Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 28

VICTORIA WILLIUM, mkazi wa

TUNSUME MLAWA, alikuwa na


KIGOMA, alikuwa na tatizo la
tatizo la UTASA kwa miaka 7,
UTASA kwa miaka 17, Baadaya
baada ya kuombewa mara kwa
kuombewa na Mtu wa Mungu
mara na Mtu wa Mungu Nabii
Nabii BG MALISA, kwa maombi ya
BG MALISA sasa ana mtoto wa
mwendelezo, (zaidi ya mara moja)
kike anaitwa DEBORAH
sasa ana mtoto wa kiume anaitwa
DANIEL

Aliyekuwa kilema
Aliyekuwa kilema, alipokea muujiza na kuanza alitembea, huko jijini
kutembea wakati wa mkutano ARUSHA (2013) MBEYA
© Haki ya nakala 2013
Nabii B.G. MALISA
Kanisa la Ukombozi Ministries For All Nations.
(UMINA)
P.O. Box 1961 Mwanza, Tanzania.

E- mail: ukombozichurch@yahoo.com

Toleo la 1:- February 2013


Toleo la 2:- November 2013
Toleo la 3:- August 2015
Toleo la 4:- February 2017
Toleo la 5:- MARCH 2018
Toleo la 6:- June 2023

Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kupiga chapa, au


kutoa nakala ya kitabu hiki kwa namna yoyote ile bila idhini
ya kanisa la Ukombozi Ministries For All Nations.

Published by:
Ukombozi Quality Media Publications
P.O.Box 1961 Mwanza, Tanzania
E- mail: ukombozichurch@yahoo.com

Printed by:
UMINA PRINTING PRESS
P.O.BOX 1961
MWANZA- TANZANIA

ISBN: 978–9987–9437– 4 – 6

ii
Yaliyomo:-

Neno la faraja ………………………………………………………………………. iv

Shukurani ……………………………………………………………………………….. v

Utangulizi ………………………………………………………………………………. vi

Sura ya 1
Madhara ya kutokurudi tena …………………………………… …….. 1

Sura ya 2
Hata wakati wa Yesu Kristo kuna baadhi ya watu hawakurudi tena
…………………………………………………………………………………………………… 3
- Kuombewa mara moja haitoshi …………………………… 3
- Kuna roho ambazo huwazuia watu kurudi tena …….. 4

Sura ya 3
Mbinu anazozitumia shetani kuwazuia watu kurudi tena kwenye
kanisa lenye nguvu …………………………………………………………………. 5
- Hofu ya kuhama kanisa…………………………………………… 13

Sura ya 4
Siri ya siku ya Jumapili …………………………………………………………. 14

Mambo ya kuzingatia ili tuukulie wokovu………………………….. 18

iii
Neno la faraja.

Napenda kuwatia moyo wale wote wanaopitia


mambo magumu kwenye maisha yao. Wengine
wamefiwa na waume wao wapenzi, ambao
walikuwa ni msaada mkubwa kwenye maisha yao.
Wengine wamefukuzwa kazi na wengine
wamepoteza biashara zao. Wengine baada ya
kukata shauri kuokoka waume zao wamekua
wakiwatesa sana
Yote haya na mengine mengi yanayowapata kila
siku katika maisha ya wokovu, MSIVUNJIKE
MOYO.
Mkumbukeni Ayubu; japo kuwa alikuwa mwana wa
Mungu, lakini alipatwa na mabaya mengi sana.
Alivumilia mpaka mwisho, na mwisho wake
ulikuwa mzuri zaidi kuliko mwanzo wake. Biblia
inasema;
“…BWANA naye akampa Ayubu mara
mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza.”
AYUBU 42:10

Unapoona unapitia majaribu makubwa, basi ujue


pia kuna Baraka kubwa ambazo Mungu
amezikusudia kwenye maisha yako, endelea kama
alivyofanya Ayubu.

iv
Shukurani

Namshukuru Roho Mtakatifu kwa kunipa ufunuo


wa kuandika kitabu hiki kitakachowaimarisha
wengi kiroho.
Pia ninamshukuru Mungu kwa kunibariki na kunipa
neema ya familia nzuri ya watoto watatu JOSHUA
pamoja na wadogo zake mapacha JOEL na SARAH.Kwa
upendo mkubwa napenda kumshukuru mke wangu
mpendwa SUZAN,anayenitia moyo kwenye vita vikali
ninavyopigana navyo kila siku kwenye huduma yangu.

Pia namshukuru Mungu kwa kunipa viongozi mashujaa


ambao hawajawahi kuniacha tangu mwanzo wa huduma
yetu, wamekuwa nguzo imara sana zisizo tetereka,
Mungu atawashibisha kwa mema yote.
Shukurani zangu ziende kwa wana Ukombozi wote
wanaodumu katika kuniombea usiku na mchana,
ninaamini maombi yao ndiyo yaliyoniweka hapa nilipo
leo.
Pia shukurani zangu ziende kwa wale wanaojitoa kwa
fedha zao kwa ajili ya kufanikisha kurusha kipindi chetu
cha “SAA YA UKOMBOZI”, kwenye “Television” kila
wiki. Mungu atawabariki kwa kipimo kilichojaa na
kushindiliwa kwani yeye siyo mwanadamu ni Mungu
wa haki.(LUKA 6:38)
Mungu wa Mbinguni awajalie neema na maarifa zaidi
mkaishi maisha ya utele.
KUMBUKUMBU LA TORATI 1:11
“BWANA, Mungu wa baba zenu, na awafanye kuwa
wengi mara elfu kuliko mlivyo, na kuwabarikia, kama
alivyowaahidi,”
v
Utangulizi.
Watu wengi wanaombewa mara moja tu na
hawarudi tena wanaanza kulalamika mbona mimi
sijapona? Kumbe walikata tamaa mapema.

