UCHAMBUZI WA KITABU "The 21 Irrefutable Laws of Leadership-JOHN MAXWELL

You might also like

Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 16

UCHAMBUZI WA KITABU “The 21 Irrefutable Laws Of Leadership” (Sheria/Kanuni 21

Zisizopingika Au Kuepukika Za Uongozi) By Dr. John C. Maxwell.

UCHAMBUZI By Mary Assenga +255683246242 Whatsapp/Call

Katika Utangulizi Mwandishi John C. Maxwell anasema “Kati ya mambo ya


uhakika aliyojifunza katika miaka zaidi 30 katika Uongozi kabla hajaandika hiki
kitabu ni kwamba; Uongozi ni uongozi bila kujali ni wapi utaenda au ni nini
unafanya.

Nyakati zinabadilika. Teknolojia inaendelea kukua na kusonga mbele zaidi na


zaidi. Tamaduni zinatofautiana maeneo tofauti tofauti. Lakini sheria/kanuni za
kweli za uongozi zinabaki ni zile zile, iwe unaangalia raia wan chi ya Uyunani Ya
Kale au Ugiriki Ya Kale, iwe unaangalia Waebrania wa agano la kale, iwe
unaangalia majeshi ya miaka mia mbili iliyopita, iwe unaangalia watawala wa
Ulaya ya kisasa, iwe ni wanasiasa wa karne ya 21, iwe unaangalia wachungaji wa
makanisa yetu ya hapa nchini au unaangalia Wafanyabiashara wa uchumi wa dunia
ya leo. Sheria/kanuni za uongozi hazibadiliki. Hazipingika wala kuepukika.”

Kuna watu wanafikiri kuwa kiongozi mpaka upate nafasi fulani mahali fulani, ndio
ukipata nafasi fulani mahali Fulani ni nafasi ya kuonyesha una uwezo kiasi gani
kama kiongozi kadiri ya kukubalika kwako na mambo utakayofanikisha katika huo
uongozi wako. Lakini unaweza kuanza kuwa kiongozi hapo hapo ulipo kwanza
kwa kujiongoza mwenyewe vyema na kujisimamia katika mambo ambayo
umeshajiahidi utafanya. Lakini pia kama unazungumza na watu wanakusikiliza na
kukuamini na kukukubali na kufuata/kufanyia kazi mambo unayowaambia na
kuhitaji muongozo wako tena na tena basi wewe unaanza kuonyesha dalili nzuri
kwamba wewe ni kiongozi kwa watu hao, sasa kadiri utaendelea kusaidia na
kukubalika zaidi na kadiri utaendelea kukubalika na wengi zaidi na ukawa gumzo
zaidi kwa watu wengi wanaozikubali juhudi zako au mawazo yako basi wewe ni
kiongozi kwao, iwe ni kazini kwako, iwe ni shuleni kwako, iwe ni nyumbani,
kanisani, mtaani au hata hapa hapa facebook, utapendwa utaheshimiwa na
kuaminiwa na kadiri unavyowagusa au kuweza kuwashiwishi wengi ndivyo hata
unaweza kuwashawishi wafanya kitu fulani au wafautilia jambo fulani au
wenyewe kwa hiari yao wanaweza kufanya hivyo na ambavyo kwalo wewe
unaweza kunufaika na kupata mafanikio makubwa na wao pia wakafanikiwa.
Sasa twende pamoja tuzichambue kanuni hizi 21 zisizopingika za Uongozi,
ambazo mwandishi Dr. John C. Maxwell ametumia miaka mingi sana kujifunza,
kufundisha na baadaye kutuandikia kitabu hiki bora sana na kilichouzika kwa
mamilioni ya nakala duniani kote. Kupitia uchambuzi huu na wewe upate kujipima
na kuwapima wale wote waliopewa nafasi mbalimbali za Uongozi kama
wanaendana na kanuni hizi au wanazivunja na matokeo yake wanaweza kuanguka
au kushindwa kuendelea kuongoza kutokana na kuvunja kanuni hizi zisizopingika.

1. Sheria ya kizibo/mfuniko(The Law of the Lid), “Uwezo wa kiuongozi wa mtu


ulipoishia utaamua hatua au kiwango cha ufanisi cha mtu huyo katika kufanikisha
mambo”.
Ukiachana na uwezo wa kufanya mambo mengine lakini kuna uwezo wa
kuongoza, uwezo wa kufanya mambo kama kiongozi na kuleta mafanikio
makubwa, sasa unaweza kuwa nao mkubwa au kuwa nao mdogo kadiri
unavyokuwa nao mkubwa ndivyo uongozi wako unaweza kuwa na mafanikio
makubwa. Kwa mfano umeamua kufungua mgahawa na kuanza kuuendesha, una
mbinu zote za kuendesha mgahawa kuanzia kuweza kuhakikisha mnatengeneza
chakula bora kabisa chenya ladha nzuri sana, katika hali ya usafi wa hali ya juu, na
kwa muda sahihi kabisa, unajua namna ya kuzungumza na wateja vizuri, na unaju
kusikiliza na kutekeleza vizuri mahitaji ya wateja na mbwembwe zote za
kibiashara na ukapata mafanikio sana katika huo mgahawa wako na kupata kipato
kizuri tu lakini uwezo wako ukaishia katika kuusimamia na kuuendesha huo
mgahawa mmoja na ukashindwa kutanuka zaidi ya hapo na kufungua maeneo
mengine zaidi na zaidi.

-Sasa kwa mtu mwenye uwezo mkubwa wa uongozi ataweza kutanuka zaidi akawa
na mbinu bora na za uhakika za kuweza kufungua matawi na kuzidi kutanuka
kidogo kidogo huku akiendelea kutoa huduma yenye ubora ule ule kama ule
mgahawa wa mwanzo na kuzidi kukua mpaka kuenea mji mzima, kisha nchi nzima
mpaka nchi jirani na dunia kwa ujumla, yote hii inatokana na uwezo mkubwa wa
kuongoza watu wengi na kutengeneza namna ambazo wataendelea kukua zaidi na
zaidi kwa ubora huo huo.

