Professional Documents
Culture Documents
UCHAMBUZI WA KITABU Mindset Saikolojia Mpya Ya Mafanikio - Sehemu
UCHAMBUZI WA KITABU Mindset Saikolojia Mpya Ya Mafanikio - Sehemu
UCHAMBUZI WA KITABU Mindset Saikolojia Mpya Ya Mafanikio - Sehemu
ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Hivyo picha ambayo imekuwa inaonekana kwenye michezo ni hii, wale wenye
vipaji vikubwa wamekuwa wanaishia kuwa kawaida, huku wanaoanza bila
vipaji wakifanya makubwa. Kwa wengi kuanza na kipaji kunakuwa kikwazo cha
kufikia mafanikio makubwa, yote ni kwa sababu ya mtazamo mgando ambao
wenye vipaji wanakuwa nao.
Wale wenye vipaji, kwa kudanganywa na ukuu ambao vipaji hivyo vinawapa
wamekuwa hawaoni umuhimu wa kuweka kazi kujiendeleza ili waweze
kufanikiwa na hilo ndiyo linawazuia kufanikiwa.
Mtazamo na tabia.
Athari ya mtazamo kwenye mafanikio ya michezo inatokana na tabia ambayo
mchezaji anakuwa amejijengea.
Tabia ndiyo inayowatofautisha wale wanaofanikiwa na baadaye kushindwa na
wale wanaofanikiwa na kubaki kwenye ushindi huo.
Kwenye michezo, hata wale wenye vipaji na wasioweka juhudi kwenye
kujiendeleza, kuna wakati vipaji vyao huwawezesha kushinda, lakini huwa
hawadumu kwenye ushindi huo.
Iko hivi, kila mchezaji kuna wakati huwa anakutana na ugumu. Hata mchezaji
mwenye mafanikio makubwa kiasi gani, huwa hapati ushindi kwenye kila
mchezo.
Kila mchezaji huwa anashindwa kwenye baadhi ya mashindano, kushinda huko
ndiyo kunakowatofautisha wale wanaofikia mafanikio makubwa na kudumu
nayo na wale wanaopotea.
Wale wanaoanza wakiwa na vipaji na kuwa na mtazamo mgando,
wanaposhindwa kwenye shindano moja, huwa wanajiona hawawezi tena,
wanakata tamaa na hawaweki tena juhudi kwenye mashindano mengine.
Wale wanaoanza bila ya vipaji na wenye mtazamo wa ukuaji, wanaposhindwa
kwenye shindano moja, wanajifunza makosa waliyofanya na wanaenda
kufanya mazoezi zaidi ili waweze kushinda mashindano yanayofuatia.
Wachezaji wengi wanaofanikiwa wamekuwa wakieleza kilichowawezesha
kufanikiwa ni uimara wa akili zao, kuweza kuendelea kujisukuma licha ya
kukutana na ugumu ambao uliwaangusha na kuwakatisha tamaa wengine.
Wachezaji wote wanaofikia ushindi wa juu, wanajua kabisa kwamba
hawajazaliwa na uwezo wa kipekee kwenye michezo yao, wanajua juhudi
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Ushindi ni mchakato.
Wale wanaofikia ushindi kwenye michezo na kubaki kwenye kilele cha ushindi
kwa muda mrefu wamekuwa wanajua kitu kimoja muhimu, ushindi ni
mchakato na siyo tukio.
Hivyo huwa wanaumiliki mchakato wa wao kufika na kubaki kwenye kilele cha
ushindi. Hilo ndiyo limekuwa linawawezesha wengi kubaki kwenye kilele cha
mafanikio kwa muda mrefu, licha ya umri wao kwenda.
Ni kwa sababu wanaujua mchakato na kuufuata kila wakati, bila ya kujisahau
kwa kuona mafanikio yao yanawapa nafasi fulani.
Kinachowafanya waufuate mchakato ni kwa sababu wanaufurahia. Wengine
wanapowaangalia washindi wanavyofanya mazoezi magumu kila siku,
wanaona kama wanajitesa, lakini wao wanakuwa wanafurahia hali hiyo, kwa
sababu wanajua ndiyo kinachowafanya wakae kwenye kilele cha ushindi.
