Professional Documents
Culture Documents
Green Star Family Planning Community Resource Kit
Green Star Family Planning Community Resource Kit
MWEZESHAJI
UZAZI WA MPANGO
Fuata nyota ya kijani, Upate mafanikio
May 2014
1
MWONGOZO
WA
MWEZESHAJI
UZAZI WA MPANGO
Fuata nyota ya kijani,
Upate mafanikio
2
Yaliyomo
Utangulizi 5
Hitimisho 18
3
4
SEHEMU YA 1:
UTANGULIZI
Mwezeshaji:
Karibisha washiriki, waeleze kuwa:
Hiki ni kipindi kuhusu uzazi wa mpango. Katika kipindi hiki tutajifunza maana,
faida na njia za uzazi wa mpango pamoja na namna uzazi wa mpango
unavyoweza kuwafanya wenza wakawa na maisha mazuri na ya furaha kwa
pamoja.
Suala hili ni muhimu pia ni nyeti na linaweza kuibua mijadala mingi, hivyo basi,
nawasihi kufuatilia kwa makini na kushiriki pamoja na kuwa huru kuchangia
kwa uwazi wakati wote wa mjadala.
SEHEMU YA 2:
5
6
SEHEMU YA 3:
Mwezeshaji:
Waeleze washiriki kwa kusema:
Tutajifunza mojawapo ya maana na faida za kupanga uzazi. Katika somo hili
tutacheza mchezo wa upandaji wa mahindi yaliyopandwa katika msimu sahihi,
lakini kwa namna mbili tofauti; moja ni mahindi yaliyopandwa kwa mpangilio
na pili ni yaliyopandwa bila mpangilio. Mchezo huu unaonyesha mojawapo ya
namna ya ustawi wa watoto katika familia.
7
SEHEMU YA 4:
MAJADILIANO KUHUSU
MCHEZO NAMBA MOJA
Mwezeshaji uliza maswali yafuatayo hapo chini. Ukishauliza swali, acha
washiriki watoe majibu yao na kisha uyalinganishe na majibu ya swali
husika yaliopo.
4. (A) Katika aina hizi mbili za upandaji wa mahindi, ni aina ipi ambayo
ungependa kuifuata?
Majibu:
• Aina ya kwanza
• Aina ya pili
8
SEHEMU YA 5:
MAJADILIANO KUHUSU
MAANA YA UZAZI WA
MPANGO
1. Ni kwa jinsi gani upandaji wa mahindi kama tulivyoona kwenye mchezo
unalingana na ustawi wa watoto katika familia?
Mwezeshaji:
Sasa waeleze au wasomee washiriki maana halisi ya uzazi wa mpango
kama ilivyo tafasiriwa katika Mwongozo wa Kitaifa wa Ujumbe kuhusu
Uzazi wa Mpango na kitendea kazi cha Mtoa Huduma za Uzazi wa
Mpango.
9
SEHEMU YA 6:
FAIDA ZA UZAZI WA
MPANGO
Mwezeshaji:
Waeleze washiriki watacheza tena mchezo mwingine ili kujua zaidi faida
za uzazi wa mpango.
Mwezeshaji:
Waeleze washiriki kuwa baadhi ya familia zimeweza kukidhi mahitaji ya
kulipa ada,chakula na mavazi ingawa bado kuna kipengele muhimu cha
matibabu ambacho kinahitaji kutengewa kipato.
10
Mwezeshaji:
Waeleze washiriki kuwa mtoto mmoja miongoni mwa watoto alionao kila
mshiriki anaumwa malaria na anapaswa kulipiwa gharama za matibabu
ambayo yanagharimu vizibo vitatu.
Mwezeshaji:
Waeleze kila mshiriki kugawa vizibo vitatu vitatu kwa kila mtoto mgonjwa.
Matokeo:
Watajikuta mshiriki namba 1 – ametumia vizibo 13 na amebakiwa na vizibo 7
Mshiriki namba 2 – ametumia vizibo 18 na amebakiwa na vizibo 2
Mshiriki namba 3 – watoto wawili waliweza kupata chakula, mavazi na
ada. Mtoto mmoja amepata chakula mavazi na nusu ya ada. Watoto
wawili wamepata mavazi na chakula na wamekosa ada. Mtoto mgonjwa
amekosa matibabu kabisa.
Mshiriki namba 4 – Watoto wote waliweza kupata mavazi, watoto sita
wamepata chakula, mtoto mmoja amepata chakula kidogo. Watoto
wote saba wamekosa ada za shule na mtoto mmoja mgonjwa amekosa
matibabu.
