Professional Documents
Culture Documents
Final Katiba Ya Kikundi Cha Ujirani Mwema
Final Katiba Ya Kikundi Cha Ujirani Mwema
1
KATIBA YA KIKUNDI CHA UJIRANI MWEMA TARAKWA.
UTANGULIZI:
(UJIRANI MWEMA TARAKWA) - Ni kikundi cha hiari chenye lengo la kusaidiana katika shida na raha pia kufanya
shughuli mbalimbali za kijamii kwa ustawi wa wanachama wake. Kikundi hiki kimeanzishwa rasmi tarehe 02/08/2020
Kwa pamoja wanachama wanaahidi kuilinda na kuitekeleza katiba hii.
Pamoja na Katiba hii, Kikundi hiki kitaendeshwa kwa mujibu wa kanuni mbalimbali ambazo zitawekwa na wanachama.
SURA YA KWANZA
1.2 Tafsiri
Kwa mujibu wa Katiba hii, maneno yafuatayo yatakuwa na maana ifuatayo;
i) Mwanachama: Mtu yeyote atakayekidhi vigezo vya kuwa mwanachama
ii) Mwanachama hai : Mwanachama anayetimiza masharti ya kuwa mwanachama kwa mujibu wa katiba hii.
iii) Kanuni: Muongozo wa jinsi ya uendendeshaji wa kikundi
iv) Kikundi: Taasisi hii inayoanzishwa kwa mujibu wa katiba ambayo inatambulika kuwa ni UJIRANI MWEMA
TARAKWA.
v) Matatizo:Ina maana ya misiba, na ugonjwa wa muda mrefu kwa mujibu wa katiba hii.
vi) Nidhamu: Kitendo chochote kile kinacho kinzana na Katiba hii pamoja na kanuni zake.
SURA YA PILI
2.1 Aina ya Kikundi
UJIRANI MWEMA TARAKWA ni Kikundi cha Kijamii cha kusaidiana katika shida na raha pamoja na maendeleo ya
Kiuchumi na elimu.
2.2 Madhumuni na Malengo ya Kikundi.
2
Kikundi hiki kipo kwa kutimiza au kutekeleza yafuatayo:-
i) Kuanzisha mfuko wa kikundi wa kuweka na kukopa.
ii) Kushirikiana na kusaidiana nyakati za shida na raha kama misiba, magonjwa ya muda mrefu na sherehe.
iii) Wanakikundi kuwezeshana katika kuimarisha hali zao za Kipato ili kuweza kuwa na maisha yaliyo bora zaidi.
iv) Kuanzisha miradi mbalimbali ya kukuza mfuko wa kikundi pale kikundi kitakapokuwa kikubwa na fedha za kutosha.
2.3. Matarajio ya Kikundi
Ili kuweza kufikia matarajio ya Kikundi kitafanya yafuatayo:-
i) Kuweka utaratibu mahsusi MICHANGO YA FEDHA kwa wanakikundi ikiwa ndio msingi wa chanzo cha mapato.
ii) Kubuni Miradi mbalimbali itakayosimamiwa na kuendeshwa Wanakikundi wenyewe au hata kwa msaada wa kiufundi
kutoka nje ya kikundi.
iii) Kuimarisha ushirikiano na wanakikundi wenye changamoto mbalimbali kama vile; Maradhi, Misiba,Harusi, Elimu na
Sherehe, Majanga ya Kiasili na matukio mengine yanayolingana na hayo.
iv) Taratibu hizo zitakuwa ni sehemu ya Katiba hii.
SURA YA TATU
3.0 UANACHAMA.
Ni mtu yeyote yule ambaye ametimiza taratibu zote za kujiunga na Kikundi au Umoja huu kwa mujibu wa Katiba na
Kanuni zake ikiwa ni pamoja na kulipa ada na Michango stahiki.
