Download as doc, pdf, or txt
Download as doc, pdf, or txt
You are on page 1of 37

37

IMBA WIMBO WETU


KWA KRISTU MFALME

KIRO, MFALME ANAKUNGOJA

(Kiro, soyons prêts) Kiro chante p.1

Kiro, mfalme anakungoja wewe !


Usikie mwito moyoni
Mapenzi yake yanaleta nguvu;
Tumtum(i)kie pasipo woga!
Kiitikio
Imba wimbo wetu
Kwa Kristu Mfalme,
Kwani Kristu anatuita !
Hatupigani bure
Kwa Mfalme wetu
Kwani Kristu anatukinga
Wakiro mubaki wamini kwetu
Musikose uaminifu !
Musiwe na woga kwa watu bure
Muonyeshe tabia yenu !

Twendeni pamoja kwa Mfalme Mkubwa


Kupigana kwa sifa yake !
Tabia ya Kiro ibaki kwetu
Rohoni mwa wakiro wote.
KRISTU MFALME
(Chant de la promesse) Kiro chante p.2

Kristu Mfalme, nitabaki mwamini


Usafi wangu utanipea furaha !
Unifanye bora kwa mapigano
Askari wa kweli, rafiki mwema !
Kiitikio
Ubariki maagano mamini
Utashi ya kweli, mapendo mema !
Ahadi yangu ibarikiwe vizuri
Katika moto moyoni mwa Yesu.
Kristu Mfalme napigana kwa inchi
Unipe mapendo kwa watu wote
Usiache niregee moyoni
1
37

Katika magumu ya inchi yetu.


TUTASHINDA
Sisi tutashinda (bis)
Tutashinda siku moja.
Kiitikio
Ee, rohoni mwangu nasadiki
Yakama tutashinda !
Hatutaogopa (bis)
Tusiogope leo

Tutakuwa ndugu (bis)


Tutakuwa ndugu wote.

BENDERA KAMA INGEPANDA

Bendera Kama ingepanda juu,


Iko sala ya wakiro.
Kila siku Mungu anayotupa
Ni zawadi takatifu.
Kiitikio
Bebeni bendera yetu
Ni alama ya Kristu !
Ni alama ya ushindi
bis
Njooni wote kwa vita
Tubebe bendera uvugutoni
Wakati wa mwendo mgini mwetu
Na vita ya kila siku, kila saa
Itatuona tayari.

Wakati jua linatua kwetu


Tunalinda bendera yetu
Hatutaacha kumtolea Mfalme
uchungu wetu na kicheko.

MBELE YA KUENDA
(Descente du drapeau) Kiro chante p.4

Mbele ya kuenda
Tushushe bendera !
Ikashuke ndani ya roho amini
Iko nguvu, furaha,
Na Baraka kwa wakiro !
2
37

Mfalme tutalinda bendera


Ubariki zamu wako.
Na kwa heri Kristu Mfalme
Na kwa heri bendera yetu
Na kwa heri wakiro wote
Na kwa heri Kristu Mfalme.
ULIE
(Sonnez des trompettes) Kiro chante p.5

Ulie katika……………………..
(Ao : ulie mu inchi ya…………….)
Mwito wetu kwa Kristu Mfalme !
Mfalme!
Tumfuate, tumsifu popote Mfalme
Waaskari wake wema
Tutalia popote na nguvu
Kama Kristu ni Mfalme wetu.
Tipige tarumbeta (trompette) za Mfalme :
Zilie kitumaini.
Sisi wakiro, tayari kweli
Kwa Mfalme wetu, Kristu !
KATIKA UMOJA
(Collections pilote) Kiro chante p.12

Mu kundi letu nzuri


Wako wakiro wengi.
Na urafiki wetu
Alama ya Kristu.
Furaha ya wakiro
Katika umoja
Kiitikio
Tuwe na furaha ka tika umoja
Urafiki wetu ubakie daima.
Wakiro wetu wote
Wapendana sana.
Katika kundi letu
Hakuna ugomvi.
Na nguvu ya wakiro
Katika umoja.

Tupende watu wote


Pasipo kutengana.
Twataka kufurahi
3
37

Na dunia nzima
Mipaka yaondoshwe,
Umoja ubakie !
MAMA MWEMA
(Noble Dame) Kiro chante p.6

Mama mwema, mama mpendelevu,


Upo mfano wa usafi !
Ee Malkia mzuri wa vijana
Utuone mbele yako.
Kiitikio
Utukufu wako bora.
Uwe malkia mioyoni.
Unajua, bikira mpole,
kama nitakupenda daima !
Mama mpole, mama mkamilifu
We Bikira mwamini,
Utufanye hodari tupigane
Na kumshinda adui wetu.

Twakuomba ubaki karibu yetu


Na watoto wa inchi yetu.
Na twataka kubaki waminifu
Kama wewe kwa Mfalme Yesu !
MAMA WETU WA MBINGUNI
Kiro chante p.7
Mama wetu wa mbinguni,
Mama na Bikira,
Sikia watoto wako
Wanakwomba msaada
Wakupenda siku zote
Kwa mapendo mamini.
Utulinde kwa hatari
Tuepuke zambi.
Kiitikio
Ee Bikira wa mbinguni,
Uliye mama wetu,
Utusaidie sasa
Tufurahi mbinguni!
Mama pia duniani
Kwa watoto weusi,
Tungependa inchi yetu
Iwe inchi ya Kristu !
4
37

Sisi wote tutasali


Na kufanya sadaka
Tuipate neema hii
Inchi iwe yako.
Mama uliteswa sana
Chini ya msalaba.
Utaweza kusikia
Mateso ya inchi.
Utusaidie sisi
Na wandugu wetu
Tuonyeshe siku zote
Mapendo kwa wote.
TUNAKUSALIMU
(Vierge incomparable) Kiro chante p.8

Tunakusalimu, Maria mpole,


Utuangilie, Maria mwema !
Kiitikio
Maria utubarikie
Ukinge wakiro wako !
Nyota ya asubui, Maria mpole,
Mulango wa mbingu, Maria mwema !

