Professional Documents
Culture Documents
Asomaye Na Afahamu
Asomaye Na Afahamu
Asomaye Na Afahamu
"ASOMAYE NA AFAHAMU"
Bila kila mtu kumjua huyo, Yesu Kristo hawezi kuja duniani.
Tutaendelea kusumbuka na magonjwa, umaskini, na dhiki. Je! si
jambo la muhimu kabisa kuijua mamlaka hiyo ili kujua la kufanya
kuokoa maisha yetu, si yale ya kimwili, bali ya kiroho ili
tupate kuishi milele? (Mt. 10:26-33; Yoh.6:39-40; Ufu.12:11).
Kufa au kutokufa si hoja, bali kujiweka tayari kumlaki Yesu
Kristo atakapokuja juu ya mawingu ya mbinguni (Ufu. 2:10; Mt.
24:29-31).
Mpendwa Msomaji, je! kwa neema yake Mungu unataka kuwa
tayari kujiunga na watakatifu ulimwenguni kote? Soma Danieli,
na ufahamu. Kabla hujaanza kusoma somo, omba ili Mungu akupe
Roho wake atakayekufundisha kweli yote (Yohana 16:13-15). Mungu
na akubariki!
M. Mwamalumbili.
(SEHEMU YA PILI)
Mungu hataki watu wake wawe gizani kuhusu ufalme huu, japo
kwa sasa ulimwengu unauinua juu sana. Hatimaye utakapotawala
kama alivyoruhusu Mungu itakuwa kwa maangamizi ya ulimwengu
mzima na dunia itafikia mwisho wake (Ufu. 17:8-11; 6:14-17;
19:11-21). Watakatifu watakwenda mbinguni kutawala pamoja na
Yesu kwa miaka 1000 (l The. 4:16,17(18); Ufu. 20:4). Dunia hii
itakuwa imeharibika vibaya katika kipindi chote cha miaka 1000
(Yer. 4:23-27). Baada ya kwisha miaka 1000 watakatifu watarudi
hapa pamoja na Mji Yerusalemu Mpya (Ufu. 21:10). Ndipo waovu
watakapofufuliwa na kujaribu kuuteka Mji Yerusalemu Mpya au
Kambi ya Watakatifu. Moto utawala (Ufu. 20:7-10,15). Hiyo ndiyo
Jehanum au Ziwa la Moto au Mauti ya Pili (Ufu. 20:14). Jehanum
haiwaki sasa. Itawaka baada ya miaka ile 1000 kwisha.
Watakaoingia humo watateketezwa na kuwa majivu pamoja na Shetani
na malaika zake( Mal. 4:1-3; Eze. 28:14-19). Hawatafufuliwa
tena milele! Ndipo watakatifu watakapoirithi nchi mpya (Ufu.
21:1; Mt. 5:5; 2 Pet. 3:10-13; Zab. 37 yote).