Professional Documents
Culture Documents
UCHAMBUZI WA KITABU Mindset Saikolojia Mpya Ya Mafanikio - Sehemu
UCHAMBUZI WA KITABU Mindset Saikolojia Mpya Ya Mafanikio - Sehemu
ME/SOMAVITABUTANZANIA
Kuhusu mwandishi.
Carol S. Dweck (kuzaliwa Oktoba 17, 1946) ni mwanasaikolojia wa nchini
Marekani. Ni profesa wa saikolojia kwenye chuo kikuu cha Stanford lakini pia
amefundisha kwenye vyuo vikuu vikubwa kama Columbia, Harvard na Illinois.
Carol anafahamika zaidi kupitia tafiti zake kwenye eneo la uwezo wa binadamu
pamoja na motisha. Ni kupitia kazi hizo ndiyo ameweza kuja na kitabu hiki
kinachoelezea aina mbili za mtazamo ambao watu wanakuwa nayo na jinsi
zinavyoathiri mafanikio yao.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Hatari na juhudi.
Ni kitu kinachojulikana wazi kwamba huwezi kufanikiwa bila ya vitu hivi viwili;
juhudi na hatari. Ni lazima uweke juhudi kwenye kile unachofanya na lazima
uchukue hatua za hatari, kwa kujaribu vitu vipya ambavyo havijazoeleka
vyenye hatari ya kushindwa.
Lakini jinsi watu wanavyochukulia juhudi na hatari inatokana na mtazamo
walionao.
Wale wenye mtazamo wa ukuaji huwa wanakuwa tayari kuchukua hatua za
hatari na kuweka juhudi, kwa sababu wanajua wana uwezo mkubwa,
hawakwami katika kufanya yaliyo makubwa.
Lakini wale wenye mtazamo mgando huwa hawapo tayari kuweka juhudi na
kuchukua hatua za hatari. Wao wanaamini kiwango cha uwezo walichonacho
ndiyo ukomo, hakuna namna wanaweza kukibadili, hivyo wanapaswa kufanya
kile walichozoea kufanya badala ya kujaribu vitu vipya na kushindwa.
Kwa wenye mtazamo wa ukuaji, kujaribu vitu vipya ni kujifunza na kukua
wakati kwa wenye mtazamo mgando kujaribu vitu vipya ni kushindwa na
kujidhalilisha.
Hii inaelezea kwa nini wale watoto wanaoonekana kuwa na uwezo mkubwa
utotoni huwa hawafanikiwi sana, wakati wale ambao wanaonekana hawana
uwezo mkubwa wakija kufanikiwa zaidi. Hiyo ni kwa sababu wanaoanza na
uwezo mkubwa wanakuwa na imani kwamba uwezo wao ndiyo huo na
haubadiliki, huku wanaoanza na uwezo mdogo wakiamini wanaweza kubadili
uwezo wao zaidi.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Hatua za kuchukua.
Hatua za kuchukua hapa ni kujua aina ya mtazamo ulionao. Kujua aina yako ya
mtazamo, jibu maswali haya kwa kujitafakari na kuona kama ni NDIYO au
HAPANA.
1. Unaamini uwezo wako wa kiakili ni kitu ambacho hakiwezi kubadilika.
2. Unaamini unaweza kujifunza vitu vipya, lakini huwezi kubadili uwezo wako
wa kiakili.
3. Unaamini haijalishi una akili kiasi gani, unaweza kuongeza uwezo wako wa
kiakili.
4. Unaamini mara zote unaweza kujiongeza na kuwa na akili zaidi.
Swali la 1 na 2 yanaonesha mtazamo mgando, huku swali la 3 na 4 yakionesha
mtazamo wa ukuaji. Je wewe unakubaliana na maswali yapi?
Unaweza kuwa na mchanganyiko wa mtazamo wa ukuaji na mgando, lakini
wengi huegemea upande mmoja, mtazamo wa ukuaji tu au mtazamo mgando
tu.
Pia unaweza kupima mtazamo wako kwa maswali hayo kwenye maeneo
mengine, badala ya akili, weka kitu kingine kama sanaa, uandishi, biashara na
kadhalika.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Tambua mtazamo ulionao sasa ili uweze kujua hatua sahihi za kuchukua na
kufanikiwa zaidi kwenye maisha yako.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Mtazamo na kujifunza.
Mtazamo ambao mtu anao, una athari kubwa kwenye utayari wake wa
kujifunza.