Mama mpendelevu, Maria mpole,


Bikira mwamini, Maria mwema !

KUJA NDUGU
(Viens, ami, prends place dans la ronde)

Kuja ndugu yangu tufurahi.


Tutaimba wote mu umoja.
Kiitikio
Sisi wote tutatengeneza
bis
Urafiki, urafiki wetu
Tusahau teso na uchungu
Na magumu siku ya leo.

Tutacheza wote na furaha


Na kicheko midomoni mwetu.

Kama, kisha, tutaenda wote,


Tufahamu uzuri wa leo.
5
37

TWAJUWA KAMA MAISHA


(Comment sont tous les gars) Kiro chante p.9

Twajua kama maisha


Yapo mazuri, ohio,
Sababu hatuna woga :
Kristu yuko na Kiro !
Tukipigana kwa Mfalme
Tutashinda adui :
Kiitikio
Ohio, wakiro,
Ohio, tumo !
Atashinda watu
Kwa Kristu nani ?
Kiro !
Twajua kama wakiro
Wapo hodari ohio !
Twasema kama uzuri
Wa kweli uko ndani.
Tukipendana, wakiro
Tutapendeza Mfalme.

Twajua Kiro ni sisi


Tuwe wamini daima.
Na wote watatufuata
Twende mbele na heri !
Wengine wakitufuata
tutashinda pamoja !

TUKIONA INCHI YETU


(Le Kiro voit dans ses rêves) Kiro chante p.10

Tukiona inchi yetu


Yenyi rangi nyingi nzuri,
Tukamate pennon,
Mapigano yaanza !

Kiitikio
6
37

Wakiro njooni wote.


Tutamfuata mfalme.
Mfalme wetu atuita
Kwa kushinda naye !

Tukionya uaminifu,
Marafiki watakuja ;
Tutazidi pamoja
Mapigano kwa Mfalme !

Wote wataona haya


Wakitaka kutushinda.
Tutabaki wamini
Mpaka mwisho wa vita !

WAKATI WA SIKU NZIMA


(Au cours d’une journée) Kiro chante p.11

Wakati wa siku nzima


Twacheza na kicheko.
Wenzetu wapo wamini :
Twashinda pamoja nao !
Kiitikio
Ee, njooni watoto,
Wenyi nguvu kubwa !
Inchi yetu yaomba
uhodari (1° fois)
bis
Uaminifu (2° fois)
Wakiti wa mwendo murefu
Twaimba na furaha,
Sababu tupo wakiro
Twashika roho safi !

Wakati wa mchezo mgumu


Hatutaregeza moyo
Twataka kuwa hodari
Tushinde magumu yote !
WIMBO WA MANGARIBI
(Chant du soir) Kiro chante p. 12

Tupige aksanti kwa Mungu mwema


7
37

Kwa msitu na nyama wanamoishi.


Huwezi kupima uwema wake  :
Maua yavaa bushuti nzuri.
Tupige aksanti kwa Mfalme wetu.
Katika misitu : wimbo muzuri !
Na pepo yapashwa kumsifu Mungu.
Vidudu vyaimba kwa kumshukuru !

Aksanti Mungu kwa urafiki


Wa wale walio karibu yetu.
Aksanti Mwenyizi twapiga zamu ;
Bariki wakiro usiku huo !

KWA HERI MARAFIKI


(Quittons en paix) Kiro chante p.13

Kwa heri, marafiki,


Tutaenda kisha mkusanyiko.
Tutafuate mwito wa ngoma ;
Tuzime moto hapa !
Kiitikio
Marafiki, ngoma yaita :
Wakiro muwe tayari !
Kuenda pamoja kwa ushindi
Katika mapendo ya kweli.
Twende wakiro (wakiro)
Twende wakiro !
Wewe rafiki yangu,
Unipe mkono mwamini.
Wakati wa mapigano
Nitakumbuka urafiki.

Tuonye, marafiki,
Uhodari katika vita !
Utashi wa uaminifu
Kumpigania Kristu mfalme !
NDIYO CHEFU
Kiro chante p.14
Namtumainia chefu :
Ni rafiki mu mapigano.
Ataonyesha mfano :
Hataweza kujifanya mtumwa !
Kiitikio
8
37

Ndiyo chefu, nakufuata :


Ni nia yangu ya kikiro !
Nawe na kando yako
Naona uhodari !
Ndiyo chefu : neno kamili
Itaniendelesha vizuri.
Nawe na kando yako
Niko na nguvu na furaha !
Na wewe nitabaki
Mwaminifu mpaka mwisho.
Nikikufuata vizuri
Nitaweza kubeba bendera.