3.2.1 Sifa za kuwa Mwanachama
i) Awe na Umri usiopungua miaka 18.
ii) Awe mwenye nia na awe tayari kuwa mwanachama
iii) Awe tayari kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kikundi
iv) Awe na akili timamu.
v) Awe tayari kutii na kufuata masharti ambayo yameainishwa kwenye Katiba na Kanuni za kikundi
vi) Awe tayari kulipa kiingilio, adhabu pale ambapo ataenda kinyume na taratibu, michango itakayo ainishwa
kwenye kanuni ya ada, michango na adhabu pamoja na ada ya uanachama ya kila mwezi
vii) Awe anaishi kata ya Tarakwa au maeneo ya karibu ya Tarakwa pamoja na yeyote ambaye ana nia ya kuwa
mwanachama na ananidhamu ya kuwa mwanachama ila haishi maeneo ya Tarakwa.
3.3.1 Haki za Mwanachama
3
i) Kutoa maoni yake kwa uhuru
ii) Kuchagua au kuchaguliwa katika nafasi yoyote ile ya Uongozi katika Kikundi au Umoja huu.
iii) Kuwasiliana na Uongozi/Viongozi ikiwa ni pamoja na kupokea na kutoa taarifa zinazohusu Kikundi au Umoja
huu.
iv) Kuhudhuria na/au kuwakilisha katika jambo lolote lile linalohusu Kikundi au Umoja huu kwa kufuata taratibu na
kanuni zilizowekwa kwa mujibu wa Katiba hii.
v) Kupewa nafasi ya kujieleza na kujitetea pindi anapokabiliwa na tuhuma zozote zile dhidi yake katika umoja
huu.
vi) Kutumia Mali za Kikundi kwa kufuata utaratibu na Kanuni za Umoja huu.
vii) Ana haki ya kutoa hoja yake na kusikilizwa wakati wa kushiriki majadiliano kwenye vikao.
viii) Kufahamu mapato na matumizi ya Kikundi kwa kutumia na kuzingatia Kanuni.
ix) Kusaidiwa linapomtokea tatizo.
x) Kusaidiwa kimawazo au kiuchumi kulingana na hali itakavyo ruhusu.
3.3.2 Wajibu wa Mwanachama.
i) Kuilinda na kuitetea katiba hii wakati wote.
ii) Kutekeleza majukumu atakayopewa na viongozi au wanachama wenzake.
iii) Kushiriki katika shughuli zote za kikundi kwa mujibu wa katiba hii ikiwa ni pamoja na vikao halali vya Umoja
huu.
iv) Kulipa ada pamoja na michango mbalimbali itakayo pitishwa na Kikundi au Umoja huu.
v) Kueneza sifa nzuri za Umoja huu.
vi) Kutii na kufuata maagizo na maazimio ya Mkutano/Mikutano halali ya Umoja huu, hata ikiwa hatakuwepo
kwenye Mkutano huo, au hakushiriki katika kupitisha azimio hilo.
vii) Kuwa na nidhamu wakati wa Mikutano ama shughuli nyingine zozote za Kikundi.
viii) Kutunza siri zote za Umoja huu
3.4.1 Kujiunga na Kikundi.
a) Kujaza Fomu ya maombi itakayotolewa kwa ada itakayokuwa imepangwa.Maombi haya ni lazima yapitiwe na
kukubaliwa na Uongozi.
b) Baada ya kukubaliwa Mwombaji atatakiwa kulipa Ada ya kiingilio cha kiasi kitakachokuwa kimepangwa na
Mkutano Mkuu.
c) Pamoja na Ada ya kiingilio Mwanachama mpya atalazimika kulipa Michango ambayo itahainishwa kwenye
kanuni.
3.4.2 Michango
(a) Ada ya Uanachama
4
Kila Mwanachama atalazimika kulipa ada ya Uanachama kama ilivyoainishwa katika Ibara ya 3.4.1.(b) na (c) ya Katiba
hii.
Kiasi atakacho lipa mwanachama mpya ambaye alikuwa hana taarifa kabisa ya uanzilishi wa kikundi hiki, kitahainishwa
kwenye kanuni za ada ana michango.
(b) Michango Mingine.
Kila Mwanachama atawajibika kuwasilisha mchango mwingine wowote ule utakaoamuliwa kuchangishwa kwa azma
ya kukidhi miongoni mwa matarajio ya Umoja huu kama yalivyoainishwa katika ibara 2.3 ya Katiba hii na kima
kitakachokuwa kimeamuliwa.
( d) Adhabu
Mwanachama akichelewa kikao baada ya mwenyekiti kufungua kikao atapaswa kulipa adhabu, ambayo itaainishwa
kwenye kanuni ya ada, michango na adhabu.
