Professional Documents
Culture Documents
Mama Yangu Jini Jet
Mama Yangu Jini Jet
Kimeandikwa na
HUTOLEWA NA KUSAMBAZWA
NA A $ S DESIGNING
SIMU: 0713 335560
0788 943433
DAR ES SALAAM
TANZANIA
ONYO
******************
Mwezi mmoja baadaye nikiwa nimeshaanza kazi, siku hiyo akaja dada
mmoja ambaye aliajiriwa kwa kazi ya kwenda kununua vifaa mbalimbali
vya ofisi (purchasing) akaniambia kuna mgeni wangu mapokezi anaitwa
Henry.
15 mama YANGU NI JINI
Nilitoka mbio ili nikamlaki Henry ambaye ni mdogo wangu, nilimkuta
amekaa kwenye benchi la wageni, mkononi ameshika begi.
Aliponiona alisimama, akanikaribia, tukakumbatiana na kuulizana hali
pamoja na habari za safari kisha nikampeleka nyumbani.
Cha ajabu, tukiwa njiani tunakwenda, sikumuuliza habari za nyumbani
atokako wala yeye hakuniambia nyumbani kukoje au mama anaendeleaje
baada ya kufika kwangu.
Nilisukuma mlango, sebuleni alikaa msichana wa kazi, anaitwa Sekindole.
Huyu ni mwenyeji wa Kijiji cha Kidamali, Iringa, nilizoea kumwita Segito
kwa sababu nilijua ni mhehe, halafu mwanamke.
“Segito kuna mgeni, mpokee begi,” nilimwambia nikikaa kwenye kochi
kubwa.
Henry naye alikaa kwenye kochi dogo akiwa ameshapokelewa begi lake
na Segito.
Usoni, Henry alionesha alikuwa na mambo mengi ya kuzungumza na
mimi, lakini alikuwa akisita.
“Segito,” nilimwita msichana.
“Abee kaka.”
“Mama yuko wapi?”
“Amelala.”
“Aaa, sasa sikia.”
“Abee kaka,” aliitikia Segito akija sebuleni na kupiga magoti pembeni
yangu.
“Huyu mdogo wangu anaitwa Henry, kaja kutoka nyumbani. Mtengee
maji ya kuoga, mpe chakula kisha utamuonesha chumba kile cha mwisho
atapumzika kidogo mpaka mimi nitakaporudi, sawa?”
“Sawa kaka.”
Nilisimama ili kurudi kazini huku nikimpa Segito maelekezo mengine:
“Halafu mama akiamka aje sebuleni kusalimiana na mgeni.”
“Sawa kaka.”
Nikamuaga Henry ili nirudi kazini. Nikiwa njiani sina hili wala lile, nilisikia
nikiitwa:
“We Damas…Damas wewe.”
Niligeuka kwa mshtuko, kumbe alikuwa msichana mmoja anaitwa
16 mama YANGU NI JINI
Salome anatoka kwenye ukoo unaoitwa Mangula. Niliwahi kuwa na
uhusiano naye, nilipokutana na marehemu Jennifer nikambwaga, lakini
pia kwa sababu alikuwa machepele f’lani.
“Za siku Damas?”
“Nzuri Salome, vipi za siku na wewe?”
“Nzuri, za safari, za Ulaya?”
“Salama, nimerudi salama.”
“Nasikia umerudi na mwanamke wa kizungu?”
Niliishia kucheka kwani haikuwa kweli, lakini nilishtuka jambo moja,
alipendeza na kuvutia kuliko wakati akiwa na mimi.
“Nasikia umeolewa, ni kweli?”
“Wala sina huo mpango Damas, mimi mume wangu ni wewe tu, najua
Jennifer hayupo basi nafasi yangu ipo palepale.”
Maneno yake yalinifanya nishawishike kupanga naye muda wa kukutana
na mahali gani ili tuongee kwa kirefu, akakubali, tukaachana mimi
nikaendelea na safari ya kwenda kazini.
Hatua kama saba toka niachane naye, niligeuka kumwangalia lakini
sikumuona, nikajua aliingia kwenye vichochoro.
Nikiwa kazini, muda mwingi niliwaza kuhusu Salome. Kwamba ni
mwanamke anayeweza kuchukua nafasi ya maisha yangu kwa kuwa
mke. Niliamini ametulia kwani hata mwonekano wake ulionesha hivyo.
Nikaamua kujipa moyo mi mwenyewe kwa kupania kwamba lazima
nimuoe Salome.
Basi, nilipotoka kazini nilikwenda kwenye baa ambayo tulipanga kukutana
na Salome, sikutaka kumpigia simu licha ya kwamba tulibadilishana namba
ya simu. Lengo langu kujua yeye alikuwa na nia na mimi moyoni mwake?