Wale wenye mtazamo mgando, huwa wanakuwa tayari kujifunza pale vitu
vinapokuwa rahisi kwao. Lakini vitu vinapokuwa vigumu, wanaacha kujifunza
kwa sababu wanaamini uwezo wao una ukomo.
Kwa wenye mtazamo wa ukuaji, huwa tayari kujifunza vitu viliwa rahisi, lakini
huendelea kujifunza hata vitu vinapokuwa vigumu, huwa wanaendelea
kujifunza kwa sababu wanajua ugumu huo unawafanya wafikie uwezo mkubwa
ulio ndani yao.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Kujilinganisha na wengine.
Changamoto kubwa ya mtazamo mgando ni kujilinganisha na wengine, na hili
huwa na madhara ya aina mbili.
Moja ni pale mtu anapokuwa anajiona ana uwezo mkubwa kuliko wengine,
hapo husukumwa kuthibitisha uwezo wao mkubwa na hivyo kuacha kujifunza.
Upande wa pili ni pale mtu anapojiliganisha na kuona wengine wana uwezo
mkubwa kuliko yeye na hivyo kujidharau na kuona hawezi.
Kwa wenye mtazamo wa ukuaji, hawajilinganishi na wengine, bali
wanajilinganisha na wao wenyewe, kwa kujipima jinsi wanavyoendelea kukua
na kuwa bora zaidi kila siku.
Tafiti pia zinaonesha pale wenye mtazamo mgando wanaposhindwa, huwa
wanatafuta walioshindwa zaidi yao ili kujilinganisha nao, kitu kinachowafanya
wajisikie vizuri.
Badala ya kuangalia wale waliofanikiwa kuliko wao na wajifunze kwao, wao
wanatafuta walioshindwa zaidi, lengo siyo kujifunza, bali kujisikia vizuri, kwa
sababu wanaamini uwezo wao una ukomo.
Mtazamo na Lawama.
Wenye mtazamo mgando na wa ukuaji huwa wanatofautiana pia kwenye
lawama wanazotoa pale wanaposhindwa.
Kwa wenye mtazamo mgando, mara zote huwa wanawalaumu watu wa nje.
Kwa sababu wanaamini ndani yao wana uwezo fulani, kama wanashindwa basi
kuna mtu wa nje anayehusika. Mfano mzuri ni mwanafunzi anayefeli mtihani
na kusingizia mwalimu kumsahihishia vibaya.
Wenye mtazamo wa ukuaji huwa wanamiliki makosa na kushindwa kwao. Kwa
kuwa wanajua wana nafasi ya kukua zaidi, huwa wanaangalia wapi
walipokosea na kuona hatua zipi za tofauti wanaweza kuchukua ili
wasishindwe tena.
Mwandishi anamnukuu mmoja wa makocha bora kabisa John Wooden,
aliyewahi kusema hujashindwa mpaka pale unapoanza kulaumu wengine.
Akimaanisha kwamba kama unashindwa lakini hulaumu wengine, maana yake
unajifunza na kupiga hatua, hivyo hujashindwa ila uko kwenye mchakato wa
mafanikio. Ila unaposhindwa na kutupa lawama kwa wengine, basi hapo wewe
ni mshindwa na hakuna hatua unazoweza kupiga.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Mtazamo na Sonona.
Kushindwa huwa kunawaumiza sana wale wenye mtazamo mgando kiasi cha
kuwapelekea kupata sonona. Hiyo ni kwa sababu wanaposhindwa wanajiona
hawafai na hilo linawafanya waingie kwenye sonona na kukata tamaa.
Wale wenye mtazamo wa ukuaji huwa hawapati sonona wanaposhindwa, kwa
sababu wanajua kushindwa siyo hukumu ya maisha yao, bali ni mchakato wa
kufanikiwa zaidi. Hawatumii muda mwingi kufikiria jinsi walivyoshindwa, bali
wanaangalia jinsi gani wanaweza kupiga hatua zaidi.
Ubaya wa sonona ni kwamba ikishamuingia mtu, inamkatisha tamaa na hawezi
kujaribu tena. Ndiyo maana wenye mtazamo mgando huwa wanakata tamaa
mapema na hawafanikiwi, kwa sababu sonona wanayoipata inawafanya
wajione hawawezi tena.
Mtazamo na juhudi.
Wenye mtazamo mgando wanaamini hawahitaji kuweka juhudi sana kwa
sababu haziwezi kubadili uwezo wao. Na kwa kuwa wanataka kuthibitisha kwa
wengine uwezo wao, hawapo tayari kujisukuma zaidi, maana wakionekana
wanaweka juhudi, watu watajua hawana uwezo.
