Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 24

Ushiriki + Ufuatiliaji + Uwazi = UWAJIBIKAJI

Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM


Uzoefu wa Sikika, 2012/13
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Shukrani
Kitabu hiki kimeandaliwa na Sikika kwa lugha rahisi na kwa ufupi ili kuviwezesha vikundi vya kijamii au mashirika
ya hiyari katika ngazi ya msingi, kuendesha shughuli za Ufuatiliaji na Uwajibikaji wa Jamii (UUJ/SAM).

Ujuzi, uzoefu na umahiri wauongozi na wafanyakazi wa Sikika katika kuandaa na kuendesha mafunzo ya SAM
kwenye huduma za afya ndio uliofanikisha uandishi wa kitabu hiki. Shukrani za kipekee kwa timu za UUJ/SAM za
Iramba, Kondoa, Kiteto, Mpwapwa, Singida vijijini, Kibaha, Simanjiro na wilaya za mkoa wa Dar es Salaam kwani
bila ushiriki na kujitolea kwao, uzoefu wa SAM usingepatikana.

Uandaaji wa mafunzo ya SAM katika wilaya hizo pia usingefanikiwa bila ushiriki wa viongozi wa Halmashauri hizo
ambao walisaidia katika kutoa taarifa na nyaraka muhimu na pia kuandaa mazingira ya utekelezaji wa UUJ/SAM.

Irenei Kiria
Mkurugenzi Mtendaji

Hatimiliki © 2013
Shirika la Sikika
Tarehe ya kuchapishwa 2013
Kimeandaliwa na: Lilian R. Kallaghe, Idara ya Habari na Mawasiliano
Kimechapishwa na: Digitall Ltd.

i
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Orodha ya Vifupisho
UUJ Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii
SAM Social Accountability Monitoring
BOQ Bill of Quantities (Makadirio ya Mzabuni)
CAG Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali
TAMISEMI Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

ii
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Yaliyomo
1. Orodha ya Vifupisho ii
2. Utangulizi 1
3. Umuhimu wa kitabu hiki 2
4. Hatua kuu Muhimu kwa shughuli ya UUJ/SAM 3-16
5. Hitimisho 17

iii
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Utangulizi
Sikika ilianza kutekeleza rasmi shughuli ya Ufuatiliaji na kuzingatia uzoefu, dhana na malengo ya Sikika ya kufanya
Uwajibikaji kwa Jamii (UUJ), maarufu kama SAM - Social tathmini ya mifumo ya uwajibikaji katika ngazi zote za jamii
Accountability Monitoring) katika ngazi ya serikali ya mitaa/ na kisha kutetea, kwa lengo la kufikia upatikanaji wa huduma
vijiji mwanzoni mwa mwaka 2011. SAM/UUJ ni mchakato bora za afya kwa watanzania wote.
wa kuwawezesha wananchi kudai utawala bora na uwajibikaji
Tunatarajia kwamba kitabu hiki kitakuwa na manufaa kwenu;
katika utoaji wa huduma za jamii. Lengo ni kuwajengea
kitawawezesha wananchi kunufaika na kupata huduma bora
wananchi uwezo wa kutafuta taarifa na kuzichambua ili waweze
za kijamii hususani huduma za afya, ambazo ni haki yao
kufuatilia na kusimamia mipango, bajeti na utekelezaji wa
ya msingi na ya kikatiba. Ufuatiliaji utafanikiwa iwapo kila
miradi mbalimbali ya kijamii katika maeneo yao.
mdau, (mwananchi, diwani, kamati na bodi mbalimbali na
Kupitia SAM/UUJ, jamii husika inakuwa na uwezo wa watumishi wa umma) watatimiza wajibu wao kwa kushiriki
kuhoji uwajibikaji wa watendaji na watoa huduma, mathalan kikamilifu katika kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii.
huduma za afya katika sekta ya umma ili hatimaye waweze
kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji ya wananchi. Licha ya kulenga mifano ya sekta ya afya,
Matarajio ya UUJ/SAM ni kuona viongozi wanawajibika tunaamini kwamba, misingi na hatua za UUJ/
zaidi kwa wananchi wanaowatumikia na wananchi nao SAM zilizoainishwa katika kitabu hiki zinaweza
wanafahamu na kutekeleza wajibu wao kwa kufuatilia haki pia kutumika katika sekta nyingine za huduma
zao za msingi na kuwawajibisha watoa huduma wasiowajibika. zinazogusa maslahi ya wananchi.
Mifano ya kitabu hiki imejikita upande wa afya kwa

1
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Nini Umuhimu wa Kitabu Hiki?