Ile nakaa tu, simu ya Salome ikaingia, nikaipokea na kumjulisha
nimeshafika, nimeshakaa. Akasema anakuja ndani ya dakika saba tu.
Ikawa hivyo kweli, alifika akiwa amevaa tofauti na alivyovaa awali, safari
hii alipendeza sana.
Salome alionekana amekuwa mpya kwa tabia na mwonekano, alijionesha
ni mwanamke mtulivu, mwenyewe kujiheshimu.
Siku hiyo tuliongea mengi sana na msichana huyo, hadi ikafika mahali
nikamwambia nia yangu ya kumuoa, akakubali bila kuzuizi huku akisisitiza
kuwa, hata nilipomwacha mara ya kwanza aliamini kisa ni Jennifer lakini
alijua kuna siku tutarudiana kwa sababu siku zote ndoto zake mimi kuwa
mumewe.
17 mama YANGU NI JINI
Basi, kwa jinsi nilivyotokea kumpenda sana kwa mara nyingine,
nilimsimulia kuhusu mama kuwepo nyumbani, akanitaka tuongozane
hadi huko akamsalimie na kumfahamu pia.
Tulifika nyumbani na kukuta msichana wa kazi, Segito, akatupokea mimi
na Salome mpaka sebuleni, baada ya salamu nilimuuliza aliko Henry,
akasema alikwenda kulala.
Mara mama alitokea kabla sijamuulizia…
“Mama vipi, ulilala?”
“Eee, ndiyo naamka”
“Pole sana mama yangu. Huyu anaitwa Salome.”
“Aaa, hujambo mwanangu?”
“Sijambo mama, shikamoo.”
“Marahaba.”
“Habari za safari, habari za nyumbani?”
“Kwema tu.”
“Mama.”
“Abee.”
“Huyu ni mchumba wangu, ndiye ambaye natarajia kumuoa.”
Mama alimkazia macho Salome kisha akasema:
“Nimebariki, lakini msichezeane.”
“Hakuna kuchezeana mama,” Salome alimjibu.
Pia nilimwita Segito na kumtambulisha kwa Salome, Salome naye
nikamtambulisha kwa Segito.
Nilimuuliza mama kama amekutana na Henry, akaonekana kushtuka,
lakini niliona ni sawa kushtuka kwani hakujua kama amefika.
“Ngoja nimwamshe,” nilisema nikitoka kwenye kochi kwenda chumbani
kwa Henry. Nilimwamsha Henry nikimwambia mama anataka kumsalimia,
akatoka kitandani akionekana kuchoka sana.Lakini nilipofika sebuleni,
mama hakuwepo, alibaki Salome tu.
“Yuko wapi mama?”
“Ameingia ndani,” alisema Salome.
Nilimtambulisha Salome kwa Henry, wakasalimiana na palepale Salome
alianza kumwita Henry shemeji. Nilisimama, nikamsimamisha na Salome,
tukaenda chumbani tukimwacha Henry pale sebuleni.
Kule chumbani nilimwonesha Salome chumba kilivyo, akafurahi sana
akisema anatamani awe mama mwenye nyumba kuanzia siku hiyo,
nikambusu. Tulipotaka kutoka, alishika tumbo akisema linamkata ghafla,
18 mama YANGU NI JINI
nikashangaa. Nilimwomba akae kitandani hadi litulie kwanza, akafanya
hivyo na mimi nilikaa jirani yake.
Baada ya dakika tano akasema limetulia, tukatoka mpaka sebuleni.
Nilimuuliza Henry kama mama alitoka, akasema wameshasalimiana,
amerudi chumbani kwake anasema anajisikia kuchoka.
“Oke, haina shida, mimi namsindikiza shemeji yako.”
“Sawa kaka.”
Salome alimuaga Henry tukatoka. Tulitembea kwa kushikana
mikono, njiani Salome aliniambia nienda naye hadi nyumbani kwake,
nikamkubalia.
Salome alipanga kwenye nyumba yenye sebule na chumba kimoja,
lakini vidogo sana, baadhi ya vitu alivibebanisha kutokana na udogo wa
vyumba.
“Hapa lazima uhame Salome,” nilimwambia.
“Sasa baba si niko chini yako, wewe ndiyo utanipangia siku ya
kuhama.”
Kifupi tuliongea mambo mengi sana na Salome, tukapigana mabusu
mazito mazito. Nilitumia kama masaa matatu pale, mpaga giza liliingia,
nikarudi nyumbani.
Nilikuta Henry amelala akimwambia Segito anahisi maumivu ya kichwa,
lakini alishakunywa dawa. Mama pia alilala, hata hivyo wote walishakula
chakula cha usiku.