Lakini wenye mtazamo wa ukuaji, wako tayari kuweka juhudi zaidi kwa sababu
wanajua wanaweza kuwa zaidi ya walivyo sasa. Hawahangaiki kujionesha na
kupata uthibitisho wa wengine, bali wanakazana kupiga hatua zaidi wao
wenyewe.
Hili la kutokutaka kuweka juhudi limejengwa sana kwenye jamii zetu, ambapo
mashujaa huwa wanaonekana ni watu waliozaliwa na uwezo wa kipekee na
hawahitaji kusumbuka kama wengine. Huku wale wanaoweka juhudi sana
wakionekana kama wanalazimisha kitu ambacho hawana uwezo nacho.
Lakini ukiangalia kwenye uhalisia, wale wote ambao wamefikia mafanikio
makubwa ni matokeo ya kuweka juhudi kubwa, walianzia chini kabisa,
wakapambana na kuanguka mara kadhaa kabla hawajafika kwenye kilele cha
mafanikio.
Kuna sababu kuu mbili kwa nini wenye mtazamo mgando wanahofia sana
kuweka juhudi;
Sababu ya kwanza ni kuamini kwenye ujiniazi. Wenye mtazamo mgando
wanaamini uwezo wa mtu ni wa ukomo na wale wenye uwezo wa juu ni
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
yako yakabadilika kabisa. Kwa kujifunza sifa hizi mbalimbali za mitazamo hiyo
miwili, unajua wapi ulipo na hatua zipi za kuchukua ili kubadili mtazamo wako.
Pamoja na kwamba juhudi ni muhimu kwenye mafanikio, lakini pia mazingira
na ‘koneshneni’ ambazo mtu anakuwa nazo zina mchango mkubwa kwenye
mafanikio yake. Mtu anapoanza na mtazamo sahihi, ni rahisi kwake kuyatumia
mazingira yake vizuri kufanikiwa.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Haya ndiyo yaliyo ndani ya mtazamo miwili wanayokuwa nayo watu na ndiyo
yanayoathiri matokeo ambayo mtu anayapata kwenye maisha.
Hatua za kuchukua.
Kila mtu huwa anazaliwa akipenda kujifunza, lakini mtazamo mgando
unapoingia, mapenzi ya kujifunza yanaondoka. Kumbuka kipindi ambacho
kulikuwa na kitu unapenda sana kujifunza, inaweza kuwa mchezo fulani au
hata mafumbo, lakini kujifunza kulipoanza kuwa kugumu ukawa unaacha.
Kuanzia sasa unapoamua kujifunza kitu na kukutana na ugumu usikubali
kuacha, bali endelea kujifunza na hapo utakuza zaidi uwezo wako.
Epuka kuchagua kuzungukwa na watu wanaokusifia na kukusujudu, badala
yake chagua watu walio tayari kukuonesha makosa na madhaifu yako, hilo
litakusaidia kukua zaidi. Kama unataka kuzungukwa na wanaosifu, nenda
kanisani, lakini kwenye maisha yako, zungukwa na walio tayari kukuonesha
ukweli usioupenda.
Je kuna matokeo yoyote umewahi kuyapata kipindi cha nyuma kwenye maisha
yako na kuyatumia kujipa hali fulani? Labda ulifeli mtihani na kujiona wewe
huwezi, au ulipata hasara kwenye biashara na kujiona wewe huwezi biashara?
Sasa badili hilo, badala ya kujiona mshindwa, jione ulikuwa mafunzoni, angalia
kila ulichofanya kisha jiulize ni yapi umejifunza na unawezaje kufanya kwa
ubora zaidi ili upate matokeo mazuri zaidi. Kisha anza kuchukua hatua hizo
mpya.
Unapopanga kufanya kitu kisha ukashindwa, huwa unajisikiaje? Unakata tamaa
na kupata sonona au unaona ni sehemu ya kujifunza? Kuanzia sasa kila kikwazo
unachokutana nacho usione kama ni mwisho, bali ona kama darasa ambalo
linakufundisha kile unachopaswa kujua ili upate matokeo makubwa.
Je kuna kitu chochote umekuwa unapanga kufanya kwenye maisha yako lakini
huanzi kwa sababu unajiona hujawa tayari? Usiendelee kusubiri, weka
mipango na anza kukifanya, ukiwa tayari kuweka juhudi na kuchukua hatua za
hatari, ukijifunza na kukazana kwa ubora zaidi. Kwa njia hii utaweza kupiga
hatua kuliko kuendelea kusubiri mpaka uwe tayari, kitu ambacho huwa
hakitokei.
kufikia mafanikio. Tunaoneshwa mtu mmoja ambaye alianzia chini kwa sababu
ya uwezo mkubwa alionao au juhudi kubwa alizoweka akaweza kufanya
makubwa.