Kitabu hiki kinaelezea uzoefu wa Sikika katika kuandaa f. Kudai ufafanuzi, uhalali na uthibitisho juu ya matumizi
Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii (UUJ kwenye ngazi ya ya rasilimali za umma katika kutekeleza mipango na
Halmashauri/Manispaa. Kwa kufuata hatua zilizoainishwa shughuli mbalimbali.
ndani ya kitabu hiki, tunaamini kwamba vikundi vya
wanajamii au mashirika yataweza kuendesha kazi ya UUJ/
SAM katika ngazi ya jamii kwa:
a. Kushirikiana na wanajamii na wadau wengine na kuunda
timu ya UUJ.
b. Kuainisha shughuli mbalimbaliza maendeleo
zilizopangwa pamoja na bajeti zake katika eneo husika.
c. Kuchambua na kutathmini utekelezaji wa mipango hiyo
ikilinganishwa na bajeti iliyotengwa.
d. Kufuatilia uwajibikaji wa viongozi na kamati mbalimbali
kupitia taarifa za vikao, maazimio na ufuatiliaji wa
utekelezaji wa maazimio au maamuzi.
e. Kutathmini uadilifu wa viongozi katika kutoa huduma
kwa wananchi.

2
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hatua ya 1
Kupanga na Kuandaa Utekelezaji wa Uuj/SAM
 Andaa malengo makuu na ainisha mwaka wa fedha  Ni muhimu kufanya mawasiliano na madiwani
unaolenga kuufanyia tathmini. na watendaji wa kata mbalimbali za wilaya husika
 Andaa barua za utambulisho yenye maelezo ya kina ili kuwajulisha nia ya kufanya zoezi la UUJ. Hii
juu ya lengo la kuunda timu ya UUJ. Katika barua itarahisisha uekelezaji, hususan wakati wa kutembelea
hiyo, unaweza kuainisha aina ya nyaraka zenye taarifa miradi mbalimbali iliyopo kwenye kata na itapunguza
mbalimbali ambazo utahitaji kupewa kutoka katika ofisi vipingamizi kutoka kwa viongozi/watendaji.
ya halmashauri ya Wilaya/Manispaa ikiwemo mipango Muhimu: Kabla ya kuanza zoezi hili,
ya shughuli za maendeleo, bajeti na taarifa za utekelezaji hakikisha una nyaraka zote zinazostahili.
ambazo timu yako ingependa kuzitumia kuendesha
zoezi la UUJ.
 Peleka barua kwa viongozi husika: Mkurugenzi
Mtendaji wa Wilaya na Mkuu wa Wilaya. Hawa
watawafahamisha viongozi wengine kama Katibu Tawala
wa Wilaya, Mganga Mkuu wa Wilaya, wakuu wa Idara
ama kiongozi mwingine wa wilaya au kata, kulingana na
sekta unayolenga kuifanyia kazi.

3
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hatua ya 2
Kuchagua Wajumbe wa Timu ya Uuj/Sam
Uchaguzi wa wajumbe wa UUJ ufanyike kupitia mikutano zinatumika kwa maslahi binafsi badala ya kunufaisha
ya hadhara ya vijiji/kata. Ili kuendesha zoezi la UUJ kwa wananchi,
mafanikio, ni muhimu kushirikiana na viongozi wa kijiji/  Elezea kwamba ni haki yao kudai uwajibikaji wa
kata ili kupata uhalali na msaada katika kuandaa mikutano watendaji na viongozi wao ikiwemo kuwataka
ya wananchi kwenye eneo husika. kurekebisha dosari za utekelezaji zinapojitokeza,
Katika mikutano hiyo, mambo yafuatayo ni muhimu
yafanyike:

 Elezea umuhimu wa ushiriki wao na kwamba ni haki


yao kikatiba, kama walipa kodi wa nchi hii,
 Fafanua kwamba ni haki yao ya msingi kudai maelezo na
ufafanuzi kutoka kwa watendaji na viongozi wao kuhusu
mambo mbalimbali yanayogusa maisha yao ya kila siku,
mfano masuala ya afya,
 Wakumbushe mamlaka waliyonayo ya kudai maelezo
na ufafanuzi pale ambapo wataona rasilimali za umma

4
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

 Toa muda wa kutosha kwa wananchi kuuliza maswali


juu ya mfumo wa SAM/UUJ ili waelewe manufaa yake
na
 Kutoa fursa kwa wananchi kuchagua mwakilishi
atakayejiunga na wajumbe wengine kuunda Timu ya
wilaya.