-Au kiongozi amepewa nafasi ya kuiongoza taasisi labda ni ya kidini au shirika


binafsi au shirika la kiserikali, kama ana uwezo mkubwa wa kiuongozi anaweza
kulikuza na kwa kutumia ushawishi wake akiliimarisha na kulijengea misingi
imara sana ya kimfumo, kiutendaji, sambamba na kuanzisha michakato mbalimbali
inayoweza kulifikisha mbali na akabaki kukumbukwa sana kwa miaka mingi
mbele.
-Au inaweza kuwa ni kiongozi wa nchi, amepewa nafasi ya kuiongoza nchi utaona
jinsi anavyoweza kufanikisha mambo mengi ambayo yamekuwa ni changamoto na
kuyatatua kwa kushawishi mabadiliko, kutia saini sheria mbalimbali zinazoweza
kuleta mabadiliko chanya, kuanzisha michakato inayopelekea kuleta mabadiliko
katika nyanja mbalimbali na kutatua au kuzitengenezea njia za utatuzi changamoto
nyingi na sugu katika nchi na utaona jinsi watu wanakubaliana naye katika
kukabiliana na mambo hayo kwa vitendo. Sasa kama ana uwezo mdogo utaweza
kuona jinsi hana jipya mambo yapo vile vile tu hakuna matumaini wala dalili za
kutatua changamoto sugu ambazo zimekuwa zikiwaumiza watu kwa miaka mingi,
na utaona mivutano mingi, malalamiko, manung’uniko na kila namna ya watu
kutoridhishwa na namna nchi inaendeshwa.

-Kwa hiyo kadiri uwezo wako wa kiuongozi unavyozidi kuwa mkubwa ndivyo
kadiri unavyoweza kufanikisha mambo makubwa katika kile unachokiongoza
lakini kadiri uwezo wako wa kiuongozi unavyokuwa finyu ndivyo kadiri
utakavyokosa ushawishi na kuwa na mafanikio kiduchu sana na kushindwa kutatua
changamoto nyingi unazokutana nazo katika uongozi wako.

2. Sheria/Kanuni ya ushawishi(The Law of Infuence), “Kipimo Halisi Cha Uongozi Ni


Ushawishi” NA SIO VINGINEVYO.
-Ushawishi ni ile hali ya kukubalika, kuheshimika na kuaminiwa sana na watu kwa
mambo uliyofanya au unayofanya yakawagusa sana. Mtu anayependwa,
akazungumzwa na akaweza kuwashiwishi watu wafanye jambo fulani na
wakafanya kwa sababu wanamheshimu na kumuamini sana na kuwa tayari
kufanya lolote kwa hiari yao kutokana na ushawishi wake, huo ndio tunaita
ushawishi. Mara nyingi watu maarufu wako kwenye nafasi nzuri ya kuweza
kutengeneza ushawishi kutokana na namna wanaishi au mambo wanayofanya au
wakaharibu na kuonekana wasiofaa pia kadiri ya matendo yao na namna
wanavyoishi. Mwandishi ametoa mfano wa Princess Diana jinsi alivyokuwa mtu
wa kawaida na umaarufu wake ulianza baada ya kufunga ndoa na mtoto wa Malkia
Elizabeth wa Uingereza, Prince Charles mwaka 1981 ambayo ilitazamwa kupitia
luninga na zaidi aya watu bilioni 1 duniani kote. Kwa nafasi hiyo aliweza kukutana
na watu mbalimbali wakubwa duniani na aliitumia katika kusaidia kufanikisha
mambo mbalimbali yaliyopelekea kutatua changamoto nyingi zinazowagusa watu
duniani, hivyo umaarufu wake ulikuwa maradufu na alipendwa, kuheshimika na
kusikilizwa sana. Alikuwa akisaidia kuhamasisha michango mbalimbali
inayosaidia watu, kupigania sheria mbalimbali zenye maslahi kwa watu ambao
hawana sauti ya kutosha kujipigania na mambo mengine mengi ya kujitolea.
Mpaka kufikia mwaka 1996 wakati anaachana na mume wake alikuwa tayari ni
maarufu kuzidi familia ya kifalme ya mume wake na alipofariki mwaka 1997
msiba wake ulishuhudiwa na zaidi watu bilioni 2.5, yaani duniani kote, yaani watu
mara mbili zaidi ya wale walioishuhudia harusi yake. Huo ndio tunaita ushawishi.
Mwandishi pia amemzungumzia Mother Teresa akijaribu kuonyesha kuonyesha
maana halisi ya ushawishi.
-Colin Powell aliyekuwa (Secretary General) wa Marekani anasema “Unaweza
kusema umefikia kiwango cha juu cha uongozi endapo tu watu wataamua
wenyewe kukufuata kila mahali kwa sababu tu wanavutiwa sana na wewe”. Kwa
maana hiyo ukiweza kuwa na nguvu hiyo inakuwa rahisi kuwaambia watu wafanya
yale unayohitahi yafanyike wakafanya tena kwa kujitoa sana na kwa kukukubali,
au kukuunga mkono kwa moyo wote wakiamini njia mnayokwenda ndio wote
wanatamani kuiendea.
-Harry A. Overstreet anasema “Umuhimu wa nguvu ya ushawishi upo katika
kumfanya mtu ashiriki kile kinachopaswa kufanyika”. Kwa hiyo nguvu hii ya
ushawishi inaleta maana pale wewe kama kiongozi unaitumia kuhakikisha watu
wanashawishika kufanya yale muhimu na wanajitoa kiasi cha kuweza kufanya
vizuri sana kadiri ya wanavyohitajika kufanya.

