Professional Documents
Culture Documents
Annie Oscar Bwanali
Annie Oscar Bwanali
IDARA YA UTAFITI
NA
2023
NINI CHANZO CHA WAKRISTO KURUDI NYUMA
KIIMANI KATIKA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE?
ENEO LA UTAFITI NI WILAYA YA KIGAMBONI MKOA
WA DAR ES SALAAM, TANZANIA.
NA
2023
UTHIBITISHO
Aliyetia sahihi hapa chini, anathibitisha kuwa amesoma utafiti huu unaosema “Nini
Chanzo cha Wakristo kurudi nyuma kiimani katika makanisa ya Kipentekoste? Eneo la
ikubaliwe na Chuo cha New Life Academy of Leadership kwa ajili ya kutimiza sehemu ya
…………………………….
Msimamizi
i
HAKIMILIKI
Hairuhusiwi kuiga au kunakili kwa namna yoyote sehemu yoyote ile ya utafiti huu kwa
njia yoyote kama vile, kielektroniki, kurudufu nakala, kurekodi au njia yoyote nyingine
bila ya idhini ya mwandishi au Chuo cha New Life Academy of Leadership kwa niaba.
ii
TAMKO LA UTAFITI
Mimi, Annie Oscar Bwanali, nathibitisha kuwa utafiti huu ni kazi yangu halisi na
haijawahi kuwasilishwa katika Chuo Kikuu kingine chochote kwa ajili ya kutunukiwa
_______________________
Saini
iii
SALAMU
iv
SHUKRANI
Kukamilisha kazi hii mpaka katika hatua hii iliyofika ni jambo la kumshukuru sana
Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya
njema na akili timamu katika kipindi cha mwaka mmoja nilichotumia katika kusoma
Pia, namshukuru msimamizi wangu wa kazi hii kwa kunisimamia vizuri tangu katika
uandishi wa pendekezo la utafiti, uandishi wa ripoti ya utafiti kama ilivyo hivi sasa.
Namshukuru sana kwa kunitia moyo kila mara nilipokwama na kutokuiona njia yeye
aliniongoza na kunishauri.
Nawashukuru pia familia yangu ilikuwa bega kwa began na mimi mpaka kukamilisha kazi hii
ya utafiti.
v
IKISIRI
Mada ya utafiti huu ni kutathmini chanzo cha Wakristo kurudi nyuma kiimani katika
Salaam, Tanzania. Malengo mahususi ya utafiti huu yalikuwa ni kujua kwanini watu
wanahama makanisa. Ili kukamilisha malengo haya mahususi, data za utafiti zilikusanywa
kwa kutumia mbinu za usomaji makini na upitiaji wa nyaraka. Utafiti umepata matokeo
kuokoka ili wasirudi nyuma kiimani, pia kuwepo na ufuatiliaji wa mara kwa mara kwa
wale waliookoka ikiwezekana kujua mahitaji yao ya kiroho na kimwili ili ikiwezekana
yajibiwe, pia kufanyike maombi ya mara kwa mara kwaajiri ya watu wapya waliookoka.
vi
YALIYOMO
UTHIBITISHO..........................................................................................................i
HAKIMILIKI............................................................................................................ii
TAMKO LA UTAFITI............................................................................................iii
SALAMU.................................................................................................................iv
SHUKRANI..............................................................................................................v
IKISIRI..................................................................................................................... vi
YALIYOMO...........................................................................................................vii
SURA YA KWANZA...............................................................................................1
UTANGULIZI..........................................................................................................1
1.1 Utangulizi............................................................................................................1
SURA YA PILI.........................................................................................................8
MAPITIO YA NYARAKA.......................................................................................8
2.1 Utangulizi............................................................................................................8
SURA YA TATU....................................................................................................15
vii
MBINU ZA UTAFITI.............................................................................................15
3.1 Utangulizi..........................................................................................................15
3.6.2 Dodoso...........................................................................................................18
3.6.3 Mahojiano.......................................................................................................18
SURA YA NNE......................................................................................................21
4.1 Utangulizi..........................................................................................................21
SURA YA TANO...................................................................................................38
HITIMISHO NA MAPENDEKEZO.......................................................................38
5.1 Utangulizi..........................................................................................................38
5.2 Hitimisho...........................................................................................................38
5.3 Mapendekezo.....................................................................................................40
viii
MAREJEO..............................................................................................................42
VIAMBATANISHO...............................................................................................43
ix
SURA YA KWANZA
UTANGULIZI
1.1 Utangulizi
Sura hii inawasilisha utangulizi wa utafiti huu. Vipengele vilivyomo ndani ya sura hii ni
Mithali 1:32-33 Biblia mahali hapo inasema; “Maana kurudi nyuma kwao wajinga
atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya.” Ni muhimu kuwa na ufahamu kuwa
sio wakristo wote wanaopata neema ya kuzaliwa mara ya pili au kuokoka wanapata neema
vilevile ya kuukulia wokovu, wengine wanarudi nyuma na hata kufa kiroho kutokana na
watu wanarudi nyuma na hatimaye kufa kiroho, lakini katika somo hili tutajaribu
Luka 8:13 Biblia inasema “Na wale penye mwamba ndio wale ambao wasikiapo hulipokea
lile neno kwa furaha; nao hawana mizizi, huamini kitambo kidogo, na wakati wa
kujaribiwa hujitenga.” Ni muhimu kufahamu kuwa mara baada ya kuokolewa kila mtu
aliyeokoka anapaswa kuhakikisha kuwa analifanyia kazi neno la Mungu na kujijengea juu
ya msingi huu, kila mmoja anapaswa kuota mizizi na sio tu kuota lakini kuhakikisha kuwa
mizizi yake inashuka chini sana, tatizo kuu la wakristo wengi sana wako katika kundi hili
linalotajwa na Yesu Kristo kama watu au mioyo inayolipokea neno la Mungu kwa furaha
lakini hawana mizizi, hawaendelei mbele wanadumaa na hatimaye kuiacha imani, Hawa
1
pia wanaweza kufananishwa na mtu aliyejenga nyumba yake kwenye Mchanga Mathayo
mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja,
pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu
mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja,
pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.”
Unaweza kuona tatizo kubwa la wapendwa wengi sio tu kulitendea kazi neno lakini hata
kulielewa hawalielewi,wako wakristo ambao hata hawajui kwanini wanatoa sadaka, kwa
nini wanahudhuria ibada katika kanisa wanalohudhuria, kwa nini wanaomba, kwa nini
kuchanganyikiwa, Hwawezi kuitetea imani, Hawana ujuzi wala uzoefu katika kutembea na
Mkristo mwenye Misingi imara anapaswa kusimama mwenyewe haijalishi hata kama mtu
aliyekuingiza katika ukristo amehama imani na kujiunga na imani potofu, yeye anaendelea
kusimama kwa gharama yoyote, wazazi ndugu jamaa au rafiki wa karibu hawezi
kubadilisha msimamo wa mtu mwenye mizizi, utashangaa kuona mtu aliyeokoka hajui
hata tofauti ya Mashahidi wa Yehova na hata wasabato yeye kila aina ya fundisho na imani
mbaya kuhusu kiongozi wako wa kidini haiwezi kuwa sababu yaw ewe kuiacha imani,
unaweza kuwepo kanisani lakini kama mimani yako haijajengwa kwenye misingi na
2
zinauhusiano gani na wokovu wako?uwapo duniani je unafikiri unaweza kumuacha Yesu
kwa sababu ya dhambi ya kiongozi wako?mkristo anayeweza kumuacha Yesu kwa sababu
Mkristo aliyesimama vema ni yule ambaye amesimama hawezi kutikiswa na kurudi nyuma
kwa wengine Yohana 6:66-69 “Kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi wake
wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena. Basi Yesu akawaambia wale Thenashara, Je!
Ninyi nanyi mwataka kuondoka? Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani?
Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe
Yesu kwa sababu walitambua kuwa Yesu anao uzima wa milele, Mtu ambaye hajajengwa
kwenye msingi na hana mizizi kwake ni rahisi kukata tamaa, ni vigumu kwake kupokea
nyuma Biblia haitutii moyo kumfuata kiongozi awaye yote anapokuwa amekengeuka
badala yake inatutia moyo kumfuata Yesu au kumfuata kiongozi kama anamfuata Yesu
pale anapokengeuka sisi tunasonga mbele na Yesu tu, tukimuombea yeye au kumuacha na
ukengeufu wake Paulo mtume alisema tumfuate yeye kama anavyomfuata Kristo 1
kiroho ni rahisi sana washirika wako kukutii katika jambo lolote utakalowaamuru,
kumfuata Yesu na sio mtu au dhehebu, wengi tumewaharibu washirika katika makanisa
kwa sababu ya kuwaaminisha katika Dhehebu na katika mtu, badala ya Yesu na kuwafanya
tunauwezekano mkubwa sana wa kufanya dhambi tena kubwa na za aibu tu, hivyo ni
3
lazima ieleweke wazi kuwa kama tutawaambia washirika wetu kutenda jambo ambalo sio
la kibiblia basi wawe na uwezo wa kusema hapana kubwa, na kama tutafundisha fundiso
lisilo la kibiblia pia wawe na uwezo wa kutuambia Mchungaji, Mwinjilisti, Nabii, Mtume,
watumishi wanafikia ngazi hata ya kuoga na mshirika kwa madai kuwa ni oga takatifu,
wengine wameweza kuwaibia wakristo mali zao zote kwa kisingizio cha kumtolea Bwana,
haya na mauchafu mengine mengi yanaweza kufanyika kwa sababu wakristo wengi
wamedumaa kiroho na hawataki kujijenga juu ya msingi na kuota mizizi mikali katikia
imani hivyo wanazolewa na kila mbwembwe za kila upepo wa kila elimu hata zile zisizo
Nikwa sababu kama Hizi Paulo alisema mnifuate mimi kama ninavyomfuata Kristo hii ni
kwa sababu Paulo mtume alikuwa na uhakika wa mwenedo na tabia yake katika Kristo,
hatusomi katika maandiko kuwa Haruni aliruhusu makutano kuabudu sanamu Hapo Musa
kushindwa kusimama katika zamu yao na kuabudu miungu ya sananu huku wakisema
kuwa ndio mungu aliyewaokoa katika mikono ya Farao huko Misri? Ni wazi kuwa watu
hawana mizizi katika ujuzi wao binafsi na Mungu kumbuka kuwa Mungu si wa mkumbo,
kila mmoja anapaswa kujijengea uzoefu binafsi katika kuwa na uhusiano wako na Mungu
4
Wengi wa walioabudu sanamu chini ya uongozi wa Haruni walikuwa ni watu waliofuata
kupiga kelele wakisema asulubiwe asulubiwe hawakuwa na msimamo wao thabiti bali
walikuwa watu walifuata umati au mkumbo, kufuata mkumbo katika kutenda uovu ni
tatizo kubwa sana kwa wakristo wa nyakati za leo hebu komaa kiroho, hebu kataa
kudumaa, hebu kubali kuongozwa na neno na uote mzizi ya ujuzi wako mwenyewe
mfanye Mungu kuwa Mungu wako na neno lake kuwa neno lako, usikubali kwenda kwa
mkumbo Muombe Mungu akupe neema ya kusimama kwa miguu yako na uwe mkristo
Kanisa la kwanza ambalo lilikuwa la mitume pamoja na waliookoka baada yao lilidumu
katika misingi minne ukisoma kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume 2:42 inasema
mkate na kusali” na nyongeza yake ni Matendo ya Mitume 4:32 ambayo inasema “Na
jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja
aliyesema ya kuwa kitu chochote alichonacho ni mali yake mwenyewe bali walikuwa na
vitu vyote shirika. Ukiangalia mistari utagundua ya kwamba kanisa lilidumu katika imani
maana watu hawakuweza kurudi nyuma kiimani wala kuacha wokovu waliimarika
walipata mafundisho sahihi, walijibiwa mahitaji yao, walipata amani ya moyo maana yake
waliridhika. Ili kwasasa imekuwa tofauti ndio maana kunatokea kurudi nyuma kwa imani
za Wakristo na kuacha wokovu. Hivyo basi utafiti huu umekusudia kutathmini chanzo cha
5
Wakristo kurudi nyuma kiimani katika makanisa ya Kipentekoste: Eneo la Utafiti ni
Lengo kuu la utafiti huu ni kutathmini chanzo cha Wakristo kurudi nyuma kiimani katika
makanisa ya Kipentekoste.
Utafiti huu una umuhimu sana katika kanisa. Kwa upande wa taaluma, utafiti huu utakuwa
6
kuwaimarisha Wakristo makanisani ili wasirudi nyuma kiimani. Wanafunzi wa taaluma ya
ambao wataufanya baadae. Kwa upande wa kanisa utafiti huu utasaidia kulijulisha kanisa
namna sahihi ya kuwasaidia watu wanaookoka makanisani ili wasirudi nyuma kiimani na
Utafiti huu unafanywa kwa lengo la kutathmini chanzo cha Wakristo kurudi nyuma
wa Dar es Salaam, Tanzania, lakini kulingana na malengo ya utafiti huu ilionekana kuwa
eneo hilo moja linatosha. Utafiti huu ulichukua miezi mitatu ili kukamilika.
Utafiti huu una jumla sura tano ambapo sura ya kwanza inahusu utangulizi na usuli wa
tatizo la utafiti, sura ya pili inahusu mapitio ya kazi tangulizi na mkabala wa kinadharia na
sura ya tatu inahusu mbinu za utafiti. Sura ya nne inahusu uwasilishaji, uchambuzi na
7
SURA YA PILI
MAPITIO YA NYARAKA
2.1 Utangulizi
Mkristo: Kwa tafsiri kutoka kamusi ya Webster mkristo ni “mtu mwenye kukiri imani
ndani ya yesu kama kristo au dini yenye msingi wa mafundisho ya yesu.” Ijapokuwa huu
ni mwanzo mwema wa kufahamu mkristo ni mtu gani, kama maelezo mengi ya kidunia
Neno mkristo limetumika mara tatu katika agano jipya (Matendo 11:26; Matendo 26:28; 1
Petro 4:16). Wafuasi wa yesu kristo waliitwa kwa mara ya kwanza “wakristo” antiokia
(Matendo 11:26) kwa sababu tabia zao, matendo yao na hotuba zao zilikuwa kama za
kuwadhihaki wakristo hao. Ina maana sawa na “Kuwa mmoja wa kundi la kristo” au
“mfuasi wa kristo,” ambayo imefanana na tafsiri ya Neno hili katika kamusi ya Webster.
Kwa bahati mbaya, neno mkristo limepoteza kwa kiwango kikubwa usawa wa matumizi
yake na Linatumika mara kwa mara kumaanisha tu mtu mwenye dini au pengine muadilifu
kinyume cha Mfuasi halisi wa yesu kristo aliyezaliwa mara ya pili. Watu wengi
wasioamini na kuwa na tumaini ndani ya yesu kristo hujichukulia tu kuwa ni wakristo kwa
sababu wanahudhuria ibada za kanisa ama wanaishi katika taifa la kikristo. Lakini, kuenda
hakufanyi mtu kuwa mkristo sawa na mtu kuenda gereji hakumfanyi kuwa gari.” Kuwa
8
mshirika wa kanisa anayehudhuria ibada kila mara na kutoa kwa ajili ya kazi za kanisa
hakuwezi kukufanya wewe kuwa mkristo. Biblia inatufundisha ya kwamba matendo yetu
mema tunayoyatenda hayawezi kutufanya tukubalike mbele za Mwenyezi Mungu. Tito 3:5
inatuambia ya kwamba “si kwa matendo ya haki tuliyoyatenda, ila kwa huruma zake
alituokoa kwa kutuosha na kutufanya upya kwa roho Mtakatifu.” Kwa hivyo mkristo nimtu
aliyezaliwa mara ya pili na Mungu (Yohana 3:3; Yohana 3:7; Petero wa kwanza 1:23) na
aliyeweka imani na tumaini lake lote ndani ya yesu kristo. Waefeso 2:8 inatuambia ya
kwamba “Kwa neema mmeokolewa kupitia imani wala si kwa ajili yenu wenyewe bali ni
kipawa cha Mungu.” Mkristo wa kweli ni mtu aliyetubu dhambi zake na kuweka imani na
tumaini lake ndani ya Yesu kristo pekee. Imani yao haimo ndani ya kufuata dini ama
kanuni Fulani za uadilifu ama miongozo ya kusema fanya hiki na usifanye kile. Mkristo
wa kweli ni mtu aliyeweka imani na tumaini lake lote ndani ya utu wa Yesu kristo na
kukubali ya kwamba alikufa msalabani kwa fidia ya dhambi zetu na akafufuka tena siku ya
tatu kupata ushindi dhidi ya kifo ili awape uzima wa milele wote wamwaminio. Yohana
1:12 inatuambia ya kwamba “wote waliomwamini aliwapa uwezo kuwa wana wa mungu,
kwa wale waliaminio jina lake.” Mkristo wa kweli ni mwana wa Mungu halisi, sehemu ya
jamii halisi ya mungu na aliyepewa maisha mapya ndani ya kristo. Alama ya mkristo wa
kweli ni upendo kwa wengine na utiifu kwa neno la Mungu (Yohana wa kwanza 2:4;
Imani: Waebrania 11: 1 inatuambia kuwa imani ni "Basi imani ni kuwa na hakika ya
nyingine ya maisha ya Kikristo ni muhimu zaidi kuliko imani. Hatuwezi kununua, kuuza,
au kuipa marafiki zetu. Kwa hiyo imani ni nini jukumu gani imani inahusika katika maisha
ya Kikristo? Neno hili linafafanua imani kama "Imani katika, kujitolea, au kuamini mtu
fulani au kitu, hasa bila uthibitisho wa kimantiki." Pia inafafanua imani kama "kuamini na
9
kujitolea kwa Mungu." Biblia ina mengi zaidi ya kusema juu ya imani na jinsi ni muhimu.
