Professional Documents
Culture Documents
Kiswahili Isimu Jamii
Kiswahili Isimu Jamii
Muhadhara wa kwanza
1.0.Lugha ni nini?
Mtu anapouliza swali hili (Lugha ni nini?) inaweza kuonekana kana kwamba ni swali la kijinga.
Labda kwa sababu huwa hatupendi kutilia maanani katika vitu ambavyo tunadhani ni vya
kawaida. Kwa bahati mambo hayapo kama tunavyoweza kuyaona au kuyatafakari. Kwa maana
hiyo basi, hata swali la kwamba “lugha ni nini?” siyo rahisi na wala siyo la kawaida kama
ambavyo tunaweza kulichukulia. Kwa maelezo hayo tunaweza kufasili dhana ya lugha kwa
mitazamo miwili: Mtazamo finyu (narrow conception) na Mtazamo mpana (Broad conception).
1.1.Mtazamo Finyu:
i. Lugha ni chombo cha mawasiliano
Kuitazama lugha kama tu chombo cha mawasiliano kunawezesha ufahamu wa kawaida. Kwa
maana hiyo, bado kuna taarifa muhimu zinakosekana katika fasili na hii inatupatia mapungufu ya
fuatayo: kwanza, kueleza lugha kama chombo cha mawasiliano ni kueleza kazi ya lugha na sio
lugha yenyewe. Pili, kama mtu atapiga ngoma ili kuwaita watu na watu wakaja basi milio ya
ngoma itakuwa ni lugha. Na kwamaana hiyo kila kitakacho wawezesha watu kuwasiliana
kitakuwa ni lugha. Kama lugha ni chombo tu cha mawasiliano, maana yake hakuna tofauti
yoyote kati ya kuzungumza na milio mbali mbali kama honi ya gari, filimbi ya refa uwanjani, au
kengere ya kanisani au hata sauti inayotokana na kugonga mlango wakati mtu anabisha hodi.
Hivyo jambo hili sio la kweli na linatupeleka mbali zaidi na kutufanya tuanze kuitazama fasili ya
lugha kwa mtazamo mwingine zaidi – mtazamo mpana.
1.2.Mtazamo Mpana.
Katika mtazamo huu kunawanaisimu wengi ambao wamejaribu kutoa fasili zao mbali mbali.
Baadhi ya fasili hizo ni kama zifuatazo:
i. Todd (1987) anasema lugha ni mfumo wa ishara ambazo kwazo watu huwasiliana.
ii. Kamusi ya Isimu na lugha (1990) inaeleza kuwa lugha ni mfumo wa sauti nasibu
zinazotumiwa na watu wa jamii wenye utamaduni unaofanana ili kuwasiliana.”
iii. Cook,1969:12 anaeleza kuwa lugha ni mfumo wa sauti nasibu na ishara za kisarufi
ambazo kwazo watu wa jamii Fulani ya lugha huwasiliana na kupokezana utamafuni
wao.
iv. Bloch and Trager (1942): “A language is a system of arbitrary vocal symbols by
means of which a social gorup co-operates”.
1
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
viii. Language: “The system of arbitrary vocal symbols we use to encode our experience
of the world”
[Lugha ni mfumo wa sauti za nasibu ambazo tunazitumia kusimba uelewa na uzoefu
wetu wa ulimwengu.]
ix. Nae Sapir (1921:7) anasema: “Language is a purely human and non-instinctive
method of communicating ideas, emotions and desires by means of voluntarily
produced symbols.”
[Lugha ni njia ya mawasiliano ambayo ni maalumu kwa mwanadamu na isiyo silika
ambayo hutumiwa kuwasilisha mawazo, hisia na matakwa kwa kutumia ishara
ambazo hutolewa kwa hiyali].
x. Mario Pei & Frank Gaynor (1954) Kamusi ya Isimu (A Dictionary of Linguistics)
anasema: Language is a system of communication by sound, i.e., through the organs
of speech and hearing, among human beings of a certain group or community, using
vocal symbols possessing arbitrary conventional meanings.