Wajumbe wa timu ya UUJ lazima wawe ni watu makini,


wenye upeo mpana wa masuala yanayowagusa katika jamii,
moyo wa kujitolea na wanaowakilisha makundi maalum
katika jamii, na ni muhimu wajue kusoma na kuandika kwa
lugha ya Kiswahili.

Muhimu: Kazi ya kuchagua timu ya UUJ/SAM


ifanyike kupitia mkutano wa kijiji ili wananchi
wachague wawakilishi wao wenyewe, ambao
wanakubalika katika jamii husika. Wajumbe wa
UUJ/SAM watawajibika kwa jamii iliyowachagua.
Mfumo kama huu utumike pia kupata wawakilishi
wa makundi maalum na jinsia mfano;-WAVIU, watu
wenye ulemavu nk.

5
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hatua ya 3
Kuandaa Mikutano ya Wadau Wakuu
Hatua hii ya tatu itakuwa na mikutano mikubwa miwili.
Mkutano wa kwanza ni wa Baraza la Madiwani ambao Muhimu: Mkutano wa Baraza la Madiwani
ndiyo wawakilishi rasmi wa wananchi. Hivyo basi, anza kwa ufanyike kabla ya Mkutano wa Wadau ili kupata
kuandaa mkutano na madiwani. Ni vyema kuandaa mkutano uhalali wa kuendelea na hatua zingine zote.
huo kabla au baada tu ya mkutano wa kisheria wa Baraza
la Madiwani ili kupata ushiriki mkubwa kwa wakati mmoja halmashauri ambao ni Mkurugenzi wa Halmashauri, wakuu
na pia kupunguza gharama. Katika mkutano wa idara za halmashauri pamoja na wawakilishi
huu, Madiwani waelezwe kuhusu: wa makundi muhimu yanayounda timu ya
SAM/UUJ. Makundi hayo ni;
 Dhana ya UUJ na mchakato wake pamoja
na umuhimu wa madiwani kushiriki ili a. Wawakilishi wa wananchi ambao ni
kuleta ufanisi na kupata matokeo mazuri. watumia huduma,
 Jinsi zoezi la UUJ litakavyo wasaidia b. Wawakilishi kutoka kamati za UKIMWI
katika kufuatilia na kusimamia utekelezaji na vituo vya afya,
wa miradi ya maendeleo iliyopangwa,
c. Uwakilishi wa wajumbe wa Bodi ya Afya
kwa manufaa ya wapiga kura wao.
ya Halmashauri,
Mkutano wa pili unahusu wadau wakuu wa d. Uwakilishi wa makundi ya watu wenye
sekta ambayo utaifanyia ufuatiliaji. Wadau mahitaji maalum; watu wenye ulemavu, watu
hawa ni pamoja na watendaji wa serikali/

6
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

wanaoishi na virusi vya UKIMWI (WAVIU), kuelezea umuhimu wake katika kuimarisha uwajibikaji
e. Viongozi wa dini, wa wananchi na viongozi, lengo likiwa ni kuboresha
utoaji na upatikanaji wa huduma bora za jamii kwa
f. Wawakilishi wa wananchi ambao ni Madiwani, watanzania wote.
g. Mwakilishi mmoja  Pili, kutoa fursa
kitoka mashirika ya kwa wadau kuchagua
hiyari, wawakilishi wao kujiunga
h. Mtu mashuhuri katika timu ya UUJ.
anayekubalika na Fursa hii ni kwa asasi
kuheshimika katika za kiraia, viongozi wa
dini, Maafisa Watendaji
jamii,
Kata na wawakilishi
i. Watendaji wa kata na wa Halmashauri.
j. Uwakilishi kutoka Kumbuka; katika
katika timu ya mkutano huu, wajumbe
uendeshaji ya kutoka ngazi ya jamii,
Madiwani na makundi
halmashauri, kwa Source: sambweti.blogspot.com
maalumu watakuwa
mfano, ya huduma za
wameshachaguliwa.
afya.
 Tatu, kutambulisha rasmi timu nzima ya wilaya na
Malengo ya mkutano wa pili wa wadau ni: kusomewa hadidu za rejea na Mkuu wa Wilaya au
 Kwanza, kutambulisha zoezi la SAM/UUJ kwa wadau na mwakilishi wake.