Wewe ulinitolea
Maisha yako ya kijana.
Sababu sikupoteza
Uhodari wangu wa roho.
MUONE WANA-NGOMA
(L’écuyer chante) Kiro chante p.15

Muone wana-ngoma
Wenzetu wema.
Tunapendana sana
Twaimba popote.
Kiitikio
Mutazame pennon zetu,
Halihi, halihe, haliho !
Kundi letu linafurahi :
Hali, halihe, haliho !
Mucheze bila woga,
Wenzetu wema.
Tufuate mwendo mwema
Pamoja na Savio !

Mupige ngoma nguvu


Watoto wa Kiro !
Tutajikaza sana
Tubaki wamini !
KATIKA JAMAA YA WAKIRO
(My sarie marais) Kiro chante p.16

Katika jamaa ya wakiro wa………..(1)


Mapendo ya kweli
9
37

Katika jamaa ya wakiro wa…………


Tabia ya urafiki.
Kiitikio
Kujeni wote
Ku Kiro yetu !
Mutafurahi.
Mu Kiro yetu
Umo urafiki mzuri bis
Uaminifu bora
Wakiro wetu watabaki wamini
Wakati wa vita !
Wakiro wetu watabaki wamini
Wakati wa ugumu.

Wachefu wetu watukinga daima


Katika hatari
Wachefu wetu watukinga daima
Na nguvu ya urafiki.
(1) Kwa mfano :……Lubumbashi

TWAJUA WANA-NGOMA
(Voyez les écuyers) Kiro chante p.17

Twajua wana-ngoma
Wakati wa mwendo
Walia na kusema :
“siwezi kufuata !”
Lakini kila Kiro
Apima kufuata.
Kiitikio
Donn, donn, donn, diridonn
bis
Donn, donn, diridonn
Lakini mwana-mkuki
Azani : « ni nzuri. »
Anajikaza kabisa ;
Siwezi kumfuata.
Mikulu yake mirefu ;
Lakini nguvu ni wapi ?

Muone mwana-ngao
Wakati wa mwendo.
Acheka siku zote
10
37

Hajui hatari.
Na kila mtoto ndugu
Anayempenda sana.

RAFIKI KUJA KWETU


Kiro chante p.18
Rafiki kuja kwetu,
Unipe mkono.
Tufanye kundi kubwa
La urafiki.
Kiitikio
Kijana kuja kwetu,
Pigana nami.
bis
Ujana uwe mfano
Wa vita hodari !
Rafiki cheza nami,
Sasa na daima,
Tuweze kufurahi
Katika ujana.

Rafiki twimbe nyimbo


Na nguvu pamoja.
Maisha yatakuwa
Mazuri kabisa.
TUNATEAMBEA NA FURAHA
Kiro chante p.19
Tunatembea na furaha
Marafiki wa Kiro.
Jua kali juu yetu ;
Tunaimba daima.
Ee marafiki wenyi nguvu,
Kamateni bendera !
Mukiunga kundi letu
Mutabaki hodari !
Kiitikio
Tupo wana-ngao wenyi nguvu
11
37

Ha ha ha ha ha ha ha ha ha !
Nyimbo zetu zaleta furaha
Ha ha ha ha ha ha ha !
Tutaingia misituni
Wana-ngao wa Kiro.
Tutacheza pale vema
Na furaha kabisa.
Ee we, rafiki ukipenda
Kuingia ku Kiro
Utasema mbio sana
Sitatoka kabisa.

Tunaporudi mangharibi
Tutachesa zaidi.
Kila siku kwetu nzuri
Inajaa furaha.
Sababu ya furaha hii
Ni usafi wa roho
Wote wanaweza kuja
Na kupata furaha.
WAKATI VIJANA WAKIIMBA
Kiro chante p.20
Wakati vijana wakiimba
Pamoja nami na wewe,
Bendera yetu yatukokota
Katika mwendo njiani.
Kiitikio
Najua vijana hodari
Karibu bendera yetu
bis
Watabaki wamini popote
Wengine wakituacha.
Wakati wakiro watembea
Kwa nguvu ya uaminifu,
Wachefu wetu watatuonya
Mifano yao popote.

Wakati wachefu wakiomba


Mapashwa magumu sana,
Wakiro wema watawatii
Katika furaha tena.

RAFIKI HODARI
12
37

(Mon ami est un gars) Kiro chante p.21

Rafiki hodari ni mwamini.


Siku zote ananikinga.
Atanipigaina mpaka kufa ;
Tutakufa na kicheko. (bis)

Kiitikio
Unipe mkono,
Popote njiani.
Tutaimba na furaha,
Tataimba na furaha
Rafiki, na furaha
Twende kwa ushindi,
Juani na pa baridi
Kwa kristu wetu mfalme !
Nampenda Rafiki: ni mwamini !
Na moyo wake ni ngao nzuri,
Tayari kulinda inchi yetu,
Atashindana na kicheko kweli. (bis)

Tumfuate rafiki : ni mwamini !


Pamoja tushike ujana mzuri.
Tupende bendera mpaka kufa
Tutajulisha uaminifu. (bis)

KAMA CHEFU ANABEBA


(Ami qui tient la bannière) Kiro chante p.22

Kama chefu anabeba bendera yetu


Tutamfuata siku zote na uaminifu.
Kiitikio
Nyimbo zetu hewani
Zitaalika watoto
Wamtum(i) kie Mfalme
Waaskari wake wema !
Ndugu ukitolea damu kwa Mfalme
Mimi sitaacha kupigana kwa Kristu.
13
37

Ndugu ukiona nzala, beba mkate wangu


Sisi pamoja tutashinda wote kwa Kristu.