[Lugha ni mfumo wa mawasiliano kwa njia ya sauti, yaani, kwakutumia alasauti na
kusikia, miongoni mwa binadamu wa kundi fulani au jumuiya kwa kutumia ishara-
sauti ambazo maana zake hueleweka kwa unasibu tu.
2.0.Tathmini ya Fasili za Lugha
Ukichunguza fasili hizi na nyingine nyingi ambazo hazijatolewa hapa utagundua kuwa swali letu
tuliloliuliza hapo mwanzo yaai “Lugha ni nini?” sio swali la kijinga wala sio swali rahisi
kulijibu. Hivyo basi, kutokana na fasili hizo tunaweza kusema kuna maana mbali mbali za lugha
2
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
kulingana na mzingira, mazoea, taaluma na hata mahala mtu alipobobea kitaaluma. Lakini,
pamoja na tofauti hizi mbali mbali zinazojitokeza, tunaona kuna mambo kadhaa ya msingi
ambayo takribani wataalamu wote wanayagusia wanapofasili dhana ya ‘lugha’. Mambo hayo ni
kama yafuatayo: Lugha ni mfumo, Lugha ni mfumo wa sauti nasibu, Lugha ni maalumu kwa
binadamu, Lugha ni mfumo wa ishara, Lugha hutumia sauti, Lugha ni kwa ajili ya mawasiliano.
Kimsingi mambo haya ndiyo yanayogusiwa katika fasili hizi. Lakini ikumbukwe kuwa, sio kila
fasili zilizotajwa hapo juu zinajumuisha vipengele vyote hivi. La hasha! Fasili moja inaweza
ikawa inakipengele kimoja wapo au viwili kati ya hivi. Kila kimoja kinaelezewa hapa chini kama
ifuatavyo.
2.1.Lugha ni mfumo
Ishara zinazotumiwa katika lugha zinampangilio wenye kutawaliwa na sheria na unaruwaza
zinazotambulika na watumiaji wa lugha hiyo. Kila lugha ya mwanadamu imeundwa katika
mifumo miwili mikuu; mfumo wa sauti na mfumo wa maana. Lugha huundwa kwa sauti ambazo
huunganishwa kuunda neno au sehemu ya neno, maneno nayo huungana kuunda miundo
mikubwa zaidi yenye maana kama virai, vishazi, sentensi na aya.
Katika muunganiko huu wa maneno na miundo mbali mbali, huwa kuna kanuni na sheria
zinazidhibiti mfuatano wa kila kipashio. Kuna kanuni zinazo dhibiti mfuatano wa sauti,
mfuatano wa mofimu, mfuatano wa maneno na hata mfuatano wa sentensi. Hivyo basi, mtu
hawezi kuunganisha tu sentensi kwa matakwa yake bila kujali kanuni hizi, akifanya hivyo
atasababisha kutokea kwa kitu ambacho siyo lugha na wala hakikubaliki katika lugha. Kwa
maana hiyo, lugha ya mwanadamu ni mfumo wenye kanuni, sheria na taratibu maalumu ambazo
zikikiukwa basi kuna kuwa hakuna utimilifu wa lugha husika. Lugha inaonesha utaratibu katika
mahusiano ya viunzi vya lugha. Sheria hizi zinazotawala mpangilio wa viunzi vya lugha hiyo
ndizo zinazowawezesha watumiaji wa lugha fulani kuelewana.
