Professional Documents
Culture Documents
Nyumba Ya Majini
Nyumba Ya Majini
Nyumba Ya Majini
NILIPAngA NYUMBA
MOJA NA MAJINI
Irene Ndauka
KIMETAYARISHWA NA KUSAMBAZWA NA:
A & S DESIGNING
SIMU: 0713 335560
0788 943433
DAR ES SALAAM
1
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
DHAHABU Imefika
Ni kitabu kizuri kiutakachofanya ujue chimbuko
la makabila ya watu wa tanzania pamoja na
tamaduni zao. kwa kadili muda unavyokwenda
watu tunazidi kuzarau na kusahau asili, mila
na tamaduni zetu hivyo kitabu hiki na kitunzwe
ili kiwe kumbukumbu kwa vizazi vijavyo kwani
bila ya kitabu hiki hawatakuwa wakijua asili na
tamaduni za mababu zao
kwa maulizo piga 0713 335560
3
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
“KAMA
kuna watu hawayajui haya
nitakayoyaongea basi nawataka kuanzia
sasa wajue kwamba, hapa Dar kuna
mambo makubwa sana ambayo ukisimuliwa unaweza kusema
si kweli, lakini wale wanaoyapata wanajua. Ila wewe omba
yasikukute hata siku moja...”
Ndivyo alivyoanza kusimulia Bw. Humuli Samaki (43), mkazi
wa Buguruni (kwa sasa) ambaye alipata mkasa mzito akidai
alipanga nyumba moja na majini Magomeni, Dar es Salaam.
Anaendelea…
5
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
***
Baada ya nusu saa nilitoka benki nikiwa na hela, nikampigia
simu dalali, akasema na yeye alishatoka Dawasco na wakati
huo alikuwa anakunywa soda kwenye mgahawa wa Shibam,
upo palepale Mapipa.
Nilimfuata pale, nikampa fedha, akatoa mkataba, nikajaza
kwani kwa madai yake, yeye ndiye aliyepewa jukumu lote na
mwenye nyumba.
“Kwa hiyo upo huru kwenda kuhamia,” dalali aliniambia
huku akinikabidhi funguo.
“Sawa, nitahamia usiku wa leo.”
Nilirudi nyumbani kwa awali na kupangapanga vitu tayari
kwa usiku kuhamia makazi mapya, Magomeni. Niliwaambia
wapangaji wenzangu wote, nao wakanitakia maisha mema
huku wakisema tukumbukane kwani hata wao walikuwa
kwenye mchakato wa kuhama kwenye nyumba ile.
6
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
MARUWERUWE YANAANZA
Asubuhi niliamka nikiwa nimechoka sana. Wakati nakwenda
bafuni kuoga niligundua ni mimi peke yangu ndiye niliyekuwa
nimetangulia kuamka, kwani bafuni hakukuwa na maji
yaliyomwagika kwa muda huo.
Baada ya kuoga nilirudi chumbani kwangu kujiandaa kwenda
kazini. Wakati najiandaa, nilisikia mlango ukifunguliwa, nikajua
ni wenzangu wanakwenda kuoga au chooni kama ilivyo kawaida
kwa wanadamu wakiamka asubuhi.
Niliamua kutumia nafasi hiyo kuwatambua. Nilivizia pale
niliposikia mlio wa maji bafuni na mimi nikatoka kwenda
kupiga mswaki kwa mara ya pili. Sehemu niliyosimama, mtu
akitoka bafuni kwenda ndani ilikuwa lazima nimuone kwa vile
ilikuwa kiasi cha kugeuka tu.
Lakini cha kushangaza, nilikuwa sisikii maji yakimwagika,
nikageuka na kuuona mlango wa bafuni upo wazi. Mbali na
mlango kuwa wazi, pia chini nikaona alama za kandambili nne
zikiwa zimekanyaga, nikajua wametoka.
“Lakini wamepitaje hapa?” nilijiuliza.