Mbinu kubwa anayoitumia SHETANI siku hizi za


leo ni mbinu hii ya kuwakatisha TAMAA watu ili
wasiendelee kumtafuta Mungu.

Hata ukienda hospitalini kama wewe ni


mgonjwa, ni lazima umalize “dozi” yote ya dawa
ndipo utakapopona,ukishindwa kumaliza “dozi’
hiyo, kama hautapona tatizo siyo la daktari bali
ni la kwako mwenyewe.

Ndivyo ilivyo kwenye mambo ya KIROHO.


Unapoanza kuombewa, endelea mpaka kieleweke
usiishie njiani kwani kuishia njiani kuna madhara
makubwa. Kuombewa na kuishia njiani ni afadhali
usiombewe kabisa.

Ni sawa na kumpiga simba “risasi‟ moja au


“mshale” mmoja, hapo unamuongezea nguvu na
hasira za kuleta madhara makubwa zaidi. Ukitaka
kumuua simba mpige mpaka mwisho.

Ndivyo ilivyo kwenye maombezi, endelea kuombewa


hadi mwisho utakapopokea muujiza wako.
Kwa kusoma kitabu hiki, utajifunza mbinu nyingi
za shetani anazozitumia kuwarudisha watu nyuma
ili wasiendelee na wokovu na maombezi.

vi
Sura ya 1
Madhara ya kutokurudi tena

Kazi kubwa ya shetani ni kuwazuia watu


kurudi tena kanisani. Watu wengi wanakuja
kuombewa mara moja tu na hawarudi tena.
Wengi wanakuja kanisani kuokoka tena kwa
machozi, lakini utashangaa hawarudi tena!

Utafiti unaonesha kwamba kati ya watu 100


wanao kata shauri kuokoka ni watu 7 pekee
ndiyo wanao endelea na wokovu mpaka
mwisho. Kwa nini inakuwa hivi? Ni kwa
sababu hii ni kazi ya shetani.

USHUHUDA
Namkumbuka mama mmoja aliyekuwa TASA
kwa miaka 22, alipokuja kuombewa mama yule
kumbe alikuwana majini mahaba yaliyo mfunga
asiweze kuzaa kwamiaka yote hiyo “22”. Baada
ya maombezi Mama huyu alifunguliwa na
akabeba mimba, cha ajabu hakurudi tena
kanisani. Kwa bahati nzuri, siku moja
nilikutana naye mjini, nikamuuliza, “mbona
hukurudi tena kanisani”?
1
Akanijibu, mambo yalikuwa mengi. Akasema,
kweli uliponiombea tu, nilifunguliwa na nika
beba mimba ilipofikisha miezi saba (7), mimba
ilitunga nje ya mfuko wa uzazi. Madaktari
wakaitoa.

Huyu mama alifikiria kwamba kuombewa


mara moja ilikuwa ni tayari, kumbe yale
majini yalikuwa yanamfuatilia.

- Unapo-ombewa na mtumishi wa
Mungu mwenye nguvu kubwa ya
Mungu halafu ukatoka ukaenda kwa
mtumishi mwenye nguvu ndogo lazima
matatizo yako yatarudi tena. Lazima
ufahamu kuwa watumishi wa Mungu
wanatofautiana kwa viwango vya
upako

- Unapotoka kwenye kanisa lenye


nguvu kubwa ya Mungu na kurudi
kanisa lenye nguvu kidogo ni lazima
mapepo yaliyotoka yatakurudia tena.

Usitoke kwenye kanisa lenye nguvu

2
Sura ya 2
Hata wakati wa Yesu Kristo kuna baadhi
ya watu hawakurudi tena.

Yesu Kristo aliwaponya watu 10 wenye ukoma, lakini


aliyerudi kumshukuru alikuwani mmoja tu. Yesu Kristo
alisikitishwa sana na kitendo hiki. LUKA 17:11-19
“… Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi,
huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu; akaanguka
kifudifudi miguuni pake , akamshukuru, naye alikuwa
Msamaria. Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa
wote kumi? Wale kenda wa wapi? Je! Hawakuonekana
waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?
Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako
imekuokoa.”

Yesu aliuliza; “ wale kenda wako wapi? Yaani wengine


tisa wako wapi? Hii inathibitisha wazi kwamba,
unapoombewa na kupokea muujiza ni lazima urudi pale
ulipopokelea muujiza wako uweze kumpa Mungu utukufu!
Ndivyo ilivyo hata mimi mtumishi wa Mungu huwa nasikitika
sana pale ninapotumia muda wa kumuombea mtu na
akapokea muujiza lakini harudi tena.

Kuombewa mara moja haitoshi!!


Watu wengi wanajidanganya kwamba ukiombewa mara moja
inatosha, kumbe sivyo. Kuna watu ambao vyanzo vya
matatizo yao ni vizito sana.
- Mtu mwenye majini “200” ni tofauti na mtu mwenye
majini “3”. Mtu mwenye majini mengi anatakiwa
atumie nguvu kubwa sana ili afunguliwe, hivyo
akiombewa siku moja haitamsaidia kabisa.
3
- Kumbuka Jemadari Naamani aliyekuwa na ukoma
alipona pale alipojichovya MARA 7 kwenye mto
Jordani kwa agizo la NABII ELISHA, ingawa kwanza
alikasirika mwisho alikubali na akapona ukoma wake.
SOMA 2 WAFALME 5:1 -15

- Hata Yesu Kristo, kuna mtu aliyekuwa KIPOFU


alimuombea mara mbili (2). Mara ya kwanza
hakufunguliwa. Yesu alirudia tena.
Soma MARKO 8;22 - 25
“... Ndipo akaweka TENA mikono yake juu ya macho yake,
naye akatamaza sana; akawa mzima, akaona vyote wazi
wazi.”

