Download as docx, pdf, or txt
Download as docx, pdf, or txt
You are on page 1of 5

YALIYOMO

1.0 UTANGULIZI ……………………………………………………………………… 2


2.0 MAJINA NA MAWASILIANO YA WANACHAMA HAI ….……..……………… 3
3.0 DHUMUNI LA KIKUNDI …………………………………………………………… 3
4.0 MUONGOZO KATIKA YATAKAYOKUWA YANASAIDIWA NA KIKUNDI…..
4.1 KUFIWA ………………………………………………………………………………
4.2 WAKATI WA MSIBA ………………………………………………………………
4.3 UGONJWA ……………………………………………………………………. ……..
4.4 KUSADIA WAKATI WA UGONJWA ……………………………………………. ..
4.5 UZAZI …………………………………………………………………………… …...
4.6 KUSAIDIA MWANACHAMA ALIYE KWENYE UZAZI.HARUSI……………….
4.7 KUSAIDIA MWANACHAMA MWENYE HARUSI ………………………………..
5.0 MASHARTI, ADA NA FAINI/ ADHABU BKWA MIJUIBU WA KATIBA ……… 4

1.0 UTANGULIZI
1
Kikundi cha Upendo Group kilianzishwa tarehe 10/7/2021 kikundi kilianza na wanachama apatao
kumi na nane (18). Kikundi makao yake makuu ni Machimbo.
Hadi Dec 2022 kikundi kina wanachama hai wanaoelewa malengo ya kikundi wapatao kumi tano (15)
wakipatikana machimbo Dar salaam.

2.0 MAJINA NA MAWASILANO YA WANACHAMA HAI WA KIKUNDI


CHA
UPENDO GROUP
NA JINA LA MWANACHAMA CHEO/ADHIFA MAWASILIANO/

1. WARDA .E. LYIMO 0752 8917 45


2. K .LUKULU 0719 6314 22
3. TATU RASHIDI 0714 8869 05
4. MWANAIDI NURUDINI 0684 6686 96
5. ZELINA IDD 0716 9324 42
6. SOPHIA SAMSON 0762 3053 97
7. SWAUMU RAMADHANI 0786 1463 44
8. SALIMA TAWAKALI 0688 9874 23
9. OLVA TEMU 0763 5692 12
10. KHADIJA JUMA 0786 7029 03
11. ANJELINA MREMA 0753 3525 93
12. EMMA FLOMENA
13. MOSI MANDA 0654 3300 25
14. HALIMA THABITI 0642 3866 81
15. SIFA MGONJA 0762 1981 78

3.0 DHUMUNI LA KIKUNDI;


Dhumuni kuu la kikundi cha upendo group ni kusaidiana kwenye shida na raha ikiwemo;-
MSIBA /KUFIWA
UGONJWA
UZAZI
HARUSI AU SHEREHE

2
4.0 MUONGOZO WA KATIBA KATIKA MAMBO YATAKAYOKUWA
YANASAIDIWA NA KIKUNDI
Katiba hii ya kikundi cha upendo group inatoa muongozo kwenye mambo yatakayokuwa yanasaidiwa
na kikundi kiujumla ifuatavyo;-

4.1 KUFIWA.
Katiba inaelekeza kuwa kikundi cha upendo group kitasaidia au kutoa msaada iwapo msiba utakuwa
ni wa;-
I. Mwanachama Mwenyewe
II. Baba Mzazi au Mlezi
III. Mama Mzazi au Mlezi
IV. Mtoto
V. Mama Mkwe au Mlezi
VI. Baba Mkwe au Mlezi
VII. Mume
VIII. Ndugu wakaribu ambae unaishi nae kama mwanao na ambae hana wazazi.

4.1.0 UTARATIBU WA KUSAIDIA WAKATI WA MSIBA KWA MUJIBU WA KATIBA

4.1.1 IKIWA MSIBA UTAKUWA UMEGUSA NAMBA 2 MPAKA NAMBA 8


I. Ikiwa mwanachama hai wa kikundi atakuwa amepatwa na msiba wa yoyote kati ya
walioorodheshwa kuanzia nanba 1 hadi 8 hapo juu. Utaratibu wa kusaidiwa huyo
mwanachama kwa mujibu wa katiba ni kama ifiatayo; -
II. Kikundi cha upendo group kitatoa fedha taslimu kiasi cha shilingi laki na thelathini
(130,000/=) za kitanzania na kumkabidhi mfiwa.
III. Na baada ya fedhda hiyo kutoka kwenye mfuko wa chama kukabidhiwa kwa mfiwa, Kila
mwanachama itapaswa kuchangia kiasi cha fedha taslimu cha shilingi Elfu kumi (10000) ili
kujazia mfuko wa kikundi cha upendo group kwa kiasi kilichopungu.
IV. Na kwa mujibu wa katiba, muda wa kujazia mfuko wa kikundi kwa kiasi kilichopungua ni
kipindi kisichozidi mwezi (1)

4.1.2 IKIWA MSIBA UTAKUWA UMEGUSA NAMBA 1 (msiba wa mwanachama


mwenyewe)
Ikiwa imetokea kuwa mwanachama mwenyewe ndiye aliyefariki, kwa mujibu wa katiba kikundi
kitatoa msaada kama ifuatavyo;-
a) Kikundi cha upendo group kwa kila mwanachama atapaswa kuchangia kiasi cha Elfu kumi na
tano (15,000) na atakabidhiwa Ndugu /jamaa/Rafiki wa karibu ambaye alipendekezwa na
mwanachama mwenyewe kabla ya umauti haujamfika.
b) Na kwa mujibu wa katiba kila mwanachama inapasa kuwasilisha jina la Ndugu/Jamaa/Rafiki
wa karibu ambapo kama mwanachama akifariki kiasi atakabidhiwa huyo mtakaye mteuwa.

