Download as docx, pdf, or txt
Download as docx, pdf, or txt
You are on page 1of 2

Y9 lesson 2 zoezi

Zoezi

PAA NA BUIBUI

SIKU moja baba na mama yake Juma waliuchoma moto msitu uliokuwa karibu na nyumba yao.
Buibui mmoja akamwambia paa, 'Tafadhali, rafiki yangu, nichukue juu ya pembe zako ili
msiteketee katika moto huu. Siku moja na mimi nitakusaidia vile vile; watu wamesema,
'Ukimfaa mwenzio kwa jua, naye atakufaa kwa mvua.''

Paa akamwambia, ' Ha, ha, ha, mdudu mdogo kama wewe utawezaje kunisaidia mnyama
mkubwa na mwenye nguvu kama mimi ? Unanidanganya tu.' Lakini halafu paa akakubali
kumchukua juu ya pembe yake.
Baadaye Ali na Mwangi, wawindaji, wakaja katika msitu ule. Paa alikuwa amejificha kwa mbali
kidogo. Mara Ali akaona alama za nyayo za paa. Akamwambia Mwangi, 'Mwangi eh, naona
mwanzo wa alama za nyayo za paa ; hayuko mbali.'
Buibui akasema, ' Sasa wakati wa kukulipa fadhili zako umefika, Bwana Paa.' Basi buibui
akauzungusha uzi mahali pale alipokuwapo paa. Kisha akauzungusha mwingine juu ya zile
alama za nyayo zilizokuwa karibu na paa. Ali na Mwangi walipoona ule uzi, wakasema, ' Ah,
bila shaka amepitia njia nyingine.' Basi wakaenda zao moja kwa moja bila ya kuzidi kumtafuta
paa yule.

Basi kama wenzetu wakitusaidia wakati wa shida au dhiki, nasi hatuna budi kuwasaidia
wapatwapo na mambo kama hayo. Wadogo nao huweza kuwasaidia wakubwa.

MAZOEZI

I. Jibu maswali haya:


1. Baba na mama yake Juma walifanya nini ?

Baba na mama yake Juma waliuchoma moto msitu uliokuwa karibu na nyumba yao.

2. Buibui alimwambia nini paa ?

Akamwambia amchukue kwenye pembe zake ili asiungue kwa moto.

3. Paa alijibuje ?

Yeye akacheka na kusema, vipi mdudu mdogo kama unamlinda mnyama mkubwa kama
mimi.
4. Ali na Mwangi walikuwa watu gani ? Walifanyaje?

Ali na Mwangi walikuwa wawindaji na waliona nyayo za paa.

5. Eleza jinsi paa alivyookoka katika hatari ya kuuawa na Ali na Mwangi.

Buibui akauzungusha uzi mahali pale alipokuwapo paa. Kisha akauzungusha mwingine
juu ya zile alama za nyayo zilizokuwa karibu na paa.

IV. Andika majina ya wazee wako, rafiki zako na miji minne yoyote. Tunga sentensi utumie
majina hayo.

Wazazi wangu na mimi tunapanga kutembelea Paris, Singapore, London na Rome.

V. Andika sentensi utumie majina ya wanyama wenye pembe tu katika hawa wafuatao:

sungura, kifaru, mbwa, simba, paa, twiga, ndovu, punda. mbuzi.

vifaru, paa na mbuzi wana pembe.

VI. Badala ya kila mstari, andika neno litakalokamilisha sentensi hizi:

asali, ndovu, buibui, mishale, wadogo, wawindaji, moto, shimo, sumu, maziwa.
1. Ali na Mwangi walikuwa wawindaji hodari.

2. Sungura alitumbukia ndani ya shimo.

3. sumu ya nyoka yule ni kali sana.

4. Koka moto tuchome nyama yetu.

5. wadogo huwezi kuwasaidia wakubwa.

6. Ng’ombe hutupa maziwa.

7. buibui ni mdudu tu.

8. Nitakupa asaliya nyuki.

9. Wawindaji walivunja mishale yao.

10. ndovu ana pembe kubwa mbili.

You might also like