3. Sheria/Kanuni Ya Mchakato(The Law of Process) “Uongozi Huendelea Kukua Kila


Siku Na Sio Siku Moja”.
-Uongozi sio kitu kinachokuwa siku moja, uwezo wa mtu kuongoza ni kitu
kinachoendelea kukua siku hadi siku kadiri mtu anavyoendelea kujifunza kupitia
uzoefu katika maeneo mbalimbali na kuimarika zaidi na zaidi kama kiongozi.
Kama wewe uko kwenye miaka ya 20 au 30 au 40 au hata mpaka 50 ujue uwezo
wako kiuongozi ni kitu kinaendelea kukua cha msingi ni wewe kujitahidi kujifunza
sana kadiri unavyoendelea kukabiliana na changamoto na hali mbalimbali katika
maeneo unayopitia katika maisha na hasa katika nafasi mbalimbali za uongozi
ulizopo, lakini pia unaweza kujifunza kupitia watu wengine walioko katika nafasi
nyingine za uongozi. Ndio maana utakuta hata nchi mbalimbali zimeweka kiwango
cha umri ambao watahitaji mtu kuwa nao ili kuwa na kigezo cha kuweza kushika
nafasi za uongozi kwa sababu wanategemea uwezo wake wa kuongoza utakuwa
umeshaimarika kiasi kinachoridhisha.
-Namna kiwango cha Uongozi kinavyokuwa kwa mtu ni kama vile uwekezaji wa
mtu unavyokuwa katika kampuni kama amewekeza uwekezaji wa aina ya
“compound interest” kwamba amewekeza kiasi fulani cha fedha kwa kununua hisa
sasa linapotoka gawio la faida yeye anawekeza tena na ile faida, kwa hiyo gawio
likija tena linakuja kubwa zaidi maana ile faida alitumia kununua hisa zaidi hivyo,
kisha gawio likija kubwa zaidi tena anarudisha zote na faida, kisha linakuja kubwa
zaidi tena, kwa maana hiyo baada ya muda utakuta uwekezaji wake umekuwa sana
na amezidi kutajirika sana kadiri ya muda unavyosonga mbele. Hivyo ndivyo
namna Uongozi wa mtu unavyokuwa, kama ni mtu anayejifunza uongozi basi
muda unavyokwenda uwezo wake unakuwa sana na anakuwa na uwezo wa
kufanikisha mambo mengi kadiri ya uwezo wake wa kiuongozi alioendelea
kuukuza kwa kujifunza kupitia uzoefu binafsi na uzoefu wa watu wengine walioko
katika nafasi za juu zaidi za uongozi.
-Kiongozi ni mtu anayejifunza kila siku, anaaza kwa kutojua kabisa mambo
anaendelea kufahamu na kuelewa michakato yake, anaendelea kujifunza kila kitu
kinachotokea na kujua nini kinatakiwa kufanyika pale jambo fulani linapotokea au
anapaswa kufanya nini na nini wakati gani. Ili kuweza kuwa kiongozi wa kesho
unapaswa kujifunza leo,na siku zote lazima uwe mtu wa kuchukua hatua. Mimi
mwenyewe ni mtu ambaye naendelea kupata mwanga kuhusu uongozi taratibu na
kupitia kusoma hivi vitabu vya uongozi naendelea kuelewa zaidi na zaidi na wakati
mwingine miaka kadhaa baadaye nikizungumzia uongozi nitakuwa nimeendelea
kuimarika zaidi na zaidi.

4. Sheria/Kanuni Ya Ubaharia (The Law of Navigation) “Mtu yeyote anaweza kuiwasha


Meli ikaanza safari, lakini inamhitaji kiongozi kuweza kuiongoza katika safari
nzima ya baharini iliyojaa kila aina ya misukosuko na hatimaye kuiweza kuimaliza
safari iliyokusudia”
-Kiongozi yeyote hufanya maandilizi kwa umakini mkubwa kabla ya safari
kuanza. Kiongozi hutumia uzoefu wa watu wengine katika jambo analotaka
kuliendea au analokabiliana nalo ili kulifanikisha katika namna na kwa kiwango
anachokikusudia. Kiongozi hutazama mpaka mwisho wa safari kabla hajaianza
safari. Leroy Eims anasema “Kiongozi ni Yule anayeona zaidi yaw engine,
anayeona mbali zaidi ya wengine, na anayeona kabla wengine hawajafanya”.
-Katika sheria hii ya mabaharia mwandishi anakwambia mabaharia huangalia
uzoefu wa siku za nyuma. Mabaharia husikiliza maoni ya wengine, kwa sababu
hata kama umejifunza mengi kiasi gani kutokana na uzoefu haitaweza kukwambia
kila kitu unachotakiwa kujua kwa ajili ya sasa. Mabaharia hutazama kwa makini
hali iliyopo kabla hawajaamua kuingia. Mabaharia hukakishi hitimisho lao
linawakilisha vyote imani na uhalisia, kwa sababu kujidanganya kunaweza
kuhatarisha maisha yao. Mwandishi anasema ni vigumu kutofautisha kati ya
matumaini na uhalisia, ubunifu/akili na mipango, imani na uhalisia lakini hayo
ndio yanayotakiwa ili kuwa bora katika safarini. Mwandishi anasema pia kama
kiongozi akishindwa kuwavusha katika nyakati za dhoruba baharini basi
ataizamisha meli.
-Mwandishi ametolea mfano wake mwenyewe yeye wakati akiwa kiongozi wa
kanisa baada ya kuhamishwa kutoka kanisa lingine na kuhamishiwa katika kanisa
hilo ambapo alikuta kuna uhitaji mkubwa wa kujenga kanisa lingine kubwa zaidi
kwani hilo lilikuwa linaelekea kushindwa kumudu waumini ambao walikuwa
wanaongezeka kwa kasi. Anasema alikuwa tayari ana uzoefu kiasi kwa sababu
alishafanya hilo wakati akiwa kwenye kanisa lake la kwanza lakini hili la sasa
lilikuwa ni kubwa sana ukilinganisha na lile na pia lina changamoto sana hasa
katika kuwashawishi watu wakubaliane na mpango huo wa kujenga kanisa kwa
sababu ni jambo lililowahi kujadiliwa lakini likaleta mtafaruku na mivutano na
halikuweza kufanyika. Mwandishi anasema alijitahidi kujipanga kwa kila kitu
kinachotakiwa kisha akawaita wale viongozi wote wenye ushawishi kila mmoja
kwa nafasi yake akakaa kaa nay echini na kujadili naye jambo hilo akajitahidi
kumshawishi kuhusu mchakato mzima kisha baada ya kuwa ameelewana na
viongozi wote akawaruhusu nao wakawashawishi waumini kila mmoja kwa
sehemu yake kwa kuwaeleza na kusisitiza hasa yale maeneo yanayoonekana kuzua
maswali na mijadala na mwisho wengi wakaelewa, na ndipo walipoitisha mkutano
mkuu kuwasilisha taarifa kamili na mpango mzima wa mradi huo huku akiwa
amejibu maswali mengi ambayo yanaweza yakaulizwa baada ya kuwakilisha
katika maelezo yake. Mwisho kazi ilikuwa rahisi kwa zaidi ya 98% waliunga
mkono na mradi ukaweza kufanyika vizuri na kufanikiwa bila tatizo. Haya
tunasema ni maandilizi mema kabla ya kuanza safari.

