Professional Documents
Culture Documents
KESI YA ELIZABETH MOHAMED Vs ADOLF JOHN MAGESA, KWA KISWAHILI
KESI YA ELIZABETH MOHAMED Vs ADOLF JOHN MAGESA, KWA KISWAHILI
Haya ni baadhi ya maswali machache ambayo utapata majibu yake ndani ya hii kesi.
1: Je, mtu anaweza kufunga ndoa inayoruhusu kuoa mke mmoja tu, na baadaye akaoa tena mke
2: Je ndoa ya Kikristo nayo ni ndoa ya mke mmoja inayotambulika kwenye Sheria ya Ndoa au ni
3: Je, ukifunga ndoa ya Kikristo, sheria inakukataza kuoa tena mwanamke au wanawake wengine?
4: Je, ukifunga ndoa ya Kiislam, tayari (automatic) unakuwa umeruhusiwa kisheria kuoa
5: Au je, ukifunga ndoa ya Kiislam ina maana huwezi kuoa wanawake zaidi ya wanne? Je sheria
6: Sheria gani itatumika kugawa mirathi kwa Mkristo akifa bila kuacha wosia? Je Wakristo wana
profession.
-Marehemu, John Cosmas Magesa, alikuwa anafanya kazi ya utabibu (medical officer).
-Ndoa yao ilibarikiwa kupata watoto wawili (Adolf John na Anna John).
-Lakini huyu mwanamume, kabla hajafa alikuwa anaishi na wanawake wengine wawili, mmoja
anaitwa Elizabeth Mohamed, ambaye hadi alifunga naye ndoa ya kimila, akalipa mahari Shilingi
-Hivyo marehemu alikuwa na wake watatu, wa ndoa mmoja na wengine wawili pamoja na watoto
watano jumla
-Mgogoro ulikuwa ni je, hawa watoto watatu ambao marehemu alizaa na yule mwanamke
-Mahakama ya Mwanzo iliamua kwamba, wale watoto watatu ambao huyu mwanamke alizaa na
hawastahili.
-Mahakama ya Wilaya ikasema hivi, “ikiwa huyu mwanamke na marehemu walikuwa na
mahusiano ya kimapenzi, wale watoto watatu waliozaa walizaliwa kwenye mahusiano ya uzinzi
mwanamke na watoto wake haramu kushiriki matunda ya mirathi ya marehemu iwekwe kando.”
Elizabeth ametinga Mahakama Kuu, analalamika kwamba, Mahakama ya Wilaya ilikosea kuamua
kwamba, watoto aliozaa na marehemu walikuwa haramu hivyo hawana haki ya kurithi.
-Kumbuka mgogoro Mahakamani sio uhalali wa ndoa ya pili aliyofunga marehemu, ila ni uhalali
-Wakili wa huyu Mwanamke akaiambia Mahakama kwamba, irejee maamuzi yake kwenye kesi
nyingine ya Chacha Malima dhidi ya Mwita Kitogo ya mwaka 1986, ukurasa wa 119 ambapo
Mheshimiwa Jaji Katiti kwenye hiyo kesi, alizungumzia jinsi ya kuhalalisha mtoto haramu.
-Jaji Katiti alisema, kwa mujibu wa vifungu vya 181A and B vya sheria ya kimila, (the Customary
Law (Declaration) order 1963), kuna njia mbili ambazo zinaweza kutumika kumhalalisha mtoto
haramu.
-Ambapo baba wa mtoto (kibayolojia) aliyetajwa na mama au ambaye anakubalika kama baba
1: Moja, ama kwa kumuoa mama wa mtoto (by either marrying the mother).
2: Au, pili bila kumuoa mama wa mtoto ila kwa kulipa shilingi 100 (or without marrying the child’s
haramu haijapigwa marufuku na Mahakama nchini. Mi nakuelezea kesi husika kama ilivyokuwa)
-Tuendeleee.
-Kwa kifupi Mahakama ikasema, vitu vya kuzingatia ili kuamua haki ya mtoto kurithi ni ama,
marehemu awe ni baba kibayolojia (biological farther) au anayekubalika kuwa baba wa mtoto (or
-Na kwenye hii kesi, vyote viwili vilikuwepo, maana marehemu alikuwa baba mzazi (kibayolojia)
-Na hata Adolf, kijana wa marehemu anakubali hilo kwa maelezo yake aliyotoa Mahakamani
ambapo alisema, “Marehemu alikuwa na miji mitatu, mkubwa ukiwa Magu. Katika mji wa katikati
kuna watoto lakini sipaswi kuwaweka katika faili hili kwa kuogopa kutenda dhambi kushuhudia
-Adolf alichokuwa anapinga ni uhalali wa ndoa ya marehemu baba yake na hao wanawake
wengine.