Kwa kweli, ni muhimu sana kwamba bila imani hatuna nafasi na Mungu, na haiwezekani
kumpendeza (Waebrania 11: 6). Imani ni kumwamini Mungu mmoja, Mungu wa kweli,
hata bila kumwona Yeye. Imani inatoka wapi? Imani sio kitu tunachojishughulisha
wenyewe, wala si kitu ambacho tunazaliwa nacho, wala imani nkuwamatokeo ya bidii
katika kujifunza au kufuata kiroho. Waebrania 2: 8-9 inafanya wazi kwamba imani ni
zawadi kutoka kwa Mungu, sio kwa sababu tunastahili, tumeipata, au tunastahili kuwa
nayo. Sio kutoka kwetu; ni kutoka kwa Mungu. Haipatikani kwa nguvu zetu au mapenzi
mpango Wake takatifu na kusudi, na kwa sababu hiyo, Yeye anapata utukufu wote. Mungu
alifanya njia ya kutofautisha kati ya wale ambao ni wake Yeye na wale ambao sio wake, na
inaitwa imani. Kwa urahisi tu, tunahitaji imani ili kumpendeza Mungu. Mungu anatuambia
kwamba inampendeza Yeye kuwa tunamwamini hata ingawa hatuwezi kumuona. Sehemu
kwa bidii." Hii sio kusema kwamba tuna imani kwa Mungu tu kupata kitu kutoka kwake.
Hata hivyo, Mungu anapenda kuwabariki wale wanaomtii na waaminifu. Tunaona mfano
kamili wa hili katika Luka 7:50. Yesu anahusika katika majadiliano na mwanamke
mwenye dhambi wakati anatupa maelezo ni kwa nini imani inastahili sana. "Imani yako
imekuokoa; nenda kwa amani." Mwanamke aliamini kwa Yesu Kristo kwa imani na
akampa thawabu kwa ajili yake. Hatimaye, imani ni chombo kinachotuwezesha hadi
mwisho, kwa kujua kwa imani kwamba tutakuwa pamoja na Mungu milele. " Naye
na kufurahi sana, kwa furaha isiyoneneka, yenye utukufu, katika kuupokea mwisho wa
imani yenu, yaani, wokovu wa roho zenu" (1 Petro 1: 8-9). Mifano ya imani; Waebrania
sura ya 11 inajulikana kama "sura ya imani" kwa sababu ndani yake matendo makuu ya
10
imani yanaelezwa. Kwa imani Abeli alitoa sadaka ya kupendeza kwa Bwana (mstari wa 4);
Kwa imani Nuhu alijenga safina wakati ambapo mvua haijulikani (mstari wa 7); Kwa
imani Ibrahimu alitoka nyumbani kwake na kutii amri ya Mungu ya kwenda penye hajui,
kwa hiari alimtolea mwanawe pekee (8-10, 17); Kwa imani Musa aliwaongoza wana wa
Israeli kutoka Misri (mstari wa 23-29); Kwa imani Rahabu alipokea wapelelezi wa Israeli
na akaokoa maisha yake (mstari wa 31). Wengi wa mashujaa wa imani wanatajwa "ambao
kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa
vya simba, walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu
wageni."(mstari wa 33-34). Kwa wazi, kuwepo kwa imani kunaonyeshwa kuwa wa hatua
(kitendo). Imani ni jiwe kuu la Ukristo; Bila kuonyeshe imani na uaminifu kwa Mungu
hatuna mahali pamoja naye. Tunaamini katika kuwepo kwa Mungu kwa imani. Watu
wengi wana wazo lisilo wazi, lisilojumuishwa kuwa Mungu ni nani lakini hawana heshima
inayofaa kwa nafasi yake iliyoinuliwa katika maisha yao. Watu hawa hawana imani ya
kushindwa wakati mwingine, lakini kwa sababu ni zawadi ya Mungu, iliyotolewa kwa
watoto Wake, hutolewa nyakati za majaribu na mateso ili kuthibitisha kuwa imani yetu ni
"furaha safi" kwa sababu kujaribiwa kwa imani yetu hutoa uvumilivu na kukua, kutoa
Wengine wanarudi nyuma kwa sababu ya kute nda zambi ya mwili: Citoyen Bumani
alifanya hivi. Alikuwa amekaa pamoja na mke wake kwa miaka 15 na alishiriki ndani ya
kazi ya Mungu kanisani vilevile. Alikuwa tu namna ya Wakristo wote, lakini alifurahia
11
wanawake zaidi. Alipenda kuwaambia maneno matamu na kugusagusa miili yao. Halafu
siku moja ilimpasa kufanya safari kwa ajili ya bwa na wake wa kazi na kule katika mji
mwingine ali anguka. Tangu siku ile anafikia nyumba ya Mungu siku moja moja tu. Hana
furaha tena nyumbani mwake kama mbele. Watu hawajui nini imetokea na kwa sababu
gani roho yake ni baridi naye hakai na furaha pamoja na watu. Anakusudi kuficha za mbi
Watu wengine wanafanana na mwana mpotevu katika Luka 15: Tuwaze juu ya citoyen
Bulabanga. Alipata nguvu nyumbani mwa Wakristo na aliokolewa mwaka mmoja mbele
ya kuingia kazi ya askari. Alifurahi sana siku alipoondokea nyumba ya wazazi wake na
hakuwa chini ya amri yao tena. Alikusudi kutimiza mapenzi yake yote. Askari wenzake
hawakuweza kujua ya kwamba yeye ni Mkristo. Alishiriki ndani ya zambi zao zote . . .
lakini kule ndani zamiri yake ilimshitaki naye hakuwa na furaha hata kidogo.
Wakristo wengine huacha njia ya Bwana kwa sababu ya kujifunza zaidi: Mfano ni Citoyen
Kularaba aliyekuwa mwenye akili nyingi. Nyuma ya kumaliza chuo ya Biblia alikwenda
kwa chuo cha elimu nyingi. Alitaka sana kuendelea na alijifunza elimu ya asili ya mambo
yote na vitu vyote. Nyuma ya mwezi mmoja tu alipata shaka rohoni juu ya imani yake kwa
sababu ya mafundisho aliyopata pale. Hakuwaka tena kwa Bwana. Aligeuka mtu wa
Wakristo wengine wanarudi nyuma kwasababu ya ulevi: Alianza kunywa malofu nusu
nusu tu wakati alipokuwa nyumbani mwa watu wengine, lakini alikunywa zaidi saa
pombe inamtawala kabisa. Anapata haya kubwa kila mara anapowaza juu ya kanisa na
rafiki zake Wakristo. Halafu anakunywa chupa kingine cha pombe kwa kulalisha dhamiri
yake.
12
Wakristo wengine wanarudi nyuma kwa sababu wameoa hasiyeamini: Tubakori alikuwa
msichana wa furaha aliyependa Bwana sana. Alipasha rafiki zake zote habari za Mwokozi
wake. Kijana mmoja alipatana naye kwa kumwoa na nyuma ya majuma machache kijana
huyu alisema kwamba ameamini Kristo vilevile. Leo Tubakori anafikili mume wake
hakuamini kweli kweli. Yeye na mume wake ha washiriki pamoja ndani ya ma neno ya
Mungu na nyumba yao ni nyumba ya ma gomvi tu. Watoto wao hawajui kutii. Mume wake
nyuma ya kazi anakwenda kukaa pamoja na rafiki zake, akiacha Tubakori peke yake
nyumbani na huzuni na machozi. Tubakori alijaribu kufuata Bwana kwa miaka michache
Wakristo wengine wanarudi nyuma kwa sababu ya kazi yao: Hawafanyi zambi kubwa sana
lakini wanaacha kazi yao kula saa zao zote hata hawana saa tena kwa jamaa yao wala kwa
Mungu. Hawaweki saa kwa kusoma Biblia na kwa maombi na wanakutana pamoja na
Wakristo wengine kuabudu Mungu siku moja moja tu. Masumbuko ya maisha ya sasa
yamepunguza nguvu yao ya roho na kuwaacha zaifu sana kwa maneno ya Mungu. Tamaa
kabisa. Wengine wanapata hasara na halafu roho zao zinageuka baridi. Hawakubali ya
kwamba mambo haya ni mapenzi ya Mungu kwa maisha yao. Hawafahamu ya kwamba
taabu yao itageuka baraka kwao nyuma, hivi wanakasirika na kupoa rohoni. Wengine
wanakataa kusamehe watu wengine ambao waliwaumiza. Wanakaa na roho nguvu, bila
rehema. Basi Mungu Baba hawezi kusamehe watoto wake wanaokataa kusamehe ndugu
Wakristo wengi wanarudi nyuma kwa sababu ya magomvi madogo madogo nyumbani
13
kusemezana vizuri, na hawa - ombi tena pamoja. Wao wawili wanakataa kukubali ya
wao wawili walikuwa wamekwenda mbali na Bwana. Kwa nini watu wanarudi nyuma?
kuwatawala, wanapenda mali na vitu vya dunia hii kupita Mungu, wanakataa kusamehe
wenzao, vivi hivi. Unashangaa kusikia ya kwamba waamini wanaweza kwenda mbali na
Mungu hivi?
