Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 12

YOUNG INVESTORS FORUM

RIPOTI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA WAJASILIAMALI WANAVYUO


DAR ES SALAAM 2021
RIPOTI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA WAJASILIAMALI WANAVYUO DAR ES
SALAAM 2021.

IMETOLEWA NA:-

Afisa Mtendaji mkuu, Young Investors Forum


Christopher Y Ngonyan,

MADA : -

Elimu ya uwekezaji katika masoko ya mitaji Tanzania.

WALENGWA: -
Washiriki wa maonesho

MAHALI ILIPOFANYIKA: -

Viwanja vya Kijitonyama, chuo kikuu cha Dar es salaam- ndaki ya technolojia za habari na
mawasilianao.

WAANDAJI: -
UNI TRADE FAIR.

TAREHE YA MAONESHO: -

06/02/2021

TAREHE YA RIPOTI: -

18/02/2021.

1
YALIYOMO

MADA UKURASA

1.0 UTANGULIZI ................................................................................................................................. 3


2.0 MAANDALIZI. ............................................................................................................................... 4
3.0 UTOAJI WA ELIMU KATIKA MAONESHO ................................................................................ 4
4.0 MADA MBALIMBALI ZILIZOTOLEWA ..................................................................................... 5
5.0 NAMNA MADA ZILIVYOTOLEWA ............................................................................................ 7
6.0 MATOKEO YA JUMLA YA MAONESHO .................................................................................... 8
7.0 UJUMBE WA MGENI RASMI ....................................................................................................... 9
8.0 MAOMBI NA MAONI YA WASHIRIKI. ......................................................................................10
9.0 HITIMISHO ...................................................................................................................................11
11

2
1.0 UTANGULIZI

Ripoti hii inahusu elimu ya uwekezaji katika masoko ya mitaji Tanzania iliyotolewa na Young Investors
Forum kwa wanavyuo katika maonesho maalumu ya biashara ya wajasiliamali wanavyuo yaliyofanyika
tarehe 06/02/2021 katika viwanja vya Kijitonyama, Dar es salaam.

Walengwa wakuu walikuwa ni wajasiliamali wanavyuo na wasilo wanavyuo, pamoja na wanavyuo


waliohudhuria katika maonesho.
Wakufunzi ni vijana wawekezaji kutoka taasisi isiyo ya kiserikali ya YOUNG INVESTORS FORUM
ambayo ipo katika hatua za usajili. Ambao ni;
1. Christopher Y Ngonyani
2. Samwel Maguzu
3. Elifrida Phisso
4. Agness Kalinga
5. Kaiza Ilomo
Sehemu ilipofanyikia maonesho haya ni viwanja vya Kijitonyama, chuo kikuu cha Dar es salaam- ndaki
ya technolojia za habari na mawasilianao.

Mada kuu katika maonesha haya ilikuwa:-

“Elimu ya uwekezaji katika masoko ya mitaji Tanzania.”

Tathmini iliyomo ndani ya ripoti hii ni kutoka kwa wakufunzi kwa siku Ishirini na Tano walizowezesha.

Ripoti ni kama ifuantavyo:

3
2.0 MAANDALIZI.

Maandalizi yalifanyika kwa muda wa wiki mbili kabla ya maonesho. Miongoni ya maandalizi hayo ni ;
 Uandaaji wa tisheti za maonesho
 Uandaaji wa nakala na vitabu
 Uandaaji wa chakula kwa ajili ya watoa huduma
 Uandaaji wa banda kiujumla, viti, meza na mwamvuli
 Semina fupi kwaajili ya wahudumu wa siku ya maonesho.

3.0 UTOAJI WA ELIMU KATIKA MAONESHO

Maonesho yalifanyika kwa muda wa siku moja, yalianza saa tatu kamili asubuhi na kumalizika saa kumi
na mbili jioni. Tuliweza kuwahudumia washiriki kwa namna ya kipekee, ikiwemo kutoa elimu ya jumla
juu ya masoko ya mitaji na fedha, kuruhusu washiriki kuuliza maswali na hatimae kuwagawia vitabu
vya uwekezaji vinavyochapishwa na Mamlaka ya Soko la Mitaji na Fedha Tanzania pamoja na Soko la
Hisa la Dar es salaam

Picha 1. Christopher Ngonyani akimwelezea mjasiliamali wa bidhaa za chakula

namna ya kuwekeza katika hisa na vipande.

