Professional Documents
Culture Documents
Katiba - Ya - Kikundi - Ycsc
Katiba - Ya - Kikundi - Ycsc
(YCSC)
KATIBA
YA
KIKUNDI
(YCSC)
FOUTH DRAFT
YALIYOMO
2. SEHEMU YA PILI................................................................................................................5
8. SEHEMU YA NANE........................................................................................................... 16
Malengo mahususi:
(a) Kushirikiana na kusaidiana wakati wa shida na raha.nk
(b) Kuwezesha wanakikundi kuimarishana kiuchumi na hali ya maisha kwa:-
i. Kupokea na kuweka michango ya fedha za wanakikundi
ii. Kuanzisha na kuendeleza shughuli zozote halali za kiuchumi kwa manufaa ya
wanakikundi kama itakavyokubaliwa katika mkutano halali wa wanakikundi
iii. Kuwezesha kifedha shughuli binafsi za wanakikundi kwa masharti yaliyokubaliwa na
wanakikundi
iv. Kuhamasisha ushirikiano na wanakikundi wenye changamoto mbalimbali kama ulemavu,
uzee, uyatima, uathirika wa ukimwi na watoto wa mitaani.
3. SEHEMU YA TATU
3.1 UANAKIKUNDI
1. Kuchangia fedha kila mwezi (ada) na michango mingine yoyote kama itakavyoanishwa
kwenye kanuni au iliyopendekezwa na kuidhinishwa na wanakikundi
5. Kutii na kufuata maazimio yote ya Mkutano wowote halali hata ikiwa hakuwepo kwenye
mkutano huo, au kutoshiriki katika kupitisha azimio hilo
4.1 Michango
(b) Endapo mwanakikundi atachelewa kulipa kiasi hicho, au asipolipa kabisa, utaratibu wa faini
(penalty) na adhabu nyingine zilizokubaliwa katika kanuni za kikundi zitatumika.
(c) Mtunza fedha wa kikundi atatoa taarifa sahihi za michango yote iliyokusanywa siku ya
mkutano akionyesha wale waliolipa, wanaodaiwa, aina ya michango iliyokusanywa na habari
nyingine inayofaa kadiri ya utaratibu wa hesabu za fedha.
(b) Kila mwanakikundi atatakiwa kulipa kiasi cha fedha kilichopitishwa kwa wakati sahihi, na
kwa utaratibu uliowekwa; na atakayekiuka, kipengele cha faini kitatumika.
(b) Kiasi cha faini na utaratibu wa kulipa faini utaratibiwa kadiri ya kanuni za kikundi.
(c) Ikiwa wanakikundi wataona inafaa na wakaridhia kwa zaidi ya theluthi mbili (2/3), na
kutegemeana na kosa, mwanakikundi atasimamishwa uanachama na kushitakiwa kwenye
vyombo vya sheria.
(i) Kundi A
Kundi hili litajumisha kamati kuu tendaji yaani Mwenyekiti, Makamu mwenyekiti, Katibu,
na Katibu Msaidizi. Kama mmoja wa kiongozi hayupo, mfumo utazingatia mtiririko Katika
uongozi kutoka juu kwenda chini.
(ii) Kundi B
Bila kuathiri matakwa ya kuidhinisha malipo, iwapo watajwa katika ibara 4.4(c) (i) na (ii)
watakuwa na mgongano wa kimaslahi aidha ya kindugu ama kwa namna yeyote ile basi ni
lazima ikaepukwa kwa maslahi ya kikundi.
5. SEHEMU YA TANO
(b) Ikiwa kiongozi yeyote atasitishwa uongozi kama inavyoelezwa katika kipengele cha
6.3.4, utaitishwa mkutano maalum wa uchaguzi kwa nafasi yake.
6.2 Utoaji wa Taarifa za Mikutano au Vikao.
(a) Taarifa za mkutano zitatolewa kwa wanakikundi wote kwa kutumia taratibu
zinazokubalika. Taarifa hii itabidi ionyeshe waziwazi tarehe ya Mkutano, Idadi ya
wanakikundi waliohudhuria, muda, mahali pa mkutano na dhumuni la mkutano.
(b) Taarifa yoyote ya dharura inayohusu kikundi itatakiwa kufikishwa kwa uongozi kwanza
na uongozi utatoa utaratibu wa kuwafahamisha wanakikundi wote na taratibu nyingine.
i. Mwenyekiti
ii. Makamu Mwenyekiti
iii. Katibu
iv. Katibu Msaidizi
v. Mweka Hazina
(b) Kundi linaweza kuwa na wadhamini mpaka watatu (3) ambao watapendekezwa na
kamati kuu na kuidhinishwa na mkutano mkuu wa wanakikundi. Hawa watakuwa ni
washauri wakuu wa masuala mbalimbali yatakayohusu maendeleo ya kikundi.
(b) Viongozi waliomaliza muda wao wanaweza kuchaguliwa tena lakini wasiwe wamekalia
nafasi hiyo hiyo kwa zaidi ya vipindi vitatu mfululizo.
iii. Wanachama watakosa imani nao/naye kwa idadi ya thelulthi mbili ya wanachama
wote.
iv. Ataamua kujiuzulu kwa ridhaa yake mwenyewe kwa maslahi ya kikundi; na zaidi
ya nusu ya wanakikundi wamekubaliana na ombi lake la kujiuzulu
(b) Kiongozi aliyesitishwa kuongoza atawajibika kukabidhi mali na taarifa sahihi kwa
kikundi (au kiongozi mwingine aliyechaguliwa) kwa utaratibu ulioanishwa kwenye
kanuni za kikundi.
7. SEHEMU YA SABA
(b) Kamati nyingine zozote za Muda zinaweza kuundwa katika mikutano ya kawaida ya
mwezi kulingana na matukio au umuhimu wa kuwepo kamati hizo.
(b) Ikiwa jambo husika linahitaji maamuzi ya wanakikundi wote, Kamati Tendaji itawasilisha
mapendekezo yao kwenye mkutano wa wanakikundi wote kwa uamuzi wa mwisho.
(b) Ikiwa njia ya kwanza itashindikana, msaada wa mahakama na taratibu za kisheria zinaweza
kufuatwa.
(b) Endapo Kikundi hiki kitavunjwa, Mali zote za kikundi zitafilisiwa ili kulipia madeni
yatakayokuwa yanakikabili kikundi hadi wakati huo
(c) Fedha zitazobakia baada ya kulipa madeni, zitagawanywa kwa wanakikundi wote kulingana
na muda na kiasi cha michango ya kila mmoja.
(d) Endapo fedha zilizopo hazitoshi kulipa deni, salio la deni litagawanywa kwa utaratibu sawa
na wa kipengele 9.1 (c) hapo juu.
MWISHO.