Tukumbuke kwamba watu wa Mungu wa zamani walirudi nyuma vilevile: Daudi alirudi
nyuma kwa sababu ya tamaa ya mwili. Alizini na kuua mtu (2 Samweli 11:1-27). Mungu
aliokoa Noa toka garika, lakini nyuma yake Noa alishindwa na ulevi (Mwanzo 9:20-21).
Loti alirudi nyuma kwa sababu ya kazi yake. Alitafuta heshima na utajiri katika mji wa So
- domo (Mwanzo 13:7-11; 19:1-28). Watu hawa wote walitubu na kurudi karibu na
Mungu. Walikuwa na upatano mzuri naye tena. Basi kila mwamini wa kweli aliyeacha njia
ya Bwana anaweza kurudi karibu naye vivyo hivyo kama akitubu na kuacha dhambi zake.
14
SURA YA TATU
MBINU ZA UTAFITI
3.1 Utangulizi
Katika sura hii tumefanya uwasilishaji wa mbinu na vifaa vya utafiti ambavyo
wetu. Mbinu za utafiti ni jumla ya kanuni, taratibu, sheria na miongozo ambazo hufuatwa
hatua kwa hatua katika kukamilisha utafiti uliokusudiwa kufanyika (Babbie, 1999). Hivyo,
katika utafiti huu vipengele ambavyo vimetumika ni usanifu wa utafiti, eneo la utafiti,
Mtindo wa utafiti ni kipengele muhimu katika kutoa picha kamili ya namna utafiti
ulivyofanyika tangu mwanzo hadi mwisho. Mtindo wa utafiti ni ramani inayotoa taswira
kamili ya namna utafiti ulivyofanyika tangu katika kukusanya data mpaka kufanya
uchambuzi wa data (Kothari, 2008). Utafiti huu umetumia mbinu ya mbinu ya case study.
Hii ni mbinu ya kuteua eneo moja maalumu ambalo ndilo lililofanyiwa utafiti na kutoa
data ambazo ndizo zimejibu maswali ya utafiti wetu. Hivyo, katika utafiti huu wilaya ya
Wakristo kurudi nyuma kiimani katika makanisa ya Kipentekoste. Mbinu hii ni nzuri kwa
sababu inamfanya mtafiti kutumia muda mfupi na kuweza kupata data nyingi ambazo
15
3.3 Eneo la Utafiti
Eneo la utafiti ni mahali ambapo utafiti umefanyika ili kukusanya data za utafiti kwa lengo
la kukamilisha malengo mahususi ya utafiti (Kothari, 2008). Eneo la utafiti katika utafiti
huu ni Wilaya ya Kigamboni Mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania.. Eneo hili limeteuliwa
Sampuli ni wawakilishi ambao wanateuliwa kutoka katika kundi kubwa la watafitiwa ili
kutoa data ambazo zitawakilisha kundi zima (Robson, 2007). Sampuli ya utafiti huteuliwa
kwa sababu si jambo rahisi kwa mtafiti kuweza kutafiti watafitiwa wote wanaopatikana
katika sehemu au eneo fulani wote kwa ujumla wake na akaweza kukamilisha malengo ya
utafiti wake. Sampuli ya utafiti huu ni jumla ya watu 20 ambao ni washirika 15, viongozi
(Cresswell, 2000). Katika utafiti huu tumetumia mbinu ya usampulishaji lengwa katika
mtafiti huteua sampuli yake akiwa na imani kwamba sampuli hiyo ndiyo inayoweza
kumpatia data za utafiti. Hivyo, mtafiti alikuwa na imani kuwa idadi ya watu 20 iliweza
kumpatia data alizozihitaji na kuweza kukamilisha malengo mahususi ya utafiti wake. Data
zilizokusanywa katika utafiti huu zilihusu kutathmini chanzo cha Wakristo kurudi nyuma
Utafiti huu umekusanya data za aina mbili ambazo ni data za msingi na upili. Lengo la
16
3.5.1 Data za Msingi
hazijawahi kukusanywa na mtafiti mwingine yeyote yule kwa minajili ya utafiti kama huu
uliofanywa na mtafiti huyu wa sasa (Furlong, 1984). Data za msingi kwa jina lingine
hujulikana kama data ghafi yaani data ambazo hazijawahi kufanyiwa kazi. Katika utafiti
Data za upili ni aina ya data ambazo tayari zilikwishakukusanywa na watafiti wengine kwa
ajili ya kukamilisha malengo ya utafiti wao (Yin, 1994). Data hizi hukusanywa kwa lengo
la kujazilishia data za msingi ilikuzifanya zisionekane kuwa mpya kabisa. Data za upili
zinazopatikana katika tovuti na wavuti. Hivyo, data za upili katika utafiti huu zilikusanywa
Data za utafiti huu zilikusanywa kwa kutumia mbinu za upitiaji wa nyaraka, mahojiano,
dodoso na uchunguzi. Mbinu hizi mbili zimewezesha kupatikana kwa data za utafiti kama
Upitiaji wa nyaraka ni mbinu ya kukusanya data za upili ambazo kama ilivyosemwa hapo
kukusanya data kwa mtafiti kutafuta machapisho ambayo yanahusiana na mada ya utafiti
wake na kisha kuyasoma machapisho hayo ili kupata data ambazo alizitumia kushadadia
hoja zinazojitokeza kutoka katika data za msingi (Babbie, 1999). Mbinu hii ni nzuri kwa
17
sababu iliwezesha kupatikana kwa data ambazo ziliusaidia utafiti wetu kutokupwaya kwa
sababu ulipewa misingi imara na data za hizo za upili. Nyaraka zilizopitiwa kupitia mbinu
hii ni tasinifu, vitabu, makala, majarida, magazeti, vipeperushi na makala pepe katika
wavuti na tovuti.
3.6.2 Dodoso
Utafiti ulitumia mfumo wa maswali binafsi ambao ulitumiwa kwa wakristo. Maswali yana
uhalali wa majibu. Kutoka katika njia hii, mtafiti alipata majibu ya maswali aliyoyaandaa.
3.6.3 Mahojiano
Utafiti ulitumia mahojiano ili kupata taarifa kutoka kwa viongozi wa kanisa na mchungaji.
Hii inajumuisha mahojiano ya kina ya ana kwa ana. Maswali kiongozi yamelenga katika
Vifaa vya utafiti ni jumla ya vitu na zana zote ambazo zimetumika katika zoezi zima la
ukusanyaji na uchambuzi wa data za utafiti tangu unaanza mpaka mwisho wa utafiti huo.
Data za utafiti huu zilikusanywa na kuchambuliwa kwa kutumia vifaa mbalimbali kama
ifuatavyo:
Kalamu na Karatasi; kalamu na karatasi ni vifaa muhimu sana katika kusaidia kukamilika
kwa utafiti wa aina yoyote ule uwao. Katika utafiti huu vifaa hivi vilitumika katika
kuchukua madondoo kutoka katika mahojiano na kuyaweka madondoo hayo katika daftari
ambalo ndilo ndani mwake mna makaratasi ya kuandikia. Data hizo zilizokusanywa
18
zilihifadhiwa vizuri katika daftari hilo mpaka wakati wa kuandika andiko la utafiti
ulipofika.
Kompyuta; kifaa hiki kimetumika katika kukusanya na kuchambua data za utafiti kwa
namna mbili. Kwanza kilitumika katika kukusanya data za upili kwa kusoma makala pepe
zinazopatikana katika wavuti na tovuti. Pili, kifaa hiki kilitumika katika kuchapa kazi hii
Simu ya Mkononi; kifaa hiki kilitumika katika kuweka miadi ya kukutana na msimamizi
wangu wa utafiti kwa ajili ya kupatiwa maelekezo ya namna ya kuboresha kazi yangu. Pili,
simu hiyo hiyo ilitumika katika kupewa maelekezo ya moja kwa moja kutoka kwa
msimamizi juu ya namna bora ya kuifanya kazi yangu iwe nzuri na ikamilike kwa wakati.
Wakati mwingine msimamizi alinipigia simu kuniuliza mbona sipeleki kazi yangu kwake
na muda alionipatia wa kufanya marekebisho ukiwa umekwisha. Pia kifaa hiki kilisaidia
kwa namna moja au nyingine kifaa hiki kilitoa msaada mkubwa wa kuweza kukamilisha
data zilizokusanywa ili ziweze kujibu maswali ya utafiti uliokusudiwa. Uchambuzi wa data
ni zoezi lililo na umuhimu mkubwa katika utafiti kwani bila ya uchambuzi wa data ripoti
Kimsingi, zipo mbinu na mikabala mbalimbali ya uchambuzi wa data lakini katika utafiti
huu tulitumia mkabala wa kimaelezo. Huu ni mkabala ambao hutumika kuchambua data za
utafiti kwa kuzitolea maelezo ya kina kwa mwelekeo ambao unasaidia kutimiza lengo kuu
19
la utafiti. Data za utafiti huu ziliwasilishwa kwa njia ya madondoo na kisha kuchambuliwa
kwa madondoo hayo kwa kutolewa maelezo ya kina yaliyoweza kujibu maswali ya utafiti
chuo ambacho kilimsaidia kuendelea na utafiti hasa katika zoezi la ukusanyaji wa taarifau.