Nilirudi ndani, mlangoni kwao nilikuta kandambili pea mbili
zikiwa bado na majimaji kwa mbali, jambo hili lilinifanya
nijiuliuze sana.
Nilijipa ujasiri na kuamua kuchungulia ndani ya chumba hicho
8
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
9
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
MAAJABU YANAZIDI
Nje nilikuta mfuko wa rambo mweusi, ndani yake ulionekana
kuwa na kitu kwani ulikuwa umetuna sana. Niliinama
kupekenyua ili nijue ndani kulikuwa na nini, nilishangaa kuona
10
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
11
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
lakini sikubahatika.
Nilitoka, nikaenda sebuleni ambako nako nilianza kuangalia
kila kona ya sebule. Nilishangaa kuona glasi ya maji ya kunywa
ambayo niliitumia asubuhi kisha nikaacha maji yamejaa, ikiwa
haina hata tone la maji mbaya zaidi, iliwekwa juu ya kabati
ambapo mimi niliiweka kwenye meza ya katikati ya sebule.
“Mh! Hii kali sasa,” nilijikuta nikisema kwa sauti, mara
nikasikia kicheko tena kutokea upande wa pili kule kwa
wenzangu. Sasa nikaanza kama kuhisi kitu kuhusu watu hao.
Kwanini kila nilipoongea kwa sauti ndipo na wao waliangua
kicheko?
Niliamua kujaribu tena, nikasema kwa sauti:
“Nitakuja kuua mtu, kweli tena.” Nikasikia kicheko tena,
safari hii kilidumu kwa muda.
Moyoni nikasema naanza kufanyia kazi uhusiano wa maneno
yangu na vicheko vya wale majirani.
Nilitoka kurudi chumbani, wakati napita kwenye korido,
nilisimama jirani na mlango wao. Walikuwa wakiongea, lakini
niliposimama mimi, kukawa kimya ghafla kama hakuna watu.
Nilipozama chumbani, nyuma wakaanza kuongea tena.
Sikufunga mlango ili niweze kusikia wanachokiongea, lakini
jamani kwa kusema ule ukweli wa Mungu, sikujua walikuwa
wakitumia lugha gani katika kuwasiliana hata pale nilipojitahidi
kutega masikio kwa umakini wa hali ya juu sana.
Kuna wakati utadhani wanatumia sana neno dotikom, lakini
ukisema usikilize zaidi unasikia wakisema sana kotoko au
kiburate, wakati mwingine sauti ya kike ilisema kaunto, ya
kiume ikarudia hivyohivyo, kaunto.
Nia yangu kubwa ilikuwa kuwaona kwa sura na kufahamu
kama ni ngozi nyeusi au nyeupe. Hilo peke yake lingenipa
mwanga ni watu wa aina gani ninaoishi nao pale ndani ya
nyumba.
Nilisikia mlango wa chumbani kwao ukifunguliwa na mimi
nikatoka haraka sana, cha ajabu sikuona mtu akitoka lakini
mlangoni kulikuwa na kandambili pea moja tu wakati zilikuwa
12
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
14
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
17
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
18
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
19
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
20
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
***
Asubuhi, niliamka nikiwa nimechoka sana, lakini kabla
sijatoka kitandani nilisikia nje ya mlango kukiwa na hali ya
watu kutembeatembea tena kwa kasi, niliinua shingo ili nione
kama nitasikia zaidi, lakini kukawa kimya.
Niliamka, nikatoka, nilikwenda sebuleni kwanza kuangalia
kama kuko salama. Nilishangaa kukuta mezani kuna mfuko
wa rambo uliojaa chipsi kuku kama nilivyonunua mimi, lakini
zangu nilikula, sasa zile sikujua zilitoka wapi.
Niliubeba ule mfuko nikatoka nao,nilifungua mlango mkubwa
wa nje nikautupia pembeni kidogo, niliporudi, nikaenda
chooni. Mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani kwani hata
niliposhika kitasa na kukivuta kilikuwa kigumu.