Katika picha inayoonekana hapo juu kuna neno ‘mti’ na mmea wenyewe ambao umebatizwa jina
hilo. Katika hali halisi hakuna watu waliokaa nakusema kuanzia leo huu utaitwa mti. Vile vile
3
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
hakuna uhusiano wowote kati ya neno “MTI” an umbo linalomaanishwa. Uhusiano wake ni wa
nasibu tu na hutofautiana kutokana na lugha na lugha. Hii ndiyo maana Waingereza wataita tree,
Wahehe wataita mubiki, Wasukuma wataita mpiki n.k. Ukweli kwamba hakuna uhusiano wa asili
kati ya umbo la neno na maana ambazo umbo hilo linapewa ndiyo sababu inayofanya kuwe na
namnatofauti ya kuuelezea ulimwengu. Ferdinand de Saussure katika kile alichokiita ishara za
kiisimu anabainisha sawia mbili za mahusiano haya; kwanza ni “signifie” ambacho ni kiashiria
yaani umbo la kifonolojia (kutamkwa) au kiothografia (kuandikwa) na ambalo huwakilisha
dhana Fulani. Kitu cha pili ni “significant” ambacho ni kiashiriwa ambacho ni kitu chenyewe
kilicho katika ulimwengu halisi wa vitu na dhana. Hivyo basi, uhusiano kati ya kiashiria na
kiashiriwa ndio unlio wa unasibu.
Kwa ujumla, kuna sababu kuu tano zinazotuwezesha kukubaliana kuwa msingi wa lugha ni sauti
za kutamkwa.
4
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
2.7.Fasili ya jumla
Hivyo basi, baada ya kuchunguza fasili hizo za lugha na vipengele vinavyojibainisha kwenye
kila fasili mojawapo, tunaweza kusema kuwa lugha ni mfumo wa sauti za nasibu zilizokubaliwa
na watu au jamii ili zitumike katika mawasiliano yao ya kilasiku kueleza hisia, mawazo,
matakwa na mahitaji yao.
3.1.Unasibu
Kama tulivyokwisha eleza mwanzo, unasibu wa lugha ya ninadamu unaangaliwa katika mambo
yafuatayo:
5
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
3.3.Uambukizaji wa utamaduni
Lugha ya mwanadamu inauwezo wa kuambukiza utamaduni kutoka katika kizazi kimoja kwenda
kizazi kingine au kutoka katika jamiilugha moja kwenda katika jamiilugha nyingine. Ieleweke
kuwa, uwezo huu wa kuambukiza maarifa ya lugha hufanyika kwa njia ya kusoma au kujifunza
na sio kurithi. Kwa mfano, mtu anaweza kurithi maumbile kutoka kwa wazazi wake, mathalani
aina ya nywele, aina ya macho, lakini mtu hawezi kurithi lugha. Lugha inamfikia kwa
kuambukizwa katika jamiilugha anayokulia. Yatupasa tukumbuke kuwa, ingawa mwanadamu
anazaliwa na uleuwezo (kitengo cha lugha) wa kujifunza lugha “Language Acquisition Device”
kama anavyoeleza mwanaisimu Noam Chomsky, lakini hazaliwi na lugha. Hii ndiyo sababu
mwanadamu anaweza kujifunza lugha yoyote ile na kwa wakati wowote maadamu yupo katika
mazingira na hali ya kawaida na saidizi.
6
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
lugha ya mwanadamu kwani kwa kutumia sauti hizi chache mzungumza lugha anaweza kutoa au
kuzungumza sentensi nyingi au tungo nyingi na zenye maana tofauti tofauti bila kikomo.
Suala jingine la msingi ni kwamba, tunaposema kuwa lugha imegawanyika katika viwango
viwili, kiwango cha sauti na kiwango cha maana haimaanishi kwamba binadamu anatumia
viwango hivi kiupeke peke. Hata sikumoja mwanadamu hasemi kwamba sasa naanza kutamka
sauti, mathalani, baba halafu ndiyo niweke maana yake. La hasha! Binadamu hutamka kwa
maramoja sauti pamoja na maana vikiwa vimebebana ndani kwa ndani (hutamka sauti pamwe na
maana). Yaani, wakati anatamka sauti na kuziunganisha ndiyo wakati anaambatanisha na maana
ndani yake. Hii ndiyo sifa ua uwili katika lugha ya mwanadamu.