Kwa nyongeza, kila swali lilijumuisha barua ya utambulisha ambayo ilihitaji ushirikiano
mahojiano.
20
SURA YA NNE
4.1 Utangulizi
Sura hii inahusu uwasilishaji, uchambuzi na mjadala wa data za utafiti ili kufanikisha lengo
Dhana ya kurudi nyuma: Maneno kurudi nyuma, katika mazingira ya Kikristo, yana maana
ya kuondoka mbali na Kristo badala ya kuenda kwake. Aliyerudi nyuma ni mtu ambaye
anaenda njia mbaya, kiroho. Anadidimia badala ya kuendelea. Aliyerudi nyuma alikuwa
kwa wakati mmoja ameonyesha kujitoa kwa Kristo au aliweka kiwango fulani cha tabia,
lakini hajawahi rejea kwa njia za zamani. Kurudi nyuma kunaweza kujionyesha kwa njia
kadhaa, k.m., kuacha kanisa, kupoteza juhudi katika Bwana, kutembea mbali na huduma
Watu wengine hutumia maneno kurudi nyuma kumaanisha kuwa mtu amepoteza wokovu
wake. Hata hivyo, mtu aliyeokoka ako salama katika Kristo (Yohana 10: 28-29). Mungu
hatatupa watoto wake nje ya familia yake hatutatumia maneno hayo hivyo. Badala yake,
tunapozungumza juu ya kurudi nyuma, tunamaanisha kwamba mtu anazidi kuwa baridi
katika Kristo. Hali ya kurudi nyuma iliyorejeshwa inaweza kuonyesha kwamba mtu
hakuwahi kamwe kuokolewa ili aanze-katika hali hiyo, aliyerudi nyuma anaonyesha tu
rangi zake za kweli. Lakini pia inawezekana kwa watoto wa Mungu kurudi nyuma, kwa
muda.
21
Bibilia inatumia maneno kuanguka mbali badala ya kurudi nyuma, lakini wazo ni sawa.
Katika Bibilia "kuanguka" inaweza kumaanisha mambo mawili tofauti. Katika mfano
mmoja, mtu huyo anaokolewa lakini anapata muda wa kujiuliza maswali ambayo tunaweza
kuiita "mgogoro wa imani." Kwa upande mwingine, mtu huyo hakuwahi kamwe
kuokolewa lakini anajifanya tu kama mtu aliyeokolewa. Tutaita hii kuchukua Ukristo kama
"gari la mtihani."
Katika Marko 14:27 Yesu anawaambia wanafunzi wake, "Ninyi nyote mtaanguka."
imani zao. Ilikuwa usiku wa kosa, usiku wa kuwakumbusha kwao. Lakini hii ilikuwa hali
ya muda. Siku tatu baadaye, Yesu alifufuka kutoka kwa wafu na akaonekana kwa
wanafunzi. Imani na matumaini yao yalirejeshwa, imara zaidi kuliko hapo awali.
nyuma: "Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lolote, ninyi mlio wa Roho mrejesheni
upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe
amepotelea mbali na kweli. . . mtu anapaswa kumleta mtu huyo "(Yakobo 5:19). Aliyerudi
nyuma ametembea kutoka mahali ambapo anapaswa kuwa na ana "kushikamana" katika
dhambi, lakini kanisa litafanya kazi kumrejesha na kumrudisha katika njia ya haki.
Kuna matukio katika maisha, kama kifo cha mpendwa, ambacho kinaweza kutufanya
tuulize Mungu. Hii ni sawa, ili mradi tuende kwa Mungu na maswali hayo badala ya
kuyatumia kama sababu za kuishi katika uasi. Matokeo ya mgogoro wa imani ni mara
nyingi kwamba tunamjua Mungu zaidi kwa karibu kuliko hapo awali. Wakati wa
22
majaribio, tunapaswa kuingia ndani ya Neno, kuomba kwa uvumilivu (Luka 18: 1), na
Tunaona aina nyingine ya "kuanguka" katika Waebrania 6: 4-6 na Luka 8:13. Waebrania 6
inaelezea mpotofu, mtu ambaye "aliwahi onja tu uzuri wa neno" (mstari wa 5) na baadaye
analikataa. Katika Luka 8:13 Yesu anafananisha upotofu na udongo wenye mwamba-
baadhi ya watu huanguka au kurudi nyuma kwa sababu "hawana mizizi." Katika kila fungu
hili, mtu huonekana kwa nje kuwa Mkristo, angalau kwa muda, lakini hajajitolea kwa
Mungu. Mtu kama huyo anaweza kuhudhuria kanisa, kusoma Bibilia yake, kusikiliza
mazuri na urafiki mzuri ambao kuwa karibu na Wakristo hutoa. Lakini moyo wake
Alikuwa amechukua Ukristo kama gari la mtihani na akaamua kuwa hakuwa anunue.
Wokovu huja kwa njia ya kukiri halisi wa Yesu kama Bwana kwa moyo unaoamini katika
kifo cha Yesu na ufufuo (Warumi 10:9-10). Ikiwa mtu aliyeokolewa ya kweli hurudi
nyuma itakuwa ya muda mfupi. Adhabu ya Bwana itamrudisha (angalia Waebrania 12:4-
Ikiwa mtu ambaye hakuwahi okolewa lakini anaweka tu kurudi nyuma ya uzuri-yaani,
anaacha matone na kuonyesha rangi yake ya kweli-hali yake ya mwisho itakuwa mbaya
nyuma kutoka kwa nyingine? Hatuwezi daima, isipokuwa tu kupewa wakati, na hata hivyo
hatujui muda gani Mungu atachukua katika kurejesha aliyerudi nyuma. Mungu pekee
23
Sababu zinazosababisha wakristo kuhamahama makanisa: Wachungaji wengi wanapoona
wangelikaa pamoja nasi.” Huu mstari hauzungumzii watu ambao wanaondoka kanisa moja
kwenda kanisa lingine! Unazungumzia watu ambao kwa nje wanaonekana wamepokea
neema ya wokovu lakini kwa ndani hajapoke! Kwa hiyo tusihukumu kupitia msitari huo.
Hata hivyo ukiachilia mbali kwamba siku hizi watu wamekuwa na masikio ya utafiti, yaani
hawawezi kutulia sehemu moja, ni wazi kwamba kuna sababu zinazosababisha hayo yote
Tangu zamani ni watu wachache sana wanaoenda kanisani pasipo kupitia changamoto
nyingi katika maisha yao. Watu wengi wanaposikiliza mikutano ya injili na jinsi watumishi
wa Mungu wanavyowaahidi kwamba ukimpokea Yesu kristo mambo yako yatakuwa safi.
Sasa mara wanapokaa kanisani kwa muda wa mwaka mmoja wanaona hali zao zinazidi
lingine, haijalishi wewe uko katika kiwango gani, hao bado hawajapata majibu ya maswali
yao au zile ahadi walizoahidiwa siku ya kumpokea Bwana Yesu kuwa Bwana na mwokozi
wa maisha yao. Hili nalo wewe kama mtumishi wa Mungu liweke kwenye kumbukumbu
kwamba lazima ugundue hitaji la mioyo yao na ahadi walizoahidiwa mara ya kwanza ni
zipi.
Watu kujisikia kubadilisha mazingira ya kuabudu: Kuna watu wengine ambao hawapendi
sana. Watu kama hawa nimewaita mimi “wageni ziku zote” kwa maana ya kwamba
24
wanapenda sana kubakia kuwa wageni popote pale wanapokuwa. Ukiangalia kwa undani
zaidi kinachowasumbua watu wa namna hiii ni kwamba wanapenda sana kupokea misaada
mwavuli wa upya wao kujipatia vipato. Kama ambavyo Paulo alimwambia Timotheo kuwa
Udhaifu wa mahali mtu alipokuwa anaabudu unaweza kuchangia mtu kuhamia sehemu
nyingine: Udhaifu ndani ya ibada husababisha watu wengi sana kuhama makanisa na
kuelekea sehemu nyingine ambako roho zao zinaweza kuridhika kumwabudu Mungu. Hata
hivo hoja hii tunaweza kuiweka kwamba; kwa kutegemea na hitaji la mwabudu anaweza
kuhama kanisa kwa sababu anadhani zile ibada za mahali hapo haziendani pamoja naye.
