Professional Documents
Culture Documents
Kilimo Bora Cha Nyanya PDF
Kilimo Bora Cha Nyanya PDF
MAGONJWA NA WADUDU
Utangulizi
Nyanya ni zao la chakula na biashara. Kilimo cha zao hili hufanyika majira yote
(masika na kiangazi), na faida hupatikana haraka na ni ya kuridhisha ikilinganishwa
na mazao mengine. Pamoja na umuhimu wa zao hili, wadudu waharibifu na
magonjwa huathiri uzalishaji na ubora wa matunda. Ili mkulima aweze kupata faida
na kuongeza pato la kaya yake ni vema kuzingatia udhibiti wa magonjwa na wadudu
wa zao hili. Kipeperushi hiki kinatoa maelezo ya udhibiti wa magonjwa na wadudu
muhimu ya zao la Nyanya.
MAGONJWA YA NYANYA
Udhibiti
• Nyunyiza dawa ya kuzuia ukungu hasa wakati wa masika, Dawa
zinazopendekezwa ni Ridomil, Dithane 45, Bravo, Funguran, milraz.
• Fanya mzunguko wa mazao. Usipande nyanya sehemu moja kila msimu au
palipolimwa mazao jamii ya nyanya km viazi mviringo, bilinganya, aina zote
za pilipili na nyanya chungu.
• Tumia mbegu safi
• Panda aina za nyanya zinazovumilia ugomjwa
Udhibiti
• Nyunyiza dawa ya Kocide, Funguran
• Teketeza mabaka ya mazao baada ya kuvuna
• Tumia mbegu safi na bora
Udhibiti
• Tumia mbegu safi na bora
• Tumia mzunguko wa mazao. Nyanya zisizungushwe na mazao jamii yake
• Teketeza masalia ya mimea
• Choma kitalu cha nyanya kabla ya kusia mbegu
Mnyauko bacteria (Bacterial wilt)
Ugonjwa husababishwa na vimelea vya bacteria vinavyoishi kwenye udongo.
Huenezwa na kusambazwa na mbegu na udongo wenye vimelea. Mirija ya mimea ya
kupitishia maji na chakula hushambulia na mimea hunyauka ghafla. Mmea hukauka
na kufa.
Udhibiti
• Panda mbegu safi
• Panda nyanya sehemu ambayo haijawahi kupandwa viazi mviringo,
bilinganya au nyanya chungu
• Tumia mzunguko wa mazao
• Hakikisha mfereji wa maji ya kumwagilia hayapiti kwenye shamba lenye
historia ya ugonjwa huu.
• Choma kitalu cha nyanya kabla ya kusia mbegu
Udhibiti
• Tumia mzunguko wa mazao usiopungua miaka mine
• Ondoa mabaki ya nyanya shambani
• Tumia mbegu bora na safi
Udhibiti
• Panda mbegu bora na safi
• Tumia mzunguko wa mazao
• Teketeza masalia ya mazao
• Nyunyizia dawa ya funguran, Kocide101, Cobox, Bravo
Udhibiti
• Tumia mbegu bora na safi
• Teketeza masalia ya mazao
• Tumia mzunguko wa mazao
2
Rasta (Yellow leaf curl)
Ugonjwa huu husababishwa na virusi na huenezwa na nzi wadogo weupe. Hutokea
zaidi wakati wa kiangazi. Mimea hudumaa na majani yaliyoshambuliwa huwa na
rangi ya manjano na pengine rangi ya zambarau. Nyanya hupasuka.
Udhibiti
• Nyunyiza dawa za sumu za kuua wadudu (Selecron, Dursburn, Actelic)
• Ng’oa mimea yenye ugonjwa
• Tumia mzunguko wa mazao
• Weka shamba katika hali ya usafi
Udhibiti
• Tumia mbegu bora na safi
• Ng’oa mimea iliyoshambuliwa
• Teketeza masalia ya mazao
• Weka shamba katika hali ya usafi
WADUDU WAHARIBIFU
Udhibiti
Nyunyizia dawa ya kuua wadudu. Dawa hizo ni pamoja na Actelic 50EC, Selectron,
Dursbaan, Maji ya majani ya mwarobaini au utupa pia huua wadudu.
Udhibiti
• Nyunyizia dawa za sumu. Dawa hizo ni pamoja na Actellic, Selecron,
Dursbarn na Thionex
• Mwagilia maji mara kwa mara
• Weka shamba katika hali ya usafi
3
Udhibiti
Nyunyizia dawa za sumu za kuulia wadudu kama Selecron, Actellic, Dursban na
thionex. Pia maji ya majani ya mwarobaini na utupa.
Udhibiti
Nyunyizia dawa za sumu za kuulia wadudu kama Rogor, Actellic, Selecron, Dursban
maji ya majani ya mwarobaini na utupa, maji ya pilipili.
Minyoo (Nematodes)
Ni minyoo midogomidogo ambayo hushambulia mizizi na kuweka vifundo. Mizizi
hushindwa kuchukua maji na chakula kwenye udongo. Mimea hudumaa na
kushindwa kuzaa
Udhibiti
• Tumia mzunguko wa mazao
• Choma udongo wa kitalu kabla ya kusia mbegu kwa kutumia karatasi la
plastiki jeusi na nishati ya jua
• Choma masalia ya mazao
Sota (Cutworms)
Udhibiti
• Nyunyiza dawa za kuua wadudu kwenye shina usawa wa udongo
• Hakikisha miche inapata maji ya kutosha.
Kimetolewa na:
4
5