Wenye mtazamo mgando na ambao hawakai kwenye kilele cha ushindi kwa
muda mrefu, huwa hawachukulii ushindi kama mchakato. Huwa wanaona ni
kitu ambacho tayari wameshapewa, ni wao kukichukua tu.
Kwa mtazamo huu hawaweki juhudi kwenye kujifunza au mazoezi na hilo
hupelekea wao kufanya vibaya. Wanapofanya vibaya, huwa hawaangalii wapi
wanakosea, badala yake wamekuwa wanatafuta nani wa kumlaumu. Kwa kuwa
tayari kutupa lawama kwa wengine, hawajifunzi na hivyo wanazidi kupotea.
Mchango wa timu.
Japokuwa wachezaji wengi wenye mafanikio makubwa huwa wanaelezewa
wenyewe, lakini wote hawajafika kwenye mafanikio yao peke yao.
Wamesaidiwa na timu ambazo wamekuwa nazo katika michezo wanayofanya.
Hakuna mchezaji yeyote ambaye ameweza kufikia mafanikio makubwa yeye
peke yake, hata kwa michezo inayohusisha mchezaji mmoja kama golf au
ngumi, bado mchezaji anahitaji kuwa na kocha wa kumfundisha na kumpa
miongozo mbalimbali.
Wenye mtazamo mgando na wa ukuaji wanatofautiana kwenye timu.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Hatua za kuchukua.
Je kuna michezo yoyote ambayo umekuwa unaipenda lakini unajiambia huna
kipaji nayo? Hiyo siyo sababu ya kushindwa kufanikiwa kwenye michezo hiyo,
kama kuna mchezo unaoupenda sana, jijengee mtazamo wa ukuaji na nenda
kaweke juhudi kwenye mchezo huo, utafanikiwa.
Je kuna mchezo uliokuwa una kipaji nao ulipokuwa unaanza lakini baadaye
ukaona huwezi tena? Hapo umekutana na laana ya kipaji, ambayo ilikuzuia
usiweke juhudi. Unaweza kufanikiwa kwenye mchezo huo ukiwa na mtazamo
wa ukuaji na kuweka juhudi.
Tabia ni hitaji muhimu kwenye mafanikio ya michezo na tabia nzuri zinatokana
na mtazamo wa ukuaji. Je ni tabia zipi unazohitaji kujijengea ili uweze
kufanikiwa kwenye mchezo wowote uliopo au unaotaka kuingia?
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
mafanikio hayo kwa muda mrefu. Hiyo ni kwa sababu watu hawajifunzi wala
kuweka juhudi ili kuwa bora zaidi.
Kampuni yoyote ambayo haiwezi kukubali makosa yake na kuyarekebisha,
haiwezi kudumu muda mrefu.
Uongozi na mafanikio.
Kwenye kitabu cha Good to Great kilichoandikwa na Jim Collins alilinganisha
makampuni ambayo yameweza kufikia mafanikio makubwa na yale
yaliyoshindwa, kisha kuja na vitu vinavyotofautisha makampuni hayo. Kimoja
kikubwa kilikuwa ni uongozi.
Uongozi wa kampuni zilizofanikiwa ulikuwa tofauti kabisa na wa kampuni
zilizoshindwa. Kwenye kampuni zilizoshindwa, kiongozi ndiyo alikuwa kila kitu,
alionekana ni anayejua kila kitu na kila mtu kumsujudu. Aina hiyo ya uongozi
iliamini zaidi kwenye vipaji kuliko juhudi. Hivyo kilichotokea ni kampuni
kushindwa kukabiliana na changamoto na kufa.
Kwenye kampuni zilizofanikiwa, kiongozi hakuwa kila kitu, hakuonekana kuwa
anajua kila kitu na hivyo alizungukwa na washauri wazuri, ambao aliwaamini.
Waliamini kwenye juhudi kuliko vipaji na hivyo waliajiri watu kwa kigezo cha
juhudi na siyo kipaji.