Watu ndani ya makanisa kwa kawaida wako tofauti tofauti. Kuna wengine wanapenda sifa
ya muda mrefu, na kuna wengine wanapenda sifa ya muda mfupi tu. Kuna mwingine
anataka kuomba kwa muda mrefu, na mwingie anataka kwa muda mfupi tu. Kuna
mwingine anataka kuomba kwa sauti kuu na kulia huku kuna mwingine anaona hiyo ni
kero kwake, anaumiza kichwa kwa nini mwenzake anafanya hivyo. Kwa sababu hiyo
ndiyo maana unakuta mtu badala ya kuendelea kugugumia hapo hapo anaamua kuchomoka
Siku hizi kuna ibada za kitume na kinabii, haijulikani imeanzia wapi na imeishia wapi, sasa
kama mtu akihamia kwako na wewe huna wito (kama inavyodaiwa) wa kitume-basi ujue
mtu huyo hawezi kutulia. Vivyo hivyo hata wewe unapokuwa unaenda kwenye kanisa la
kitume (kama inavyodaiwa), huwezi kwenda kuingia viutaratibu vyako hapo. Kaa tulina!
Mwabudu Mungu kwa uzuri wake. Taratibu za ibada zote zimeandaliwa kwa lengo la
kuwaongoza watu wamwabudu Mungu katika hali ya uzuri na utakatifu, sidhani kama
25
kuna kanisa ambalo huandaa utaratibu unaoenda kinyume na matakwa ya waabuduo.
Nia Ya Kutafuta Uongozi Ndani ya Makanisa: Kama tujuavyo kwamba kanisa linakuwa na
uongozi, na ule uongozi ni watu ndio wanaowachagua. kama mtu alienda kwenye kanisa
fulani kwa nia ya kupata uongozi, anapokuwa hajapewa uongozi alioutaka, ni dhahiri
kwamba atahama tu. Tangu zamani hata tunaposoma historia tunaona kwamba watu
Kwamba, nia ya watu wa namna hii ni kuongoza na wala siyo kuongozwa, kwa kifupi wao
hawana karama ya kuongozwa (kama ipo) na wala hawajawahi kuota ndoto ya kuongozwa
hata siku moja. Wao wakikaa katika kanisa kazi yao kubwa ni kukosoa uongozi uliopo
wakati mwingine inatokeaa kwamba makanisa mengine labda yanatumia vyombo vya
mziki, ilhali katika kanisa lako bado unategemea mikono tu au wenzio wanatangaza
kwenye runinga, wewe hujui hata hiyo runinga ikoje. Sasa mtu anapokutana na watu wa
kundi fulani huanza kuelezea mafanikio ya kanisa lao, naye hushawishika kabisa na
kujiona kwamba ile sehemu anayosali siyo salama kabisa. Kuna wengine hutumia
anamweleza kwamba “unajua mchungaji wetu yuko hivi na hivi” sasa mtu huyu
anapolinganisha anamwona mchungaji wake hana hizo sifa, basi huamua kuhama kabisa.
Kukosa ushirikiano katika kanisa jipya ambalo amehamia: Watu huondoka kanisa wakati
wanapokosa ushirikiano ndani ya kanisa husika. Hii ni moja ya sababu ambayo inaweza
kutumika kama sababu ya watu kuja kanisani lakini pia wakati huo huo ikawa sababu ya
watu kuondoka.
26
Mafundisho fulani fulani: Mojawapo ya sababu ya kuwepo kwa madhehebu mengi ni
tofauti za kimafundisho ndani ya kanisa. Kwa hiyo siku hizi ni vigumu sana
kuwaunganisha watu wakawa kitu kimoja kwa sababu kuna tofauti katika mafundisho,
ingawa wakati mwingine tofauti hizo zinaweza kutatuliwa na kutatua changamoto kadhaa
wangine ambao kwa asili ni watata tu, yaani wao hawaelewani na watumishi jirani na
makanisa yao. Watu wanapokuja kusali kwako wakati mwingine siyo kwamba kule
walikuwa wamehama, lakini kwa sababu wewe huna mahubiri zaidi ya kuwasema
watumishi wengine tu, hii inakujengea chuki wewe na waumini wa kanisa hilo.
Waumini wanapoona kwamba ninyi wenyewe hamuelewani, wao huchukua huo mwanya
kupenya na kwenda kwenye makanisa mengine. Hivi mchungaji unajua kwamba hiyo kazi
unayofanya ni kazi kubwa sana mbele za Mungu ambayo kwayo unapaswa kusimama
Kutokujua nini maana ya kuokoka: Ama kwa kushindwa kufundishwa vizuri, ama kwa
sababu ya uzembe wao wenyewe, kuna wakristo ambao mpaka leo hawajui maana ya
wokovu nini katika maisha yao. Wanadhani kwamba wanapokuwa wameokoka shida na
Kushindwa Kutimiza Vigezo vya Kanisa Husika: Siku hizi watu wanapenda sana kujua
mkazo wa kanisa husika. Ni jambo la muhimu sana kwa sababu bila kujua mafundisho ya
msingi ya kanisa husika watu watu huingia katika matatizo makubwa. Lakini huja yangu
hapa ni kwamba kuna waumini mbalimbali ambao huhamia makanisa fulani tu kwa sababu
27
Wachungaji kushindwa kuona upande wa waumini wao: Kumekuwepo na kasumba ya
wachungaji kusubiri waumini waje kanisani bila kujua kile ambacho kwa wiki nzima
aina mbalimbali kuhodhi muda wa waumini wao kwa kigezo cha kwamba wanamtumikia
Mungu. Unaweza kushangaa watu wanakuja kanisani kuanzia saa kumi na mbili asubuhi
mpaka saa kumi na mbili jioni. Halafu kesho yake tena alfajiri kuna ibada ya maombi kila
siku, halafu pia mtu huyohuyo anapaswa kwenda kufanya kazini kila siku. Sasa watu
kuhamia makanisa mengine. Kuwepo na ratiba za ibada kila siku ni vizuri sana lakini
Ubinafsi wa Waumini: Mojawapo ya tatizo kubwa ambalo linakabili kanisa kwa leo ni
ubinafsi wa waumini kanisani. Watu wengi hushindwa kukaa katika kanisa moja na
kuendelea kuzunguka makanisani kwa sababu mioyo yao imejaa ubinafsi na hawataki
Kikristo ni maisha ya ushirikiano na uhusiano. Mtu anapokuwa amekaa katika kanisa moja
matokeo. Kwa sababu hiyo watu wengine wamekuwa wakihama makanisa kwa sababu ya
matoleo zaidi ya saba, na kila matoleo hayo unapaswa kutoa; kwa mfano unapaswa kutoa
28
kwaya, ununuzi wa vyombo, pamoja na michango mingine midogomidogo. Nakumbuka
kanisa langu la zamani, viongozi wa ibada walikuwa wanatumia muda wa zaidi ya masaa
mawili wakiomba michango ndani ya ibada. Tena wengine mpaka wanafanya na minada
kanisani kwa ajili ya kuuza vitu. Hivyo basi, kuna wakati mwingine watu wanahama
makanisa kwa sababu ya kuogopa kwamba watatoa nini kwenye ibada. Wanaogopa
Unadhifu ndani ya kanisa: Kuna watu wengine ambao huhama makanisa kwa sababu ya
unadhifu ulio ndani ya kanisa hilo. Hapa ninaamisha kwamba kuna wakati mtu anaingia
kanisani anakuta watu wote wamevaa nguo za maana (suti na nguo za gharama kubwa).
Halafu wakati huo yeye akijiangalia amevaa mitumba ambayo gharama yake haizidi elfu
tano. Moja kwa moja mtu wa namna hii anakata tamaa ya kuingia ndani ya kanisa hilo na
kuendelea kusali hapo. Mara kwa mara huduma yangu imekuwa ikishutumiwa kwa kuwa
na watu wanaovaa nguo za gharama kubwa na kusababisha watu wengine kuogopa kuingia
ndani ya kanisa. Kuna siku niliwahi kuwaambia kwamba ni lazima waangalie mavazi yao
ili yasiwazuie wengine kuingia ndani ya kanisa kwa hofu ya kusemwa vibaya.
Majungu ndani ya Kanisa: Watu wengi sana wamekuwa wakihama makanisa kwa sababu
na majungu ndani ya kanisa wanalosali. Ingawa kwa kweli sababu hii inawalenga hasa
Wakristo wachanga ambao bado hawana mizizi ya neno, lakini ni muhimu kuijua.
mwenzake sehemu nyingine bila kibali chake. Jambo analosemwa huyo mtu si lazima liwe
na uongo, hata kama ni la ukweli lakini kwa sababu hakuna kibali kutoka kwake kwamba
29
Madhara ya majungu ni kuagamiza ushirika kati ya muumini mmoja na mwingine na
mwishowe watu kuamua kutengana. Nadhani kitu kinachoweza kuharibu mwili wa Kristo
kuliko vitu vingine vyote ni uvumi wa majungu. Majungu husabababisha watu waanze
huleta uchonganishi ndani ya kanisa na kuwafanya watu waishi kwa hofu. Biblia inasema
karibu" (Mithali 16:28). Kama kanisa, tunahitaji kuwa makini sana na maneno kutoka
upande fulani fulani. Tusiwe wepesi wa kuyashabikia maneno hayo. Hata hivyo kumbuka
hufunua hali ya mioyo yao. Maneno yaliyosemwa yana nguvu sama. Maisha na kifo
vinaweza kuamuliwa kwa maneno yetu. Maneno pia yanaelezwa kama silaha na mishale
(Zaburi 57:4, 64:3, Yer 9:8). Yakobo anaelezea uwezo wa ulimi kama mwendo wa meli au
Dhambi za Watumishi: Ama kwa hakika hakuna mtu asiyetenda dhambi hapa duniani!