Lakini huo siyo ukweli, kila aliyefanya makubwa kwenye maisha yake, kulikuwa
na watu wengi waliohusika, kumsaidia kukamilisha kile alichofanya. Kulikuwa
na walimu, washauri, wenza na hata wengine wa kusaidia kwa namna fulani
mpaka kufikia pale.
Hapa mwandishi anatupa nafasi ya kuona mchango mwingine wa mafanikio
ambao huwa hauzungumziwi sana, mchango unaowatofautisha wale
wanaofanya makubwa na wale wanaoshindwa kufanya makubwa.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
zaidi kwenye masomo. Walitumia muda huo kujaribu vitu tofauti tofauti ili
wajue nini wanapendelea zaidi kufanya.
Wanafunzi hao waliendelea kufuatiliwa kwa miaka miwili na matokeo yalizidi
kutofautiana. Wenye mtazamo wa ukuaji waliendelea kufanya vizuri na hata
walipofeli mtihani mmoja, baadaye walifanya vizuri. Lakini wanafunzi wenye
mtazamo mgando walikuwa wakifanya vibaya na pale alipofeli somo moja,
hakuweza kufanya tena vizuri.
Walipofuatiliwa zaidi kwenye mtindo wa usomaji, kulikuwa na tofauti kubwa.
Kwa wanafunzi wenye mtazamo mgando walisoma kwa mtindo huu,
walichukua kitabu cha somo husika na kupanga kukisoma na kukariri kila kitu
kwenye kitabu hicho. Hivyo walipofanya vibaya, walijiambia pamoja na
maandalizi makubwa waliyofanya wamefeli, hivyo hawana uwezo kwenye
somo husika.
Wanafunzi wenye mtazamo wa ukuaji walijifunza kwa mtindo tofauti, badala
ya kusoma kwa kukariri, wao walisoma kwa kuelewa, walitafuta kuelewa
misingi mikuu ya dhana husika na kujifunza kwa namna wanavyoweza
kuielezea vizuri. Kwa njia hii walijifunza na kuelewa na kwenye mtihani
walifanya vizuri. Walifanya vizuri siyo kwa sababu walikuwa na uwezo kwenye
somo hilo, ila kwa kuwa walikuwa na mtazamo mzuri.
Kingine kilichoonekana ni wanafunzi wenye mtazamo wa ukuaji walikuwa
tayari kushirikiana na wengine, huku wenye mtazamo mgando wakiwa hawapo
tayari kushirikiana na wengine wakati wa kujifunza.
Hitimisho la utafiti huu ilikuwa kwamba kile ambacho mtu kuna mtu
amejifunza hapa duniani, basi na wengine pia wanaweza kujifunza iwapo
watakuwa na mtazamo sahihi na mazingira sahihi ya kujifunza kitu hicho.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Mafanikio yoyote yale kwenye maisha yanahitaji mtu kuweka umakini kwenye
kile anachofanya, kuweka juhudi kubwa, kuwa na mikakati sahihi pamoja na
kuwa na watu ambao mtu anashirikiana nao. Kwa kuwa wenye mtazamo wa
ukuaji wapo tayari kwa yote hayo, wanapata nafasi ya kufanikiwa zaidi kuliko
wenye mtazamo mgando, ambao wanayapinga hayo.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Mtazamo na ubaguzi.
Kwenye jamii kuna makundi mbalimbali ambayo huwa yanatofautiana na
makundi hayo yamekua yanatumika kujenga ubaguzi. Mfano ni kwenye jinsia
(wanawake na wanaume) na rangi (weusi na weupe).
Mwandishi anatushirikisha utafiti uliofanyika ambapo pale mtu
alipokumbushwa kuhusu kundi alilopo, iliathiri sana uanisi wake. Lakini athari
zilitegemea mtazamo ambao mtu anao.
Kwa utafiti ambao mwandishi ameshirikisha, pale mshiriki alipowekwa kwenye
nafasi ya kufikiria kuhusu kundi lake, wale walio kwenye kundi la kubaguliwa
(wanawake na watu weusi) walifanya vibaya kuliko wakiwa kwenye mazingira
ambayo hayawafanyi kukumbuka kundi walilopo. Hiyo inaonesha kitendo cha
kujiweka tu kwenye kundi linalobaguliwa, kinamfanya mtu ajione ana uwezo
wa chini.