MISITU YATUITA
(Déjà sont revenus) Kiro chante p.23

Misitu yatuita tufurahimo.


Kujeni wote tutaenda.
Mabonde na milima vyatungoja
Tutoke mbio nyumbani mwetu.

Kiitikio
Kamata mfuko na vitu vyako.
Katika furaha twendeni porini.
Usiogope rafiki :
Wakiro wako hodari.
Maua yananuka kando yetu.
Uzuri wao musangae.
Angalieni : Mungu yuko mwema.
Atutolea mwanga na yote !

Jua ni kali pale juu hewani.


Lakini haturegei.
Twataka kuonyesha nguvu yetu
Kuendelea bila shuruli.

NGOMA YAPIGWA NGUVU


Kiro chante p.24
Ngoma yapigwa nguvu
Muone mwendo :
Tupo wakiro sisi,
Munatutambua ?
Wote twaimba nyimbo
Tunapotembea !
Kiitikio
Ungeni kundi letu
Twendeni kwetu !
Ungeni kundi letu !
Twendeni kwetu !
Waamini, wahodari,
Mutazame bendera
14
37

Yetu daima :
Yarukokota, yataonyesha
Mwendo wetu
Katika maisha yote.
Bendera, peperuka!
Tutakufuata.
Tupo tayari wote
Kukupigania.
Kristu atatulinda
Katika vita !

Ngao mbele ya mwili


Tutoke mbio !
Tuwe hodari sasa
Pasipo woga:
Kristu atusaidia
Tushinde kwake !

TUKITOKA NA NGOMA
(Écoutez notre joie) Kiro chante p. 25

Tukitoka na ngoma na pennon zetu


Na vinanda vipigavyo nyimbo zetu,
Twafurahi wakati wa wimbo wetu,
Twafahamu uzuri wa kundi letu.

Kiitikio
Ona jua juu,
Na wakati mzuri,
Na kicheko chetu
Midomoni mwetu.
Tunapenda kucheza na marafiki
Na watoto wamini wa kundi letu.
Kwa wakiro maisha mazuri sana
Na ujana ni mfano wa furaha.

Twapigana kwa Kristu na sifa yake


Kwa silaha za furaha na mapendo.
Kristu Mfalme ni nguvu na msaada wetu
Tueneze popote ufalme wake.
15
37

KUJENI MBIO
(Allons les gars…) Kiro chante p.26

Kujeni mbio nyinyi wakiro,


Muangilie uzuri
Wa kundi letu likitembea
Na wimbo mzuri wa furaha.
Kiitikio
Sikiliza ngoma
Ikipigwa nguvu
Kiro anakuja !
Piga ngoma nguvu, bis
Imba wimbo wetu
Wimbo wa ushindi !
Bendera zetu zapeperuka :
Alama nzuri za Mfalme.
Na siku zote tunazifuata
Juani na mvulani

Na Kristu Mfalme atutazama


Na kubariki wakiro !
Wakati tukipita mbele
Tumsalimie Mfalme !

WAKIRO WAKO WAMINI


(Nos bandes marchants) Kiro chante p.27

Wakiro wako wamini,


Wakiro wapigana.
Kwa Kristu Mfalme wao
Popote bila woga.
Kiitikio
Roum… roum…roum…
Ni mwito mzuri wa ngoma.
Na vibendera vyetu vinakuja
Sisi wakiro tutalinda bendera
Katika mapigano kila siku
Twabaki wamini kwa Mfalme.
Ufuate, Kiro, vizuri :
Mapendo yakuita.
Uone uzuri wa vita
Kwa Kristu Mfalme wa kwetu
16
37

Vijana kujeni wengi


Twendeni kwa ushindi ;
Bendera ya Kiro mbele
Na sisi wote hodari.

JAMAA YETU YA KIRO


(Nos bandes Kiro s’élancent) Kiro chante p.28

Jamaa yetu ya Kiro


Yamtum(i)kia Mungu wake.
Twamletea silaha zetu.
Hatuna woga kwake! (bis)

Kiitikio
Nia yet(u) ni moja tu kwetu,
Ni nia ya kila Kiro !
Kumtum(i)kia Kristu Mfalmewe,
Vitani kuona hodari !
Tazama mwendo wa Kiro,
Sangaa nguvu yake.
Katika njia za inchi
Waimba heri wao (bis)

Wengine wakitufuata
Wataona furaha nasi
Fuateni wote watoto
Mpaka ushindi mkubwa (bis)

TUFUATE BENDERA
(Ami, la route est devant nous) Kiro chante p.29

Tufuate bendera ya Kiro


Wakati wa mwendo !
Upepo unaimba ndani
Ya bendera zetu.
Kiitikio
Wakiro imbeni
Vizuri njiani !
Sisi tutamsifu
Kristu popote njiani.
17
37

Wakiro mubaki waminifu !


Vijana, twatembea vizuri
Katika urafiki !
Tutajulisha uaminifu!
Popote duniani !

Rafiki piga ngoma nguvu


Hatusimami sisi
Jamaa inaendelea
Tufuat bila woga

Bendera inatangulia
Wakiro wafuata.
Upepo inacheza nayo
Tupende bendera.

SISI WAKIRO
(Pleins d’allégresse) Kiro chante p.30

Sisi wakiro twafurahi daima.