3
4.1.3 Kila mwanachama itatazimika kujumuika kwa kumpa pole mwanachama aliyefiwa, na kama
msiba ni wa kusafirisha (mkoani) basi itasubiriwa arudi na wanachama wote kwa pamoja wataenda
nyumbani kwa mfiwa kumpa pole.
4.2 UGONJWA
Kwa mujibu wa katiba watu watakaopaswa kusaidiwa na kikundi wakati wa ugonjwa ni hawa
wafuatao;-
a) Mwanachama mwenyewe
b) Mume
c) Mtoto
4.2.0 UTARATIBU WA KUSAIDIA WAKATI WA UGONJWA KWA MUJIBU WA KATIBA
a) Ili kikundi kiweze kutoa msaada wa ugonjwa kwa mwanachama anayeuguza au kuuguliwa ni
lazima mgonjwa awe amelazwa kwa muda wa siku tatu (3) na wanakikundi wawe na Taarifa
kupitia kwa kamati ya kuona kytembelea wagonjwa.
b) Baada ya kujiridhisha na hatua ya awali (1) kikundi kitatoa fedha kiasi cha shilingi 70000 na
atakabidhiwa muuguzi
c) Na baada ya fedha hiyo kutoka kwenye mfuko wa chama na kukabidhiwa kwa muuguzi kila
mwanachama itampasakuchangia kiasi cha taslimu cha shilingi Elfu tano (5000) ili kujazia mfuko
wa kikundi kwa kile kilichopungua.
4.3 UZAZI
4.3.0 UTARATIBU WA KUSAIDIA MWANACHAMA ALIYE KWENYE UZAZI
a) Ikiwa mwanachama amejifungua basi kila mwanachama atachanga kiasi cha shilingi Elfu 5000 na
kukabidhiwa mwanachama aliyejifungua.
b) Wanakikundi kwa pamoja watamtembelea mwanachama aliyejifungua.
4.4 HARUSI
4.4.0 UTARATIBU WA KUSAIDIA MWANACHAMA MWENYE HARUSI
a) Ikiwa mwanachama ana harusi basi atagawa kadi kwa wanakikundi ili waweze kuchangia.
b) Kwa mujibu wa katiba hii, mwanachama mwenye harusi ni lazima atoe Taarifa kwenye kikundi
miezi mitatu kabla iwapo harusi hiyo ni ya kikristo na iwapo harusi hiyo ni ya kiislamu basi atatoa
Taarifa kwa kikundi mwezi mmoja kabla.
c) Iwapo mwanachama atakuwa na sherehe ya mtoto wa kumzaa atachangiwa kiasi cha eifu ishirini
na tano kwa kila mwanachama.
d) Kampani ni elfu tano kwa mtu unaeishi naye.

5.0 MASHARTI, ADA, NA FAIDA ADHABU KWA MUJIBU WA KATIBA


a) Ni lazima kwa kila mwanachama wa kikundi cha upendo group kutoa ada ya kila mwezi ya kiasi
cha fedha shilingi elfu tano (5000) bila kukosa. Na iwapo mwanachama atapitisha miezi mitatu (3)
hajatoa kila mwezi, kwa mujibu ya katiba hatakuwa mwanachama hai na adhabu yake ni
ataondolewa uanachama wa kikundi cha upendo group

4
b) Iwapo ikitokea mtu anataka kujiunga na kikundi cha upendo group itamlazimu kulipa kiasi cha
shilingi ………………………………………………………… ili awe mwanachama.
c) Kwa mwanachama mpya ataanza kupata msaada wa kikundi baada ya kumaliza miezi mitatu (3)
tangu kujiunga kwake.
d) Kwa kila mwanachama mpya itamlazimu kulipa shilingi Elfu mbili(2000) kwa ajili ya kupata
katiba ya kikundi
e) Kwa mujibu wa katiba, idadi ya wanachama wa kikundi cha upendo group kuzidi ishirini na moja
(21)
f) Wanachama kwa kikundi cha upendo group watakuwa wanakutana kwenye kikao cha pamoja
walau mara moja (1) kwa mwezi.
g) Kwa mujibu wa katiba maudhurio ya kikao cha kikundi hayana udhuru. Iwapo mwanachama
hataudhuria kikao kwa sababu moja au nyingine hata kama ni msiba atapaswa kulipa faini ya kiasi
cha shilingi Elfu mbili (2000).
h) Iwapo kuna mwanachama hajaelewa sehemu au kifungu chochote cha katiba anaweza kuomba
ufafanuzi au maelezo kwa katiba.

KATIBA HII IMETHIBITISHWA NA KUSAINIWA NA; -


JINA …………………………………………… JINA
…………………………………………….
SAHIHI ………………………………………. SAHIHI
………………………………………….
TAREHE ……………………………………. TAREHE
……………………………………….
MWENYEKITIWA KIKUNDI KATIBU WA KIKUNDI

You might also like