Ndivyo ilivyo hata leo, wengi wakiombewa mara moja tu


wanakata tamaa eti hawajapona. Huo ni uongo wa
shetani. Endelea kuja mpaka kieleweke!

Siri kubwa!
Matatizo yanafanana na miti. Mti wenye umri wa miaka 50,
siyo sawa na mti wenye umri wa miezi 2. Ni rahisi sana
kuung‟oa mti wenye umri wa miezi miwili au mwezi mmoja
lakini isiwe rahisi kuung‟oa mti wenye umri wa miaka 50.
Ndivyo ilivyo kwenye matatizo sugu.

Kuna roho huwazuia watu kurudi tena.


Kuna “MAPEPO” huwazuia watu kurudi tena, hiyo inatokea
hata wakati wa Yesu Kristo, kwani shetani hajaanza upinzani
wake siku za leo, bali alianza wakati wa siku za Yesu Kristo.

Soma LUKA 17:-11 - 19


Yule mmoja alipoona amepona ALIRUDI kwa Yesu Kristo na
Yesu Kristo alimuongezea UPAKO mwingine.
Shetani anafahamu utakapozidi kuhudhuria kwenye KANISA
lenye NGUVU KUBWA za Mungu utazidi kufunguliwa kwa
VIWANGO vya JUU, ndiyo maana lazima akuletee upinzani.
4
Kumbuka shetani ni roho, wala hauwezi kumuona kwa
macho ya kawaida ila unapoona kuna mambo
“yanaibuka” ili kukuzuia kuja kanisani mahali ambapo
uliponywa na kufunguliwa ujue huyo ndiyo shetani.

USHUHUDA
Mwaka 2008 nilifanya kongamano la uponyaji ndani
ya ukumbi wa shinyanga “guest” jijini Mwanza.
Mama mmoja alikuja akiwa analia machozi kwa
sababu alikuwa TASA kwa miaka zaidi ya 11. Kweli
mama huyu nilimuombea na baada ya miezimichache
alifunguliwa na kupokea muujiza akawa mja mzito
yaani akabeba mimba. Mama huyo nilimpa agizo
kwamba anapaswa kuendelea kuombewa sana na
kufundishwa kwani alikuwa amefungwa sana na
nguvu za giza, lakini yeye alipuuza na HAKURUDI
TENA!!

Baadaye mimba yake ILIHARIBIKA kwa sababu ya


kukosa mwendelezo wa maombezi na mafundisho.
Aliamua kurudi tena, kweli yule mama nilimuombea
tena akafunguliwa kutoka kwenye roho ya utasa na leo
hii ana mtoto wa kiume. Kama asingerudi tena,
angekuwa bado amefungwa na roho ya utasa
nakuendelea kuteseka.
Ukiwa na roho ya kukata tamaa hauwezi
kupokea muujiza

5
Sura ya 3
Mbinu anazozitumia shetani kuwazuia watu
kurudi tena kwenye kanisa lenye nguvu.

1. Mbinu kubwa na ya kwanza anayoitumia shetani


KUWAKATISHA TAMAA wageni kurudi tena kanisani
ni mbinu ya MANENO YA UONGO.
Watu wengi wameacha kabisa kuendelea kuja kanisani
kwa sababu ya kusikiliza maneno ya uongo na kuyaamini
ujue kanisa letu ndilo linaloongoza kusemwa VIBAYA.
Watu wengi huwa wanayaamini maneno pasipo
kuchukua muda wa kufanya UCHUNGUZI wa kutosha.

Watu wengi wanaolisema vibaya kanisaletu la


Ukombozi ukweli wote hawajawahi hata kuhudhuria
kwenye ibada zetu.Ukweli ni kwamba hata Yesu Kristo
mwanzilishi wa wokovu wetu yeye pia alisemwa vibaya
sana na wengine “WALIMWAMBIA ANA MAPEPO”. Soma
vizuri kwenye kitabu cha YOHANA 8:48
“Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Je!sisi hatusemi
vema ya kwamba wewe u Msamaria, nawe una pepo”?

Hata kanisa la Mitume walilisema vibaya kilamahali.


Soma MATENDO YA MITUME 28:22
“… kwa maana katika habari za madhehebu hiyo imejulikana kwetu
kwamba inanenwa vibaya kila mahali.”

Vita hii ya maneno inatoka kwa shetani mwenyewe,


kwani shetani hayapendi makanisa yenye nguvu za
Mungu.

6
2. Mbinu nyingine anayoitumia shetani kuwafanya
watu wasirudi tena ni hii; SHETANI HUWAFANYA
WATU WAONE KWAMBA KANISA LIKO MBALI
SANA. Hii ni mbinu kubwa sana anayoitumia shetani
kuwafanya watu wasirudi tena. Watu wanatafuta pesa
kutoka mbali. Kuna watu wanaishi MUSOMA na kila siku
wanakwenda MWANZA kufanya biashara, na wala
hawalalamiki kwamba Mwanza ni mbali! Kwenye masuala
ya PESA watu huwa hawaangalii umbali.