Njia ya furaha : njia yetu.
Kicheko chetu kinakokota
Wengi ku Kiro.
Maisha yote kwa Kristu Mfalme!
Kiitikio
Falderi, yupi, yupi, ee
Ha, ha, ha ! bis
Falderi, yupi, yupi, ee !
Katika vita, Kiro, uwe hodari,
Ukajaribu kujitolea.
Fuata wachefu katika vita
Mpaka ushindi
Maisha yote kwa Kristu Mfalme.

Tutaeneza utawalo wa Kristu


Sisi na wote wanaopenda.
Tukipigana kwa Kristu Mfalme
Katika furaha,
Dunia yote itakufuata.
KIPWA INAPOKARIBIA

(Toi qui veux conquérir) Kiro chante p. 31


18
37

Kipwa inapokaribia
Twasikia nguvu ;
Nguvu kubwa ya damu
Inatukokota inje.
Kiitikio
Twendeni wote wakiro
Fuateni bendera.
Wakiro wanapenda
Kuimba njiani ;
Twataka kundi lifike
Katika furaha.
Don Bosco awe mulinzi wetu
bis
Katika mwendo.

Tukirudi mangharibi
Twaonyesha kicheko.
Tukichoka kabisa
Hata moja halalamiki.

Mvua inatupigilia
Sawa fimbo kali
Hatuoni uchungu
Tunavumilia yote.

TUONGEZE MWANGA
(Plus de joie) Kiro chante p .32

Tuongeze mwanga ,furaha,


Mwanga na furaha
Siku zote mgini mwetu.
Tufurahi sisi sote
Tufukuze teso na uchungu
Kwa kicheko.
Kiitikio
Cheka ! Mtu wa kweli
Anapanda furaha
Kando yake !
Cheka ! dawa ile
Yakuponya.
19
37

Cheka! Siku zote !


Usizani kama furaha
Yaangaze siku zote
Na popote bure.
Tukitaka kufurahi
Sherti tuwatumikie
Ndugu na jirani.

Kwa kicheko kundi letu


Litajitolea
Kwa kuwapa watu furaha.
Na sadaka hii nzuri
Itatuletea mwanga
Na furaha pamoja.

NJIA YA WA KIRO
(La route que suivent…..) Kiro chante p.32

Njia ya wakiro
Ni njia nzuri sana.
Njia ya urafiki na furaha
Njia nzuri !
Kuja wewe rafiki,
Uunge kundi letu.
Njia ya wakiro
Ni njia nzuri sana.

Nyimbo za wakiro
Zinapanda hewani.
Nyimbo za urafiki wa jamaa
Nyimbo nzuri.
Imba wewe pia
Pamoja na wakiro.
Nyimbo za wakiro
Zinapanda hewani.

Tabnia ya Kiro
Tabia nzuri sana.
Tabia ya uwema na furaha
20
37

Tabia nzuri!
Usingoje rafiki
Kuunga kundi letu.
Tabia ya Kiro
Tabia nzuri Sana.
JUA LIKO JUU YETU
Kiro chante p.33
Jua liko juu yetu,
Ndege zinaruka.
Vipepeo na vidudu
Vinamsifu Mungu
Sisi pia tutaimba
Nyimbo zetu za aksanti !
Kiitikio
Sifu Kristu Mfalme wetu !
Beba bendera na furaha.
Kuja kwetu na ushindi,
Mwana-ngao wa Kristu !

Pepo ikivuma kwetu


Kiro hana woga !
Watembea na bendera
Wakiimba nyimbo !
Siku zote wanaimba
Mgini mwao na popote !

Na wakati wa baridi
Mutaona Kiro !
Wakipita kwenu mbio
Na bendera mbele !
Wanapenda kujikaza
Kwa mapashwa ya vijana !
KESHO TUTAONDOKA
(Demain nous partirons) Kiro chante p.34

Kesho tutaondoka kwa vita


Tama ya ushindi ni kubwa.
Kiitikio
Tuwe hodari
Pasipo woga
bis
Kristu apigana
21
37

Na wakiro !
Kule adui atungojea ;
Ataka kutupiga na nguvu.

Kiro, twendeni mbio pamoja,


Rafiki wa kweli mpaka kufa.

Labda nitaanguka mu vita.


Lakini we pigana zaidi.
WAKIRO MUBAKI WAMINI
(Les Kiro combatant) Kiro chante p.34

Wakiro mubaki wamini


Kwa Mfalme wa mbinguni.
Twataka kushinda pamoja.
Ao kufa na kicheko.
Kiitikio
Adui akitupiga
Hatutamwogopa ! bis
Sababu na nguvu ya Kristu
Tutamshinda vyepesi !
Tukiona vijana wa sasa,
Twasikia uchungu,
Sababu wanasikiliza
Adui wa roho.

Lakini wakiro wa kweli


Wamfuata Chefu wao.
Wajua matuzo mazuri
Tayari kwa kila moja.
TWATEMBEA WOTE PAMOJA
Kiro chante p.35
Twatembea wote pamoja
Tukiimba nyimbo zetu.
Kando yetu ona porini
Maua yachanuao bis

Misikie mwito wa miti


Yarudisha nyimbo zetu !
Zinapanda mbio hewani
Zabeba furaha yetu ! bis

Twatembea wote pamoja


22
37

Mpaka jua litatua.


