Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 3

MAGONJWA YA KUAMBUKIZA YA ZINAA SWAHILI

Sexually Transmitted Infections

Magonjwa ya kuambukiza ya zinaa (STIs) ni magonjwa yanayosababishwa na vijidudu (vijidudu vidogo) vinavyoweza
kuambukia kutoka kwa mtu kufikia kwa mwengine kupitia kitendo cha zinaa, kulawiti na kulamba sehemu za siri.

KLAMIDIA *
• Ugonjwa wa kuambukiza (STI), unaosababishwa na bakteria.
• Mara nyingi hauna dalili.
• Unaweza kutokeza maumivu wakati wa kukojoa, usaa utoka kwenyi uume ama uke, ao maumivu kwenyi pande ya chini
ya tumbo ya mama.
• Unaweza kuwa hatari kwa maana unaweza kusababisha ugonjwa wa maumivu ya kiuno kwa wakinamama na uondoa
rutuba kwa wakinababa na wakinamama ikiwa kama hawakutibiwa.
• Uvumbuliwa haraka kupitia vipimo vya mkojo ao pamba.
• Unatibiwa na antibiotiki.
• Waliojamiana wanalazimika kutibiwa ili kuepukana na maambukizi ya magonjwa.

Vivimbe vigumu kwenye sehemu za siri


• Yasababishwa na virusi vya mtu vya aina papiloma (HPV).
• Vinaweza kujitokeza kama glopu kandokando ya kuma ao ndani ya sehemu ya siri ya uke, kwenyi uume ao kandokando
na ndani ya mkundu.
• Yanawezakutoleta maumivu Au kusababisha muwasho.
• Vivimbe vigumu vinavyoonekana vinaweza kutolewa kwa kuviwekea baridi nyingi ao kuvipakaa rangi maalumu.
• Tukio za kurudilia zinaweza kujitokeza zikiwa na dhiki ao magonjwa.
• Sio viungo vyote vinaonekana.
• Baadhi ya virusi sugu vinaambukiza mlango wa kizazi na baada ya muda vinaweza kusababisha kansa ya kizazi.

Virusi vya herpes vinavyohathiri sehemu za siri


• Usababishwa na virusi vya herpes.
• Kila mara ujitokeza kama lengelenge yenye maumivu mwanzoni, hugeuka kuwa madonda maanga na yenye kufunikwa
kwa ganda gumu na upona.
• Tukio la kwanza linakuwa mbaya zaidi na linaweza kudumu wiki mbili. Bahadhi ya watu hawapati tukio lingine.
• Tukio za kurudilia mara nyingi hazina hasara na zaweza kusababishwa na inaweza kuleta dhiki ao magonjwa.
• Ijapokuwa vidonda vinawezakupotea, virusi vinaweza penginepo kubaki mwilini kwa mda wote wa maisha.
• Dawa maalum dhidi ya virusi yaweza kuagizwa na daktari kwa matibabu ya matukio. Vidonge vinaweza kutumiwa kwa
kukinga matukio mengine.

Kisonono *
• Husababishwa na bakteria.
• Inaweza kusababisha kuongezeka kwa usaa ndani ya uke ao maumivu makali ya chini ya tumbo kwa wakinamama na
kutoka kwa usaa kwenyi uume ao maumivu makali wakati wa kukojoa kwa wakinababa.
• Inaweza kutokuwa na dalili.
• Inatambuliwa haraka kupitia vipimo na hutibiwa na antibiotiki.
• Magumu yanaweza kujitokeza kama hakuna matibabu.
• Matibabu ya haraka dhidi ya mgonjwa na mwenzi wake ni ya muhimu kwa kuzuia maambukizo.

Kaswende *
• Husababishwa na bakteria.
• Matokeo ya mwanzo yanaweza kuleta kidonda kwenye sehemu za siri.
• Upele kwenye ngozi, kungoleka nyele sehemu mbalimbali kichwani, kusononeka kwa mwili ao kuotwa na majipu zenye
unyevu kandokando ya sehemu za siri na mkunduni zinaweza kujitokeza baadaye.
• Inatambuliwa kwa dalili na kupimwa damu.
• Hutibiwa na antibiotiki.

Sexually transmitted infections: Swahili Page 1 of 3


Last updated: June 2012
Trichomonasi
• Usababishwa na vijidudu.
• Inaweza kusababisha kutoka kwa maji mepesi, yenye rangi ya mchanganyiko njano na kijani yanayotoka ukeni na
yanayoweza kusababisha maumivu makali na harufu mbaya. Wakinababa wanawezakupatikana na hali ile ile ao bila
dalili hata moja.
• Uvumbulikana haraka kupitia vipimo.
• Matibabu ya haraka dhidi ya mgonjwa na mwenzi wake ni ya muhimu kwa kuzuia maambukizo.