7
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hatua ya 4
Mafunzo kwa Timu ya Uuj/SAM
Mafunzo ya UUJ/SAM ni muhimu ili kuwajengea uwezo na
kuipa timu uelewa mpana zaidi kuhusu hatua kuu tano za
mchakato, kuzifahamu nyaraka na taarifa husika zikiwemo za
mipango na ripoti za utekelezaji wa miradi ya umma.

Lengo la kupitia na kuchambua nyaraka ni:

 Kutambua mipango na miradi iliyopangwa kutekelezwa


katika jamii.
 Kufahamu bajeti iliyotengwa na halmashauri husika kwa
ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.
 Kufanya uchambuzi wa kina na ufuatiliaji wa taarifa na
mfumo mzima wa utendaji wa idara mbalimbali, kama
ya afya.
Nyaraka zinazohitajika kwa shughuli ya uchambuzi ni zile
zinazohusu mipango ya shughuli za maendeleo ya jamii
husika, mathalan, kwa upande wa afya, taarifa/nyaraka
zifuatazo ni za muhimu;

8
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Na. Nyaraka/Ripoti Na. Nyaraka/Ripoti


1 Mpango Mkakati wa Halmashauri 7 Ripoti ya Mkaguzi wa Ndani
2 Mpango Kabambe wa Afya wa Halmashauri (CCHP) 8 Mihutasari ya vikao vya Baraza la Madiwani
3 Mpango/Mfumo wa Matumizi wa Muda wa Kati 9 Ripoti zinazohusu mipango ya masuala ya
(MTEF) UKIMWI na Virusi vya UKIMWI
4 Ripoti ya Utekelezaji wa Mpango Kabambe wa Afya wa 10 Taarifa za Utekelezaji wa Mipango na shughuli za
Halmashauri ya mwaka UKIMWI na Virusi Vya UKIMWI.
5 Ripoti za utekelezaji za kila robo mwaka 11 Muhtasari wa Vikao vya Kamati za kudhibiti
UKIMWI za Halmashauri
6 Ripoti za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za 12 Taarifa ya Uchambuzi wa mahitaji ya
Serikali–CAG Halmashauri

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na


Serikali za Mitaa (TAMISEMI), imetoa agizo kwa taasisi
za serikali zikiwemo halmashauri kote nchini, kutoa taarifa
muhimu kwa wananchi na mashirika ya hiyari, pindi
wanapoombwa kufanya hivyo.

Muhimu: Inashauriwa kwamba, nyaraka na taarifa


zote zitakazochambuliwa kama zilivyoainishwa hapo
juu, ziwe ni za muda wa mwaka mmoja wa fedha
uliopita.

9
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Mafunzo ya UUJ/SAM yanachukua wastani wa wiki 2 hadi 3 yakijikita katika hatua kuu tano za mchakato wa kufikia
huduma bora za jamii:

