Professional Documents
Culture Documents
#0008.ahadi Za Mungu
#0008.ahadi Za Mungu
#0008
2 Wakorintho 1:20
[20]Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin;
Mungu apate kutukuzwa kwa sisi.
#1Ahadi zote za Mungu ziko ndani ya Kristo Yesu. Huwezi kupokea ahadi ya Mungu Nje ya Kristo Yesu.
Mtu ambaye hajampokea Kristo hawezi kupokea ahadi yeyote ya Mungu “ Uponyaji, kufunguliwa,
Amani, Furaha, Mafanikio ”
Kwahiyo haujamwamini Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa Maisha yako hauna kigezo chochote cha
kupokea ahadi za Mungu.
Ndio maana sio sawa Mtu kupokea Uponyaji halafu ukamkataa Yesu. Lazima kwanza Akubali kuwa
Yesu ni Bwana !
Maana yake chochote alichokisema Mungu unapaswa kukipokea kama Mtoto MCHANGA, bila maswali
na wasiwasi na mashaka.
maana yake Chochote anachosema Mungu kwa habari za maisha yako ni NDIYO
Unapaswa kuwa na jibu Moja tu
“ NDIO BWANA ”
Hupaswi kuwa na maswali, wala haupaswi kuingiza Elimu yako ya Darasani na Ya kimaisha
Mungu akisema
“ Ndiyo Bwana Ninaamini kabisa bila maswali - Kuwa Sipaswi kuwa mgonjwa, kwasababu
umeyachukua Magonjwa yangu ili mimi nisiwe nayo ”
Neno la Mungu
liko juu Sana sana sana ya ELIMU YA DARASANI. Elimu ya Darasani ni elimu ya chini sana
kulingamisha na Neno la Mungu. Hiyo ni mitizamo ya Watu kwa kutumia akili zao za kibinadamu
wanajaribu kubashiri masuluhisho ya matatizo fulani.
Ahadi za Mungu sio kwa ajili ya wachungaji, Waalimu, Wainjilisti na Mitume. Ahadi za Mungu ziko
ndani ya Kristo Yesu, na Kama Mtu amemwanini Yesu kama Bwana Na Mwokozi wa maisha yake Ahadi
za Mungu ziko kwa ajili yake, na zinapaswa kutimia katika maisha yake.
unapoiona Ahadi ya Mungu juu ya Afya au Uchumi, au Ndo “ Unapaswa kusema na iwe kwa kwangu ”
bila maswali- ukijua ndivyo Mungu anavyotaka iwe.
Isaya 1:19
Kwahiyo Ahadi za Mungu ziko kwa ajili yako na zinapaswa kutimia kwenye maisha yako, na kwahizo
uungu utaanza kudhihirika kwenye maisha yako.
watu wengi wamekubali Elimu ya dunia na Akili zao ndogo walizonazo kwa habari ya maisha, na
wameziacha ahadi za Mungu ambazo tayari ziko ndani yao ambazo zitawapelekea kuishi maisha huru
kabisa.
Tambua kwamba ziko tayari kwa ajili yako kwasababu zimekamilika ndani ya Kristo Yesu
harrisonhumphrey25@gmail.com
Ubarikiwe sana Na nakuomba unisaidie kuishare kwa marafiki zako ili na wao wajifunze Neno la Mungu