Na bendera inatangulia
Alama ya Mfalme wetu ! bis

………………..NCHI YETU NZURI


(Viens chez nous) Kiro chante p.36

…, nchi yetu nzuri


Jiwe la zahabu !
…, nyumba nzuri
Furaha ya Kiro

Strophe 1
Nyama, ndege, vidudu,
Nzige nyingi tena,
Zaimba bila neno
Mufalme Mwenyezi.

Mu………… roho ina


Moto kabisa.
Na tama zakimbia
Na jua kali.
2
………… twakuita
Sifa ya Afrika.
Tutaimba daima
Uhodari wako !

3
Inchi yetu………………..
Twakupenda kweli.
Kwa sababu wakiro
Watabaki kwako.

JUA LIKIANGAZA
Kiro chante p.37
Jua likiangaza vizuri
Maua yachanua porini.
Fungua vyepesi roho,
Moyo wako.
Uzuri huo usitupwe.
Kiitikio
Tembea njiani
23
37

Na kundi letu la furaha.


Uimbe nyimbo zako na wakiro.
Pandisha bendera :
Itaonyesha popote
Huku ni Kiro kweli!

Upepo ukivuma na nguvu


Bendera zetu zapeperuka.
Mwanga wa jua :
zahabu mitini.
Vipepeo vinaruka !

FUATENI DOMINIKO SAVIO1


(Voici les Kiro qui s’avancent) Kiro chantep.38

Fuateni Dominiko Savio


Kijana na kicheko
Alikuwa rafiki kwa wote
Yuko mfano wa Kiro mwema. Bis

Kiitikio
Tukimweshimu mlinzi wa Kiro
Tutamfwata katika mwendo
Hatutamwogopa adui
Savio atatukinga. bis
Fuateni furaha ya Savio
Mapendo na urafiki
Mutaona uzuri wa Kiro
Mukifuata mifano yake. bis

Fuateni usafi wa Savio


Asili ya furaha
Tukitaka kubaki wamini
Atakuwa rafiki wetu. bis

1. Wakiro wanawake wanaweza kuimba


Fuateni Maria Goretti

TUKITEMBEA
Kiro chante p.39
24
37

Tukitembea tunafurahi
Tunapoimba watu watusangaa.
Misitu, milima yajibu nyimbo
Uzia ukiwa hatusimami.
Kiitikio
Maisha mazuri
Katika ujana.
bis
Bendera yetu
Yapiga zamu !
Tukichukua bendera zetu
Katika wimbo : nguvu na furaha.
Tusiwe na woga, twendeni mbio
Kushinda dunia kwa Kristu Mfalme.

Tukiondoka kwa safari ndefu


Tunasahau teso la darasa,
Na mwanga wa jua yaleta furaha.
Wakiro kujeni ; hatusimami !

WAKIRO WAIMBA
(Les bandes Kiro que de joie) Kiro chante p.40

Wakiro waimba wakipigana


Kwa Kristu na sifa yake.
Wakiro waimba kitumaini
Kwa Mfalme wa jeshi letu.
Tunajujua sisi wakiro
Kama Kristu ni Mfalme Mwenyezi.
Kiitikio
Kwa sababu tuna furaha
Wakati wa mapigano.
Tiralala, tiralala,
Tiralala, tiralala.
KIRO
Kwa sababu tuna furaha
Wakati wa mapigano.

25
37

Wakiro wapenda uaminifu


Mpaka mwisho wa mapigano,
Na kila kijana atumaini
Uhodari katika wote.
Kila Kiro ni rafiki
Mwaminifu katika magumu.

Siwezi kuacha rafiki wangu


Peke yake mu mapigano
Najua : pamoja twashika vema
Urafiki katika Kiro.
Sisi marafiki wa kweli,
Twapendana na kulindana !

RAFIKI MWEMA WA KIRO


(Venez, garcons chez le Kiro) Kiro chante p.41

Rafiki mwema wa Kiro,


Tembea na sisi.
Usafi wako ushike,
Usafi mzuri mno !

Kiitikio
Kicheko usoni na kusudi bora
Ukarimu utatuongoza
Na tutafana na Don Bosco
Tukifurahi, tukifurahi,
Tutashinda wote, tutashinda wote
Kwa kicheko chetu. bis

Watoto wema wa kwetu


Mucheze na sisi
Katika mchezo : furaha
Kwa mwili na roho !

Rafiki, mwema wa Kiro


Uimbe na sisi !
Sauti yako ilie
Katika Katanga !
26
37

MARAFIKI KUJENI WOTE


(A travers les forêts) Kiro chante p.42

Marafiki kujeni wote


Na kuona furaha leo.
Tungependa mufike mbio
Na kucheza vizur mno
Popote twatembeamo
Nyimbo zetu zitaleta furaha
Tutaonyesha kwa mwendo wetu
Urafiki katika Kiro.

Mukiona wakubwa wetu


Musangae myendo yao.
Kundi la mwana-ngao wetu
Linafuata na kicheko.
Na wana-ngoma wafanya nguvu
Hawataachwa katika mwendo
Jamaa yote yapashwa kufika
Karibu ya kikomo.

WAKIRO WAPO HODARI


(Les Kiro sont toujours joyeux) Kiro chante p.43

Wakiro wapo hodari


Vijana wamini, wamini,
Wanaenda pa ushindi
Hawana woga bis
Juni valle valle valle valle lala
Juni valle valle valle valle lala
Wanaenda pa ushindi,
Hawana woga.