3.5.Uhamisho au Urejelezi
Sifa hii inamaanisha kuwa binadamu wenyewe kama watumia lugha wanauwezo wa
kubadilishana taarifa. Kila mmoja wao anaweza kuwa mtumaji au mpokeaji wa taarifa kwa
kutumia lugha.
3.7.Upeke
Lugha hundwa na viunzi vidogo vidogo ambavyo ni peke peke na haipo katika mfululizo. Kila
kipashio kinachotumika kuunda tungo za lugha kipo peke peke na kinaweza kuunganishwa na
vingine kupata muundo wa juu mkubwa zaidi. Hivyo, lugha inawezwa kugawanywa tena kwa
kukusayna vipashio hivyo kuunda tungo kubwa zaidi.
4.0.Asili ya Lugha
Hakuna maafikiano kati ya wanaisimu juu ya wapi, lini, namna gani na nani hasa alianzisha
lugha. Hii inatokana na ukweli kwamba binadamu alianza kuishi tangu kale wakati ambapo hata
hivyo bado hauja julikana. Suala ambalo lina uhakika ni kuwa lugha inatumiwa na mwanadamu
7
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
na kila jamii ina lugha yake. Hata hivyo kuna nadharia mbali mbali zinazoeleza chanzo na asili
ya lugha. Baadhi ya nadharia hizo ni kama zifuatazo:
Nadhari hii ya uungu pia huchagizwa na kisasili kingine cha Wamisri, Wababiloni, na Wahindi.
Kwa mujibu wa kisasili cha Wababiloni, inasemekana hapo kale Mfalme wa Babeli aliamuru
kujenga mnara mrefu ulioitwa Mnara wa Babeli ili kumfikia Mungu. Kwa lengo hilo Mungu
alikasirishwa sana akaamua kuwachanganya lugha wajenzi wa mnara huo hivyo wakashindwa
kuelewana na hatimaye azma yao ikasitishwa. Kwa hiyo kutokana na imani hiyo waamini
wengine wanakubali kuwa yawezekana lugha nyingi zinazoonekana leo ni tokeo la mnara wa
Babeli.
Kama hivyo haitoshi, Wamisri wanachagiza nadharia hii kwakuwa na Mungu wao aliyeitwa
Thoth ambaye ni Mungu wa Lugha. Wahindu walihusisha uwezo wa mwanadamu wa
kuzungumza na mungu wao wa kike aliyeitwa Brahma ambaye kwa imani yao Brahma ndiye
Mungu muubaji wa ulimwengu lakini lugha alipewa mwanadamu kutoka kwa mke wake
aliyeitwa Sarasvati.
Suala la msingi katika nadharia hii ni kwamba lugha za mwanadamu zinakianzo kimoja na ndio
maana wanaisimu wa baadaye wamekuwa wakizungumzia suala la sarufi bia. Udhaifu wake
nikwamba zinashindwa kujibu maswali kama- kwanini lugha nyingine zinazuka tu sikuhizi bila
ya kuwa nazo zimetoka kwa Mungu. Vile vile, mtazamo huu haujajikita katika tafiti za sayansi
ya lugha yaani Isimu, pia haujafuata taratibuza kiuchunguzi wa kiisimu ambayo ndio sayansi ya
lugha.
8
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
Pamoja na uthibitisho unaoweza kutolewa kwa maneno hayo machache ambayo huenda kila
lugha inayo, bado kuna udhaifu katika nadharia hii. Nadharia hii haijitoshelezi kwakuwa kuna
maneno mengi tu mbayo kwa asili yake hayatokani na milio ya vitu, kama majina, na vitenzi
ambayo ni matokeo ya njia nyingine za uundaji wa maneno na siyo uigo wa sauti asilia.