Niliingia chumbani kwangu, nikatoa nguo na kuvaa taulo kisha nikaenda
kuoga. Niliporudi nilikaa sebuleni kuangalia tivii kisha nikaenda kulala.
Usiku nilijikuta nina mawazo kuhusu mama na Henry, kwamba
kibinadamu nilitakiwa nikae nao kwa pamoja na kuongea mambo mengi
ya kijijini walikotoka, Henry ndiye angeweza kunipa mwanga kuhusu
safari ya mama.
“Itabidi asubuhi nifanye hivyo kabla sijaenda kazini,” nilisema moyoni,
nikapitiwa na usingizi, nikalala.
Usiku niliota ndoto bado niko nchini Sweden, Henry kanipigia simu,
nikaipokea:
“Shikamoo kaka.”
“Marahaba Henry, za huko, mbona kama unalia?”
“Kaka, mama amefariki dunia?”
“Ha! We Henry, unathubutu vipi kumsingizia mama kitu kikubwa kama
hicho? Una akili kweli wewe?”
19 mama YANGU NI JINI
“Kama ni kweli.”
“Alikuwa anaumwa?”
“Ndiyo kaka.”
“Nini?”
“Tatizo lake ni lile lile ulilomwacha nalo.”
“Ha! Mnazika lini? Maana mimi sidhani kama nitaweza kuwahi mazishi,
kuna muda wa kuandaa safari kutoka huku kuja huko.”
“Mimi nimekutaarifu kaka ili ujue huna mama,” simu ikakatika kwa
ghafla, baada ya hapo sikumpata tena hewani. Nililia sana, nikaishiwa
nguvu. Kuanzia hapo niliichukia Sweden. Ghafla niliamka, machozi
yalikuwa bado usoni, nikajifuta nikiamini nipo Sweden kwenye chumba
amacho nilikuwa nakitumia, lakini nilipoangaza kulia na kushoto
nikagundua niko Njombe na ile ni ndoto tu, nikanyoosha mkono juu
kumshukuru Mungu ingawa nilijiuliza tafsiri ya ndoto ile ni nini, sikupata
jibu.
***
Asubuhi niliamka, nikaenda kuoga, nilipotoka nilikutana na Segito.
“Mama na Henry wameamka?”
Nilimuuliza Segito kabla hata ya kumjulia hali. Mapigo ya moyo wangu
yalibadilika kila sekunde moja ilipoondoka kwenye dunia. Kilichonishtua
zaidi ni kuona Segito hajibu nilichomuuliza licha ya kuamini kwa asilimia
mia moja kuwa alisikia nilichomuuliza.
“We Segito, si naongea na wewe au hunisikii?” nilirudia huku safari hii
nikitoa sauti yenye ukali na mamlaka kidogo.
“Mmh, kaka samahani,” Segito alishtuka sana huku akijitahidi kukaa
sawa na kunijibu:
“Henry aliamka kaka, akaja sebuleni, lakini akarudi tena chumbani.
Mama yeye sijamuona,” alisema Segito huku akiondoka kwenda
kuendelea na shughuli zake.
“Karudi chumbani?”
“Ndiyo kaka.”
“Oke, mimi najiandaa niende kazini.”
“Sawa kaka.”
Wakati wote huo kumbukumbu ya ile ndoto ilizidi kujirudia akilini
mwangu mfano wa sinema kali ya kusisimua kutoka kwa Mel Gibson.
Akili ikazidi kuchanganyikiwa, kwa mara ya kwanza nikajikuta nikiingiwa
20 mama YANGU NI JINI
na wasiswasi mkubwa.
“Lakini waswahili wanasema ndoto huja baada ya shughuli nyingi,
sasa kwa vyovyote vile ile ni ndoto tu baada ya kuwaza sana,” nilisema
moyoni.
Niliwaza kwa muda mrefu juu ya suala lile huku midomo ikinitetemeka
kwa woga. Nilianza kuhisi mauti mbele yangu.
“Salome.”
“Abee,” aliitika akitetemeka.
“Kifo kinanijia. Hii hali itaniua.”
44 mama YANGU NI JINI
“Si ndiyo maana nilikwambia uende nyumbani.”
“Mimi nadhani hakuna hata haja ya kwenda kwa waganga, niende tu
nyumbani Songea.”
“Itakuwa vizuri Damas.”
“Sasa kule nyumbani nimwache Segito na wewe au?”
“Hapana Damas, tutakwenda wote Songea.”
“Halafu mama tunaenda naye au?”
“Walio pale nyumbani tunawaacha wote. Ilimradi tuwaachie pesa za
matumizi tu.”