Waimba wimbo wao


Na nguvu porini na njiani
Waingia ku maisha
Ya kweli bis
27
37

Juni valle…
Waingia…

Vijana musikie
Katika furaha aminifu
Munapashwa kukokota
Wengine wengi bis
Juni valle…
Munapashwa…
WATU WOTE KUJENI
(Admirez le Kiro) Kiro chante p.44

Watu wote kujeni muone Kiro


Muone Kiro : wanapita njiani. bis
Mutaona kundi la furaha
Watoto waminifu.
Watu wote mushike ukumbuko
Ukumbuko wa furaha ya Kiro.

Watu wote kujeni mus(i)kie Kiro


Mus(i)kie Kiro : wanaimba njiani ! bis
Mutaona kundi la furaha
Watoto waminifu.
Na vijana ungeni Kiro yetu
Kiro yetu katika furaha.

Nyinyi wote kujeni mufuate Kiro,


Mufuate Kiro : mutaona furaha. bis
Mutakuwa pia wamini
Watoto wema sana.
Nyinyi wote onyeni urafiki
Urafiki kwa vijana wa Kiro.

TUNAPOAMKA ASUBUI MAPEMA


(Sous le soleil) Kiro chante p.45

Tunapoamka asubui mapema


Jua linatuita.
Tunatembea vyepesi ku Kiro
Kwani ni kundi nzuri.
Kiitikio
Na virongozi wa kundi letu
28
37

Wapo vijana na furaha.


Sisi wakiro, tunaimba (bis)
Tunapoimba wakati wa mwendo
Njia si ngumu kwetu.
Tunapocheza pamoja vizuri
Siku ni fupi kwetu !

Tunaporudi kiisha michezo


Kicheko midomoni,
Tunatakia kurudi vyepesi
Katika Kiro yetu.
TUNAPENDA KUTEMBEA
(Le soleil dore la route) Kiro chante p. 45

Tunapenda kutembea
Tukiimba nyimbo.
Tunajua kama leo
Ni wakati mzuri.
Kiitikio
Tembea Kiro,
Bila mashuruli.
Beba bendera
Kwa Kristu !
Kama mfuko uko mzito
Tusionye uchungu.
Moyo wetu utabaki
Na furaha daima.

Mangharibi tukirudi
Tunachoka sana.
Siku ilikuwa nzuri
Twimbe tena pamoja.
KUJA NASI RAFIKI
(Viens avec nous) Kiro chante p.46

Kuja nasi rafiki


Tufurahiwe pamoja.
Furaha ya kikiro
Iwe yako !
KIITIKIO
Alio, alio, alio, alio
29
37

Twimbe, tucheke na furaha


Ha ! Ha !
Alio, alio, alio, alio,
Heri yako mu Kiro !
Oh ! Oh !
Kuja nasi rafiki
Kucheza msituni, ha, ha !
Vilima na mabonde
Yatungoja.

Kuja nasi rafiki


Njiani mwenyi kunyoka
Itatusimamisha
Katika mwanga.

Kuja nasi rafiki


Tuimbe nyimbo za furaha
Hatutasononeka
Sisi wakiro.
VUTENI MAKASIA
(Rame avec cran) Kiro chante p.47

Vuteni makasia
Na nguvu ya wimbo.
Mtumbwi wetu ukifika
Tutasahau teso.

Kiitikio
Ohe rafiki (Ohe rafiki)
Twende rafiki (Twende rafiki) bis
Funga nguo ya mtumbwi
Bendera juu kabisa.
Imbeni wote wakiro
Nyimbo zenu za furaha
Tukiziimba vizuri
Tutajulisha Kiro.

Fuateni wengine wote :


Tumtumikie Mfalme.
Alama yake ni nzuri
Tutaikinga vema.
30
37

SASA WAKIRO WENGI


(Le beau soleil se lève) Kiro chante p.48

Sasa wakiro wengi waimba njiani


Sababu wanaona wakati mzuri
Wakati mzuri !
Na wengi watakuja
Waunge kudi letu.
Tuimbe Kwa Kristu Mfalme wetu. (bis)

Wakiro wetu wote wanafurahi.


Katika macho yetu mwanga muzuri
Mwanga muzuri !
Twapigana na nguvu
Kwa Kristu Mfalme wetu
Na moto wa moyo hauzimiki. (bis)

Myoyo yetu mema : tunapendana,


Sababu Kristu Mfalme atuongoza
Atuongoza.
Katika inchi yetu
Wakiro watakuja.
Tukokote wenzetu kwa Mfalme. (bis)

KWA DON BOSCO


(A ta gloire, ô Don Bosco) Kiro chante p.49

Zamani mu Italia
Padri mmoja alifika,
Kwa watoto waliokuwa
Na hatari kubwa sana.
Leo pia anakuja
Akalinde watoto
Weusi na weupe
Wamupende Mungu mwema.
Kiitikio
Don Bosco utupe baraka yako
31
37

Uitwe Baba na Mlinzi wetu.


Don Bosco utupe msaada wako
Uitwe Baba na Mlinzi wetu.
Tupigane kama Don Bosco
Kwa ufalme wake Kristu.
Roho zetu ziwe hodari
Na amini siku zote.
Padri mwema wa mbinguni
Tunataka kukufuata.
Katika njia njema
Twatembea na furaha.

TEMBEA NJIANI
(Quittant les rues de nos cités) Kiro chante p.50

Tembea njiani, Kiro,


Katika furaha.
Na nyimbo zako za Mfalme
Zipande hewani.
Kiitikio
Ee, Kiro, Kiro, Kiro twende
Pamoja njiani (Njiani)
Ee, Kiro, Kiro, Kiro twende
Majeshi ya Kristu !
Tembea njiani Kiro
Kikomo ni karibu.
Furaha yetu ingare
Daima usoni.