Kuna watu ambao mimi nawafahamu wanaishi mkoa wa


Kilimanjaro na kilasiku wanakwenda mkoa wa Arusha
kufanya kazi kila siku lazima waende Arusha na wala
hawaangalii umbali
Badala ya kumtafuta Mungu kwanza ambaye ndiye
chanzo cha MAFANIKIO yetu, tunasemani mbali. Biblia
inasema, Malkia wa kushi (ETHIOPIA) alitoka Ethiopia
mpaka Israeli kutafuta hekima ya Suleimani, na wala
hakuangalia UMBALI .Soma MATHAYO 12:42

Ukimpa Mungu nafasi ya kwanza na yeye


lazima atakupa nafasi ya kwanza

3. ROHO YA KUKATA TAMAA


Hii ni MBINU kubwa anayoitumia sana shetani
kuwafanya watu wasirudi tena kanisani. Watu wengi
wamekamatwa nahii roho ya kukata tamaa.
Wanapokuja kuombewa kwa mara ya kwanza,
wanakuja wakiwa na “moto” wakiwa na shauku
kubwa lakini wanapoona hawaja pokea muujiza
wanaanza kukata tamaa na baadaye hawarudi
tena kanisani. Wengi wanasema tulikuja kanisa la
Ukombozi lakini hatujaona lolote, kama ni ugonjwa
bado sijapona! Huo ni uongo wa shetani

7
USHUHUDA
Baba mmoja aliyekuwa ameathirika kwa UKIMWI, baba
huyu hakukata tamaa. Hakuacha kuhudhuria kwenye
ibada na kwenye maombezi kila alipoambiwa aende
kupima damu yake, alikuta damu ina virusi vya ukimwi.
Yule baba hakukata tamaa bali aliendelea kuhudhuria
kanisani na kuhudhuria maombezi. Siku moja baba huyo
alienda kupima tena ikiwa ni mara ya kumi (10) Bado
majibu yalikuwa mabaya lakini alipokwenda mara ya 11
alishangazwa na majibu kwani alikuta damu yake ni
“NEGATIVE” yaani alipona.
Kama angekata tamaa mara ya kwanza au mara ya pili au
mara ya tano au mara ya kumi asingepona. Hili ndilo
tatizo la watu wengi kushindwa kupokea miujiza yao kwa
sababu ya kukata tamaa mara ya kwanza tu!

Mungu alipomuahidi Baba yetu Ibrahimu kwamba


angempa mtoto, ilipita miaka 25 lakini Ibrahimu
hakukata tamaa, hatimaye ahadi ya Mungu ilitimia
kwake.SOMA WARUMI 4:20 – 21
“Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwakutokuamini, bali
alitiwa nguvukwa imani, akimtukuza Mungu; huku akijua hakika ya
kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.”

4. VIONGOZI WA DINI
Viongozi wa dini ndiyo walio msumbua sana Yesu Kristo
alipokuwa duniani. Hao ndiyo waliomuua Yesu, ndiyo
walio lisumbua kanisa la Mitume kule Yerusalemu.
Ulipokuwa unasali kwenye dini zao, walishindwa
kukusaidia ndiyo maana ulikuwa umefungwa na
majini, mizimu,umaskini, magonjwa na laana za kila
aina, sasaiweje leo umefunguliwa kwenye kanisa la
Ukombozi halafu wakwambie umepotea?
Soma LUKA 22:1 - 2
8
Ibilisi anaweza kuwatumia viongozi wa dini kule
ulikokuwa unasali wanaanza kukufuatilia kwa vitisho na
kukukatisha tamaa ili uache wokovu/ usiende kwenye
kanisa lenye nguvu. Wanaweza kukuambia, „yaani wewe
umeacha dini yako nzuri; dini ya baba zako,
umepotea; hilo kanisa uliloenda ni la mashetani,
wachawi, n.k
Viongozi hawa hutumia kila mbinu ili kukufanya uiache
imani ya wokovu wanatumia mafundisho ya uongo
wakiwa ni mfano wa watu wanaokusaidia kumbe lengo ni
kukuangamiza.

5. NDUGU ZA UONGO.
Hii ni mbinu nyingine kubwa sana anayoitumia shetani ili
kuwarudisha watu wengi kwenye dhambi. Wengi
wamekatishwa tamaa na hawa wanaoitwa ndugu za
uongo.

NDUGU ZA UONGO NI WATU GANI?


Hawa ni watu waliotangulia kuujua wokovu kwa miaka
mingi lakini maisha yao siyo kielelezo, hawana mfano
wowote wa kuigwa. Maisha yao ni maovu pamoja na
kuwa wengine ni viongozi wa kanisa. Watu hawa
walimsumbua sana Mtume Paulo. Angalia maandiko:-
“... hatari kwa ndugu za uongo.” 2WAKORINTHO 11:26
Biblia inasema; “ndugu za uongo” inamaanisha watu
wanaojiita wameokoka na huku hawana kielelezo. Yesu
Kristo aliwaita mbwa- mwitu waliovaa ngozi ya
KONDOO.MATHAYO 7:15
Biblia inatuonya sana kwamba tunapokata shauri na
kuokoka tusiwaangalie wanadamu tumuangalie mmoja
tu YESU KRISTO, aliyeishi maisha makamilifu yeye
hakuwahi kutenda dhambi yoyote alipokuwa akiishi
hapa duniani.
Huyu ndiye wakumwangalia.“Umwangalie sana mtu
mkamilifu....” ZABURI 37:37
9
Usijenge msingi wako wa wokovu kwa kuwaangalia
wanadamu, kwani KILA mwanadamu ana mapungufu
yake. Wengine wamekatishwa tamaa na VIONGOZI
WA KANISA, wanapoacha wokovu wanasema; “kama
huyu aliyekuwa kiongozi wangu amefanya dhambi
ya uzinzi, mimi je nitaweza kushinda? Afadhali
niache wokovu”
Hapana! Usithubutu kuacha wokovu eti kwa sababu
kiongozi wa kanisa ameshindwa kuendelea na wokovu.
Mtu wa kumwangalia ni YESU KRISTO PEKE YAKE.
Yeye ndiye mwanzilishi wa wokovu wetu.Unapokata
shauri na kuokoka, msikilize Mtumishi wa Mungu
uliyepewa, yaani ndiye baba yako wa KIROHO. Usiwe
na walimu wengi watakupoteza. Kuna msemo usemao:-

Kichwa kimoja hakinyolewi na vinyozi wawili.