5. Sheria/Kanuni Ya E. F. Hutton (The Law of E. F. Hutton), “Kiongozi Halisi Akiongea,


Watu Husikiliza”.
Kiongozi wa kweli anayo nguvu ya kusikilizwa na watu na sio tu nafasi ya
uongozi. Kama ukiona kuna utofauti mkubwa kati ya anayeongoza kikao na
anayesikilizwa na watu, basi anayeongoza kikao sio kiongozi halisi. Ushahidi wa
kwamba mtu ni kiongozi halisi upo katika wafuasi wake.

6. Sheria/Kanuni Ya Iliyojichimbia Chini Kabisa Ardhini. (The Law of The Solid Ground)
“Imani Kwa Kiongozi Ndio Msingi Wa Uongozi”
-Linapokuja suala la uongozi, huwezi tu kupita njia za mkato kupelekesha watu, ni
lazima upitie mchakato mzima wa kuwaelewesha lengo na umuhimu wa kila
utakachofanya, tofauti na hapo watakosa imani na wewe, kukubeza na mwisho
kukupuza na kukataa kukusikiliza. Kujenga imani kiongozi lazima aonyeshe
mfano kwa kuwa mahiri, kujenga mahusiano na mwenye sifa njema. Ni vigumu
kwa kiongozi kufika mbali zaidi ya zile tabia au hulka zake.
-Ni kwa namna gani viongozi huheshimika? Ni kwa kufanya maamuzi sahihi,
kukubali makosa na kuyapa kipaumbele maslahi ya wafuasi wao na taasisi au jamii
kuliko ajenda zao binafsi. “Kitu pekee kinachotoka nje ya kaburi na kuungana na
waombolezaji na kukataa kuzikwa ni sifa au tabia za mtu huyo”. Sifa bora za
kiongozi hujenga imani kwa wanaongozwa. Kwanza watu hujenga imani na
kiongozi ndipo humuunga mkono. Na kiongozi yeyote anapovunja imani kwa
wafuasi wake ni lazima atalipa gharama kubwa sana kuirudisha imani hiyo.
7. Sheria/Kanuni Ya Heshima, (The Law of Respect) “Kwa Asili Watu Hufuata Viongozi
Imara Kuliko Wao”
-Kwa asili kabisa mtu akiwa kiongozi bora zaidi watu ambao ni bora kuliko wao
hujikuta wanamfuata bila kujali cheo chake, rangi, au hata kiwango cha elimu,
anaweza kuwa hata ni mfanyakazi wa ndani, mkulima, mwanafunzi au hata
mhudumu wa mgahawa lakini kama ameonyesha kuwa kiongozi imara watu
hujikuta wanamfuata na kumheshimu kuliko hata viongozi wakuu wa nchi endapo
viongozi hao wameonyesha udhaifu katiak uongozi wao.
-Watu wanapomheshimu mtu kama mtu, huvutiwa naye. Wanapomheshimu kama
rafiki, humpenda. Wanapomheshimu kama kiongozi humfuata. Kadiri mtu
anapokuwa na uwezo mkubwa wa kuongoza ndipo kadiri anapoweza kuona
kiwango cha uwezo wa kuongoza kwa wetu wengine.
-Kiongozi ni lazima awe anajua, na anatakiwa awe anajua kwamba anajua, na
anatakiwa awe ana uwezo wa kudhihirisha na kuwaonyesha watu vizuri kabisa
kwamba anajua. Kipimo cha kujua kama kiongozi anaheshimika kiasi gani ni pale
atakapokuwa anafanya mabadiliko makubwa katika uongozi wake.

8. Sheria/Kanuni Ya Akili Za Kujiongeza (The Law of Intuition), “Viongozi Huamua Kila


Kitu Kwa Faida Ya Kiuongozi”.
-Kiongozi anatakiwa kuwa na uwezo wa kuisoma hali iliyopo na kujua nini
kinapaswa kufanywa hata kama watu wengine bado hawajaona ili kufanikisha
lengo linalotazamiwa. Kiongozi anatakiwa kuwa na uwezo wa kubadilisha hali
mbaya iliyopo kwa kujiongeza kiakili kujua nini kinapaswa kufanywa kubadilisha
namna mambo yanaenda. Watu huwa wanahitaji lengo kutoka kwa kiongozi wao
kuhamasika.
-Uwezo wa asili pamoja na kujielimisha sana kunaitengeneza akili iwe na uwezo
wa kujiongeza ambayo inafanya mambo ya kiungozi yaonekana katika mtu.
Viongozi wanaotaka kufanikiwa huongeza thamani ya kila rasilimali waliyonayo
kwa faida ya taasisi au shirika wanaloliongoza. Kitu utakachoona kitasababishwa
na wewe ni wa namna gani, kama una wewe ni kiongozi utaona kwa namna tofauti
na wengine wanavyoona.
-Kila mara viongozi halisi wanapokutana na tatizo, kwa kawaida huwa wanalipima
tatizo na kuanza kulitatuta kwa kutumia sheria hii ya akili za kujiongeza.
Maboresho na maendeleo hayawezekani bila kubadili uongozi.