Wa Kiro tusisahahu
Kicheko nyumbani.
Popote tunapitamo
Tulete furaha.

Na uhorari wa Kiro
Ni kitu cha ajabu.
Wapata uzuri wote
Karibu na Kristu.

MUONE BENDERA YA KIRO


32
37

(Ecoutez le chant de nos bandes) Kiro chante p. 51

Muone bendera ya Kiro  :


Inapeperuka mbele.
Wakiro wanafuata
Na nyimbo zao nzuri. (bis)

Kristu Mfalme anatuita


Tuulinde ufalme wake.
Tuwaze kama Kiro
Ni kundi jaminifu. (bis)

Jua juu yetu ni kali


Wakati wa mwendo wetu.
Wakiro wanataka
Kuonya uhodari. (bis)

Sikia : ni mwito wa Mfalme


Rohoni mwa kila Kiro !
« Tayari ! », tutajibu
« Kufa kwa Kristu Mfalme ». (bis)

WIMBO USIO NA JINA


(Chantons ensemble) Kiro chante p.51

Sikia wimbo muzuri wa


Tralalalalalalala tralala.
Hakuna mzuri zaidi ya
Tralalalalalalala tralala.

Kiitikio
Trala tralalalala
Trala tralalalala lalalala
Tralala tralala lala !
Sikia msemwa wa kwanza ; ni : tralala…
Habadiliki kabisa ; ni : tralala…

Na strophe ya pili ni sawa ; ni : tralala…


Inasimulia vizuri na : tralala…

Unatambua ya tatu ; ni : tralala…


33
37

Ni sawasawa daima ; ni : tralala…

Hatutaacha kuimba ya : tralala…


Na pole pole ni bora ; ya : tralala…

Na tukiimba na nguvu ya : tralala…


Dunia yote yafurahi na : tralala…

Tuimbe mara ya mwisho ya : tralala…


Ajabu hii ya wimbo ; ni tralala…

WANA-NGOMA, WANA-NGAO
(Vois la route) Kiro chante p.52

Wana-ngoma, wana-ngao,
Wana-mkuki wa Kiro,
Tutakuja, tutashinda
Tukipiganiamo.
Kiitikio
Holai, holao,
Holai lai lai lai lao bis
(1° fois : hilalala !)

Marafiki, twatembea,
Tunaimba na furaha,
Kila siku ni zawadi
Mungu mwema kabisa !

Marafiki tukicheza
Na wenzetu wa Kiro,
Kila moja atasema
Kiro : kundi nzuri mno !

Na kiisha tukirudi
Kwa wazazi nyumbani,
Bila shaka watesema  :
Mtoto ni muzuri, oh !

RAFIKI UTABEBA BENDERA


(Ami, tiens haute….) Kiro chante p.53

Rafiki utabeba
34
37

Bendera, bendera mu vita.


Pamoja tutakokoka
Vijana, vijana ku Kristu.

Kiitikio
Katika vita tuwe hodari
Twataka kushinda.
Hodari wakiro,
Musiache kupigana.
Rafiki utashinda
Adui, adui mu vita.
Popote utaonyesha
Uwema, uwema wa Kiro.

Rafiki utumaini
Daima, daima kwa Kristu.
Sababu unafahamu
Uwezo, uwezo wa Mfalme.

Rafiki usisahau
Imara, imara ya Kiro.
Wakiro watatolea
Maisha, maisha kwa Mfalme.

BANS CHANTES
1. Bravo, bravo, bravo,
Bravissimo !
Bravo, bravo, bravissimo!
Kiro chante p.15

2. Brabrabra bravo !
Brabrabra bravo!
Bravo, bravo, bravo, bravo !
Kiro chante p.16

3. Ni nzuri, nzuri, nzuri, ee !


Ni vema, vema, vema, ee !
Ni nzuri, nzuri,nzuri kabisa !
Ni vema, vema, vema, ee !
TUNAKUFWA NZALA
Kiro chante p.35
Tunakufwa nzala, wana !
Nguvu yetu inaisha.
35
37

Mama yangu, ee mama !


Nzala, nzala, nzala, ee !

NDUGU YANGU (CANON)


(Frère Jacques) Kiro chante p.50

Ndugu yangu, ndugu yangu


Walala ? Walala ?
Pigeni kengele, pigeni kengele !
Bim-bam, bim-bam, bum !
UNAJUA WAKIRO
(Connais-tu les Kiro) Kiro chante p.52
Unajua wakiro
Vijana wema ?
Watembea wima
Na wanaimba.
Kiitikio
Heri na Ki
Heri na Ro !
Heri na Kiro
Na kwa vijana !
Unaona watoto
Wadogo sana ?
Wana-ngoma wa kweli :
Hawana woga.

Wana-ngao kujeni
Kuonyesha nguvu !
Wapenda kucheza
Na kufanya mzaha !

Na wale wakubwa,
Wana-mkuki wetu !
Marafiki wamini,
Wacheza nguvu !

Wachefu wa Kiro,
Hodari sana !
Hawachoki kabisa
Wakichunga mchezo !

Munajua jamaa
Ya Kiro yetu !
36
37

Mukitaka kufuata
Mutapata heri.

37

You might also like