Kila mtu anaamini hilo kwa sababu ya anguko la mwanadamu pale Edeni. Dhana hii ya
dhambi haipo miongoni mwa waumini kwamba mchungaji au mama mchungaji anaweza
kutenda dhambi. Ikitokea kwamba mmojawapo kati ya watu hawa amefanya dhambi, basi
watu huwa wanakata tamaa kabisa na kuamua kuhamia kwenye makanisa mengine
suala la dhambi basi, lazima tujiangalie mara mbili mbili. Ninaamini kwamba dhambi zote
ni sawasawa mbele za Mungu lakini naamini kwamba kuna dhambi moja ambayo
mchungaji akiifanya kwa namna yoyote ile watu hawawezi kumsamehe na kumruhusu
kuendelea kuwa mchungaji wao! Dhambi hiyo ni “uzinzi.” Mchungaji ukifanya uzinzi
30
kanisani na watu wakajua, hata kama ukiwaeleza na kuomba msamaha hawawezi kukubali
kubaki na wewe. Kwa hiyo ni lazima kuwa makini sana. Mchungaji Lee Jae Chul
alipoulizwa kuhusu suala la uzinzi kwa watumishi wa Mungu alisema alisema hafikirii
kama kuna mtumishi wa Mungu anaweza kufanya hivyo. Yule aliyemuuliza swali alimpa
mfano wa mfalme Daudi aliyezidi na Bathsheba, yeye alijibu kwamba “Daudi alikuwa
huwa tunashindwa kujitathimini utumishi wetu. Kuna wakati mwingine tunatumika kwa
mazoea mazoea tu. Unakuta mchungaji maisha yake hayana tofauti na watu wa kawaida.
Ninamkumbuka mhubiri mmoja aliwahi kusema “mchungaji siyo mtu.” Katika ufafanuzi
wake walisema kuwa mchungaji lazima ajitofautishe na watu wa kawaida. Kanisa haliwezi
kukua zaidi ya mchungaji alivyo. Kama mchungaji ni dhaifu kanisa lazima litakuwa
dhaifu. Watu wengi hawapendi kuona mchungaji wao akiwa dhaifu. Udhaifu tunaousema
Jinsi ya kudumu katika Imani bila kuhamahama: Yesu anasema nasi, “kaeni ndani yangu
nami ndani yenu” ambapo tunaona mawili, Yesu kukaa ndani yetu na sisi kukaa ndani ya
Yesu. Katika sehemu iliyopita tumeona Yesu kukaa ndani yako, kwamba ni kumpokea
Yesu ndani ya moyo wako; yaani “kuokoka”. Leo tunaona Yesu kukaa ndani yako; yaani
“maisha ya wokovu”.
ndiyo kuishi katika wokovu. Kwa hiyo ukiweza kuishi kwa kuzishika mari za Yesu
Yesu anakuwa ameingia ndani yako na sasa tunakwenda kujifunza maisha katika wokovu
ambayo kwa lugha nyingine tunaita kukaa ndani ya Yesu. Maisha ya wokovu ni maisha ya
31
hapa duniani tangu mwanadamu anapookoka hadi atakapokufa (hatima ya maisha ya
Baba katika ufalme wake Mbinguni. “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia
sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye
pamoja nami. Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi,
kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha
enzi” (Ufunuo 3:20-21).
Bwana Yesu ni wa kwanza, anabisha hodi, ukifungua mlango (ukimruhusu aingie) yaani
ukimwamini na kumkiri… anaingia ndani yako na kufanya makao. Atakula pamoja nawe,
nawe pamoja Naye (kila utakachokuwa unafanya, atakuwa pamoja nawe), katika mawazo
yako yupo nawe, katika matendo yako yupo nawe, na kila sehemu utakapokuwepo Yeye
yupo nawe. Akiisha ingia kwako inakupasa nawe ukae ndani yake, yaani uyaishi maisha ya
Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa,
ili azivunje kazi za Ibilisi. Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu
uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa
kutokana na Mungu. Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao.
Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.” 1
Yohana. 3:8-10
Yesu akikaa ndani yako nawe unapokaa ndani ya Yesu, unakuwa umeruhusu utatu wote
utakao tembea ni mtembeo wa kimbingu, maana akikaa ndani yako anayeishi sasa siyo
wewe bali yeye aliye ndani yako na laiye ndani yako ni ufalme wote wa Mbinguni. Biblia
32
wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilionao sasa katika mwili ninao
tena katika imani ya mwana wa Mungu, ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwaajili
yangu.”
Mungu. Mungu wetu ni mtakatifu, kwa hiyo watoto wake waliozaliwa naye wanapaswa
kuwa watakatifu. “…Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao
wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na
Mungu…”
dhambi. Na kwasababu umeshatolewa kwenye ule utu wa kale, yaani kuishi kimwili na
ukawa mfu kimwili na kuanza kuishi kiroho, vivyo hivyo unapaswa uenende kwa namna
ya rohoni. Paulo katika waraka wake wa pili kwa Timotheo anasema “nimevipiga vita
sasa, maisha ya wokovu ni maisha ya vita. Vita ni mapambano. Siyo maisha ya starehe na
raha, bali ni maisha ya kusimama imara. Shetani kila kukicha anapambana kuiteka Imani
yetu, sisi tunapaswa kuilinda hii Imani. Haya maisha ya wokovu ni maisha ya utakatifu.
Mtu anapookoka anakuwa mtakatifu (bila dhambi) na hivyo baada ya kuokoka mtu
anapaswa kupambana kuishi katika utakatifu, na haya ndiyo maisha katika wokovu. “Basi
kama mlivyompokea Kristo Yesu, Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye; wenye shina
na wenye kujengwa katika yeye; mmefanywa imara kwa imani, kama mlivyofundishwa;
mkizidi kutoa shukrani. Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na
33
Neno la Mungu: Ili kuishi maisha ya wokovu kwa ushindi unapaswa kusoma, kulishika na
kulifuata neno la Mungu. Biblia inasema “ni kwa jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa
lenye pumzi ya Mungu linafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na
kwa kuwaongoza na kuwaadibisha katika haki… ili mtu wa Mungu awe kamili, aweze
Silaha yetu kubwa katika hiyo vita ni neno la Mungu. Biblia inasem ahivi “Neno la mungu
li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena
lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena
wa Nuni alipokabidhiwa kundi la wana wa Israel alifikishe nchi ya ahadi, alipewa maagizo
na Mungu. Aliambiwa, “kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari
yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapofanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi
sana”. Baada ya kufuata masharti hayo, Yoshua alikuja kuwa na mafanikio sana na ushindi
mno. Tumesoma kuwa alivuka maji ya mto Jordan na pia aliangusha ukuta wa Jeriko na
kuiteka miji yote ng’ambo ya Jordan. Hatimaye Yoshua anasema, “Mimi na nyumba yangu
tutamtumikia Bwana Mungu wetu, nyinyi chagueni hii leo mtakaye mtumikia” kwa maana
ameiona siri ya ushindi alionao utokanao na Neno kukaa ndani yake. Neno la Mungu
likikaa ndani yako, utaishi maisha wokovu kwa ushindi siku zote. Utayaishi maisha ya
kuzimia moyo. Hatimaye utaurithi ule uzima wa milele ambayo ndiyo ahadi
tunayoishindania.
34
Roho mtakatifu: Ili kuishi kwa ushindi maisha ya wokovu, tunahitaji sana msaada wa Roho
mtakatifu. Biblia inasema Basi nasema, “enendeni kwa Roho, wala hutazitimiza kamwe
na Roho mtakatifu hampo chini ya sharia tena… ukisoma Yohana 14:25. Roho mtakatifu
kulisoma Neno kila mara, kuliweka ndani yako Neno na kulitenda Neno; Roho mtakatifu
Yesu alikosa kuwa na ujasiri kuenenda na kukiri wokovu hata akamkana Yesu mara tatu…
Lakini alipokuwa pamoja na kanisa la kwanza pale ghorofani Jerusalem, Roho mtakatifu
alishuka na kuwajaza wote wakanena kwa lugha nyingine… Petro alipata ujasiri mkubwa
Maombi: Maombi ni silaha nzito sana ili tuwe na ushindi katika maisha yetu ya wokovu.
Maombi hupenya pasipopenya silaha yoyote ile. Maombi ni silaha katika ulimwengu wa
kiroho. Shetani anapambana nasi kila saa ili sisi tushindwe kuishi maisha ya wokovu.