9. Sheria/Kanuni Ya Sumaku (The Law of Magnetism), “Namna Vile Ulivyo Wewe Ndio
Aina Ya Watu Utakaowavutia”.
-Kila mtu anapenda kufanya kazi na watu wa tabia fulani fulani au aina fulani
Fulani, mtu atakwambia mimi napenda kufanya kazi na mtu mchangamfu, mtu
bora, napenda kufanya kazi na watu wazima zaidi sipendi vijana, mwingine
atakwambia mimi napenda zaidi kufanya kazi na vijana au mtu msafi lakini huwa
hajiangalii yeye ni mtu namna gani. Sheria namba tisa ya uongozi inakwambia
namna ulivyo ndio aina ya watu utakaowavutia kufanya kazi na wewe.
-Yule utakayempata kufanya naye kazi hatokani na nini unataka, atatokana na vile
ulivyo wewe. Kama wewe ni kiongozi wa shirika au taasisi fulani na ni mtu
unayependa kufanya kazi kwa haraka basi baada ya muda fulani utajikuta una
umezungukwa na watu wengi wanaopenda kufanya kazi kwa haraka. n.k., Watu
wenye kufanana na wewe watakutafuta kufanya kazi na wewe. Inawezekana
kiongozi akatafuta watu wa kufanya naye kazi asiofanana nao tabia lakini kwa asili
hatakuwa anawavutia sana yeye kama kiongozi.
-Kama unafikiri watu wako wana mitazamo hasi, basi ni vizuri kujiangalia upya
vizuri wewe una sifa gani. Hata kama kuna mambo mnatofautiana lakini utakuta
kuna mambo mengi sana mnaendana. Mara nyingi utakuta mnafanana mitazamo,
umri unaoendana, pengine mliishi mazingira ya pamoja kama mtaani au shuleni,
tabia kama vile labda wote ni waovu au walevi au wenye kupenda hulka fulani au
watu wa namna fulani, saa nyingine ni wacheshi au wahuni, wapenda ibada sana.
-Pia kadiri unavyokuwa kiongozi bora ndivyo kadiri unavyoweza kuvutia viongozi
bora kufanya nao kazi. Kama unafikiri watu unaowavutia wanatakiwa kuwa bora
basi ni muda wa kujiboresha wewe binafsi kuzidi viwango unavyotaka watu
unaotaka kufanya nao kazi wawe wamefikia.

10. Sheria Kujiunganisha (The Law of Connection), “Viongozi Hugusa Mioyo Ya Watu
Kabla Hawajaomba Kuungwa Mkono”
-Huwezi kuwafanya watu waingie kwenye vitendo kama hujaingia mioyoni mwao
na kuwagusa hisia zao. Mioyo hutanglia kabla hata ya akili kichwani . Kadiri
mahusiano na ukaribu vinavyokuwa imara ndivyo kadiri mfuasi anavyokuwa tayari
kutaka kumsaidia kiongozi. Ukitaka kujiunganisha na watu katika kundi jitahidi
kujenga mahusiano nao kama mmoja mmoja.
-Baadhi ya viongozi hufikiri kazi ya kujiunganisha na kujenga mahusiano ni kazi
ya wafuasi wake. Ni jukumu la kiongozi kujiunganisha na kuimarisha mahusiano
yake na watu. Jitahidi kuimarisha mahusiano na mmoja kwa kujitahidi kujua
majina yao mengi kadiri unavyoweza na kuwaita kwa majina yao moja kwa moja,
pia jitahidi kusalimiana nao kwa kushikana mikono na kila mmoja kadiri
unavyoweza. Watu hawajali unafahamu kiasi gani mpaka wajue unawajali kiasi
gani. Kujiongoza mwenyewe unaweza kutumia kichwa chako, lakini kuongoza
wengine unapaswa kutumia moyo.
11. Sheria/Kanuni Ya Watu Wa Karibu Wanaokuzunguka (The Law Of The Inner Circle),
“Ubora au Umahiri Wa Kiongozi Unatokana Na Wale Walioko Karibu Naye”.
-Hata ujitahidi kujituma na kujihangaisha kiasi gani kuna watu hawawezi
kukuvusha kutoka chini kupanda juu zaidi. Unapokuwa na watu sahihi unaofanya
nao kazi, mafanikio na matazamio yanakwenda juu sana. Hakuna kiongozi wa
peke yake, kama wewe ni kiongozi wa peke yake maana yake hakuna
unachoongoza. Angalia mtu yeyote ambaye anaonekana ni kiongozi mahiri na
utaona watu wengi bora anaofanya nao kazi wamemzunguka. Kila taasisi yenye
mafanikio ina watu bora wanaoifanya ipige hatua kubwa hizo.
-Unapaswa ujitahidi kuajiri watu bora kadiri utakavyopata, jitahidi kuwakuza na
kuwaendeleza kadiri utakavyoweza, na uwakabidhi majukumu yote kadiri
utakavyoona inafaa.

12. Sheria/Kanuni Ya Kuwapa Wengine Nguvu Za Kimamlaka (The Law of


Empowerment), “Ni viongozi Wanaojiamini Pekee Ndio Huwapa Wengine Wa
Chini Yao Nguvu Za Kimamlaka”
“Kiongozi bora ni Yule ambaye anijielewa kiasi cha kuweza kuchukua watu
wazuri wafanye kila ambacho anataka kifanyike na kuwaacha wafanye bila
kuwaingilia”, Theodore Roosevelt
-Kiongozi anapokuwa hatoi kwa wengine nguvu za kimamlaka ili wawe huru
kufanya kazi kwa uwezo wao wote na ubunifu wa hali ya juu anatengeneza ugumu
katika taasisi na hiyo inaweza kupelekea kupoteza baadhi ya watu wazuri ambao
wangeweza kuisaidia taasisi kupiga hatua kubwa. Uwezo wa watu kufanikiwa
unatokana na uwezo wa kiongozi wao kuwapa nguvu za kimamlaka.
-Kuna viongozi wanaogopa kwamba wakiwapa nguvu za kimamlaka watu wa
chini yao watahatarisha nafasi zao na kukubalika kwao au kupata wafauasi wengi
kuwazidi wao hivyo kuzidiwa nguvu lakini katika sayansi ya uongozi inaonyesha
njia pekee ya kiongozi kuwa imara zao na kuwa tegemeo ni kuwapa nguvu za
kimamlaka watu walioko chini yao, hiyo itapelekea wao kuwa bora zaidi kwani
ndio walifanya uamuzi wa kuwapa nguvu wengine iliyopelekea wao kuonekana.