10
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

1. Mipango na Mgawanyo wa Rasilimali: Ni kiasi gani 3. Usimamizi wa Utendaji/Ufanisi: Je, watoa huduma
cha fedha kilichopo? Nini kimepangwa kufanyika? wanatekeleza wajibu wao kwa ufanisi? Hatua hii pia
Watoa huduma wamepanga kuzitumia vipi? Mgawo inaangalia kama je, watumishi wa umma wanatoa huduma
wa fedha/rasilimali za umma hutolewa kulingana na bora za jamii? (Angalia: Ripoti ya Mkaguzi wa Ndani,
Mpango Mkakati ulioainisha shughuli zote kwa kina Muhtasari wa vikao vya Baraza la Madiwani, Ripoti ya
na kuidhinishwa, ili kusaidia vyombo vya usimamizi mwaka ya Utekelezaji wa Mpango Kabambe wa Afya wa
kufuatilia. Uchambuzi ufanywe kwa kuangalia Mpango Halmashauri, Mpango Mkakati wa Halmashauri, BOQ).
Mkakati na vipaumbele vyake, kuona jinsi Mpango kazi 4. Usimamizi wa Uadilifu: Hii inaangalia mifumo iliyopo:
wa mwaka husika unavyoendana na vipaumbele vya Je, inawazuia watoa huduma za jamii kutotumia vibaya
Mpango Mkakati. Pia, kuangalia jinsi mgawanyo wa rasilimali za umma? Je, wanaotumia vibaya rasilimali
rasilimali unavyoendana na vipaumbele hivyo. za umma wanachukuliwa hatua gani? (Angalia: Ripoti
ya Mkaguzi wa Ndani, Muhtasari wa vikao vya Baraza
2. Usimamizi wa Matumizi: Je, ni jinsi gani fedha za la Madiwani, Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
umma zinatumika? Hatua hii inaangalia utaratibu wa Hesabu za Umma-CAG, taarifa za magazeti).
kusimamia matumizi na mapato kwa kipindi cha mwaka
5. Usimamizi wa Uwajibikaji: Je, maafisa na watumishi
wa fedha; kuhakikisha kuwa taarifa za matumizi ya
wa umma wanawajibishwa na Vyombo vya Usimamizi?
fedha zinatolewa kwa usahihi, zinaaminika, zinawezesha
(Bunge, Baraza la Madiwani, Taasisi za Ukaguzi: Ofisi
ufuatiliaji makini wa matumizi na kusaidia kufikia ya CAG). Moja ya shughuli zao kuu ni kuwasimamia
maamuzi sahihi. (Mfano wa nyaraka za uchambuzi watendaji wa serikali ili wafanye kazi kwa uwazi na
katika hatua hii ni MTEF , CCHP, Ripoti za utekelezaji ufanisi na kuwajibika kutokana na matumizi ya rasilimali
za kila robo/mwaka na Ripoti ya Mkaguzi wa Ndani, za umma. (Angalia: Muhtasari wa vikao vya Baraza la
BOQ) Madiwani, Ripoti za CAG.)

11
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hatua ya 5
Kutembelea Miradi/Maeneo ya Utekelezaji
Katika hatua hii, kazi kubwa ya timu ya UUJ/SAM itakuwa  Andaa ratiba.
ni kulinganisha taarifa za utekelezaji zilizofanyiwa uchambuzi  Andaa ripoti ya awali ambayo itaainisha maswala
na hali halisi: Je, kilichoandikwa ndicho kilichofanyika? yanayohitaji kuhakikiwa na kufuatiliwa wakati wa
Shughuli zilizopangwa zimetekelezwa au la? Kwa kiwango kutembelea maeneo, miradi ama sehemu shughuli hizo
gani? Je, utekelezaji unaendana na thamani ya fedha zilipotekelezwa.
zilizotengwa na kutumika? Je, miradi iliyoandikwa kwenye
 Andaa ratiba ya usafiri.
taarifa ni halisi na inaendana na mipango na bajeti au fedha
Wasiliana na viongozi (diwani, wenyeviti wa mitaa/vijiji na
zilizotengwa?
watendaji wa mitaa/kata) ili kupata wananchi kwa ajili ya
kupata maelezo, ufafanuzi na uzoefu wao.
 Gawa majukumu kwa wajumbe wote wa timu ya SAM/
UUJ.
 Tumia nyenzo za kukusanya kumbukumbu kama vile
kamera za picha mnato na ikibidi kamera ya video.
Baada ya kuona hali halisi ya utekelezaji wa miradi katika maeneo
mbalimbali, timu ya UUJ/SAM iandike ripoti ya matokeo.
Ripoti hii italinganisha hali halisi kutoka katika vitongoji/vijiji/
kata, ikilinganishwa na bajeti na mipango iliyoandikwa kwenye
taarifa za Halmashauri zilizochambuliwa awali.

12
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hatua ya 6
Kuwasilisha Matokeo ya Awali kwa halmashauri/Sekta husika
Baada ya kukamilisha mafunzo na kufanya uchambuzi, taarifa ya awali iandaliwe kuonesha mambo yaliyobainika. Timu ikae
upya kulinganisha taarifa za Halmashauri au Idara husika na hali halisi ya utekelezaji kwenye maeneo yaliyotembelewa.