Lakini hilo halikutokea kwa watu wa aina zote, walioathiriwa zaidi na hali hiyo
ni wale wenye mtazamo mgando. Wenye mtazamo mgando wanapofikiria
kuhusu kundi walilopo, wanajiona hawana uwezo kama ambavyo kundi hilo
limekuwa linachukuliwa na hali hiyo inawapelekea kutokuwa na ufanisi mzuri.
Lakini wenye mtazamo wa ukuaji, kukumbushwa kuhusu kundi walilopo
haikuwa na athari kwenye ufanisi wao. Hii ni kwa sababu wanaamini uwezo
wao hauna ukomo, hivyo kuwekwa kwenye kundi fulani hakuhusiani na uwezo
ulio ndani yao. Hata pale wanapojikuta wako nyuma ya wengine, hawakati
tamaa, badala yake wanaweka juhudi zaidi na hilo linawapelekea kufanya
vizuri.
Hili linatupa funzo kubwa kwamba mtazamo unaathiriwa sana na hali za
kijamii. Mtu anapokuwa na mtazamo mgando, akipewa sifa nzuri au mbaya
zote zinamuathiri. Akipewa sifa nzuri anaogopa hataifikia na hivyo kuacha
kuweka juhudi, akipewa sifa mbaya anaona ndiyo anayostahili na kukubaliana
nayo.
Njia pekee ya kuweza kufanikisha makubwa kwenye maisha ya mtu, ni
kuondokana na mtazamo mgando ambao unamfanya mtu kuwa mwathirika wa
yale wanayofanya wengine. Mtazamo mgando unathamini zaidi vile wengine
wanavyomchukulia mtu kuliko anavyojichukulia mwenyewe. Kama unataka
kuweza kuishi uwezo wako na kufanya makubwa, unapaswa kuwa na mtazamo
wa ukuaji.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Hatua za kuchukua.
Fikiria kuhusu mashujaa ambao unao kwenye maisha yako, wale
unaowaangalia na wanakuhamasisha, je unawaona kama watu waliozaliwa na
uwezo mkubwa au watu walioweka juhudi kufika walikofika? Kama hujaingia
kwa kina kujifunza kuhusu watu hao, utakuwa unawaona kwa uwezo, sasa
nenda kayaangalie kwa kina maisha yao na utaona jinsi juhudi zimewafikisha
pale walipofika.
Kumbuka kipindi ambacho watu wengine walikushinda kwenye kitu
mlichokuwa mnafanya pamoja. Jiulize ulichukuliaje, je uliona wana uwezo
kuliko wewe au wameweka juhudi zaidi? Kama uliona ni uwezo ulijidanganya,
angalia tena na utaona ni juhudi, na jua kwamba hata wewe unaweza kuweka
juhudi zaidi na ukafanya makubwa.
Huwa unawasifiaje watoto wako, je unawasifia kwa uwezo au juhudi? Kuanzia
sasa anza kuwasifia watoto na hata watu wengine kwa juhudi walizoweka na
siyo kwa uwezo walionao. Angalia juhudi fulani waliyoweka na isifie hiyo,
utamsukuma kuweka juhudi zaidi.
Sehemu kubwa ya watu kwenye jamii wapo kwenye kundi ambalo limekuwa
linabaguliwa, inaweza kuwa kwa sababu ya jinsia (wanawake) au rangi (watu
weusi). Unapokuwa kwenye kundi linalobaguliwa, usijipime uwezo wako kwa
kujilinganisha na kundi, badala yake kazana kuweka juhudi kwenye chochote
unachofanya. Na kama uko kwenye kundi lisilobaguliwa, basi wasaidie walio
kwenye kundi linalobaguliwa ili hali hiyo isiwe kikwazo kwao.
Huu ni mwisho wa sehemu ya kwanza ya uchambuzi wa kitabu cha MINDSET
ambapo tumejifunza kuhusu mitazamo ya aina mbili, kilicho ndani ya mitazamo
hiyo na kuhusu uwezo na ufanikishaji.
Kwenye sehemu ya pili itakayofuatia tutajifunza athari za mitazamo hii kwenye
maeneo matatu; michezo, biashara na mahusiano. Usikose uchambuzi huo ili
uone jinsi mitazamo tunayokuwa nayo inavyoweza kupelekea kufanikiwa au
kushindwa kwenye maeneo hayo.
Umejifunza mambo muhimu sana kupitia uchambuzi huu wa kitabu. Sasa kazi
ni kwako kwenda kuyaweka kwenye matendo ili uweze kupiga hatua na
kufanikiwa kwenye maisha yako.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007