Kwa mtazamo wa nje, viongozi wa kampuni zilizoshindwa walionekana wana
mafanikio makubwa, kwa sababu wanakuwa wamejijengea sifa kubwa, lakini
kampuni zao ziliishia kuanguka. Huku viongozi wa kampuni zilizofanikiwa
wakionekana ni wa kawaida kwa sababu hawajengi sana sifa zao, lakini
kampuni zao zilifanikiwa sana.
Kwa tabia hizo tu, tunaona wazi madhara ya mtazamo kwenye uongozi na
mafanikio. Kampuni zinazofanikiwa zina viongozi wenye mtazamo wa ukuaji,
huku kampuni zinazoshindwa zikiwa na viongozi wenye mtazamo mgando.
Kwenye kitabu cha Collins, ameonesha zaidi tabia hizo, mfano kwenye
makampuni yanayoshindwa, viongozi huwa wanajiona wako juu ya kila mtu
kwenye kampuni, huwa wanachukua mafanikio ya wengine na kuyafanya kuwa
yao na huwashusha wengine ili kuonesha mamlaka waliyonayo. Lakini kwenye
kampuni zilizofanikiwa hali ni tofauti kabisa, viongozi hawajioni wakiwa juu ya
kila mtu, kwani huheshimu na kujali michango ya wengine, hawachukui
mafanikio ya wengine na kuyafanya yao na hawakazani kuwashusha wengine ili
waonekane wako juu.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Viongozi wa aina hii hutumia muda na nguvu kubwa kujenga sifa zao kuliko
kujenga kampuni. Na pia huwa tayari kuua kampuni kulinda sifa zao, kuliko
kuweka pembeni sifa zao na kuisaidia kampuni kukua.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
watumishi wao. Wale walio chini yao na hujifunza njia bora ya kwenda nao na
kuwa watu wa kujipendekeza ili wasifukuzwe, kitu kinachoficha matatizo na
kuyapa nafasi ya kukua zaidi.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Kufuata mkumbo.
Kuna hali huwa zinajitokea kwenye kundi ambapo watu wanakuwa wanafikiria
kitu kimoja, hakuna anayehoji wala kukosoa pale mambo yanapoonekana
hayaendi vizuri. Wanasaikolojia wanaita hali hii groupthink na imekuwa chanzo
cha matatizo makubwa kwenye taasisi nyingi.
Kufikiri kwa kufuata mkumbo huwa kunachochewa zaidi na mtazamo mgando.
Pale taasisi inapokuwa na kiongozi ambaye anachukuliwa kuwa na uwezo
mkubwa na kuwa mwenye mtazamo mgando, kila mtu anaweka imani yake
kwa kiongozi huyo na kuona kila analofanya kuwa sahihi.
Mwandishi anatupa mfano wa jinsi hali hii ya kufikiri kwa kufuata mkumbo
ilivyowahi kuwa na madhara kwenye uvamizi wa siri uliopangwa na Marekani
ili kumpindua Castro wa Cuba (Bay of Pigs invasion).
Hilo lilikuwa tukio la kushindwa kwa aibu kwa taifa hilo kubwa dhidi ya taifa
dogo na uchunguzi unaonesha kilichopelekea uvamizi huo kushindwa ni watu
kuacha kufikiria kwa usahihi na kufuata mkumbo.
Chanzo kikuu cha kushindwa kwa uvamizi huo ilikuwa ni kiongozi wa wakati
huo, Rais Kennedy ambaye alikuwa amejijengea sifa ya kufanya mambo mengi
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
kwa usahihi. Watu walimwamini sana na kuona ana maono makubwa na yaliyo
sahihi, ambayo hayapaswi kuhojiwa wala kukosolewa.
Hivyo alipopendekeza uvamizi wa Cuba, japo mpango haukuwa sahihi,
washauri wake wote walikubaliana naye. Yeye alifikiri wanakubaliana naye kwa
sababu mpango ni sahihi, kumbe wanakubaliana naye kwa sababu ya imani
waliyonayo kwake.
Kilichotokea ni uvamizi kushindwa vibaya kwa sababu ya watu kufuata
mkumbo kwenye kufikiri.