Pia hakuna gari linaloendeshwa na
MADEREVA WAWILI kwa wakati mmoja

“Kwa kuwa ijapokuwa mna walimu kumi elfu katika Kristo, walakini
hamna baba wengi. Maana mimi ndimi niliyewazaa katika Kristo Yesu
kwa njia ya Injili.” 1WAKORINTHO 4:15

Uwe makini pale unapookoka usikubali kuchanganya


mafundisho. Siyo mafundisho yote ni mabaya, lakini
mafundisho mengine ni mabaya. Mtume Petro aliyaita
mafundisho (neno) yaliyoghoshiwa. 1PETRO 2:2. Neno
„GHOSHIWA” maana yake “ILIYO CHANGANYWA”

Ili uweze kukua kiroho, ni muhimu sana upate mafundisho


yasiyo-changanywa. Kumbuka, maziwa ni NENO LA MUNGU.
Na kama ilivyo kwa mtoto, ili akue vizuri anahitaji chakula
kizuri chenye vitamini zote. Ndivyo ilivyo kwako; ni muhimu
sana wewe uliyeokoka usichanganye mafundisho ili usije
UKACHANGANYIKIWA KI-IMANI.

10
6. SAUTI ZA SHETANI
IWAKORINTHO 14:10; “Yamkini ziko sauti za namna nyingi
duniani, wala hakuna moja isiyo na maana.”
Shetani anaweza kutumia sauti za ki-geni ili akurudishe
nyuma na uache wokovu. Shetani hutumia sauti
zisizosikika katika masikio ya kawaida.
“Yamkini ziko sauti za namna nyingi duniani, wala
hakuna moja isiyo na maana” 1WAKORINTHO 14:10
Shetani ni roho isiyo-onekana kwa macho ya kawaida,
kwa hiyo ili akudanganye atatumia sauti kwenye
ulimwengu wa roho.
Wakati wa Yesu
Shetani alikwenda kumjaribu Yesu Kristo, pale
alipomwambia,
“Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe
Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya
yawe mikate.” MATHAYO 4:3

Hii ilikuwa ni SAUTI lakini shetani aliyetamka


hakuonekana kwa macho ya damu na nyama. Yesu
Kristo alikuwa na uwezo wa kupambanua tofauti ya
sauti ya Mungu na sauti ya shetani.Wengi
wameshindwa kupambanua kati ya sauti ya Mungu
nasauti ya shetani na hivyo kupata madhara makubwa.
Unaweza kushangaa kwamba baada ya wewe kuokoka
mawazo ya ajabu- ajabu yanaanza kuumbika ndani
yako.Mfano:-
- Utasikia mara kitu kinakwambia; “Leo usiende
kwenye ibada, umechoka sana”
- Utasikia kitu kinakwambia; “kanisa lile liko
mbali tafuta kanisa lililo karibu na wewe”
- Utaanza kushangaa unaanza hata “kumzoea
mtumishi wa Mungu na kumuona mtu wa
kawaida”
11
Hebu nikuulize swali:-
Kwani MTU anapoamua KUJINYONGA huwa
anaanzaje?Huwa inaanza sauti kwenye nafsi yake na
kumshawishi achukue uamuzi wa KUJIUA.”
Ndivyo ilivyo katika wokovu. Wengi wameacha wokovu kwa
sababu ya kusikiliza sauti za shetani.

7. Pia shetani anaweza kutumia ndoto, ili tu


awarudishe nyuma watu waache wokovu.
Unaweza kushangaa ya kuwa unaota ndoto za ajabu (ndoto
mbaya). Pengine unaweza kuona sura ya mtumishi wa
Mungu kwenye mazingira ya ajabu, usiwe mwepesi kuamini
kilandoto; nyingine ni za shetani.

Ushuhuda
Dada mmoja aliamini kwamba mtumishi mmoja wa Mungu
siyo mtumishi wa kweli wa Mungu bali anatumia nguvu za
giza eti kwa sababu alimuota usiku yupo kifua wazi.
Nilijaribu kumsaidia kwamba, asijenge msingi wake kwenye
NDOTO na MAONO na hatimaye aliweza kufunguka

Lakini ilikuwa ni hatari kwa yule dada ingekuwa rahisi


sana kwayeye kurudi nyuma na kuacha wokovu kwa
sababu ya ndoto ya ki-shetani aliyo-ota. Hii ni mbinu
kubwa anayoitumia shetani ili kuwatega watu wengi
walio-okoka kupitia NDOTO na MAONO.
“Wanaodhani ya kuwa watawasahaulisha watu wangu
jina langu kwa ndoto zao, wanazomhadithia kila mtu
jirani yake …” YEREMIA 23:27

Ni kweli Mungu anatumia ndoto ili aseme na watu, lakini pia


shetani anatumia ndoto kuwapotosha watu. Kumbuka kila
ndoto lazima ipimwe na NENO LA MUNGU.
- Ndoto unayoota unaoneshwa kwenda kuchimba mizizi
ya madawa porini, hiyo ni ya shetani.
- Ndoto inayokutoa kwenye kanisa ulilopokelea wokovu
uende kuabudu kwenye dini zinazokataa wokovu, ni
ndoto ya shetani.
12
Sauti ya shetani iko kinyume na mapenzi ya Mungu.
Ndiyo maana neno la Mungu linatuambia kuangusha
ngome za mawazo.
“tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya
elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo.
2WAKORINTHO 10:5