-“Njia pekee ya kukufanya wewe kuwa tegemeo ni kujiweka kutokuwa tegemeo”,


kwa kuwapa wengine nguvu za kimamlaka watekeleze majukumu yao kwa ufanisi
na ubora zaidi wakati wewe ukiwafuatilia na kuwasimamia.

-Ongoza kwa kuwanyanyua wengine. “Mambo makubwa hutokea pale tu


unapowapa wengine sifa na pongezi”. “Ukitaka kuwapeleka wengine chini
utatakiwa kwenda chini pamoja nao”
13. Sheria/Kanuni Ya Uzalishaji (The Law of Reproduction), “Inahitaji Kiongozi
Kumkuza/Kumtengeneza Kiongozi”
Ni Namna Gani Watu Huwa Viongozi Halisi?
-Kama umefuatilia kwa ukaribu utaona kwamba kuna kundi dogo la watu huwa
viongozi kwa sababu yametokea majanga makubwa au maafa ya kutisha na
kupelekea uhitaji wa mtu kuwatoa watu katika kipindi hicho kigumu, ambapo
hutokea mtu na kuwa kiongozi kuchukua majukumu hayo. Pia kuna kundi lingine
dogo la watu wachache huzaliwa tu na uwezo mkubwa wa kuongoza hivyo huwa
viongozi moja kwa moja na kushughulika na mambo muhimu yanayohitaji
uongozi wao. Lakini ukifuatilia vizuri ni kwamba watu wanne kati ya watano
ambao ni viongozi huwa viongozi kutokana na ushawishi na malezi ya viongozi
wengine walio mamenta wao. Hii hutokea kutokana na sheria/kanuni ya uzalishaji
kwamba “Inahitaji kiongozi ili kumtengeneza na kumkuza kiongozi”.
“Watu hawawezi kuwapa wengine kitu ambacho wao hawana, wafuasi hawawezi
kuendeleza kiongozi”
-Kiongozi hutengeneza viongozi wanaofanana na wao na sio wanaofanana na kile
wao wanataka. “Tunafundisha kile tunachokijua lakini tunazalisha kinachofanana
na sisi”. Kama jinsi ilivyo inahitaji shujaa kutengeneza shujaa, inahitaji kiongozi
kutengeneza kiongozi.

14. Sheria/Kanuni Ya Kumkubali (The Law of Buy In), “Watu humkubali kwanza
kiongozi, ndipo hukubali maono yake”
-Kiongozi huwa na ndoto kwanza ndipo hutafuta watu, ila watu hutafuta kiongozi
kwanza ndipo huwa na ndoto. Kama kiongozi unatakiwa kwanza kutafuta
ushawishi na kukubalika ndipo uje na ndoto au maono kuwashikrikisha watu na
wakubali kushirikiana na wewe katika kuyatimiza.
-Kiongozi ni kama ujumbe, ujumbe wowote watu wanaoupokea hutegemea na
mjumbe anayeufikisha, kama mjumbe huyo ni mtu mwenye kuaminika na
kukubalika basi watu huamini ujumbe huo una thamani, nah ii ndio sababu utakuta
makampuni makubwa huwatumia watu mashuhuri katika kufikisha ujumbe wa
matangazo yao ya bidhaa na huduma mbalimbali. Watu wanaweza kununua labda
pepsi kwa sababu wanamkubali Lionel Messi waliyemuona akinywa pepsi hiyo.
-Ni vigumu kumtenganisha kiongozi na kile anachokipigania au kukisimamia,
yaani iko hivyo kiongozi awe mtu anayefaa kwanza ndio kile anachokipigania au
kukisimamia kitapewa nafasi.
Kwa mfano;-
1. Kama kiongozi hafai, na anapigania jambo lisilokuwa muhimu na lisilo na
manufaa sana kwa watu hapo watu watatafuta kiongozi mwingine.
2. Kama kiongozi hafai, lakini anapigania jambo muhimu na lenye manufaa sana
kwa watu, bado watu watatafuta kiongozi mwingine.
3. Kama kiongozi anafaa, lakini anapigania jambo lisilo muhimu na lisilo na
manufaa sana kwa watu, watu watatafuta jambo lingine.
4. Kama kiongozi anafaa, na anapigania jambo muhimu na lenye manufaa sana
kwa watu, watu watakuwa nyuma yake kumuunga mkono.
-Unahitaji kuwa kiongozi bora ili watu waunge mkono agenda yako, haijalisha
kama una agenda muhimu na iliyo bora kiasi gani, kama wewe mwenyewe sio
kiongozi watu hawatahangaika kujali unabeba ujumbe, maoni/ndoto au agenda
bora kiasi gani.

15. Sheria/Kanuni Ya Ushindi (The Law of Vision), “Kiongozi Hutafuta Njia Ya Timu
Kushinda”
-Viongozi halisi huwa hawakubaliani na swala la kushindwa au kufeli, kiongozi
halisi huhisi swala la kushindwa ni jambo lisilokubalika kabisa na hufanya kila
linalowezekana na kwa namna zote kuweza kupata ushindi. Kiongozi halisi
huamini ushindi ndio kitu cha kwanza, ushindi kwa gharama yoyote bila kujali
itachukua muda gani na safari itakuwa ngumu kiasi gani.
-Wakati mambo yanapochachamaa sana viongozi bora huonyesha uwezo wao wa
juu kabisa kwani chochote bora kilichopo ndani yao huonekana. Viongozi ambao
wanaiishi hii sheria ya ushindi huwa hawana mpango mwingine wa pili tofauti na
ushindi.