Tulijiandaa, tukaenda nyumbani na Salome, nikamwachia maagizo
Segito lakini sikumwambia nakwenda wapi, ila nilimwambia nitakuwa
sipo kwa siku mbili.Nikiwa sebuleni, nilimuuliza kama mama ameamka,
akasema aliamka akaniulizia, kisha karudi tena kulala, nikamwomba
akaniamshie.
Mara, mama alitokea akiwa anatembea kwa kujikongoja.
“Shikamoo mama.”
“Marhaba.”
“Vipi baba, kaamka?”
“Jamani, mbona sijui kama baba yako amekuja?”
“Basi mama. Sasa wewe kapumzike.”
Mama aligeuka na kuondoka, nikamuita Segito. Nilimuaga nikimwachia
pesa za matumizi. Nilimpigia simu bosi mmoja wa ofisini kumwomba
ruhusa ya dharura, lakini sikumwambia naondoka nje ya mji wa Njombe.
Tulipata basi la kwenda Songea, sikumbuki muda gani tuliingia. Pale
tukapanda basi jingine la kwenda kijijini. Tulifika saa kumi na moja
jioni. Wakati tunashuka na Salome, nilihisi ugeni, lakini baadhi ya watu
niliwafahamu, nao walinifahamu wakaja kunipokea.
“Za siku bwana Damas?”
“Nzuri tu,” tulisalimiana. Wa shikamoo niliwaamkia, wa marhaba
waliniamkia.
Nje nyumbani, alikaa mzee mmoja simfahamu, lakini nilipomwakia tu,
nikasikia sauti ya mdogo wangu Henry ikisema:
“Ha! Kaka.”
Alikuja mbio na kunikumbatia. Mimi na Salome tulishtuka sana. Wakati
tunasalimiana na Henry, wale walionipokea walishaondoka wakisema
watakuja kunisalimia vizuri kesho yake.
“Habari za Ulaya kaka?”
45 mama YANGU NI JINI
“Nzuri Henry. Huyu ni nani?” nilimuulizia yule mzee sasa.
“Tunaishi naye hapa kaka, muda mrefu. Alitokea Nyasa.”
“Sawa. Vipi mama, vipi baba?”
Henry aliangusha kilio palepale.
“Vipi Henry?” nilimuuliza kwa hofu kuu…
Henry aliendelea kuangua kilio kiasi cha kushindwa kuongea mpaka
Salome naye akaingilia kati kumbembeleza…
“Shemeji nyamaza, jikaze we ni mwanaume, kaka yako ni mgeni hapa
mpe maelekezo.”
Nilimgeukia yule mzee sasa…
“Eti, kuna nini kinaendelea hapa nyumbani?”
“Mama yako alishafariki dunia…”
“Aaaash,” nilishtuka nikishika kichwa na hapohapo machozi yalianza
kunitoka.
Yule mzee akanishika mkono na kunikalisha kwenye kiti kingine ambacho
ni imara zaidi kuliko kile nilichokalia kwanza.
“Nyamaza mjukuu wangu,”yule mzee alisema.
Nilijikaza nikatulia kidogo maana hata Salome aliniomba ninyamaze.
“Na baba?”
Safari hii alijibu Henry kwa haraka sana.
“Baba naye arobaini yake ilikuwa wiki iliyopita.”
Hapo nilijikuta nimeanguka chini na kupoteza fahamu.
Nilipokuja kurudiwa na fahamu, mwili ulikosa nguvu hata baada ya
kuzinduka, nilijikuta nikihisi kifo nakijua tofauti na zamani. Lakini akili
kichwani zilikuwa zikijichanganya na ile hali niliyoiacha nyumbani
kwangu, Njombe.
“Kwa hiyo Henry, mama alikufa siku zilezile nilivyosafiri?”
“Ndiyo kaka. Kama wiki moja baada ya wewe kuondoka.”
“Na baba naye alikuwa akiumwa nini?”
“Baba yeye alishikwa na tumbo, akalalamika kwa siku mbili akafariki
dunia.”
Mwanaume ni mwanaume, nilijikaza yakaisha yote.
Mimi na Salome tulikwenda makaburini kwa msaada wa Henry na mzee
mmoja mtani wetu. Baadaye tuliporudi nyumbani, nilikaa na Salome tu
na kujadili mambo fulani:
“Ina maana ni kweli wale nyumbani hakuna mama wala Henry, si ndiyo
46 mama YANGU NI JINI
sweet?”
“Hakuna hata baba pale.”
“Sasa tukirudi watatuambia nini?”
“Hatutawakuta.”
“Kweli?”
“Kwa vyovyote vile.”
MWISH0.