Atalipa adhabu hiyo kwa muda wa vikao vitatu mfululizo kama atashindwa kufika kwenye vikao ivyo mfululizo, baada
yah apo kiasi kikubwa zaidi kitatozwa dhidi yake, kiasi hicho kitahainishwa kwenye kanuni ya ada, michango na
adhabu.
(e ) Ugonjwa
Michango kwa ajili ya ugonjwa itachangwa kutokana na taratibu zitakazo hainishwa kwenye kanuni ya ada,michango
na adhabu.
(f ) Sherehe
Aina ya sherehe inayopaswa kuchangiwa, kiwango cha kuchangia, wanaopaswa kuchangiwa yatahainishwa kwenye
kanuni ya ada, michango na adhabu.
3.4.3 Kukoma Uanachama.
5
iv) Kushindwa kulipia ada ya kila mwezi kwa miezi mitatu mfululizo bila sababu yoyote ya msingi.
v) Kupuuza taarifa zinazotaka ushiriki wake katika shughuli za wanachama.
vi) Kupoteza sifa kutokana na mambo ya kinidhamu
vii) Ikiwa mwanachama atafariki.
viii) Kushidwa kufuata Katiba na Kanuni za Kikundi.
SURA YA NNE.
4.0 UONGOZI.
4.2 Muda wa kikomo cha uongozi kwa viongozi wote itakuwa ni miaka miwili, baada ya hapo viongozi wapya
watachaguliwa katika kikao cha halmashauri kuu. Kiongozi wa zamani anaweza kuchaguliwa tena upya kwa kipindi
kindine, ila hatapaswa kuchaguliwa kwa zaidi ya awamu mbili.
4.3 Endapo kiongozo ataonesha utovu wa nidhamu kama matumizi amabaya ya fedha za chama, ugombanishi, kuwa
chanzo cha migogoro ambayo itahatarisha uhai wa chama au kuivunja katiba hii kwa makusudi au kwa kutokukusudia,
Kamati ya nidhamu itashughulika na swala hilo ikiwa pamoja na kumuita kiongozi huyo na kumuhoji, endapo
itadhibitika maswala aliyo yafanya kiongozi huyo ni kweli basi mapendekezo ya kumfukuza yatatolewa na kamati ya
nidhamu kwa wanachama. Wanachama watatoa maamuzi ya adhabu hiyo.
6
2. Makamu Mwenyekiti
3. Katibu
4. Katibu Msaidizi
5. Mweka Hazina
6. Wajumbe wawili watakaochaguliwa na Mkutano Mkuu.
SURA YA TANO.
5.0 KAZI ZA VIONGOZI
5.1 Kazi za Mwenyekiti.
i) Atakuwa msemaji mkuu wa kikundi.
7
ii) Ataitisha mikutano yote ya kikundi.
iii) Ataitisha mkutano wa dharura pale itakapokuwa inahitajika.
iv) Ataongoza mikutano yote ya wanachama wote.
v) Atakuwa ndio Kiongozi Mkuu wa Kikundi au Umoja huu.
vi) Atakuwa mtuia sahihi kwenye akaunti ya benki
5.3 Kazi za Katibu.
i) Atakuwa Mtendaji Mkuu wa kikundi.
ii) Kuandaa ajenda za vikao vyote.
iii) Ataandika miniti za vikao vyote vya kikundi.
iv) Atakuwa anatoa taarifa ya maendeleo ya kikundi mara moja kwa mwezi
v) Kwa kushirikiana na Mwenyekiti atakuwa anaandaa yatokanayo na vikao vilivyopita
vi) Atakuwa mtunza kumbukumbu na nyaraka mbalimbali za kikundi.
vii) Atakuwa katibu wa kamati ya utendaji.
viii) Atakuwa mjumbe wa kamati ya Fedha na Mipango.
ix) Atawajulisha wanachama taarifa zote za vikao.
x) Atafanya kazi zote kadri atakavyoelekezwa na Mwenyekiti.
8
SURA YA SITA.
6.0 Vikao
Kikundi hiki kitaongozwa kwa kufanya vikao mbali mbali kama vifuatavyo.