Papasi na vigaga kwenye sehemu za siri


• Papasi ao vigaga ni aina ya chawa ndogo zipatikanazo kwenye katika mavuzi, mapaja ya juu na kwapani. Mayai yana
ukubwa wa milimeta moja and yanaonekana kwenyi chongo ya nyele.
• Vigaga ni torotoro wadogo wanaotoboa ngozi kwa kutaga mayai. Hii inaweza kutokea mahali popote kwenye ngozi.
• Zote husababisha muwasho mkali.
• Zote uambukizwa kwa kukaribiana na siyo kila mara kwa njia ya zinaa.
• Matumizi ya dawa ya kupaka mara moja ao mbili kwenyi ngozi kutauwa vidudu na mayayi kila mara.
• Waweza kutapakaa kwa kutumia kwa pamoja shuka, blanketi nguo na taulo zisizo safi.
• Yeyote alieweza kukaribiana na aliepatikana anaitaji matibabu.

Virusi vinavyosababisha ukimwi na ukimwi *


ƒ Virusi vinavyosababisha ukimwi na ukimwi. Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini.
ƒ Virusi vya ukimwi uambukiza kupitia mwili uilioathirika, maji ya mwilini (damu, shahawa, maji kutokea ukeni, na
mkunduni). Uambukizaji huyu unaweza kujitokeza kupitia zinaa ao njia nyingine kama vile kuchangia shindano.
ƒ Watu wanaopatikana na virusi utokewa na kinga mwilini (nguvu ilio mwilini inayopigana dhidi ya vijidudu) na wanaweza
kuugua mafua kwa mda mfupi.
ƒ Vipimo vya damu vinaweza kugundua virusi kutoka miezi mitatu kiisha kuwepo kwa virusi ndani ya damu.
ƒ mtu anapokuwa na virusi vya ukimwi inaimanisha anaweza kuambukiza wengine. Haiimanishi ya kwamba yupo
muhathirika wa ukimwi. Ukimwi unaweza kukua mwilini kwa kipindi cha myezi ao myaka baada ya kuambukizwa na
virusi.
ƒ Dalili za ukimwi zaweza kuwa kutoka kwa jasho mara kwa mara, kupoteza uzito, kukohoa, kuharisha, madonda ao
uvimbe.
ƒ Japo kuna matibabu kwa kulinda afia ya walioathirika na virusi vya ukimwi pia ukimwi, hakuna kupona.

Homa ya manjano A
• Ugonjwa wa kuambukiza wa virusi unaoweza kuathiri maini.
• Utapanyika ukila kiwango kidogo cha mavi ya mtu alieathirika. (e.g. kulamba kandokando ya mkundu ao nafasi ingine ya
mwili ambao imeambatana na mkundu, kama vile vidole), pia utapanyika kupitia chakula na maji yalioathirika.
• Inatambuliwa kwa dalili na haraka kupimwa damu.
• Kuna chanjo ya kinga ya Homa ya manjano A

Homa ya manjano B *
• Ugonjwa wa kuambukiza wa virusi unaoweza kuathiri maini.
• Utapanyika kwa kupeana ugiligili wa mwili (damu, shahawa, uchafu utokao kwenye uke na kamasi za mkundu) wakati wa
kitendo cha zinaa kisicho na kinga kupitia uke, mkundu ao kulambula sehemu za siri na kuchangia shindano.
• Uvumbulikana haraka kupitia vipimo vya damu.
• Karibuni asili mbili juu ya mia ya Waustralia wana ugonjwa wa homa ya manjano B unaoweza kusababisha maini
kuathirika vikali.
• Kuna chanjo ya kinga ya Homa ya manjano B na matibabu yanapatikana.

