Professional Documents
Culture Documents
BibliaNiJibu UnatambulikajeUlimwenguWaRoho
BibliaNiJibu UnatambulikajeUlimwenguWaRoho
Advertisements
Merito Tagalile
~0657 048393
~0625 610925
Marko 1:23-26
Katika vita yoyote ya rohon adui huwa anakuona wewe unaweza usimuone na
usimfahamu lakin yeye anakuona vizuri na anakufahamu vizuri,
Na mfano ukiwa unalindwa na moto wewe unaweza usijue labla yule adui yako
iwe mchawi mganga aseme kwa watu aah huyu ndugu ni hatari haingiliki au
ukiingia utakuta moto au bahari na akishasimulia ndipo wewe uje kuambiwa na
watu, au waweza muombea mtu kisha mapepo yakalipuka na kusema huyu mtu
tulimtafuta sana, hiyo ipo
Sasa hiyo huwa haitokei ukiwa huna ratiba special yamaombi na kusoma Neno+
kufunga ili uongeze viwango, ili rohon uonekane moto nilazima uwe na ratiba
special, hakika nakuhakikishia utayasikia, watu watakusimulia na utayapata tu,
Nakwambia haya ili uongeze bidii ya ukaribu na Mungu katika Maombi, Neno na
kufunga, ukiweka bidii kutaka Mungu adhihilike kwako Mungu atadhihilika tu,
Hata kama unafunga sana na kuomba na hujaona matokeo, badilika anza upya,
tubu na mwambie Bwana aonekane kwako acha wokovu wa mazoea usio na
udhihilisho wowote wa nguvu za Mungu kwako na katika jamii yako, ukidhamilia
kumtafuta Mungu kweli maisha yako yatabadilika, familia yako itabadilika na jamii
yako itabadilika sababu ya Maombi yako na kujituma kwako,
Hata kama unajiona una nguvu za Mungu kidogo USIRIDHIKE, ongeza bidii ili
Mungu aonekane kwa viwango vikubwa kwako, mwana wa Mungu Mungu wetu
hana ubaguzi ukimtafuta kwa bidii atadhihilika tu katika maisha yako.
Omba mamlaka ya Ki-Mungu ijae ndani yako na nguvu za Ki-Mungu zijae ndani
yako ili Mungu adhihilike zaburi 105:4
Ili uwe moto rohon weka ratiba ya mifungo iwe kila wiki, kila mwezi itegemee vile
ndani yako unasukumwaje, unapokua unafunga unaupa nguvu utu wako wa ndani
kutawala na kuweza kusikia Mungu anasema nini na utaweza kusikia maelekezo
toka wa Mungu sababu ya kufunga, Neno, na Maombi, ukiweka ratiba hiyo
nakuhakikishia muda si mrefu, utakua mtu wa tofauti na WA kipekee kiroho.
Tafuta na taman kutambulika rohon, taman kuwa mbabe rohon ili usichezewe
wala kushambuliwa na chochote.
Kama umebarikiwa na ujumbe huu share kwa ndugu jamaa na rafiki zako popote
pale facebook, whatsup na kwenye magroup ya Whatsup hutaachwa hivyo hivyo
bali utabarikiwa kwa kuitangaza injili kwa kushare.
Ukipenda kutumiwa masomo ya Neno la Mungu kila siku kwa Whatsup tuma
majina yako mawili inbox, whatsup kwa namba ya Tigo 0657 048393 kuomba
kuunganishwa kupewa masomo kila siku na utatumiwa, pia kwa ushauri na
maombi piga namba zilizopo hapo chini, na Mungu wambinguni akubariki sana.
https://biblianijibulako.wordpress.com
Advertisements
Share with:
Related
MAMBO YA MSINGI
KATIKA MAOMBI:
August 12, 2020
With 2 comments
Categories: Uncategorized
Leave a Comment