16. Sheria/Kanuni Ya Kupata Uelekeo/Kukaa Sawa (The Law of Momentum), “Hali Ya


Kupata Uelekeo/Kukaa Sawa Ni Rafiki Bora Wa Kiongozi”.
-Siku zote kiongozi hutafuta njia kuweka mambo yakae sawa katika uelekeo sahihi
na kwa kiwango kinachostahili ambapo huanza taratibu mpaka kufikia kiwango
ambacho mambo yametulia katika uelekeo unaoridhisha.
-Mambo yakishakuwa yamekaa sawa katika uelekeo sahihi ni rahisi kufanya
mabadiliko yoyote bila shida. Ni rahisi kuendeleza mambo yaliyo katika uelekeo
sahihi kuliko kuanza kuyatengeneza yakae sawa. Kama unatamani kufanya mambo
makubwa katika kampuni au taasisi au shirika unaloliongoza ni vyema kuzingatia
sana sheria/kanuni hii ya kuweka mambo yakae sawa katika uelekeo sahihi,
ukiweza kuiendeleza utaweza kufanikisha kitu chochote.

17.Sheria/Kanuni Ya Vipaumbele (The Law of Priorities), “Kiongozi Anaelewa Vizuri


Kwamba Shughuli Au Utekelezaji Sio Mafanikio.
-Kiongozi hata awe bora na imara kiasi gani hawezi kuacha kuwa na vipaumbele,
ni kitu ambacho viongozi bora hufanya bila kujali anaongoza kundi dogo au kubwa
kiasi gani. Kiongozi ni yule anayepanda mti mrefu kabisa na kuangalia hali iliyopo
na kusema tumeingia chaka.
-Kutokana na kuwa na mambo mengi sana yanayowahitaji, viongozi bora hufuata
sheria ya ufanyaji kazi inayoitwa “sheria ya pareto”. Ni sheria ambayo inasema
kwenye kila kitu unachofanya kuna 20% ya mambo yako ambayo yanachangia
80% ya mafanikio yako, yaani ukifuatilia kila unachokifanya utagundua 80% ya
mafanikio yako yanachangiwa na 20% ya nguvu unazoweka. Kwa mfano kama
unamiliki biashara utagundua 80% ya mapato yako kwenye biashara inachangiwa
na 20% ya wateja wako kisha hao 80% waliobaki wanachangia 20% pekee.
Utakuta 20% ya wafanyakazi wako wanachangiwa 80% ya mafanikio ya kampuni
yako n.k., hii inafanyakazi kwenye kila kitu. Sasa utakuta viongozi wengi makini
wanaendana na sheria kama hii kwa kiasi Fulani yaani yale maeneo ambayo ndio
yanawapa mafanikio zaidi wanayapa kipaumbele zaidi na muda. Lakini hili swala
la kipaumbele kinaingia sehemu nyingi sana unaangalia kipi unaweza kufanya
vizuri kwa wakati Fulani na unakitanguliza kwa sababu ambazo unazijua wewe.

18. Sheria/Kanuni Ya Kujitoa (The Law of Sacrifice), “Kiongozi Lazima Ajitoe Sana Ili
Kwenda Juu”
-Kiongozi ni lazima awe mtu wa kujitoa sana, kuanzia muda wake, hapaswi kuwa
mtu wa kujifikiria yeye muda mwingi anafikiria anaowaongoza na
anachokiongoza, wanasema unapokuwa kiongozi unapoteza haki ya kujifikiria
mwenyewe sana. Kiongozi ni mtu anajikuta anakubaliana na usumbufu mwingi na
kufanya kazi kwa moyo sana, na hiyo ndio gharama ya mafanikio ya kiuongozi.
Hii sheria ya kujitoa inasisitiza kwamba kujitoa mara moja ni mara chache sana
inaweza kuleta mafanikio, kiongozi anapaswa kujitoa na kujitoa zaidi na zaidi
mpaka kufanikisha lile analoliazimia. Uongozi unamaanisha kuwa mfano,
ukijikuta katika nafasi ya uongozi watu hufuata kila unachofanya.
-Kujitoa ni jambo endelevu sio swala la mara moja tu. Kama viongozi wanapaswa
kujitoa waende juu, basi wanapaswa kujitoa zaidi ili wabakie juu. Kadiri
unavyoenda juu zaidi ndivyo kadiri unavyojitoa zaidi na zaidi. “Kwa kila kitu
ulichokosa kuna ambacho umepata, na kwa kila ulichopata kuna ambacho
umekosa” alisema Ralph Waldo Emerson. Ukifuatilia viongozi wakubwa wengi
wamejitoa sana maeneo mengi ya maisha yao na kadiri mafanikio yao yanakuwa
makubwa zaidi wanazidi kujitoa zaidi.
-Kadiri kiwango chako cha uongozi kinavyozidi kwenda juu ndivyo kadiri
unavyotakiwa kujitoa zaidi.
19. Sheria/Kanuni Ya Muda Muafaka (The Law of Timing) “Muda wa Kuongoza Una
Umuhimu Sawa Na Nini Cha Kufanya Au Wapi Pa Kwenda”
-Pale kiongozi anapoonekana anafanya maamuzi ya hovyo hata katika vitu vidogo
watu wanaanza kufikiri kwamba yeye kuwa kiongozi wao yalifanyika makosa
makubwa.
-Muda muafaka ni kila kitu,kiongozi yeyote hufahamu hilo na ndio maana mara
zote unapofanya jambo litakuletea matokeo ya aina nne tofauti kama ifuatavyo;-
(i) Ukifanya jambo lisilo sahihi katika muda usio sahihi itapelekea majanga.
(ii) Ukifanya jambo sahihi katika muda usio sahihi litapata upinzani.
(iii) Ukifanya jambo lisilo sahihi katika muda sahihi litakuwa ni kosa
(iv) Ukifanya jambo sahihi katika muda sahihi litapelekea mafanikio.
-Kiongozi sahihi na muda muafaka vinapokutana mambo makubwa hutokea