Mwandishi anatushirikisha kiongozi mwingine ambaye alijua madhara ya
kufikiri kwa mkumbo na kuzuia hali hiyo isiwe kikwazo kwake. Huyu alikuwa
waziri mkuu wa Uingereza Winston Churchill, ambaye alitengeneza kitengo
maalumu ambacho kazi yake ilikuwa kumpa habari zote mbaya na kuonesha
madhaifu na makosa ya kila mpango.
Kwa kuwa na watu aliowapa kazi hiyo, Churchill alijua kila kinachoendelea kwa
uhalisia wake na siyo kwa kudanganywa na wale wanaojipendekeza kwake.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Katika kusifia na kutoa zawadi kwa wafanyakazi, weka mkazo kwenye juhudi na
siyo uwezo au kipaji, pale mtu anapoonesha juhudi ambazo ni za tofauti,
atambuliwe na kupewa sifa au zawadi. Hilo litawafanya wengine nao kuwa
hivyo.
Pale taasisi inapokuwa ya mtazamo wa ukuaji, inapata manufaa mengi, baadhi
ni;
1. Wafanyakazi kuwa waaminifu zaidi kwa kampuni na kuwa tayari kujitoa kwa
maendeleo ya kampuni.
2. Wafanyakazi kumiliki kile wanachokifanya na hivyo kukifanya kwa ubora
zaidi.
3. Wafanyakazi kushirikiana vizuri katika kutekeleza majukumu yao.
4. Wafanyakazi kukaa kwenye taasisi kwa muda mrefu, huku wakiendelea
kuwa bora hivyo taasisi haiingii gharama kuajiri watu wapya kila wakati.
5. Taasisi kupata viongozi wengi na wazuri kutoka ndani ya wafanyakazi wake.
Hatua za kuchukua.
Je eneo lako la kazi lina mtazamo wa ukuaji au mtazamo mgando? Je wale
wanaokuzunguka wanakuhukumu au kukusaidia uwe bora zaidi? Je wewe
mwenyewe umekuwa unajichukuliaje kwenye kazi zako? Unakua zaidi au
umeganda pale pale? Anza kwa kujijengea mtazamo wa ukuaji kuhusu kazi
yako na eneo lako la kazi, kwa kutumia fursa za kujifunza na kufanya kwa ubora
zaidi.
Kama wewe ni kiongozi kwenye eneo lako la kazi au biashara yako, je
unawachukuliaje wale walio chini yako? Je unawaona ni watu wenye uwezo
ulio na ukomo au watu wanaoweza kukua zaidi? Je huwa unapenda wakuone
uko juu na wao wako chini yako? Huwa unapokeaje pale aliye chini yako
anapokupinga au kukukosoa? Unaona anahatarisha nafasi yako? Kama
kiongozi, anza kujijengea mtazamo wa ukuaji ili uweze kuongoza watu wako
vizuri.
Angalia njia zipi unazoweza kutumia kuwaendeleza wafanyakazi wako. Angalia
kila mmoja na changamoto zake kisha weka mpango wa kumsaidia kuwa bora
zaidi.
Unaepukaje kufikiri kwa mkumbo kwenye eneo lako la kazi? Je watu wanatoa
maoni yao kwa kufikiri wenyewe au wanaungana na kile ambacho wengine
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
namna mahusiano hayo yanaweza kwenda kwa hali hiyo, kwa sababu
hawaamini madhaifu hayo yanaweza kuboreshwa.
Mahusiano ya urafiki.
Mahusiano ya urafiki ni mahali ambapo watu hupata nafasi ya kusukumwa ili
kuwa bora zaidi na pia kusifiwa kwa hatua nzuri wanazopiga.
Marafiki wanapeana ushauri mzuri wa hatua sahihi za kuchukua na pia
wanasifiana kwa yale matokeo ambayo mtu ameyapata.