Biblia inasema, “kesheni mkiomba, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi lakini mwili ni
dhaifu”, Mathayo. 25:41; Efeso 6:18, “Kwa sala zote na maombi, mkisali kila wakati
katika Roho, mkikesha katika jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote”
Mungu kila wakati. Katika maisha ya wokovu maombi yanatufanya kuzidi kukaa katika
ulimwengu wa roho na kuishi kiroho. Ndiyo maana Bwana Yesu alitusihi kukesha katika
wakajaa Roho mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri”, Matendo. 4:31. Pia Biblia
inasema, “…huu ndiyo ujasiri tulionao, tukiomba kitu chochote katika mapenzi yake
atusikia, kama tunajua atusikia basi tunazo zile haja tumwombazo…” (1Yohana 5:13-15).
Kusanyiko/Kanisa: Ili tuwe na ushindi katika maisha ya wokovu, ni muhimu sana kuwa
kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao”, Mathayo 18:20 Bwana Yesu
alipowatuma wanafunzi wake kwenda kuhubiri injili, aliwapanga wawili wawili na siyo
mmoja mmoja. Biblia inasema “Basi baada ya hayo, Bwana Yesu aliweka na wengine
sabini, akawatuma wawili wawili waende kila mji na kila mahala alipokusudia kwenda
Aliwatuma wawili wawili kwasababu kila walipo wawili watatu au shirika kwa jina lake
Tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri. Wala tusiache
kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya
hivyo, kwa kadri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia” (Waebrania 10:24-25), pia ukisoma
Yakobo. 5:16. Biblia inasema “ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana
Yerusalem walipoomba kwa bidii ndipo Roho mtakatifu alishuka, wanafunzi na kanisa la
kwanza wakaanza kunena kwa lugha mbalimbali. Mungu alishuka kwa nguvu kubwa sana.
36
Kuwepo katika ushirika kwa jina la Mungu kunakufanya kukaa katika uwepo wa Mungu
37
SURA YA TANO
HITIMISHO NA MAPENDEKEZO
5.1 Utangulizi
Sura hii inatoa hitimisho na mapendekezo ya utafiti mzima. Sura hii inatoa ufupisho wa
mambo yote muhimu yaliyowasilishwa katika utafiti huu ili mtu anaposoma sura hii
5.2 Hitimisho
Utafiti huu umegundua kwamba Wakristo wanarudi nyuma kiimani kwasababu mbalimbali
ndio wale ambao wasikiapo hulipokea lile neno kwa furaha; nao hawana mizizi, huamini
anapaswa kusimama mwenyewe haijalishi hata kama mtu aliyekuingiza katika ukristo
amehama imani na kujiunga na imani potofu, yeye anaendelea kusimama kwa gharama
yoyote, wazazi ndugu jamaa au rafiki wa karibu hawezi kubadilisha msimamo wa mtu
mwenye mizizi, utashangaa kuona mtu aliyeokoka hajui hata tofauti ya Mashahidi wa
Yehova na hata wasabato yeye kila aina ya fundisho na imani na kila aina ya upepo wa
Elimu unamzoa tu. Mkristo mwenye mizizi kamwe hawezi kuyumbishwa na jaribu la aina
yoyote,taarifa mbaya kuhusu kiongozi wako wa kidini haiwezi kuwa sababu yaw ewe
kuiacha imani, unaweza kuwepo kanisani lakini kama mimani yako haijajengwa kwenye
misingi na haijaota mizizi ni rahisi kujikuta matatani, Dhambi za kiongozi wako wa kidini
kwa sababu ya dhambi ya kiongozi wako?mkristo anayeweza kumuacha Yesu kwa sababu
ya tatizo la mtumwingine huyo hana misingi wala hajaota mizizi hajakomaa. Mkristo
aliyesimama vema ni yule ambaye amesimama hawezi kutikiswa na kurudi nyuma kwa
Ninyi nanyi mwataka kuondoka? Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani?
Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe
kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.” Mkristo ambaye ni debe
tupu ana maisha hatarishi shetani atatafuta kila namna ili aweze kuhakikisha kuwa
namna ya udunia ambayo hujawahi hata kuwa nayo kwa sababu, huna kitu, lazima mkristo
huu wa sasa, akasafiri kwenda Thesalonike; Kreske amekwenda Galatia; Tito amekwenda
Dalmatia.” Kama mtu akikipenda kitu uko uwezekano mkubwa wa kukifuata, Dema
akimpenda kijana anaaacha wazazi wake na kuambatana na yule kijana kupenda kuna enda
Uchungu: Waebrania 12: 14-15 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo
utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; mkiangalia sana mtu
Maisha ya dhambi: Wakristo wanaoishi katika maisha ya dhambi pia hawawezi kufurahia
kanisa ambalo linakaza kukataza dhambi, hawawezi kujisikia salama kuweko mahali
39
hawataki kukemewa wanahitaji jumbe za kuwatia moyo tu ukianza kunyoosha
Uongo: Uwongo ni dhambi, watu wengi sana hujifunza kusema uongo tangu utoto,
damu. Wakaenda nayo ile kanzu ndefu, wakamletea baba yao, wakasema, Tumeona hii;
basi, utambue kama kanzu hii ni ya mwanao, ama siyo. Akaitambua, akasema, Ndiyo
wakati wote vikundi vya aina hii vinavyopigana na serikali kwa sababu ya madai kadhaa
kama mfano hapa Afrika vimepewa jina la waasi, Hali kadhalika watu waliomtii Mungu
huitwa wana wa kutii na kinyume chake watu wanaomuasi Mungu huitwa wana wa
kuasi (1Petro 1:14).
Uzembe/ ujinga/upumbavu: Biblia ina maneno magumu sana kwa mtu aliyerudi nyuma
anu kudumaa kiroho, hakuna maneno ya kutia moyo kwa mkristo anayemuacha Yesu,
watu wengi sana wanapoishi maisha ya dhambi hujifikiri kuwa wao ni wajanja lakini biblia
inamuita mtu anayerudi nyuma kama mjinga na mpumbavu mimi naita uzembe, Mithali 1:
32.
5.3 Mapendekezo
Utafiti huu umetathmini kutathmini chanzo cha Wakristo kurudi nyuma kiimani katika
40
namna moja ama nyingine, kama yatazingatiwa yatasaidia kanisa. Kwa hiyo imetupasa
kuyaangilia zaidi ya hayo yaliosikiwa tusije tukayakosa. Kwa maana ikiwa lile neno
lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa uasi ulipata ujira wa haki, sisi je!
Tutapataje kupona tusipojali wokovu mkuu namna hii? (Waebrania 2:1-3). Kuna mifano ya
kibiblia ya makanisa ya mara moja yenye nguvu ambayo yalimalizikia kwa kurudi nyuma.
Katika Ufunuo, tunasoma juu ya kanisa la Efeso likiumiza Kristo kwa kujiweka mbali na
upendo wao wa kwanza (Ufunuo 2:4). Vilevile, kanisa la Laodikia liliporudi nyuma kwa
kujiweka katika hali ya joto (3:15), na kanisa la Sarde likageuka kifo cha kiroho (3:2).
msalaba wa Kristo na walikuwa wamegeuka nyuma kwa kazi za mwili (tazama Wagalatia
1:6-7).
Paulo anaonya hivi, "Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na
hekima bali kama watu wenye hekima" (Waefeso 5:15). Unawezaje kujilinda dhidi ya
kuludi nyuma kutoka kwa Kristo na kukataa "wokovu mkubwa"? Paulo anatuambia
"tujali" kwa mambo tuliyoyasikia. Kusoma kasi kwa njia ya Neno la Mungu kunaweza
kuwa na hisia moja ya kufanikiwa, lakini jambo muhimu zaidi ni kwamba "kusikia" yale
unayosoma na masikio ya kiroho. Fikiria juu ya Neno ili ulisikie moyoni mwako.
Paulo anasema, "Jitathmini wenyewe kwamba mmekuwa katika imani. Jaribu mwenyewe.
Je, hamjui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu?" (2 Wakorintho 13:5).
katika imani. Kwa hiyo kwa kuhitimisha utafiti huu mapendekezo yaliyotolewa
yanatokana na mtazamo wa mtafiti. Hii inamaanisha mtu mwingine aweza kuona tofauti,
41
MAREJEO
Bible Society of Kenya. (1992). Biblia. Habari Njema. Nairobi: Bible Society of Kenya.
Bible Society of Tanzania. (1997). Biblia. Maandiko Matakatifu. Dodoma: Bible Society
of Tanzania.
Kothari, C. R. (2008). Reserch Methodogy: Methods and Techiniques, New Delhi: New
Yin, R. K., (1994). Case Study Research: Design and Methods, (2 nd eds.) Thousand Oaks
42
VIAMBATANISHO
Naitwa Annie Oscar Bwanali, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha New Life Outreach
Maendeleo ya Jamii. Hojaji hii ina maana ya kujazwa na wahojiwa. Ninatarajia ushirikiano
wako, pia, majibu yako yatahifadhiwa kwa siri na yatatumika hasa kwa kusudi moja la
2. Jina la Kanisa.........................................................................................
Ndiyo ( ) Hapana ( )
43