Pamoja na hayo, nadharia hii bado inatunyima majibu ya swali letu la msingi juu ya asili ya hizo
sauti zilizozalishwa. Kama chanzo cha lugha ni mahusiano ya kijamii, kuna wanyama wengine
wanaoishi katika makundi makundi kama tumbili na ngedere lakini mawasiliano haya
hayaendelei kuwa matamshi ya lugha.
5.0.Utangulizi wa Isimu
5.1.Isimu ni nini?
Fasili iliyozoeleka na pengine inakubalika na wataalamu wengi wa lugha ni kuwa Isimu ni elimu
ya sayansi ya lugha. Ni uchunguzi wa kisayansi na wa kimantiki kuhusu vipengele na sifa mbali
mbali za lugha. Swali ambalo tunaweza kujiuliza ni kwamba; “Kwa nini isimu ni sayansi?”
Verma et al (1989:29), wanasema kuwa isimu ni sayansi kwakuwa hufuata na kutumia mbinu za
kimsingi za utafiti wa kisayansi. Mbinu hizo ni kama zifuatazo:
i. Uchunguzi uliodhibitiwa
ii. Uundaji wa mabunio
iii. Uchanganuzi
iv. Ujumlishi/ujumuishi
v. Utabiri
9
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
5.2.1 Uwazi
Dhana hii inamaanisha kuwa maswala katika isimu huelezwa kwa udhahiri usio na utata wowote.
Hoja huelezwa bila kuleta vugu vugu lolote la kimaana hii ni kinyume na mawasiliano yasiyo
kisayansi.
5.2.2. Utaratibu
Habwe na Karanja, (2003) wanaeleza kuwa utaratibu na uwazi ni dhana zinazokaribiana sana.
Bila kuwa na uwazi ni vigumu kuwa na utaratibu na kinyume chake. Utaratibu ni kufanya jambo
kwa mpangilio mzuri wenye kubainika. Utaratibu unaweza kuhusisha wakati, idadi, umuhimu na
hata ukubwa
5.2.3. Urazini/Uhoromo
Mtafiti hatakiwi kughosha hisia zake na kuzitumia kueleza jambo fulani. Hii ina maanisha kuwa
mtafiti hatakiwi kuruhusu hisia zake kuathiri utafiti wake wa kisayansi hatakama suala la mguso
linatafitiwa. Katika utafiti, kitu chamsingi ni data na matokeo ya uchunguzi yanayotokana na
data zilizotumika. Utetezi wa matokeo vile vile lazima utokane hatua madhubuti za kisayansi na
kiutafiti.
i. Lugha ni nini?
ii. Asili ya lugha ni nipi?
iii. Lugha hufanya kazi namna gani katika mawasiliano?
iv. Lugha inahusiana namnagani na asasi nyingine maishani?
v. Kujua lugha ni nini?
vi. Namna gani mtoto anajifunza lugha?
vii. Kwa nini lugha hubadilika?
viii. Lugha zinatofautiana kwa kiasi gani?
Hivyo katika kujaribu kujibu maswali haya, mwanaisimu hujikuta akiwa na kazi ya kutimiza
majukumu yafuatayo:
10
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
Katika sehemu hii ni muhimu kwa kila msomaji wa lugha au mwanaisimu kuzifahamu na
kuweza kuzitofautisha istilahi zifuatazo kama zinavyotumika katika taaluma ya lugha.
Utendi (aji) ni kile asemacho mjua lugha katika muktadha wa mawasiliano ikiwa ni pamoja na
makosa ya kiutendaji ya bahati mbaya nay ale ya kukusudiwa. Vile vile tunaweza kusema ni
udhihirikaji wa ujuzi wa lugha alionao mjua lugha.
11
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
haielezi wala kuagiza namna mtu anavyotakiwa kutumia lugha bali namna lugha ilivyo na
inavyotumika na wamilisi wa lugha hiyo.