8. Anaweza kumtumia mtu wako wa karibu sana


kufanyika kizuizi katika wokovu wako. Mfano
anaweza kutumia wazazi, marafiki, ndugu, mkuu wa
kazi (mwajili wako), n.k. Ukiokoka, usije ukakubali
kuacha wokovu kwa sababu yoyote. Kumbuka neno
la Mungu linasema;“Maana kila mtu atalichukua
furushi lake mwenyewe.” WAGALATIA 6:5
Na siku za mwisho hakuna kujitetea eti fulani alinizuia
nisiokoke au nisiendelee na wokovu.
Unapookoka tayari vita inaanza ndiyo maana Yesu
mwenyewe akasema katika kitabu cha MATHAYO 10:34- 39

“... Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani


duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga. Kwa
maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti
na mamaye, na mkwe na mkwe mtu; na adui za
mtu ni wale wa nyumbani mwake. Apendaye baba
au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye
mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Wala mtu
asiyechukua msalaba wake akanifuata hanistahili.
Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye
mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu
ataiona.”
Yesu Kristo ana maanisha kuwa mtu yeyote mwenye
kupenda chochote kuliko kumpenda yeye (Yesu) huyo
hastahili kabisa mbele zake na ataangamia. Kwa hiyo
usikubaliane na maneno ya mtu ye yote anaye
kushawishi kuacha wokovu.

13
Lazima ukubali kupandwa kwenye kanisa moja!
Hakuna mti unaoweza kuzaa matunda kama haujapandwa,
kwenye udongo na mizizi yake kwenda chini ya udongo. Mimi
sijawahi kuona mti upo hewani na umezaa matunda, hii
haiwezekani!!
Ndivyo ilivyo, kuna kupandwa ki- roho. Biblia imefundisha siri
hii.Soma ZABURI 92:13
“Waliopandwa katika nyumba ya BWANA Watastawi
katika nyua za Mungu wetu.”
Watu wengi wanakwenda kwenye makanisa kwa ajili ya
kuombewa tu, hawataki kupandwa kwenye hayo makanisa.
Wengi wanakuja kwenye kanisa letu la Ukombozi kwa ajili ya
kuombewa tu na wala hawako tayari kupandwa kwenye kanisa
letu ndiyo maana hawapokei muujiza wowote. Kama umetoka
kwenye dini yako na ukaja kanisani kwetu ili kuombewa, hii
inamaanisha huko uliko toka kwenye dini yako hakukuwa
na MSAADA; sasa kwa nini usikubali kupandwa kwenye
kanisa letu?

HOFU YA KUHAMA KANISA

Wengi wametishwa sana baada ya kuhama DINI zao na


wakazidiwa na vitisho na mateso wakaamua kurudi tena
kwenye dini zao za zamani.Biblia imewaruhusu watu kutanga-
tanga na kutafuta chakula cha kiroho.Soma
“Watatanga-tanga hao wakitafuta chakula; Wasiposhiba watakesha usiku
kucha.” ZABURI 59:15
Usitishwe na viongozi wa dini wanaosema una roho ya
kutangatanga. Biblia ndiyo imeturuhusu kutanga-tanga ili
kutafuta chakula cha ki-roho.Hata katiba ya Jamhuri ya
muungano wa Tanzania imetoa uhuru wa kuchagua dini yoyote
na kujiunga. Hii ndiyo inayoitwa UHURU WA
KUABUDU.Usikubali mme wako akuzuie kuja kanisani. Mume
anaye kupenda atampenda na Mungu wako.Kumbuka huyo
mume amekuoa mwili tu na wala siyo roho. Huyo mume wako
au mzazi wako hajui kabisa roho yako iko wapi.
Soma WAGALATIA 6:5
“Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe
14
Sura ya 4

Siri ya siku ya Jumapili

Jumapili ina siri kubwa sana.


- Siku ya jumapili ndiyo siku aliyo fufuka Yesu
Kristo.
- Siku ya Jumapili ndiyo siku aliyo shuka Roho
Mtakatifu
- Siku ya Jumapili ndiyo siku ambayo mtume
Yohana alipopewa ufunuo mkubwa sana
alipokuwa kwenye KISIWA CHAPATMO
- Biblia inatuamuru lazima tukusanyike pamoja.
soma WAEBRANIA 10:25
- Siri ya utajiri wa Mfalme Daudi ni kwasababu
alikuwa na Roho ya Kuabudu, alitamani kukaa
kwenye nyumba ya Mungu siku zote. Soma
ZABURI 84:4, 10
- Yesu Kristo alipokuwa na umri wa miaka 12
alipenda kwenda hekaluni na alikaa hekaluni
siku 3 mpaka wazazi wake wakaanza kumtafuta.
Soma kitabu cha LUKA1: 46 – 49
Watu wengi hawana shauku ya kumtafuta
Mungu, wana shauku ya kutafuta PESA, ndiyo
maana hata hizo pesa wanazotafuta hawazipati.
Yesu alisema tafuteni kwanza ufalme wakena
mengine yote mtazidishiwa. MATHAYO 6:33

15
Wengi wanauliza maswali, “kwa nini kanisa la
Ukombozi wana chukua muda mrefu sana
kushinda kanisani yaani siku yote ya Jumapili
wanaimalizia kanisani.”

Lazima tuwe na misingi ya kiroho, Mungu mwenyewe


alitoa agizo kwamba siku moja katika wiki lazima tuitoe
kwake yeye kwa ajili ya kumfanyia IBADA. Ni siku yote
siyo nusu siku

Mungu ndiye mkuu kuliko wote hivyo anahitaji


kupewa nafasi ya kwanza yenye uzito. Ukimpa
Mungu nafasi ya kwanza na yeye atakupa nafasi ya
kwanza. Ukimpa nafasi ya kumi na yeye atakupa
nafasi ya kumi. Watu wengi leo hawampi Mungu nafasi
kubwa na ya kwanza, na yeye amewatupa. Mungu
anahitaji muda mwingi wa kutosha ili kumuabudu yeye,
siyo nusu saa au saa moja.