-Anasema, kwa sababu baba yake alikuwa Mkristo na alikufa na kuzikwa Kikristo, hiyo ndoa yake
ya pili sio halali, hivyo hata hao watoto waliopatikana huko ni haramu.
- Kabla ya kuendelea kuamua kuhusu uhalali au uharamu wa watoto ambao Elizabeth Mohammed
alizaa na marehemu, Jaji akaanza kwanza na hoja ya ndoa kati ya marehemu na huyu mwanamke.
-Akaanza kuichambua sheria ya ndoa, akasema “kwa mujibu wa kifungu cha 38, kifungu kidogo
cha kwanza, aya c (Section 38(1) c) of the Law of Marriage Act [Cap 29 R.E. 2002] (sasa hivi ni
R.E 2019).
Shughuli yoyote yenye mwelekeo wa kuwa ndoa ni batili kama, mmoja wa wahusika ana ndoa
Section 15(1) ya sheria hiyo hiyo inasema, hakuna mtu ambaye ameoa kwa aina ya ndoa
inayoruhusu mwanamke mmoja tu, atakayeruhusiwa kufunga ndoa nyingine tena (no man while
-Kijana wa marehemu anadai kwamba hiyo ndoa nyingine kati ya marehemu na Elizabeth
Mohammed ni batili kwa sababu bado kulikuwa na ndoa nyingine inayoendelea kati ya baba yake
-Na mke wa kwanza Juliana Gerald (mama yake Adolf) alishuhudia mbele ya Mahakama ya
Mwanzo akidai alikuwa mke halali wa marehemu, lakini hakutoa ushahidi wowote kama vile cheti
cha ndoa au kithibitisho chochote n.k, ili Mahakama ijue kama aina ya ndoa waliyofunga ni ile
-Jaji akasema, ingawa hoja hii haikupingwa Mahakamani, lakini kukosekana kwa huo ushahidi,
na ukizingatia mwenzi mmoja wa ndoa ni marehemu hawezi kuja kutoa ushahidi, basi haikuwa
sahihi kwa kitendo cha Mahakama ya Wilaya kubatilisha maamuzi ya Mahakama ya Mwanzo na
-Jaji akaendelea kusema, haitoshi tu Juliana kuiambia Mahakama kwa mdomo kwamba aliolewa
YA KIKRISTO NA NDOA YA MKE MMOJA ni kitu kile kile? (Whether Christian Marriage is
the same thing as Monogamous marriage contemplated under the provisions of Section 15(1) of
kwamba ilikuwa halali kisheria au la, au je kwamba marehemu angeweza kuoa mke mwingine
wakati kuna ndoa ya kwanza ya Kikristo kati yake na Juliana Gerald? (Issue haikuwa hiyo).
-Ila mgogoro ni kuhusu hawa watoto marehemu aliozaa na Elizabeth Mohammed, je wana haki ya
-Mahakama ikasema, ingawa huo ndo mgogoro hapa, lakini bado ilikuwa ni muhimu kwa
wawili, ili iweze kuamua vizuri hadhi (status) ya wale watoto wa marehemu kwenye mirathi ya
baba yao.
- “Tuchukulie kwa mfano, kwamba marehemu alikuwa na ndoa ya Kikristo inayoendea na Juliana
Gerald, swali linalofuata ni je, hiyo tu inaweza kuwa sababu tosha ya kubatilisha ndoa yake ya pili
(ya kimila) na Elizabeth Mohammed, hivyo kufanya watoto aliozaa naye wawe haramu?” Aliuliza
Mheshimiwa Jaji.
- “Kama nilivyokwisha sema, hoja ya ndoa ya Kikristo na Juliana sio mgogoro kwenye hii kesi,
lakini hadi kufikia hapa, nalazimika awali ya yote, ku deal (kushughulika) na hii hoja, ambayo
kwa mawazo yangu, hupelekea mkanganyiko mkubwa sana katika mahakama zetu.” Alisema
Mheshimiwa Jaji.
- “Pili, nitajadili hoja ya watoto wanaozaliwa katika mahusiano kama hayo aliyokuwa nayo
Jaji akaendelea kusema, “kuoa kwa kulingana na imani ya dini ya mtu ni suala la kiimani zaidi
kuliko kisheria… Na masuala ya imani au dini yanalindwa na Katiba, lakini yako nje ya Mamlaka
ya Mahakama.”
