Professional Documents
Culture Documents
CEOrt - Engagement With Hon. Makamba PR - August 2022
CEOrt - Engagement With Hon. Makamba PR - August 2022
Taarifa za hivi karibuni katika sekta ya nishati nchini ni pamoja na mipango kuhusu bomba la
EACOP, maendeleo ya mitambo ya gesi ng’ambo, makubaliano katika mradi wa gesi asilia
iliyosindikwa (LNG) na mapendekezo kadhaa ya mradi wa nishati mbadala. Katika wakati
ambapo mabadiliko ndani ya sekta ya nishati yanaendelea duniani, washikadau wanatilia
maanani matokeo yake kwa fursa zinazoibuka barani na pia maamuzi ya uwekezaji
yanayopaswa kufanywa. Awamu inayofuata katika sekta ya nishati nchini Tanzania inatarajiwa
kujikita katika kukuza uwekezaji na ukuaji, hivyo basi kuwafanya viongozi wa sekta binafsi kuwa
kipengele muhimu kwa kutegemea michango yao ya kimkakati na ushiriki wao katika kufungua
fursa chipukizi nchini.
CEOrt ina heshima kubwa kumkaribisha Mhe. January Makamba, Waziri wa Nishati wa
Tanzania, akiwa Mgeni Rasmi katika hafla hiyo. Mhe. Makamba amesisitiza azma ya Serikali ya
kuweka uwiano wa maendeleo ya nishati vijijini na mijini, na kutaja vipaumbele kuwa ni pamoja
na kuboresha ufanisi wa nishati sambamba na kuongeza utegemezi wa sekta hiyo, na kuhimiza
ushiriki wa sekta binafsi ya ndani katika mnyororo wa thamani wa nishati mbalimbali nchini.
Madhumuni mengine muhimu ya sekta hii ni kupunguza ukataji miti, lengo ambalo CEOrt
inakusudia kusaidia kulifanikisha kwa vile linaendana na msimamo wa jukwaa hilo wa kuchukua
hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.