Yesu Kristo alisema, haki yenu isipowazidi hao


WAANDISHI na MAFARISAYO, kamwe hatuwezi
kuurithi ufalme wa Mungu. MATHAYO 5:20

Mafarisayo ni watu wa dini, wao “wana Sali” mara 5


kwa siku na kila siku alfajiri na mapema “wanasali‟.
Sasa angalia Wakristo walivyo nyuma kwenye kuabudu,
Yesu alisema, Lazima tuwazidi watu wa dini ndipo
tutaingia kwenye ufalme wa Mungu.
Mifano ipo wazi kabisa,hebu angalia jinsi ambavyo watu
wanavyotoa muda mwingi kwenye biashara zao, kwenye
kazi walizoajiriwa kila siku, wafanyabiashara wengine
wanaingia asubuhi na kutoka usiku kwa siku sita kila wiki
ni masaa mengi sana, hali kadhalika walioajiriwa.

16
Mimi huwa nashangaa kwa nini Mungu huwa
tunampa muda mdogo namna hii? Ambaye yeye ndiye
chanzo cha Baraka zetu. Tunaona nyakati za zamani
watu waliofanikiwa sana na kuwa na afya na utajiri ni
kwa sababu walimpa Mungu nafasi kubwa sana ya
“kumuabudu”.

Angalia siku za Nehemia. Soma NEHEMIA 8:3


“Akasoma humo mbele ya uwanja uliokuwa
ukikabili lango la maji, tangu mapambazuko
hata adhuhuri,….”

Biblia inasema kwamba, ibada ilianza ASUBUHI na


MAPEMA, mpaka ADHUHURI, hiyo ndiyo ibada
inayompendeza Mungu. Angalia tena
“… wakasoma katika kitabu cha torati ya BWANA,
Mungu wao, muda wa robo siku; na robo nyingine
wakaungama, wakamwabudu BWANA, Mungu wao.”
NEHEMIA 9:3

Hapa Biblia inasema, walisoma neno la Mungu kwa


robo ya siku maana yake ni “masaa 6”, na robo
nyingine waliungama maana yake ni masaa 6 pia. Sasa,
linganisha na makanisa ya leo kama kuna kanisa
linalofanya ibada siku ya Jumapili kwa masaa 6.
Hakuna kanisa la jinsi hiyo. Je ni kanisa lipi ambalo
linachukua muda wa masaa 6 kwa ajili ya MAOMBI YA
TOBA ili Mungu awatakase?

Ibada za leo zinashangaza ni ibada zinaitwa “express”


eti watu wana haraka! Mahubiri dakika 30, maombi
dakika 10, ibada ni lisaa limoja. Hizo siyo ibada za Roho
Mtakatifu ni ibada za DINI ambazo Mungu anazichukia
sana. Soma AMOSI 5:21 – 23.

17
Mfano mzuri wa Yesu Kristo Bwana wetu alichukua
muda mrefu sana kwenye ibada zake. Kuna siku moja
aliwafundisha watu kwa muda wa siku 3 usiku na
mchana. Soma MATHAYO 15:32 Hapa Yesu Kristo
alikaa na watu hawa wanaume na watoto pia wanawake
kwa siku 3 na palikuwa “nyikani”yaani jangwani. Yesu
hakuangalia kuna wake za watu au kuna watoto Yesu
hakujali kama wana njaa. Hii ndiyo siri ya miujiza
aliyokuwa nayo Yesu Kristo. Siri ilikuwa ni kumpa
Mungu BABA muda mrefu wa kutosha wa kumuabudu.

Angalia tena, nyakati za Mtume Paulo, ibada zake


zilikuwa ni ibada ndefu sana. Biblia inasema
walipokutanika kwenye ibada siku ya wiki maana yake
“JUMAPILI” (living bible). Mtume Paulo alifululiza
mahubiri yake mpaka usiku wa manane hadi ndugu
mmoja aliyeitwa EUTIKO alilemewa na usingizi
akaanguka kutoka ghorofani mpaka chini na akafa,
lakini mtume Paulo alimfufua kwa jina la Yesu Kristo.

( Soma MATENDO YA MITUME 20:7 – 12) na siyo tu mpaka


usiku wa manane aliendelea mpaka alfajiri. Hizi ndizo ibada
zinazompendeza Mungu.
Sasa, tujiulize maswali hivi hizi ibada za “NUSU SAA”
zilianzishwa na nani? Na je hizi Ibada fupi za haraka- haraka
kweli Mungu anazikubali?
Mtu aliniambia, “kama hili kanisa lingekuwa linafanya
IBADA kwa muda mfupi kanisa hili lingejaa sana watu”.
Eti watu wanalalamika wake zao wanachelewa kutoka
kanisani. Huyu mtu ni mpumbavu, hajui kwamba njia ya
mbinguni ni nyembamba (MATHAYO 7:13 – 14 )
Na Yesu akasema ni wachache watakao ingia mbinguni. Tena
akasema wengi watajaribu kuingia lakini wasiweze.
SOMA LUKA 13:24

18
Kama wanaume wetu, tunawapa muda wa kutosha/ wake
zetu tunawapa muda wa kutosha na kama biashara tunatoa
masaa karibu 60 kwa wiki kwa nini Mungu tusimpe hata
masaa 10 tu kwa wiki?

Mungu anatafutwa kwa bidii ndipo anaonekana.


Soma MITHALI 8:17.
Kumbuka chochote unachokipa nafasi kubwa na ya kwanza
ndicho kinachokuwa Mungu wako na ni moja ya ibada ya
sanamu. Wengi Mungu wao ni matumbo yao kwani
wanachukua muda mrefu kutafuta kwa sababu ya matumbo
yao, hii ni hatari sana. Soma andiko hili la AJABU.
“mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo,…” WAFILIPI 3:19.