-Mfano, Mahakama haiwezi kumuuliza mtu kwa nini ameamua kubadili dini au kwa nini hashiki
-Ibara ya 19(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inampa mtu haki na uhuru wa
- “Ibara hiyo ya 19(1) inahusisha pia na haki ya kuchagua kushika au kutoshika baadhi ya maagizo
-Mfano Muislam ana uhuru na haki ya kuchagua kutii au kutotii utaratibu wa kuswali swala tano
kwa siku, na maamuzi yake hayawezi kuhojiwa katika Mahakama yoyote, kwa sababu uhuru na
haki yake vinalindwa Kikatiba. (Lakini hana huo uhuru au haki kwenye Qur'an).
-Vivyo hivyo, Mkristo, mfano marehemu John Cosmas Magesa kwenye hii kesi, alikuwa na haki
na uhuru Kikatiba, wa kufata au kutofata kanuni ya mume mmoja - mke mmoja (had the right and
freedom under the Constitution of this country to observe or not to observe the Canon norm of one
-Mahakama Kuu ikasema, “Kuna kifungu kwenye Biblia, ambapo Yesu aliulizwa na Mafarisayo
-Yesu alijibu kwa kuwauliza swali, “Musa aliwaamuru nini?” Waliposema, “Musa alitoa ruhusa
- Yesu akawaambia, “Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii. Lakini tangu
mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha
Yesu Akawaambia, kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake, na mke,
-Kwa hiyo kwa mujibu wa Biblia, kitendo cha marehemu kumuoa Elizabeth, ilikuwa ni uzinzi,
kulalamikiwa na Juliana Gerald (mke wake) ambaye ndiye walikuwa na mkataba wa ndoa, na eneo
-Vinginevyo, Juliana akitaka kulalamika mbele ya Mahakama ya kisheria, basi lazima atoe cheti
cha ndoa, kuthibitisha kwamba, ndoa yao haikuwa tu ya Kikristo, ila pia ya mke mmoja tu. (Upon
producing a certificate of marriage certifying that their marriage was not only a Christian, but also
a monogamous marriage).
-Lakini kama marehemu alimuoa Juliana ndoa ya Kikristo, na kama ndoa ya Kikristo inakataza
kufunga ndoa ya pili wakati bado ile ya kwanza haijavunjika, hilo ni suala la kuamuliwa na
Mahakama za Kanisa.
-Jaji akaendelea kukazia hii hoja, akasema “Imekuwa kawaida kwa mahakama zetu, zinapokutana
na kesi inayohusu ndoa, zinachukulia kwamba, ikiwa watu wameoana ndoa ya Kikristo basi lazima
itakuwa ya mke mmoja tu (that where the parties are married according to Christian rites, the
- Na ikiwa watu wameoana ndoa ya Kiislam, ndoa yao lazima itakuwa ya wanawake wengi (and
where parties are married in accordance with Islamic law, their marriage must be polygamous
one).
-Hiyo haiko hivyo wakati wote, (that is not always the case and courts should never make findings
on assumption where there are specific prescribed procedures for proving the alleged facts).
-Mahakama zisiwe zinatoa maamuzi kwa kudhani/kukisisia pale kunapokuwa na hatua maalum
-Kisheria, hadhi na uwepo wa ndoa vinaweza tu kuthibitishwa kwa kutoa Mahakamani cheti cha
ndoa au kupitia kutoa ushahidi wa ndoa kama ilivyoelezwa katika kifungu cha 55(a) cha Sheria ya
Ndoa.
-Kisheria, ndoa ya Kikristo na ndoa ya mke mmoja haimaanishi ni kitu kimoja. (In law Christian
marriages & monogamous marriages are not necessarily the same thing.
-Jaji akasema, Mahakama katika nchi hii hazina mamlaka ya kuhoji migogoro ya ndoa za Kikristo,
-Mfano, sio wajibu wa Mahakama hii kumuuliza mwanamume Mkristo, kwa nini ameshindwa
kufata kanuni inayomtaka mwanamume kuoa mke mmoja tu? Hili ni suala la kidini, ambalo
-Mahakama zijikite tu kuamua ndoa ambazo zimefungwa kwa mujibu wa sheria ya ndoa, bila
Mwisho, Jaji akamalizia hii hoja kwa kusema kwamba, njia pekee iliyopo ya kuhoji kukosa utii
kwa marehemu juu ya dini yake, itakuwa ni siku ya UFUFUO, mbele ya Mwenyezi Mungu.