Hii iliashiria kwamba kuna mtu, kwa hiyo moyoni nilisema
nisimame palepale nje ya mlango hadi atoke. Nilisimama
eneo ambalo akitoka tu, uso kwa uso na mimi.
“Tuone leo, wao si wajanja, leo nimemnasa mmoja wao,”
nilisema moyoni.
Dalili zote zilionesha kwamba mle chooni mlikuwa na mtu
kwani niliweza kusikia hata kuhema kwake, mara mlio wa
maji, mara alikohoa, tena kwenye kukohoa nikabaini mtu
mwenyewe alikuwa ni mwanamke ndiye aliyekuwa mle.
“We kuhoa mpaka utapike, lakini mimi nipo hapa mpaka
utoke,” nilisema moyoni.
21
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
22
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
***
Asubuhi kulikucha salama kabisa, tena usiku wa siku hiyo
sikuona mauzauza wala dalili zake.
Nilikwenda kuoga bila kukagua mazingira, moyoni nilisema
liwalo na liwe kwa maana kwamba, wawepo wasiwepo sawa
tu.
Bafuni niligundua wameshaoga kwani kulikuwa na majimaji
ya muda mfupi uliopita. Nilipomaliza kuoga, nilijiandaa na
kutoka. Nje nilikutana na mtu ana mkokoteni, akanisalimia.
“Za asubuhi bwana mkubwa?”
“Salama, karibu sana.”
“Asante, kuna watu fulani wanaishi humu nina shida nao.”
Aliposema hivyo nilishtuka sana, niliamini yeye ni mmoja
wa wale ila amejigeuza kwa kujifanya ana shughuli za
mkokoteni.
“Unawajua kwa sura?” nilimuuliza huku nikiwa na wasiwasi
maana alinikazia macho.
“Siwajui.”
“Sasa una shida nao kivipi watu usiowajua kwa sura?”
“Ni kwamba, kuna binti mmoja huwa wanamtuma niwaletee
maji, nikifika hapa huyo binti anabeba madumu kupeleka
ndani, sasa jana nilikutana na huyo binti nikamuuliza kuhusu
malipo yangu ya mwezi, akasema nije nifuatilie mwenyewe.”
Nilishangaa sana kusikia hivyo. Nijuavyo mimi mle ndani
mna watu wawili, mwanamke na mwanaume, sasa kama kuna
binti hilo lilikuwa jipya kwangu, labda lakini.
“Huyo binti naye anaishi humu au?” nilimuuliza.
“Sidhani, inaonekana kama huwa wanamtuma tu.”
“Kwa nini huamini kama anaishi humuhumu ndani? Hafanani
23
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
25
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
26
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
28
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
hiyo?
Baada ya dakika mbili, nilimsikia akirejea chumbani kwake
huku akisema:
“Mimi mtu anayevuta bangi siku yoyote na mahali popote pale,
nikimwona nampeleka polisi ajue mimi ni nani. Haiwezekani
watu wawe wanavuta bangi hovyo tu.”
Moyoni nikasema hata iweje, hii bangi leo lazima niichome
humu ndani. Mkienda polisi msipoenda mtajua wenyewe.
“Mimi siwezi kuishi katika mazingira magumu namna
hii wakati pesa ni yangu. Kwa nini ustaarabu usiwepo?”
nilisema moyoni nikipeleka mkono mfukoni ili kutoa ile bangi
niliyonunua mara ya pili.
Niliipata, nikaitoa. Niliiweka kwenye meza kisha nikaendelea
kulala nikiusaka usingizi kwa nguvu zangu zote maana
nilijisikia kuchoka sana. Hapo nilikuwa sijaenda chumbani
kwangu.
Sikumbuki ni muda gani nilipitiwa na usingizi, ila nakumbuka
wakati nalala ilikuwa saa kumi na moja. Nilipokuja kushtuka
ilikuwa saa kumi na mbili na nusu. Ina maana nililala kwa saa
moja na nusu.