Ili mahusiano ya urafiki yawe bora, sifa zinapaswa kutolewa kwenye juhudi
ambazo mtu ameweka na siyo kwa uwezo ambao anao. Kama tulivyoona, mtu
anaposifiwa kwa juhudi anaendelea kuweka juhudi zaidi. Lakini akisifiwa kwa
uwezo, anaona uwezo huo una ukomo.
Mahusiano ya urafiki yanaathiriwa sana na mtazamo mgando ambapo marafiki
huwasifia wenzao ili tu kutokuwaumiza na hilo limekuwa haliwasaidii.
Ushauri maarufu kwenye mahusiano ya kirafiki umekuwa huu; utawajua
marafiki zako wa kweli unapokuwa na shida. Na hii ni kweli, wale
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Hatua za kuchukua.
Unajisikiaje pale unapokataliwa na wengine au mahusiano kuvunjika? Je huwa
unaona kama umeumizwa sana na kupanga kulipa kisasi? Au unakuwa tayari
kusamehe, kusahau na kusonga mbele huku ukijifunza na kuwa bora zaidi?
Kumbuka mahusiano uliyowahi kuwa nayo na yakavunjika na kukuumiza sana,
fikiria ulichukuliaje hali hiyo kipindi inatokea, kwa mtazamo mgando au
mtazamo wa ukuaji? Jiulize sasa ni kipi ulijifunza kwenye mahusiano hayo. Na
kama bado hujamsamehe yeyote ambaye mahusiano yenu yamewahi
kuvunjika, chukua hatua ya kuwasamehe sasa na kujifunza ili kuwa bora zaidi
kwenye mahusiano yako mengine.
Tengeneza picha ya mahusiano bora ya kimapenzi kwako, unapenda yaweje?
Je unapenda mahusiano ambayo mnaendana na kukubaliana kwa kila kitu,
mahusiano ambayo hayahitaji kuweka kazi ili kuyajenga? Kama hii ndiyo picha
uliyonayo basi tambua una mtazamo mgando kwenye mahusiano. Badilika na
kuwa na mtazamo wa ukuaji, ukijua kila mahusiano yana changamoto zake na
ili yawe bora lazima kazi iwekwe.
Inapotokea changamoto kwenye mahusiano, huwa unakimbilia kutoa lawama?
Hicho ni kiashiria cha mtazamo mgando, acha sasa kutoa lawama na angalia
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
tatizo liko wapi na hatua gani za kuchukua kwa pamoja ili kuondokana na
changamoto hiyo.
Je umewahi kuwa kwenye mahusiano ambayo ulikuwa unaonewa? Je
ulichukuliaje hali hiyo, uliona unastahili na kupanga kulipa kisasi au uliona
anayekuonea ana matatizo yake binafsi? Kuanzia sasa, pale mtu mwingine
anapokuonea bila sababu yoyote, jua ana matatizo yake binafsi na kubwa
kabisa ni mtazamo mgando alionao, hivyo epuka kabisa watu wa aina hiyo.
Huu ni mwisho wa sehemu ya pili ya uchambuzi wa kitabu cha MINDSET
ambapo tumeona madhara ya mtazamo kwenye michezo, uongozi na
mahusiano. Kwenye sehemu ya tatu tunaona jinsi mtazamo unavyojengwa
tangu utotoni na jinsi ya kubadili mtazamo wako kwa hapo ulipo sasa. Usikose
uchambuzi huo wa sehemu ya tatu na ya mwisho ya kitabu hiki.
Umejifunza mambo muhimu sana kupitia uchambuzi huu wa kitabu. Sasa kazi
ni kwako kwenda kuyaweka kwenye matendo ili uweze kupiga hatua na
kufanikiwa kwenye maisha yako.
Kuendelea kupata chambuzi za kina za vitabu na vitabu vilivyochambuliwa,
jiunge na channel ya SOMA VITABU TANZANIA, kwa kufungua
www.t.me/somavitabutanzania
Rafiki, karibu upate na kusoma vitabu vizuri vya maendeleo binafsi na
mafanikio kwa lugha ya Kiswahili. Pakua na weka app ya SOMA VITABU na
upate maarifa sahihi. Kwa maelezo zaidi fungua;
https://amkamtanzania.com/somavitabuapp
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007