6.1 Mkutano Mkuu
Kutakuwa na mkutano mkuu utakaofanyika mara moja kwa mwaka. Ili mkutano huu ufanyike idadi ya wajumbe
watakohudhuria kikao hicho ni lazima iwe siyo chini ya mbili ya tatu (2/3) au (67%) ya wajumbe wote walio hai
9
6.6 Kikao cha kamati ya Fedha na Mipango.
Kamati hii itakua na vikao kadri itakavyohitajika kufanya hivyo.
SURA YA SABA
7.0 Taarifa za Uchaguzi
Kutakuwa na chaguzi mbali mbali za viongozi wa kikundi, ambazo zitafanyika kila baada ya
Miaka miwili (2) katika Mkutano Mkuu wa Kikundi wa mwaka. Kama ifuatavyo:-
Kutoka miongoni wa wajumbe wa kikundi yatapendekezwa majina matatu na kupigiwa kura kwa pamoja, ambapo
Mwenyekiti na makamu wake watapatikana kutokana na wingi wa kura utakao patikana. Mwenyekiti atachaguliwa
endapo atapata kura zaidi ya asilimia hamsini (50%). Atakae fuatia kwa kura nyingi ndio atakuwa Mwenyekiti Msaidizi.
7.2 Katibu wa Kikundi
Kutoka miongoni mwa wajumbe wa kikundi yatapendekezwa majina matatu na kupigiwa kura kwa pamoja. Katibu
atapatikana kwa kupata kura zaidi ya asilimia hamsini (50%) ya kura zote. Atakayefuatia kwa kura nyingi ndio atakuwa
Mwenyekiti Msaidizi.
Kutoka miongoni mwa wajumbe wa kikundi yatapendekezwa majina matatu na kupigiwa kura kwa pamoja. Mweka
hazina atapatikana kwa kupata kura zaidi ya asilimia hamsini (50%) ya kura zote.
10
SURA YA NANE
8.0 ADA
8.1 Kutakuwa na michango na ada mbali mbali ambazo zitaainishwa kwenye kanuni za kikundi . Michango na ada hizo ni
kama ifuatavyo:
i) Kiingilio kwa wanachama
ii) Ada ya kila mwezi kwa kila mwanachama,
iii) Misiba,
iv) Sherehe na
v) Magonjwa
SURA YA TISA
SURA YA KUMI
10.0 Utatuzi wa Migogoro
Ufuatao ni utaratibu wa kikundi kutatua migogoro itakayo jitokeza ndani ya kikundi:
Migogoro yote ya kikundi itatatuliwa Kamati ya Sheria na Nidhamu. Kama Mgogoro huo utashindikana
kutatuliwa na Kamati ya Sheria na Nidhamu mgorogoro huu utapelekwa
i) Kamati ya utendaji
ii) Na endapo mwanachama/ wanachama watakataa kufuata makubaliano ya utatuzi wa
shauri, basi watakuwa wamejifukuzisha uwanachama wao wenyewe /mwenyewe.
i) Kikundi kitakuwa kimevunjika endapo asilimia 99% ya wanachama hai watapiga kura ya
ndio ya kuvunja kikundi katika mkutano mkuu wa kikundi.
ii) Au endapo kwa mujibu wa sheria ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
iii) Endapo kikundi kitavunjika kila mwanachama atakuwa na haki sawa ya kurudishiwa
michango yake kulingana na hali ya fedha itakavyokua. Mali yote iliyopatikana itagawanywa sawa kwa kila
mwanachama.
Jina ____________________ _____ Jina _____________________________
Sahihi.................................................. Sahihi …………………….……...............
Tarehe …………………………............ Tarehe ………………………..................
31.............................................................. .............................................
32.............................................................. ............................................
33.......................................................... ............................................
34........................................................... ............................................
35............................................................. .............................................
36............................................................ ............................................
37................................................................ .............................................
38............................................................ .............................................
39.............................................................. .............................................
40................................................................ .............................................
41.................................................................. ..............................................
42................................................................... ...............................................
43.................................................................... ...............................................
44................................................................... ...............................................
45................................................................... ................................................
46................................................................... ................................................
47................................................................... ................................................
48.................................................................... ................................................
49......................................................................... ................................................
14
50....................................................................... ................................................
15