Homa ya manjano C *
• Ugonjwa wa kuambukiza wa virusi unaoweza kuathiri maini na unaoweza kusababisha hasara kali.
• Haiainishi ya kwamba ni ugonjwa wa kuambukiza kwa maana hautapanyiki kwepesi kupitia zinaa. Unatapanyika kupitia damu,
hivyo kuchangia shindano, chale kwa kutumia shindano au kutoboa mwili kwa kutumia sindano / vifaa,, na hao wanaopewa damu
kuanzia 1990 wanaweza kuhatarika.
• Uvumbulikana kupitia vipimo vya damu.
• Musichangie shindano, wembe, miswaki ao vyombo vingine vinavyoweza kuambatana na damu.
• Mtu akiambukizwa home ya matumbo C inaweza kutibiwa. Kuwasiliana na homa ya matumbo C Baraza au kliniki ya 275 kwa
maelezo. Hakuna chanjo.
Sexually transmitted infections: Swahili Page 2 of 3
Last updated: June 2012
Kuzuia magonjwa ya kuambukiza
• Uwe tayari! Tumia mipira.
• Tenda kitendo cha zinaa kwa adhari. Ukamilishe ya kwamba shahawa, damu, ugiligili wa uke ao kutokea mkunduni
havimgusi patna mwengine.
• Jadiliana juu ya maambukizi yoyote ya zamani ya ngono na mpenzi wako.
• Kila mara tumia shindandano zilizo safi.
• Pakiwa vidonda, majipu ao vidonda kandokando ya kinywa ao kwenye sehemu ya siri, ao uchafu ukitoka usio wa
kawaida, epuka kuambatana na uke, mkundu na kulama sehemu ya siri ao kitendo chochote kinachoambatana na ngozi
ilioathirika.

Kutoa kulio kwa kawaida kwa wakinamama


Kila mwanamama utoa maji yanayosafisha na kuloanisha uke. Yapo safi ao yakiwa na rangi sawa kidogo na maziwa na
yanaonekana ya njano yakikauka. Sehemu ya siri inayo harufu ndogo. Kiwango cha ugiligili kitokacho kwenyi uke ubadilika.
Ongezeko yaweza kutukia wakati fulani, ikiwemo:
• kwenyi kipindi cha kati cha hedhi mbili
• wakati ya matumizi ya vidonge vya kuzuia mimba ao chombo cha kuingiza ndani ya uterasi
• kwenyi kipindi cha mimba

Kutoa kwa kawaida kwa wakinababa


Tofauti ya mkojo na shahaba, wakinababa kawaida hawatoi uchafu mwengine kwenye uume. Wakinababa wasiotairiwa utoa
kiwango kidogo cha smegma, ilio na kazi ya kulainisha na kusafishia chini ya ngozi. Sehemu ya siri inayo harufu ndogo, ilio
ya kawaida.

Lini kumuona daktari


Unapashwa kumuona daktari wakati vitambulisho vya magonjwa ya kuambukiza vinajitokeza kwa mara ya kwanza ao ikwa
patna uliehusiana naye kupitia zinaa anavumbuliwa na magonjwa ya kuambukiza ao yupo na vitambulisho vya hayo
magonjwa. Hata kama huna dalili, unaweza kufanyiwa unchunguzi wa magojwa ya zinaa kwa daktari au kliniki ya afya.

* Magojwa ya zinaa yanayotambuliwa


Baadhi ya magonjwa ya zinaa yabatambulika (Klamidia, Gonorrhoea, Kaswende, VVU / UKIMWI, Homa ya manjano BC).
Hii ina maana kuwa mtu yeyote akikutwa na maambukizi haya atatakiwa kutoa mawasiliano yao ya kujamiiana katika kipindi
cha miezi 3-6. Watu hawa binafsi watafikiwa kwa mawasiliano (taarifa) kueleza hatari ya kuambukizwa na haja ya upimaji
na tiba kama inafaa.

Habari zaidi
Kwa habari nyingi zaidi kuhusu magonjwa ya kuambukiza uhusiane na Clinic 275:
Tel: 8222 5075
Wanaoita inchini: 1800 806 490
Address: 275 North Terrace, Adelaide
Website: www.stdservices.on.net

Njia ya kuhusiana na Shine SA


East/West Primary Health Care Team: 8300 5300
Northern Primary Health Care Team: 8256 0700
Southern Primary Health Care Team: 8186 8600
Library & Resource Centre: 8300 5312
SHine SA’s Sexual Healthline
Upatikana 9 am – 1 pm, Monday – Friday
Tel: 1300 883 793
Wanaoita inchini (bila malipo): 1800 188 171
Email: sexualhealthhotline@health.sa.gov.au

Ukiitaji mkalimali unaweza kuita idara inayohusika nayo kwenyi namba


131 450 mwanzo wa kuomba uunganishwe na 1300 883 793.

Website www.shinesa.org.au

Sexually transmitted infections: Swahili Page 3 of 3


Last updated: June 2012

You might also like