Mshiriki namba 3 na 4 vizibo vyote vitakuwa vimekwisha na wao watakuwa
hawajakamilisha mahitaji kwenye familia zao (mshiriki namba 3 anahitaji
vizibo 28 na mshiriki namba 4 anahitaji vizibo 38 ili kukamilisha mahitaji
yote ya familia zao)
11
SEHEMU YA 7:
MAJADILIANO KUHUSU
MCHEZO WA UGAWAJI WA
KIPATO KATIKA FAMILIA (VIZIBO)
Mwezeshaji uliza maswali yafuatayo hapo chini. Ukishauliza swali, acha
washiriki watoe majibu yao na kisha uyalinganishe na majibu ya swali
husika yaliopo.
12
5. Je Changamoto kama hizi zinajitokeza katika jamii yetu?
• Ndiyo
kwa nini?
• mila na desturi zinaruhusu kuwa na watoto wengi
• Sheria ya ndoa inaruhusu mtoto wa kike (umri 15) kuolewa akiwa na
umri mdogo kwa idhini ya wazazi
• Mengineyo
13
SEHEMU YA 8:
Kila mtu ana haki ya kupanga idadi ya watoto ambayo yeye na mwenza
wake wanahitaji kuzaa na kwa wakati gani. Katika sehemu hii tutaona na
kujifunza njia mbalimbali za uzazi wa mpango ambazo wenza wanaweza
kuchagua.
Mwezeshaji:
Baada ya kumaliza kuwaonyesha, waeleze washiriki kuwa pamoja na kuwa
kuna njia nyingi za uzazi wa mpango, njia zote hizi zimegawanyika katika
makundi matatu:
• Kuna njia za muda mfupi.
• Njia za muda mrefu na
• Njia za kudumu.
14
15
SEHEMU YA 9:
Msemo namba 1.
Uzazi wa mpango si jukumu la wanawake tu.
• Matumizi ya njia za uzazi wa mpango ni jukumu la wote yaani akinababa,
akinamama na vijana. Ni hiari ya mtu au wenza kuamua njia ipi ya uzazi
wa mpango wanaipenda kuitumia baada ya kupata ushauri toka kwa
wataalam. (wajadili kwa pamoja ni lini waanze kuzaa, wazae watoto
wangapi, wapishane kwa muda gani na lini waache kuzaa, waende kwa
pamoja kupata ushauri na elimu ya njia za uzazi wa mpango n.k)
Msemo namba 2.
Si wanawake walioolewa tu ndiyo wanapaswa kutumia njia za uzazi wa
mpango
• Mtu yeyote (mwanaume, mwanamke na kijana) aliyeolewa na asiyeoolewa,
mwenye watoto na asiye na watoto na wenye ulemavu walio kwenye
umri wa kuzaa anaweza kuamua kutumia huduma ya njia za uzazi wa
mpango bila kubaguliwa. Ni haki ya msingi kwa kila binadamu kupata
elimu, taarifa pamoja na huduma za uzazi wa mpango.
16
17
SEHEMU YA 10:
HITIMISHO
Mwezeshaji:
Kabla hujahitimisha waulize / waruhusu washiriki kama wana maswali
kutokana na yale waliyojadiliana na kisha fanya majumuisho kwa kurejea
yafuatayo;
• Uzazi wa mpango ni maamuzi ya hiari ya mtu au wenza juu ya wakati
gani waanze kuzaa watoto, wazae watoto wangapi3, wapishane kwa
umri gani na lini waache kuzaa.
• Uzazi wa mpango si kuwa na watoto wachache tu bali ni jinsi gani mtu na
mwenza wake wanapanga idadi ya watoto wa kuzaa.
• Uzazi wa mpango hukuwezesha kutoa huduma na malezi kwa watoto
kadri ya mahitaji yao na kukupa nafasi nzuri kimaisha.
• Uzazi wa mpango hukuwezesha kusimamia vizuri raslimali ulizonazo.
• Uzazi wa mpango humuwezesha mama na watoto kuwa na afya bora.
• Uzazi wa mpango unasaidia kukuza uchumi na maendeleo ya familia,jamii
na nchi kiujumla.
• Kuna njia nyingi za uzazi wa mpango ambazo zinaweza kuwasaidia wenza
kupanga familia yao.
• Ni juu ya wenza kuamua ni aina gani ya njia ya uzazi wa mpango
wanayoona inafaa kuitumia baada ya kushauriwa na watalaam katika
kituo cha huduma za Afya.
• Kwa maelezo zaidi kuhusu uzazi wa mpango waone watoa huduma wa
afya katika kituo cha kutolea huduma za Afya kilichopo karibu nawe.
• Unaweza ukatuma ujumbe wa simu ulioandikwa m4RH kwenda namba
15014 BILA MALIPO
Mwisho:
Maliza kwa kuwashukuru kwa ushiriki wao katika zoezi zima.
18
19
Fuata nyota ya kijani, Upate mafanikio
20