Uelekezi (isimu elekezi) ni mtazamo unaojaribu kuweka kanuni za usahihi wa namna watu
wanavyotakiwa kutumia lugha.
5.5.2. Isimu jamii - Isimu Jamii (social linguistcs) - ni tawi la isimu (elimu ya lugha)
linalochunguza namna lugha inavyotumika katika jamii na uhusiano baina yake.
Tawi hili huzingatia matumizi ya lugha katika mazingira tofauti; aina mbali mbali
za lugha na mazingira yake; uhusiano kati ya lugha na utamaduni wa jamii
inayoitumia. King’ei (2010), anaeleza kuwa, kwanza lugha ni zao la jamii, na ni
kipengele muhimu sana cha utamaduni wa jamii husika. Pili, lugha hutumiwa na
jamii kuhifadhi amali na utamaduni wake na hasa kama chombo maalumu cha
kuwezesha wanajamii kuwasiliana. Hivyo isimu jamii hueleza na kufafanua
mahusiano ya karibu kati ya lugha na jamii ambayo ndiyo mama wa lugha.
5.5.3. Isimu anthropolojia – tawi hili la isimu hukijita katika kutafiti na kueleza historia
ya na miundo ya lugha ambazo bado hazijaandikwa.
5.5.5. Isimu tumizi – huchambua na kueleza matumizi ya nadharia mbali mbali za lugha
na maelezo ya kufundishia lugha.
12
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
6.0.Muundo wa Lugha
Hoja kuwa lugha ni mfumo inamaanisha kuwa lugha inamuundo unaohusisha viambajengo
mbali mbali. Viaambajengo au vipashio hivi ni sauti, neno na sentensi. Kwa pamoja, vipashio
hivi hushirikiana kuunda tungo zenye maana na kama tungo hizo hazina maana au kama
haziwasilishi ujumbe wowote basi tunasema haziwi lugha. Viambajengo hivi, hushughulikiwa na
tanzu tofauti tofauti za isimu muundo. Tanzu hizi ni Fonetiki na fonolojia – ambazo
hushughulikia sauti za lugha, mofolojia – ambayo hushughulikia maumbo ya maneno na jinsi
lugha inavyounda maneno yake, sintaksia – ambayo hushughulikia namna senteni zinavyoundwa
na kanuni zinazotawala uundwaji wake na mwisho ni semantiki – ambayo hushughulikia maana
katika viwango vyote vya vya lugha tulivyo vitaja. Kwa ujumla tanzu hizi zote zinahusiana kwa
ukaribu, zina shirikiana, na kukamilishana. Tazama mchoro ufuatao:
FONOLOJIA/ SEMANTIKI
SINTAKSIA
FONETIKI
MAANA
SENTENSI
SAUTI
MOFOLOJIA
MANENO
13
Chuo Kikuu (cha) Mzumbe (Mzumbe University)
KSW101: Utangulizi wa Lugha na Isimu (Mwaka wa Kwanza 2012/2013)
Mhadhiri: Mr. Simile, O.
E-mail: osimile@gmail.com
Cook, V.J. (1969), 'The analogy between first and second language learning', International
Review of Applied Linguistics, VII/3, 207-216
Halliday, M.A.K. (2003). On Language and Linguistics, Jonathan Webster (ed.), Continuum
International Publishing
King’ei, K. (2010). Misingi ya Isimu Jamii. Taasisi ya Taaluma za Kiswahili: Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam. Tanzania.
OUT na Rubanza, Y.I. (2003). Sarufi Mtazamo wa Kimuundo. The Open University of Tanzania.
Sapir, E. (1921). An introduction to the Study of Speech. New York: Harcourt, Brace, 1921;
Bartleby.com, 2000. www.bartleby.com/186/.
TUKI. (1990). Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Yule, g. (2010). The Study of Language (4th edition). Cambridge University Press.
14