Taarifa ipelekwe kwenye mkutano wa ndani (watendaji wa Halmashauri) ili kutoa fursa kwa Idara husika kutoa ufafanuzi.

xvi
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hatua ya 7
Mkutano wa Pili wa Wadau
Hii ni hatua muhimu inayolenga kutoa mrejesho wa kazi  Timu ya UUJ/SAM isome taarifa ya matokeo
zilizofanyika kuanzia mafunzo hadi ziara ya maeneo husika ya ufuatiliaji. Ni muhimu kutoa uthibitisho wa
ili kupata ufafanuzi, hali halisi kwa kutumia
uthibitisho na uhalalisho vielelezo vya picha.
kutoka kwa watendaji wa
 Watendaji watoe
serikali (watumishi wa
Ufafanuzi, Uthibitisho
umma). Katika hatua
na Uhalalisho kutokana
hii, wadau wote walioitwa
na maamuzi waliyofanya.
awali huitwa tena kwa
mara ya pili ili washiriki  Kufikia
kupokea mrejesho. Ni makubaliano na kupanga
vyema mkutano huu tarehe ya kutoa mrejesho
ukaandaliwa, kusimamiwa katika mkutano wa
na kuendeshwa na wajumbe wa timu ya UUJ/SAM na hadhara.
Mkuu wa Wilaya awe Mwenyekiti wa Mkutano.

14
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hatua ya 8
Kuwasilisha Matokeo kwa Walipa Kodi-Wananchi
Wananchi ndio walipa kodi, watumiaji wa huduma za jamii
na wenye mamlaka na haki ya kufahamu jinsi rasilimali
zao zinavyotumika. Hivyo, ni muhimu wapewe mrejesho
wa shughuli nzima ya UUJ/SAM. Mrejesho huu ufanyike
kupitia mikutano ya jamii, machapisho na ripoti. Hii itawapa
mwangaza na ari wananchi wengine ambao hawakushiriki
kwenye shughuli hiyo:
 Kufuatilia masuala yanayowahusu ikiwemo kudai
taarifa mbalimbali za mapato na matumizi.
 Kutoa malalamiko na maoni yao kwa wahusika ili
yashughulikiwe.
 Kushiriki katika mikutano ya jami, kuhoji na kujadili
miradi/shughuli za maendeleo yanayowahusu.
Muhimu: Upatikanaji wa taarifa unahamasisha uwazi
na kukuza ushiriki wa jamii hivyo kutimiza haki na
wajibu wa kuwawajibisha watendaji wasiotekeleza
majukumu yao.

15
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hatua ya 9
Kuandaa Mpango wa Ufuatiliaji

Wakati wa mkutano wa mrejesho, viongozi mara


nyingi huahidi kutatua maswala ambayo wananchi na
timu ya UUJ/SAM inakua imeyaibua. Katika hatua
hii, timu iandae mpango mkakati ambao utawaongoza
katika kufuatilia mambo ambayo viongozi wameahidi
kuyatekeleza.

Wananchi wengine ambao hawako kwenye timu


wanaweza kushiriki katika ufuatiliaji na kutoa taarifa
kwa timu ya SAM/UUJ na kwa ngazi husika; viongozi
wa kijiji, kata, madiwani n.k
Mfano: Ripoti ilionesha kwamba vitanda kadhaa vya
wagonjwa vilinunuliwa katika kituo cha afya lakini
wakati wa kuhakiki havikuwepo.

16
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Hitimisho
Shughuli za UUJ/SAM ni endelevu na zinamhusu kila mmoja wetu;
iwe mwananchi, mtendaji, diwani, mbunge au kiongozi yeyote!

Boresha Huduma
Wajibika Shiriki
za Jamii

17
Hatua 9 za Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii – UUJ/ SAM

Sikika inafanya kazi


kuhakikisha usawa katika
upatikanaji wa huduma bora
za afya, kwa kutathimini
mifumo ya uwajibikaji katika
ngazi zote za serikali.

Nyumba Na.69 Simu: +255 22 26 663 55/57 Nyumba Na. 340


Ada Estate, Kinondoni Ujumbe mfupi: 0688 493 882 Mtaa wa Kilimani
Barabara ya Tunisia Faksi: +255 22 26 680 15 S.L.P 1970
Mtaa wa Waverley Barua pepe: info@sikika.or.tz Dodoma, Tanzania.
S.L.P 12183 Tovuti: www.sikika.or.tz Simu: 0262321307
Dar es Salaam, Tanzania. Blog: www.sikika-tz.blogspot.com Faksi: 0262321316
Twitter: @sikika1
Facebook: Sikika Tanzania

xxii

You might also like