-TURUDI KWENYE MGOGORO WA KESI SASA
-Baada ya hayo, Jaji akaja sasa kuamua suala ambalo ndo mgogoro hasa kwenye hii kesi.
yalikataza watoto waliozaliwa nje ya ndoa kurithi, kama vile maamuzi ya Mahakama ya Rufani,
kwenye kesi ya Violet Ishengoma Kahangwa and Jovin Mutabuzi v. The Administrator General
-Jaji akasema, hadhani kama maamuzi kwenye hiyo kesi bado ni sheria nzuri kwa Tanzania leo
hii. Hasa baada ya kutungwa kwa Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, kifungu cha 5, 9 na 10.
-Kwa sababu wakati maamuzi hayo yanafanyika Sheria ya Mtoto ya mwaka, 2009 haikuwepo.
-Pia maamuzi hayo yalijikita (walitumia) sana kwenye sheria za kimila za Wahaya, ambazo
zilikuwa zinakataza watoto haramu kurithi, ambayo ndio sheria pia iliyotumika mwaka 2010, na
Mahakama ya Wilaya kwenye hii kesi kuwakataa wale watoto wa Elizabeth wasirithi.
-Mahakama ikasema, sheria ya kimila ya Wahaya kwa wakati huo haikuwa kwa kweli inapingana
-Lakini kwa sasa, sheria kama hizo zinazokataa watoto waliozaliwa nje ya ndoa kurithi
-Hivyo, Mahakama ikasema sheria ya Kimila ya Wahaya iliyotumika kwenye hii kesi na
Mahakama ya Wilaya kuwakatalia watoto waliozaliwa nje ya ndoa wasirithi haifai, kwanza
ambaye amezaliwa na wazazi ambao hawajaoana, ambapo kimsingi inamaanisha sio mtoto halali
kisheria. (It is discriminative and inhumane to call a child born of parents who are not married to
each other an illegitimate child which in essence means that he/she is an unlawful child.
-Mahusiano ya wazazi yanaweza kuwa haramu au sio halali kisheria, kulingana na kanuni za jamii
au dini husika, LAKINI KILICHOPATIKANA katika muungano huo, yaani binadamu aliyezaliwa
kama matokeo ya mahusiano hayo, hawezi kwa maana yoyote kisheria kuwa sio halali katika taifa
lisilo na mfungamano wa itikadi kama la kwetu. (The association of the parents may be illegitimate
or unlawfully according to the norms of a given society and/or religion but the product of such
association, that is a human being born as a result of such association cannot by any legal definition
-Bahati nzuri, watunga sheria wa nchi hii waliligundua hilo kosa la ukoloni, na wakafuta huko
kukataliwa kwa kutunga Sheria ya mtoto (the Law of Child Act, 2009).
-Utangulizi wa sheria hiyo unasema, ilitungwa kutekeleza (it was enacted to give effect) mikataba
-Kifungu cha 5(2) cha sheria hiyo (ya mtoto) kinapiga marufuku ubaguzi wa aina yoyote dhidi ya
mtoto.
-Kifungu cha 10 cha sheria hiyo hiyo kinampa mtoto haki ya kunufaika na mali ya mzazi wake.
-Kifungu cha 9 cha sheria hiyo hiyo kinampa mzazi wajibu wa kumtunza mtoto wakati wa uhai
wake. Na kuna ushahidi kwamba marehemu alitimiza wajibu wake kwa kuwatunza watoto wake,
Elizabeth hawana haki ya kurithi kwa sababu, Mkristo hawezi kuoa mke mwingine, wakati ndoa
-Mahakama ikasema hata ndoa ya huyu kijana na mama yake (Juliana-mke wa kwanza) pia haiko
-Mwisho, Mahakama ikaamua kwamba, hawa watoto watatu wa Elizabeth wanastahili kurithi.
-Mahakama ikakubali rufaa ya Elizabeth Mohammed, na kuamuru watoto wake waingizwe kweny
-Mwisho Mahakama ikahama kwenye hiyo hoja, ikaendelea kutafuta sheria gani itumike kugawa
-Wakatumia sheria ya serikali (Indian Succession Act) maana Wakristo hawana Sheria maalum
Yours sincerely,
Zakaria Maseke.
(0754575246).
(zakariamaseke@gmail.com)
-Hizi kesi zipo mtandaoni ukitaka kujiridhisha au kusoma mwenyewe, ila nyingi bado ziko kwa
-Kind regards-