4
4.0 MADA MBALIMBALI ZILIZOTOLEWA

Mada zilizotolewa katika maonesho haya ni kama ifuatavyo:-


 Masoko ya Mitaji Tanzania.
 Uwekezaji katika soko la hisa la DSE.
 Uwekezaji katika hatifungani
 Uwekezaji katika mifuko ya uwekezaji wa pamoja ya UTT AMIS

4.1.1 MASOKO YA MITAJI TANZANIA.


-Maana ya masoko ya mitaji.
-Historia ya masoko ya mitaji Tanzania.
-Wahusika wakubwa katika masoko ya mitaji Tanzania.
-Bidhaa zilizopo katika masoko ya mitaji Tanzania.
-Namna ya kushiriki katika masoko ya mitaji.

Picha 2. Agness Kalinga akitoa maelezo kuhusu masoko ya mitaji kwa msihiriki wa maonesho
aliyetembelea meza ya YIF.

5
4.1.2 UWEKEZAJI KATIKA SOKO LA HISA LA DSE.
-Maana ya soko la hisa la DSE
-Historia ya soko la hisa la DSE
-Faida na changamoto za kuwekeza katika hisa
-Namna ya kutumia DSE Hisa Kiganjani.
-Namna ya kupata mitaji kupitia soko la hisa.

4.1.4UWEKEZAJI KATIKA HATIFUNGANI.


-Maana na aina za hatifungani.
-Faida na changamoto za kuwekeza katika hatifungani.
-Namna ya kushiriki katika soko la awali la hatifungani za serikali.
-Namna ya kuwekezaa kwenye hatifungani katika soko la upili.
-Manufaa kwa serikali kwa kuuza hatifungani

4.1.5Uwekezaji katika mifuko ya UTT AMIS


-Maana na historia ya UTT AMIS.
-Namna mifuko ya uwekezaji wa pamoja inavyofanya kazi.
-Mifuko ya uwekezaji wa pamoja inayosimamiwa na UTT AMIS
 Mfuko wa hatifungani
 Mfuko wa umoja
 Mfuko wa watoto
 Mfuko wa jikimu
 Mfuko wa ukwasi
 Mfuko wa wekeza maisha
-Faida na changamoto za uwekezaji katika mifuko ya UTT AMIS

6
5.0 NAMNA MADA ZILIVYOTOLEWA

Mada zilitolewa kwa njia ya ushirikishi, washiriki waliweza pia kuchangia uelewa wao katika mada
zilizotolewa. Hii ilisaidia kujua mawazo mbalimbali na namna watu wengi wanavyolichukulia suala la
uwekezaji. Pia kila mshiriki aliyeweza kufika katika banda letu alipewa mtaalam mmoja hadi wawili
kuweza kumuelimisha mshiriki huyo katika mada zilizotajwa hapo juu. Mbali na hivyo washiriki
waliweza kupatiwa vitabu na nakala mbalimbali zinazoelezea uwekezaji katika masoko ya mitaji
kiundani zaidi. Ili kuboresha uhusiano wetu na washiriki wapya tuliweza kuchukua taarifa zao za
mawasiliano na kuwajumuisha katika makundi ya mtandao wa Whatsapp kuendelea kujifunza zaidi.

Picha 3. Christopher Ngonyani anamwelezea mshiriki wa maonesho namna ya


Kutumia DSE hisa kiganjani.

7
6.0 MATOKEO YA JUMLA YA MAONESHO

6.1.1Masoko ya mitaji Tanzania.

Washiriki wa maonesho haya waliweza kufahamu wahusika wakubwa katika masoko ya mitaji Tanzania
pamoja na kazi zao, bidhaa zilizopo na namna ambavyo wanaweza kushiriki kama wawekezaji katika
dhamana mbalimbali zilizopo sokoni.

6.1.2Uwekezaji katika soko la hisa la DSE.