Kumbuka hizi ibada za haraka- haraka ni ibada feki zinazo


mdhihaki Roho Mtakatifu siyo ibada ni makusanyiko ya dini
yasiyo na nguvu yoyote ya Mungu, ndiyo maana makusanyiko
hayo ya dini hauwezi kuona muujiza wowote kwa sababu wao
ndiyo wanampangia Mungu muda wa kumaliza IBADA na siyo
Mungu anayewapangia wao muda wa kumaliza ibada. Kama
unaabudu kwenye makanisa kama hayo hapo unapoteza muda
wako ondoka haraka kwa Jina la Yesu Kristo.

Mpe Mungu nafasi ya kwanza, na yeye atakupa


nafasi ya kwanza.

SIRI KUBWA

Pale unapoacha kuhudhuria ibada ya jumapili na ukaanza


kufanya BIASHARA, ukipata hizo pesa hazitafanya kitu
chochote, ni pesa zenye laana
- Jumapili siyo siku ya kutembelea ndugu
- Jumapili siyo siku ya kufanya biashara

Mungu kwanza na vingine vinafuata

19
MAMBO YA KUZINGATIA ILI TUUKULIE WOKOVU

- Tujiunganishe na kanisa lenye nguvu


ya Mungu.
Kumbuka Mkaa mmoja wa kuni hauwezi
kuivisha chakula. Kama dini yako ya zamani
ilikuwa haijakusaidia kwa lolote, basi hauna
budi kuhama na kutafuta kanisa litakalo
kusaidia kiroho.
“Basi, mwanadamu, funga tayari vyombo kwa
uhamisho, ukahame wakati wa mchana mbele ya
macho yao; nawe utahama toka mahali pako hapa
mpaka mahali pengine mbele ya macho yao....”
[EZEKIELI 12:3]

- Ili tuzidi kuukulia wokovu ni MUHIMU


KUHUDHURIA IBADA ZOTE.
Usikubali kukaa nyumbani siku za ibada,
kwani unapokosa ibada moja kumbe ndipo
ilikuwa siku yako ya kufunguliwa.
“wala tusiache kukusanyikapamoja,....”
[WAEBRANIA 10:25]

Kwa msaada zaidi ili uzidi kuukulia wokovu


nakufunguliwa zaidi; wasiliana nasi :-

KANISA LA UKOMBOZI MINISTRIES FOR ALL


NATIONS,
P.O.BOX 1961, MWANZA- TANZANIA.
Barua pepe:-ukombozichurch@yahoo.com
Simu:- 0768 321321; 0747 321 322; 0754 088938; 0739 088938
20
NI NGUVU YA YESU KRISTO PEKEE
INAYOWEZA KUSABABISHA MUUJIZA
WAKO

Kama hujakata shauri kuokoka ujue utazidi kuishi kwenye


mateso na kukandamizwa na ADUI. Ukimpokea Yesu Kristo
moyoni mwako kwa imani yeye atakuponya, atakufungua na
kukupa nguvu ya kushindi kila aina ya mateso kwenye maisha
yako.
OMBA SALA HII KWA IMANI:-
Ee, Bwana Yesu, mimi ni mwenye dhambi, kwa kuzaliwa na kwa kutenda
mimi mwenyewe; kuanzia leo naomba UNIOKOE. Unipe NGUVU YA
KUSHINDA DHAMBI; Ulifute jina langu kwenye kitabu cha hukumu,
uliandike jina langu kwenye kitabu cha uzima. Zifute dhambi zangu zote
kwa DAMU YA YESU KRISTO. Ninaamini nimeokoka kuanzia leo.
AMINA.

JINSI YA KUFIKA KANISANI - MWANZA.

Panda magari ya NYANSHANA, shukia kituo cha mwishoni


(Nyanshana stendi) ulizia kanisa la ukombozi lililoko
michungwani.
Au
Panda magari ya maduka tisa shukia kituo cha maduka tisa,
ulizia kanisa la ukombozi lililoko michungwani.
Piga simu no:-0763 710426 / 0755 008642/ 0754 088938
0768 321321; 0747 321 322; 0711 66 68 68

Ukiwa jijini Mwanza; sikiliza


UKOMBOZI FM REDIO 104.1
21
PATA NAKALA ZA VITABU MBALIMBALI,
VILIVYOANDIKWA NA MTU WA MUNGU NABII BG
MALISA, VITAKAVYOKUSAIDIA KATIKA
MAISHA YAKO:-

Vitabu hivyo ni kama:-

- NGUVU YA MAOMBI YA REHEMA


- MAOMBI YA KUFICHUA
- MAOMBI YA KUFUNGULIWA
- MAOMBI YA UKOMBOZI
- SIR 50 ZA USHINDI
- KANUNI ZA KUKAMATA MZUNGUKO WA PESA
- JINSI YA KUISHINDA ROHO YA UTASA
- JIFUNGUE WEWE MWENYEWE!
- MWANAMKE JITAMBUE!
- NIDHAMU KWENYE MASUALA YA FEDHA
- UFANYE NINI WAKATI HUJUI CHA KUFANYA
- SILAHA 30 ZA MUNGU
- MAOMBI YA KUVUNJA MAAGANO
- HATARI YA ROHO YA KUACHA
- SIRI YA KUWEKA AGANO KWENYE MADHABAHU
MOJA
- AGANO LA FUNGU LA KUMI
- JINSI YA KUWASHINDWA WACHAWI, Na vingine
vingi:-
Pata nakala yako ya vitabu hivi kwa kuwasiliana nasi kwa
namba:-
0763 710426 / 0768 321321, 0747 321 322; 0711 66 68 68

You might also like