Jicho langu moja kwa moja lilitua kwenye bangi pale mezani,
sikuiona.
Nilihamaki kwa kusema ha! Nani amechukua bangi yangu?
Sikujibiwa na mtu, ukimya ulitawala huku akili ikiniambia wale
wapangaji wenzangu watakuwa wanahusika moja kwa moja.
Baada ya muda nilitoka mle sebuleni, nikaenda chumbani.
Nilifungua mlango na kusimama kwanza kabla ya kuzama
ndani. Niliangaza kila kona, nikabaini kitu.
Niligundua kwamba, kuna mtu alikaa kitandani maana
nilipoondoka asubuhi nilikuwa nimekitandika, muda huo kwa
pembeni upande wa mbele kulikuwa na alama za makalio.
Alama hiyo ilinipa picha kuwa, aliyekaa alikuwa na makalio
makubwa! Nilipoangalia chini kwenye kapeti nikabini kitu
kingine kwamba, aliyekaa alikuwa na mafuta kwenye miguu
kwani iliweka alama kuzunguka miguu yake.
30
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
***
Asubuhi niliamka kwa kushtuka, lakini sijui nini kilinishtua ila
ni kama kuna mtu alinivuta mguu mmoja. Hakukuwa na kitu
chochote chumbani mwangu. Nilitoka na kwenda kusimama
kwenye dirisha, nikachungulia nje. Kulikuwa shwari.
Nilipotoka kuoga nikiwa navaa nguo ili kuondoka, nikasikia
wenzangu wakitoka.
Nilisimama tena dirishani kwani kwa mtu anayetoka kwenye
nyumba ile na kwenda popote ilikuwa lazima apite mbele ya
dirisha langu.
Baada ya muda walifungua mlango mkubwa, nikasikia
wakiufunga, lakini baada ya hapo sikumwona mtu yeyote yule
akipita mbele ya dirisha.
Na mimi nilipomaliza kujiandaa, nilitoka, nikafungua mlango
na kutembea zangu. Mbele kidogo nilikutana na watu kama
kumi wamesimama wakiongea.
Niliwasalimia nikawauliza kama kuna usalama.
“Usalama ni mdogo bwana, kuna kijana mmoja amepotea.
Tangu jana usiku alipotoka kwa mkewe akasema anafuatilia
madeni ya biashara zake hajarudi,” alisema mzee mmoja
ambaye alisimama akiwa amejishika mikono kwa nyuma.
“Ni biashara gani anafanya?” niliuliza.
“Huwa anauza maji kwenye mkokoteni.”
“Ha! Ni yule muuza maji?”
“Huyo huyo,” alisema yule mzee.
Akili za haraka nikasema hapa ndipo pa kujua wale wapangaji
ni akina nani, inabidi niseme ukweli ili waende polisi, najua
polisi watakuja kukagua ndani.
“Lakini mbona jana usiku alikuja kwangu kudai pesa yake?”
nilihoji kwa uso wa wasiwasi.
“Ulipomlipa aliondoka?” mwanamke mmoja aliniuliza.
32
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
hasa usiku wa siku hiyo ambapo najua wale watu wakija ndiyo
balaa litakuwa kubwa zaidi.
“Halafu usiku wa leo lazima watakuja kunifanyia maajabu
yao, lakini dawa yao nisilale. Oke, kumbe bangi itapulizwa leo,
kidogo itakuwa nafuu,” nilisema moyoni, nikashtuliwa na sauti
ya kike nyuma yangu iliyoita jina langu.
Nilipogeuka nyuma, nikamwona dada mmoja aitwaye
Mwantumu Seleman niliwahi kuishi naye Mwananyamala.
Akaniuliza habari za siku.
Niliamua kumsimulia janga langu, lakini ghafla likaja gari,
akaingia huku akiniambia atanitafuta siku nyingine.