Washiriki wa maonesho haya waliweza kufahamu kwa undani kuhusu historia ya soko la hisa la DSE,
fursa za uwekezaji zilizopo, namna ya kutumia DSE hisa kiganjani katika kununua , kuuza hisa na
kupata taarifa mbalimali za soko kwa urahisi. Baadhi walipakua DSE hisa kijanjani na kuanza kufanya
usajili. Wajasiliamali wanavyuo walioshirikiki maonesho haya walivutiwa sana na uwepo wa soko la
kukuza mitaji kwa wajasiliamali (Enterprise Growth Market) ambalo limewapa fursa za kukuza mitaji
ya biashara zao kupitia soko la hisa.

6.1.3 Uwekezaji katika hatifungani.


Washiriki wa maonesho waliweza kufahamu ni namna gani serikali na makampuni yanavyoweza
kukopa fedha kutoka kwa umma. Kiasi cha chini katika kuwekeza katika hatifungani za muda mrefu na
mfupi. Washiriki waliweza kutambua ni namna gani wanaweza kushiriki katika aina iyo ya uwekezaji.

6.1.4 Uwekezaji katika mifuko ya UTT AMIS


Washiriki waliweza kufahamu faida, changamoto na namna ya kuwekeza katika mifuko ya uwekezaji
wa pamoja ya UTT AMIS ikiwemo mfuko wa umoja, watoto, jikimu, wekeza maisha, ukwasi na mfuko
wa hatifungani.

8
7.0 UJUMBE WA MGENI RASMI

Picha 4. Mgeni rasmi wa maonesho haya, Mr Suleman Malela kutoka Baraza la Taifa la uwezeshaji
kiuchumi akiwa katika meza ya Young Investors Forum

Katika meza yetu tulipata nafasi ya kutembelewa na mgeni rasmi wa maonesho


haya, Mr Suleman Malela kutoka Baraza la Taifa la uwezeshaji kiuchumi -
National Economics Empowerment Council (NEEC) (www.uwezeshaji.go.tz). Mgenj
rasmi alipendezwa Sana na kazi inayoifanya YIF ya kuelimisha umma hasa
vijana kushiriki katika masoko ya mitaji Tanzania.
Pia alisema, kazi ambazo YIF inaifanya ni njia mojawapo ya kutekeleza sera
namba sita ya Balaza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi, amabyo inasema,
nukuu

" Privatisatision
1 Issue
Tanzanian citizens have not been effectively involved in the privatisation
process.
2 Statement
The Government will design strategies to be used to assist Tanzanians to
own property or
purchase shares in state enterprises.
3 Strategies
The Government will take measures which will ensure that Tanzanians are
empowered and are
able to purchase shares in the state enterprises that are being privatised"

Hivyo akasema tunasaidia katika utekelezaji wa sera hii.


Mwisho alisema ataongea na Uongozi wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji naDhamana (CMSA)
waendelee kuisaidia YIF ili kuwafikia vijana wengi na
kuifanya YIF kuwa endelevu (sustainable)

9
8.0 MAOMBI NA MAONI YA WASHIRIKI.

Washiriki wote walishukuru sana huduma zetu na walitoa maoni na mapendekezo mbalimbali ikiwemo:-
 Maonesho na semina zinazotoa elimu ziwe zinafanyika mara kwa mara kusaidia kuongezeka
kwa washiriki katika masoko ya mitaji na fedha
 Washiriki pia walipendekeza jukwaa la mtandaoni (online forum) iweze kukamilika kwa haraka
ili kutoa nafasi kwa watu wengine waliopo mbali ambao hawawezi kufikiwa moja kwa moja’

Picha 5. Vitabu vilivyotumika katika maonesho

10
9.0 HITIMISHO

Hatuna budi kushukuru uongozi mzima wa UNI TRADE FAIR, uongozi wa chuo kikuu cha dar es
salaam ndaki ya technolojia za habari na mawasilianao.(CO-ICT) na washiriki wote walioweza
kujitokeza. Pia shukurani za kipekee kwa wafadhili wetu , Mamlaka ya masoko ya Mitaji na Dhamana
(CMSA). Uongozi wa Young Investor Forum unaahidi kuendelea kufanya majukumu yake kwa ufanisi
zaidi kuweza kuwafikia watu wengi zaidi.

“Learn|Practice|Invest”

11

You might also like