20. Sheria/Kanuni Ya Kukua Kwa Kasi Na Haraka (The Law of Explosive Growth)
“Kujumlisha Ukuaji Ongoza Wafuasi, Kuzidisha Ukuaju Ongoza Viongozi”
-Ni jukumu la kiongozi kujenga watu ambao wataenda kuijenga
taasisi/kampuni/shirika.
-Kiongozi anayeifanyia kazi sheria hii ya kukua kwa kasi na kwa haraka huacha
kuongoza wafuasi na kuanza kuongoza viongozi. Unapoongoza viongozi ukuaji
unakuwa wa kasi haraka na wa ubora sana, hii hupelekea uwezo wa kampuni kuwa
mkubwa na mambo kufanyika katika ubora wa hali ya juu hata kama kiongozi
Mkuu ana dharura. Ni jukumu la kiongozi kuwajenga wafuasi kuwa viongozi kwa
kuzingatia sheria hizi za uongozi au kutafuta watu ambao tayari wana uwezo
mkubwa wa kuongoza na kuwapa majukumu.
-Tuangalie tofauti kati ya kiongozi anayeongoza wafuasi na kiongozi anayeongoza
viongozi;-
(i).Wakati kiongozi anayeongoza wafuasi anahitaji kuhitajika, kiongozi
anayeongoza viongozi anataka kurithiwa au mtu mwingine kuweza kusimama
kwenye nafasi yake kwa uhakika kabisa.
(ii).Wakati kiongozi anayeongoza wafuasi huangalia zaidi madhaifu katika wale
anaowaongoza, kiongozi anayeongoza viongozi huangalia zaidi uimara wa wale
anaowaongoza
(iii).Wakati kiongozi anayeongoza wafuasi huwachukulia anaowaongoza kwa
usawa, kiongozi anayeongoza viongozi huwachukulia viongozi anaowaongoza
kama watu anaowategemea walete matokeo makubwa kwa nafasi walizopo.
(v).Wakati kiongozi anayeongoza wafuasi hutumia muda wake kukaa na watu,
kiongozi anayeongoza viongozi huwekeza muda kwa watu.
(vi).Wakati kiongozi anayeongoza wafuasi hukua kwa kujumlisha, kiongozi
anayeongoza viongozi hukua kwa kuzidisha.
(vii).Wakati kiongozi anayeongoza wafuasi huwa na madhara kwa watu hao
anaowaongoza peke yake, kiongozi anayeongoza viongozi huwezi kuwafikia
mpaka watu walioko mbali kabisa hata asiowafahamu.
(ix).Wakati kiongozi anayeongoza wafuasi huweza kuwagusa watu yeye
mwenyewe moja kwa moja, kiongozi anayeongoza viongozi huwagusa mpaka
watu walioko mbali asio na ukaribu nao
(x).Wakati kiongozi anayeongoza wafuasi huhangaika kuwaendeleza wale watu wa
chini, kiongozi anayeongoza viongozi huendeleza wale viongozi wa juu na
kuhakikisha wamekuwa bora sana ambapo na wao huendeleza wa chini yao na wa
chini zaidi mpaka taasisi nzima kuwa imejaa viongozi wenye uwezo mzuri.
-Baadhi ya viongozi hupenda kutengeneza wafuasi, lakini viongozi bora hutaka
kutengeneza viongozi, na sio tu kutengeneza viongozi bali kutengeneza viongozi
wa viongozi. Kisha kutengeneza viongozi wa viongozi wa viongozi.
-Njia pekee ya kukua kwa kasi, kwa haraka na kwa ubora ni kufanya hisabati,
hisabati ya viongozi, tengeneza viongozi wa viongozi wa viongozi wa viongozi.

21. Sheria/Kanuni Ya Urithi/Wosia (The Law of Legacy) “Thamani Ya Mwisho Ya


Kiongozi Hupimwa Kwa Mafanikio Yanayokuja Baada Yake”
-Urithi/Wosia unatokea tu pale ambapo mtu huweka taasisi/shirika/kampuni katika
nafasi ambayo itaweza kufanya mambo makubwa bila yeye kuwepo.
-Kiongozi ni yule anayefikiria kampuni itakuwa katika hali gani muda mrefu baada
ya yeye kuondoka, ni yule anayetengeneza mazingira kwamba akiondoka mambo
yaendelee kuwa mazuri na kampuni/shirika lisiyumbe na liendelee kuwa katika
kiwango cha juu.
-Kiongozi huendelea kukumbukwa muda mrefu baada ya yeye kuondoka kutokana
na mazingira aliyokuwa amejenga yatakayoendelea kuisadia taasisi kwa muda
mrefu baada ya yeye kuondoka.
-Tumefikia mwisho wa uchambuzi wetu, hizo hapo juu na kanuni 21 za uongozi
ambazo hazipingiki na utakutana nazo popote katika uongozi.
-Jambo la kwanza ninashauri ni watu kutafuta hiki kitabu na kukisoma, hapo
nimechambua juu juu sana tena bila hata mifano, Mwandishi wa kitabu hiki Dr.
John Maxwell ameandika mambo mengi sana na kila sheria ya uongozi katika zote
21 ametoa mifano mingi hai ambayo unaweza kujifunza moja kwa moja kupitia
mifano hii, pia amejitahidi kudadavua kiasi kwamba unaweza kuelewa vizuri zaidi.
Huu uchambuzi nimeufanya kukupa mwanga na kukupa mtazamo wa namna
uongozi ulivyo na unavyofanya kazi, unaweza kuzisoma vizuri hizi kanuni na
kujaribu kuwaangalia kwa ukaribu watu walioko katika nafasi mbalimbali za
uongozi na ushawishi mkubwa uone ni kwa jinsi gani wanaendana na sheria hizi na
kunufaika au kwenda kinyume na sheria hizi na inawagharimu sana.
Uongozi ni jambo muhimu sana kwa mtu yeyote mwenye mipango ya kufika mbali
kimafanikio
Haijalishi ni katika taalamu au katika fani gani, soma kitabu hiki ni muhimu sana
katika kupata uelewa wa mambo ya kiuongozi nap engine hujawahi kukutana na
elimu hii, iwe ni mwanzo kwako kupata kuelewa zaidi katika nyanja hii muhimu
sana

You might also like