

You might also like