Baadaye nilirudi kazini huku nikiwa na hali ya wasiwasi, hata
kazi zangu zikuzifanya sawasawa kama ilivyo kawaida yangu.
Iliniuma sana!
Muda wa kazi ulipokwisha, niliondoka moja kwa moja
hadi nyumbani. Sikutaka kupitia mahali siku hiyo, lakini
nilishakubaliana na yule mfanyakazi mwenzangu aliyesema
atakuja na bangi yake.
Wakati nafungua mlango mkubwa nilibaini wenzangu
walisharudi maana mlango haukufungwa na funguo, nikaingia
ndani. Nilipofika kwenye mlango wangu wa kuingilia sebuleni,
wakati naufungua nikasikia mlango wa chooni unafunguliwa,
yaani ilimaanisha kwamba kuna mtu anatoka.
Ukisimama mlangoni mwangu, mtu akitoka chooni unamuona
bila kificho, hususan kama anakuja vyumbani. Lakini pia
hata akiwa anatoka kwenda uani, utamuona kwa mgongoni.
Nilisita kuingia nikiamini nitamwona mtu huyo. Nilianza kuona
miguu ikitoka, moyo wangu ukashtuka, mara nikamwona mtu
mwenyewe.
Nilijikuta nikisisimka mwili, niliamini naona kivuli chake na si
yeye. Ni mtu mweusi, wakati nilitarajia angekuwa mweupe.
Alivyozidi kunisogelea, nikabaini kuwa, ni yule kijana muuza
maji kwenye mkokoteni.
“Ha! Wewe vipi, unatafutwa sana unajua?” nilimwambia.
Badala ya kunijibu, alikata kona kuufuata mlango mkubwa.
36
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
37
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
38
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
39
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
“Ndiyo langu.”
Niliangalia mazingira mengine ya mle ndani na kubaini
kwamba, kuna vitu vingi sana vilikuwa ndivyo sivyo.
“Si umeona hayupo?” yule mzee aliniuliza, nikamjibu ndiyo,
akasema twende tukachukue simu yetu kwenye kile chumba
ambacho ilikuwa inaita.
Moyo wangu ulikuwa mzito sana, nilihisi kizunguzungu,
nilitamani kukaa chini na kumwona yule mzee asichukue
uamuzi wa kuifuata ile simu, lakini ningeipataje simu yangu
wakati ina namba kibao?
“Kijana, ngoja nikuoneshe dawa moja ya hao viumbe
wasiotaka kuonekana,” alisema yule mzee, nikamuuliza ni ipi
hiyo?
“Tulia wewe,” alisema huku akiingiza mkono mfukoni na
kutoa kimfuko kidogo, akakifungua akatoa kitu. Nilipomuuliza
ni nini akajibu:
“Ni bangi.”
“Sawa kabisa, hiyo ndiyo dawa, ngoja nikupe kiberiti.”
Katika mambo yalinishangaza ni hilo, tulitafuta kiberiti
chumbani hadi sebuleni lakini hakikuonekana, mbaya zaidi
mimi nilikuwa na kawaida ya kununua viberiti bunda zima,
lakini pia sikuona popote.
“Kweli una kiberiti ndani?” yule mzee aliniuliza.
“Kiberiti kipo na uzuri ni kwamba, nina bunda zima, lakini
pia nashangaa silioni.”
Nilimwona yule mzee akisimama wima na kunyoosha mikono
juu kama mtu anayeomba dua kwa Mungu.
“Kijana nimejua sasa, ngoja kidogo,” alisema huku akitoka na
mimi nikimfuata kwa nyuma.
Wakati tunapita kwenye korido jirani na vyumba vile vya
wenzangu, nikaisikia simu yangu ikiita.
“Mzee mzee, hiyo bwana,” nilisema, mzee akasimama na
mimi nikasimama nyuma yake, tukasikia sauti ya mwanaume
ikipokea simu yangu:
40
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
42
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
43
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
44
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
46
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
47
NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
MWISHO.
48